23-0226 Chujio La Mtu Mwenye Busara

Ujume: 65-0822e Chujio La Mtu Mwenye Busara

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Kusanyiko la Ndugu Branham,

Ningependa kualika ulimwengu kuungana nasi kwa njia ya mawasiliano ya simu Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA , saa za Jeffersonville, (ni Saa 2:00 MBILI USIKU ya Tanzania) Wakati sisi Tai tunapokusanyika pamoja kila maili mia mbili mraba katika mojawapo ya makanisa ya nabii. Tutamsikia Mungu akinena kupitia malaika-mjumbe wake wa saba na kutuambia:

Ujumbe huu, na Jumbe zote zingine ambazo ninazungumzia, zinaelekezwa kwenye kusanyiko langu. Si kwa ajili ya kusanyiko lako isipokuwa wawe wanataka kulipokea. Bali limeelekezwa kwa watu hawa hapa.

Yeye anazungumza nasi, UTUKUFU, kusanyiko lake. Si ninyi mnaosema, “Ndugu Branham ni nabii, bali yeye si mchungaji wetu. Mchungaji wetu anasema kuzicheza kanda kanisani hakulingani na Neno la Wakati huu.” “Mchungaji wetu anatuambia yatupasa tumsikilize Yeye. Kulingana na Neno, anatuongoza sasa hivi kwa Roho Mtakatifu .”

Nabii aliwaeleza ninyi na mchungaji wenu.

kwa ajili ya wahudumu wo wote mahali po pote, wakati wo wote, hili halielekezwi kwa madhumuni ya kudharau mafundisho yenu, hili hata halielekezwi kwa kondoo wenu.

Hatutaki kubishana nanyi ndugu na dada. Tunaelewa, halielekezwi kwenu, bali kwetu sisi, tunaoamini kwamba Roho Mtakatifu amemweka malaika-mjumbe Wake wa saba kuwa mchungaji wetu na kutuongoza sisi, kanisa Lake. Tunaamini kuzicheza kanda ndiyo NJIA PEKEE YA KWELI. Mko sahihi na mnafanya kile nabii alichowaambia NINYI mfanye:

Na sikuzote mimi huwarejesha, kama wao ni washiriki wa kanisa fulani, “Mwoneni mchungaji wenu.”

Yawabidi mfanye jinsi mchungaji wenu anavyosema.

Kisha nabii anamwambia mchungaji wenu kwa mara nyingine tena, ili tu kuhakikisha ameelewa.

Sasa, ewe mchungaji, nataka ujue jambo hilo, ya kwamba, ninazungumza haya kwa ajili ya kusanyiko langu peke yake. Nami nina haki ya kutenda jambo hilo, kwa maana nimewekwa na Roho Mtakatifu kuwachunga kondoo hawa.

Yeye Ametumwa kutuchunga sisi, kondoo wake; wale ambao Mungu amempa KUWATUNZA. Roho Mtakatifu ndiye mchungaji wetu anapotuzungumzia na kutuongoza kila siku kwa Sauti yake iliyothibitishwa.

Hivi ndivyo Bwana atuongozavyo kufanya. Hatuko dhidi yenu ama mchungaji wenu, au jinsi mnavyohisi kuongozwa na Bwana kufanya. Kila mmoja yampasa kufanya jinsi anavyohisi Bwana anamwongoza kufanya kulingana na Neno.

Tuna chujio moja, UJUMBE HUU. Kila kitu tunachokisikia lazima kipitie kwenye chujio hilo. Sauti tunayoisikia kwenye kanda hizi ndiyo Sauti pekee tunayoamini kwa 100% kuwa Bwana Asema Hivi.

Hivi unaamini ya kwamba huko kutiwa mafuta juu ya watu hao kunamaanisha ya kwamba ni upako wa Roho Mtakatifu?” Naam, bwana, Roho Mtakatifu halisi wa Mungu juu ya mtu, na hata hivyo wao ni wa uongo.

Kikomo chetu cha milele kinategemea kile YEYE ALICHOSEMA KWENYE KANDA, si kile mtu mwingine yeyote ama kundi la watu wanachosema. Kwa hiyo, hatuwezi, na hatutamsikiliza mtu mwingine . anawezaje Mtu yeyote kubahatisha ?

Njooni mkusanyike pamoja nasi zaidi sana kama mwonavyo ile siku ikikaribia.

Watu wanaweza kuketi moja kwa moja nyumbani mwao ama nini hii mwao…wakusanyike makwao, makanisani mwao, na kadhalika, na kusikiliza ibada.

Hilo, marafiki , kulingana na nabii wa Mungu, si kulingana na fasiri ya mtu fulani ya kile Biblia inachosema, ni kukusanyika pamoja kulizunguka Neno zaidi sana kama tunavyoona ile siku ikikaribia.

Sanduku lina faida gani bila Mungu? Ni sanduku tu la mbao, meza mbili za mawe.

Njoo ukusanyike pamoja nasi tunaposikiliza chujio lililoandaliwa na Mungu, anapotuletea Ujumbe: Chujio La Mtu Mwenye Busara 65-0822E.

Ndugu. Joseph Branham

Chunguzeni kile mnachopigania. Chunguzeni kilichowaleta hapa. Chunguza kwa nini unaenda kanisani. Nini kinachowafanya… Ni vyema kwenda kanisani, bali usiende kanisani tu; jambo hilo halitawaokoa.