All posts by admin5

23-0618 Wakati wa Kanisa La Laodikia

Ujume: 60-1211E Wakati wa Kanisa La Laodikia

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Waamini wa Neno lisilokosea,

Jinsi gani imekuwa ni jambo lakupendeza sana kusikia na kusoma Nyakati hizi Saba za Kanisa. Kwa kila Ujumbe tunaousikia, kila sura tunayosoma, Yeye anatupa Ufunuo zaidi. Tunajiona waziwazi tukishuka kuja kupitia kila wakati wa kanisa…Bibi-arusi Wake, ambaye alidumu na Neno la asili.

Katika nyakati zote tunaziona roho hizo mbili kwa uwazi; Udanganyifu na uongo wa Shetani, kulipotosha Neno la Mungu, kuwadanganya, kuwapotosha na kuwashinda watu. Lakini wakati wote kumekuwa na kundi dogo la Mungu la watu waaminifu, Bibi-arusi Wake, wakishikilia kila Neno.

Wakati wote kuna onyo moja la daima linalotolewa kwa watu, yawabidi KUDUMU NA NENO. Mara tu unapopata kutoka nyuma ya Neno hilo, unanaswa katika utando wa buibui mkuu wa Shetani; kama Hawa alivyofanya tangu mwanzo. Alishindwa kulitumia Neno. Adamu alishindwa katika kutolitii Neno moja kwa moja. Lakini Yesu, katika Maisha Yake binafsi, akishindana na nafsi yake, alishinda kwa utii kwa Neno la Mungu.

Alisema kama tunataka kuketi katika kiti Chake cha enzi, lazima tuwe Neno lililo hai. Maombi yetu, kufunga kwetu, au hata toba zetu hazitatupa majaliwa hayo. Bibi-arusi NENO tu ndiye atakayejaliwa.

Kunayo mengi ningependa kusema, na nukuu nyingi ningependa kuzishiriki na kila mmoja wenu; hayaishi. Ninajua Ujumbe Huu unawaka katika kila mojawapo wa mioyo yenu na mnapenda kila Neno, jinsi tu nami ninavyolipenda. Yote Tunayotaka kufanya ni kuzungumza na kulishiriki. Tunataka ulimwengu ujue: Ndiyo, sisi ni watu wa kanda. Ndiyo, sisi tunabonyeza Play . Ndiyo, sisi tunaamini ile Sauti iliyo kwenye kanda hizi ndio itakayomkamilisha Bibi-arusi. Ndiyo, kanda ndizo zitakazomuunganisha Bibi-arusi. Ndiyo, Kubonyeza Play ndio Mapenzi Makamilifu ya Mungu. Ndiyo, mimi ndiye Bibi-arusi Wake.

Ninajua mimi ninarudia Kwa barua nyingi, lakini nina furaha sana, ninashukuru kweli, ni hakika … ni jambo lisilo na shaka, huu ndio Mpango wa Mungu kwa Bibi-arusi Wake.

Kwa kila Ujumbe tunaousikia, tunashangaa kwa mshangao, Wao Wanakosaje kuona, kusoma au kusikia yale tunayosikia? Liko papo hapo, kwenye kanda, kanda baada ya kanda, baada ya kanda. Inanifanya nijisikie kuwaambia wao kama vile Yesu alivyomwambia Nikodemo: “Je! wewe u mwalimu wa Israeli, na mambo haya huyafahamu?”

Hebu Sikiliza jinsi gani malaika huyu anavyolifanya rahisi.

Juu ya msingi wa tabia za wanadamu peke yake, mtu ye yote anajua ya kwamba palipo na watu wengi kuna hata na maoni yasiyopatana juu ya mambo madogo-madogo ya fundisho muhimu ambalo wote wanashikilia pamoja.

Juu ya msingi wa tabia za wanadamu PEKE YAKE, hakuna ufahamu wa kiroho unaohitajika, mtu ye yote anajua watu wawili watakuwa na maoni yasiyopatana juu ya MAMBO MADOGO- MADOGO ya fundisho muhimu.

Wote wanaweza kukubaliana na kusema kama watu hawafanyi wanalosema wao, ama wakiondoka, basi maangamizi yatafuata. Lakini nabii wa kweli daima atamwongoza mtu kwenye Neno na kuwafunga watu kwa Yesu Kristo naye hatawaambia watu wamwogope yeye ama yale anayosema, Lakini waogope yale Neno lisemayo.

Neno linasemaje? Nitawapelekea Eliya nabii. Katika siku za SAUTI. Kutakuwa na nabii wa Neno MMOJA…MMOJA tu…kwa kuwa Mungu ameukabidhi Ufunuo kwa HUYO MMOJA PEKE YAKE. Yeye ndiye atakayemrudisha Bibi-arusi Wangu.

Jinsi kulivyo na sauti nyingi hivi na maoni mengi na nukuu nyingi, mtu anawezaje kuwa na HAKIKA?

Ni nani basi atakayekuwa na mamlaka ya kutokosea ambayo itarudishwa katika wakati huu wa mwisho, kwa kuwa wakati huu wa mwisho utarudi kwenye kumdhihirisha Bibi-arusi wa Neno Halisi?

Huyo ndiye ambaye Bibi-arusi anataka kumsikiliza, huyo aliye na mamlaka ya kutokosea; kwa maana Yeye atakuwa ndiye wa KUMRUDISHA Bibi-arusi. Yeye Hatakuwa na maoni yasiyopatana, Yeye ni Neno.

Swali: Bwana, tunataka kujua, ni nani mtu huyo atakayekuwa na Maneno ya kutokosea?

Nitakwambia ni nani atakayekuwa nalo. Itakuwa ni nabii aliyethibitishwa kinaganaga, ama hata aliyethibitishwa kinaganaga zaidi kuliko nabii ye yote katika nyakati zote tangu Henoko hata siku hii, kwa sababu mtu huyu itambidi kuwa na huduma ya jiwe la kifuniko , na Mungu atamtambulisha. Haitambidi kujitetea , Mungu atamtetea kwa sauti ya ishara. Amina.

Jibu: William Marrion Branham.

Hebu nikutie moyo leo Ewe Bibi-arusi Mteule. HUWEZI, NA HAUTA, PUMBAZWA. Je, ulilipata jambo hilo? Hakuna mtu anayeweza kukupumbaza. Paulo hangeweza kumpumbaza mteule ye yote, kama angalikuwa amekosea. Hata katika wakati ule wa kanisa la kwanza la Efeso, wateule hawakuweza kupumbazwa. Waliwajaribu mitume wa uongo na manabii wa uongo na kuwaona kuwa ni waongo na Wakawaondosha.

UTUKUFU EWE BIBI-ARUSI …. Wewe ni Kondoo WAKE nawe unaisikia Sauti yake na kumfuata YEYE. WEWE NI BIBI-ARUSI-NENO LILILO HAI!!

Hakuna kitu kilicho kikuu zaidi kuliko kujua Maneno haya. Kujua ndani ya moyo wako na nafsini mwako, kuwa wewe ni Bibi-arusi Wake. Siku zile ambazo ulimwengu ulikuwa ukingoja zimefika. Bibi-arusi anajitambua naye anafanyika MMOJA NA YEYE; sisi ni UUMBAJI MPYA WA MUNGU.

Kwa mara nyingine tena ninawasihi, ISIKILIZENI SAUTI YA MUNGU siku ya Jumapili, popote mkutanikapo. Haijalishi ni Ujumbe gani Mnaousikiliza mradi tu mnasikiliza Sauti ya Mungu iliyothibitishwa. Sauti hiyo ilikuwa ndio Sauti ambayo Mungu aliyoiita na kuichagua kumrudisha na kumkusanya Bibi-arusi Wake.

Kwa makanisa yote, watu wote, mnaalikwa kusikiliza pamoja nasi Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA.,masaa ya Jeffersonville,( ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) tunaposikia:  Wakati wa Kanisa la Laodikia 60-1211E.

Ndugu. Joseph Branham

23-0611 Wale Wanawali Kumi, Na Wayahudi Mia Na Arobaini Na Nne Elfu

Ujume: 60-1211M Wale Wanawali Kumi, Na Wayahudi Mia Na Arobaini Na Nne Elfu

PDF

pakua – mp3

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Wapendwa, Wapendao Mana,

Tuna furaha kwa sababu kwamba tunaweza kula Chakula kisicho na mfupa wala mbegu ndani yake. Mikate myembamba ilishuka kutoka Mbinguni, iitwayo “Mana,” inafunika kila mahali kwa utamu wa Mbinguni.

Kwa Ufunuo wa Kiroho, Yeye ametufunulia kuna mahali pamoja tu tunaweza kupata hii Mana Safi isiyo na mbegu: kwa kuisikia Sauti ya Mungu aliyoiandaa kwa ajili ya Bibi-arusi Wake.

Ni ombi lake la daima katika kila wakati kwamba makanisa waisikie Sauti ya Bwana. Katika Wakati huu wa mwisho, ombi Lake ni la nguvu zaidi kuliko wakati mwingine wo wote ; kwa maana hii ndio siku ya Kuja kwa Bwana. Ametuonya, kwa dharura yote, kwamba hatuna budi kuisikia Sauti Yake ya kweli, iliyothibitishwa.

Loo! kuna sauti nyingi sana ulimwenguni—shida nyingi sana na mahitaji yanapaza sauti yapate kushughulikiwa; lakini kamwe hakutakuweko na sauti iliyo muhimu sana na inayostahili kushughulikiwa kama sauti ya Roho. Kwa hiyo, “Yeye aliye na sikio la kusikia, na alisikie Neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa.”

Hilo hapo, onyo lake kwa makanisa, jinsi gani ilivyo muhimu kusikia SAUTI ya Roho. Hakika hapo ndipo adui atakaposhambulia, akijaribu kuondoa kwa watu umuhimu wa kuisikia SAUTI HIYO.

Yeye anatuambia kuna SAUTI NYINGI. Kuna shida nyingi sana na mahitaji, yanapaza sauti yapate kushughulikiwa, lakini usisahau kamwe, lazima usikie SAUTI YAKE ILIYOTHIBITISHWA.

Ikiwa niliwahudhi kwa kusema hivyo, nisameheni, lakini, nilihisi yaweza kuwa huko ni kuchukizwa, lakini, mimi ni Sauti ya Mungu kwenu.

Hilo hapo jibu: MIMI NI SAUTI YA MUNGU KWENU.

Ni wazi sana kwa Bibi-arusi Wake. Halijafichwa, Liko papo hapo wazi kabisa; mtu yeyote anaweza kulisoma. Mimi Siwaambii watu jambo ambalo Yeye Hakusema… mimi silibuni jambo hili. Yeye anatuambia waziwazi ni jambo gani lililo muhimu zaidi tunalopaswa kufanya. Mapenzi makamilifu ya Mungu ni KUSIKIA SAUTI YAKE NA YEYE NDIYE SAUTI YA MUNGU KWETU.

Ndugu na dada, sisemi kuwa hamwezi kuwasikia wachungaji wenu. Sisemi kwamba ni wa uwongo ama ni makosa ikiwa watahudumu. Ni wazi Bwana ametuweka hapa ili tuwe msaada kwa Bibi-arusi na kuwaelekeza ninyi KURUDI kwenye Neno la asili; kuiweka Sauti hiyo mbele zenu kuwa iliyo muhimu zaidi mnayopaswa kuisikia. Tunatakiwa kurudi kwenye MAPENZI MAKAMILIFU YA MUNGU. Yule Adamu aliyerejeshwa kikamilifu, akilindwa na Neno. Mungu alinena kila siku na Adamu mdomo kwa sikio katika ile Bustani, na leo hii, Yeye Anafanya jambo lile lile.

Tunapaswa kuwa tukisimama katika pengo na kusema, “Sisi ni ndugu!” Hatujagawanyika, Sisi sote ni mwili mmoja; Mmoja katika tumaini na fundisho, (Fundisho la Biblia.)

Sisi ni ndugu. Mimi Sijaribu kuyagawanya Makanisa, ninajaribu kutuleta pamoja kwa jambo PEKEE linaloweza kumleta Bibi-arusi pamoja. Hatuwezi sote kukubaliana na MTU YOYOTE, AMA KUNDI LA WAHUDUMU; wote wametofautiana, na wanasema mambo yaliotofautiana. Kuna malaika-mjumbe wa saba MMOJA tu . Kuna Sauti ya Mungu MOJA tu . Sauti ambayo Mungu ameiandaa kwa ajili ya Bibi-arusi Wake kwenye kanda.

Nitakuwa wazi. Ufunuo wangu ni: Kusikiliza Sauti ya Mungu kwenye kanda NDIO MAPENZI MAKAMILIFU YA MUNGU.

Kama katika siku za Samweli, wakati watu walipomwendea na kumwambia walitaka mfalme wakuwatawala. Ilihuzunisha moyo wake. Alimwendea Mungu na kumwambia kile walichotaka. Mungu alimwambia Samweli, hawakukukataa wewe, Samweli, wamenikataa Mimi, ili Nisiwe mfalme juu yao .

Je, Yeye alikuwa akiwatawala namna gani? KWA NABII WAKE, SAMWELI. Hayo yalikuwa ndio MAPENZI YAKE MAKAMILIFU, nao wakamkataa. Ili uwe Bibi-arusi Wake ni lazima Urudi kwenye Mapenzi Makamilifu ya Mungu. Huwezi kuwa na MAPENZI MAKAMILIFU 2.

Jinsi gani ningependa Bibi-arusi wote wakusanyike pamoja kutoka ulimwenguni kote ili kusikia Sauti ya Mungu wote kwa wakati mmoja. Si kwa sababu “Mimi” nasema hilo, bali kwa sababu Mungu ANAFANYA HIVYO. Ndilo jambo pekee la kumkusanya Bibi-arusi Wake pamoja.

Ninakualika uje kusikiliza pamoja na sehemu ya Bibi-arusi, Jumapili saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville( Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki), kusikia: Wale Wanawali Kumi, Na Wayahudi Mia Na Arobaini na Nne Elfu 60-1211M.

Ikiwa huwezi kuungana nasi, mtie moyo mchungaji wako msikilize Sauti ya Mungu Jumapili hii asubuhi kanisani mwenu. Je! Waweza kuwazia, Bibi-arusi kote ulimwenguni, katika kila kanisa, kila nyumba, ama popote ulipo, wakisikia Mana Mpya ikifunika kila mahali kwa utamu wa Mbinguni.

Ndugu. Joseph Branham

23-0604 Wakati Wa Kanisa La Filadelfia

Ujume: 60-1210 Wakati Wa Kanisa La Filadelfia

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

Mpendwa Bibi Yesu Kristo,

Je! hilo halisikiki lakupendeza? Mwana-Kondoo na Bibi-arusi Wake wametulia milele katika ukamilifu wote wa Mungu. Ati tutoe sifa ya jambo hilo? Tunalifikiri. Tunaliota. Tunasoma kile Neno lisemacho kulihusu. Tunamwona Yeye akishiriki Utakatifu Wake NASI. Ndani yake, tumekuwa haki halisi ya Mungu.

Inatuletea furaha jinsi gani wakati tunapobonyeza Play, na kumsikia Mungu Mwenyewe akizungumza nasi kupitia malaika Wake mwenye nguvu na kutuambia mambo haya.

Hakuna kitu cho chote katika maisha haya, hata kiridhishe namna gani, kiwe kizuri na chema vipi, ila utapata jumla ya ukamilifu wote katika Kristo. Kila kitu hufifia kabisa mbele Zake.

Yeye anatuambia tutakuwa na jina jipya, Jina Lake. tutapewa jina lake wakati atakapotupeleka kwake. Itakuwa lakupendeza sana kuliko tunavyoweza kuwazia. Tutaenda popote Bwana-arusi alipo. Hatutaachwa Naye kamwe. Hatutaondoka Ubavuni mwake. Tutashiriki kiti cha enzi pamoja naye. Tutatiwa taji kwa utukufu na sifa zake.

Na wakati anapojithibitisha Mwenyewe kwa ulimwengu, na ulimwengu wote unasujudu miguuni Pake, wakati huo ulimwengu wote utasujudu miguuni pa watakatifu, ikithibitisha ya kwamba walikuwa sahihi katika msimamo wao pamoja Naye. Mungu na abarikiwe milele!

Yeye alitujua tangu zamani kwa uamuzi wa Kiungu ya kwamba tungekuwa Bibi-arusi Wake. Yeye Alituchagua SISI; hatukumchagua Yeye. Yeye ndiye Aliyetuita SISI ; hatukuja kwa hiari yetu. Yeye Alitufia SISI. Alitusafisha katika Damu Yake Mwenyewe. Yeye Alitununua SISI . Sisi ni mali yake, na wake peke yake. Tumejitoa Kwake kabisa naye Anakubali jukumu hilo. Yeye ni kichwa CHETU. Yeye Ananena nasi kupitia malaika wake nasi tunatii, kwani hiyo ndiyo furaha yetu.

Tangu mwanzo hata mwisho, Ujumbe ulio kwenye kanda yote ni MUNGU kwetu SISI. Hebu hayo Maisha na yawe ndani YETU. Hebu na iwe ni Damu yake inayotuosha SISI. Hebu iwe ni Roho Wake anayetujaza SISI. Hebu na liwe ni Neno lake ndani ya moyo na mdomo WETU. Na yawe ni Mapigo Yake yanayotuponya SISI. Na iwe ni Yesu, na Yesu peke yake. Si kwa matendo ya haki, ambayo tumefanya. Kristo ndiye uzima wangu. Ujumbe huu ni uzima wetu, kwa maana ni Kristo.

Loo! kuna sauti nyingi sana ulimwenguni—shida nyingi sana na mahitaji yanapaza sauti yapate kushughulikiwa; lakini kamwe hakutakuweko na sauti iliyo muhimu sana na inayostahili kushughulikiwa kama sauti ya Roho. Kwa hiyo, “Yeye aliye na sikio la kusikia, na alisikie Neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa.”

Mungu anayo Sauti kwa ajili ya siku hii. Imethibitishwa na Nguzo ya Moto kuwa ni Sauti ya Mungu. Kamwe hakutakuwa na Sauti ILIYO MUHIMU SANA NA YENYE THAMANI SANA KUSHUGHULIKIWA kama ile Sauti iliyo kwenye kanda kwa ajili ya siku ya leo.

Njoo uungane nasi Jumapili saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville. ( Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki )Tuna mfuko mzima wa maandiko uliyojaa Asali. Tutaiweka kwenye Mwamba, si juu ya kanisa lolote; juu ya Mwamba, Kristo Yesu. Basi ninyi kondoo anzeni kuiramba. Hakika mtapata afya mara moja. Shida zote za dhambi zitakwisha utakapouramba Mwamba. Hivyo tu ndivyo unavyopaswa kufanya, njoo uisikie Sauti ya Mungu ikituambia yote kuuhusu: Wakati wa Kanisa la Filadelfia 60-1210.

Ndugu. Joseph Branham

23-0528 Wakati Wa Kanisa La Sardi

Ujume: 60-1209 Wakati Wa Kanisa La Sardi

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Wanaostahili, Wenye Haki,

Enyi Tai, mko tayari kukusanyika pamoja Jumapili hii kusikia Sauti tamu ya Yesu ikinena nanyi na kusema:

“ninyi Mnastahili.” “Ninyi ni wangu.” “Ninyi ni wenye Haki.” “Mtatembea pamoja nami katika mavazi meupe.” “Majina yenu yameandikwa Mbinguni.”

Haya si maneno yangu, bali ni Maneno hasa ya Baba yetu wa Mbinguni akinena na WEWE, Bibi-arusi Wake mteule. Roho Mtakatifu amekuja tena na kuishi katika mwili wa mwanadamu, ili aweze kunena mdomo kwa sikio na Bibi mteule wake Maneno haya ya ajabu.

Inapendeza kuyasikia kutoka kwangu, au mtu ye yote ambaye angesema “Yesu alisema”, lakini kumsikia YEYE akisema kupitia Sauti yake teule; ile
aliyozoea kukuambia, kibinafsi… hakuna kabisa kilicho kikuu zaidi.

Kuna sauti nyingi ambazo Mungu hutumia kuleta Neno lake ulimwenguni. Amewachagua na kuwaweka wawe baraka kwa ulimwengu na kwa Bibi-arusi Wake.

Yesu alipokuwa hapa duniani katika mwili wa mwanadamu, Alikuwa pia amewachagua watu, mitume Wake, wamfuate Yeye na kusema kwa niaba Yake yale walioona kuzidiwa na waliosikia. Watu hawa ndio aliowatuma kuieneza Injili, habari njema kwamba Masihi amekuja; Alikuwapo, duniani pamoja nao. Aliwatuma wawili wawili kutangaza Habari Njema hii na kuwaleta watu wote kwake yeye.

Alipokuwa amewakusanya pamoja usiku mmoja, aliwauliza, “Watu huninena mimi kuwa ni nani?” Wakamjibu, “Wengine husema Wewe ni Eliya; wengine husema Wewe ni Yohana Mbatizaji.” Lakini yeye akasema, “Lakini NINYI MNASEMA Mimi kuwa ni nani?” Ndipo Petro akanena maneno hayo makuu, “Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai.” Yesu akamjibu, akasema, Mwili na damu havikukufunulia hili, Petro, bali Baba yangu aliye mbinguni amekufunulia hili, na juu ya mwamba huu(Ufunuo) nitalijenga kanisa langu.”

Ulimwengu umejikwaa pande zote kwenye siri hii kuu. Watu wengine wanaamini alikuwa akimaanisha Petro. Wengine wanaamini kuwa ni mwamba uliokuwa umelala pale. Wengine wanaamini ilikuwa ni Yesu. Lakini kwa Ufunuo, tuliopewa na Roho Mtakatifu, tunajua ulikuwa ni UFUNUO WA YEYE ALIKUWA NANI.

Baada ya kifo cha Yesu, kuzikwa na kufufuka, siku ya Pentekoste, walitumwa kuuambia ulimwengu Habari hii Kuu. Petro alichaguliwa tena kuwa msemaji na kwenda mbele ya watu na kutangaza jinsi ya kupokea Roho wake Mtakatifu. Alisema, hamna budi kutubu na kubatizwa katika Jina la Bwana Yesu Kristo.

Ni nafasi iliyoje ambayo Roho Mtakatifu alikuwa ameweka juu ya Petro. Tunaweza tu kuwazia jinsi watu walivyomtazama. Yeye alitembea pamoja na Yesu alipokuwa hapa duniani katika mwili. Yeye alikuwa rafiki Yake. Alikuwa kando Yake kila siku. Yule ambaye alikuwa amemchagua kumpa ule Ufunuo. Lakini Mungu alikuwa amemchagua MTU MWINGINE kuwa nabii Wake: Paulo.

Wakati Petro alipofika Antiokia kuwa pamoja na Paulo, alikuwa akila na kunywa pamoja na watu wa mataifa. Lakini kundi la watu lilipokuja kutoka kwa Yakobo, alijitenga na kuogopa. Paulo alimkemea waziwazi mbele ya wale wengine na kusema haenendi sawa sawa na ile kweli naye alistahili hukumu. Ndugu Branham alisema Petro alizidiwa na wale wa Dini ya Kiyahudi.

Je, jambo hili linatuambia nini kwa ajili ya siku hii? Haijalishi ni nani. Kiasi gani walivyo na Roho Mtakatifu. Wana mamlaka gani ama wito gani. NI LAZIMA UKAE NA NABII MTEULE WA MUNGU KUWA YAKINI YAKO. KWA MAANA YEYE, NA YEYE PEKE YAKE, NDIYE MFASIRI WA KIUNGU WA NENO LA MUNGU.

Hili si kinyume na Petro au mwanafunzi yeyote aliyechaguliwa na Mungu, wakati huo ama sasa. Wamechaguliwa kueneza Injili, lakini Mungu alikuwa amemchagua MTU MMOJA juu ya Kanisa Lake. Yeye peke yake ndiye aliyekuwa nabii aliyechaguliwa na Mungu akiwa na Bwana Asema hivi, si wao. Wana mahali pao, lakini Yeye ana NABII MMOJA wa kuliweka Kanisa Lake katika utaratibu, akiwa na Neno la mwisho kwa ajili Bibi-arusi Wake.

Hili linatuonyesha jinsi gani tunavyopaswa kuwa waangalifu kuisikia Sauti ya Mungu iliyothibitishwa kwa ajili ya wakati wetu. YULE Aliyemchagua kuwa mfasiri wa kiungu wa Neno Lake. HAKUNA KITU KIKUBWA kuliko kuisikia Sauti yake ikinena kupitia malaika Wake; Sauti ya chaguo Lake , si letu.

Tunaona katika nyakati zote jinsi Mungu alivyo na kundi teule la watu ambao wangekaa NA NENO LAKE na mjumbe Wake mteule. Sauti hiyo inatutangazia sisi kila siku sisi ni nani, MMOJA WAO.

Yeye angetuma watengenezaji kwenye kanisa Lake, lakini LEO HII, Yeye alimtuma mrejeshaji Wake; “Nitarejesha, asema Bwana, nami nitaigeuza mioyo ya watoto, kwa kuwa ninayo mengi ya kuwaambia katika siku za Sauti Yangu.”

Umealikwa kuja kuisikiliza hiyo Sauti, Jumapili saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville, ( ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki ) anapozungumza nasi na kutuonyesha Lile Kanisa la Kweli na la uwongo Katika kipindi cha: Wakati wa Kanisa la Sardi 60-1209.

Ndugu. Joseph Branham

23-0521 Wakati Wa Kanisa La Thiatira

Ujume: 60-1208 Wakati Wa Kanisa La Thiatira

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Nyota Katika Taji Yake,

Furahi Bibi-arusi. Tunakuwa mmoja na Yeye. Kila siku, Anatupa Ufunuo zaidi wa yeye Mwenyewe na wetu sisi. Tunazidi kufahamu zaidi ile Nguvu ya Kuhuisha inayoishi na kukaa ndani yetu.

Hatuwezi hata kueleza jinsi tunavyojisikia. Tumemezwa na Roho wake. Ndio yote tuwazayo. Hakuna kitu kingine muhimu kwetu. Tunaona Neno Lake likifanyika Neno ndani yetu. Linalisha nafsi zetu. Tunaishi kila siku kumwabudu yeye, kumsifu, na kumshukuru kwamba tunaweza kusikia Sauti yake ikinena nasi.

Tunaposoma Kitabu chetu cha nyakati za Kanisa, ni vigumu kwetu kukiweka chini; mioyo yetu inalipuka. Kila siku huleta Ufunuo zaidi. Tunataka kuruka juu na kupaza sauti, kukimbia huku na huku chumbani na kupiga kelele: “Utukufu, Haleluya, Bwana apewe sifa.” “je, umelisoma hili?” “Nimeliwekea alama kwenye marejeo yangu pendwa, lakini sijawahi, KAMWE, kulisoma kama hivi hapo awali.” Yeye anatufunulia Biblia nzima kutoka Mwanzo hadi Ufunuo, nami najiona SISI WENYEWE KATIKA NENO LAKE.

Tunamwona Bibi-arusi huyo wa Kweli ambaye aliyedumu na Neno katika nyakati zote na hakudanganywa na udanganyifu mkuu wa Shetani. Alitaka kuabudiwa kama Mungu. Lakini wakati wote kulikuwa na yule BIBI-ARUSI WA KWELI, akidumu mwaminifu kwa Neno Lake. Hilo kundi dogo teule lililokaa na mjumbe Wake. Kama sisi tu, hawakuweza, na wasingeweza, kupatana. Walijua kulikuwa na NJIA MOJA PEKEE ya kuwa na hakika: kudumu na Njia Yake aliyoiandaa, Neno Lake, malaika Wake.

Jinsi gani Shetani amekuwa akidanganya wakati wote. Amefanya kazi katika Nyakati mbalimbali za Kanisa mpaka ametimiza malengo yake. Yeye Sasa amefanana sana na YULE ALIYE MKAMILIFU ili aweze kuwapoteza walio wateule kama yamkini….lakini Mungu apewe sifa, HAIWEZEKANI, HATUDANGANYIKI. Kwa nini? TULIKAA NA SAUTI YA MUNGU, NENO LAKE LILILOFANYIKA MWILI.

Hakuna njia ya mkato. Sauti ya Mungu ndiyo Njia Yake aliyoiandaa kwa ajili ya wakati huu. Tumeendelea kufanya kazi zake kwa uaminifu hadi mwisho. Tumepewa mamlaka juu ya mataifa, na ni watawala wenye nguvu, wenye uwezo, wasiokunjika ambao wanaoweza kukabiliana na hali yoyote kwa nguvu sana. Hata adui yetu aliyedhikika sana amevunjika. Udhihirisho wetu wa utawala, kwa Nguvu zake, ni kama ule wa Mwana.

Loo, jinsi tulivyotamani tungeweza kueleza kwa maneno jinsi tunavyojisikia. Siku moja tutafanya hivyo enyi marafiki. Tutaishi Milele na Bwana wetu, Malaika Wake, na sisi kwa sisi.

Kama yule bibi mzee mweusi huko Memphis, nasi tulijua alikuwa ndiye tulipomsikia. Kwa nini? Loo, sisi ni MMOJA WAO.

Je, ungependa Roho Mtakatifu azungumze nawe na kukuambia wewe ni nani? Njoo ujionee uwepo wa Bwana pamoja nasi Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,( ni saa MOJA JIONI ya Afrika Mashariki ) tunaposikia: Wakati wa Kanisa la Thiatira 60-1208 . Itabadilisha maisha yako.

Ndugu. Joseph Branham

23-0514 Wakati Wa Kanisa La Pergamo

Ujume: 60-1207 Wakati Wa Kanisa La Pergamo

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Wapendwa watoto wa Nabii,

Sisi ni Neno lililodhihirishwa, tukitiwa nguvu na Roho, tukisikia Sauti ya Mungu, kama anavyotutangazia, sisi ni BIBI-ARUSI WAKE.

Baba amelipatia Kanisa lake karama TISA za Roho, na huduma-TANO, lakini Yesu alisema: Katika KILA wakati nitamwandikia mtu MMOJA TU. ni Mjumbe MMOJA tu kwa kila wakati atakayepokea yale ninayouambia wakati huo. MJUMBE HUYO MMOJA ndiye mjumbe wa Kanisa la kweli.

Yeye anazungumza kwa niaba ya Mungu kwa ufunuo. Ujumbe huo ndipo unatangazwa kwa wote, lakini unapokelewa tu na kundi fulani linalostahili kwa njia fulani. Kila mtu binfsi wa kundi hilo ni yule aliye na uwezo wa kusikia yale Roho anayosema kwa njia ya mjumbe huyo. Wale wanaosikia hawapati ufunuo wao wa Kipekee, wala kundi fulani halipati ufunuo wao wa pamoja, BALI KILA MTU ANASIKIA NA KUPOKEA AMBAYO HUYO MJUMBE AMEISHAPOKEA TAYARI KUTOKA KWA MUNGU.

Jinsi tunavyopaswa kuwa waangalifu kusikia sauti MOJA, kwa kuwa Roho hana ila sauti moja ambayo ni sauti ya Mungu.

Kuna SAUTI MOJA YA MUNGU nayo haihitaji kuthibitishwa kama zile TISA, wala kuchujwa kama zile TANO; ni SAUTI MOJA TU, NENO SAFI!!

Je, tunaweza kuwasikiliza wahudumu wengine? Ndiyo, lakini msingi ni kusema TU yale yaliyonenwa na nabii. Wengine wanaweza, na wanapaswa, kuhimiza, kufundisha na kuhubiri; lakini Mungu ametutengenezea njia leo ZAIDI YA SIKU NYINGINE YOYOTE. Tunaweza kusikia yale hasa Mungu anayoliambia Kanisa.

Yeye alituambia tunapaswa kuwa waangalifu sana. YEYE ALITUAMBIA, SI MIMI, ya kwamba wao wanaongeza hapa, ama wanaondoa pale, na mara ujumbe si Halisi tena. Wakati tunaposikiliza kanda, Ni Neno kwa Neno, Bwana Asema hivi.

Thibitisho la Roho akaaye ndani ya mtu lilikuwa ni kukubali na KUFUATA yale nabii wa Mungu aliyotangazia huo wakati wake akiliweka kanisa kwenye utaratibu.

Ndio maana TUNAFUATA, na kusema, mchungaji wetu ni malaika-mjumbe wa saba na tunataka tu kusikia yale yeye anayosema. Kwetu sisi, Ni Mana Iliyofichwa.

Ufunuo ulimwagwa juu ya malaika-mjumbe wetu. Ufunuo wa Neno ulitolewa na kuandikiwa YEYE kwa ajili ya wakati wetu. Yeye ana Ufunuo mkubwa zaidi kidogo wa kile Kristo Alicho; wito wa juu zaidi kidogo, kuliko wengine wote. Ikiwa hatuwezi kuishi juu zaidi ya mchungaji wetu, basi sisi tunamtaka William Marrion Branham kama mchungaji wetu.

Tunajua wengine hawataona yale tunayoona, na Hawataamini mambo tunayoamini, lakini bado ni ndugu na dada zetu, nasi tutaishi Milele nao. Lakini lazima tubaki waaminifu kwa kile tunachoamini kuwa ni njia ambayo Mungu ametuonyesha kumwabudu na kumfuata.

Ni vyepesi sana kwa wengine kusema tunamwinua sana mjumbe, lakini kwa kweli, tunamnukuu yeye tu. Yakubidi kumshutumu hilo Bwana. Kwa maana ni Sauti ya Mungu inayosema mambo haya.

Hebu na tufungue mioyo na akili zetu na tusome yale Roho aliyotuambia kupitia malaika Wake:

Anayekuja ulimwenguni hivi karibuni, yule malaika mkuu wa Nuru atakayetujia, atakayetuongoza tutoke, Roho Mtakatifu mkuu, akija mamlakani, naye atatuongoza kwa Bwana Yesu Kristo. Labda hatajua hilo, bali atakuwa hapa moja ya siku hizi. Atafanya…Mungu atamtambulisha. Haitambidi kujitambulisha mwenyewe, Mungu atamtambulisha. Mungu atamthibitisha aliye Wake. Hivyo ndivyo Yeye alivyosema wakati Yesu alipokuwa hapa wala hawakumtambua, mnaona. Alisema, “Nisipozitenda kazi za Baba Yangu, basi msiniamini; bali nikizitenda kazi za Baba Yangu, wala hamwezi kuniamini Mimi, basi ziaminini zile kazi.” Hiyo ni kweli?

Je, Yeye si anajiita malaika mkuu wa Nuru wa wakati huu? Tunajua ni Roho Mtakatifu ndani yake, lakini yeye alisema: Labda hatajua hilo, bali atakuwa hapa moja ya siku hizi. Roho Mtakatifu hatamjua Yeye ni nani? Haitambidi kujitambulisha mwenyewe; Mungu atamtambulisha.

Kwa hiyo Yeye anasema, nabii wa wakati wetu ndiye malaika mkuu wa Nuru atakayetuongoza tutoke na kwa Yesu Kristo kwa njia ya Roho Mtakatifu kupitia yeye. Huo hapo Ufunuo wa Wakati wetu.

Ni nani atakayemtambulisha Bibi-arusi kwa Bwana? MCHUNGAJI WETU.

Lakini huyu nabii atakuja, na kama vile yule mtangulizi wa kule kuja kwa kwanza alivyopaza sauti, “Tazama Mwana-Kondoo wa Mungu aichukuaye dhambi ya ulimwengu,” vivyo hivyo bila shaka naye atapaza sauti, “Tazama Mwana-Kondoo wa Mungu anayekuja katika utukufu.” Atafanya jambo hili, kwa maana kama vile Yohana alivyokuwa mjumbe wa ile kweli kwa wateule, ndivyo alivyo na huyu mjumbe wa mwisho kwa wateule na kwa bibi-arusi aliyezaliwa kwa Neno.

Kuzijua Kweli hizi, na kuwa na Ufunuo MKAMILIFU wa Yeye katika siku hii, tumekuwa Bibi-arusi Wake aliyezaliwa kwa Roho, aliyejazwa na Roho.

FURAHI BIBI-ARUSI, HUYU NDIYE SISI TULIYE!

Wakati mtu aliyezaliwa kwa Roho, aliyejazwa na Roho anapoingiza Neno hilo ndani ya moyo wake na kuliweka kwenye kinywa chake kwa imani, mbona hilo ni kama tu Mungu akinena. Kila mlima hauna budi kuondoka. Shetani hawezi kusimama mbele ya mtu huyo.

Sasa upatanifu mkamilifu wa kweli upo kati ya Bwana Arusi na sisi, Bibi-arusi Wake. Yeye ametuonyesha Neno Lake la uzima, nasi tumelipokea. Hatutalitilia shaka kamwe. Kwa hiyo, hakuna kitu kinachoweza kutudhuru, hata kifo chenyewe.

FURAHI BIBI-ARUSI, HUYU NDIYE SISI TULIYE!

Neno limo ndani ya bibi-arusi (kama vile lilivyokuwa ndani ya Mariamu). Bibi-arusi ana nia ya Kristo kwa kuwa anajua kile Yeye anachotaka kifanywe kwa Neno. Anatekeleza maagizo ya Neno katika jina Lake kwa kuwa yeye anayo “Bwana asema hivi.” Ndipo Neno linahuishwa na Roho nalo linatimia. Kama vile mbegu ambayo imepandwa na kumwagiwa maji, inafikia mavuno kamili, ikitimiza kusudi lake.

Tumefika kwenye mavuno kamili na sasa tunatimiza kusudi Lake. Sisi hufanya tu mapenzi yake. Hakuna ye yote anayeweza kutufanya tutende vinginevyo. Tuna “Bwana Asema hivi,” la sivyo tunanyamaza. Tunajua ya kwamba ni Mungu ndani yetu, akifanya kazi, akilitimiza Neno Lake Mwenyewe.

Tunashangilia, kwani nabii alituona ng’ambo ya pazia la wakati sote tulipoziinua sauti zetu na kupaza sauti kwa upatanifu, “Tunategemea hilo!”

Njoo ukusanyike pamoja nasi Jumapili saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville, ( ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Tanzania )tunaposikia Sauti ya Mungu ikituletea siri ya: Wakati wa Kanisa la Pergamo 60-1207.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya Kusoma kwa maandalizi ya Kusikiliza Ujumbe :

Hesabu 23:8-9
Ufunuo 2:12-17, 17:1-5, 17:15

23-0507 Wakati Wa Kanisa La Smirna

Ujume: 60-1206 Wakati Wa Kanisa La Smirna

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Waamini Wa Kweli,

Sisi ni kama wana wa Israeli waliotoka Misri na wakakoma karibu na Nchi ya Ahadi. Sote tumesafiri pamoja. Sote tumeona miujiza ile ile ya Mungu; sote tumeshiriki mana ile ile na maji kutoka kwenye Mwamba uliopigwa. Sote  tumedai kuwa tunafuata Nguzo ya Moto. Lakini WAWILI TU ndio waliofika kwenye Nchi ya Ahadi wakati huo. Kwa nini? WAWILI TU NDIO WALIOKUWA WA KWELI AMA WAAMINI HALISI. Tofauti ilikuwa ni kitu gani kati ya wakati huo na sasa? Waamini wa kweli walidumu na Neno.

Kuna kundi moja tu maalum sana la watu ambao wanaweza kusikia yale Roho anayosema. Kundi moja maalum linalopokea Ufunuo wa kweli. Kundi hilo ni la Mungu. Wanasikia yale Roho anayosema na wameyapokea.

Sisi ndio kundi hilo maalum ambalo lina Roho wa Mungu. Sisi ndio tuliozaliwa na Mungu. Sisi ndio tuliobatizwa katika mwili wa Bwana Yesu Kristo kwa Roho Wake.

Ushuhuda wa kweli ni KUSIKIA Yale Roho asemayo. Roho ananena. Roho anafundisha. Hivyo ndivyo hasa Yesu alivyosema angefanya atakapokuja. Yohana 14:26, “Naye atawafundisha yote, na kuwakumbusha yote niliyowaambia.”

Yesu alituahidi kwamba angekua akiishi ndani ya kila mmoja wetu. Angetuongoza, kutusimamia na kutuelekeza kama watu binafsi. Lakini miaka 72 iliyopita leo, Mungu alinena kupitia malaika Wake mwenye nguvu na kuutangazia ulimwengu, “Mimi ni Sauti ya Mungu kwenu”. Aliambia kila kiumbe hai “Mimi, Roho Mtakatifu, nina SAUTI nitakayoitumia kusema nanyi na kuzifunua siri zangu zote”. Hakuwahi kamwe kupata nafasi ya Sauti Yake kurekodiwa ili tuweze kusikia Sauti Yake ikituzungumzia mdomo kwa sikio.

Kwa kusikia Sauti yake kwenye hizo kanda haitakubidi kushangaa, kutumaini, au hata kuomba kujua ikiwa kile unachosikia kama ni kweli. KILA mtu anachopaswa kufanya ni Kubonyeza Play, nao wanaweza kusikia Sauti ya Mungu ikiwatangazia, “Bwana Asema hivi”.

Je, unahitaji uponyaji: Bonyeza Play.
Unahitaji kuolewa: Bonyeza Play.
Unahitaji kuzikwa: Bonyeza Play.
Una swali moyoni mwako: Bonyeza Play. Una jambo unalopitia na unahitaji ushauri nasaha: Bonyeza Play.
Una uamuzi muhimu unaohitaji kufanya: Bonyeza Play.
Hujui ufanye nini na maisha yako: Bonyeza Play na usikilize Sauti ya Mungu, Roho Mtakatifu, aseme nawe mdomo kwa sikio.

Roho Mtakatifu ndiye nabii wa wakati huu. Aliuambia ulimwengu, hii ndiyo Sauti Niliyoichagua tangu asili iwe Sauti Yangu kwenu. Nitawajaza wengine na Roho wangu Mtakatifu, nami Nimewatuma kuwasaidia, Lakini Mimi Nina Sauti Moja tu ninayotangaza kuwa SAUTI YANGU. Hata nimepiga picha yangu pamoja naye ili kuuthibitishia ulimwengu, Msikieni Yeye.

Tafadhali msinielewe vibaya. Ndiyo, kuna watu wa Mungu waliojazwa na Roho Mtakatifu ambao amewaita kuwasaidia watoto Wake. Naomba ya kuwa mimi ni mmoja wao. Wao pia wanaweza kuwapa ushauri, faraja, na kuwaongoza katika safari ya maishani. Mungu amewaweka hapa kwa kusudi. Lakini ushauri uliyo MUHIMU zaidi, faraja na uongozi unaoweza kupokea ni Sauti ya Mungu ikizungumza nawe kwa Kubonyeza Play. Chochote ninachowaambia, ama mtu mwingine ye yote, lazima kwanza kitoke kwenye Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda.

Hakuna kitu kilicho muhimu zaidi katika maisha yako, kuliko kusikiliza Sauti ya Mungu ikisema nawe. Jiulize, je, kuna jambo lolote katika ulimwengu huu KUBWA ZAIDI ningaliweza kufanya, au ni muhimu zaidi katika maisha yangu, kuliko kusikiliza SAUTI ya Mungu iliyothibitishwa? Je, ni Kumsikiliza ndugu Joseph, HAPANA. Je, ni Kumsikiliza mtu mwingine yeyote, HAPANA. Hakuna CHOCHOTE KILICHO KIKUBWA ZAIDI YA SAUTI HIYO.

Ikiwa mtu yeyote ana Ufunuo wowote na wanaye Roho Mtakatifu katika maisha yao wanapaswa kusema AMINA. Hakuna kitu chochote kikubwa zaidi katika ulimwengu huu kuliko Kubonyeza Play .

Tunapaswa kuwa waangalifu jinsi gani katika wakati huu wa mwisho kukaa na Neno hilo. Kuanzia maneno ya papa, anayedai kuwa Halifa wa Mungu, hadi kubadilisha nukta moja ama deshi ya kile kilichonenwa. Machoni pa Mungu, WOTE ni UPINGA-NENO, UPINGA-KRISTO.

Sisi hatutaki kuwa kama watu wa siku za Samweli.

Wakati walipomwendea Samweli na kuomba wapewe mfalme, Samweli alifadhaika sana hata roho yake karibu izimie. Mungu alikuwa anawaongoza watu Wake kupitia kwa nabii huyu aliyewekwa wakfu, aliyethibitishwa kwa Maandiko naye akaona kwamba alikuwa amekataliwa…

Tunaifurahia miujiza, hekima, chakula na ulinzi wa Mungu. Tunauamini. Tunaupenda. Na isitoshe hatutaki kuukosa. Ni kwamba tu tanataka mfalme wa kutuongoza vitani…

“…TUNATAKA MFALME AMBAYE NI MMOJA WETU APATE KUTUONGOZA.”

Ndipo Mungu akamwambia Samweli. “Unaona, wao hawakukukataa wewe, lakini wamenikataa MIMI nisiwatawale.”

Kinyume Chake, sisi tunajisikia kama vile Elisha wakati akizungumza na Eliya. Eliya ALIMWAMBIA WAZIWAZI, (leo ingekuwa Kile alichosema kwenye kanda,) wewe kaa hapa niendapo. Elisha hangefanya hivyo, na hangeweza kufanya hivyo, alikuwa na UFUNUO wa Neno la Wakati Wake.

Sasa, tunawaona wakiendelea na safari, kuja shuleni. Naye akasema, “Kaa hapa sasa. Kuwa hapa, na utulie uwe mwalimu mzuri wa theolojia, na kadhalika. Na pengine, siku moja, unaweza kuwa mkuu wa chuo hapa. Lakini sina budi kushuka kwenda mbele kidogo.”

57 Unaweza kumwazia mtu wa Mungu akiridhika kuwa mkuu wa chuo, wakati Nguvu za Mungu zikiwa pale pale alipokuwa amesimama? La, bwana. Akasema, “Kama Bwana aishivyo na roho yako iishivyo, sitakuacha.” Napenda hilo.

Kaa nalo, haidhuru umeshushwa moyo kiasi gani, hata kama inatoka kwa mama yako, baba yako, au kutoka kwa mchungaji wako. Kaa Naye.

Kama Bwana aishivyo, nitakaa na Sauti ya Mungu kwa Kubonyeza Play, kwa maana ni Bwana Asema Hivi Kwangu.

Njoo uungane na kundi letu, Jumapili saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville, (Ni saa 1:00 MOJA JIONI Ya Tanzania na Kenya pia)tunapokusanyika ili kuisikia Sauti Yake ikizungumza nasi na kutuletea Ufunuo wa: Wakati wa Kanisa la Smirna 60-1206.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya Kusoma kabla ya Kusikiliza Ujumbe :

Ufunuo 2:8-11

23-0430 Wakati Wa Kanisa La Efeso

Ujume: 60-1205 Wakati Wa Kanisa La Efeso

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Dhahabu Safi Iliyofuliwa,

Jinsi gani Ninavyoshukuru kuungana pamoja na kila mmoja wenu, tukiingia katika Roho na kumsikiliza Mungu akizungumza nasi, mdomo kwa sikio. Hakuna mwisho kwa kile anachotufunulia. Mioyo yetu imejaa furaha. Nafsi zetu zinabubujika. Anawezaje mtu kuelewa kile tunachosikia?

Sikilizeni tu kile Bwana Mwenyewe anachotuambia: “Ninyi ndio Kanisa Langu la kweli, Bibi-arusi Wangu. Kwangu mimi, mmefananishwa na dhahabu SAFI. Haki yenu ni haki yangu. Sifa zenu ni sifa ZANGU mwenyewe tukufu. Utambulisho wenu wenyewe unapatikana ndani Yangu. Kile MIMI NIKO, mnakihakisi. Kile NILICHO NACHO, mnakidhihirisha.

KWANGU mimi, hakuna kosa ndani yenu, ninyi ni watukufu ndani na nje. Tangu mwanzo hadi mwisho, ninyi ni kazi Yangu…na kazi ZANGU zote ni kamilifu.

Hamtasimama kamwe hukumuni, kwa sababu dhambi haiwezi kuhesabiwa kwenu. Hata kabla ya misingi ya dunia, kusudi Langu lilikuwa ni kushiriki Uzima Wangu wa Milele pamoja NANYI.

Je, mtu anawezaje kufahamu Maneno haya? Akili zetu zinawezaje kufahamu kile kinachotendeka? Ni nini kimefunuliwa? Wazia jambo hilo, hatupaswi kulia mioyoni mwetu na kusema, “Loo, laiti ningalikuwa kule nyuma katika wakati wa kwanza wakati mitume walipotumwa kwanza.” HAKUNA haja ya sisi kuangalia nyuma, kwa sababu Yeye, ambaye habadiliki kamwe katika tabia au katika njia zake, Yeye yuko katikati yetu SASA, akizungumza nasi na kutuambia kuwa Yeye ni yeye yule jana, leo na hata milele. Huu ni wakati MKUU zaidi katika historia ya ulimwengu kuishi ndani yake.

Tunapigwa na kutakaswa, na kujazwa na mateso ambayo Kristo aliacha. Tunahesabiwa kama kondoo wa kuchinjwa. Tunauawa siku nzima. Tunateseka sana, lakini katika hayo yote, hatulipizi kisasi, wala hatusababishi wengine wateseke. Kwake, sisi ni dhahabu safi iliyofuliwa, sio kukunjwa, sio kuvunjwa, sio kuharibiwa, bali kufanywa kitu chenye uzuri na furaha milele kwa majaribu na majaribio ya maisha haya.

Sasa Yeye anawaonya wengine wote, “Rudini kwenye Upendo wenu wa Kwanza”. Jinsi gani Wanavyopaswa kuwa waangalifu kwani hupaswi kubadilisha HATA NENO MOJA, hata nukta au dashi. Hiyo ilikuwa ndio hila ya asili ya Shetani katika bustani ya Edeni. Neno moja tu likiongezwa, Neno moja tu likiondolewa, basi ni Mpinga-Neno.

Katika wakati huu wa mwisho anatuonya kutakuwa na manabii wengi wa uongo watakaotokea, wakiwaambia watu ya kwamba wasipowaamini wao na yale wanayosema , mtapotea.

KUNA NJIA MOJA PEKEE ya kuwa na Hakika HAKUNA KITU Kilichoongezwa, hakuna kilichoondolewa, hakuna kilichobadilishwa… kwa kusikiliza SAUTI YA MUNGU safi…KUBONYEZA PLAY.

Mshukuru Bwana kwa ajili ya mhudumu wa kweli, aliyefundishwa kwa uaminifu, ambaye si tu anawaambia kondoo wao umuhimu wa kusikiliza Ujumbe kila siku majumbani mwao, bali kwa kuwa viongozi wa kweli, kuweka Ujumbe Huu, Sauti Hii, Kanda Hizi, NAFASI YA KWANZA NA ILIYO YA KWANZA KABISA kwa watu walio katika makanisa yao.

Kwa kusema mambo haya, naeleweka vibaya na ninatuhumiwa kwa kuyagawa makanisa na kuwaambia watu wasiende makanisani. Hiyo si kweli. NENO linawatoa watu kutoka katika makanisa haya ambayo hayaweki kanda NAFASI YA KWANZA katika makanisa yao. Wana njaa ya kusikia Neno kutoka kwa Nabii wa Mungu. Wanajisikia HUO ndio Ujumbe na Sauti iliyo muhimu zaidi wanayotaka kusikiliza. Wanajisikia Ni Mapenzi Makamilifu ya Mungu kuzicheza kanda kanisani mwao.

Daima nimewaambia watu, “NENDENI KANISANI”. Wanapouliza: “Je, unahisi wahubiri bado wanaweza kuhubiri?” “Ndiyo.” Sijawahi kusema ama kuwazia kwamba hawapaswi. Kwa urahisi Ninawaambia wahubiri, waalimu, wachungaji, “Fanyeni kile Mungu alichowaitia, LAKINI TAFADHALINI, iwekeni hiyo Sauti yenyewe ya Mungu iliyo kwenye Kanda NAFASI YA KWANZA, SI HUDUMA YENU”.

Huo ndio UFUNUO WANGU. Wao yawabidi wafanye vile WANAVYOJISIKIA KUONGOZWA KUFANYA. Nina haki ya kuhubiri na kufundisha kile ninachojisikia. Kama Wao wanataka kusema Ndugu Branham kamwe hakuwahi kusema Kubonyeza Play Kanisani, Sauti yenyewe hasa ya Mungu wanayodai kuwa wanaifuata, hiyo ni juu yao.

Roho Mtakatifu ndiye, na daima amekuwa, akimwongoza Bibi-arusi Wake. Tunaamini Yeye anatuambia, “BONYEZENI PLAY, KAENI NA NABII WANGU, SAUTI YANGU, ROHO WANGU MTAKATIFU.”

Vema, tutakuwa na mashindano ya jambo hilo, basi, kama nabii Eliya kabla ya hapo . Na iwapo wewe ni mwana wa Mungu, utakaa pamoja na nabii wa Biblia hii. Ni Neno. Angalia ile saa, huo wakati.

Nabii wa Biblia ni nani, Neno, Roho Mtakatifu!

Roho Mtakatifu ndiye Nabii wa wakati huu; Yeye analihakikisha Neno Lake, akilithibitisha . Roho Mtakatifu alikuwa ndiye Nabii wa wakati wa Musa. Roho Mtakatifu alikuwa Nabii wa wakati wa Mikaya. Roho Mtakatifu, aliyeliandika Neno, anakuja na kulithibitisha Neno.

Roho Mtakatifu wa wakati huu anatuongoza Kupitia nabii Wake, kama jinsi alivyofanya katika kila wakati. Mungu kamwe habadilishi mpango Wake.

Kwa hiyo, unaalikwa kuja kuungana nasi katika kile tunachojisikia kuwa ndio Mpango wa Mungu kwa kumsikiliza Roho Mtakatifu akizungumza kupitia nabii Wake, na kutuongoza anapotuletea Ujumbe: 
Wakati Wa Kanisa La Efeso 60-1205 , saa 6:00 SITA MCHANA. Masaa ya Jeffersonville. ( ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Tanzania na Kenya pia .)

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma Kwa ajili ya maandalizi ya Kusikiliza Ujumbe :

Matendo 20:27-30
Ufunuo 2:1-7

23-0423 Ono La Patimo

Ujume: 60-1204E Ono La Patimo

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Wapendwa, Wapenzi Wa Neno la Mungu,

Inapendeza jinsi gani kuweza kuongea na kila mmoja wenu kama Wapenzi wa Neno la Mungu. Hakuna kitu kinachoweza kupachukua mahali Pake. Kuwa na nafasi ya kumsikiliza Bwana wetu kila siku ya maisha yetu, akisema nasi kupitia midomo ya mwanadamu, na kutuambia Yeye ni nani na SISI NI NANI. Hakuna mahali, hakuna sauti, hakuna kanisa, na hakuna mtu anayeweza kukuambia mambo haya kama SAUTI YA MUNGU.

Alituambia uvuvio wa Neno ulikuwa kwenye kanda. Yote tunayopaswa kufanya ni Kubonyeza Play na Roho Mtakatifu anakijaza chumba. Mjumbe wetu alikuwa akivuta Uzima, na nuru, kutoka kwenye rasilimali za bakuli hilo kuu. Utambi wake ulikuwa umezamishwa humo ndani.

Maisha yake yanawaka moto wa Roho Mtakatifu. Utambi wake (uhai) umezamishwa ndani ya Kristo. Kupitia huo utambi anaunyonya uzima ule ule wa Kristo, na kwa huo, anatupa mwangaza sisi, Bibi-arusi.

Kisha anatuambia sio tu kwamba utambi wa mjumbe Wake mwenye nguvu upo mle, bali sote tunanyonya kutoka kwenye chanzo kimoja. Sote tumetumbukizwa kwenye bakuli moja. Tumekufa kwa nafsi zetu na uhai wetu umefichwa katika Mungu kwa njia ya Kristo, umetiwa muhuri na Roho Mtakatifu.

Hakuna mtu anayeweza kututoa kutoka kwenye mkono Wake. Maisha yetu hayawezi kuchezewa. Uhai unaoonekana unawaka na kuangaza ndani yetu, ukitoa nuru na madhihirisho ya Roho Mtakatifu. Maisha yetu ya ndani, yasiyoonekana yamefichwa ndani ya Mungu na kulishwa kwa Neno la Bwana. Tunao Ufunuo wa Yesu Kristo katika siku yetu.

Jinsi gani Neno linavyolisha nafsi zetu. Hakuna lakulinganishwa nalo. Jinsi gani ameandaa njia ambayo Bibi-arusi, kutoka ulimwenguni kote, wanaweza kukusanyika pamoja ili kusikia Sauti ya Mungu kwa wakati mmoja. Haijalishi wakosoaji ama wanaoshuku wanasema nini, Mungu ametengeneza njia na ni harufu nzuri ya manukato Kwake. Ndio kwanza Atuambie kwamba atatukusanya pamoja sote mwishoni mwa siku ya tatu. Utukufu!!

Hebu sote na tukusanyike pamoja Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA , saa za Jeffersonville,( ni saa 1:00 MOJA JIONI Ya Tanzania)kusikia Sauti ya Mungu ikituletea Ufunuo wa Neno tunaposikia: Ono la Patmo 60-1204E.

Kwanza, ni lazima TUINGIE KATIKA ROHO kama tutakavyosikia;

Ile sauti iliyotangaza Neno Lake katika Bustani ya Edeni na juu ya Mlima Sinai, sauti ambayo ilisikika pia katika utukufu mkuu wa Mlima wa Kugeuzwa Sura, ilikuwa inatangaza mara nyingine tena, na wakati huu kwa yale makanisa saba pamoja na ufunuo mkamilifu na wa mwisho wa Yesu Kristo.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma ili kujitayarisha Kusikiliza Ujumbe.

Kumbuka kusoma na kusikiliza kitabu cha Nyakati Saba za Kanisa.

Isaya 28:8-12
Danieli 7:8-14
Zekaria 4:1-6
Malaki 4:1-2, 4:5
Mathayo 11:28-29, 17:1-2
Yohana 5:22
Waebrania 4:3-4, 4:7-10, 4:12
Ufunuo 1:9-20, 19:11-15

23-0416 Ufunuo Wa Yesu Kristo

Ujume: 60-1204M Ufunuo Wa Yesu Kristo

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa mti wa bibi-arusi,

Ni yubile iliyoje aliyonayo Mti wa Bibi-arusi. Mioyo na roho zetu zinawaka ndani yetu kuliko hapo awali. Anatembea na kuzungumza nasi, akifunua Neno Lake. Mambo yanatokea haraka sana hatuwezi kuendana nayo.

Tunalisikia Neno kamilifu la Mungu likidhihirishwa na Mti mkamilifu wa Nabii, ukihubiri Neno kamilifu la Nabii, likizaa tunda kamilifu la Nabii, kwa Neno kamilifu la Mungu.

Kila kitu kilichoharibiwa na kuliwa na wale wajumbe wanne wa mauti walioua Mti, sasa kimerudishwa tena na wajumbe wanne wa Uzima. Si wajumbe WATANO, si wajumbe wa huduma tano, si kundi; WAJUMBE wanne ndio wameurudisha Mti wa Bibi-arusi.

Tangu mwanzo wa wakati, Mungu amengojea siku na majira haya yatimie ili aweze kuliona tunda lake, katika wakati Wake, kwa majira ya nabii. Sisi ndio Tunda hilo. Haya ndio majira yenyewe. Wakati wa mavuno umefika.

Wikiendi hii ya Pasaka ilikuwa kama hakuna Pasaka nyingine ambayo mtu yeyote amewahi kuiona. Hatutakuwa kamwe jinsi tulivyokuwa. Uwepo kama huo wa Bwana. Nilikuwa nikingojea Unyakuo kufanyika sekunde yoyote.

Katika Biblia, Daudi alisema Maneno haya: Walinizua mikono na miguu yangu. Naweza kuihesabu mifupa yangu yote: Wao wanitazama na kunikodolea macho.

Watu walikuwa wamesoma na kusikia kifungu hicho kwa mamia ya miaka, lakini Yesu alipokuwa akining’inia pale mbele ya macho yao msalabani, Bibi-arusi lazima yawezakuwa alimtazama na kutambua, Leo, Maandiko Haya Yametimia mbele ya macho yetu.

Jinsi ambavyo lazima walijisikia walipotambua kwamba walikuwa wanaona, kwa macho yao, Maandiko hayo yakitimizwa, na walikuwa sehemu ya Neno lililoandikwa.

Ndio sisi SASA. Tunaishi katika siku ambazo Maandiko yote ya mwisho yanatimizwa mbele ya macho yetu; na sisi ni sehemu ya Maandiko hayo.

Yeye anatembea moja kwa moja kati yetu. Ni mwisho wa siku ya tatu. Ametokea na kutuonyesha ishara ya kufufuka kwake. Ni yeye yule jana, leo, na hata milele. Sisi ni matunda hai ya Uwepo Wake. Amedhihirishwa na anaonekana kwetu sote, Kanisa Lake.

YEYE ANALIFANYAJE JAMBO HILO?

Nabii ameondolewa kutoka katika dunia hii, Lakini Roho Mtakatifu yuko kwenye kanda, naye anaenda kwenye mataifa na ulimwenguni kote. NI HUDUMA HAI YA BWANA YESU KRISTO. Anamkusanya Bibi-arusi Wake wote pamoja kwa jambo moja pekee linaloweza, na litakalofanya hivyo: Neno Lake. Sauti yake. KUBONYEZA PLAY!

Leo, Maandiko haya Yametimia.

Yeye ndiye Mti wa Bwana-arusi kutoka katika Bustani ya Edeni. Lakini Mti wa Bwana-arusi bila wakike, hauwezi kuzaa matunda; Hana budi kuwa na Mti wa Bibi-arusi. Huyo ni WEWE. Mlizaliwa kwa kitu kile kile. Neno limefanyika mwili ndani YENU. Maisha yale yale yaliyo ndani ya Bwana-arusi yako sasa hivi ndani YENU.

Bibi-arusi anapaza sauti: Haleluya, Amina, Utukufu!!

Je, ni mambo gani aliyotuwekea akiba hapo mbele?

Lakini sababu ya wakati huu maalum ilikuwa ni kwamba tungeninii…Juu ya moyo wangu Roho Mtakatifu alikuwa ameweka ilani hii ya kusadiki, kwamba, “Kanisa katika siku hizi linapaswa kupata Ujumbe huu.” Kwa sababu, ninaamini ya kwamba ndio Ujumbe ulio muhimu sana wa Biblia, kwa sababu unamfunua Kristo katika Kanisa Lake kwenye wakati huu.

Kwa hiyo, Bibi-arusi atakuwa anakusanyika Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA , saa za Jeffersonville ,(Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Tanzania ) tunaposikia: Ufunuo Wa Yesu Kristo 60-1204M.

Ningependa kuwahimiza msikie, au kusoma, kila wiki katika Kitabu cha Nyakati za Kanisa, sura ambayo tumesikia kila Jumapili. Tutakuwa tukichapisha audio kwa Kiingereza kwenye Lifeline – Redio ya Sauti kila siku kwa nyakati tofauti, lakini jisikie huru kukisoma, kukisiklizia na kukisoma wiki nzima wakati wowote.

Hebu na tushangilie na kufurahi. Msiukazie ulimwengu huu na dhambi na fadhaa zinazotuzunguka pande zote. Hebu tusherehekee kwa yote anayotufanyia kila siku.

Katika siku za Musa, nina hakika watu waliendelea kumuuliza Musa,
“Tutaondoka lini mahali hapa? Tutatoka lini hapa?”

Naweza tu kumsikia Musa akiwatuliza watu na kusema:

“Mungu akiwa tayari. Lakini kwa sasa, furahieni yote anayowafanyia NINYI”.

Je! Mna vyura nyumbani mwenu? HAPANA.
Je! Mna nzige zilazo mimea yenu? HAPANA
Je! Mna maji ya kunywa yenye damu? HAPANA. Mnakunywa maji safi ya kisima kinachobubujika. Ninyi kaeni kitako tu na mfurahie yote Anayofanya na kuwafunulia.

Ni kifo, maangamizi na hukumu kwao. Lakini kwako wewe, hizi ni siku zilizo kuu zaidi duniani. Kuwa mwenye furaha, amani na shangwe. Msifu tu Bwana kwa yote anayofanya, na utarajie yale atakayofanya hapo mbele.

Ndugu. Joseph Branham