22-0313 Maswali Na Majibu Juu Ya Mihuri

Ujume: 63-0324M Maswali Na Majibu Juu Ya Mihuri

PDF

pakua

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi aliyepumzika,

Leo hii dunia inasoma vichwa vya habari kusikia yaliyojiri duniani jana: Hofu, wasiwasi, Makombora, Mabomu ya Nyuklia, maangamizi , Uongo, Udanganyifu, Siasa, Mauti.

Lakini Bibi-arusi wana Bonyeza Play, na kusikia Sauti ya Mungu ikinena nao na kusema: Nguo ndefu Nyeupe, Kuhesabiwa haki, Kuchaguliwa tangu awali, changamko, Ufunuo, Kweli, Kunyakuliwa, Uzima wa Milele.

Usiogope ewe kipenzi, Mimi niko pamoja nawe, kila sekunde ya kila siku. Huu ndio mpango Wangu mkuu wote ambao Nimewaambia yote kuuhusu. Sasa, utazameni wote ukiwekwa wazi mbele ya macho yenu.

Wao : Hizi ni siku mbaya zaidi za maisha yetu; kila kitu kinaweza kufikia mwisho kesho.

Sisi : Hizi ndizo siku kuu za maisha yetu; kila kitu kinaweza kufikia mwisho kesho.

Mungu ana njia iliyoandaliwa, NENO LAKE. Yeye Alimtuma malaika-nabii wake pamoja na Neno Lake kumwita Bibi-arusi Wake atoke na kuwaongoza kwenye Makao yao Mapya aliyowaandalia.

Ikiwa ungependa faraja , amani, na uhakikisho huu huu tulionao; kama ungependa kuja kuishi katika Makao hayo ambayo yeye amemwandalia Bibi-arusi Wake; njoo uungane nasi Jumapili saa 6:00 Sita Mchana, saa za Jeffersonville, ( ni saa 2:00 mbili Usiku ya Tanzania), kusikia Njia pekee ya Mungu iliyoandaliwa kwa ajili ya siku hii, na kusikiliza sauti Yake iliyothibitishwa ikinguruma kwetu : Maswali Na Majibu juu ya Mihuri 63-0324M.

Muhtasari mdogo wa vichwa vya habari utakavyosikia Jumapili.

Ni kitu gani kitakachomuunganisha Bibi-arusi: Neno .

Neno humjia nani: Nabii .

Nani Aliye mfasiri wa kiungu wa Neno hilo: Nabii .

Sauti ya Mungu kwako ni nani: Nabii .

Tutahukumiwa kwa Maneno ya nani: Neno la Mungu lililonenwa na: NABII .

Ndugu. Joseph Branham