23-0528 Wakati Wa Kanisa La Sardi

Ujume: 60-1209 Wakati Wa Kanisa La Sardi

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Wanaostahili, Wenye Haki,

Enyi Tai, mko tayari kukusanyika pamoja Jumapili hii kusikia Sauti tamu ya Yesu ikinena nanyi na kusema:

“ninyi Mnastahili.” “Ninyi ni wangu.” “Ninyi ni wenye Haki.” “Mtatembea pamoja nami katika mavazi meupe.” “Majina yenu yameandikwa Mbinguni.”

Haya si maneno yangu, bali ni Maneno hasa ya Baba yetu wa Mbinguni akinena na WEWE, Bibi-arusi Wake mteule. Roho Mtakatifu amekuja tena na kuishi katika mwili wa mwanadamu, ili aweze kunena mdomo kwa sikio na Bibi mteule wake Maneno haya ya ajabu.

Inapendeza kuyasikia kutoka kwangu, au mtu ye yote ambaye angesema “Yesu alisema”, lakini kumsikia YEYE akisema kupitia Sauti yake teule; ile
aliyozoea kukuambia, kibinafsi… hakuna kabisa kilicho kikuu zaidi.

Kuna sauti nyingi ambazo Mungu hutumia kuleta Neno lake ulimwenguni. Amewachagua na kuwaweka wawe baraka kwa ulimwengu na kwa Bibi-arusi Wake.

Yesu alipokuwa hapa duniani katika mwili wa mwanadamu, Alikuwa pia amewachagua watu, mitume Wake, wamfuate Yeye na kusema kwa niaba Yake yale walioona kuzidiwa na waliosikia. Watu hawa ndio aliowatuma kuieneza Injili, habari njema kwamba Masihi amekuja; Alikuwapo, duniani pamoja nao. Aliwatuma wawili wawili kutangaza Habari Njema hii na kuwaleta watu wote kwake yeye.

Alipokuwa amewakusanya pamoja usiku mmoja, aliwauliza, “Watu huninena mimi kuwa ni nani?” Wakamjibu, “Wengine husema Wewe ni Eliya; wengine husema Wewe ni Yohana Mbatizaji.” Lakini yeye akasema, “Lakini NINYI MNASEMA Mimi kuwa ni nani?” Ndipo Petro akanena maneno hayo makuu, “Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai.” Yesu akamjibu, akasema, Mwili na damu havikukufunulia hili, Petro, bali Baba yangu aliye mbinguni amekufunulia hili, na juu ya mwamba huu(Ufunuo) nitalijenga kanisa langu.”

Ulimwengu umejikwaa pande zote kwenye siri hii kuu. Watu wengine wanaamini alikuwa akimaanisha Petro. Wengine wanaamini kuwa ni mwamba uliokuwa umelala pale. Wengine wanaamini ilikuwa ni Yesu. Lakini kwa Ufunuo, tuliopewa na Roho Mtakatifu, tunajua ulikuwa ni UFUNUO WA YEYE ALIKUWA NANI.

Baada ya kifo cha Yesu, kuzikwa na kufufuka, siku ya Pentekoste, walitumwa kuuambia ulimwengu Habari hii Kuu. Petro alichaguliwa tena kuwa msemaji na kwenda mbele ya watu na kutangaza jinsi ya kupokea Roho wake Mtakatifu. Alisema, hamna budi kutubu na kubatizwa katika Jina la Bwana Yesu Kristo.

Ni nafasi iliyoje ambayo Roho Mtakatifu alikuwa ameweka juu ya Petro. Tunaweza tu kuwazia jinsi watu walivyomtazama. Yeye alitembea pamoja na Yesu alipokuwa hapa duniani katika mwili. Yeye alikuwa rafiki Yake. Alikuwa kando Yake kila siku. Yule ambaye alikuwa amemchagua kumpa ule Ufunuo. Lakini Mungu alikuwa amemchagua MTU MWINGINE kuwa nabii Wake: Paulo.

Wakati Petro alipofika Antiokia kuwa pamoja na Paulo, alikuwa akila na kunywa pamoja na watu wa mataifa. Lakini kundi la watu lilipokuja kutoka kwa Yakobo, alijitenga na kuogopa. Paulo alimkemea waziwazi mbele ya wale wengine na kusema haenendi sawa sawa na ile kweli naye alistahili hukumu. Ndugu Branham alisema Petro alizidiwa na wale wa Dini ya Kiyahudi.

Je, jambo hili linatuambia nini kwa ajili ya siku hii? Haijalishi ni nani. Kiasi gani walivyo na Roho Mtakatifu. Wana mamlaka gani ama wito gani. NI LAZIMA UKAE NA NABII MTEULE WA MUNGU KUWA YAKINI YAKO. KWA MAANA YEYE, NA YEYE PEKE YAKE, NDIYE MFASIRI WA KIUNGU WA NENO LA MUNGU.

Hili si kinyume na Petro au mwanafunzi yeyote aliyechaguliwa na Mungu, wakati huo ama sasa. Wamechaguliwa kueneza Injili, lakini Mungu alikuwa amemchagua MTU MMOJA juu ya Kanisa Lake. Yeye peke yake ndiye aliyekuwa nabii aliyechaguliwa na Mungu akiwa na Bwana Asema hivi, si wao. Wana mahali pao, lakini Yeye ana NABII MMOJA wa kuliweka Kanisa Lake katika utaratibu, akiwa na Neno la mwisho kwa ajili Bibi-arusi Wake.

Hili linatuonyesha jinsi gani tunavyopaswa kuwa waangalifu kuisikia Sauti ya Mungu iliyothibitishwa kwa ajili ya wakati wetu. YULE Aliyemchagua kuwa mfasiri wa kiungu wa Neno Lake. HAKUNA KITU KIKUBWA kuliko kuisikia Sauti yake ikinena kupitia malaika Wake; Sauti ya chaguo Lake , si letu.

Tunaona katika nyakati zote jinsi Mungu alivyo na kundi teule la watu ambao wangekaa NA NENO LAKE na mjumbe Wake mteule. Sauti hiyo inatutangazia sisi kila siku sisi ni nani, MMOJA WAO.

Yeye angetuma watengenezaji kwenye kanisa Lake, lakini LEO HII, Yeye alimtuma mrejeshaji Wake; “Nitarejesha, asema Bwana, nami nitaigeuza mioyo ya watoto, kwa kuwa ninayo mengi ya kuwaambia katika siku za Sauti Yangu.”

Umealikwa kuja kuisikiliza hiyo Sauti, Jumapili saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville, ( ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki ) anapozungumza nasi na kutuonyesha Lile Kanisa la Kweli na la uwongo Katika kipindi cha: Wakati wa Kanisa la Sardi 60-1209.

Ndugu. Joseph Branham