24-1124 Wakati Wa Kanisa La Filadelfia

UJUMBE: 60-1210 Wakati Wa Kanisa La Filadelfia

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bi Yesu Kristo,

Je! Jumapili hii itashikilia kitu gani kwa ajili ya Bibi-arusi wa Yesu Kristo? Ni yapi yote Roho Mtakatifu atakayotufunulia? Utimilifu Mkamilifu. Sasa tutafahamu kikamilifu kwa Ufunuo, kitu chenyewe ukilinganisha na mfano wake na kitu chenyewe na kivuli chake. Yesu ndiye mkate wa kweli wa Uzima. Yeye ndiye wote wa Hilo. Yeye ni Mungu Mmoja. Yeye ni Waebrania 13:8. Yeye ndiye MIMI NIKO.

Kristo, akiisha kutokea katika mwili na kumwaga Damu Yake mwenyewe, ameziondoa dhambi zetu mara moja na kwa yote kwa toleo la nafsi Yake; kwa hiyo sasa ametufanya sisi kuwa WAKAMILIFU. Uhai Wake mwenyewe umo ndani yetu. Damu Yake imetusafisha. Roho Wake hutujaza. Mapigo Yake TAYARI yametuponya. Neno Lake liko ndani ya mioyo na mdomo wetu. Ni Kristo katika maisha yetu na si kitu kingine chochote, kwani kila kitu maishani mwetu hufifia na kuwa duni, isipokuwa Yeye na Neno Lake.

Mioyo yetu itajawa na furaha anapotuambia kwamba kwa uamuzi wa kiungu, Yeye alijua ni nani hasa angalikuwa Bibi-arusi Wake. Jinsi alivyotuchagua. Yeye alituita. Alitufia sisi. Alitununua na sisi ni mali Yake, na ni Wake peke Yake. Yeye hunena, nasi tunatii, kwa maana hiyo ndiyo furaha yetu. Sisi ni mali Yake peke Yake Naye hana mwingine ila SISI. Yeye ni Mfalme wetu wa Wafalme nasi ni ufalme Wake. Sisi ni mali Yake ya milele.

Yeye atatutia nguvu na kutuangazia kwa Neno la Sauti Yake. Ataeleza waziwazi na kufunua kuwa Yeye ndiye Mlango wa kondoo. Yeye ni Alfa na Omega. Yeye ni Baba, Yeye ni Mwana, na Yeye ni Roho Mtakatifu. Yeye ni Mmoja, nasi tu Mmoja na Naye na ndani Yake.

Yeye atatufundisha subira, kama alivyomfundisha Ibrahimu, kwa kueleza jinsi tunavyopaswa kungojea kwa subira na kuvumilia ikiwa tunataka kupata ahadi yoyote.

Yeye atatuonyesha waziwazi siku hasa tunayoishi. Jinsi zile pilikapilika za ekumeni zitakavyopata nguvu kisiasa, na kuishurutisha serikali kuwafanya wote waungane nao aidha moja kwa moja ama kwa kufuata kanuni zilizofanywa sheria hivi kwamba hakuna watu watakaotambuliwa kama makanisa isipokuwa chini ya uongozi wa moja kwa moja ama usio wa moja kwa moja wa halmashauri yao.

Yeye atafunua jinsi gani wengi sana watakubaliana nao, wakidhani wanamtumikia Mungu katika utaratibu uliowekwa wa shirika. Bali Yeye anatuambia sisi, “Msiogope, kwa maana Bibi-arusi hatadanganywa, sisi tutadumu na Neno Lake, Sauti Yake.”

Litakuwa jambo lakutia moyo jinsi gani kumsikia Yeye akituambia: “Shika sana, vumilia. Usife moyo, bali vaa silaha zote za Mungu, kila silaha, kila karama niliyokupa iko mikononi mwetu. Usivunjike moyo kamwe kipenzi, endelea tu kuangalia mbele kwa furaha kwa sababu utatiwa taji na Mimi, Mfalme wako wa Wafalme na Bwana wa Mabwana, Mumeo.”

Ninyi ndio kanisa Langu la kweli; hekalu halisi la Mungu kwa Roho Wangu Mtakatifu aishiye ndani yenu. Mtakuwa nguzo katika hilo hekalu jipya; ule msingi utakaoshikilia sehemu ya juu. Nitawaweka kama washindi pamoja na mitume na manabii, kwa maana Nimewapa Ufunuo wa Neno Langu, wa Mimi Mwenyewe.

Yeye atatufunulia waziwazi kwamba majina yetu yaliandikwa katika Kitabu Chake cha Uzima cha Mwana-Kondoo kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu. Kwa hiyo tutakuwa mbele ya kiti Chake cha enzi usiku na mchana kumtumikia hekaluni Mwake. Sisi tuko chini ya ulinzi maalum wa Bwana; sisi ni Bibi-arusi Wake.

Tutakuwa na jina jipya kwa kulichukua jina Lake. Litakuwa ndilo jina tulilopewa sisi wakati anapotuchukua Kwake. Tutakuwa Bi Yesu Kristo Wake.

Yerusalemu mpya ukishuka kutoka mbinguni kwa Mungu, Bibi-arusi aliyekwisha kupambwa kwa Mumewe. Mauti haitakuwapo tena, huzuni, wala kilio. Wala maumivu hayatakuwapo tena kwa kuwa mambo ya kwanza yamekwisha kupita. Ahadi zote nzuri za Mungu zitatimizwa. Badiliko litakamilika. Mwana-Kondoo na Bibi-arusi Wake watakaa milele katika ukamilifu wote wa Mungu.

Mpendwa Bi Yesu Kristo, OTA JUU YAKE. Itakuwa nzuri zaidi kuliko vile unavyoweza kuwazia.

Ninamwalika kila mtu aje kuungana nasi Jumapili hii saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,( saa 2:00 MBILI USIKU ya Afrika Mashariki ) wakati Mume wetu, Yesu Kristo, anenapo kupitia malaika-mjumbe Wake wa saba mwenye nguvu na kutuambia mambo haya yote.

Ndugu. Joseph Branham

Ujumbe: Wakati Wa Kanisa la Filadelfia 60-1210