23-0903 Maswali Na Majibu Juu Ya Mihuri

UJUME: 63-0324M Maswali Na Majibu Juu Ya Mihuri

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Ndugu Branham,

Ninaamini kwa moyo wangu wote wewe ndiye malaika-mjumbe wa Saba wa Mungu aliyetumwa kumwita Bibi-arusi Wake atoke. Wewe ni Sauti ya Mungu uliye na Bwana Asema Hivi kwa ulimwengu. Ninaamini wewe ndiye yule aliyemchagua kumfunulia siri zote za Biblia. Ninaamini kila Neno unalosema kwenye hizo kanda.

Nina swali moyoni mwangu ambalo ningependa kukuuliza. Kuna watu wengi sana, sauti nyingi sana, zinazosema mambo mengi tofauti kuhusu kile tunachopaswa kufanya ili kuwa Bibi-arusi wa Kristo. Ninataka kuwa katika Mapenzi yake makamilifu. Nataka kuwa na Imani kamilifu. Simpingi mtu yeyote, lakini nataka kusikia wewe unasemaje.

Ni kitu gani kitakachomkusanya Bibi-arusi pamoja na kutupa Imani ya kunyakuliwa tunayohitaji?

Nami naamini ya kwamba, kupitia Ngurumo hizo Saba, zitafunuliwa katika siku za mwisho ili kumkusanya Bibi-arusi pamoja kwa ajili ya kupata imani ya kunyakuliwa.

Ndugu Branham, Je, zile Ngurumo Saba ambazo ni sawa na siri saba zimekwisha kufunuliwa? Je, zilifunuliwa katika zile Muhuri Saba, ila bado hazijajulikana kwetu kama zile Ngurumo?

La, zilifunuliwa katika zile Muhuri Saba; hivyo ndivyo zile ngurumo zilivyokuwa. Ilibidi zifunue…Zile Ngurumo Saba zilizotoa sauti zao na hakuna ye yote angetambua ilikuwa nini…Yohana alijua zilikuwa nini, lakini yeye alikatazwa kuandika habari zake. Yeye alisema, “Bali yule malaika wa saba, katika siku za kupiga baragumu yake, zile siri saba za zile Ngurumo Saba zitafunuliwa.” Na yule malaika wa saba ndiye mjumbe wa ule Wakati wa Saba wa Kanisa.

Utukufu kwa Mungu. Hilo hapo jibu langu. Siri ya zile Ngurumo Saba imefunuliwa. Ni Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda na sasa inamuunganisha Bibi-arusi pamoja na kutupa ile IMANI YA KUNYAKULIWA, tunayohitaji.

Asante, Ndugu Branham, kwa kujibu swali langu. Nilijua kuwa jibu la swali nililokuwa nalo moyoni mwangu lingekuwa kwenye kanda.

Hayo ndiyo yote ninayohitaji kujua. Nitaendelea Kubonyeza Play kila siku na kupokea IMANI YA KUNYAKULIWA zaidi.

Njoo upokee Imani ya Kunyakuliwa pamoja nasi Jumapili hii saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville, ( ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki ) tunaposikia: Maswali na Majibu Juu ya Mihuri. 63-0324M.

Ndugu. Joseph Branham