21-1017 Nawe Hujui

UJUMBE: 65-0815 Nawe Hujui

PDF

pakua – m4a

pakua – amr 11MB (use Firefox to download)

BranhamTabernacle.org

Tai wanakusanyika Pamoja.

Tai Wapendwa Wanaokusanyika,

Loo, ni kipindi cha namna gani, ni wakati wa jinsi gani! Hakuna kitu ambacho kimeachwa bila kutimia . Tai wa Mungu wanakusanyika kwenye Mzoga. Unabii unatimia. Hakuna hata wakati mmoja ambapo imekosea, wala haitakosea, kwa kuwa sisi, tuliochaguliwa tangu zamani kuliona, tunaliona.

Tangu Baba alipompeleka Nabii Wake Nyumbani, Bibi-arusi Wake hajawahi kuungana kwenye Sauti Yake kama ilivyo leo hii. Alichagua njia ambayo Neno Lake lingekuja, na hiyo ilikuwa kwa manabii Wake, ambao walichaguliwa na kuteuliwa kimbele . Nasi tumeridhika, na kushawishika, ya kwamba huyu ni Yesu Kristo akijitambulisha Mwenyewe , akijitambulisha Mwenyewe katika unabii.

Jinsi Ilivyokuwa kwamba aliwaongoza wana wa Israeli kupitia jangwani, katika safari yao, kama mfano wa watu walioitwa watoke leo hii. Huyu hapa, kwa utafiti wa kisayansi, hata alijitambulisha mwenyewe mbele ya sayansi. Na kwa matendo Yake yenyewe na kwa unabii Wake mwenyewe, mambo ambayo yametabiriwa kwake yeye kuyafanya katika siku hii, kumfanya Yeye kuwa yeye yule jana, leo, na hata milele, yamethibitishwa kikamilifu. Je! Haitoshi kufanya mioyo yetu kuwaka ndani yetu?

Kama Hao mitume wa siku hiyo, tumekusudiwa Uzima, Jambo tu litupasalo kufanya ni kuifanya Sauti Yake ijulikane; Na sauti hiyo ni mawazo ya Mungu mwenyewe yaliyotamkwa. Tunaamini kila sehemu yake . Si lazima tuthibitishe lo lote kisayansi, ama kumuuliza Msadukayo ye yote ama Mfarisayo, ama Mtu Yeyote yule, juu ya jambo hilo. Yeye Alilisema hilo nasi tunaliamini. kondoo Wake huisikia Sauti Yake, ikinena kupitia Nabii wake.

Ujumbe huu ni Sauti ya Mungu kwenye kanda. Ndiyo Ufunuo wote wa Yesu Kristo, Agano la Kale na lile Jipya yakiwekwa pamoja. Siri zote zimefunuliwa. Hatuongezi kwenye hilo au kuondoa kutoka Kwake. Tunafanya hasa kama vile Yeye alivyotuamuru tufanye, DUMUNI NA NENO.

Haya basi. Ni huyo mtu wa ndani. Huyo wa ndani ambaye ataliitikia Neno, atadumu na Neno, haidhuru.

Alitabiri na kutuambia nini kingetokea.
Ulimwengu mzima ungerundikana katika ukichaa, na utaendelea kuwa mbaya na mbaya na mbaya, hata watakuwa kundi la wenye kichaa.

Alisema ile saa imekaribia wakati tutakapoona jambo fulani likitukia, jambo fulani litatukia. Na Jumbe Hizi zote Zilikuwa utangulizi na Zimekuwa zikiweka msingi kwa ajili ya Ujumbe mfupi, na wa haraka ambao utatikisa mataifa yote. Ninaamini sasa tunayaona mambo haya yakitukia sasa hivi.

Nami najua ya kwamba, baada ya kuondoka kwangu kutoka dunia hii, hizo kanda na vitabu vitaendelea kuwepo, na wengi wenu ninyi watoto wadogo mtaona, katika siku zijazo, ya kwamba jambo hili ni Kweli kabisa, kwa maana nanena katika Jina la Bwana .

Hebu na tusikilize na tuangalie kwa undani maelezo yote ya ndoto ambazo nabii alizotuambia . Jinsi walivyomwona amesimama kwenye mwamba uliotandaa kutoka mashariki kwenda magharibi, katika umbo lililochongoka kama piramidi, jinsi alivyokuwa juu ya farasi ambaye hawajawahi kuona kitu kingine kama yeye maishani mwao mwote; farasi mkubwa sana mweupe, mwenye manyoya ya shingoni yamening’inia chini.

Jinsi Wingu jeupe lilivyokuja na likamchukua na likamuondoa , kisha Baada ya kitambo kidogo likamketisha upande wa mbele wa ile meza naye alikuwa mweupe kama theluji Alikuwa Amesimama pale Akinena kwa mamlaka. Hakukuweko na kukisia katika jambo hilo. Kila mtu alifahamu yale hasa Aliyokuwa Anasema.”

“ Nitapanda farasi kupitia njia hii tena !”

Ninaamini tunaliona Jambo hilo Likitendeka leo hii. Jumbe hizi Zimepanda farasi kupitia njia ile tena . Mungu anawaita Tai wake pamoja kutoka kote ulimwenguni. Wanaungana kwenye Neno Lake, Sauti Yake, Ujumbe Huu.

Ulimwengu ni uchi, mnyonge, wenye Mashaka, kipofu, nao haujui. Lakini Bibi-arusi amevikwa Neno, mwenye utukufu wa Roho, akifurahi kwa Neema yake, na tunaweza kuona na kujua sisi ni nani: BIBI-ARUSI WAKE .

Alitueleza kwa kadiri alivyojua, hakuona chochote cha kuzuia, wakati huu, Kuja kwa Bwana Yesu, nje ya utayari wa Kanisa Lake.

Enyi Tai, hebu na Tujifanye wenyewe tayari. Ninakualika kukusanyika pamoja nasi kwenye Mzoga Jumapili saa 8:00 Nane Mchana , saa za Jeffersonville,( Ni saa 3:00 tatu Usiku ya Tanzania), kusikia Sauti ya Mungu kwa ajili ya wakati wetu ikitufanya tayari kwa Unyakuo unaokuja hivi karibuni tunaposikia: 65-0815 Nawe Hujui .

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma :

Ufunuo 3: 14-19
Wakolosai 1: 9-20