All posts by admin5

21-1010 Matukio Yakidhihirishwa Na Unabii

UJUMBE: 65-0801e Matukio Yakidhihirishwa Na Unabii

PDF

pakua – m4a

pakua – amr 11MB (use Firefox to download)

BranhamTabernacle.org

Tai wanakusanyika Pamoja.

Mpendwa Kundi dogo Bibi-arusi Neno Bikira wa Kristo,

Sisi ni Bibi-arusi Neno wake tukisubiri Bwana harusi Neno wetu na fungate yake ya utawala wa miaka Elfu . Tutasikiliza Sauti moja tu . “Kondoo Wangu wanaijua Sauti Yangu. Mgeni Hawatamfuata. ” Sauti yake ni nini?

Sauti ya mtu ye yote ni neno lake. Nalo ndilo Hili, Biblia, neno moja lisiongezwe Kwake au kuondolewa Kwake. Dumuni waaminifu tu kwa Sauti hiyo. “Mgeni hawatamfuata,” madhehebu.

Sauti hiyo ni Sauti Yake, izungumzayo kwenye Kanda kupitia Mfasiri pekee wa Kiungu wa Neno Lake, nabii Wake, William Marrion Branham. Ni Yesu Kristo akinena kupitia midomo ya mwanadamu. Sisi Hatujali maneno ya mwanadamu, mawazo ya mwanadamu au Fasiri ya mwanadamu, Tunaijali tu Sauti iliyothibitishwa kwa ajili ya wakati wetu. Ni BWANA ASEMA HIVI.

Mungu aliiongoza mikono ya nabii wetu. Mungu aliyaongoza macho yake katika maono. Hakuweza kusema kitu chochote ila kile alichokuwa anaangalia. Asingeweza kunena kitu, Maana Mungu Alitawala kabisa ulimi wake, kidole chake, kila kiungo cha mwili wake kilikuwa katika utawala Mkamilifu wa Mungu. Si ajabu kwamba Biblia ilisema manabii Wake walikuwa miungu; walikuwa ni sehemu ya Mungu! Yeye Alikuwa ndiye Neno la Mungu lililodhihirishwa kwa ajili ya wakati wetu.

Biblia hii inatabiri, kwa unabii, ni siku gani tunayoishi, na wakati gani tunaoishi, na ni matukio ya namna gani yanayopaswa kutukia. Inatabiri jambo hilo kikamilifu kabisa, wala haijakosea hata kizazi kimoja, wakati wote. Hakuna hata wakati mmoja ambapo imekosea, wala haitakosea, kwa kuwa waliochaguliwa tangu zamani kuliona wataliona. Ni Neno Likiungana na Neno

Katika Kila wakati, watu wanamwachilia mtu aweke fasiri yao kwenye Neno hili, na inawafanya watu wasione matukio yaliyotukia. Jambo lile lile limefanyika kwa Mafarisayo na Masadukayo.

Waliwaambia watu, “Sisi tumetiwa mafuta na Mungu. Mnatuhitaji sisi kuwambieni kile Neno linachosema. Mnatuhitaji sisi tuwafasirie ninyi. ”

Kama ilivyokuwa katika siku hiyo ndivyo ilivyo leo hii. Upande wa kudanganya ni kwamba wamepakwa mafuta na Roho Mtakatifu. Wana wito kutoka kwa Mungu kufanya huduma ya Neno. Wapo kuwaambia watu kile nabii alichosema, lakini wengi wao huweka FASIRI YAO KWAKE kwa kufanya huduma yao kuwa muhimu zaidi kuliko Sauti ya Mungu.

Angalia jinsi wanavyotaka kujaribu kukusanya watu pamoja kwenye huduma yao, kwenye fasiri yao ya kile manabii wa Mungu walichosema, lakini hawawezi kufanya jambo hilo.

Wanaficha na kuwatisha watu ili kuhalalisha kutocheza kanda katika makanisa yao kwa kusema, “Hao watu wanaweka mkazo sana kwa mtu huyo na wanamwabudu yeye na sio Yesu Kristo. Ni udhehebu kusikiliza ujumbe sote kwa wakati mmoja kutoka sehemu moja. Ndugu Branham hakuwahi kusema chezeni kanda kanisani ”, hivyo kuepuka hasa sababu Yenyewe, hawataki tu kucheza kanda katika makanisa yao. Huduma yao, ufahamu wao, wito wao, ni muhimu zaidi kuliko kusikiliza kanda kanisani. Hawatathubutu kusema kuwa, HAPANA , lakini vitendo vyao vinawasemea.

Mhudumu yeyote wa kweli, anayedai kuamini huu ni Ujumbe wa kweli wa wakati wa mwisho, ni Sauti ya Mungu kwa ajili ya wakati wetu, hangekuwa kamwe na Udhuru wa kutocheza kanda katika kanisa lao. CHUNGUZA TAMSHI HILO PAMOJA NA BIBI-ARUSI NENO.

Sijawahi kusema ni lazima kila Mtu asikilize saa 8:00 nane mchana , saa za Jeffersonville, la sivyo wewe si Bibi-arusi, KAMWE. Sijawahi kumwabudu mtu . Ni Yesu Kristo ndiye anayepokea utukufu wote. Ninamwabudu Mungu aliye ndani ya huyo Mtu kama vile NENO lilivyotuambia tufanye. Jinsi gani walivyo wadanganyifu na vipofu . Soma tu Maandiko ndugu yangu, liko papo hapo.

Ibilisi ANAJUA kwamba mhudumu yeyote, au kundi la wahudumu, HAWAWEZI KAMWE kumuunganisha Bibi-arusi; Hata hawakubaliani wao kwa wao. Kama tu vile Wamethodisti, Wabaptisti, Wapresbyteri na Wapentekoste, anawezaje yeyote mmoja wao au mchanganyiko wao kumuunganisha Bibi-arusi… HAWAWEZI kabisa.

KITU PEKEE KINACHOWEZA KUMUUNGANISHA BIBI-ARUSI NI SAUTI YA MUNGU KWENYE KANDA .. ​​NA INAFANYA HIVYO !

Adui analichukia jambo hilo, kwa hivyo anajaribu kuliangamiza, lakini haitawezekana kufanya hivyo ….UTUKUFU!

Kama kawaida, wao daima, katika mwisho wa wakati, wameingia katika mchafuko kama huo kwa wanatheolojia wao na makasisi mpaka daima_ ni mchafuko. Daima fasiri yao ni mbaya, hakuna hata wakati mmoja imeshindwa kuwa mbaya. Wala hakuna hata wakati mmoja Neno la Mungu limeshindwa kuwa kweli. Hiyo ndiyo tofauti.

Kuna njia moja rahisi tu ya kuwa na hakika, Dumu na Neno, Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda. Soma Biblia yako, itakuambia ni matukio gani yatakayotokea katika siku hii. Itakuambia juu ya malaika Wake mwenye nguvu ambaye atakuja katika siku hii. Itakuambia kudumu na Sauti Hiyo, Kudumu na mjumbe Wake Aliyemchagua.

Ikiwa Shetani anachukia Kitabu chochote cha Biblia, ni kitabu cha Ufunuo. Kiliandikwa na Kristo mwenyewe. Halafu kulingana na roho hiyo, Kristo mwenyewe lazima aweke msisitizo mwingi kuhusu malaika wake wa 7.

Baada ya hayo naliona malaika mwingine akishuka kutoka mbinguni, mwenye Mamlaka kuu; na nchi ikaangazwa kwa utukufu wake.

Kristo Mwenyewe alisema dunia nzima iliangazwa kwa UTUKUFU WAKE. Yeye Hakusema iliangazwa kwa “Utukufu Wangu”. Halafu kulingana na uelewa wako, unamshtaki Kristo mwenyewe kwa yeye kuweka msisisitizo mwingi juu ya Mjumbe wake malaika wa 7.

Mjumbe huyo wa duniani alifanana sana na Kristo mwenyewe, Yohana alijaribu kumwabudu, MARA MBILI, lakini akasema, “HAPANA!, Mwabudu Mungu.” Hilo ndilo hasa tunalofanya, kumwabudu Mungu. Hatuwekei mkazo sana juu ya mtu huyo, tunasema tu kile KRISTO NENO ALICHOSEMA…. “Nchi ikaangazwa kwa utukufu wake”. Hilo Linatupa Changamko Kwa Ufunuo.

Mungu hujichagulia Mwenyewe, kwa kuchagua tangu zamani, akawachagua manabii kwa ajili ya kila wakati. Angalia jambo hilo. Yeye huweka tabia ya huyo nabii ipate kulingana na wakati huo. Mnaona, Yeye huweka mtindo wake, cho chote afanyacho. Yeye humweka kama ana elimu ama hana elimu. Yeye humwekea vipawa, namna atakavyohubiri, karama atakazokuwa nazo. Na Ujumbe wa wakati huo fulani, Mungu alichagua tangu zamani kitu hicho maalum kitendeke wala hakuna kitu kingine kinachoweza kuchukua mahali pake .

Cheza kanda, kanda yoyote , Jumapili, hakuna kinachoweza kuchukua mahali pake. Ikiwa unataka kuungana na Maskani ya Branham tunaposikiliza kanda, unakaribishwa na umealikwa kuungana nasi Jumapili saa 8:00 Nane mchana, saa za Jeffersonville,( ni saa 3:00 tatu Usiku ya Tanzania) tunaposikia: Matukio Yakidhihirishwa Na Unabii 65-0801E .

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko:

Mwanzo: 22: 17-18

Zaburi: 16:10 / Sura 22 yote/ 35:11 / 41: 9

Zekaria 11:12 / 13: 7

Isaya: 9: 6/40: 3-5 / 50: 6/53: 7-12

Malaki: 3: 1/sura ya 4 yote

Yohana Mtakatifu 15:26

Luka Mtakatifu : 17:30 / 24: 12-35

Warumi: 8: 5-13

Waebrania: 1: 1/13: 8

Ufunuo: 1: 1-3 / Sura ya 10 yote

21-1003 Mungu Wa Wakati Huu Mwovu

UJUMBE: 65-0801m Mungu Wa Wakati Huu Mwovu

PDF

pakua – m4a

pakua – amr 13MB (use Firefox to download)

Mpendwa Bibi-arusi Changamko kwa Ufunuo,

Ni nini kilikuwa kinatukia kote ulimwenguni wikendi hii iliyopita? Ni kitu gani kilikuwa kinatendeka? Vifijo hivyo vyote vilikuwa ni vya nini? Bibi-arusi kutoka kote ulimwenguni waliungana pamoja, na kutengeneza milima kwa plasta, udongo, mchanga na vijiti. WakiKukusanyika kwenye mioto iwakayo , kuimba nyimbo za ibada na kumsifu Bwana. Vijana kwa wazee wote namna moja, wakiwa wamevaa fulana sinazosema Changamko Kwa Ufunuo. Walikuwa kutoka Michigan hadi Florida, kutoka Maine hadi California, kutoka Amerika Kaskazini hadi Amerika Kusini, Ulaya, Afrika, Asia, Australia, kila kona ya dunia. Walikuwa wakisikiliza kwa kuunganishwa katika nyumba zao, wakisikia Sauti ya Mungu ikiwazungumzia moja kwa moja.

Nini kilichovutia? Uzao wa Mungu uliochaguliwa tangu awali ambao hauwezi kufanya vinginevyo isipokuwa kufuata Ujumbe wa wakati huu , ambao wanaamini kila Neno lililonenwa na kinywa cha Mungu, walikuwa wamekusanyika pamoja katika sifa, katika kuabudu, na katika kusherehekea tukio kuu lililotukia katika siku yetu juu ya Mlima Sunset.

Ilikuwa ni Mungu akithibitisha Neno Lake. Ndio maana ya kelele zote hizi . Angalia, ni Mungu akitimiza Neno Lake lililoahidiwa tena, la Ufunuo 10: 1 hadi 7, “Na katika siku za kutangazwa kwa Ujumbe wa malaika wa saba, siri ya Mungu itatimia .”

Ilikuwa ni Mungu akifanya historia. Ilikuwa ni Mungu akitimiza unabii. Lilikuwa jibu la unabii wa nabii. Na tulitamani kuwapo pale ili kupata na kusikia chochote ambacho Yeye alichofanya kupitia nabii Wake.

Tunapuuza ukosoaji wa Asiyeamini na waamini wa kujifanya. Hatuna hoja nao. Tuna jambo moja la kufanya, hilo ni kuamini na kupata kila sehemu yake tuwezayo. Tunakusanyika pamoja kila wiki kama wa moja kusikia Sauti ya Mungu, tunapongojea kuja kwa Masihi.

Ni Saa kuu jinsi gani tunayoishi. Kuona Maandiko yanatimizwa katika maisha yetu. Lakini Alituonya katika Neno Lake kwamba upako wa uwongo ungefanana sana, ungewapoteza KAMA Yamkini walio wateule wa Mungu. Lakini Mungu asifiwe, haitawezekana kumpoteza Bibi-arusi Wake, kwa maana wao watadumu na ile Sauti ya Mungu ya asili, iliyodhihirishwa, na iliyothibitishwa na hawatabadilisha nukta moja au yodi moja. Hawataongeza fasiri yao wenyewe Kwake, lakini kirahisi wataamini KILA NENO.

Tunapaswa kuwa waangalifu sana jinsi gani kama WATAFANANA SANA . Tunashangaa, je yatakuwa ni haya makanisa ya kimadhehebu? Wao Wanaonekana wako nje mbali sana na hata hawafanani. Basi Atakuwa ni nani?

Sasa, makanisa tu baridi, ya kawaida, magumu, na kadhalika, ya theolojia za kujitengenezea, hayo hayangeweza; walio Wateule wasingewajali. Lakini ni kule juu karibu sana na jambo lililo halisi. Kuacha tu Neno moja ndivyo tu unavyopaswa kufanya.

Alisema Hawa hakuondoka tu kirahisi akasema siamini Mungu.Yeye aliamini kosa. Shetani yeye alikubali hilo lilikuwa Neno la Mungu, lakini shida ilikuwa aliweka fasiri yake mwenyewe kwake na ilimfanya hawa aamini uwongo na alihukumiwa nao.

Jalada limeondolewa. Piramidi imefunguliwa. Maandiko yamefunuliwa. Ufunuo Amepewa Bibi-arusi. Ni Yesu Kristo yeye yule jana, leo na hata milele.

Hilo Linamfanya Shetani atukasirikie sana. Anajua amefikia mwisho wake. Yeye Anataka tujiulize sisi ni akina nani. Tunapitia mitihani na majaribu magumu kuliko tulivyowahi kupitia. Wakati mwingine tunajiuliza, kwa nini haya yote yanatutokea?

Sababu yake ni kwamba, ni kumjaribu Yeye, Bibi-arusi Wake. Ni ku-…Wakati amedhihirishwa, akajaribiwa, kuthibitishwa, akathibitishwa kwa Shetani

Utukufu !!! Majaribu na mitihani yetu ni Yeye tu akimthibitishia Shetani SISI NDIYE BIBI-ARUSI WAKE ALIYETHIBITISHWA

Tunaona sasa, wakati huu mwovu ni kuthibitisha, kwa Shetani, Yeye si kama Hawa, ya kwamba Yeye si mwanamke wa namna hiyo. Naye atajaribiwa kwa Neno Lake , Bibi-arusi, kama bibi-arusi wa Adamu alivyojaribiwa kwa Neno. Na bibi-arusi wa Adamu aliamini kila sehemu ya Neno, lote, ila akachanganyikiwa kwenye ahadi moja .

Lakini hatutachanganyikiwa hata kwa Neno moja au kufuata mapokeo yao, Fasiri zao za Neno, tutadumu na NENO LA ASILI.

Kama tuna kinasasauti, tutakusanya kundi la watu pamoja, na tuicheze, na kusikiliza kwa makini, kama vile alivyotuambia tufanye!

Ni kama tu vile uhai wako wa kawaida na tabia inavyoridhiwa na kuzaliwa kwa asili kwa baba yako, ndivyo alivyo Roho wa Mungu, aliyechaguliwa tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu.

Tunashukrani jinsi gani kwamba Roho wa Mungu, kuzaliwa kwetu, kulichaguliwa kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu kuwa na Ufunuo wa Kweli wa Ujumbe Huu.

Unakaribishwa kuja kupata Changamko lile lile kwa ufunuo pamoja nasi Jumapili saa 8:00 nane mchana , saa za Jeffersonville , (ni saa 3:00 tatu Usiku ya Tanzania) tunaposikia: 65-0801M Mungu Wa Wakati Huu Mwovu.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma:

Mathayo Mtakatifu 24/27: 15-23

Luka Mtakatifu 17:30

Yohana Mtakatifu 1: 1 / 14:12

Matendo 10:49

1 Wakorintho 4: 1-5 / 14 sura yote

2 Wakorintho 4: 1-6

Wagalatia 1: 1-4

Waefeso 2: 1-2 / 4:30

2 Wathesalonike 2: 2-4 / 2:11

Waebrania sura ya 7

1 Yohana Sura ya 1 / 3:10 / 4: 4-5

Ufunuo 3:14 / 13: 4 / Sura ya 6-8 na 11-12 / 18: 1-5

Mithali 3: 5

Isaya 14: 12-14

21-0919 Watiwa Mafuta Katika Wakati Wa Mwisho

UJUMBE: 65-0725m Watiwa Mafuta Katika Wakati Wa Mwisho

PDF

pakua

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi Aliyeteuliwa,

Sababu ya Walioteuliwa, Yesu alisema, hawatadanganywa, ni kwa sababu wao ndio Neno hilo. Hawawezi kuwa kitu kingine. Hawawezi kusikia kitu kingine. Hawajui kitu kingine.

Hakuna kitu kikubwa maishani kuliko kujua kwamba Mungu alimchagua nabii Wake kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu kunena Maneno haya. Kisha, Aliruhusu Sauti Yake kurekodiwa, kwa hivyo sisi, Bibi-arusi Wake aliyechaguliwa kimbele , tunaweza kurejea nyuma na kusikia Sauti Yake ambayo iliyorekodiwa na kuhifadhiwa, kwa sababu alitaka tujue:

. Sisi ni Neno.
. Hatuwezi kudanganywa.
. Hatuwezi kuwa kitu kingine.
. Hatuwezi kusikia kitu kingine.
. Hatujui kitu kingine.

Yeye Alijua tungehitaji kutiwa moyo leo zaidi ya siku nyingine yoyote katika historia. Vita vingerindima zaidi ya hapo awali. Bibi-arusi wake angejaribiwa. Bali kama angeweza kumkumbusha Bibi-arusi wake wao ni akina nani, wangefurahi mioyoni mwao wakijua wao ndio Wapenzi Wake katika mapenzi Yake Makamilifu.

Chochote kile Shetani anachotutupia, lolote lile tunalopitia,
sasa tunajua, Yeye Anachagua Bibi-arusi, na sisi ndio Bibi-arusi huyo. Hatuonei haya Ufunuo wetu wa Neno. Hatutajaribu kamwe Kumtendea Mungu kazi Bila Mapenzi Yake. Kwetu sisi, ni Chakula cha Kiroho Kwa wakati Wake. Tunatambua kwamba kutakuwepo na Watiwa mafuta katika Wakati wa Mwisho, lakini sisi Tuta KAA NA NENO.

Ikiwa ungependa hakikisho lili hili, njoo uungane nasi Jumapili saa 8:00 nane mchana , saa za Jeffersonville, ( ni saa 3:00 tatu Usiku ya Tanzania) kusikia: 65-0725M Watiwa mafuta Katika Wakati wa Mwisho.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma :

Mathayo Mtakatifu 5: 44-45 / 7:21 / 24: 15-28

Luka Mtakatifu 17:30 / 18: 1-8

Yohana Mtakatifu 14:12

Waefeso 1: 5

2 Timotheo 3: 1-8

Waebrania 6: 1-8 / 11: 4

Ufunuo 10: 1-7 / 16: 13-14

Malaki 4: 5

I Wafalme 22: 1-28

Yeremia: Sura ya 27 yote na 28 yote

21-0912 Chakula cha Kiroho kwa Wakati Wake

UJUMBE: 65-0718e Chakula Cha Kiroho Kwa Wakati Wake

PDF

pakua

BranhamTabernacle.org

Tai wanakusanyika Pamoja.

Mpendwa Kondoo wa Zizi la kondoo wa Mungu,

Katika siku ambazo Bwana wetu Yesu alipokuwa hapa duniani katika mwili, wakosoaji na wasioamini walimwambia:

Hata Lini utatuhangaisha Nafsi Zetu? Kama wewe ndiwe Kristo, utuambie waziwazi.

Kwa mara nyingine, Atazungumza nasi waziwazi na kuwaambia wakosoaji Wake na Bibi-arusi Wake, “Mimi ni mtu anayetoka kwa Mungu, aliyetumwa kutoka kwa Mungu, aliyeteuliwa na Mungu, nikiwa na BWANA ASEMA HIVI ya Kweli . Nimekaa kwa muda mrefu sana katika uwepo wake , nitanena na wewe kama Mungu mwenyewe.

Nataka kusiwe na shaka, na kwako wewe kuamini, mimi ni mjumbe wa Mungu kwako. Ujumbe ambao mimi Ninaounena , na mjumbe, ni kitu kile kile . Sisi ni Mmoja na kitu kimoja. Alinituma kwako kuwakilisha BWANA ASEMA HIVI, Neno kwa Neno.

Kumbuka, Neno la Mungu linasema Yeye hatafanya neno lolote mpaka kwanza anifunulie mimi. Watu wanataka kuweka fasiri zao wenyewe kwa yale ninayosema, lakini Maneno ambayo ninayo Nena na wewe hayahitaji Fasiri yoyote. Wewe sema TU Yale ninayosema.

Nataka pia utambue kwamba Neno lile lile ninalokuambia, pia linaishi ndani yetu. Una mamlaka ya Mungu aliye hai ndani yako. Wewe ndiye Bibi-arusi Kanisa Lililo Hai.

Baada ya Mimi kuondoka, lakini kabla ya ukame kuanza, Mungu amekuandalia mahali pa siri pa kujificha kabla ya hukumu kuipiga dunia. Utakuwa pale unasubiri, unakula Chakula hiki kilichofichwa ambacho atakachokuachia. Utakuwa ukiishi juu ya wema na rehema za Ufunuo wa Yesu Kristo anavyojithibitisha kwako kila siku.

Kwenu ninyi , Kitakuwa Chakula cha Rohoni kwa wakati wake. kingewachefua wengine tumbo. Nitakuwa mnono sana kwao. Lakini kwa ajili yenu, Kondoo Wake, Utakuwa ni Mkate wa Uzima, Yesu Kristo yeye yule jana, leo, na hata milele.

Usisahau, nitakulisha “HUKO”; si mahali pengine, “HUKO”. Watu watakucheka na kusema wewe una kichaa, lakini kile wanachokiita kichaa na Upuuzi , Mungu ataita kikuu . “

Alituambia kwamba huduma kuu ambayo Mungu aliyompa ilikuwa vinafanana kabisa na wakati wa Eliya. Baada ya ukame kuwa unakaribia kwisha, yeye Alimwita atoke na kumpeleka kwenye NYUMBA ya mjane mpaka ukame ulipoisha.

Alisema mjane huyu hakuwa Ameshirikiana na wasioamini au kuchukua alama ya mnyama wakati wa ukame, kwa hiyo alimwita Eliya kumlisha huyu mjane . Alikuwa tayari kufa kwani alikuwa amebaki na keki moja ndogo, kitu kimoja kidogo yule mama alichokuwa anashikilia.

Eliya akamwita huyo mwanamke , “Nipe hicho mimi, kwanza. Kwa kuwa, BWANA ASEMA HIVI, lile pipa halitapunguka wala ile chupa haitaisha, hata siku ile Bwana Mungu atakapoleta mvua juu ya nchi.”

Ilimbidi kumweka Mungu kwanza . Ilimbidi kuamini na kushikilia kila Neno ambalo mjumbe huyo alilosema. Alijua kwamba mjumbe na Ujumbe wake walikuwa kitu kimoja. Maneno aliyomwambia yangetimia , kwa maana ilikuwa Bwana Asema Hivi.

Ndivyo ilivyo leo, ya kwamba Chakula cha Uzima ambacho watoto wanakula, kinafuata Ujumbe wa Mungu, kuwahifadhi katika wakati wa ukame.

Neno lilo hilo limekuja kwetu na liko ndani yetu na tunakula mambo ya siri ya Mungu ambayo ulimwengu umefichwa. Ametufunulia kwamba Ujumbe na mjumbe ni kitu kimoja. Chakula cha kiroho kiko tayari, na kiko katika wakati sasa.

Unakaribishwa kwenye SIKU SIKUU NYINGINE KWA AJILI YA BIBI-ARUSI . Tutatwaa chupa la Mafuta, na Litakuwa Limefurika tena . Kisha tutachota ndani ya pipa la unga, na litajaa tena mpaka juu. Tutaketi mahali pamoja katika ulimwengu wa Roho kutoka kote ulimwenguni, tukiwa tumefichwa mahali petu pa siri, tukiifurahia mana iliyofichwa wakati Mungu anapojithibitisha mwenyewe kwetu.

Njoo ukusanyike katika zizi la Kondoo pamoja nasi Jumapili saa 8:00 nane Mchana , saa za Jeffersonville, (ni saa 3:00 tatu Usiku ya Tanzania)
Tunaposikia Mjumbe wa Mungu akituletea Ujumbe wa Mungu: Chakula cha Kiroho Kwa Wakati Wake 65-0718E.

Sisi tukiwa na dola moja
na senti themanini za kujenga Maskani , watu wengi wa gereji tayari walikuwa wameamua itakuwa gereji yao. Lakini ingali ni zizi la kondoo kwa ajili ya Kondoo wa Mungu.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma

1 Wafalme 17: 1-7
Amosi 3: 7
Yoeli 2:28
Malaki 4: 4
Luka 17:30
Yohana Mtakatifu 14:12

21-0905 Kumtendea Mungu Kazi Bila Mapenzi Yake

UJUMBE: 65-0718m Kumtendea Mungu Kazi Bila Mapenzi Yake

PDF

pakua

BranhamTabernacle.org

Tai wanakusanyika Pamoja.

Mpendwa Kanisa la Sauti Ya Mungu,

Sisi ni Kanisa lake la Sauti Ya Mungu, kipenzi chake Bibiarusi_Neno, na tunangoja kwa hamu kusikia kile Baba atakachonena na kutufunulia Jumapili hii.

Tunayo Sauti ya Mungu iliyo hai kiganjani mwetu. Kwa mguso mmoja wa kidole chetu tunaweza kumsikia Mungu akinena kupitia midomo ya mwanadamu, Maneno ya uzima wa Milele. Kwa kidole kimoja Anasema nasi na kutufunulia siri zote zilizokuwa zimefichwa tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu.

Kwa kidole kimoja Anajibu swali lolote tulilo nalo mioyoni mwetu. Kwa kidole kimoja Anatuambia chochote tunachohitaji kujua. Kwa kidole kimoja tunaweza kusikia Sauti ya Mungu ikisema nasi na kutupa Imani ya Kunyakuliwa . Kwa kidole kimoja tunaweza kumsikia Mungu akinena na kutuambia, umeponywa.

Wakati adui anatuambia sisi sio Bibi-arusi wa Mungu, wewe ni uliyeshindwa tu, kwa kidole kimoja tunabonyeza Play na tunaweza kumsikia Baba akinena nasi na kutuhakikishia, “WEWE ni Bibi-arusi wangu mteule. Nilikuchagua kabla ya kuwekwa misingi ya Ulimwengu. ”

Tunaposhushwa Moyo na adui anatushambulia kutoka kila kona, kwa kidole chetu kimoja tunaweza kumsikia akisema nasi na kutamka tu, “Habari za asubuhi Marafiki,” na Amani ya Roho Mtakatifu inakijaza chumba.

Tunaposikia ADUI ANASEMA ninyi mnamfuata tu mtu na mnaweka mengi kumhusu , kwa kidole kimoja tu tunasikia Sauti ya Mungu ikituambia:

Yeye aliniambia ikiwa nitawafanya watu waniamini. Hilo linaonekana kuwa la ajabu mimi kusema hivi, “Unaniamini ?” Kasema, “Je! Haikubidi kumwamini Mungu ?” Unapaswa kuamini hilo. Yakubidi umwamini Mungu na umwamini Kristo, na umwamini Roho Mtakatifu. Halafu baada ya kuwaamini wote, Mungu anakutaka uniamini .

Wakati adui anajaribu kutuambia, “Si Maandiko na ni makosa kukusanyika kwa wakati fulani na kusikiliza tu kanda,” kwa kidole kimoja tu tunasikia Sauti ya Mungu ikituambia:

Na kwa kanisa hili, na kwenye kanda— watu wanaosikiza kanda , na watu katika sehemu zilizounganishwa kwa redio wanaosikiza nchini kote, nawatakeni msikilize hili kwa makini na msikose .

Wakati adui anaposema Ndugu Branham alisema kaa na Neno, sio kanda, kwa kidole kimoja tunasikia Sauti ya Mungu IKIPIGA KELELE kusema:

Nasema vivyo hivyo katika Jina la Yesu Kristo : Usiongeze kitu. Usiondoe—kuliwekea mawazo yako. Wewe sema tu yaliyosemwa katika kanda hizo. Tenda sawasawa kabisa na vile Bwana Mungu amekuamuru kutenda. Usiongezee Kwake!

Sauti hiyo hata hivyo inatueleza jinsi ya kulichunguza kwa Neno ili tusikosee.

Lazima zako tano ndizo hizo. Lazima iwe hivyo;

. Wakati Wake
. Majira Yake
. Mtu yule aliyemchagua
. Lazima ije kwa nabii
. Nabii yule lazima awe nabii aliyethibitishwa

Nabii wetu ni Yesu Kristo.

Neno lililothibitishwa la saa hii !
Neno lililothibitishwa la siku za Musa lilikuwa Yesu. Neno lililothibitishwa la siku za Isaya, Eliya, Yohana, wote, lilikuwa Yesu. Na Neno lililothibitishwa leo ni Yesu, yeye yule jana, leo na hata milele .

Kwa kidole kimoja tunaweza kubonyeza play na kumsikia Yesu Kristo mwenyewe akinena na kutufunulia:

. Huu ndiyo wakati ,
. Haya ndiyo Majira ,
. Huyu ndiye mtu niliyemchagua,
. Huyu ndiye nabii wangu,
. Nabii huyu amethibitishwa zaidi ya manabii Wangu wote wengine .

Leo, sio tu kwamba tuna yule Mungu wa Mbinguni anayetuzungumzia , lakini yeye yuko ndani yetu, anakaa, na anaishi Maisha yake kupitia sisi. Inapita ufahamu wetu.

Hebu na Tujiweke Tayari. Wakati umekaribia. Tunaona Maandiko yakitimizwa kila siku. Ujumbe unasomeka kama habari ya leo:

” Mshangao wa wakati huo, dhiki kati ya mataifa, matetemeko ya nchi mahali mahali, bahari ikivuma, na moyo wa mwanadamu ukikoma kwa hofu “

Hata maumbile yenyewe hutuambia leo, tunapoona mataifa yakivunjika, dunia ikididimia, maandiko kwenye ukuta.

Tunaona kanisa na hali lilimo. Twamuona Bibi-arusi na hali aliyomo. Nasi twajua kwa mambo ya asili kwamba Kanisa linajiweka tayari kuondoka.

UTUKUFU, tunajiandaa kuondoka. Kwa kidole kimoja tu unaweza kujifanya mwenyewe tayari. Ninakualika uungane nasi Jumapili saa 8:00 nane mchana , saa za Jeffersonville,(ni saa 3:00 tatu Usiku ya Tanzania) kusikia: Kumtendea Mungu Kazi Bila Mapenzi Yake 65-0718M.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma Kabla ya ibada :

Kumbukumbu la Torati 4: 1-4 / 4: 25-26
1 Mambo ya Nyakati 13
1 Mambo ya Nyakati 15:15
Zaburi 22
Marko Mtakatifu 7: 7
Yoeli 2:28
Amosi 3: 7
Malaki 3
Mathayo Mtakatifu11: 1-15
1 Wakorintho 13: 1

21-0829 Kuonea Haya

UJUMBE: 65-0711 Kuonea Haya

PDF

pakua

BranhamTabernacle.org

Tai wanakusanyika Pamoja.

Wapendwa Maskani ya Branham,

Tunashukuru sana alituteua Sisi Tangu Asili kuchagua kanisa linalofaa kuziingiza familia zetu.

kama nilikuwa ninachagua kanisa, ningalichagua kanisa la kweli, lenye mafundisho ya kimsingi, linaloamini Injili Yote, kanisa la Biblia, kama ningelikuwa nachagua moja kuwaingiza familia yangu.

Tunashukuru sana tunauambia ulimwengu mchungaji wetu ni Nani, na kwamba tunatenda tu kama yeye.

kama utachunguza tabia ya hilo kanisa, hebu mwangalie tu mchungaji kwa muda mfupi, na mara nyingi utaona ya kwamba kanisa hutenda kama mchungaji wake .

Tunashukuru sana haijalishi tuko wapi ulimwenguni, Yeye hukutana nasi .

Aliahidi kukutana nao popote wawili watatu wamekusanyika pamoja. Hakika. Hapo ndipo mwaminio wa kweli huweka matumaini yake, ni katika hilo Neno la Mungu linalodhihirishwa katika Kweli.

Tunashukuru sana tunamwamini Nabii Wake, na kila Neno lililonenwa.

Kama unaniamini mimi kuwa nabii wa Mungu, sikiliza yale niliyokwambia.

Je! Nabii wake alikuwa ahubiri nini?

Ujumbe mkamilifu , kurudi kwenye Neno ,

Alitumwa kwa kusudi gani?

“ Nenda ukamlete Bibi-arusi huyo!” Ndilo jukumu. Hiyo ndiyo sababu ya mimi kuwapo hapa. Hilo ndilo ninalojaribu kufanya , ni kumwita Bibi-arusi atoke .

Je! Vipi Ikiwa tutatoka nje ya Mstari?

Na hivyo ndivyo nilivyopaswa kufanya , kumweka Bibi-arusi huyo kwenye mstari, nimtafute mtu huyo.

Sasa Baba amemwekea Akiba nini Bibiarusi wake?

Ninarudi nyumbani, nifanye upya nadhiri zangu tena, na kuanza upya.” Kwa hiyo hilo ndilo tunalopanga kufanya, hiyo ndiyo sababu nipo hapa.

Bwana asifiwe, tunaanza lini ibada zetu za kufanya upya?

Halafu basi, Bwana akipenda, Jumapili ijayo asubuhi tutaanza ibada. Nanyi nyote mnisaidie, nasi tutaomba, kwa maana lilikuwa moyoni mwangu kujaribu…Wao walisema, “Vema, tungeenda Louisville ama tungeshuka twende huko New Albany.” Lakini mkutano huo ulipaswa kuwa ni wa Jeffersonville. Nitaenda Louisville na New Albany, katika nyakati tofauti, lakini huu unapaswa kuwa hapa Jeffersonville.

Tuko tayari Baba. Tai wako watakusanyika na kusikiliza. Ni kitu Gani kitakachotukia wakati huu?

“… Ninafikia mahali, ninahitaji imani zaidi.” Hiyo ndiyo sababu niko nyumbani sasa ni kupata ujazo m—mpya wa imani.

Bwana asifiwe, hilo ndilo tunalohitaji pia Baba, Ujazo Mpya wa IMANI.
Tunajua imani huja kwa kusikia, kusikia Neno lako, na Neno lako Linamjia Nabii.

Ujumbe huu, Nguvu za Mwenyezi Mungu , Zimeenea kote ulimwenguni , lakini wakati wa Kutengana unatukia sasa. Mungu anamwita Bibi-arusi, naye shetani analiita kanisa. Sisi ni sehemu ya Ujumbe huu, Neno Lake, Bibi-arusi Wake!

Tuna hakikisho na tunajua tunalozungumzia. Hatuonei haya kwamba tunaamini Ujumbe huu na Mjumbe Wake, kwa kuwa wao ni kitu kimoja. Hatu haya kusema: “Tunaamini kila Neno”. Hatuonei haya kusema: “Tunacheza kanda kanisani mwetu”. Hatuonei haya kusema: “Sisi ni Watu wa Kanda”.

Ni ngumu kwetu kuelewa kwamba mwamini yeyote, au mhudumu wa huduma tano, anayedai kuamini Ujumbe huu, na kusema Ndugu Branham ni Nabii na Mjumbe wa Mungu, Kisha Angeamini na kuwaambia watu kuwa ni makosa na sio kulingana na Neno kucheza hasa Sauti ya Mungu iliyothibitishwa katika kanisa Lao.

Na tuwe tayari, wakati ufaao na wakati usiofaa; karipia, kemea na … kwa uvumilivu wote na mafundisho. Kwa sababu utakuja wakati watakapoyakataa mafundisho yenye uzima ;

ila kwa kuzifuata nia zao wenyewe watajipatia pamoja waalimu makundi makundi ; kwa kuwa wana masikio ya utafiti ;

Nao watageuzwa … _
wasisikie yaliyo kweli ,…
watazigeukia hadithi za uongo .

Inapofikia Neno la Mungu Halisi, lisiloghoshiwa, lililothibitishwa na Mungu, Sauti ya Mungu iliyothibitishwa, Inaonekana kulitahayarisha hata kundi hilo lingine. Wana tahayari kwa jambo hilo nao wanaamini Kwamba kuwa Kanisa la Kanda ni kuwa kinyume cha Neno.

Bali kwetu sisi, Ni Halisi. Hatuonei haya. Wakati tulipopokea Ufunuo huo, kulikuwa na kitu ambacho kilitulia ndani yetu, na sasa hakuna kinachoweza kupachukua Mahali pake. Tunajivunia kuitwa Mmoja wao, Kanisa la Kanda, Kundi la Kanda, Watu wa Kanda.

Tunakualika uje kusikiliza pamoja na Maskani ya Branham kwenye huduma ya Kanda ya Mungu, Jumapili saa 8:00 Nane Mchana, saa za Jeffersonville,( Ni Saa 3:00 Usiku ya Tanzania) tunapokusanyika kwa matarajio makubwa; kuzifanya upya nadhiri zetu tena, na kuanza upya, kwa kusikia: Kuonea Haya 65-0711 .

Ndugu. Joseph Branham

Marko Mtakatifu 8: 34-38

21-0822 Kuchagua Bibi-Arusi

Ujumbe: 65-0429e Kuchagua Bibi-Arusi

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Tai wanakusanyika Pamoja.

Mpendwa Bibi-arusi aliyechaguliwa na Mungu,

Baba alimchagua Bibi-arusi Wake kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu. Alitaka Bibi-arusi atakayeonyesha tabia Yake. Alitaka Bibi-arusi ambaye angevutia usikivu Wake kwa kushika Neno Lake.

Bibi-arusi ambaye angejitolea sana Kwake na kwa Neno Lake lililoahidiwa, hata Nia ile ile iliyokuwa ndani Yake ingekuwa ndani yao. Wangekuwa mwili Wake uleule, mifupa ile ile, Roho yule yule, kila kitu kile kile, wamejengwa sawa sawa kabisa mpaka hao wawili wangekuwa Mmoja.

Alitaka kuunda tabia Yake hasa ndani yao, kwa maana Anatakiwa awe kama tu Yeye . Amengojea tangu alipoweka Adamu na Hawa wake wa kwanza duniani ili kumrejesha Bibi-arusi wake mkamilifu. Amekuwa akimfikiria sana, kumrudisha katika Dhihirisho lake kamilifu; kwa maana watakuwa Bibi-arusi _Neno Lililonenwa wake.

Alipomwona bibi-arusi, Alifurahi sana, Hatimaye alikuwa na Bibi-arusi ambaye hatapatana hata kwa Neno moja. Bibi-arusi ambaye hangetilia shaka hata moja wapo ya hilo , bali Atalichukua vile tu lilivyo. Wangeuambia ulimwengu Halihitaji Fasiri yo yote, kwa maana ni Sauti Safi Ya Mungu.

Alipokuwa akimwangalia Mke wake kipenzi mdogo mkamilifu , Alijisifia kwa ajili yake, Ilibidi tu amwonyeshe wazi. Kwa hivyo alimwita malaika wake wa 7 mwenye nguvu, ili aweze Kumkagua huyo bibi-arusi kimbele . Alimtaka amwone bibi-arusi, na amwonyeshe wazi, ili aweze kumwelezea huyo Bibi-arusi jinsi alivyo mzuri. Kwa hivyo angeweza kumtia moyo bibi-arusi na kumfanya atambue kwamba yeye Anamjua bibi-arusi ni nani.

Kwa hivyo Alimchukua malaika Wake na kumweka mahali pa juu ili aweze kumkagua bibiarusi kimbele. Alipotazama, Roho wa Mungu akamwambia kusema, “ Huyo hapo Bibi-arusi.” Akatazama, na akawaona NINYI pale. Moyo wake Ulifurahi.

Kila mmoja WENU alikuwa amevaa vazi la kitaifa la huko ambapo mnakotoka: Uswizi, Ujerumani, kote ulimwenguni, kila taifa. Nywele ndefu zilizotengenezwa vizuri huku nyuma, nguo zenye mikono mirefu, na sketi ndefu Nadhifu. NANYI mlikuwa Mkipiga Hatua Taratibu, ” Twendeni, Askari Wakristo, tukitembea kama waendao vitani.” Alipotazama, Tulianza kupiga hatua hata Angani; Tulikuwa Neno.

Asante Baba. Jinsi gani jambo hilo linavyotutia moyo mioyo yetu leo hii. Tunakupenda wewe na Neno lako kwa yote yaliyo ndani yetu. Tunaamini kila Neno. Ujumbe huu unatutoshea kama glavu mkononi.

Tunataka kuwa Bibi-arusi-Neno wako Mkamilifu. Hatujui njia nyingine ya kufanya jambo hilo ila kukaa na Neno lako, hii manna iliyohifadhiwa uliyomwachia Bibi-arusi wako ili ajifanye Mwenyewe tayari.

Tunaona wakati huo umekaribia. Ulimwengu unatetemeka chini yetu kwa Matetemeko ya ardhi. Malaika wako wapelelezi wote wanazunguka karibu . Ulimwengu umepinduliwa-juu-chini. Vita, mapigano, mauaji, virusi na magonjwa kila mahali. Adui anakasirika bila kukoma, anajaribu kumtesa Bibi-arusi Wako, lakini Mke wako kipenzi aliyechaguliwa yuko THABITI akishikilia Neno Lako.

Tusaidie Baba tusitoke nje ya hatua. Hebu na tukuangalie wewe na kushikilia Mkono Wako usiobadilika. Ongeza IMANI yetu, utupe kile tunachohitaji. Njoo uwe na Bibi-arusi wako Jumapili hii, saa 8:00 Nane mchana, saa za Jeffersonville,( ni saa 3:00 Tatu usiku ya Tanzania) tunapokusanyika kuizunguka Sauti Yako kwa ajili ya siku hii na kukusikia Ukinena: Kuchagua Bibi-arusi 65-0429E.

Haya ni Maombi yetu Baba:

Ee Mungu wa Mbinguni, hurumia ulimwengu wenye dhambi na watu wenye dhambi, Bwana, kama tulivyo usiku wa leo. Mungu, ninajaribu kusimama pengoni na kuomba rehema ya Kiungu, kwamba utalizungumzia kundi hili usiku wa leo na kumhamasisha Bibi-arusi Wako, Bwana, akapige hatua taratibu si kwa ishara za kanuni zozote za imani, bali kwa sauti ya Injili ya Bwana Yesu Kristo. Tujalie, Ee Mungu. Na ijulikane, usiku wa leo, ya kwamba Wewe ni Mungu, na Neno Lako ni Kweli. Huku, kwa uchaji, mbele ya macho ya watu hawa, tunawahamasisha Neno Lako.

Ndugu. Joseph Branham

Mwanzo 24: 12-14
Ufunuo 21: 9

21-0815 Ile Mbegu Haitarithi Pamoja na Kapi

Ujumbe: 65-0429b Ile Mbegu Haitarithi Pamoja na Kapi

PDF

pakua

BranhamTabernacle.org

Tai wanakusanyika Pamoja.

Mpendwa Mwili wa Mwili Wake,

Nina furaha sana kwamba Mungu habadilishi nia Yake kuhusu Neno Lake. Yeye ni yeye yule jana, leo na hata milele. Jinsi alivyofanya mambo tangu mwanzo, anafanya vile vile leo. Mungu, Mwenyewe, aliyejidhihirisha katika mwili wa mwanadamu, kwa Damu ya Yesu Kristo, kutakasa maisha ili Aweze kujiakisi mwenyewe kupitia huo .

Mjumbe wetu leo hii ​​ana Utambulisho wake wa Kimaandiko kati yetu. Ni Roho Mtakatifu, Mwenyewe, akijifasiria Mwenyewe. Hakuna haja ya kwenda kutoka kwa hili kwenda kwa Lile ili kupata ukweli au fasiri; Roho Mtakatifu amelipa Kanisa Lake Waefeso 4, yote katika mtu mmoja, nabii Wake aliyethibitishwa.

Mtume : Mtume maana yake ni “aliyetumwa,” au, “mmishenari.” Mimi ni mmishenari.

Nabii : Je! Unaniamini mimi kuwa nabii wa Mungu?

Mwinjilisti : “ Fanya kazi ya mhubiri wa injili. Timiliza huduma yako. Utakuja Wakati watakapoyakataa mafundisho Yenye uzima. “

Mchungaji : Mwaniita, “mchungaji wenu”; nanyi mwasema vema, kwa maana ndivyo nilivyo.

Mwalimu : Nataka kuzungumza juu ya Neno, ama kufundisha somo hili la shule ya Jumapili, juu ya Neno la Ile Ishara .

Ni sawa na = Ninajua ninyi, ndugu zetu, mnanitazama mimi kuwa Yakini kwa kile… maadamu ninamfuata Mungu, kama vile Paulo alivyosema katika Maandiko, “nifuateni mimi, kama mimi ninavyomfuata Kristo.”

Ujumbe huu ni Yakini yetu, hivyo tunamfuata yeye kama anavyomfuata Kristo.

Wala Sipuuzi kuwa kuna wengi ambao Mungu anawaita Waefeso 4 watu ambao wamewekwa na kuitwa na Mungu kutimiza ofisi hizi; kwa NEEMA YAKE, mimi ni mmoja wao. Lakini sisi ni wadogo, nabii malaika wa 7 wa Mungu ndiye MKUU.
Kwa wale ambao kote ulimwenguni huiita “Maskani ya Branham ” “kanisa Lao la nyumbani”: mchungaji wetu, huduma yetu iliyo hai, Yakini yetu, Waefeso 4 yetu yote ipo kwenye kanda. Tunaamini ni huduma ya asili ambayo alikuwa nayo wakati alipokuwa hapa duniani.

Ni amani iliyoje, pumziko jinsi gani, hatujawahi kuwa na wasiwasi au kumvuka kiongozi wetu au chujio letu wakati tunaposikia Neno. Ni Neno la Mungu lililohakikishwa na lililothibitishwa, mana safi kila tunapolisikia na tunachotakiwa kufanya ni kuketi chini na kufurahiya mioyo yetu ikiwaka ndani yetu anapozungumza nasi njiani.

Na wote alionipa Baba, watakuja. Kondoo wangu, hua Wangu, huisikia Sauti Yangu. Mgeni hawatamfuata.” Na Sauti ya Mungu ni nini? Ni Neno la Mungu. Sauti ya mtu ye yote ni nini ila ni neno lake? Ni Neno la Mungu; watalisikia Neno la Mungu .

Halafu bado kuna mengi ZAIDI kwa ajili ya Kanisa Lake. Sio tu kwamba tunatambua siku hii na mjumbe wake, Neno la siku hii, Bali furaha kuu ambayo mwanadamu aliyowahi kupewa hatimaye imetimia. SISI NI sehemu ya Roho Wake, sehemu ya Mwili wake; nyama ya nyama Yake, mfupa wa mfupa Wake; Neno la Neno Lake, Maisha ya Maisha yake, SISI NI Bibi-arusi wa Kristo!

Utukufu !! Lisifikiwe Jina la Bwana !! Haleluya !! Bibi-arusi Wake Amejitambua na Anajifanya Mwenyewe Tayari kwa Neno Lake.

Hivyo ndivyo kanisa linavyofanya siku hizi, kwa kuwa Yesu ni Neno Naye ni Bwana Arusi, na Bibi-arusi ni sehemu ya Bwana Arusi. Kwa hiyo Neno ambalo itapaswa litimizwe siku hii ni sehemu ile ile ya Neno lililotimizwa katika siku Zake, na ni Neno lile lile, tukio lile lile, Maisha yale yale .

Njoo upate uzoefu wa Neno lile lile, tukio lile lile, Maisha yaleyale Jumapili hii saa 8:00 Nane mchana, saa za Jeffersonville,( ni Saa 3:00 tatu usiku ya Tanzania) kusikia: Ile Mbegu Haitarithi Pamoja Na Kapi 65-0429B.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya Kusoma:

Mathayo 1: 18-20 / 24:24
Luka 17:30
Yohana mtakatifu 5:24
Wagalatia 4: 27-31
Mwanzo 2:15
Isaya 9: 6
Malaki 4

21-0808 Je! Mungu Hubadilisha Nia Yake?

Ujumbe: 65-0427 Je! Mungu Hubadilisha Nia Yake?

PDF

pakua

BranhamTabernacle.org

Tai wanakusanyika Pamoja.

Mpendwa Bibi_arusi wa Mapenzi Makamilifu,

Ee Mungu mpendwa, hatutaki mapenzi Yako ya kuruhusia, Baba. Jalia tutembee katika mapenzi Yako makamilifu. Hebu tuninii tu—tusichukue tu Neno moja hapa na pale, na kulifanya liafikiane na fundisho fulani la sharti ama kanuni fulani ya imani, ama jambo fulani. Hebu na tuchukue Neno jinsi lilivyo, tukiamini Injili kamili, yote ambayo Yesu alitufundisha kufanya .

Hiyo ndiyo hamu yetu kubwa na ya kina kabisa, ni kuwa katika mapenzi Makamilifu ya Mungu. Hatutaki kamwe kumchukiza, bali kumpendeza katika yote tunayosema na tunayofanya. Tunataka kuwa wana na binti zake wenye Mamlaka na waliyodhihirishwa.

Ni wapi tunapata kujua jinsi ya kuwa katika mapenzi yake Makamilifu na kumpendeza? Ni Lazima tuende kwenye Neno Lake, kwani tunajua Neno Lake ndio kweli na uzima. Neno Lake daima ni lile lile, mpango Wake daima ni ule ule, kwani Yeye hawezi kubadilika.

Neno linatuambia, jinsi alivyofanya mambo mara ya kwanza, atafanya vile vile kila wakati. Lazima yeye abaki vile vile milele. Kusudi lake daima limekuwa lile lile. Matendo yake daima yamekuwa yale yale . Jinsi anavyofanya mambo, jinsi anavyowaponya watu, na jinsi anavyowaongoza watu Wake, daima atabaki vile vile .

Biblia inatuambia katika Neno Lake lisilobadilika kuwa Neno la Bwana huja kwa manabii Wake peke yao. Yeye kamwe hawafunulii makasisi ama mwanatheolojia, manabii Wake tu. Alisema pia hakufanya neno lolote mpaka kwanza alipowaonyesha hilo manabii wake .

Mwanadamu daima amekuwa akitaka mfumo uliotengenezwa na mwanadamu, kundi la watu kuwaongoza. Lakini hiyo kamwe haikuwa njia ya Mungu , Yeye daima alimtuma kiongozi wa kiungu aliyeitwa, nabii aliyeteuliwa akiwa na Neno kuwaongoza watu Wake. Nabii huyo alithibitishwa na alichaguliwa kuwa kiongozi wao wa saa hiyo.

Mungu alichagua na kuweka viongozi wengine wengi waliowekwa wakfu waliojazwa na Roho Mtakatifu; na wana nafasi zao, lakini aliwaonya hao viongozi, “Kaeni mbali na hiyo Nguzo ya Moto.” Je! Nguzo hiyo ya Moto hufanya nini… HUONGOZA WATU MCHANA NA USIKU.

Kisha Neno linatuambia, “Kama ilivyokuwa katika siku za Sodoma, Hivyo ndivyo itakavyokuwa siku Ile atakayofunuliwa Mwana wa Adamu .” Kulingana na Neno Lake katika Malaki 4, na Maandiko mengi, atarudi tena katika Kanisa Lake katika umbo la mwili; katika watu, katika wanadamu, kwa njia ya kuwa nabii.

Tutamtambuaje nabii huyu? Yeye atathibitisha yeye ni nani kwa Neno. Yeye atajua siri za mioyo. Atawafunulia watu Neno lote. Atathibitishwa na Nguzo ya Moto kumwongoza Bibi-arusi. Mungu hata atapigwa picha pamoja na nabii wake.

Wengine watakuwa kama Yohana kwenye kisiwa cha Patmo na kujaribu kumwabudu, lakini atasema, “Angalia usifanye hivyo, mimi ni mjoli wako, na wa manabii, mwabudu Mungu.” Bibi-arusi atajua sio kumwabudu yeye, yule mtu, lakini kumwabudu Mungu KATIKA MTU HUYO.

Atatambua kuwa ndiye yule aliyechaguliwa na Mungu kunena Maneno ya kutokukosea. Atatambua kuwa alikuwa yule malaika_mjumbe wa 7 aliyechaguliwa na Mungu. Ulimwengu utaona na kusikia Sauti ya Mungu ikinena kupitia Yeye na utaona Adamu wa kwanza aliyerejeshwa Kikamilifu.

Atamwongoza Bibi-arusi kwa Nguzo ya Moto. Atakuwa akipata taarifa yake kutoka kwa Logos na kumpa Bibi_arusi njiani mwao kuelekea nchi ya ahadi. Bibi-arusi atakuwa na Ufunuo na kutambua huyu ni mjumbe aliyeandaliwa na Mungu. Hii ndio njia iliyoandaliwa na Mungu. Haya ni MAPENZI MAKAMILIFU ya Mungu .

Njoo uungane nasi Jumapili saa 8:00 Nane Mchana, saa za Jeffersonville (Ni saa 3:00 Tatu Usiku ya Tanzania), Kusikia: Je! Mungu Hubadilisha Nia Yake? 65-0427.

Ndugu. Joseph Branham

Hesabu 22:31