All posts by admin5

21-0815 Ile Mbegu Haitarithi Pamoja na Kapi

Ujumbe: 65-0429b Ile Mbegu Haitarithi Pamoja na Kapi

PDF

pakua

BranhamTabernacle.org

Tai wanakusanyika Pamoja.

Mpendwa Mwili wa Mwili Wake,

Nina furaha sana kwamba Mungu habadilishi nia Yake kuhusu Neno Lake. Yeye ni yeye yule jana, leo na hata milele. Jinsi alivyofanya mambo tangu mwanzo, anafanya vile vile leo. Mungu, Mwenyewe, aliyejidhihirisha katika mwili wa mwanadamu, kwa Damu ya Yesu Kristo, kutakasa maisha ili Aweze kujiakisi mwenyewe kupitia huo .

Mjumbe wetu leo hii ​​ana Utambulisho wake wa Kimaandiko kati yetu. Ni Roho Mtakatifu, Mwenyewe, akijifasiria Mwenyewe. Hakuna haja ya kwenda kutoka kwa hili kwenda kwa Lile ili kupata ukweli au fasiri; Roho Mtakatifu amelipa Kanisa Lake Waefeso 4, yote katika mtu mmoja, nabii Wake aliyethibitishwa.

Mtume : Mtume maana yake ni “aliyetumwa,” au, “mmishenari.” Mimi ni mmishenari.

Nabii : Je! Unaniamini mimi kuwa nabii wa Mungu?

Mwinjilisti : “ Fanya kazi ya mhubiri wa injili. Timiliza huduma yako. Utakuja Wakati watakapoyakataa mafundisho Yenye uzima. “

Mchungaji : Mwaniita, “mchungaji wenu”; nanyi mwasema vema, kwa maana ndivyo nilivyo.

Mwalimu : Nataka kuzungumza juu ya Neno, ama kufundisha somo hili la shule ya Jumapili, juu ya Neno la Ile Ishara .

Ni sawa na = Ninajua ninyi, ndugu zetu, mnanitazama mimi kuwa Yakini kwa kile… maadamu ninamfuata Mungu, kama vile Paulo alivyosema katika Maandiko, “nifuateni mimi, kama mimi ninavyomfuata Kristo.”

Ujumbe huu ni Yakini yetu, hivyo tunamfuata yeye kama anavyomfuata Kristo.

Wala Sipuuzi kuwa kuna wengi ambao Mungu anawaita Waefeso 4 watu ambao wamewekwa na kuitwa na Mungu kutimiza ofisi hizi; kwa NEEMA YAKE, mimi ni mmoja wao. Lakini sisi ni wadogo, nabii malaika wa 7 wa Mungu ndiye MKUU.
Kwa wale ambao kote ulimwenguni huiita “Maskani ya Branham ” “kanisa Lao la nyumbani”: mchungaji wetu, huduma yetu iliyo hai, Yakini yetu, Waefeso 4 yetu yote ipo kwenye kanda. Tunaamini ni huduma ya asili ambayo alikuwa nayo wakati alipokuwa hapa duniani.

Ni amani iliyoje, pumziko jinsi gani, hatujawahi kuwa na wasiwasi au kumvuka kiongozi wetu au chujio letu wakati tunaposikia Neno. Ni Neno la Mungu lililohakikishwa na lililothibitishwa, mana safi kila tunapolisikia na tunachotakiwa kufanya ni kuketi chini na kufurahiya mioyo yetu ikiwaka ndani yetu anapozungumza nasi njiani.

Na wote alionipa Baba, watakuja. Kondoo wangu, hua Wangu, huisikia Sauti Yangu. Mgeni hawatamfuata.” Na Sauti ya Mungu ni nini? Ni Neno la Mungu. Sauti ya mtu ye yote ni nini ila ni neno lake? Ni Neno la Mungu; watalisikia Neno la Mungu .

Halafu bado kuna mengi ZAIDI kwa ajili ya Kanisa Lake. Sio tu kwamba tunatambua siku hii na mjumbe wake, Neno la siku hii, Bali furaha kuu ambayo mwanadamu aliyowahi kupewa hatimaye imetimia. SISI NI sehemu ya Roho Wake, sehemu ya Mwili wake; nyama ya nyama Yake, mfupa wa mfupa Wake; Neno la Neno Lake, Maisha ya Maisha yake, SISI NI Bibi-arusi wa Kristo!

Utukufu !! Lisifikiwe Jina la Bwana !! Haleluya !! Bibi-arusi Wake Amejitambua na Anajifanya Mwenyewe Tayari kwa Neno Lake.

Hivyo ndivyo kanisa linavyofanya siku hizi, kwa kuwa Yesu ni Neno Naye ni Bwana Arusi, na Bibi-arusi ni sehemu ya Bwana Arusi. Kwa hiyo Neno ambalo itapaswa litimizwe siku hii ni sehemu ile ile ya Neno lililotimizwa katika siku Zake, na ni Neno lile lile, tukio lile lile, Maisha yale yale .

Njoo upate uzoefu wa Neno lile lile, tukio lile lile, Maisha yaleyale Jumapili hii saa 8:00 Nane mchana, saa za Jeffersonville,( ni Saa 3:00 tatu usiku ya Tanzania) kusikia: Ile Mbegu Haitarithi Pamoja Na Kapi 65-0429B.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya Kusoma:

Mathayo 1: 18-20 / 24:24
Luka 17:30
Yohana mtakatifu 5:24
Wagalatia 4: 27-31
Mwanzo 2:15
Isaya 9: 6
Malaki 4

21-0808 Je! Mungu Hubadilisha Nia Yake?

Ujumbe: 65-0427 Je! Mungu Hubadilisha Nia Yake?

PDF

pakua

BranhamTabernacle.org

Tai wanakusanyika Pamoja.

Mpendwa Bibi_arusi wa Mapenzi Makamilifu,

Ee Mungu mpendwa, hatutaki mapenzi Yako ya kuruhusia, Baba. Jalia tutembee katika mapenzi Yako makamilifu. Hebu tuninii tu—tusichukue tu Neno moja hapa na pale, na kulifanya liafikiane na fundisho fulani la sharti ama kanuni fulani ya imani, ama jambo fulani. Hebu na tuchukue Neno jinsi lilivyo, tukiamini Injili kamili, yote ambayo Yesu alitufundisha kufanya .

Hiyo ndiyo hamu yetu kubwa na ya kina kabisa, ni kuwa katika mapenzi Makamilifu ya Mungu. Hatutaki kamwe kumchukiza, bali kumpendeza katika yote tunayosema na tunayofanya. Tunataka kuwa wana na binti zake wenye Mamlaka na waliyodhihirishwa.

Ni wapi tunapata kujua jinsi ya kuwa katika mapenzi yake Makamilifu na kumpendeza? Ni Lazima tuende kwenye Neno Lake, kwani tunajua Neno Lake ndio kweli na uzima. Neno Lake daima ni lile lile, mpango Wake daima ni ule ule, kwani Yeye hawezi kubadilika.

Neno linatuambia, jinsi alivyofanya mambo mara ya kwanza, atafanya vile vile kila wakati. Lazima yeye abaki vile vile milele. Kusudi lake daima limekuwa lile lile. Matendo yake daima yamekuwa yale yale . Jinsi anavyofanya mambo, jinsi anavyowaponya watu, na jinsi anavyowaongoza watu Wake, daima atabaki vile vile .

Biblia inatuambia katika Neno Lake lisilobadilika kuwa Neno la Bwana huja kwa manabii Wake peke yao. Yeye kamwe hawafunulii makasisi ama mwanatheolojia, manabii Wake tu. Alisema pia hakufanya neno lolote mpaka kwanza alipowaonyesha hilo manabii wake .

Mwanadamu daima amekuwa akitaka mfumo uliotengenezwa na mwanadamu, kundi la watu kuwaongoza. Lakini hiyo kamwe haikuwa njia ya Mungu , Yeye daima alimtuma kiongozi wa kiungu aliyeitwa, nabii aliyeteuliwa akiwa na Neno kuwaongoza watu Wake. Nabii huyo alithibitishwa na alichaguliwa kuwa kiongozi wao wa saa hiyo.

Mungu alichagua na kuweka viongozi wengine wengi waliowekwa wakfu waliojazwa na Roho Mtakatifu; na wana nafasi zao, lakini aliwaonya hao viongozi, “Kaeni mbali na hiyo Nguzo ya Moto.” Je! Nguzo hiyo ya Moto hufanya nini… HUONGOZA WATU MCHANA NA USIKU.

Kisha Neno linatuambia, “Kama ilivyokuwa katika siku za Sodoma, Hivyo ndivyo itakavyokuwa siku Ile atakayofunuliwa Mwana wa Adamu .” Kulingana na Neno Lake katika Malaki 4, na Maandiko mengi, atarudi tena katika Kanisa Lake katika umbo la mwili; katika watu, katika wanadamu, kwa njia ya kuwa nabii.

Tutamtambuaje nabii huyu? Yeye atathibitisha yeye ni nani kwa Neno. Yeye atajua siri za mioyo. Atawafunulia watu Neno lote. Atathibitishwa na Nguzo ya Moto kumwongoza Bibi-arusi. Mungu hata atapigwa picha pamoja na nabii wake.

Wengine watakuwa kama Yohana kwenye kisiwa cha Patmo na kujaribu kumwabudu, lakini atasema, “Angalia usifanye hivyo, mimi ni mjoli wako, na wa manabii, mwabudu Mungu.” Bibi-arusi atajua sio kumwabudu yeye, yule mtu, lakini kumwabudu Mungu KATIKA MTU HUYO.

Atatambua kuwa ndiye yule aliyechaguliwa na Mungu kunena Maneno ya kutokukosea. Atatambua kuwa alikuwa yule malaika_mjumbe wa 7 aliyechaguliwa na Mungu. Ulimwengu utaona na kusikia Sauti ya Mungu ikinena kupitia Yeye na utaona Adamu wa kwanza aliyerejeshwa Kikamilifu.

Atamwongoza Bibi-arusi kwa Nguzo ya Moto. Atakuwa akipata taarifa yake kutoka kwa Logos na kumpa Bibi_arusi njiani mwao kuelekea nchi ya ahadi. Bibi-arusi atakuwa na Ufunuo na kutambua huyu ni mjumbe aliyeandaliwa na Mungu. Hii ndio njia iliyoandaliwa na Mungu. Haya ni MAPENZI MAKAMILIFU ya Mungu .

Njoo uungane nasi Jumapili saa 8:00 Nane Mchana, saa za Jeffersonville (Ni saa 3:00 Tatu Usiku ya Tanzania), Kusikia: Je! Mungu Hubadilisha Nia Yake? 65-0427.

Ndugu. Joseph Branham

Hesabu 22:31

21-0801 Kuthibitisha Neno Lake

Ujumbe: 65-0426 Kuthibitisha Neno Lake

PDF

pakua

BranhamTabernacle.org

Tai wanakusanyika Pamoja.

Wapendwa Watoto Wachanga Wanaoweza kujifunza,

Ni Hali ya kimbinguni jinsi gani tulikuwa tumeketi siku ya Jumapili wakati Bibi-arusi wa Kristo alipokusanyika pamoja katika Uwepo wa Roho Mtakatifu. Tungeweza kuhisi Ikihuisha miili yetu inayokufa.

Hakuna upako mkuu zaidi, hakuna hali kuu zaidi, kuliko wakati Ukibonyeza Play na kusikia Sauti ya Mungu ikizungumza nawe. Mungu ameweka masikio yetu kusikia na kuamini kila Neno, kwani si mwingine isipokuwa El, Elah, Elohim, Yule aliyekuwepo, anayejitosheleza, mwenye nguvu, akiongea na kila mmoja wetu na kutufunulia sisi Kuwa ni wana na binti zake waliodhihirishwa.

Jinsi gani ilivyokuwa yenye nguvu wakati Uzao wa Mungu uliochaguliwa awali, kutoka kote ulimwenguni, walipoweka mikono yao mitakatifu juu ya mmoja kwa mwingine. Nyumba zetu na makanisa yetu yalijazwa na Uwepo wa Roho Mtakatifu. Imani yetu ilikuwa imejengwa, kwani tulijua ni nani anayesema nasi. Kisha akatuambia kuwa ile nguvu ya kuhuisha ilikuwa NDANI YETU. Tuliamini kwa mioyo na roho zetu zote, kwa sababu alisema hivyo.

Ndipo akatuambia tuseme, “Bwana Mungu, naamini kwa moyo wangu wote.” Tulirudia kila Neno kutoka kwenye kina cha mioyo yetu. Alisema, “Ugonjwa hauwezi kusimama katika kundi kama hili.” Roho yetu ilifurahi tuliposikia Maneno haya, kwa maana tulijua kilichokuwa kinatendeka.

Alisema, “Kila mtu anayemtaka Roho Mtakatifu, inua mikono yako, POPOTE ULIPO unayetaka hilo… ninaamini kwamba Mungu atamjaza kila mmoja wenu, SASA HIVI, na Roho Mtakatifu.”
Wakati huo huo, tulijazwa, na kujazwa upya, na Roho Wake Mtakatifu, Sauti ya Mungu ilitamka hivyo.

Kisha kwa wale ambao waliyohitaji uponyaji katika miili yao, Alisema, “Ninakuamuru, katika Jina la Yesu Kristo, simama kwa miguu yako na kukubali uponyaji wako.” Wakati huo huo, kila mwamini, kutoka kote ulimwenguni, ambaye alikuwa na IMANI na aliamini, ALIPONYWA.

Je! Hili lilitendeka wapi? Katika kundi moja dogo la watu lililokusanyika pamoja? Hapana, ilikuwa kutoka ULIMWENGUNI kote wakati Bibi-arusi alipoketi pamoja katika Ulimwengu wa Roho kusikiliza Sauti ya Mungu kwa ajili ya siku yetu.

HAIWEZEKANI kwa mtu yeyote, au kundi la watu, kumuunganisha Bibi-arusi namna hiyo. Ni Roho Mtakatifu peke yake ndiye anayeweza kufanya hivyo kwa kunena kupitia mjumbe wake aliyeandaliwa kwa ajili ya siku hii. Ujumbe huu ni BWANA ASEMA HIVI. Hakuna kushangaa, hakuna kubahatisha, Mungu amethibitisha hii ndiyo njia yake iliyoandaliwa kwa ajili ya leo hii.

Tunalo pumziko na amani jinsi gani. Hatujawahi kamwe kuwa na wasiwasi au kuhoji kile tunachoambiwa. Hatujawahi kamwe kurudi kwenye Neno kulikagua, maana tunasikiliza Neno la Mungu lililothibitishwa kwa ajili ya siku yetu. Tunaketi tu, tukifungulia mioyo yetu, akili na roho zetu, na kusema AMINA, AMINA, AMINA.

Hapana, hatustahili. Hapana, hatuelewi kila kitu. Lakini Tuna AMINI kila Neno. Alisema hiyo ilikuwa ndiyo ishara ya kweli kwamba una Roho Mtakatifu, na ni Bibi-arusi Wake peke yake ndiye atakayeamini na kukaa na kila Neno. SISI NDIYO BIBI_ARUSI HUYO….Haleluya !.

Linapita juu ya wanaodhaniwa kwamba wana akili nyingi sana, na unalifunulia watoto wachanga wanaoweza kujifunza .

Ninashukuru sana ya kuwa mimi ni mtoto mchanga Ninayeweza kujifunza.

Amethibitisha kupitia karne zote Kuwa yeye alikuwa Nani katika kila kizazi. Yeye alithibitisha jambo Hilo kupitia kwa manabii Wake. Alilithibitisha hilo wakati alipokuja katika mwili, akachukua dhambi zetu na kutundikwa msalabani, kisha akafufuka na Akamtuma Roho Mtakatifu.

Sasa amethibitisha katika siku yetu kwa kurudi na kujifunua mwenyewe katika mwili wa mwanadamu Kwa mara nyingine tena kama alivyoahidi angefanya katika Neno Lake. Alijithibitisha kuwa ni Mwana wa Adamu, huduma ya Yesu Kristo Mwenyewe, ikiwa imefichwa katika mwili wa mwanadamu.

Na sasa, sura Yake ya mwisho, sababu yenyewe ya mpango huu mkuu, kuja kwetu, Bibi-arusi Wake aliyerejeshwa Kikamilifu, aliyethibitishwa, ambaye aliyekaa Na Neno.

Je! Ungalipenda Kuwa kwenye mlima siku hiyo wakati Yesu alipoongea na wale 5000? Je! Ungalipenda kumwona akiuthibitishia ulimwengu kuwa Yeye alikuwa nani kwa kutoa mikate na samaki? Je! Ungalipenda kukaa chini ya upako huo, kusikia tu Sauti Yake ikifariji moyo wako kwa Maneno Yake ya Uzima wa Milele?

Unaweza, ikiwa unaamini Ujumbe huu kwa moyo wako wote.

Njoo uketi pamoja nasi chini ya upako huo juu ya mlima Jumapili hii saa 8:00 Nane mchana, saa za Jeffersonville ( Ni saa 3:00 tatu usiku ya Tanzania), na umsikie Mungu akiuthibitishia ulimwengu kuwa Yeye ni nani katika siku yetu. Luka 17:30 Akinena nawe na kukuambia B-R-A-N-H-A-M ni Sauti Yangu iliyothibitishwa na iliyochaguliwa kwako. Njoo umsikie Yeye: Kuthibitisha Neno Lake 65-0426 .

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma:

Mathayo Mtakatifu 11: 4-19 / 28:20
Marko Mtakatifu 11: 22-26
Luka Mtakatifu 8: 40-56 / 17:30
Yohana Mtakatifu 14:12
Waebrania 4: 12-15 / 13: 8
Malaki 4

21-0724 Mahali Pa Kuabudia Palipoandaliwa Na Mungu

Ujume: 65-0425 Mahali Pa Kuabudia Palipoandaliwa Na Mungu

PDF

pakua

BranhamTabernacle.org

Tai wanakusanyika Pamoja.

Wapendwa Waliyouishwa ,

Jinsi gani tunavyopenda kukusanyika pamoja kila wiki kula Manna ya Kiroho aliyowaandalia Bibi-arusi Wake. Inatupa nguvu tunayohitaji kwa ajili ya safari yetu. Ni Maisha yenyewe ya Masihi, yaliyodhihirishwa, yakifanya Kanisa Lake liwe tayari kwa Unyakuo.

Nguzo ya Moto imetuita kutoka, na inatuongoza kwenda kwenye Nchi ya Ahadi, chini ya upako wa nabii Wake Mwenye nguvu, William Marrion Branham.

Ndugu Branham sio ile Nguzo ya Moto. Yeye Ndiye kiongozi aliyepakwa mafuta, chini ya ile Nguzo ya Moto. Nguzo ya Moto inathibitisha tu Ujumbe wake kwa ishara na maajabu. Ni Roho wake Mtakatifu Mkuu aliyejidhihirisha kati yetu na ni mara elfu zaidi ya manabii wengine wote wa hapo awali.

Hivi huwezi kumwona Mwana wa Adamu, Mwana wa Adamu katika mfano wa Ujumbe wa kinabii, akirudi tena katika Kanisa Lake, katika unabii, akimfunua Yesu Kristo kwamba ni yeye yule jana, leo, na hata milele? Halijawahi kufanyika kote katika wakati huu, mpaka kufikia saa hii.

Akili zetu za Kiroho zimelishika. Tunaliona na tunaamini kila Neno. Ujumbe Huu, Kanda hizi, ni Njia iliyoandaliwa na Mungu ili kuikamata akili hiyo huko nje ambapo mbegu hiyo imepandwa. Tumesikia Sauti hiyo na Nuru imetugusa na tumetwaa Uzima.

Inatuketisha katika makao ya kimbinguni, SASA HIVI. Sio tutakuwa, tuko sasa. Tayari tumefufuliwa, Nguvu tendaji na mitambo ipo kazini. Imetuhuisha katika Uwepo wa Mungu, alipo Roho Wake. Sio kile utakachokuwa, tayari uko! Ni shetani tu akijaribu kutufumba kutoka Kwenye hilo.

Swali: Je! Umekuwa Hai?
J: Ndio

Swali: Je! Kristo amekuwa halisi kwako?
J: Ndio

Swali: Je! Nguvu za Mungu zimedhihirishwa?
J: Ndio

Swali: Je! Uko katika Kanisa hilo, Kanisa lililoandaliwa na Mungu?
J: Ndio

Swali : Unakuaje ndani Yake, unajuaje kuwa umehuishwa ndani Yake?
J : Mawazo yetu yote; Utu wetu wote, uko ndani ya Kristo. Kristo yuko katikati yetu, akijithibitisha kuwa hai, akithibitisha kuwa yuko hapa.

Sisi ni nyama ya nyama Yake, na mfupa wa mfupa Wake, mwili wa mwili Wake, Jina la Jina Lake, Bibi-arusi Wake. Tuko ndani yake. Sisi ni mwili Wake na mifupa yake.

Hatuwezi kufa, tumehuishwa. Nguvu ile ya kuhuisha iliyotufufua kutoka kwenye maisha ya dhambi, na kubadilisha Utu wetu, imetufufua kwa uwezekano katika Kristo Yesu, ambapo, ufufuo utatuleta katika ukomavu kamili.

Tumezaliwa mara ya pili na kuzaliwa upya, tumebatizwa na Roho Mtakatifu, ndani ya Yesu Kristo. Tumehuishwa kwa kila Neno. Tunaitikia kila Neno kwa “amina”.

Tunapokusanyika pamoja katika Yesu Kristo; kwa nia moja, na kwa umoja , chochote tunachohitaji, ikiwa tutakuwa na IMANI na kuamini, Yeye atatupatia.
Hebu na tutambue ya kwamba Yeye atakuwa katika kila moja ya nyumba zetu, makanisa yetu, au mahali popote tutakapokusanyika, kwani sisi ni wana na binti zake, Kanisa la Bibi-arusi Wake.

Ninajua Yeye yuko hapa. Nina hakika Yeye yuko hapa. Ninajua ya kwamba sasa kuna nguvu za kuhuisha ndani ya Kanisa kumponya kila mtu anayeketi hapa .

Je! Unaamini Ujumbe huu? Je! Unaamini ni Njia ya Mungu ya leo? Je! Unaamini ni Mwana wa Adamu akijifunua mwenyewe katika mwili wa mwanadamu? Je! Unaamini kila Neno?

Ikiwa unahitaji uponyaji wa mwili, uponyaji wa roho, au CHOCHOTE ambacho unaweza kuhitaji, basi ninakupa changamoto kuamini sauti ya Mungu iliyotiwa mafuta nakuthibitishwa kwa ajili ya siku yetu:

Jalia sasa ya kwamba nguvu hizo za kuhuisha zitaihuisha imani yao, Bwana, kwa yale wanayofanya. Kuna mwamini aliyeweka mikono yake juu ya mwamini, mwili kwa mwili, nguvu kwa nguvu. Na ni nguvu za Mungu, kwa mwana wa Mungu ama binti ya Mungu, kwa Mwana wa Mungu. Ee Mungu, jalia Shetani awaachilie watu hawa! Jalia waponywe alasiri ya leo, kwa nguvu hizo za kufufuka, kuhuisha kwa Uwepo uliotambulishwa, Yesu Kristo. Katika Jina la Yesu Kristo, na iwe hivyo!

Njoo uungane nasi chini ya: Mahali Pa Kuabudia Palipoandaliwa na Mungu 65-0425, na upokee uponyaji wako, utiwe mafuta na Roho Mtakatifu, roho yako ifurahi unapoketi katika makao ya kimbinguni na kumsikia Mwana wa Adamu akizungumza Jumapili hii saa 8:00 Nane mchana , saa za Jeffersonville ( ni saa 3:00 Tatu usiku ya Tanzania).

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya kusikia Ujumbe:

Kumbukumbu la Torati 16: 1-6
Malaki 4: 5
Mathayo Mtakatifu 1:23
Marko Mtakatifu 16:17
Luka Mtakatifu 17:30
Yohana Mtakatifu 4:23 / 10: 1-7
Warumi 8: 1-11
1 Wakorintho 12:13
Waefeso 1:21
1Wathesalonike 4:16
Waebrania 13: 8
Ufunuo 22:19

21-0718 Kutoka kwa tatu

Ujume: 63-0630m Kutoka kwa tatu

PDF

pakua

BranhamTabernacle.org

Tai wanakusanyika Pamoja.

Wapendwa Wana na Mabinti waliyodhihirishwa,

Mtu hajui ni wapi aanzie. Kufikiria, tumekuwa tukikaa pamoja katika hali ya kimbinguni, kutoka kote ulimwenguni, tukinywa kutoka kwenye maji hayo yaliyo hai, kuwa wana na mabinti zake waliodhihirishwa. Ujumbe huu unatupa ufahamu mkamilifu, unatuweka mahali petu, na unatuambia sisi ni NANI katika Kristo Yesu.

Je! Ujumbe huu unafanya nini?

“Kwa maana mimi niliwaposa, nikawachumbia kwa Kristo, kama bikira safi.”

Utukufu, Mungu alimtuma malaika-mjumbe wake wa 7 kutuposa kwake kama bikira safi. Tutahukumiwa kwa kila neno ALILOSEMA. Hiyo inamaanisha ni lazima UBONYEZE PLAY.

Aliandika Biblia yake ya kwanza angani. Kisha akaandika Biblia yake ya pili katika jiwe. Biblia yake ya tatu iliandikwa kwenye karatasi kwa ajili ya ulimwengu mashuhuri, wenye hekima wakiakili ujao. Lakini leo, siku kuu ya ufunuo, tuna Kipeo Chake kitimilifu na kikamilifu, Sauti ya Mungu yenyewe ikimwita Bibi-arusi Wake, Atoke kwa Kanda:

“Nawe UTA tukabidhi kwa Bwana Yesu atakapokuja, kama tunu za huduma YAKO.”

Na sisi sote tunapaaza sauti kwa pamoja,

“Tunajua hilo! Tunastarehe kwa uhakika . ” Kasema, “WEWE utatukabidhi kwake, na ndipo tutarudi duniani tena, tukaishi milele.”
Je! Bibi-arusi wa Kristo alipaza sauti akisema nani atatukabidhi kwa Mungu? Nabii wa Mungu kwa HUDUMA YAKE. Je! Basi Unawezaje kutotaka kucheza kanda hizi kanisani mwako?

Ni Ujumbe huu peke yake, kanda hizi, zinazoweza kulileta Kanisa katika upatano hivi na Mungu, mpaka Dhihirisho la Bwana Arusi limedhihirishwa ndani yetu. Nimejuaje kuwaambieni “kaeni na hizo Kanda,” nilirudi kwenye Ramani ili kuona kile nabii alichosema.

Ninatumaini mtu wa rohoni anaweza kulishika hilo. Nina hakika mnalishika. Lakini sijui, huko nje. Kwa vyovyote vile, huwezi kutembelea kila taifa. Unaweza kutuma kanda huko. Mungu atakuwa na njia fulani ya kumshika mtu huyo huko nje ambako mbegu hiyo inapandwa. Kweli. Na mara Nuru itakapoigusa, imetoka, imepata Uzima. Kama vile yule mwanamke pale kisimani, alisema, “ hilo hapo .” Akaishika.

Kwetu sisi ni asali mwambani, ni furaha isiyotamkika, ni dhamana iliyobarikiwa, ni nanga ya nafsini, ni tumaini na tegemeo letu, ni Mwamba wenye imara, ni kila kitu.

Nia zetu za roho hazijachafuliwa. Tunajua yakini Yeye ni nani. Tunajua yakini Yeye ni nini. Tunajua yakini sisi ni nani. Tunajua Yakini tunakoelekea. Tunajua tunayemwamini na kusadiki ya kwamba yeye aweza kukilinda kile tulichoweka Amana kwake hata siku ile.

Halafu ikiwa Mungu ametufunulia sisi ni mabalozi wake, nguvu zote zilizo Mbinguni, yote Mungu Aliyo, Malaika wake wote na nguvu zake zote zinasimama nyuma ya MANENO YETU. Mungu hana budi kuliheshimu Neno, kwa maana alisema, “Lolote Mtakalofunga duniani, hilo nitalifunga Mbinguni. Chochote Mtakachofungua duniani, hicho nitakifungua Mbinguni. Nami nawapa funguo za Ufalme. ”

Ni wakati wa kwenda Nyumbani. Kule Kutoka kumekaribia. Mungu anatuonyesha nani ni nani. Bibi-arusi wa Yesu Kristo, atatoka, kuingia katika Nchi ile iliyoahidiwa.

Katika kutoka kwake kwa kwanza, Aliwatoa katika nchi ya kawaida, akawapeleka kwenye nchi ya kawaida.
Kutoka kwa pili, Yeye aliwatoa kutoka katika hali ya kiroho, akawaingiza katika ubatizo wa kiroho wa Roho Mtakatifu.
Sasa Yeye anatuleta kutoka kwenye ubatizo wa kiroho wa Roho Mtakatifu, kurudi katika ya Milele, kwa Nguzo ile ile ya Moto, kwa mfumo ule ule uliotiwa mafuta, Mungu yeye yule akifanya mambo yale yale!

Acha upepo uvume vikali. Acha tufani itikise, tuko salama milele. Tunapumzika papo hapo kwa kila Neno.

Njoo uungane nasi Jumapili saa 8:00 nane mchana, saa za Jeffersonville, ( ni saa 3:00 tatu Usiku ya TZ), na utegemee kila Neno Alilolinena Mungu kwa ajili ya siku yetu. Jiweke Mwenyewe tayari kwa kuja kwake kwa hivi karibuni na usikie: Kutoka kwa Tatu 63-0630M.

Ndugu. Joseph Branham

Kutoka 3: 1-12

Mwanzo Sura ya 37 yote

Mwanzo Sura ya 43 yote

21-0711 Kufanywa Wana Wenye Mamlaka #4

Ujume: 60-0522e Kufanywa Wana Wenye Mamlaka #4

PDF

pakua

BranhamTabernacle.org

Tai wanakusanyika Pamoja.

Tai Wapendwa,

Hebu na tukusanyike wote pamoja kusikia Kufanywa Wana Wenye Mamlaka #4 60-0522E Jumapili hii saa 8:00 nane mchana , saa za Jeffersonville.( Ni saa 3:00 tatu usiku ya Tanzania) .

Ndugu Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya Ujumbe:
Waefeso 1: 8-22 / 2: 1 / 4:30
Waebrania 7: 1-3
Mwanzo 14: 18-24
Mathayo Mtakatifu 26: 26-29
Yohana Mtakatifu 17:17
Wagalatia 1: 8
Ayubu sura 38 yote

21-0704 Kufanywa Wana Wenye Mamlaka #3

Ujume: 60-0522m Kufanywa Wana Wenye Mamlaka #3

PDF

pakua

BranhamTabernacle.org

Tai wanakusanyika Pamoja.

Tai Wapendwa, Hebu na tukusanyike wote pamoja kusikia ujumbe Kufanywa Wana Wenye Mamlaka #3 60-0522M Jumapili hii saa 8:00 nane mchana, saa za Jeffersonville( ni saa 3:00 tatu usiku ya Tz).
Ndugu Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya Ujumbe:
Mathayo 28:19
Yohana 17: 7-19
Matendo 9: 1-6, Sura ya 18 na 19
Warumi 8: 14-19
1 Wakorintho 12: 12-13
Wagalatia 1: 8-18
Waefeso Sura ya 1 yote
Waebrania 6: 4-6, 9: 11-12

21-0627 Kufanywa Wana Wenye Mamlaka #2

Ujume: 60-0518 Kufanywa Wana Wenye Mamlaka #2

PDF

pakua

BranhamTabernacle.org

Tai wanakusanyika Pamoja.

Tai wapendwa,
hebu tukusanyike pamoja kusikia Ujumbe 60-0518 Kufanywa Wana Wenye Mamlaka #2 Jumapili hii saa 8:00 Nane kamili mchana, saa za Jeffersonville.( Ni Saa 3:00 Tatu kamili usiku ya Tz)

Ndugu Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya Ujumbe:
Mwanzo 1:26
Waefeso Sura ya 1 yote
Warumi 8:19
Wagalatia 1:6-9
Waebrania Sura ya 6 yote
Yohana 1:17

21-0620 Kufanywa Wana Wenye Mamlaka #1

Ujume: 60-0515e Kufanywa Wana Wenye Mamlaka #1

PDF

pakua

BranhamTabernacle.org

Tai wanakusanyika Pamoja.

Tai wapendwa, hebu tukusanyike pamoja kusikia Ujumbe 60-0515e Kufanywa Wana Wenye Mamlaka #1 Jumapili hii saa 8:00 Nane kamili mchana, saa za Jeffersonville.( Ni Saa 3:00 Tatu kamili usiku ya Tz)

Ndugu Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya Ujumbe:
Yoeli 2:28
Waefeso 1: 1-5
I Wakorintho 12:13
I Petro 1:20
Ufunuo 17: 8
Ufunuo 13 yote.

21-0613 Mfalme Aliyekataliwa

Ujume: 60-0515m Mfalme Aliyekataliwa

PDF

pakua

BranhamTabernacle.org

TAI WANAKUSANYIKA PAMOJA

Wapendwa marafiki wapendwa, wapenzi wa Injili, watoto waliyomzalia Mungu,

Ninashukuru sana tunamsikiliza mchungaji wetu. Sisi ni kondoo anaowachunga. Sisi ni kanisa lake. Kanda hizi zimerekodiwa na kuhifadhiwa kwa ajili yetu. Sisi ni Rafiki za malaika_mjumbe wake wa saba, na wapendwa wapenzi wa Injili. Sisi ni watoto wake aliyomzalia Mungu.

Siku moja ujumbe huu uliangaza mbele yetu na tukamsikia Yesu Kristo yeye yule jana, leo, na hata milele. Imetosheleza ladha yetu, na tunatamani zaidi. Ujumbe huu, Neno Lake, Sauti Yake, ni Bwana Yesu Kristo. Ni yote tunayohitaji, yote tunayotaka, yote tuliyonayo.

Ikiwa ufunuo wowote utawasilishwa kwetu ambao ni kinyume na Neno lililoandikwa, hatutaupokea kamwe, kwa sababu ndivyo Shetani alivyomfanyia Hawa. Alikuwa na Neno, lakini alikuwa akitafuta nuru Fulani mpya, na Shetani aliiona kwamba hawa anayo. Hatutaki kamwe kuongeza chochote kwenye Neno, au kuondoa lolote kutoka kwenye Neno; bali liache tu jinsi lilivyo. Dumu sawa sawa na Neno, kwa maana kitu chochote kilicho kinyume ni kutokuamini. Lazima TUDUMU NA HUDUMA YA KANDA.

“ Sijahubiri cho chote maishani mwangu ambacho nilionea aibu. Mimi sitaagiza kanda zo zote zirudishwe, wala rekodi zo zote. Nitadumu na anayosema Roho Mtakatifu. Hayo nitaishi nayo na kufa nayo.” Mimi sijaribu kuzungumzia juu yangu binafsi, sasa, bali ninajaribu tu kuwapa mfano wa yanayoendelea kusudi mpate kuona na kufahamu. Ni watu kutaka kuongozwa na mwanadamu.

Kanda hizi ni kile ambacho Roho Mtakatifu anachosema kumwongoza Bibi-arusi Wake. Tunaishi kwa kila Neno na tutakufa kwa kila Neno, kwa maana Ni Bwana Asema Hivi. Tutasimama na Neno la Mungu hata ikiwa itagharimu kila kitu kilicho katika maisha yetu; tutadumu na Neno.

Kila kanda tunayosikia inatuleta karibu zaidi na yeye na kufunua Neno lake zaidi. Daima ni kile hasa tunachohitaji kwa siku hiyo. Hatutaki mwana wa Kishi atuongoze, tunataka njia ya Mungu iliyoandaliwa: Nabii wake.

Ombi letu Ni, ” Ee Mungu, Usituache kamwe tupatane kwa Neno moja. Tujalie tudumu sawasawa katika Neno hilo na kuliishi. Hatujali nini kinachokuja ama kinachokwenda, kile mtu ye yote afanyacho ,tujalie tudumu na Neno lako.”

Vita vinazidi kuwa vigumu na vigumu kila siku. Shetani yuko katika ghasia kubwa zaidi ya hapo awali. Anajua wakati wake umekwisha, siku zake sasa zimehesabiwa. Ana ulimwengu chini ya udhibiti wake, kwa hiyo anamshambulia Bibi-arusi.

Wakati mwingine vita huwa vigumu sana. Tunapata uchovu sana na kuchoka tukipaza sauti.

Nina hamu ya kwetu sana na nina huzuni na nataka kumwona Yesu; Ningetaka kusikia hizo kengele tamu za bandari zikilia; Ingeangaza njia yangu na kutowesha hofu zote; Bwana, hebu tuangalie ng’ambo ya pazia la wakati. Bwana, hebu niangalie ng’ambo ya pazia la huzuni na hofu; Hebu niiangalie hiyo nchi yenye jua na inayong’aa. Ingetia nguvu imani yetu na kutowesha hofu zote; Bwana, hebu na waangalie ng’ambo ya pazia la wakati.

Baba alijua kwamba tungedhoofika na kuchoka, kama nabii Wake. Kwa hiyo asubuhi moja alimuamsha mtumishi Wake, ili kumtia moyo. Akamwacha aangalie na aende Ng’ambo ya Pazia la Wakati.

Ndipo akamrudisha kutuambia jinsi kutakavyokuwa. Hapakuwa na wivu. Hakukuweko na uchovu. Hakukuweko na kifo ama magonjwa kule. Kupatikana na Mauti hakungeweza kutufanya kuzeeka tena. Ilikuwa zaidi ya ukamilifu.

Ndipo Bibi-arusi akamchukua, na kumweka yeye juu ya mahali pamoja pa juu na kupaza sauti akisema:

“ Tunajua jambo hilo, nasi tunajua tunarudi pamoja nawe siku moja duniani.” Kasema, “Yesu atakuja, nawe utahukumiwa kulingana na Neno ulilotuhubiria sisi. Halafu, kama ukikubalika wakati huo, ambapo utakubalika,” kisha kasema, “basi wewe utatukabidhi Kwake kama tunu yako ya huduma yako.”

Kwa hivyo, wakati Bibi-arusi atakaporudi duniani, tutakuwa tunarudi pamoja naye, nabii wa Mungu, na ATATUKABIDHI “KWAKE” KAMA TUNU YA HUDUMA YAKE. Kwa hiyo, lazima tudumu pamoja na huduma ya Kanda.

Nadhani ni muhimu kuingiza hapa kile tulichomsikia nabii akisema wiki chache tu zilizopita:

kanda hizi zinaenda tu…Ninazungumzia kusanyiko langu, ndugu. Mimi siwajibiki na wale Mungu aliokupa kuwachunga; mimi ninawajibika na aina ya Chakula ninachowalisha watu hawa. Hiki ni kwa ajili ya Maskani haya pekee. Mnaona? Sasa, kama watu wanataka kusikiliza kanda, hiyo ni juu yao. Bali mimi ninawazungumzia wale Mungu alionipa.

Ndio maana tunadumu na hizi kanda. Ndio maana tunasema William Marrion Branham ndiye mchungaji wetu. Ndio maana tunasema sisi ni kusanyiko lake. Sisi ndiyo wale Mungu aliyompa. Ndio, sisi ni MMOJA WAO, UTUKUFU.

Ikiwa ungependa kuwa sehemu ya kusanyiko lake, BONYEZA PLAY . Ikiwa ungependa kusikia kanda hizi pamoja nasi, tunakualika uungane nasi Jumapili saa 8:00 nane, mchana, saa za Jeffersonville, (ni saa 3:00 tatu , usiku ya Tz), wakati tutakapoungana na waaminio wengine kutoka kote ulimwenguni kusikia: Mfalme Aliyekataliwa 60-0515M .

Ndugu. Joseph Branham

TD: Nimekuwa katika maombi kwa ajili ya kile kingefuata ambacho Baba angependa tusikilize . Nilijisikia kama alikuwa akiniongoza kuucheza, “Mfululizo wa Kufanywa Wana Wenye Mamlaka.” Nilianza kuomba na kutafuta mapenzi yake. Nilipomaliza kuomba, niliinuka, nikafungua biblia yangu bila mpangilio na kuanza kusoma, ilikuwa ni Wagalatia 4: 1-7. Baba alinihakikishia na kujibu maombi yangu kwa mara nyingine tena.

Mimi na wafanyikazi wa VGR tutachukua muda wa kupumzika kwa wiki 3 zijazo. Wakati wa likizo, nitakuwa nakutumia barua fupi ya uthibitisho wa ujumbe ambao tutakaosikiliza.

Tafadhali nikumbuke mimi na wafanyikazi wa VGR katika maombi yako.

Maandiko ya kusoma kabla ya kusikia ujumbe

1 Samweli Sura ya 8

Mtakatifu Marko 16: 15-18