UJUMBE: 60-1207 Wakati Wa Kanisa La Pergamo
- 24-1103 Wakati Wa Kanisa La Pergamo
- 23-0514 Wakati Wa Kanisa La Pergamo
- 20-1122 Wakati Wa Kanisa La Pergamo
- 19-0203 Wakati Wa Kanisa La Pergamo
- 16-0320 Wakati Wa Kanisa La Pergamo – Preliminari
Mpendwa Bibi-arusi Bikira Safi,
Je! Mmekuwa mkifurahia Nyakati Saba za Kanisa? Mungu anampa Bibi-arusi Wake ufufuo kuliko hapo awali. Yeye anatupa Ufunuo zaidi, Imani zaidi, na hakikisho zaidi kujua sisi ni nani, na kile tunachofanya kwa kukaa na Neno, Njia Yake aliyoiandaa kwa ajili ya siku hii.
Sasa Yeye anatuambia: “Kuanzia ibada ya Jumapili na kuendelea, vaeni mawazo yenu ya kiroho. Acha Roho Mtakatifu alizamishe Hilo ndani na myashike matumizi ya kiroho katika yote nitakayofanya. Ni Neno Langu lililohuishwa na Roho lililonenwa na nabii Wangu wa Malaki 4.”
Hebu na tusome na tuyapate machache ya Maneno Yake nasi tutumie mawazo yetu ya kiroho kuyahusu.
Mungu alimweka kiongozi Wake aliyejazwa Roho kwa ajili ya kundi Lake lililojazwa na Roho; malaika Wake; Naye akatia juu yake muhuri wa jina, bali haimpasi kulifunua. Hapaswi kumwambia mtu, mnaona. “Hakuna mtu ajuaye ila yeye mwenyewe.”
Kwa hiyo Mungu alimpa Bibi-arusi Wake kiongozi aliyejazwa na Roho kwa ajili ya kundi Lake lililojazwa na Roho. KIONGOZI, SIO VIONGOZI kwa ajili ya kundi Lake lililojazwa na Roho.
Anayekuja ulimwenguni hivi karibuni, yule malaika mkuu wa Nuru atakayetujia, atakayetuongoza tutoke, Roho Mtakatifu mkuu, akija mamlakani, naye atatuongoza kwa Bwana Yesu Kristo.
Malaika mkuu wa Nuru. Malaika mkuu wa Nuru ni nani kwa wakati huu wa mwisho? William Marrion Branham. Yeye hazungumzi juu ya Roho Mtakatifu. Yeye tayari amekwishakuja naye anasema atakayekuja.
Atakaye TUONGOZA TUTOKE. Kwa kweli tunajua na kuamini kwamba ni Roho Mtakatifu anayetuongoza, lakini Yeye ameweka wazi malaika Wake na Roho Mtakatifu pamoja na kusema Yeye (Roho Mtakatifu Wake) atakuwa akituongoza (KUPITIA) malaika Wake mkuu wa Nuru.
Yeye anaendelea kuwaunganisha pamoja kwa kusema:
Labda hatajua hilo,
Yeye hasemi Roho Mtakatifu hatamjua ni nani, bali malaika-mjumbe Wake wa duniani yule ambaye Yeye amemchagua KUTUONGOZA TUTOKE.
Bali atakuwa hapa moja ya siku hizi. Atafanya… Mungu atamtambulisha. Haitambidi kujitambulisha mwenyewe, Mungu atamtambulisha. Mungu atamthibitisha aliye Wake.
Tena, Yeye hasemi Roho Mtakatifu atakuwa hapa MOJA YA SIKU HIZI, bali malaika Wake mkuu wa Nuru ili kumwongoza Bibi-arusi Wake. Haitambidi kujitambulisha mwenyewe, Mungu atamtambulisha kiongozi Wake mkuu kwa Bibi-arusi Wake Mwenyewe kwa UFUNUO.
Je, umeyashika matumizi ya kiroho? Je! unaona malaika wa Nuru ni nani ambaye Mungu alimchagua kumwongoza Bibi-arusi Wake? Je! Inasema hapa ati kijiti kimepokezwa viongozi wengine?
Kamwe hutaweza kuishi juu zaidi ya mchungaji wako. Kumbuka hilo tu, unaona.
Ingawa wengine wanaweza wasituelewe na kutudhihaki, jinsi sisi tunavyofurahi na tunavyoshukuru kweli kwa Ufunuo kusema, WILLIAM MARRION BRANHAM NDIYE MCHUNGAJI WETU.
Sasa kwa kuwa kila moja ya jumbe hizi umeelekezwa kwa ‘malaika’—(mjumbe wa kibinadamu) wajibu mkubwa sana na pia majaliwa makuu sana ni fungu lake.
Ujumbe ulielekezwa kwa malaika Wake, kisha malaika Wake anampa huo Bibi-arusi; si wahudumu tu, bali kwa BIBI-ARUSI WAKE WOTE Nao upo kwenye kanda kwa wote kuusikia. Hauwezi kuongezwa kwake au kuondolewa kitu kwake, Nao HAUHITAJI FASIRI YO YOTE.
“Hivi karibuni Yeye atakuja. Na atakapokuja, Yeye atakuja kwako kwanza. Nawe utahukumiwa kulingana na Injili uliyohubiri, nasi tutakuwa raia wako.” Nikasema, “Wataka kusema ninawajibika kwa hawa wote?” Akasema, “Sisi sote. Wewe ulizaliwa kiongozi.”
Wakati siku ile kuu ya hukumu itakapokuja, Yeye anakuja kwanza kwa malaika Wake wa Nuru naye atamhukumu yeye kwanza kulingana na injili aliyohubiri. Sisi ni RAIA WAKE. Yeye anawajibika kwa kila mmoja wetu kwa kuwa yeye alikuwa KIONGOZI aliyechaguliwa na Mungu.
Weka matumizi yako ya kiroho kwenye jambo hilo. Tutahukumiwa kwa yale ambayo malaika wa Mungu aliyosema. Kwa hiyo, unataka kubahatisha kuhusu uzima wako wa milele kwa kile mtu fulani anachosema ALISEMA wakati wewe unaweza kusikia moja kwa moja kutoka KWAKE?
Anawezaje mtu yeyote kuamini kuwa kuna HUDUMA MUHIMU KULIKO ILE ILIYO KWENYE KANDA. Ikiwa unaamini hivyo, au umeshawishiwa hivyo kwa hoja, ni afadhali urudi kwenye NENO LA ASILI; kwa maana utahukumiwa kwa maneno yaliyo kwenye kanda. Dumu na Neno kama vile Lilivyonenwa.
Lakini huyu nabii atakuja, na kama vile yule mtangulizi wa kule kuja kwa kwanza alivyopaza sauti, “Tazama Mwana-Kondoo wa Mungu aichukuaye dhambi ya ulimwengu,” vivyo hivyo bila shaka naye atapaza sauti, “Tazama Mwana-Kondoo wa Mungu anayekuja katika utukufu.” Atafanya jambo hili, kwa maana kama vile Yohana alivyokuwa mjumbe wa ile kweli kwa wateule, ndivyo alivyo na huyu mjumbe wa mwisho kwa wateule na kwa bibi-arusi aliyezaliwa kwa Neno.
Ni nani atakayetutambulisha kwa Bwana Yesu? Malaika Wake mkuu wa Nuru, William Marrion Branham.
Njoo uwe Bibi-arusi Bikira Safi pamoja nasi tunapomsikia malaika-mjumbe Wake mkuu akituletea Ufunuo zaidi, Jumapili saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni saa 2:00 MBILI USIKU ya Afrika Mashariki) tunaposikia Ujumbe 60-1207 – “Wakati wa Kanisa la Pergamo.”
Ndugu. Joseph Branham