All posts by admin5

25-0105 Ufunuo, Mlango Wa Nne Sehemu Ya II

UJUMBE: 61-0101 Ufunuo, Mlango Wa Nne Sehemu Ya II

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi wa Kanisa la Nyumbani,

Hebu sote tukusanyike pamoja na kuusikia Ujumbe,   61-0101 Ufunuo, Mlango Wa Nne Sehemu ya II Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville.(Ni saa 2 MBILI USIKU ya Afrika Mashariki)

Ndugu Joseph Branham

24-1231 Lile Shindano Na Ushirika

UJUMBE: 62-1231 Lile Shindano

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi arusi,

Natumai kila mmoja wenu alikuwa na Krismasi nzuri pamoja na marafiki na familia yako. Ninayo shukurani jinsi gani leo kujua ya kwamba Bwana wetu Yesu hajakwama horini kama ulimwengu unavyomwona Yeye leo, lakini yu hai na Yuko katikati ya Bibi-arusi Wake, akijifunua Mwenyewe kupitia Sauti Yake kuliko hapo awali, BWANA ASIFIWE.

Kama nilivyokwishatangaza, ningependa tuwe na Ushirika kwa mara nyingine tena katika nyumba zetu/makanisa yetu katika mkesha wa Mwaka Mpya, tarehe 31 Desemba. Kwa wale wanaotaka kushiriki, tutasikiliza Ujumbe,  62-1231 Lile Shindano, na kisha kuingia moja kwa moja kwenye ibada ya Ushirika, ambayo Ndugu Branham anaitambulisha wakati wa kuhitimisha Ujumbe.

Kwa waamini walio eneo hili, tutaanza kanda saa 1:00 MOJA JIONI. Hata hivyo, kwa wale walio katika maeneo ya majira tofauti, tafadhali uanzeni Ujumbe kwa wakati unaofaa kwenu. Baada ya Ndugu Branham kuleta Ujumbe wake wa Mkesha wa Mwaka Mpya, tutasimamisha kanda mwishoni mwa aya ya 59, na kuwa na takriban dakika 10 za muziki wa piano wakati tunapokula Meza ya Bwana. Kisha tutaendeleza tena kanda Ndugu Branham anapofunga ibada. Kwenye kanda hii, yeye anaiacha sehemu ya ibada ya Kutawadhana miguu, ambayo na sisi pia tutaiacha.

Maagizo ya jinsi ya kupata divai, na jinsi ya kuoka mkate wa Ushirika yanaweza kupatikana katika anuani zilizo hapa chini. Unaweza kucheza au kupakua sauti kutoka kwenye tovuti, au unaweza tu kuicheza ibada kwenye Redio ya Sauti kwenye programu ya Lifeline (ambayo itachezwa kwa Kiingereza saa 1:00 JIONI saa za Jeffersonville.)

Wakati tunapoukaribia mwaka mwingine wa huduma kwa Bwana wetu, hebu na tuonyeshe upendo wetu Kwake kwa kuisikia kwanza Sauti Yake, na kisha tushiriki Meza Yake. Utakuwa wakati wa utukufu na mtakatifu jinsi gani wakati tunapoyaweka upya maisha yetu kwa ajili ya Huduma Yake.

Mungu awabariki,

Ndugu Joseph

24-1229 Ufunuo, Mlango Wa Nne Sehemu Ya I

UJUMBE: 60-1231 Ufunuo, Mlango Wa Nne Sehemu Ya I

PDF

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Watakatifu Waliovikwa Mavazi Meupe,

Wakati tunapoisikia Sauti ya Mungu ikisema nasi, jambo fulani hutokea ndani kabisa ya nafsi zetu. Utu wetu wote unabadilishwa na ulimwengu unaotuzunguka unaonekana kufifia.

Mtu anawezaje kueleza kile kinachotendeka katika mioyo yetu, akili zetu, na nafsi zetu, wakati Sauti ya Mungu inapofunua Neno Lake kwa kila Ujumbe tunaousikia?

Kama vile nabii wetu, tunahisi tumenyakuliwa hadi kwenye mbingu ya tatu nazo nafsi zetu zinaonekana kuuacha mwili huu upatikanao na mauti. Hakuna maneno ya kueleza kile tunachojisikia Mungu anapotufunulia Neno Lake kuliko hapo awali.

Yohana aliwekwa kwenye kisiwa cha Patmo naye akaombwa aandike kile alichokiona na kukiweka kwenye kitabu kiitwacho Ufunuo, ili kiende katika nyakati zote. Siri hizo zilikuwa zimefichwa hadi zilipofunuliwa kwetu kupitia malaika-mjumbe Wake wa 7 aliyemchagua.

Kisha Yohana akasikia Sauti iyo hiyo juu yake naye akanyakuliwa hadi katika mbingu ya tatu. Sauti hiyo ilimwonyesha nyakati za kanisa, kuja kwa Wayahudi, kumwagwa kwa yale mapigo, Kunyakuliwa, Kuja mara ya pili, Utawala wa Miaka Elfu, na Makazi ya Milele ya waliookolewa Wake. Alimchukua na kumwonyesha Yohana kitu hicho chote kikifanyiwa mazoezi kama Yeye alivyosema angefanya.

Lakini Yohana alimwona nani wakati alipoyaona yale mazoezi? Hakuna kweli aliyejua hadi leo hii.

Kitu cha kwanza alichoona katika kule Kuja kilikuwa ni Musa, aliyewawakilisha watakatifu waliokufa ambao wangefufuliwa; nyakati zote sita walizolala. Lakini si Musa tu peke yake aliyekuwa amesimama pale, bali Eliya alikuwa pale pia.

Yule Eliya aliyekuwa amesimama alikuwa ni nani?

Bali Eliya alikuwako; yule mjumbe wa siku ya mwisho, pamoja na kundi lake, la waliobadilishwa, Walionyakuliwa.

UTUKUFU…HALELUYA… ni nani ambaye Yohana alimuona akiwa amesimama pale?

Si mwingine ila malaika-mjumbe wa 7 wa Mungu, William Marrion Branham, pamoja na KUNDI LAKE LA WALIOBADILISHWA, WALIONYAKULIWA…KILA MMOJA WETU!!

Eliya aliwakilisha watakatifu waliokufa …Ninamaanisha Musa, na kufufuliwa. Eliya aliwakilisha kundi lililohamishwa. Kumbukeni, Musa alikuwa wa kwanza, na kisha Eliya. Eliya alikuwa awe ndiye mjumbe wa siku za mwisho, ili kwa yeye na kundi lake ungekuja ufufuo…ungekuja ninii…vema, ungekuja Unyakuo, namaanisha. Musa alileta ufufuo na Eliya akaleta kundi Lililonyakuliwa. Na, hapo, wote wawili waliwakilishwa papo hapo.

Nena kuhusu kufichua, kufunua, na Ufunuo.

Hii hapa! Tunaye moja kwa moja pamoja nasi sasa, Roho Mtakatifu, Yesu Kristo, yeye yule jana, leo, na hata milele. Wewe ni…Anawahubiria, anawafundisha, anajaribu kuwafanya muone yaliyo mema na mabaya. Ni Roho Mtakatifu Mwenyewe akinena kupitia midomo ya wanadamu, akifanya kazi miongoni mwa wanadamu, akijaribu kuonyesha rehema na neema.

Sisi ndio wale Watakatifu Waliovikwa Mavazi Meupe ambao malaika Wake aliwaona wakija kutoka kote ulimwenguni kula Mkate wa Uzima. Tumeposwa na kuolewa Naye nasi tumehisi busu Lake la posa mioyoni mwetu. Tumetoa kiapo Kwake, na kwa Sauti Yake tu. Hatuna, nasi hatutajitia unajisi kwa sauti nyingine yoyote.

Bibi-arusi anajitayarisha kupanda juu kama Yohana alivyofanya; kuingia Uweponi mwa Mungu. Tutatwaliwa juu kwenye Unyakuo wa Kanisa. Jinsi hilo linavyozizungusha nafsi zetu!

Ni kipi kifuatacho Yeye anachoenda kutufunulia?

Hukumu; jiwe la akiki, na kile linachowakilisha; kazi yake. Yaspi, na mawe yote mbalimbali. Yeye atayachukua haya yote kote kupitia kwa Ezekieli, arudi kwenye Mwanzo, arejee kwenye Ufunuo, aje katikati ya Biblia, ayafungamanishe pamoja; mawe haya yote mbalimbali na rangi.

Ni Roho Mtakatifu yeye yule, Mungu yeye yule, akionyesha ishara zile zile, maajabu yale yale, akifanya jambo lile lile kama Yeye alivyoahidi. Ni Bibi-arusi wa Yesu Kristo akijiweka mwenyewe tayari kwa kuisikia Sauti Yake.

Tunawakaribisha kuungana nasi tunapoingia katika ulimwengu wa roho saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville (Ni saa 2:00 MBILI USIKU ya Afrika Mashariki), kumsikia Eliya, mjumbe wa Mungu kwa wakati huu wa mwisho, akifunua siri ambazo zimefichwa katika nyakati zote.

Ndugu. Joseph Branham

Ujumbe: 60-1231 Ufunuo, Mlango wa Nne Sehemu ya I

. Tafadhali ukumbukeni Ujumbe wetu wa Mwaka Mpya, Jumanne usiku: Lile Shindano 62-1231. Hakuna njia bora ya kuuanza Mwaka Mpya.

24-1222 Zawadi Ya Mungu Iliyofungwa

UJUMBE: 60-1225 Zawadi Ya Mungu Iliyofungwa

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi. JEZU,

Ee Mwana-Kondoo wa Mungu, Wewe ndiwe Zawadi iliyo kuu ya Mungu iliyofungwa kwa ulimwengu. Umetupa Zawadi iliyo kuu kuliko zote iliyowahi kutolewa, Wewe Mwenyewe. Kabla haujaumba nyota ya kwanza, kabla haujaumba dunia, mwezi, mfumo wa jua, ulitujua sisi na kutuchagua tuwe Bibi-arusi Wako.

Ulipotuona wakati huo, ulitupenda. Tulikuwa nyama ya nyama Yako, mfupa wa mfupa Wako; tulikuwa sehemu Yako. Jinsi Ulivyotupenda na kutaka kushirikiana nasi. Ulitaka kuushiriki Uzima Wako wa Milele nasi. Tulijua basi, tungekuwa Bibi JEZU Wako.

Uliona tungeshindwa, kwa hivyo Wewe ulilazimika kuiandaa njia ya kuturudisha sisi. Tulikuwa tumepotea na bila tumaini. Kulikuwa na njia moja tu, Ilibidi Wewe ufanyike “Uumbaji Mpya”. Ilibidi Mungu na mwanadamu wawe Mmoja. Ilibidi Wewe ufanyike sisi, ili sisi tuweze kuwa Wewe. Hivyo, Ukauweka mpango Wako mkuu utende kazi maelfu ya miaka iliyopita katika bustani ya Edeni.

Umetamani sana kuwa pamoja nasi, Bibi-arusi Wako wa Neno kamilifu, lakini Wewe ulijua kwanza Ilikubali uturudishe sisi kwenye yale yote yaliyokuwa yamepotea hapo mwanzo. Ulingoja na kungoja na kungoja hadi siku hii kuukamilisha mpango Wako.

Siku hiyo imefika. Lile kundi dogo uliloliona hapo mwanzo liko hapa. Kipenzi chako anayekupenda Wewe na Neno Lako kuliko kitu chochote.

Ilikuwa ni wakati Wako wa kuja na kujidhihirisha Mwenyewe katika mwili wa mwanadamu kama ulivyofanya kwa Ibrahimu, na kama ulivyofanya ulipofanyika Uumbaji mpya. Jinsi Wewe umeisubiri kwa hamu siku hii ili uweze kutufunulia sisi siri Zako zote kuu zilizofichwa tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu.

Unamjivunia sana Bibi-arusi Wako. Jinsi Wewe unavyopenda kumwonyesha Yeye na kumwambia Shetani, “Hata ujaribu kuwafanyia nini, wao hawataondoshwa; hawatapatana kuhusu Neno Langu, Sauti Yangu. Wao ni BIBI-ARUSI Wangu wa NENO KAMILIFU.” Wao ni wakupendeza sana Kwangu. Hebu Watazame tu! Kupitia majaribio na majaribu yao yote, wao wanabaki waaminifu kwa Neno Langu. nitawapa zawadi ya milele. Yote niliyo Mimi, Nawapa wao. TUTAKUWA MMOJA.

Tunachoweza tu kusema ni: “JEZU, TUNAKUPENDA. Jalia tukukaribishe nyumbani mwetu. Hebu na tukupake Wewe mafuta na tuioshe miguu Yako kwa machozi yetu na kuibusu. Hebu na tukuambie jinsi tunavyokupenda Wewe.”

Yote tuliyo, tunakupa wewe JEZU. Hiyo ndiyo zawadi yetu Kwako JEZU. Tunakupenda. Tunakuhimidi. Tunakuabudu.

Ninawaalika kila mmoja wenu aungane nasi Jumapili saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni saa 2:00 MBILI USIKU ya Afrika Mashariki) na umkaribishe JEZU nyumbani kwako, kanisani kwako, ndani ya gari lako, popote uwezapo kuwa, na uipokee Zawadi iliyo kuu kuliko zote iliyowahi kutolewa kwa mwanadamu; Mungu Mwenyewe akizungumza na kushirikiana nawe.

Ndugu. Joseph Branham

60-1225 Zawadi ya Mungu Iliyofungwa

TANGAZO MAALUM

Mpendwa Bibi-arusi,

Bwana ameweka moyoni mwangu kuwa na Ujumbe Maalum na Ibada ya Ushirika katika Mkesha wa Mwaka Mpya tena mwaka huu. Ni jambo gani kubwa zaidi tunaloweza kufanya, Enyi marafiki, kuliko kuisikia Sauti ya Mungu ikizungumza nasi, kushiriki Meza ya Bwana, na kuyaweka wakfu tena maisha yetu kwa huduma Yake wakati wa kuukaribisha Mwaka Mpya. Utakuwa wakati mtakatifu jinsi gani kuufungia nje ulimwengu, na kuungana na Bibi-arusi kwa ajili ya huku kukusanyika Maalum katika Neno, tunaposema kutoka mioyoni mwetu, “Bwana, utusamehe makosa yote tuliyofanya mwaka mzima; sasa tunakukaribia Wewe, tukikuomba ikiwa utatushika mkono na kutuongoza mwaka huu ujao. Jalia tukutumikie Wewe zaidi ya tulivyowahi, na kama ni katika Mapenzi Yako ya Kiungu, jalia uwe ndio mwaka wa ule Unyakuo mkuu utakaotukia. Bwana, tunataka tu kwenda Nyumbani kuishi Nawe Milele yote.” Nasubiri kwa hamu kukusanyika kukizunguka Kiti Chake cha Enzi kwa ajili ya ibada hii maalum ya kujiweka wakfu upya, Bwana asifiwe.

Kwa waamini walio katika eneo la Jeffersonville, ningependa kuianza kanda saa 1:00 MOJA JIONI katika saa za eneo letu. Ujumbe kamili na ibada ya Ushirika itakuwa kwenye Redio ya Sauti wakati huo, kama tulivyofanya wakati uliopita. Vifurushi vya divai ya Ushirika vtapatikana Jumatano, tarehe 18 Desemba, kuanzia 7:00 – 11:00 jioni, kwa wewe kuja kuchukua kwenye jengo la YFYC.

Kwa wale ambao wanaishi nje ya eneo la Jeffersonville, tafadhali iweni na ibada hii maalum kwa wakati unaofaa kwenu. Tutakuwa na anuani ya kupakuliwa yenye Ujumbe na Ushirika hivi karibuni.

Tunapokaribia Sikukuu ya Krismasi, nataka nikutakie wewe na familia yako Msimu wa AJABU na SALAMA wa Sikukuu, na KRISmasi Njema, iliyojaa furaha ya Bwana Yesu aliyefufuka…Lile NENO.

Mungu awabariki,

Ndugu Joseph

Chanzo : https://branhamtabernacle.org/en/bt/F6/110067

24-1208 Wakati wa Kanisa La Laodikia

UJUMBE: 60-1211E Wakati wa Kanisa La Laodikia

PDF

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Wateule,

Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti Yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja Nami.

Enyi wahudumu, mfungulieni milango yenu malaika wa Mungu kabla hamjachelewa. Irudisheni Sauti ya Mungu kwenye mimbara zenu kwa kuzicheza kanda. Ndiyo Sauti pekee ya Mungu iliyothibitishwa kwa ajili ya siku yetu yenye Maneno ya kutokosea. Ndiyo Sauti pekee yenye Bwana Asema Hivi. Ndiyo Sauti pekee ambayo Bibi-arusi wote wanaweza kusema AMINA kwake.

Huu ndio wakati mkuu wa nyakati zote. Yesu anatupa sifa Yake kwa vile siku za neema Yake zinakwisha. Wakati umefika mwisho. Ametufunulia tabia Zake hasa katika wakati huu wa mwisho. Yeye ametupa mtazamo mmoja wa mwisho wa Uungu Wake mkuu wa neema. Wakati huu ni ufunuo wa jiwe la kifuniko wa nafsi Yake.

Mungu alikuja katika wakati huu wa Laodikia na kunena kupitia mwili wa mwanadamu. Sauti Yake imerekodiwa na kuhifadhiwa ili kumwongoza na kumkamilisha Bibi-arusi Neno Wake. Hakuna kabisa Sauti nyingine inayoweza kumkamilisha Bibi-arusi Wake ila Sauti Yake Mwenyewe.

Katika wakati huu wa mwisho, Sauti Yake iliyo kwenye kanda imewekwa kando; imetolewa nje ya makanisa. Hawataki tu kabisa kuzicheza kanda. Kwa hiyo Mungu anasema, “Mimi niko kinyume nanyi nyote. Nitawatapika mtoke katika kinywa Changu. Huu ni mwisho.”

“Kwa kuwa saba kati ya nyakati saba, sijaona kitu ila watu wakiliheshimu neno lao wenyewe kuliko Langu. Kwa hiyo mwishoni mwa wakati huu ninawatapika mtoke katika kinywa Changu. Yote yamekwisha. Nitazungumza basi. Naam, niko hapa katikati ya Kanisa. Amina wa Mungu, aliye mwaminifu na wa kweli atajifunua Mwenyewe na itakuwa KWA NJIA YA NABII WANGU.”

Kama ilivyokuwa hapo awali, wao wanafanya vile vile walivyofanya baba zao katika siku za Ahabu. Kulikuwa na jumla yao mia nne na wote walikubaliana; na wote wakisema jambo lile lile, waliwadanganya watu. Lakini nabii MMOJA, MMOJA TU, alikuwa sahihi na hao wengine wote walikuwa makosani kwa sababu Mungu alikuwa ametoa ufunuo kwa MMOJA TU.

Hii si kusema kwamba huduma zote ni za uongo na zinawadanganya watu. Wala Mimi sisemi mtu mwenye wito wa kuhudumu hawezi kuhubiri au kufundisha. Ninasema huduma tano ya KWELI itaweka KANDA, Sauti ya Mungu kwa Bibi-arusi, kuwa ndio Sauti iliyo muhimu sana UNAYOPASWA KUISIKIA. Sauti iliyo kwenye kanda ndio Sauti PEKEE ambayo imethibitishwa na Mungu Mwenyewe kuwa Bwana Asema Hivi.

Jihadharini na manabii wa uongo, kwa maana wao ni mbwa mwitu wakali.

Utajuaje kwa hakika njia sahihi kwa ajili ya siku hii? Kuna mgawanyiko jinsi hii miongoni mwa waaminio. Kundi moja la watu linasema huduma tano itamkamilisha Bibi-arusi, huku jingine linasema Bonyeza Play tu. Hatupaswi kugawanyika; tunapaswa kuungana kama BIBI-ARUSI MMOJA. Jibu sahihi ni lipi?

Hebu na tuifungue mioyo yetu pamoja na tusikie kile Mungu anachosema kwa Bibi-arusi kupitia nabii Wake. Kwa maana sote tunakubali, Ndugu Branham ndiye malaika-mjumbe Wake wa saba.

Juu ya msingi wa tabia za wanadamu peke yake, mtu ye yote anajua ya kwamba palipo na watu wengi kuna hata na maoni yasiyopatana juu ya mambo madogo-madogo ya fundisho muhimu ambalo wote wanashikilia pamoja. Ni nani basi atakayekuwa na mamlaka ya kutokosea ambayo itarudishwa katika wakati huu wa mwisho, kwa kuwa wakati huu wa mwisho utarudi kwenye kumdhihirisha Bibi-arusi wa Neno Halisi? Hiyo inamaanisha tutakuwa na Neno tena kama lilivyotolewa kikamilifu, na kueleweka kikamilifu katika siku za Paulo. Nitakwambia ni nani atakayekuwa nalo. Itakuwa ni nabii aliyethibitishwa kinaganaga, ama hata aliyethibitishwa kinaganaga zaidi kuliko nabii ye yote katika nyakati zote tangu Henoko hata siku hii, kwa sababu mtu huyu itambidi kuwa na huduma ya kinabii ya jiwe la kifuniko, na Mungu atamtambulisha. Haitambidi kujitetea, Mungu atamtetea kwa sauti ya ishara. Amina.

Hivyo, Ujumbe huu ulionenwa na mjumbe Wake ulitolewa kikamilifu, na unaeleweka kikamilifu.

Ni kitu gani kingine ambacho Mungu alichosema kumhusu malaika-mjumbe Wake wa saba na Ujumbe wake?

  • . Yeye atasikia tu kutoka kwa Mungu.
  • . Atakuwa na “Bwana asema hivi” na kunena kwa niaba ya Mungu.
  • . Yeye atakuwa kinywa cha Mungu.
  • . YEYE, KAMA INAVYOTANGAZWA KATIKA MALAKI 4:6, ATAIGEUZA MIOYO WA WATOTO IWAELEKEE BABA ZAO.
  • . Ata warudisha wateule wa siku za mwisho nao watamsikiliza nabii aliyethibitishwa akitoa kweli halisi kama vile ilivyokuwa kwa Paulo.
  • . Ata irudisha kweli kama walivyokuwa nayo.

Na kisha Yeye alisema nini kutuhusu sisi?

Na hao wateule walio pamoja naye katika siku hiyo watakuwa ndio wanaomdhihirisha Bwana kwa kweli na watakuwa ndio Mwili Wake na kuwa sauti Yake na kutenda kazi Zake. Haleluya! Unaliona hilo?

Kama ungali una mashaka yo yote juu ya jambo hili mwombe Mungu kwa Roho Wake akujaze na kukuongoza, kwa kuwa Neno linasema, “KWA MAANA WALIO WATEULE HAWAWEZI KUPUMBAZWA”. Hakuna mtu anayeweza kukupumbaza kama wewe ni Bibi-arusi.

Wakati Wamethodisti waliposhindwa, Mungu aliwainua wengine na kwa hiyo jambo hilo limeendelea kwa miaka mingi mpaka katika wakati huu wa mwisho kuna watu wengine nchini, ambao chini ya mjumbe wao watakuwa ndio sauti ya mwisho kwa wakati wa mwisho.

Naam bwana. Kanisa si “kinywa” cha Mungu tena. Ni kinywa chake lenyewe. Kwa hiyo Mungu analiacha. Ataliangamiza kupitia kwa nabii na bibi-arusi, kwa kuwa sauti ya Mungu itakuwa ndani ya bibi-arusi. Naam iko, kwa maana inasema katika sura ya mwisho ya Ufu. aya ya 17 “Roho na bibi-arusi wasema, njoo.” Mara nyingine tena ulimwengu utasikia moja kwa moja kutoka kwa Mungu kama ilivyokuwa wakati wa Pentekoste; lakini bila shaka huyo Bibi-arusi Neno atakataliwa kama ilivyokuwa katika wakati wa kwanza.

Bibi-arusi anayo sauti, bali itasema tu kile kilicho kwenye kanda. Kwa maana Sauti hiyo INATOKA MOJA KWA MOJA KWA MUNGU, hivyo haihitaji kufasiriwa kwa vile ilivyotolewa kikamilifu na inaeleweka kikamilifu.

Njoo uungane nasi Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni Saa 2:00 MBILI USIKU ya Afrika Mashariki) tunapoisikia Sauti hiyo ikitufunulia: Wakati wa Kanisa la Laodikia 60-1211E.

Ndugu. Joseph Branham

24-1201 Wale Wanawali Kumi, Na Wayahudi Mia Na Arobaini Na Nne Elfu

UJUMBE: 60-1211M Wale Wanawali Kumi, Na Wayahudi Mia Na Arobaini Na Nne Elfu

PDF

BranhamTabernacle.org

Habari Za Asubuhi Marafiki,

Haijawahi kutokea katika historia ya ulimwengu kuwepo na wakati ambapo Bibi-arusi wa Kristo kutoka ulimwenguni kote angeweza kuungana pamoja katika nia moja, wakati sauti kutoka Mbinguni, ile Sauti halisi ya Mungu, ingeweza kuja ikienda kasi.

Maandiko yanatimia. Ni ishara ya Mbegu ya wakati wa kuungana. Ule muungano usioonekana wa Bibi-arusi wa Kristo unafanyika tukiketi katika uwepo wa Mwana, tukiivishwa, tukijiweka wenyewe tayari kwa kuisikia Sauti ya Mungu halisi.

Sisi tunakamilishwa na huduma tano Yake.

Ni wangapi wanaoamini kwamba karama na miito havina majuto? Biblia ilisema kuna karama tano katika kanisa. Mungu ameweka katika kanisa Mitume, au wamishenari, mitume, manabii, waalimu, wainjilisti, wachungaji.

  • . Mhubiri: Ningeenda barabarani. Mtu fulani angesema, “Je, wewe ni mhubiri?” Ningesema, “Ndiyo bwana. Loo, Ndiyo, mimi ni mhubiri.”
  • . Mwalimu: Na sasa sababu sikuchukua kuhubiri asubuhi ya leo, ilikuwa ni kwamba, nilifikiri, katika kufundisha, tungelielewa vizuri zaidi kuliko kuchukua somo na kulipitia juu juu. Tungelifundisha tu.
  • . Mtume: Neno “mmishenari” linamaanisha “mtu aliyetumwa.” “Mtume” maana yake ni “mtu aliyetumwa.” Mmishenari ni mtume. Mimi—mimi, mimi ni mmishenari, kama mjuavyo, ninafanya uinjilisti, kazi ya kimishenari, karibu mara saba nchi za ng’ambo, kote ulimwenguni.
  • . Nabii: Je, unaniamini mimi kuwa nabii wa Mungu? Basi nenda ukafanye kile ninachokuambia.
  • . Mchungaji: Je, mumeelewa na hayo niliyowatendea? Ninyi mumeniita “mchungaji wenu”; nanyi mwanena vema, maana ndivyo nilivyo.

Nami nikawaona hao mamilioni wamesimama pale, nikasema, “Hivi hawa wote ni wa Branham?” Kasema, “La.” Kasema, “Hao ni waongofu wako.” Ndipo nikasema, ni—nikasema, “Ninataka kumwona Yesu.” Akasema, “Bado. Itachukua muda kabla Yeye hajaja. Ila atakuja kwako kwanza nawe utahukumiwa kwa Neno ambalo ulihubiri,

Ndipo sisi sote tutainua mikono yetu na kusema, “Tunatumainia hilo!”

Jambo fulani liko karibu kutukia. Nini kinatendeka? Waliokufa katika Kristo wameanza kufufuka pande zote kunizunguka. Ninahisi badiliko likija mwilini mwangu. Nywele zangu za mvi, zimeondoka. Angalia uso wangu… makunyanzi yangu yote yametoweka. Kuugua kwangu na maumivu…. YAMEKWISHA. Kuhisi kwangu huzuni kumetoweka mara moja. Nimebadilishwa kwa dakika moja, katika kufumba na kufumbua jicho.

Kisha tutaanza kutazama kando yetu na kuwaona wapendwa wetu. Loo, yule pale Mama na Baba…Utukufu, mwanangu…binti yangu. Babu, Bibi, loo, nimewakumbuka sana nyote wawili. Halo …yule pale rafiki yangu wa zamani. LOO, TAZAMA, ni Ndugu Branham, nabii wetu, Haleluya!! yuko hapa. Linatukia!

Kisha pamoja, wote kwa pamoja, tutanyakuliwa huko juu mahali fulani hewani ng’ambo ya nchi. Tutamlaki Bwana wakati akishuka. Tutasimama huko pamoja Naye juu ya mizingo ya dunia hii na kuziimba nyimbo za ukombozi. Tutaimba na kumsifu Yeye kwa ajili ya neema Yake ya ukombozi ambayo ametupa.

Ni mangapi yote yanayomngojea Bibi-arusi Wake. Tutakuwa na wakati ulioje katika umilele sisi kwa sisi, na pamoja na Bwana wetu Yesu. Maneno ya kibinadamu hayawezi kueleza, Bwana, jinsi tunavyojisikia mioyoni mwetu.

Kama ungependa kumsikia Yeye akikuita Bibi-arusi Wake, na kukuambia jinsi gani itakavyokuwa pamoja Naye, njoo uungane nasi Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni Saa 2:00 MBILI USIKU ya Afrika Mashariki), nawe utabarikiwa kupita kipimo.

Ndugu. Joseph Branham

60-1211M Wale Wanawali Kumi, Na Wayahudi Mia Na Arobaini na Nne Elfu

24-1124 Wakati Wa Kanisa La Filadelfia

UJUMBE: 60-1210 Wakati Wa Kanisa La Filadelfia

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bi Yesu Kristo,

Je! Jumapili hii itashikilia kitu gani kwa ajili ya Bibi-arusi wa Yesu Kristo? Ni yapi yote Roho Mtakatifu atakayotufunulia? Utimilifu Mkamilifu. Sasa tutafahamu kikamilifu kwa Ufunuo, kitu chenyewe ukilinganisha na mfano wake na kitu chenyewe na kivuli chake. Yesu ndiye mkate wa kweli wa Uzima. Yeye ndiye wote wa Hilo. Yeye ni Mungu Mmoja. Yeye ni Waebrania 13:8. Yeye ndiye MIMI NIKO.

Kristo, akiisha kutokea katika mwili na kumwaga Damu Yake mwenyewe, ameziondoa dhambi zetu mara moja na kwa yote kwa toleo la nafsi Yake; kwa hiyo sasa ametufanya sisi kuwa WAKAMILIFU. Uhai Wake mwenyewe umo ndani yetu. Damu Yake imetusafisha. Roho Wake hutujaza. Mapigo Yake TAYARI yametuponya. Neno Lake liko ndani ya mioyo na mdomo wetu. Ni Kristo katika maisha yetu na si kitu kingine chochote, kwani kila kitu maishani mwetu hufifia na kuwa duni, isipokuwa Yeye na Neno Lake.

Mioyo yetu itajawa na furaha anapotuambia kwamba kwa uamuzi wa kiungu, Yeye alijua ni nani hasa angalikuwa Bibi-arusi Wake. Jinsi alivyotuchagua. Yeye alituita. Alitufia sisi. Alitununua na sisi ni mali Yake, na ni Wake peke Yake. Yeye hunena, nasi tunatii, kwa maana hiyo ndiyo furaha yetu. Sisi ni mali Yake peke Yake Naye hana mwingine ila SISI. Yeye ni Mfalme wetu wa Wafalme nasi ni ufalme Wake. Sisi ni mali Yake ya milele.

Yeye atatutia nguvu na kutuangazia kwa Neno la Sauti Yake. Ataeleza waziwazi na kufunua kuwa Yeye ndiye Mlango wa kondoo. Yeye ni Alfa na Omega. Yeye ni Baba, Yeye ni Mwana, na Yeye ni Roho Mtakatifu. Yeye ni Mmoja, nasi tu Mmoja na Naye na ndani Yake.

Yeye atatufundisha subira, kama alivyomfundisha Ibrahimu, kwa kueleza jinsi tunavyopaswa kungojea kwa subira na kuvumilia ikiwa tunataka kupata ahadi yoyote.

Yeye atatuonyesha waziwazi siku hasa tunayoishi. Jinsi zile pilikapilika za ekumeni zitakavyopata nguvu kisiasa, na kuishurutisha serikali kuwafanya wote waungane nao aidha moja kwa moja ama kwa kufuata kanuni zilizofanywa sheria hivi kwamba hakuna watu watakaotambuliwa kama makanisa isipokuwa chini ya uongozi wa moja kwa moja ama usio wa moja kwa moja wa halmashauri yao.

Yeye atafunua jinsi gani wengi sana watakubaliana nao, wakidhani wanamtumikia Mungu katika utaratibu uliowekwa wa shirika. Bali Yeye anatuambia sisi, “Msiogope, kwa maana Bibi-arusi hatadanganywa, sisi tutadumu na Neno Lake, Sauti Yake.”

Litakuwa jambo lakutia moyo jinsi gani kumsikia Yeye akituambia: “Shika sana, vumilia. Usife moyo, bali vaa silaha zote za Mungu, kila silaha, kila karama niliyokupa iko mikononi mwetu. Usivunjike moyo kamwe kipenzi, endelea tu kuangalia mbele kwa furaha kwa sababu utatiwa taji na Mimi, Mfalme wako wa Wafalme na Bwana wa Mabwana, Mumeo.”

Ninyi ndio kanisa Langu la kweli; hekalu halisi la Mungu kwa Roho Wangu Mtakatifu aishiye ndani yenu. Mtakuwa nguzo katika hilo hekalu jipya; ule msingi utakaoshikilia sehemu ya juu. Nitawaweka kama washindi pamoja na mitume na manabii, kwa maana Nimewapa Ufunuo wa Neno Langu, wa Mimi Mwenyewe.

Yeye atatufunulia waziwazi kwamba majina yetu yaliandikwa katika Kitabu Chake cha Uzima cha Mwana-Kondoo kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu. Kwa hiyo tutakuwa mbele ya kiti Chake cha enzi usiku na mchana kumtumikia hekaluni Mwake. Sisi tuko chini ya ulinzi maalum wa Bwana; sisi ni Bibi-arusi Wake.

Tutakuwa na jina jipya kwa kulichukua jina Lake. Litakuwa ndilo jina tulilopewa sisi wakati anapotuchukua Kwake. Tutakuwa Bi Yesu Kristo Wake.

Yerusalemu mpya ukishuka kutoka mbinguni kwa Mungu, Bibi-arusi aliyekwisha kupambwa kwa Mumewe. Mauti haitakuwapo tena, huzuni, wala kilio. Wala maumivu hayatakuwapo tena kwa kuwa mambo ya kwanza yamekwisha kupita. Ahadi zote nzuri za Mungu zitatimizwa. Badiliko litakamilika. Mwana-Kondoo na Bibi-arusi Wake watakaa milele katika ukamilifu wote wa Mungu.

Mpendwa Bi Yesu Kristo, OTA JUU YAKE. Itakuwa nzuri zaidi kuliko vile unavyoweza kuwazia.

Ninamwalika kila mtu aje kuungana nasi Jumapili hii saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,( saa 2:00 MBILI USIKU ya Afrika Mashariki ) wakati Mume wetu, Yesu Kristo, anenapo kupitia malaika-mjumbe Wake wa saba mwenye nguvu na kutuambia mambo haya yote.

Ndugu. Joseph Branham

Ujumbe: Wakati Wa Kanisa la Filadelfia 60-1210

24-1117 Wakati Wa Kanisa La Sardi

UJUMBE: 60-1209 Wakati Wa Kanisa La Sardi

PDF

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Watu Wa Kanda,

Tunajivunia jinsi gani kuitwa “Watu wa Kanda”. Mioyo yetu inaenda mbio kwa changamko kila wiki tukijua tutaungana pamoja ulimwenguni kote kwa kuisikia Sauti ya Mungu ikisema nasi.

Tunajua, bila chembe ya shaka hata moja, tuko katika Mapenzi makamilifu ya Mungu kwa sisi kukaa na Neno Lake; kuisikiliza Sauti Yake kwa njia ya malaika-mjumbe Wake wa saba mwenye nguvu.

Mjumbe Aliyemchagua kwa ajili ya siku yetu ni William Marrion Branham. Yeye ndiye taa ya Mungu kwa ulimwengu, inayoakisi nuru ya Mungu. Yeye anamwita Bibi-arusi Neno Safi Wake aliyechaguliwa atoke kupitia malaika Wake.

Kwa kujifunza kwa makini Neno Lake, Ametufunulia sisi kwa Roho Wake Mtakatifu kwamba William Marrion Branham ndiye malaika ambaye Yeye aliyemchagua kumpa Ufunuo Wake na Huduma Yake kwa ajili ya siku yetu. Tunamwona malaika Wake, NYOTA YETU, katika mkono Wake wa kuume huku akimpa nguvu Zake za kufunua Neno Lake na kumwita Bibi-arusi Wake atoke.

Yeye ametupa Ufunuo mzima wa Yeye Mwenyewe. Roho Mtakatifu akijitambulisha kwetu kupitia maisha ya malaika-mjumbe Wake wa saba; malaika aliyemchagua kuwa macho Yake kwa ajili ya siku yetu.

Jinsi gani mioyo yetu inavyowaka ndani yetu wakati anapotuambia kwa kila Ujumbe kwamba ni kusudi Lake kutuleta Kwake; ya kwamba sisi ni Bibi-arusi Neno Wake.

Yeye anapenda kutuambia mara kwa mara jinsi alivyotuchagua sisi kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu NDANI YAKE. Jinsi tulivyojulikana kimbele na kupendwa Naye.

Jinsi tunavyopenda kumsikia Yeye akinena na kutuambia tulikombolewa kwa Damu Yake na HATUWEZI kamwe kuja hukumuni. Hatuwezi kamwe kuwa katika hukumu, kwa sababu dhambi haiwezi kuhesabiwa kwetu sisi.

Jinsi tutakavyoketi pamoja Na Yeye wakati akichukua kiti chake cha enzi cha duniani cha Daudi, na kutawala pamoja Naye; kama tu Yeye alivyofanya mbinguni, pamoja na uwezo na mamlaka juu ya dunia nzima. Majaribu na majaribio ya maisha haya yataonekana kuwa si kitu wakati huo.

Lakini pia Yeye ametuonya jinsi gani tunavyopaswa kuwa waangalifu. Kwamba katika nyakati zote ile mizabibu miwili ilikua pamoja. Jinsi ambavyo adui daima amekuwa akifanana sana; mdanganyifu sana. Hata Yuda alichaguliwa na Mungu, na kufundishwa katika kweli. Alishiriki maarifa ya zile siri. Alikuwa na huduma ya nguvu aliyopewa naye akawaponya wagonjwa na kutoa pepo katika Jina la Yesu. Lakini yeye hakuweza kwenda hadi mwisho.

Huwezi kuendelea na sehemu tu ya Neno, huna budi kuchukua Neno LOTE. Kuna watu wanaoonekana wanahusika na mambo ya Mungu karibu asilimia mia moja, lakini sio.

Yeye alisema wala haitoshi kwamba Yeye amejihusisha na kanisa zima, ama hata na huduma tano ya Waefeso nne. Yeye alituonya kwamba katika kila wakati kanisa hupotoka, na wala si wafuasi tu bali na kundi la makasisi – wachungaji wako makosani na kondoo pia.

Kwa hiyo kwa shauri lililokusudiwa la mapenzi Yake Mwenyewe, Yeye amejitokeza Mwenyewe katika wakati wetu kama Mchungaji Mkuu katika huduma ya malaika-mjumbe Wake wa saba kuwaongoza watu Wake wairudie ile kweli na zile nguvu nyingi za kweli hiyo.

Yeye yuko ndani ya mjumbe Wake na yeye ambaye angekuwa na utimilifu wa Mungu angemfuata huyo mjumbe kama vile huyo mjumbe alivyo mfuasi wa Bwana kwa Neno Lake.

Ninataka kuwa na utimilifu wa Mungu na kumfuata mjumbe Wake. Hivyo, kwetu sisi, Maskani ya Branham, njia pekee ya kumfuata mjumbe kama vile yeye anavyomfuata Bwana kwa Neno Lake, ni KUBONYEZA PLAY na kuisikia Sauti ya Mungu Safi ikisema nasi maneno ya kutoweza kukosea.

Haitubidi kukisia au kukagua kile tunachosikia, inatubidi tu Kubonyeza Play na kuamini kila Neno tunalosikia.

Nilimsikia Ndugu Branham akisema maneno yafuatayo mapema asubuhi moja kwenye redio ya Sauti. Nilipolisikia Hilo, ikanijia moyoni mwangu kwamba hivi ndivyo Mimi / sisi tunavyojisikia kuhusu kusema:

TUNABONYEZA PLAY TU NA KUZISIKILIZA KANDA.

Ilisikika kama tamshi la Imani yetu kwangu mimi.

Hiyo ndiyo sababu ninaamini katika uponyaji wa Kiungu. Hiyo ndiyo sababu ninaamini katika maono. Hiyo ndiyo sababu ninaamini katika Malaika. Hiyo ndiyo sababu ninaamini Ujumbe huu, ni kwa sababu unatoka kwenye Neno la Mungu. Na chochote nje ya Neno la Mungu, sikiamini. Inaweza kuwa hivyo, lakini hata hivyo nitadumu tu na yale Mungu aliyosema, ndipo niwe na hakika kwamba niko sahihi. Sasa, Mungu anaweza kufanya atakalo. Yeye ni Mungu. Lakini maadamu ninadumu na Neno Lake, basi ninajua hilo ni sawa. Ninaamini hilo.

Utukufu, yeye alilisema KAMILIFU kweli. Huduma zingine zote zinaweza kuwa, kwa sababu Mungu anaweza kufanya atakalo, na yule Yeye anayemtaka kulifanya, Yeye ni Mungu. Lakini maadamu ninadumu na Neno Lake, Sauti Yake, Kanda, basi ninajua hilo ni sawa. Ninaamini hilo.

Ninajua wengi huzisoma barua zangu na kutoelewa kile Mimi ninachosema na kile ninachoamini kuwa ni Mapenzi ya Bwana kwa kanisa letu. Nami niseme tena kwa unyenyekevu kama vile nabii alivyosema: “Barua hizi zimekusudiwa kwa ajili ya kanisa langu peke yake. Wale wanaotamani kuiita Maskani ya Branham kanisa lao. Wale WANAOTAKA KUTAMBULISHWA NA KUITWA WATU WA KANDA”.

Ikiwa hukubaliani na yale ninayosema na ninayoamini, hiyo ni sawa asilimia 100% ndugu zangu na dada zangu. Barua zangu si kwa ajili yenu au dhidi yenu au kwa makanisa yenu. Kanisa lako linajitawala lenyewe nawe ni lazima ufanye kama vile unavyohisi kuongozwa kufanya, bali kulingana na Neno, ndivyo lilivyo na letu, na hiki ndicho sisi tunachoamini kuwa ndio njia iliyoandaliwa na Mungu kwa ajili yetu.

Wote mnakaribishwa kuungana nasi kila Jumapili saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville.( Ni Saa 2:00 MBILI USIKU ya Afrika Mashariki ) Wiki hii, Nyota ya Mungu ya wakati wetu, William Marrion Branham, atakuwa akituletea Ujumbe, 60-1209 Wakati wa Kanisa la Sardi.

Ndugu. Joseph Branham