23-0326 Muungano Usioonekana Wa Bibi-Arusi Wa Kristo

Ujume: 65-1125 Muungano Usioonekana Wa Bibi-Arusi Wa Kristo

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi Mteule,

Ungetoa nini ili Bwana Yesu aje kuingia nyumbani mwako Jumapili hii, aketi kwenye kochi lako, akuangalie machoni na anene nawe moja kwa moja?

Husingeweza kuzungumza. Usingependa kuzungumza. Yote ungalitaka kufanya ni kumwangalia yeye tu na kulia. Ungeogopa hata kufungua mdomo wako. Ungeweza kusema nini? Katika mawazo yako ungekuwa unawazia, Bwana, sistahili kabisa kwako Wewe kuwa hapa nyumbani mwangu. Mimi ni wa chini kabisa kuliko walio chini. Nimekukosea mara nyingi sana Bwana, lakini Bwana, nakupenda sana.

Ndipo ungetambua moyoni mwako, Anajua kabisa yale ninayowazia, hakuna kitu kilichofichwa Kwake. Anazijua kabisa siri za moyo wangu.

Unapotazama katika Macho Yake ya thamani, ungeona huo upendo na huruma. Angeweza kuzungumza nawe bila hata kufungua kinywa chake. Ungekuwa ukiwazia, Yeye yuko hapa, nyumbani mwangu, pamoja nami.

Moyo wako ungeanza kwenda mbio hata zaidi, ulipoona Akiwa karibu kutamka kitu fulani kwako. Mara moja, ile Sauti tamu sana ambayo hujawahi kuisikia ingesema, “ mpendwa, kipenzi changu ,usihofu, jina lako limo kwenye Kitabu changu cha Uzima cha Mwana-Kondoo. Si kitabu cha zamani cha ndoa yako ya kawaida, bali Kitabu Changu kipya cha Bibi-arusi. Ni cheti chako cha ndoa na Mimi.

Kipenzi, si kwamba tu umesamehewa dhambi zako zote na kushindwa kwako, Bali kwangu mimi , UMEHESABIWA HAKI. Machoni mwangu, hujawahi kufanya lolote baya.

Wewe ni mwana na binti yangu wa thamani, mwadilifu, asiye na dhambi. Unasimama bila doa; Bibi-arusi Wangu asiyeghoshiwa ambaye ameoshwa kwa Maji ya Damu Yangu Mwenyewe.

Kabla hata hakujakuwa na mwezi, nyota, au molekuli, ulikuwa mwana na binti yangu. Wewe ni onyesho la kimwili la sifa zilizokuwa ndani Yangu hapo mwanzo.

Jeni yako ya kiroho ilikuwa ndani Yangu kwa sababu wewe ni dhihirisho la sifa Zangu, mawazo Yangu. Ulikuwa ndani Yangu hata kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu.

Wewe ni Bibi-arusi Wangu wa kiroho ambaye umekuwa ukikaa katika Uwepo wa Mwana, kuivishwa, kwa kusikiliza Neno Langu. Sasa umeanza kuwa na uamsho, kurudi na kujiweka sawa na Neno Langu. Wewe ni Bibi-arusi wangu, bibi-Mteule.

Sasa mnao muungano wa kiroho pamoja nami. Mwili wako unakuwa Neno, na Neno linafanyika mwili; likidhihirishwa na kuthibitishwa. Vile vile hasa nilivyowaambia ingetendeka katika siku hii, inatendeka, siku baada ya siku. Neno likifanyika Neno.

Mnao Ufunuo wa kweli wa siku hii ya mwisho: kukusanyika pamoja kwa Bibi-arusi Wangu kwa Ujumbe Huu. Hakuna wakati mwingine niliouahidi hilo. Niliwaahidi ninyi jambo Hilo, katika wakati huu: Malaki 4, Luka 17:30, Yohana Mtakatifu 14:12, Yoeli 2:38.

Tutakuwa na Sikukuu ya Kutoa shukrani Jumapili hii nitakapowaeleza hata na zaidi. Nitatumia muda mwingi, nikishiriki na kusherehekea Neno Langu pamoja nanyi. Nitawahakikishieni tena kwamba kwa kukaa na Neno Langu, nabii Wangu, Sauti Yangu, Kubonyeza Play, mko katika Mapenzi Yangu makamilifu .

Niliwaambia wao katika Neno Langu, Nasimama mlangoni, nabisha. Mtu yeyote akiisikia SAUTI yangu, na akaufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami. Wengi hawatasikiliza na kufungua mlango wao, lakini kwa Ufunuo, ninyi mmefungua mlango wenu na kunikaribisha ndani.

Hawakubaliani na kuicheza Sauti Yangu katika makanisa yao. Iwapo wangemwacha tu Roho Mtakatifu achunguze nia zao kwa Neno, wangekubali. Mwache Kristo, Neno lililotiwa mafuta, achunguze dhamiri yako mwenyewe. Mwache yeye aingie ndani yako, uone kama Hiyo ni kweli ama sivyo.

Niliwaambia halitakuwa dhehebu litakalowakusanya pamoja, wao hawawezi kukubaliana kwenye Neno moja au mawili katika Biblia. Je! Niliwahi kamwe kuwaambia litakuwa kundi la watu? Hapana! Niliwaambia ulikuwa ni Ujumbe wa Mtu MMOJA; na mkasikiliza na kutii.

Kwa sababu hawakusikiliza na kukubali mpango wangu wa asili tangu mwanzo, Nikawatumia wahubiri, waalimu, mitume, wachungaji na manabii. Lakini walitumwa kuwaelekeza watu KURUDI kwenye Mpango wangu wa asili na mkamilifu, Malaika Wangu mwenye nguvu. Kwa maana ni Sauti ya Mungu kwenu.

Wametiwa mafuta, lakini MIMI nina NABII-MJUMBE MMOJA WA KUWAONGOZA NINYI. ROHO MTAKATIFU ​​NDIYE NABII. Je, sijawaambia mara nyingi, NENO LANGU LILILONENWA KUPITIA KWAKE HILO HALIHITAJI KUFASIRIWA, USIONGEZE KWALO AU KUONDOA CHOCHOTE ALICHOSEMA, SEMA TU YALE ALIYOSEMA KWENYE HIZO KANDA ? Huyo ndiye nabii, Roho Mtakatifu anayewaongoza.

Yeye ndiye niliyemtuma kuwaita muwe Bibi-arusi Wangu. Yeye ndiye wa kuwatambulisha ninyi Kwangu. Yeye ndiye niliyesimama naye nilipomwonyesha kukaguliwa kwenu kimbele, Bibi-arusi Wangu. Niliwaambia yote kumhusu yeye katika Ufunuo niliposema, MIMI Yesu nimemtuma MALAIKA WANGU kuwashuhudia ninyi mambo haya KATIKA MAKANISA. Ni MIMI, natumia tu mwili wake na sauti yake kuzungumza nanyi.”

Ni siku ya ajabu jinsi gani tunayo kuwa nayo pamoja Naye. Hatujawahi kuwa wenye furaha au kuridhika zaidi hivi maishaini mwetu. Hii ndio YENYEWE . Hili ndilo tumekuwa tukingojea maisha yetu yote.

Hakuna kivuli cha shaka katika mioyo yetu ama akili zetu. Kwa maana kwa kila Ujumbe tunaosikia, anatuambia tuko katika Mapenzi yake makamilifu. Kuna Sauti moja tu itakayowaunganisha ninyi, kuwakamilisha, na kuwaleta pamoja…Mimi, MIMI NIKINENA KUPITIA NABII WANGU. SI MANENO YAKE, NI MANENO YANGU. NI NJIA YANGU ILIYOANDALIWA.

Meza imeandaliwa. Imejaa Makabeji, na matanipu, na mafigili…NENO JUU YA NENO, JUU YA NENO. Tutakuwa na Sikukuu ya Kutoa shukrani ambayo Haijawahi kutokea. Kutakuwa na yubile duniani kote wakati Bibi-arusi watakapokusanyika kandokando ya Meza zao ili kusikiliza Sauti ya Mungu ikinena nao. Nyumba zetu na makanisa yetu yatajazwa na uwepo wake. Tutaduwaa isipokuwa Utukufu, Haleluya zetu, jina la Bwana lihimidiwe.

Njoo uwe sehemu ya Kukusanyika huku kwa Familia ya Bibi-arusi kutoa Shukrani, anapotulisha. Usichelewe, kwani tutaanza kusherehekea Jumapili, saa 06:00 SITA kamili MCHANA , saa za Jeffersonville. ( ni Saa 1:00 MOJA kamili JIONI ya Tanzania na Kenya pia ) Kwa maana aliniambia angekuwepo.

NAKUJA na nitakuwa nikiwaambia yote kuhusu Muungano wenu Usioonekana wa Bibi-arusi wa Kristo 65-1125.

Nitawaoneni Pale Mezani.

Ndugu. Joseph Branham

AKA: Bibi Mteule Wake