All posts by admin5

23-1231 Kukata Tamaa

UJUMBE: 63-0901E Kukata Tamaa

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Baba mpendwa,

Tumecheza muda mrefu vya kutosha. Tumehudhuria kanisa muda mrefu vya kutosha. Tangu kuusikia Ujumbe, ile Ishara, imemtupa Bibi-arusi Wako katika hali ya kudhikika.

Tunajua jambo fulani linakaribia kutukia. Wakati umekaribia. Tunataka Uje ututoe katika ulimwengu huu. Tunataka kuwa pamoja na Wewe. Tunahisi hali ya kudhikika ndani kabisa ya nafsi zetu.

Je! hivi tutalizungumzia tu? Je! tumedhikika vya kutosha? Je! tunakulilia Wewe mchana na usiku kama tunavyopaswa?

Loo, Kanisa, amka na ujitikise! Finya dhamira yako, amka katika saa hii! Hatuna budi kukata tamaa ama tutaangamia! Kuna jambo linalokuja kutoka kwa Bwana! Ninajua jambo hilo kwamba ni BWANA ASEMA HIVI. Kuna jambo linalokuja, na ni afadhali tukate tamaa. Ni kati ya uzima na mauti. Litapita katikati yetu wala hatutaliona.

Tunajua inahitaji hali ya kudhikika kukuleta Wewe jukwaani. Hatuna budi Tulipate sasa hivi ama tuangamie. Bwana, tujalie tudhikike kuliko hapo awali, ndipo utajitokeza jukwaani na kuja kumchukua Bibi-arusi Wako anayengoja.

Tusaidie Baba kujiingiza kwa nguvu. Si kutembea tu na kuingia ndani Yake kwa urahisi, bali kujiingiza ndani yake kwa nguvu. Sio tu kulizungumzia na kuendelea na maisha yetu ya kila siku. Tunataka kukutafuta kwa mioyo yetu yote, kwa roho zetu zote na kwa akili zetu zote. Bwana, tusaidie.

Tunajua tumekukosa mara nyingi, Bwana, lakini ulituambia kama tukishindwa, hilo halina uhusiano wo wote na jambo hilo; sisi ni wenye kushindwa kwanza, lakini tuna Wewe umesimama hapo na mkono wenye nguvu na unaweza kutushika chini na kutuinua juu ya maji.

Nabii alitutangazia ya kwamba Wewe ungepita juu yetu wakati tu unapoona ile Ishara ikiwa imewekwa. Bwana, tumefuata maagizo Yako na tumeiweka ile Ishara na kufanya nyumba zetu kuwa Kanisa la Kanda, tukisikiliza na kuamini kila Neno.

Yeye hutambua tu I—Ishara. Huo ndio Ujumbe wa wakati huu! Huo ndio Ujumbe wa siku hizi! Huo ndio Ujumbe wa wakati huu! Katika Jina la Yesu Kristo, upokeeni!

Sisi tuna Hakika kabisa, na tunaamini na kuweka kila kitu kulingana na yale nabii aliyotuambia.

Tunaamini kila kitu kinafanyika na hutokea kwa wakati Wako mkamilifu. Hakuna kitu kilicho nje ya mahali. Tumeiona miujiza Yako yote, nasi tumesikia na kuja chini ya ushahidi wa ile Ishara.

Sasa wakati tukiwa chini ya ushahidi wa ile Ishara, tutaula Ushirika Jumapili hii katika hali ya kudhikika. Kwa maana tunajua Wewe uko tayari kutoa hukumu.

Jalia tuule kama mfano wa Pasaka, wakati ilipoliwa kwa dharura, katika wakati wa kudhikika. Tupo katika kudhikika tena leo Baba.

Tunashukuru, Bwana, kwamba tunaweza kutazama nyuma kwenye mwaka huu na kuona yote ambayo umetufanyia. Umelifunua Neno Lako na kutupa Ufunuo juu ya Ufunuo kuliko hapo awali.

Sasa tunajua sisi ni wana na binti Zako. Sisi ndiye Bibi-arusi-Neno kamilifu Wako ambaye Umemngojea kwa muda mrefu sana. Ni Wewe, unayeishi na kukaa ndani yetu. Ulituchagua, ukatujua sisi tangu zamani na sasa unakuja kutuchukua.

Bwana, jalia tukutafute mchana na usiku. Na tuwe wenye kudhikika sana kukulilia Wewe. Jalia tujiingize kwa nguvu zaidi ya tulivyowahi kufanya hapo awali. Huu ukawe ndio mwaka wewe utakaokuja kutuchukua. Tunakupenda Baba, na tunataka kuwa katika Mapenzi yako makamilifu. Njoo uwe nasi tunapoungana saa 11:00 KUMI NA MOJA JIONI, saa za Jeffersonville, kuizunguka Sauti Yako na kukusikia Wewe ukituambia jinsi ya kuingia katika : Kudhikika (Kukata Tamaa) 63-0901E. Kisha uwe pamoja nasi tunaposhiriki katika kudhikika, Meza ya Bwana.

Hizi ndizo siku kuu za maisha yetu Baba. Kwa maana tunajua Unakuja upesi kutupeleka kwenye Makao yetu ya Baadaye pamoja nawe. Tunatazamia kila siku kwa hamu kubwa wale watakatifu ambao wametutangulia. Tunajua pindi tuwaonapo, ule wakati wa kuja kwako umefika….UTUKUFU!!!

Tuko katika hali ya Kudhikika kwa ajili ya siku hiyo, Baba.

Ndugu. Joseph Branham.

Maandiko ya kusoma kabla ya ibada:

Kutoka 12:11
Yeremia 29:10-14
Luka 16:16
Yohana 14:23
Wagalatia 5:6
Yakobo 5:16

23-1224 Kwa Nini Bethlehemu Mdogo?

UJUMBE: 58-1228 Kwa Nini Bethlehemu Mdogo?

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi Aliyeweka Ile Ishara,

Ningependa sote tujitayarishe kwa ajili ya ibada ya kipekee sana ya Ushirika wa Nyumbani katika Mkesha wa Mwaka Mpya, Jumapili, Tarehe 31 Desemba. Tutausikia Ujumbe, 63- 0901E Kudhikika, ambao Ndugu Branham anaingia katika ibada ya Ushirika na ya kutawadhana Miguu kuelekea mwisho wa kanda.

Kwenye Voice Radio Ujumbe utachezwa(kwa Kiingereza peke yake), na mfuate mpangilio wa ibada kama jinsi tulivyofanya katika ibada zilizopita za Ushirika wa Nyumbani, ikiwemo muziki wa piano wakati wa sehemu ya ibada ya Ushirika, na Nyimbo za Injili wakati wa Kutawadhana Miguu. Tutaanza ibada saa 11:00 KUMI NA MOJA JIONI. majira ya Jeffersonville. Kwa wale ninyi mlio nchi za ng’ambo, tafadhali jisikieni huru kuicheza kanda hii na kushiriki Ushirika katika masaa ya nchi zenu ili mshiriki Ushirika kabla ya saa sita usiku ya 2023.

Siwezi kufikiri njia bora zaidi tunayoweza kuumaliza mwaka huu wa 2023, na kuuanza mwaka mpya wa kumfanyia kazi Bwana katika 2024, kuliko kunyamaza mbele zake, kudhikika zaidi Kwa ajili yake, kushiriki Meza Yake, kuombea na kusameheana mmoja kwa mwingine, kuiosha miguu ya watakatifu Wake, na kulisikia Neno Lake. Hii itakuwa jioni ya kipekee iliyoje.

Zilizoorodheshwa hapa chini ni anuani za njia za kupata na kutayarisha divai na mkate wa Ushirika.

Ninashukuru sana kwamba Bwana ameiandaa njia kwa sisi kuungana pamoja kwa ajili ya hili tukio takatifu jinsi hii. Hakika natazamia kukutana nanyi nyote Mezani Pake.

Jumapili hii, tutasikia ujumbe wa Krismasi: Kwa nini Bethlehemu Mdogo? 58-1228 saa 6:00 SITA MCHANA. saa za Jeffersonville.( Ni saa 2:00 MBILI USIKU ya Afrika Mashariki)

Mungu awabariki,

Ndugu Joseph Branham

Jumapili, Desemba 24, 2023

58-1228 Kwa Nini Bethlehemu Mdogo?
saa 6:00 SITA MCHANA. Saa za Jeffersonville ( Ni saa 2:00 MBILI USIKU ya Afrika Mashariki )

Jumapili, Desemba 31, 2023

63- 0901E Kudhikika/pamoja na Ushirika wa Nyumbani na Kutawadhana Miguu
Saa 11:00 KUMI NA MOJA JIONI saa za Jeffersonville

https://branhamtabernacle.org/en/streaming/viewservice/259609A1-17BB-458F-A4AC-C3EBFF4D53E8

https://branhamtabernacle.org/en/articles/view/1212021_InstructionsToObtainCommunionWineFeetWashingBins

23-1217 Ile Ishara

UJUMBE: 63-0901M Ile Ishara

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Kipenzi Changu,

Moyo wangu unabubujika tu ninapowaona ninyi nyote mkikusanyika pamoja kuizunguka Sauti Yangu, mkisikia Neno Langu, ninapozungumza nanyi kupitia malaika Wangu.

Inanifurahisha sana kujua kwamba mnao Ufunuo wa ni nani niliyemchagua kuwa Sauti Yangu kwenu. Kuamini kila Neno alilonena halikuwa neno lake, bali Neno Langu kwenu.

Hiyo ilikuwa ni ya muhimu sana Kwangu, Nikaifanya irekodiwe na kuhifadhiwa kwa ajili yenu, ili mweze kuisikia tena na tena. Sikutaka kamwe msahau nilichosema kutoka moyoni Mwangu. Nilijua ya kwamba hiyo ingekuwa ndio njia pekee ningeweza kuwapa ninyi ile Imani Kamilifu mliyohitaji, ili tuweze kuwa pamoja.

Daima nimemtumia mtu mmoja kunena na kulifunua Neno Langu kwa Bibi-arusi Wangu. Jinsi ile tu nilivyofanya na Musa. Kile alichoagiza, ndicho alichopata, kwa maana alinena tu Maneno Yangu. Hata nilimwambia yeye, nitakufanya wewe mungu. Utakuwa mungu, na Haruni atakuwa nabii wako. Nitachukua sauti yako, nami nitaumba kwa kukutumia wewe. Nami nitanena, nao watu hawawezi kuikana. Lolote UTAKALOSEMA, litatendeka.

Sasa mmeipata Imani Kamilifu katika Neno Langu, si kwamba mnatambua tu ni nani Niliyewatumia kuwa Sauti Yangu, lakini sasa mnatambua kwamba Neno Langu linaishi na kukaa ndani yenu, hilo limekupa IMANI KAMILIFU.

Mnajua ninyi ni nani.
Mnakaa ndani Yangu, na Neno Langu ndani yenu. Ombeni mtakalo; nanyi mtapewa. katika Jina Langu mtatoa pepo; si, Mimi nitatoa, NINYI MTATOA. Kama NINYI mkiuambia mlima huu; si kama Mimi Nikiuambia, Kama NINYI mkiuambia mlima huu.

Adui yako hana nguvu tena juu yako. Wewe na Neno Langu ni MMOJA. Ikiwa una watoto ama wapendwa wako ambao hawako mahali wanapopaswa kuwa, wadai. Kama Ilifanya kazi kwako, basi itumie IMANI yako KAMILIFU katika NENO LANGU KAMILIFU linalokaa ndani yako, nawe waweza kupokea uombacho.

Lo, nimengoja kwa muda mrefu sana wewe kujitambua ni nani. Kukuona ukijiweka mwenyewe tayari kwa kulisikia Neno Langu. Nimefurahishwa sana hatimaye wakati huo umefika.

Hilo Neno Kamilifu nililonena na kuwahifadhia ninyi ndilo Ishara Yangu kwa kila mwamini leo. Ni Roho Mtakatifu; si damu, kemia, bali ni Roho Wangu Mtakatifu, Neno Langu, linaloishi na kukaa ndani yenu.

Saa ambayo hiyo Ishara haina budi kuonyeshwa waziwazi imewadia. Huna budi kuibeba Ishara pamoja nawe usiku na mchana; sio tu Jumapili, huna budi Kubonyeza Play wakati wote.

Yeye hutambua tu I—Ishara. Huo ndio Ujumbe wa wakati huu! Huo ndio Ujumbe wa siku hizi! Huo ndio Ujumbe wa wakati huu! Katika Jina la Yesu Kristo, upokeeni!

Nje huko kuna jumbe nyingi, lakini Sauti Yangu ndio Ujumbe wa wakati huu. Huna budi kupokea na kuamini kila Neno. Haina budi kuwekwa wakati wa jioni.

Ninyi kote ulimwenguni, mnaosikiliza kwenye kanda, ishara ya wakati huu iko hapa. Kuna Ishara ambayo haina budi kuwekwa, na haingalikuja wakati mwingine wo wote …mnalipata?

Njoo uiweke ile Ishara Yangu maishani mwako pamoja na Bibi-arusi wangu Jumapili hii saa 6:00 saa SITA MCHANA, saa za Jeffersonville (Ni saa 2:00 MBILI USIKU ya Afrika Mashariki ) tunapousikia Ujumbe Wangu kwa Bibi-arusi: ile Ishara 63-0901M.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya kusikiliza Ujumbe:

Mwanzo 4:10
Kutoka sura ya 12
Yoshua sura ya 12
Matendo 16:31 / 19:1-7
Warumi 8:1
1 Wakorintho 12:13
Waefeso 2:12 / 4:30
Waebrania 6:4 / 9:11-14 / 10:26-29 / 11:37 / 12:24 / 13:8, 10-20
Yohana 14:12

23-1210 Imani Kamilifu

UJUMBE: 63-0825E Imani Kamilifu

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi mwenye Imani Kamilifu,

IMANI yetu huja kwa kusikia, kulisikia Neno. Neno humjia nabii.

Nabii ni:

Neno lililofanyika mwili! Haleluya! Neno likitenda kazi katika mwili wa mwanadamu, kwa ishara za kimwili kwa ishara za vitu, kwa ishara za Kimaandiko, kikamilifu, kuwaleteeni Imani Kamilifu kwa ajili ya Kunyakuliwa Kukamilifu.

Sisi tunafanya kile hasa Neno linasema tufanye kwa kuisikia Sauti ya Mungu pekee iliyothibitishwa ikinena na kufunua Neno Lake kupitia mwili wa mwanadamu ili kutupa Imani Kamilifu.

Inakupasa…masikio yako ni bubu kwa kinginecho chote isipokuwa neno analosema Roho. Unaona? “Kwake yeye aliye na sikio ( linalosikiza ), aone neno ambalo Roho ayaambia makanisa”; yeye aliye na mahali pa kusikizia, ambapo panapokea neno ambalo Roho ayaambia makanisa. Waona?

Sisi ndio mahali pake pa kusikizia ambapo panalipata na kuliamini kila Neno. Anapotupa amri: “Semeni tu yale yaliyo kwenye hizo kanda. MIMI NI Sauti ya Mungu kwenu. Mnaniita mimi mchungaji wenu, nanyi mwanena vema, maana ndivyo Nilivyo.” Sisi tunayatekeleza. Cho chote Asemacho, hamna tashwishi kamwe tunatembea moja kwa moja. Lolote Bwana anenalo kupitia nabii Wake, hamna mtu ulimwenguni anayeweza kutushawishi vinginevyo, tunaendelea vivyo hivyo.

Sasa unafikia Imani Kamilifu , ukamilifu mtimilifu usioweza kushindwa. Imani hiyo haishindwi.

Sasa tunayo Imani Kamilifu katika Neno Lake. Sisi hatujitazami wenyewe. Hatuogopi lolote, kama Ayubu. Hatuogopi kuyatazama mawimbi makubwa na kuzama ndani ya maji kama Petro. Siku hizo zimepita. SASA tunalitazama lile Neno Kamilifu linaloishi na kukaa ndani yetu. Tunafikia asili ya Bibi-arusi. Tunafikia katika hali ya kunyakuliwa.

Tunapoomba, tunaamini kwamba tunapokea kile tunachoomba, nasi tutakipokea; tutapewa. Wakati, mahali, hakuna kitu kitakachokibadilisha. Tunajua imetendeka. imekwisha Tayari. Tunajuaje? Kwa sababu si Neno letu, bali ni NENO LAKE, ambalo amesema na kutupa sisi. Tuna NGUVU NA IMANI KAMILIFU YA KULINENA.

Kama vile Yesu alivyofanya kwa ajili yake Mwenyewe, tunatambua mahali petu; sisi ni nani. Jambo pekee tunalopaswa kufanya basi, ni kuwa na imani na kile tulicho. Tuwe na imani katika kile NENO linasema tulicho! Ndipo Neno la Mungu linakuja ndani yetu na kujidhihirisha Lenyewe; kwa maana sisi ni waamini. Na mwamini ni “imani ya Mungu inayotenda ndani yetu.”

Na sasa, tunakuwa watiwa mafuta kwa Roho yuyo huyo, masihi watiwa mafuta, masihi wa siku za mwisho, kuangaza ufufuo wa Yesu Kristo; kuonyesha ya kwamba si mfu, bali yuko katika umbo la Roho Mtakatifu, yu ndani ya watu Wake, akitembea kati ya Bibi-arusi Wake, akimfanyia mapenzi, akijimwaga Mwenyewe Kwake. Wanakuwa mmoja kwa ajili ya Karamu ya Arusi; na ishara zile zile, zilizoahidiwa na Mungu yule yule, katika Neno lile lile zinafanya madhihirisho yale yale Yake.

Hamna kilichobaki kwetu ila kuliamini, na kwa Kuliamini ndiyo hakika ya mambo inayoumba Imani Kamilifu. Sikiliza hilo tena, KWA KULIAMINI NDIYO HAKIKA YA MAMBO INAYOUMBA IMANI KAMILIFU.

Je! kunacho kiungo katika mwili wako kinachotilia shaka hata Neno moja: HAPANA
Je! unaamini kila Neno: Ndiyo
Je! Amekupa Ufunuo wa Ujumbe huu: Ndiyo
Je! Ni Bibi-arusi peke yake ndio watakaokuwa na huo Ufunuo wa kweli: Ndiyo
Je! unajua wewe ni Bibi-arusi Wake: Ndiyo
Je! Alisema kwa kuamini kila Neno itakupa Imani Kamilifu: Ndiyo
BASI WEWE NDIYE BIBI-ARUSI-NENO MWENYE IMANI KAMILIFU!!

Ee Bwana tuandae zaidi ya wakati mwingine tunapokusanyika pamoja Jumapili hii kusikia Neno lako. Tusaidie tusijitazame wenyewe tena, bali tu kuamini Neno Lako ulilonena kwa ajili yetu. Tumeuona Mvuto wa Tatu ukitenda kazi nasi tunajua unakaa ndani yetu. Yatubidi tuwe tunalinena na kuliamini Neno Lako.

Tunajua unamjia hivi karibuni Bibi-arusi-Neno Wako mkamilifu. Lolote tunalohitaji, Baba, LOLOTE TUNALOHITAJI, tunajua tutalipokea. Kwa maana Ni Neno Lako ambalo umekwisha kulinena kwa ajili yetu. Hakuna lingine lakufanya ila KULIAMINI tu. Tunaliamini Baba, tunaliamini. Sasa hebu na tulitendee kazi NENO LAKO.

Tunakiri kushindwa kwetu, dhambi na makosa yetu yote. Tutazame kupitia Damu ya Mwanao ambapo tunahesabiwa haki kwa Neema na rehema zako. Jalia kuwe na badiliko ndani ya Bibi-arusi Wako zaidi ya hapo awali. Na Utumiminie Roho wako Mtakatifu na kutupa yote tunayohitaji.

Wagonjwa wataponywa magonjwa yote. Aliyerudi nyuma atarudi kwenye Neno. Bibi-arusi wako ulimwenguni kote wataona njia yako iliyoandaliwa kwa ajili ya siku hii na kuamini.

Kama huna mtu wa kukuwekea mikono…wewe jiwekee mikono yako mwenyewe…wewe ni mwaminio. Umekuwa Neno; unakuwa Neno, unapolipokea Neno.

Njoo Bwana Yesu, Bibi-arusi Wako anajiweka mwenyewe tayari kwa kukaa katika uwepo wa Neno Lako, kuivishwa. Tunataka kupambwa na kuvikwa kwa Neno lako.

Njoo ututie mafuta zaidi ya hapo kabla Jumapili hii saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville, ( Ni saa 2:00 MBILI USIKU ya Afrika Mashariki ) wakati sehemu ya Bibi-arusi wako inapokusanyika kukusikiliza WEWE ukinena na kutufunulia jinsi ya kupata: Imani Kamilifu 63-0825E.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya ibada:

Marko 11:22-26 / 16:15-18
Yohana 14:12 / 15:7
Waebrania 11:1 / 4:14
Yakobo 5:14
1 Yohana 3:21

23-1203 Ninawezaje Kushinda?

UJUMBE: 63-0825M Ninawezaje Kushinda?

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Yungiyungi la Kidimbwini,

Jinsi gani mioyo yetu ilivyoruka kwa furaha Jumapili tulipomsikia Bwana wetu akinena na kutuambia kile kinachotendeka sasa hivi. Tunaungana na Neno na kuwa MMOJA Naye. Hivi karibuni sana tutaungana na watakatifu waliotutangulia kuwa WAMOJA nao. Kisha sisi sote pamoja tutaungana na Kristo kama MMOJA kwenye Karamu ya Arusi ya Mwana-Kondoo.

Ni furaha iliyoje iliyojaza nafsi zetu wakati Alipotuambia kuwazia kwamba katika dakika moja, katika kufumba na kufumbua jicho, ulimwengu hata hautajua kinachoendelea; lakini kwa ghafula, tutawaona mbele ya macho yetu wapendwa wetu walioondoka, nasi tutaungana nao tena.

Ni matarajio yaliyoje yanayojaza mioyo yetu kuwazia, kwa ghafula, tutawaona wamesimama mbele yetu baba zetu, mama zetu, kaka, dada, waume, wake, watoto, hata nabii wetu. TUTAWAONA, KATIKA MWILI!!

Tutajua papo hapo, hili NDILO; wakati umefika, tumefaulu, IMEKWISHA. Nena kuhusu changamko kwa Ufunuo!! Nikiliwazia na kulinena tu sasa hivi, naweza kuwasikia mkipaza sauti, UTUKUFU, HALELUYA, JINA LA BWANA LIHIMIDIWE.

Ni Wakati wa jinsi gani tunaokuwa nao, tukila barua hizi za mapenzi tulizoachiwa. Barua za mapenzi tunazoweza kuzichomoa wakati wowote tunapotaka na kuzisoma tena na tena na tena. Si hivyo tu, bali na KUBWA ZAIDI, tunaweza KUMSIKIA Bwana wetu Mwenyewe akisema kupitia midomo ya mwanadamu na kutuambia, “Nilizihifadhi barua hizi za mapenzi kwa ajili yako tu, kipenzi Changu. Nilijua wakati ungefika ambao ungehitaji kunisikia Mimi nikikuambia jinsi ninavyokupenda na kwamba wewe ni Wangu.”

“Nilitaka kukuambia kila siku adui anapokushambulia, unapopitia mitihani na majaribu yako yote, WEWE NI WANGU. Tayari nimelipa ile gharama. Tayari nimeshinda chochote kile…umenisikia kipenzi? CHOCHOTE unachokihitaji, nimekwisha kushinda kwa ajili yako, kwa sababu Nakupenda”.

“Nilikujua kabla hata ulimwengu haujawepo. Wewe ulikuwa sehemu Yangu WAKATI HUO. Hukumbuki hilo sasa, lakini Mimi ninakumbuka. Usisahau nilichokuambia, wewe ni Mwili wa Mwili Wangu, Roho wa Roho Yangu, Mfupa wa Mfupa Wangu”.

“Ule wakati umefika sasa ambao nimekuwa nikiwaambia. Hakutakuwa na huzuni tena, hakutakuwa na mitihani na majaribu tena; siku hizo zimekwisha. Sasa ni sisi sote tu pamoja Milele yote”.

“Jipe moyo. Endelea kusonga. Kule Kupambazuka kwa siku ile kumekaribia. Mvutano wote unaopitia kila siku ni wa kukuleta karibu na Mimi”.

“Wakati jambo lolote linapokujia, na unaanza kuhisi umevunjika moyo sana, umechoka na huwezi, na kuonekana kama huwezi kuendelea mbele, inakubidi usisahau kamwe, Mimi Niko hapo pamoja nawe. Neno Langu linaishi ndani yako. Wewe ni Neno Langu.”

“Niliwaambia, mnene Neno. Lo lote mtakalo, mkisali, aminini ya kwamba mtalipokea, nanyi mtalipata. Mtapewa jambo hilo. Tayari Mimi nimekwishawashindia jambo hilo”.

Maneno haya yanamaanisha nini kwetu. Yanatuhifadhi kila siku. Linaziinua Roho zetu na kutuweka katika ulimwengu wa Roho pamoja Naye. Tunamwishia tu Mungu na Neno Lake. Tuna kusudi moja, hilo ni Yesu Kristo. Nje ya Hilo, hakuna jambo lingine linalojalisha.

Tumelipata lile Ono. Pazia limevutwa nyuma nasi tunamwona Yeye, Neno Lake lililofanyika mwili, akizungumza nasi kupitia midomo ya mwanadamu. Tuna mapenzi na Neno hili, Ujumbe huu, Sauti hiyo.

Njoo uungane nasi Jumapili saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,( Ni saa 2:00 MBILI USIKU ya Afrika Mashariki ) upate uzoefu uliyo mkuu maishani mwako. Usikie jinsi ya kushinda kila vita ambavyo Shetani anatupa mbele yako. Ujaze moyo wako kwa furaha na shangwe kujua wewe ni Bibi-arusi wa Yesu Kristo.

Ndugu. Joseph Branham

63-0825M Ninawezaje Kushinda?

Maandiko ya Kusoma kabla ya ibada :

Ufunuo 3:21-22

23-1126 Wakati Wa Kuungana Na Ishara Yake

UJUMBE: 63-0818 Wakati Wa Kuungana Na Ishara Yake

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Mwili wa Mwili Wake, Neno la Neno Lake, Uhai wa Uhai Wake, Roho wa Roho Wake,

Ndugu na dada zangu wapendwa, Hebu someni kauli hiyo moja tena na tena. Someni kile Mungu Mwenyewe alichomaliza kuwaita. Hivi angewezaje mtu yeyote kuandika kwa maneno ya kibinadamu tu kuwa hayo yana maana gani kwetu. Haiwezekani kuyaeleza. Kama tungeweza kuyafahamu kikamilifu na kuyatumia, kwa mioyo yetu yote, nia na roho zetu zote, ninaamini kweli Unyakuo ungepaswa kutukia.

Kuna nini cha kuogopa? Kuna nini cha kuhofia? Shetani anatushambulia, anatutesa, anatutupia magonjwa, anashambulia akili zetu kwa kila namna ya mawazo mabaya, lakini hakuna kitu kinachoweza kutudhuru. Je, kuna jambo lolote linaloweza kumdhuru Yesu? HAPANA, basi wala hakuna kitu cha kutudhuru. Ndio kwanza Amesema: SISI NI Mwili Wake, Neno Lake, Uhai Wake, Roho Wake.

Ni furaha na uradhi uliyoje tulio nao mioyoni mwetu tunapotafakari yale ambayo Yeye amekuwa akituambia. Ufunuo ambao Mungu amekuwa akitufunulia, mzigo wa kanda, baada ya mzigo wa kanda, baada ya mzigo wa kanda. Roho Mtakatifu anabubujika ndani yetu kama Kisima kikuu kinachofoka maji.

Sisi tumechaguliwa tangu zamani Kuliona na Kulisikia. Hatuta na hatuwezi kuanguka wala kupotoshwa. Tuko njiani kukutana na Uongozi wetu, Mkombozi wetu, Mume wetu, Mfalme wetu, Bwana wetu, Mpenzi wetu, Mwokozi wetu, katika Mahali palipoandaliwa pa kukutania!

Hebu sikilizeni hili tena: Utimilifu kamili wa Uungu kwa jinsi ya mwili unakaa ndani YETU, Kanisa Lake, ule utangulizi. Yote aliyokuwa Mungu, aliyamimina ndani ya Kristo; na yote aliyokuwa Kristo, yalimiminwa ndani ya Kanisa; sisi, Bibi-arusi Wake. Sio jambo litakalotendeka siku moja, AMESEMA LINAFANYIKA NDANI YETU SASA HIVI.

Je, waweza kuwazia, tangu mwanzo kabisa wa wakati, Mungu hakuwahi kutoa siri Yake kuu ya ajabu ambayo ilikuwa niani Mwake kwa mtu yeyote, hadi leo hii. Kwa nini alifanya hivyo? Kwa sababu Yeye alikuwa anangojea kutujulisha SISI katika siku hizi za mwisho kama alivyoahidi. Alikuwa anatusubiri sisi. Alijua kuwa sisi ndio watu pekee tungaliweza, na tungeweza, KULIELEWA KIKAMILIFU….UTUKUFU!! !

Alituchagua sisi tuwe Bibi-arusi wake kwa sababu alijua kwamba hatutaanguka. Tungeshikilia Neno hilo haidhuru ulimwengu wote ungesema nini kulihusu. Tungeshikilia Neno hilo na NENO hilo PEKE YAKE! Sisi tumechaguliwa tangu zamani kusimama hapo. SISI tumefanywa wana wenye mamlaka na Yesu Kristo.

Kunayo mengi zaidi. Sikilizeni kwa makini….jichune. Kichwa (Mungu) na Mwili (Sisi) umekuwa kitu kimoja. Ni Mungu aliyedhihirishwa ndani YETU.

  • Mungu na Kanisa Lake wao ni MMOJA, “Kristo ndani YENU.”
  • Sisi NDIO Ufunuo Mkuu wa Mungu.
  • Sisi hata tunalibeba Jina Lake; Jina Lake ni Yesu, yule Mtiwa Mafuta.
  • SISI NDIO Mwili uliotiwa mafuta wa Kristo.
  • SISI TUNA mdhihirisha Mungu kama jinsi ule mwili ulivyofanya.

Sisi ndio Bibi-arusi Wake, tumetiwa mimba kwa Roho Wake. Kanisa, linalozaa watoto, lililotiwa mimba kwa Roho Wake likibeba Jina Lake; likibeba Uhai Wake. Tuna jibu la Shetani. Uongozi uko hapa. Kristo, Bwana aliyefufuka, yuko hapa katika Nguvu zile zile za kufufuka Kwake alizowahi kuwa, akijidhihirisha Mwenyewe ndani yetu, Bibi-arusi-Neno Lake Lililonenwa.

Mungu sasa anamuunganisha Bibi-arusi Wake pamoja. Anawaunganisha kutoka ulimwenguni kote kwa Neno Lake, jambo pekee litakalomleta Bibi-arusi Wake pamoja. Roho Mtakatifu anaongoza na kumkusanya Bibi-arusi Wake. Katika kila wakati, nabii alikuwa ndiye Roho Mtakatifu kwa ajili ya siku zao.

Liwazieni jambo hili. Wakati Watu wanaposema kuwa tunampa sifa nyingi mno malaika-mjumbe wa saba, kumbuka, Mungu Mwenyewe alizikabidhi SIRI ZAKE ZOTE alizokuwa nazo Niani Mwake kabla hata ulimwengu haujawepo, kwa malaika-mjumbe Wake wa saba. Mungu Mwenyewe alikuwa na imani na mtu huyu asilimia 100%, hata akauweka Mpango wake mkuu wa wakati wa mwisho mikononi mwake. Alimpa yeye…SIKILIZENI, AKAMPA YEYE Ufunuo wa siri Zake zote kwa mtu huyo. Alimpa mtu huyo Ufunuo wa mambo ambayo hata hayakuandikwa. Alisema chochote kile alichosema duniani kilikuwa ni muhimu sana, kingerudisha mwangwi mbinguni.

Hakuna tashwishi kwamba Mungu aliwatuma watu wakuu waliojazwa na Roho Mtakatifu katika ulimwengu huu. Lakini kila mmoja wa watu hawa, hata ikiwa wamejazwa na Roho Mtakatifu, wanaweza kuwa makosani. Mungu kamwe hakuthibitisha kile wanachosema kuwa Bwana Asema hivi, na kuwaambia muamini kila neno lao. Kulikuwa na mtu mmoja tu aliyekuwa na mamlaka hayo kutoka kwa Mungu, malaika-mjumbe Wake wa saba.

Unaweza, na unapaswa, kuwa na mchungaji. Lakini kama huyo mchungaji hakuambii ya kwamba SAUTI YA MUNGU iliyo kwenye kanda ndiyo SAUTI iliyo MUHIMU SANA KUSIKIA, na kuipa nafasi ya KWANZA mbele yenu kwa kusikiliza kanda pamoja nanyi, si kwamba tu yeye awaambie ati nabii anasema hivi, basi mchungaji mliye naye hafai.

Yeyote anayekuongoza, hata kama unadai kuwa ni Roho Mtakatifu, ni afadhali awe anakuunganisha na Ujumbe huu, Ile Sauti, kwani Ndiyo sauti Pekee inayoweza kusema, “MIMI NI SAUTI YA MUNGU KWENU”.

Kama umechaguliwa tangu zamani Kuliona, Utaliona. Ikiwa hujachaguliwa tangu zamani Kuliona, hutaliona kamwe; hujaandikiwa kuliona.

Tunaona mataifa yakiungana, tunaona ulimwengu ukiungana, tunaona makanisa yakiungana. Tunaona Bibi-arusi akiungana, akiungana na Neno. Kwa nini? Neno ni Mungu. Na kama Neno…Kama vile Bwana Arusi (akiwa ni Neno), na Bibi-arusi (akiwa ni msikiaji wa Neno), wanakuja pamoja katika Muungano. Wanaungana kama vile arusi. Unaona, wanajiandaa kufanya arusi, nao—nao wanakuwa mmoja. Neno linakuwa wewe, wewe unakuwa Neno. Yesu alisema, “Katika siku hiyo mtaijua. Yote aliyo Baba, ndivyo nilivyo Mimi; na yote niliyo Mimi, ndivyo mlivyo ninyi; na yote mliyo ninyi, ndivyo nilivyo Mimi. Katika siku hiyo mtajua ya kwamba Mimi niko ndani ya Baba Yangu, Baba ndani Yangu, Mimi ndani yenu, nanyi ndani Yangu.”

Ninawaalika mje kuungana nasi kuizunguka Sauti ya Mungu Jumapili hii saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville, ( ni saa2:00 MBILI USIKU ya Afrika Mashariki), tunaposikia, Wakati Wa Kuungana na Ishara Yake 63-0818

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya ibada:

Zaburi 86:1-11
Mathayo 16:1-3

23-1119 Kristo Ni Siri Ya Mungu Iliyofunuliwa

UJUMBE: 63-0728 Kristo Ni Siri Ya Mungu Iliyofunuliwa

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Kitovu Cha Moyo Wa Nabii,

Wao ndio—ndio wamezaliwa Kwako, kwa Roho na kwa Neno la Kweli. Nami naomba ya kwamba utawabariki, Bwana, na kuwaweka wameunganishwa pamoja kwa karibu na vifungo vya upendo wa Kristo.

Jitayarisheni, tutakuwa na baraka, upako na Ufunuo kuliko awali. Twaweza kulihisi jambo hilo katika nafsi zetu, jambo fulani linakaribia kutukia. Wakati uko tayari. Tumechangamshwa sana kwa furaha na tuko chini ya matarajio makubwa ya aina yake. Bibi-arusi ulimwenguni kote anakusanyika pamoja ili kusikia kutoka kwenye kiti cha enzi cha Mungu Ujumbe ambao utatupeleka kwenye viwango vipya, na kutujaza, na kujaza, na kisha kutujaza upya na Roho Wake Mtakatifu.

Maandiko yanaenda kutimia. Onyo limefanyika. Hukumu iko karibu. Bwana anakuja kumwita Bibi-arusi Wake kwenda kwenye Karamu yetu ya Arusi. Ule wito wa mwisho umepita. Ujio wa Mungu umefika. ANAKUJA KUTUCHUKUA.

Sisi ndio ile mbegu iliyochaguliwa tangu zamani ambayo huliona na kulikubali. Dhambi zetu zimeangamizwa, zimekwisha. Zimetupwa kwenye wino wa Damu ya Yesu Kristo, wala hazitakumbukwa tena. MUNGU amezisahau ZOTE. Tunasimama kama mwana na binti wa Mungu, mbele za Mungu. Ndivyo tulivyo SASA…si tutakuwa; SASA sisi ni wana na binti za Mungu.

Tunatambua kitu kimoja, NENO. KANDA HIZI. UJUMBE HUU. Hayo ni mamoja.

Na mara moja, muda mfupi tu uliopita, ulipoonyesha lile ono, hii maskani ndogo hapa, karibu kuweka Chakula akiba, kwamba utakuja wakati ambapo haya yote yangehitajika … “Weka Chakula hiki akiba hapa kwa ajili ya huu wakati.”

Huu ndio wakati. Hiki ndicho Chakula. Sisi ndio watu hao. Sisi tunao Ufunuo.

Wengine wanaweza kuukosa umuhimu wa Huduma ya Kanda. Sisi sisi sivyo. Ni maisha yetu, ni kila kitu kwetu. Ni zaidi ya uhai kwetu. Tunapokuwa na swali kuhusu jambo fulani, hatuendi kumwomba mtu atufafanulie, ama atutafutie. Sisi tunafanya vile hasa malaika wa Mungu alivyotuagiza kufanya ikiwa tutashindwa kuelewa au tukiwa na swali.

Mnalipata? Mkishindwa, rudini kwenye kanda hii tena. Sijui nitakuwa nanyi kwa muda gani zaidi. Kumbukeni, hii ndiyo Kweli, ya BWANA ASEMA HIVI. Ndiyo Kweli. Ni Maandiko.

Mkishindwa, rudini kwenye kanda.

Msitukasirikie, hivyo ndivyo YEYE ALIVYOSEMA…PAMOJA NA, hii ndiyo KWELI YA BWANA ASEMA HIVI . Yeye hakusema kiasi chake, baadhi Yake, ama wakati mtu fulani anapofasiri kile kilicho na ambacho si Neno lililotiwa mafuta. KANDA HIZI NI BWANA ASEMA HIVI.

Huenda wewe usilipate, ama kulielewa, ama bado halijafunuliwa kwako . Lakini kwetu sisi, haya ndiyo YEYE anayotuambia kupitia nabii Wake.

Unajua jinsi unavyomwambia mke wako mambo, unajua, msichana mdogo utakayemwoa. Unampenda sana, unamwambia tu siri, na kumweka karibu nawe, na kukupenda wewe na kadhalika. Unajua jinsi ilivyo. Hivyo ndivyo Mungu, Kristo, analifanyia Kanisa. Mnaona? Anamjulisha siri, siri tu. Sio hawa wafanya utani; ninamaanisha Mke Wake.

Nasi tunayazingatia yote. Loo jinsi gani Bibi-arusi alivyo mwenye furaha na changamko la shangwe kabla tu ya arusi yake. Hatuwezi kabisa kusimama kimya. Tunazihesabu dakika …. sekunde. Yeye anaendelea kutuambia tena na tena jinsi gani anavyotupenda.

Shetani anaendelea kutushambulia kuliko awali, lakini kile hajajiandaa, ni kwamba sasa TUNAJIJUA sisi ni nani. Hakuna shaka tena, SISI NI NENO LILILONENWA. Tunaweza, na tuna, nena Neno. Tuna jibu la Shetani. Mungu amejithibitisha Mwenyewe. Mungu amejihakikisha Mwenyewe. Sisi ni Neno Lake lililo hai nasi tuna nena kwa mamlaka yote aliyotupa.

Naye huyu hapa leo, katika Neno Lake, akidhihirisha jambo lile lile alilofanya kule. Hawezi kutambua uongozi mwingine. La, bwana. Hakuna askofu, hakuna chochote. Anatambua Uongozi mmoja, huo ni Kristo, naye Kristo ni Neno. Loo, jamani! Whiu! Napenda hilo. Uh! Naam, bwana.

Sisi ni raia wa Ufalme, nao huo Ufalme ni Neno la Mungu lililofanyika Roho na Uzima katika maisha yetu wenyewe. Kwa hiyo, sisi ni Neno Lake lililo hai.

Hili Hakika lanena YOTE enyi marafiki, IKIWA UNA UFUNUO WA KWELI WA KULIPOKEA NA KULIAMINI.

Sasa angalieni. Angalieni sasa, wameunganishwa pamoja chini ya Uongozi mmoja, kwa namna ile ile, mfano wa Israeli wa kale. Sasa mnalipata? Kama Israeli wa kale; Mungu mmoja, aliyethibitishwa kwa Nguzo ya Moto, na kujifunua Mwenyewe kupitia nabii, kuwa Neno. Mungu yeye yule, Nguzo ile ile ya Moto, kwa njia ile ile; Hawezi kubadili njia Yake . Hilo ni… Kamili tu kama iwezavyo kuwa.

Nabii…Hebu hilo lizame ndani kilindini. Mungu Mmoja, aliyethibitishwa kwa Nguzo ya Moto, kupitia nabii, kuwa Neno la siku hiyo, Naye hawezi kubadilika.

Ningeweza kuendelea na kuendelea, na tungeweza kufurahia na kushiriki nukuu baada ya nukuu; nasi tutafanya hivyo, kutoka kote ulimwenguni Jumapili hii saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville, (ni saa 2:00 MBILI USIKU ya Afrika Mashariki ) tunaposikia:  Kristo Ni Siri ya Mungu Iliyofunuliwa 63-0728.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya ibada:

Mathayo 16:15-17
Luka Sura ya 24
Yohana Mtakatifu 5:24 / 14:12
1 Wakorintho Sura ya 2
Waefeso Sura ya 1
Wakolosai Sura ya 1
Ufunuo 7:9-10

23-1112 Mungu Hamwiti Mtu Hukumuni Bila Ya Kumwonya Kwanza

UJUMBE: 63-0724 Mungu Hamwiti Mtu Hukumuni Bila Ya Kumwonya Kwanza

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Kamani, Springi kuu, Mkulima na Mke nyumbani,

Chochote kile ambacho Mungu alichokupa kufanya, una utumishi kwa jambo hilo. Huna budi kuwajibika kwa hilo kwa Mungu. Haijalishi adui aweza kukuambia kuwa wewe ni mdogo jinsi gani, wewe ni muhimu sana kwa Mungu hivi kwamba saa Yake kuu haiwezi kusonga bila wewe.

Alikuita, akakuchagua, alikukusudia tangu awali, na akakupa Ufunuo wa Ujumbe Wake mkuu wa wakati wa mwisho. Ana imani na wewe asilimia 100%. Wewe ndiwe yule Bibi-arusi mwenyewe wa Yesu Kristo, Kipenzi Chake, naye Anakupenda sana.

Daima amewaonya watu kote katika mataifa, “Tubuni, la sivyo mtaangamia,” “Rudini kwenye Neno,” “Jitayarisheni, kuna jambo linaenda kutukia.” Wakati huo hatimaye umefika. Mungu anakuja kumchukua Bibi-arusi Wake, kama vile tu alivyotuahidi Angefanya. Ameliita Gurudumu Lake kutoka kwenye gurudumu.

Wengi wameanguka kutoka kwenye Ujumbe mkuu wa Mungu wa wakati wa mwisho leo hii, wakisema, “yale aliyosema yangetukia, hayakufanyika. Mambo yote yako vile vile.” Ilikuwa ni vizazi vingi vilivyopita kabla ya unabii mwingi wa manabii wa Mungu kutimia. Lakini yalitendeka hata hivyo, kama tu walivyosema, Neno kwa Neno.

Biblia yake inatuambia hivi: “Kama ilivyokuwa katika siku za Nuhu, ndivyo itakavyokuwa katika kuja Kwake Mwana wa Adamu.” Kabla Mungu hajatuma hukumu kuuangamiza ule ulimwengu uliotangulia gharika, Mungu alimtuma nabii ulimwenguni. Nabii huyo alifanya nini?

Akawatayarisha watu kwa ajili ya wakati huo. Nuhu aliwatayarisha watu, nao ulikuwa ni wito wa rehema kabla ya hukumu.

Nuhu aliwatayarisha watu kabla ya hukumu kuja aliowaonya kuihusu. Ilikuwa ndio Njia ya Mungu iliyoandaliwa kwa ajili ya siku hiyo.

Nabii wa Mungu alituambia kwamba Mungu kamwe habadilishi mpango Wake. Yale aliyoyafanya wakati huo, anayafanya vivyo hivyo leo hii. Sisi tutakaa tu na MPANGO WA MUNGU ULIYOANDALIWA KWA AJILI YA SIKU HII NA KUBONYEZA PLAY.

Kama ilivyokuwa wakati huo, watu husema tunaweka mkazo sana kwa nabii wa Mungu; Ni Roho Mtakatifu, si William Branham. Tunasema, AMINA, hatumsikilizi huyo mtu , tunasikiliza tu YALE ALIYOSEMA.

Roho Mtakatifu ndiye Nabii wa wakati huu; Yeye analihakikisha Neno Lake, akilithibitisha. Roho Mtakatifu alikuwa ndiye Nabii wa wakati wa Musa. Roho Mtakatifu alikuwa Nabii wa wakati wa Mikaya. Roho Mtakatifu, aliyeliandika Neno, anakuja na kulithibitisha Neno.

Lakini Ndugu Branham ndio kwanza awaambie juma lililopita;

Sasa, mnaona, daima nimewaomba mwe waangalifu kwa yale mnayosikiliza. Mnaona? Kuna mengi sana ambayo ni upande tu wa kibinadamu.

Sisemi ya kwamba Bwana aliniambia jambo hilo. “Mimi” naamini, unaona. Na naamini halipaswi kufanywa.

Kwangu mimi na nyumba yangu, nitachukua yale malaika-mjumbe wa saba wa Mungu ANAYOAMINI, ANAYOWAZIA AU HATA ANAYOJISIKIA kuliko ya mhudumu mwingine yeyote, askofu ama mtu.

Ni nani ambaye Mungu aliwahi kumtuma kuhukumu kile nabii Wake anachoamini, anachohisi ama hata anachofikiria ndicho ama halijavuviwa?…Hebu niwaambieni ni nani ninayefikiri.

Mwangalieni Kora, katika siku ambazo Mungu alimtuma Musa na ujumbe, naye Kora na Dathani wakawazia, wakamwendea Musa, na kusema, “Sasa, hebu kidogo, unajichukulia mengi kupita kiasi! Unafikiri wewe ndiwe changarawe ya pekee ufukoni; bata kidimbwini, ndiwe wa pekee. Nitakufahamisha wapo watu wengine walio watakatifu, pia!”

Onyo, hukumu iko karibu. Rudini kwenye NENO LA ASILI. Rudini kwenye Sauti ya Mungu iliyothibitishwa kwa ajili ya siku yetu. Rudini kwa nabii wa Mungu. Ujumbe huu, Sauti Yake. Inapaswa kuwa ya KWANZA na kuwa jambo lililo muhimu zaidi kwenu.

Bila shaka wengine wana sauti, na wito, kuhubiri na kufundisha Ujumbe huu. Bali Kanda hizo, Sauti hiyo, haina budi kuwa ndio Sauti iliyo muhimu sana mnayopaswa kuisikia katika nyumba zenu, magari yenu, na muhimu zaidi, kanisani mwenu, kama mnataka kuwa Bibi-arusi wa Mungu.

Njooni msikie hiyo Sauti pamoja nasi Jumapili saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,( ni saa 2:00 MBILI USIKU ya Afrika Mashariki ) Wakati nabii wa Mungu anapouonya ulimwengu kwamba Kuja kwa Bwana kumekaribia. Hii inaweza kuwa ndio mara ya mwisho.

Ndugu. Joseph Branham

Mungu Hamwiti Mtu Hukumuni Bila Ya Kumwonya Kwanza. 63-0724

Maandiko ya kusoma kabla ya ibada:

Isaya 38:1-5
Amosi Sura ya 1

23-1105 Yeye Hujali. Je! Wewe Unajali?

UJUMBE: 63-0721 Yeye Hujali. Je! Wewe Unajali?

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Watoto wa Injili,

Sisi ni watu waliobarikiwa zaidi ambao wamewahi kutembea juu ya uso wa dunia. Je! Hivi tunaweza kuwazia malaika-mjumbe wa saba aliyechaguliwa na Mungu kutuambia maneno haya:

Ninawapenda. Loo, ninawapenda kana kwamba mlikuwa ni watoto wangu binafsi, nanyi ni watoto wangu katika Injili. Nimewazaa kwa Kristo, kwa njia ya Injili.

Mungu anatujali sana hata Yeye alitutumia nabii Wake aliyethibitishwa akiwa na ishara ya Nguzo ya Moto kutufanya tujue ya kwamba haikuwa tu ni mtu huyu aliyekuwa akitembea pamoja nasi, bali ilikuwa ni Mungu papo hapo juu yake. Yeye ndiye anayeongoza njia.

Kwa sababu anatujali, kabla ya hukumu iliyo kuu haijaja, ameiandaa njia ambayo tutakuwa huru na hukumu zote zinazokuja. Njia hiyo ya kuepukia ni kwa ajili yetu sisi tu, Wateule. Sisi ndio tumeikubali seli zazi hii ya Uhai. Sisi ndio tuliokusudiwa tangu awali kuliona. Sisi ndio tulio na Ufunuo wa huduma hii kuu ya kanda.

Yeye aliifia huduma hii. Alikufa kusudi Roho Mtakatifu aweze kuwa hapa siku hizi kuonyesha mambo haya. Yeye alikujali. Alijali kuuleta hapa. Alijali kutoa tamshi. Alijali kwa kuwa alikupenda. Alijali vya kutosha kufanya jambo hilo, kumtuma Roho Mtakatifu kwenye hili, kuifanya huduma hii leo.

Kama umechaguliwa tangu zamani kwa Uzima wa Milele, utalisikiliza na utalifurahia. Ni Faraja yako. Ndicho kitu ambacho umekitamani maishani mwako mwote. Ni ile Lulu ya thamani kuu. Tunaachana na kila kitu kwa ajili ya Ujumbe huu, Sauti hii. Ni Bwana wetu Yesu Kristo akizungumza nasi.

Hakuna mtu anayepaswa kutubembeleza-bembeleza, SISI NI WAAMINIO, hakuna kitu kinachoweza kuliondoa kwetu. Hatujali yale mtu ye yote asemayo, tunaamini kila Neno.

Yeye anatujali sana; ikiwa tunahitaji uponyaji, tunaamini tu Neno Lake kutoka ndani kabisa ya kilindi cha moyo wetu. Basi haijalishi mshauri yeyote, mfariji ye yote, daktari ye yote, hospitali yo yote, ubaini wowote ungesema nini, tunaamini tu Neno Lake. Tunajua tu hilo! Hakuna haja ya kusema jambo lingine lolote kulihusu; tunajua hilo.

Yeye alitujali sana hata akamfanya nabii Wake akihifadhi Chakula kwa ajili ya Bibi-arusi Wake. Aliagiza hata kila mchungaji, mhudumu, na kundi la watu ulimwenguni kote kufuata maagizo yake na kuzicheza kanda hizi katika MAKUSANYIKO ama makundi yao.

Kama ninyi watu mtafanya hivyo asubuhi ya leo, mtakaoombewa Na ninyi watu mnaoisikia kanda hii, kote ulimwenguni, na baada ya kanda hii kuchezwa na mhudumu ama mtu anayeicheza katika makundi ya kusanyiko huko misituni ama popote mlipo, mnaoicheza, kwanza mtafanya toba yenu dhahiri, kisha mje bila chochote moyoni mwenu, ila imani, na kuombewa, hapo ndipo Dawa itakapofanya kazi.

Nilidhani wakosoaji wetu wanasema kuwa nabii HAKUSEMA kucheza kanda kanisani? Si tu kwamba Yeye alisema katika makanisa yao, bali katika misitu ama POPOTE mlipo…CHEZENI KANDA.

Kama utatii na kufanya yale hasa Mungu aliyonena kupitia malaika-mjumbe Wake wa saba aliyethibitishwa, basi wewe pia unaweza kuwa na IMANI kuu kuliko zote unayoweza kuwa nayo.

Kwanza, na kulikaribia hili, wasikilizaji hawana budi kutiwa mafuta kwa imani. Wewe, kama huna imani, basi hakuna—hakuna hata haja ya kuja kuombewa, kwa maana itahitaji imani yako na imani yangu pamoja; imani yangu kumwamini Yeye,imani yako kumwamini Yeye.

Sisi hatudhanii, ama kukisia, ama kutumainia ni hivyo. Kanda ndiyo Njia ya Mungu iliyoandaliwa ya siku hii. Si maneno ya mtu anayeitwa William Marrion Branham, Ni Maneno yaliyofunuliwa ya Bwana wetu Yesu Kristo. Kabisa ni, “Amina!” Ndio mkataa wetu. Ni Kweli na si kitu ila Kweli tupu.

Na unapoupata Mkataa wa Mungu, Neno Lake, ahadi juu ya jambo fulani, inakubidi kujua kwanza ya kwamba ni Neno la Mungu, ya kwamba jambo unaloliona likitekelezwa ni Mungu. Ha—hakuna—hakuna “huenda ikawa ndivyo, ingewezekana, inaonekana kana kwamba huenda ikawa.” “Ni Mungu!” Ndipo unapofikia mahali hapo, basi hiyo ndiyo ile Lulu ya thamani kubwa, huna budi kuachana na chochote mtu yeyote anachokwambia kinyume Chake. Haikupasi kuangalia kile mwanadamu ametimiza.

Tunakwenda kuwa na KARAMU KUBWA MNO YA UPENDO Jumapili hii. Tutafanya kile ambacho malalika-mjumbe wa saba wa Mungu aliyethibitishwa aliyotuambia tufanye: Bonyeza Play na kutii.

LOLOTE tunalohitaji, tutalipokea. Tutalipokea kwa sababu tutaiweka imani yetu pamoja na IMANI YAKE kumwamini Yeye. Kisha sote tutasema:

Tangu sasa na kuendelea, kuna kitu moyoni mwangu kinachoniambia ya kwamba shida zangu zimekwisha. Mimi ni—mimi ni mzima, nitapona”? Mnaamini hilo? Inueni mikono yenu, “Ninaamini Hilo!” Mungu awabariki.

Kwa sababu Mungu anajali, ninakualika uje kuungana nasi; ama umtie moyo mchungaji wako, kiongozi wako, kufuata maagizo ya nabii, na kumsikia malaika wa saba wa Mungu akinena Neno la Mungu na upokee lolote unalohitaji, Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville ( Ni saa 2:00 MBILI USIKU ya Afrika Mashariki ) tunaposikia: 63-0721 Yeye Hujali. Je! Wewe Unajali?

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya ibada:

Yohana Mt 5:24 / 15:26
1 Petro 5:1-7
Waebrania 4:1-4

23-1029 Mfungwa

UJUMBE: 63-0717 Mfungwa

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Jumamosi.

Wapendwa Wafungwa,

Maisha yako unayoishi sasa yataakisi maisha ambayo ungeishi ikiwa ungeishi katika siku za Nuhu, ama Musa, kwa sababu una roho yule yule. roho yeye yule aliye ndani yako sasa alikuwa ndani ya watu wakati huo.

Kama ungaliishi katika siku za Nuhu, ungechukua upande wa nani wakati huo? Je, ungeingia kwenye mashua pamoja na Nuhu ukiamini kwamba yeye ndiye ambaye Mungu alimchagua kujenga safina na kuwaongoza watu, au ungesema, “Mimi naweza kujenga safina pia. Mimi ni mzuri tu kama nahodha na mjenga mashua”?

Vipi kama ungaliishi katika siku za Musa? Je, ungekaa na Musa na kuamini kwamba yeye ndiye ambaye Mungu alimchagua kuwaongoza watu, ama ungeenda pamoja na Dathani na Kora waliposema “Sisi pia ni watakatifu, tunalo jambo la kusema. Mungu alituchagua sisi pia.”?

Kila mmoja wetu anapaswa kuchagua, leo hii, kati ya mauti na uzima. Sijali wewe unasema uko upande gani. Yale unayofanya, kila siku, yanathibitisha kile ulicho. Tunabonyeza Play KILA SIKU.

Je, uko katika Neno kila siku? Je, unaomba, ukitafuta Mapenzi makamilifu ya Bwana katika kila jambo unalofanya? Je, unabonyeza play na kuisikia Sauti ya Mungu iliyothibitishwa kila siku? Je, unaamini ni muhimu kabisa Kubonyeza Play? Je! unaamini hiyo Sauti iliyo kwenye kanda ni Sauti ya Mungu kwa ajili ya siku hii?

Kwetu sisi, jibu ni NDIYO. Tunauambia ulimwengu kwamba sisi ni Wafungwa wa Neno la Mungu, Ujumbe Wake, Sauti ya Mungu iliyothibitishwa kwa ajili ya siku yetu. Ndiyo, tunaamini Kubonyeza Play kwa moyo wetu wote. Ndiyo, tunaamini mjumbe wa wakati wa 7 wa kanisa ndiye aliyeitiwa kumwongoza Bibi-arusi. Ndiyo, hiyo Sauti iliyo kwenye kanda ndiyo Sauti muhimu zaidi yakusikia.

Upendo wa Mungu, Sauti Yake, Ujumbe huu, ni mkuu sana, Ufunuo kama huu kwetu sisi, kwamba hatuwezi kamwe kuuacha. Tumekuwa Mfungwa Kwa jambo hilo.

Tumeuza kila kitu kingine. Haidhuru mtu mwingine yeyote anasema nini, tumefungiwa hatamu Kwake. Kuna jambo fulani kulihusu hili ambalo kamwe hatuwezi kuliacha. Ndio furaha ya maisha yetu. Hatuwezi kuishi bila hilo.

Tuna furaha sana, tunashukuru sana, tunajivunia kuwa Mfungwa kwa ajili ya Bwana na Ujumbe Wake; maana ni mamoja. Ni zaidi ya uhai kwetu. Kila siku inakuwa wazi na halisi zaidi kwamba sisi ni Bibi-arusi Wake. Tuko katika Mapenzi yake makamilifu. Tunaweza kunena Neno, kwa maana sisi ni Neno lililofanyika mwili.

Hatujaunganishwa na chochote ila Kristo na Ujumbe Wake wa saa; hata baba zetu, mama zetu, Ndugu zetu, dada zetu, waume zetu, wake zetu, yeyote yule. Tumeunganishwa tu na Kristo, na Yeye pekee. Tumeunganishwa na kufungwa nira kwa Ujumbe huu, Sauti hii, kwa maana ndiyo Njia ya Mungu iliyoandaliwa kwa ajili ya siku hii, WALA HAKUNA NJIA NYINGINE.

Sisi si wafungwa tena wa utu wetu wenye ubinafsi, wa lengo letu. Tumejitolea kabisa na kufungwa nira Kwake. Haidhuru ulimwengu wote unawaza nini, vile hao wengine ulimwenguni wanavyofanya, tumefungwa kwa vifungo vya upendo Kwake na Sauti Yake.

Tunashukuru sana sisi kuwa Wafungwa. Nieleze, Baba, nini cha kufanya kila sekunde ya kila dakika ya kila siku. Hebu na Sauti Yako itufundishe katika kila jambo tunalofanya, tunalosema, na jinsi tunavyotenda. Hatutaki kujua kingine ila Wewe.

Njoo ufungwe hatamu pamoja nasi kwa Neno la Mungu na Sauti Yake Jumapili hii saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,( Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) tunaposikia jinsi ya kuwa: Mfungwa 63-0717.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya Kusikiliza Ujumbe:

Filemoni 1:1

Maelezo ya ziada:
Ndugu Branham, TUNAPENDA jinsi unavyotamka Filemoni, ni KAMILIFU kwa Bibi-arusi.