All posts by admin5

Pasaka 2025 – Ibada Maalum ya Ushirika na Kutawadhana Miguu

UJUMBE: 62-0204 Ushirika

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi Wa Kristo,

Ni wakati mzuri sana jinsi gani ambao Bibi-arusi atakaokuwa nao Wikendi hii ya Pasaka. Naamini itakuwa moja ya mambo muhimu katika maisha yetu; wakati ambao hatutausahau kamwe. Wikendi kuu maalum.

Kila Pasaka imekuwa wakati ulio maalum kwa Bibi-arusi, tunapoufungia milango yetu ulimwengu wa nje kwa kuvizima vifaa vyetu vyote na vikengeusha-fikira vya kilimwengu, na kuyaweka tu wakfu upya maisha yetu Kwake. Ni wikendi nzima iliyowekwa wakfu kwa ajili Yake katika ibada, tunapozungumza Naye siku nzima kila siku, na kisha kulisikia Neno Lake.

Adui ameyafanya maisha yetu kukengeuka sana na kujaa shughuli za mambo mengi sana ya maisha hadi imekuwa vigumu sana kuufungia ulimwengu nje na kuongea Naye. Hata vifaa vile vile tunavyovitumia kusikia Neno, Shetani hutumia kuhatarisha wakati wetu.

Lakini wikendi hii itakuwa tofauti, na si kama wikendi nyingine ya Pasaka ambayo tumewahi kuwa nayo.

Wakati Bwana alipoweka moyoni mwangu kusikiliza ile Mihuri, sikujua jinsi gani tarehe zingeangukia. Lakini kama kawaida, wakati Wake ni mkamilifu. Jumapili mbili zilizopita, tulikuwa na majaliwa ya kuusikia Muhuri wa 4, Wakati wa Tai, tarehe 6 Aprili, siku ya kuzaliwa ya nabii; jinsi inavyofaa.

Lakini sasa, Bwana anayo hata na zaidi mengi aliyotuwekea sisi. Kama nilivyosema, nilipojisikia Bwana ameweka moyoni mwangu kuicheza Mihuri, nilijua ingechukua wiki kadhaa kumaliza kuicheza kwani kuna Jumbe 10 katika mfululizo huo.

Nilipoitazama kalenda, niliona kwamba Pasaka iliiangia kabla hatujamaliza kuusikia huu mfululizo mzima. Nikawaza mwenyewe, nadhani inatubidi tuache kuisikiliza ile Mihuri na Yeye atanipa Jumbe kwa ajili ya Pasaka.

Mara moja niliona… itakuwa KAMILIFU. Tunaweza kuendelea kuicheza Mihuri huku Muhuri wa Saba ukichezwa Asubuhi ya Jumapili ya Pasaka. Sikuweza kuamini, hilo liliendana kabisa na ratiba. Nilijua papo hapo, HUYU NI WEWE, BWANA.

Nimekuwa nimechangamshwa na nikiwa chini ya matarajio makubwa kwa ajili ya wakati wetu wa Pasaka pamoja na kila mmoja wetu, na pamoja Naye. Nilijua Yeye ametutengenezea ratiba.

Hivyo, ikiwa Bwana akipenda, tutaendelea kuisikiliza Mihuri katika kipindi chote cha Wikendi yetu ya kipekee ya Pasaka.

ALHAMISI

Ilikuwa ni Alhamisi usiku ambapo Bwana Yesu alishiriki Karamu ya Mwisho na wanafunzi Wake, katika ukumbusho wa Pasaka kabla ya kule kutoka kwa wana wa Israeli. Ni fursa iliyoje tuliyo nayo ya kufanya ushirika na Bwana majumbani mwetu, kabla ya wikendi yetu takatifu, na kumwomba atusamehe dhambi zetu, na atupe sisi sote kile tunachohitaji katika safari yetu.

Lijalie, Bwana. Waponye walio wagonjwa. Wafariji walio wachovu. Wape furaha wanaodhulumiwa. Wape amani walio wachovu, Chakula kwa wenye njaa, Maji kwa wenye kiu, furaha kwa wenye huzuni, uwezo kwa kanisa. Bwana, mlete Yesu miongoni mwetu usiku wa leo, tukiwa tunajitayarisha kushiriki ushirika unaowakilisha mwili Wake uliovunjwa-vunjwa. Tunaomba, Bwana, kwamba Yeye atatuzuru kwa njia ya ajabu sana…

Wabariki wengine, Bwana, kila mahali ulimwenguni, ambao wanangojea kwa furaha kuja kwa Bwana, taa zimetengenezwa, na dohani zimesuguliwa kabisa, na Nuru ya Injili ikiangaza katika sehemu zenye giza.

Hebu na tuanze sote saa 12:00 KUMI NA MBILI JIONI. kwa masaa ya nchi unayoishi ili kusikia Ushirika 62-0204, na kisha nabii atatupeleka katika ibada yetu maalum ya Ushirika na Kutawadhana Miguu, ambayo itakuwa ikicheza kwenye app ya Lifeline (kwa Kiingereza), au unaweza kuipakua ibada hiyo kwa Kiingereza au lugha nyinginezo kwa kubofya anuani iliyo hapa chini.

Tukiufuata Ujumbe, tutakusanyika pamoja na familia zetu majumbani mwetu na kuishiriki Meza ya Bwana.

IJUMAA

Hebu na twende kwenye maombi na familia zetu saa 3:00 TATU ASUBUHI(Ni saa 10:00 KUMI JIONI ya Afrika Mashariki)., na kisha tena saa 06:00 SITA MCHANA, (Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) tukimkaribisha Bwana awe pamoja nasi na azijaze nyumba zetu kwa Roho Mtakatifu tunapojiweka wakfu Kwake.

Mawazo yetu na yarudi huko nyuma hadi kwenye siku ile pale Kalvari, yapata miaka 2000 iliyopita, na kumwona Mwokozi wetu akining’inia msalabani, na kisha tujitoe vivyo hivyo kufanya daima yale yanayompendeza Baba:

Iwapo siku hii ni muhimu sana, moja ya siku zilizo kuu sana, hebu na tuangalie mambo matatu ambayo siku hiyo ilimaanisha kwetu. Tungechukua mamia. Bali asubuhi ya leo nimechagua tu mambo matatu tofauti yaliyo muhimu sana ambayo tunataka kuyachunguza katika muda mfupi ujao; ambayo Kalvari ilimaanisha kwetu. Nami naomba ya kwamba itamhukumu kila mwenye dhambi aliyeko, ya kwamba itamfanya kila mtakatifu kupiga magoti yake, ya kwamba itamfanya kila mgonjwa ainue imani yake kwa Mungu na aondoke ameponywa, kila mwenye dhambi aokolewe, kila aliyerudi nyuma arudi na ajionee aibu, na kila mtakatifu afurahi na apate tumaini jipya na tumaini jipya.

Kisha saa 6:30 SITA NA NUSU MCHANA,(Ni saa 1:30 MOJA NA NUSU JIONI ya Afrika Mashariki) Hebu na tuungane pamoja majumbani mwetu kusikia: 63-0323 Muhuri wa Sita.

Kisha tuungane pamoja katika maombi mara baada ya ibada, katika ukumbusho wa kusulubiwa kwa Bwana wetu.

JUMAMOSI

Tuungane tena sote katika maombi Saa 3:00 TATU ASUBUHI (Ni saa 10:00 KUMI JIONI ya Afrika Mashariki) na saa 6:00 Saa SITA MCHANA,(Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) na kuitayarisha mioyo yetu kwa ajili ya mambo makuu Yeye atakayotufanyia miongoni mwetu.

Ninaweza kumsikia akisema, “Shetani, njoo hapa!” Yeye ni Bosi sasa. Ananyosha mkono, anaunyakua ule ufunguo wa mauti na kuzimu kutoka ubavuni mwake, akauning’iniza ubavuni Mwake Mwenyewe. “Ninataka kukupa notisi. Umekuwa laghai muda mrefu kutosha. Mimi ni Mwana wa Mungu aliye hai niliyezaliwa na bikira. Damu Yangu ingali imelowa msalabani, na deni kamili limelipwa! Huna haki tena. Umenyang’anywa zote. Nipe funguo hizo!”

Kisha saa 6:30 SITA NA NUSU MCHANA, sote tutakusanyika pamoja kulisikia NENO: 63-0324m Maswali na Majibu Juu ya Mihuri.

Hii itakuwa SIKU ILIYO MAALUM jinsi gani kwa Bibi-arusi Wake ulimwenguni kote.

Kisha tuungane pamoja katika maombi mara baada ya ibada.

JUMAPILI

Hebu kwanza na tuamke mapema kama vile Ndugu Branham alivyofanya asubuhi wakati rafiki yake mdogo, robin, alipomwamsha saa 11:00 ASUBUHI.. Hebu na tumshukuru tu Bwana kwa kumfufua Yesu kutoka kwa wafu:

Saa kumi na moja asubuhi ya leo, maskini rafiki yangu mwenye kifua chekundu aliruka dirishani akaniamsha. Ilionekana kana kwamba moyo wake mdogo ungepasuka, akisema, “Amefufuka.”

Saa 3:00 TATU ASUBUHI (Ni saa 10:00 KUMI JIONI ya Afrika Mashariki) na saa 6:00 Saa SITA MCHANA,(Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) tuungane kwa mara nyingine tena katika mnyororo wetu wa maombi, tuombeane na kujitayarisha kuisikia Sauti ya Mungu.

Saa 6:30 SITA NA NUSU MCHANA, (Ni saa 1:30 MOJA NA NUSU JIONI ya Afrika Mashariki) tutakusanyika pamoja kuusikia Ujumbe wetu wa Pasaka: 63-0324e Muhuri wa Saba.

Saa 9:00 TISA ALASIRI, Hebu na tuungane tena katika maombi, tumshukuru Yeye kwa Ajili ya WIKENDI YA AJABU ALIOTUPATIA KUWA PAMOJA NAYE NA PAMOJA NA BIBI-ARUSI WAKE ULIMWENGUNI KOTE.

Kwa ndugu na dada zangu walio nchi za ng’ambo, kama vile mwaka jana, ningependa kuwaalika kuungana nasi kwa masaa ya Jeffersonville, katika nyakati zote za maombi kwenye ratiba hii. Ninatambua, hata hivyo, kwamba kuzicheza Kanda Alhamisi, Ijumaa, na Jumamosi alasiri kwa masaa ya Jeffersonville ingekuwa vigumu sana kwa wengi wenu, kwa hivyo tafadhali jisikieni huru kuzicheza Jumbe hizo katika masaa yanayowafaa. Ningependa, hata hivyo, tuungane pamoja sote Jumapili saa 6:30 SITA NA NUSU MCHANA, saa za Jeffersonville, (Ni saa 1:30 MOJA NA NUSU JIONI ya Afrika Mashariki) ili kuusikia Ujumbe wetu wa Jumapili pamoja.

Ningependa pia kukualika wewe na watoto wako kushiriki vipindi vya Creations, Journaling, na maswali ya YF, ambayo familia yako yote inaweza kufurahia pamoja. Tunafikiri mtayapenda kwa kuwa yote yanalenga NENO tutakalosikiliza wikendi hii.

Kwa ratiba ya wikendi, taarifa ya kuhusu jinsi ya kujiandaa na ibada ya Ushirika, nyenzo zitakazohitajika kwa ajili ya vipindi vya Creations, Maswali ya Pasaka, na taarifa nyinginezo, tazama anuani zilizopo hapa chini.

Hebu na tuzifunge simu zetu kwa ajili ya wikendi ya Pasaka isipokuwa kupiga picha, kusikia Nukuu ya Siku, na kucheza kanda kwenye app ya the Table, app ya Lifeline, au anuani inayoweza kupakuliwa.

Ni heshima kubwa kwangu kukualika wewe na familia yako kukusanyika pamoja na Bibi-arusi kote ulimwenguni kwa ajili ya wikendi iliyosheheni IBADA, SIFA NA UPONYAJI. Ninaamini kweli ni wikendi ambayo itayabadilisha maisha yako milele.

Ndugu Joseph Branham

Unahitaji anuani za:

Vitu vya kupakuliwa

Ibada ya Ushirika na Kutawadhana

Kalenda ya ratiba

https://vgrwebsites.blob.core.windows.net/branhamtabernacle/48eec3f2-152c-4c94-8dd1-0a639108de49.pdf

https://vgrwebsites.blob.core.windows.net/branhamtabernacle/48eec3f2-152c-4c94-8dd1-0a639108de49.pdf

Taarifa juu ya jinsi ya kujiandaa na Ushirika

https://branhamtabernacle.org/en/articles/view/1212021_InstructionsForBakingBreadMakingWine

Nyenzo zinazohitajika kwa ajili vipindi vya Creations

https://youngfoundations.org/easter

Maswali ya Pasaka

https://youngfoundations.org/articles/TheRevelationOfTheSevenSeals

ALHAMISI– 6:00 PM (saa za ndani)

62-0204 Ushirika (Huduma Maalum ya Ushirika na Kuosha Miguu)

IJUMAA – saa 06:30 SITA NA NUSU MCHANA (saa za nchi mnayoishi)

63-0323
Muhuri wa Sita

JUMAMOSI– saa 06:30 SITA NA NUSU MCHANA (saa za nchi mnayoishi)

63-0324M
Maswali Na Majibu Juu Ya Mihuri

JUMAPILI– saa 06:30 SITA NA NUSU MCHANA (saa za Jeffersonville) (Ni saa 1:30 MOJA NA NUSU JIONI ya Afrika Mashariki)

63-0324E
Muhuri wa Saba

25-0413 Muhuri Wa Tano

UJUMBE: 63-0322 Muhuri Wa Tano

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Wapumzikao,  

Tumewasili. Tumefika. Kule Kuthibitishwa kwa Neno kumethibitisha ya kwamba Ufunuo wetu wa Ujumbe Huu unatoka kwa Mungu. Tuko katika MAPENZI Yake MAKAMILIFU kwa kudumu na Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda. 

Kubonyeza Play ni muhimu jinsi gani? Maneno tunayosikia kwenye kanda ni muhimu sana, matakatifu sana, hivi Mungu Mwenyewe hata asingeweza kumwamini kumpa hayo Malaika…hata kwa mmoja wa Malaika Wake wa Mbinguni. Ilibidi yafunuliwe na kuletwa kwa Bibi-arusi Wake na nabii Wake, kwa maana huyo ndiye Neno la Mungu humjia, nabii Wake, PEKE YAKE.

Mungu aliichana ile Mihuri, akaikabidhi kwa malaika-mjumbe Wake wa saba wa duniani, na kumfunulia Kitabu chote cha Ufunuo. Kisha, Mungu akanena kupitia malaika Wake wa duniani na kufunua KILA KITU kwa Bibi-arusi Wake. 

Kila maelezo madogo yamenenwa na kufunuliwa kwetu. Mungu ametujali sana hivi kwamba Yeye hakutuambia tu mambo ambayo yametukia hapa duniani tangu mwanzo wa wakati, bali alinena kupitia malaika Wake na kutuambia mambo yanayoendelea katika mahali kama paradiso sasa hivi.

Yeye hakutaka tuhangaike, ama tusiwe na hakika juu ya kile wakati ujao unachoshikilia kwa ajili yetu wakati tuiachapo maskani hii ya kidunia. Kwa hiyo, Mungu Mwenyewe alimchukua malaika Wake wa saba mwenye nguvu ng’ambo ya pazia la wakati, kusudi aweze kuliona, kulihisi, hata azungumze nao kule ng’ambo. Haikuwa ono, alikuwepo KULE.  

Mungu alimpeleka huko ili yeye aweze kurudi na kutuambia: “Nilikuwa huko, nililiona. Linatukia SASA HIVI… Mama zetu, baba zetu, kaka zetu, dada zetu, wanetu, mabinti zetu, wake, waume, babu, Musa, Eliya, WATAKATIFU ​​WOTE ambao waliotangulia huko wamevalia mavazi meupe, wakipumzika na wakitungojea SISI”.

Hatutalia tena, maana Itakuwa ni furaha tupu. Hatutakuwa na huzuni tena, maana itakuwa furaha tupu. Hatutakufa kamwe, maana yote ni Uzima mtupu. Hatuwezi kuzeeka, maana sote tutakuwa vijana milele.  

Ni ukamilifu…kuongeza ukamilifu…kuongeza ukamilifu, nasi tunakwenda huko!! Na kama vile Musa, hatutaacha hata ukwato, SOTE TUNAKWENDA…FAMILIA YETU YOTE.

Ni muhimu jinsi gani KUMPENDA huyo malaika wa saba mwenye nguvu? 

Nayo ikalia, ikasema, “Vyote ulivyowahi kupenda…” thawabu ya huduma yangu. Sihitaji thawabu yo yote. Akasema,“Vyote ulivyowahi kupenda, na wote waliowahi kukupenda,Mungu amekupa.

Hebu tulisome hilo tena tafadhali:  Amesema nini?….Mungu amekupa WEWE!! 

Nasi tutaungana nao na kupaza sauti, “Tunategemea Jambo Hilo”

Tumekitegemeza kikomo chetu cha milele juu ya nini? KILA NENO LILILONENWA KWENYE KANDA. Ninamshukuru sana Bwana kuwa ametupa Ufunuo wa Kweli kwamba Kubonyeza Play ndilo jambo lililo MUHIMU SANA ambalo Bibi-arusi analopaswa kufanya.

Je! ungependa kupumzika pamoja nasi? Njoo uungane nasi Jumapili hii saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) tunaposikia yote yahusuyo wakati ujao unachoshikilia, wapi tunakoenda, na jinsi ya kufika huko, tunaposikia Sauti ya Mungu ikinena na kuufungua:   Muhuri Wa Tano 63-0322.

Ndugu. Joseph Branham
    

Maandiko ya kusoma kabla ya kusikiliza Ujumbe:

Danieli 9:20-27
Matendo 15:13-14
Warumi 11:25-26
Ufunuo 6:9-11 / 11:7-8 / 22:8-9

25-0406 Muhuri Wa Nne

UJUMBE: 63-0321 Muhuri Wa Nne

PDF

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Watakatifu Waliozaliwa Kimbinguni,

Baba anatukusanya pamoja kwa Neno Lake, na kule kuthibitishwa kwa Ufunuo huo kunatupa changamko. Yeye alituchagua kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu, kwa maana Yeye alijua tungekuwa waaminifu kwa Neno Lake kwa uchaguzi wetu wenyewe.

Hebu niliseme hilo tena ili liweze kuzama ndani kabisa. Yeye Alitazama kote katika wakati, hadi mwisho kabisa wa nyakati zote, na KUTUONA SISI… hivi unalisikia hilo? ALIKUONA WEWE, ALINIONA MIMI, na akatupenda, kwa sababu kwa uchaguzi wetu wenyewe, sisi tungedumu NA NENO LAKE.

Wakati huohuo, huenda aliwaita pamoja malaika Zake wote na makerubi na kutuelekezea sisi kidole na kusema: “HUYO NDIYE MWANAMKE MWENYEWE,” “HUYO NDIYE BIBI-ARUSI WANGU,” “HAO NDIO AMBAO NIMEKUWA NIKIWASUBIRI!”

Kama vile Yohana, hiyo ndiyo sababu tunapiga makelele haya yote na kupaza sauti, na kumsifu Bwana, tumechangamshwa na Divai Mpya na tunajua, BILA SHAKA HATA CHEMBE, SISI NI Bibi-arusi Wake.

Ni kama mvua na mvua za ngurumo zote ambazo tumekuwa nazo hapa Jeffersonville wiki hii…Sisi pia tunatuma ONYO kwa ulimwengu.

Bibi-arusi anapokea MVUA YA NGURUMO YA UFUNUO, NAYO INATOA MAFURIKO YA UFUNUO. BIBI-ARUSI AMEJIWEKA TAYARI NAO WAMEJITAMBUA WAO NI NANI. NENDA MAHALI SALAMA UPESI. BONYEZA PLAY AMA UANGAMIE.

Hatuishi katika wakati wa Simba, au wakati wa Ndama, wala Wakati wa Mwanadamu; tunaishi katika WAKATI WA TAI, Naye Mungu ametutumia tai mwenye nguvu, Malaki 4, kumwita Bibi-arusi Wake atoke na kumwongoza.

Litakuwa jambo lenye manufaa jinsi gani Jumapili hii, tutakapokuwa tumeungana pamoja tukiusikiliza Muhuri wa Nne. Itakuwa ni Siku ya Kuzaliwa ya nabii-tai mwenye nguvu wa Mungu.

Hebu na tuisherehekee siku hii ya ajabu na tumshukuru Bwana kwa kututumia mjumbe-tai Wake, ambaye aliyemtuma kutuita tutoke na kilifunua Neno Lake.

Ndugu. Joseph Branham

Ujumbe: Muhuri wa Nne 63-0321

Muda: saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville (Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki)

Maandiko ya kusoma kwa ajili ya maandalizi.

Mathayo Mt. 4
Luka Mt. 24:49
Yohana Mt. 6:63
Matendo 2:38
Ufunuo 2:18-23, 6:7-8, 10:1-7, 12:13, 13:1-14, 16:12-16, 19:15-17
Mwanzo 1:1
Zaburi 16:8-11
2 Samweli 6:14
Yeremia 32
Yoeli 2:28
Amosi 3:7
Malaki 4

25-0330 Muhuri Wa Tatu

UJUMBE: 63-0320 Muhuri Wa Tatu

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Hawa Wa Kiroho,

Hebu niianze barua yangu leo ​​na bomu la atomiki la Mungu; si bunduki aina ya 22, BOMU LA ATOMIKI kwa Bibi-arusi wa Yesu Kristo.

Sasa, kama unataka kuandika mambo hayo; bila shaka, nyote mnayajua: Yesu, Yohana 14:12; na Yoeli, Yoeli 2:38; Paulo, Timotheo wa Pili 3; Malaki, mlango wa 4; na Yohana mfunuzi, Ufunuo 10, kumi na saba, moja hadi kumi na saba. Unaona, ni vile vile ambavyo ingetukia sasa!

Notisi na onyo: Nukuu ifuatayo si kwa ajili yako ikiwa wewe unaamini.

“Tunamwelezea sana nabii wa Mungu.” “Huwezi kuwa Bibi-arusi ikiwa tu unamsikiliza nabii.” “Kuzicheza kanda kanisani ni kosa.” “Mwenge umepitishwa; jambo lililo muhimu zaidi leo ni kuwasikiliza wahudumu.” “Kubonyeza play wote kwa wakati mmoja ni dhehebu.”

Kwa kanisa, ni Kitu gani? Neno lililofanyika mwili likifanywa mwili miongoni mwa watu Wake tena! Unaona?

KABUUM…Kwa hivyo kwa kubonyeza play, tunaweza kulisikia Neno lililofanyika mwili, likinena nasi mdomo kwa sikio anapolifunua Neno Lake.

Na mtu fulani anaweza kusema ati Sio SAUTI ILIYO MUHIMU ZAIDI UNAYOPASWA KUISIKIA? Sehemu hii ya nukuu ni kwa ajili yako.

Nao hawaliamini Hilo kamwe.

Kadiri Bwana anavyozidi kutupa sisi Ufunuo zaidi wa Neno Lake, na sisi ni nani, ndivyo kila mtu aliye nje ya Ufunuo huo anavyozidi kuwa mbali zaidi.

Hebu niseme jambo hilo, vizuri hasa, ili mninii… litadidimia ndani sana. Ninataka hili lilipatie hasa. Hiyo ndiyo shida yenu leo, mnaona, hamlijui Neno! Mnaona?

Mungu anao watu waliotiwa mafuta kuhubiri Ujumbe Huu, lakini kuna Yakini moja tu: Neno. Unapomsikia mhudumu, au mtu ye yote akinena, ni lazima uwe na imani ya kuamini kuwa anachokisema ndicho HASA ambacho nabii wa Mungu alichokwisha sema. Neno lao, ufunuo wao, fasiri yao inaweza kushindwa; Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda HAIWEZI KUSHINDWA KAMWE.

Nena kuhusu Mungu katika urahisi kwa kubonyeza play…Yeye analisema TENA.

Wanapitwa Naye, Neno lililo hai lililodhihirishwa katika mwili, kwa Neno lililoahidiwa. Neno liliahidi kufanya mambo haya. Ahadi ilifanywa, ya kwamba itakuwa hivi katika siku za mwisho.

Sikiliza Ngurumo Yake. Ngurumo ni Sauti ya Mungu. William Marrion Branham ndiye Sauti ya Mungu kwa kizazi hiki.

Bi-Bibi arusi hajawa na uamsho bado. Mnaona? Hakujakuwako na uamsho humo, hakujakuwako na madhihirisho ya Mungu kumwamsha Bibi-arusi bado. Mnaona? Tunautarajia huo sasa. Itahitaji hizo Ngurumo Saba zisizojulikana kule nyuma, kumwamsha Yeye tena, unaona. Naam. Yeye atazituma. Aliliahidi. Sasa angalia.

Unaweza kulipindisha hilo ukipenda, lakini zile Ngurumo Saba zitampa Bibi-arusi changamko kwa Ufunuo na imani ya kunyakuliwa, ambayo huja tu kwa Roho Mtakatifu akizungumza kupitia nabii wa Mungu. Hilo linatendeka SASA HIVI ulimwenguni kote. Mungu amemchangamsha Bibi-arusi Wake na Neno Lake.

Si hivyo tu, bali tayari Yeye amekwisha mwambia adui yetu la kufanya.

Usiwaguse. Wao wanajua wanakoenda, kwa maana wametiwa Mafuta Yangu. Na kwa kutiwa kwa Mafuta Yangu, wao wana divai ya furaha, maana wanajua Neno Langu la ahadi, ‘Nitawafufua tena.’ Usidhuru Hao! Usiende ukajaribu kuwachafua.

Yeye amemwambia adui yetu aiondoe mikono yake michafu mbali nasi. Lakini je! ugonjwa bado ungali unaweza kutushambulia? Ndiyo. Je! bado tungali tunayo matatizo? Ndiyo. Lakini Yeye pia alituambia la kufanya.

Ni la kilindi. Lisome polepole na mara tena na tena.

Kabla ya kuwa Neno, ni wazo. Nalo wazo halina budi kuumbwa. Vema. Kwa hiyo, mawazo ya Mungu yakawa uumbaji wakati yaliponenwa, kwa Neno. Hapo ndipo wakati anapoyaleta kwa—kwako kama wazo, wazo Lake, nalo linafunuliwa kwako. Halafu, lingali ni wazo mpaka wewe utakapolinena.

Mawazo Yake yakawa uumbaji wakati yaliponenwa. Kisha, mawazo Yake yaliletwa na kufunuliwa kwetu kama Neno. Sasa lingali ni wazo kwetu mpaka tutakapolinena. KWA HIYO TUNAYANENA… NA KUYAAMINI.

Mimi ni Uzao wa Kifalme wa Ibrahimu. Mimi ni Bibi-arusi wa Kristo. Niliteuliwa na kuchaguliwa tangu zamani kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu kuwa Bibi-arusi Wake, na hakuna kitu kinachoweza kulibadili hilo. Kila ahadi katika Biblia ni yangu. Ni Neno Lake kwangu. Mimi ni mrithi wa Ahadi yenyewe. Yeye ndiye Bwana Mungu aniponyaye magonjwa yangu yote. Chochote ninachokihitaji ni changu, Mungu alisema hivyo.

Mungu katika Urahisi: Imani huja kwa kusikia, kulisikia Neno. Neno huja kwa nabii.

Kila mtu anataka kuzitumia “NUKUU” kuthibitisha mawazo yao, mafikara yao, ujumbe wao. Nao wako sahihi, nafanya vivyo hivyo na mimi, ndio maana yote niwapayo ni nukuu za kuwaambia: Dumuni na Kanda. Isikilizeni hiyo Sauti. Sauti hiyo ni Sauti ya Mungu. Hamna budi kuamini kila Neno lililo kwenye Kanda, si yale mtu mwingine yeyote asemayo. Hiyo Sauti NDIO SAUTI ILIYO MUHIMU ZAIDI MNAYOPASWA KUISIKIA.

Wengine huzitumia nukuu kuwaleta ninyi kwenye huduma yao, kwenye kanisa lao, kwenye fasiri zao, ufunuo wao. “Dumuni na mchungaji wenu.” (Vema, ninaipenda hiyo pia, kwa sababu sisi tunadumu naye, ila tu mchungaji tofauti.) “Yeye siye changarawe pekee ufukoni.” “Yeye hakusema kamwe kuzicheza kanda kanisani.”

Usiweke fasiri yo yote ya kibinafsi Kwake. Yeye anataka Neno lililo safi, lisiloghoshiwa, hata ubembe wo wote usiwepo. Singetaka mke wangu afanye ubembe na mwanamume mwingine. Na unapoanza kusikiliza hoja za namna yo yote, zaidi ya Hilo, unasikiliza, unafanya ubembe na Shetani. Amina! Hilo halikufanyi ujisikie kubarikiwa? Mungu anakutaka ubakie msafi kabisa. Udumu daima hapo na Neno hilo. Dumu Nalo. Vema.

Mimi na nyumba yangu, tutabonyeza play na kulifuata Neno la Mungu lililofanyika Mwili linenalo kupitia malaika-mjumbe Wake wa saba. Hatutaongeza fasiri yetu ya kibinafsi Kwake; hatutabembana au kusikiliza hoja yoyote. TUTADUMU NA NENO HILO KAMA LILIVYONENWA KWENYE KANDA. Ni Mungu katika Urahisi.

Ni wakati mtukufu jinsi gani tutakaokuwa nao Jumapili hii saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) Tusikiapo: Muhuri Wa Tatu 63-0320. Ningependa kuwaalika mje mkaungane nasi tunapoungana katika Neno la leo.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya kusikiliza Ujumbe:

Mathayo mt. 25:3-4
Yohana Mt. 1:1, 1:14, 14:12, 17:17
Matendo Sura ya 2
I Timotheo 3:16
Waebrania 4:12, 13:8
1 Yohana 5:7
Mambo ya Walawi 8:12
Yeremia Sura ya 32
Yoeli 2:28
Zekaria 4:12

Hebu nichukue fursa hii kuliweka wazi kwa mara nyingine tena. Mimi sipingani na huduma tano. Ninaamini katika huduma tano. Sioni ni vibaya kumsikiliza mhudumu. Naamini unapaswa kumsikiliza mchungaji wako pale ambapo Mungu amekuweka. Nisemalo ni kwamba, Ninaamini Mungu alimtuma nabii katika siku yetu. Mungu alilifunua Neno Lake kwa nabii Wake. Mimi naweza kukosea, mchungaji wako anaweza kukosea, lakini LAZIMA tukubaliane (tukisema tunauamini UJUMBE HUU ni kweli na Ndugu Branham ni nabii wa Mungu) yale yaliyosemwa kwenye kanda ni Bwana Asema Hivi. Kama huamini hilo, basi wewe huamini Ujumbe huu. Hivyo, Mimi ninaamini ndio SAUTI ILIYO MUHIMU ZAIDI UNAYOPASWA KUISIKIA. Huhitaji kunisikia mimi, huhitaji kumsikia mtu mwingine yeyote, lakini LAZIMA UISIKIE SAUTI HIYO ILIYO KWENYE KANDA.

25-0323 Muhuri Wa Pili

UJUMBE: 63-0319 Muhuri Wa Pili

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Wapendwa wasikilizaji Wa Kanda,

Swali: Je! tuko katika Mapenzi Yake makamilifu kwa kuzicheza Kanda?
Jibu: NDIYO.

Swali: Je! Bibi-arusi anahitaji zaidi ya yale yaliyosemwa kwenye Kanda?
Jibu: HAPANA.

Swali: Je! tunakosa kitu kwa sisi kusikiliza Kanda TU?
Jibu: HAPANA.

Swali: Je! tunaweza kuwa Bibi-arusi kwa kusikiliza Kanda TU?
Jibu: NDIYO, KWA MSISITIZO ZAIDI!

Sasa kumbukeni, “Hakuna lo lote linaloweza kufunuliwa; Mungu hatafanya neno lo lote, hata kidogo, mpaka kwanza alifunue kwa watumishi Wake, manabii.”

Hivyo, YOTE tunayohitaji yamekwisha nenwa na yako kwenye kanda; au, wakati malaika Wake wa saba atakaporudi duniani, YEYE atatuambia basi.

Loo! Bibi-arusi, hebu na tuwazie kile kinachotendeka miongoni mwa Bibi-arusi wa Kristo ulimwenguni kote. Baba anamkusanya Bibi-arusi Wake pamoja kwa Sauti Yake Naye Ananguruma, “Bwana Asema Hivi.”

Kumbukeni, alituambia zile Ngurumo zilikuwa kitu gani: “sauti kuu ya kishindo cha Ngurumo ni Sauti ya Mungu”. Nayo Sauti ya Mungu kwa Bibi-arusi ni nini? Malaika-mjumbe wa saba wa Mungu, William Marrion Branham.

Yeye alisema kunakuja Ngurumo saba za siri ambazo hata hazijaandikwa kamwe. Na ya kwamba kupitia Ngurumo hizo Saba, zitamkusanya Bibi-arusi pamoja kwa ajili ya kupata imani ya kunyakuliwa.

Neno la Bwana huwajia manabii Wake. Kama angekuwa na utaratibu bora zaidi, angeliutumia. Yeye alichagua utaratibu bora zaidi ya wote hapo mwanzo Naye hawezi, na hatabadilika.

Kwa hiyo, Sauti ya Mungu, inayonena kupitia malaika Wake wa saba, inamkusanya Bibi-arusi Wake pamoja na kutupa Imani ya Kunyakuliwa.

Kanisa halijashangaa tangu mwaka wa 1933, kule chini mtoni siku ile, ya kwamba William Marrion Branham ndiye Sauti ya Mungu, Inayonguruma, “Bwana Asema Hivi,” naye alitumwa kumwita, kumkusanya, na kumwongoza Bibi-arusi.

Ningependa kuwaalika mje msikilize pamoja nasi Jumapili saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville, (Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) wakati Bwana wetu Yesu anapokifungua kile Kitabu, kuuvunja huo Muhuri, na kuutuma duniani, kwa malaika Wake wa saba, atufunulie huo SISI!

Ndugu. Joseph Branham

Tarehe: Jumapili, 23 Machi, 2025

Ujumbe: Muhuri wa Pili 63-0319

Muda: Saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville (Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki)

Maandiko ya kusoma kabla ya kuusikiliza Ujumbe:

Mathayo Mt. 4:8 /11:25-26 / 24:6
Marko Mt. 16:16
Yohana Mt. 14:12
2 Wathesalonike 2:3
Waebrania 4:12
Ufunuo 2:6 / 6:3-4 / Sura ya 17 / 19:11-16
Yoeli 2:25
Amosi 3:6-7

25-0316 Muhuri Wa Kwanza

UJUMBE: 63-0318 Muhuri Wa Kwanza

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Kipenzi Malkia wa Mbinguni,

Ninayo mengi sana kwa ajili yako Jumapili hii. Kwanza, utasikia kishindo cha Ngurumo. Itakuwa Sauti Yangu, Sauti ya Mungu ikinena nawe, Bibi-arusi Wangu. Nitakuwa nikikufunulia wewe Neno Langu zaidi ya hapo awali. Utaniona Mimi, yule Mwana-Kondoo aliyelowa damu ambaye aliyechinjwa tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu, nikikitwaa na kukifungua kile Kitabu, na kuichana ile Mihuri, na kukituma duniani, kwa malaika-mjumbe Wangu wa saba, William Marrion Branham, kuwafunulia NINYI siri ambazo zimefichwa tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu!

Kutakuwa na vigelegele, vifijo, na zile haleluya kutoka kote ulimwenguni wakati nizungumzapo nawe. Simba atakuwa akinguruma; watiwa mafuta, nguvu, utukufu, dhihirisho haitaelezeka. Wewe, Malkia Wangu, utakuwa umeketi pamoja katika ulimwengu wa roho Nikisema nawe na kukupa Imani ya kunyakuliwa.

Kumbuka, huna budi kuwa na hiyo Imani waliokabidhiwa watakatifu mara moja. Nilikuambia, lazima umsikilize malaika Wangu Niliyekutumia.

Yeye “atairudisha Imani ya watoto ielekee baba zao.” Ile imani asili ya Biblia itarudishwa na malaika wa saba.

Neno Langu linakuambia, katika siku za Sauti ya malaika wa saba, kupiga kwake baragumu, kupiga baragumu ya Injili; anapaswa kumaliza siri zote za Mungu. Hakuwezi kuwa na kitu hata kimoja chakuongezwa na hakuna kitu chakuondolewa kutoka kwenye yale niliyosema kwenye kanda; wewe sema tu kile Nilichosema Mimi kupitia malaika-mjumbe Wangu. Ndio maana niliirekodi, ili uweze tu KUBONYEZA PLAY na kusikia hasa kile nilichosema, na jinsi Nilivyosema. Itakupa Imani ya Kunyakuliwa.

Malkia Wangu kipenzi, Machoni Pangu, wewe ni mkamilifu, huna dhambi kabisa mbele Zangu. Usijali, HUTAPITIA katika ile dhiki; kwa kuwa umeikubali Damu Yangu, Neno Langu, malaika Wangu, Sauti Yangu, hivyo huna dhambi kabisa mbele Zangu.

Ninayo mambo makubwa sana niliyokutunzia. Unaliona Neno Langu likifunuliwa mbele ya macho yako kila siku. Nimekuwa nikiziweka ishara angani kukuambia wewe jambo fulani liko karibu kutukia. Ninakuja, jiandae. Liweke Neno Langu, Sauti Yangu, kuwa ya kwanza katika maisha yako.

Weka kila kitu kando, hakuna kitu kilicho muhimu zaidi kuliko Neno Langu. Najua adui anajaribu kukuangusha chini, lakini nilikuahidi nitakuinua. Mimi nipo pamoja nawe, hata NDANI YAKO. Wewe na Mimi tunakuwa Mmoja ninapokufunulia Neno Langu. Unajua moyoni mwako, wewe ndiwe Bibi-arusi Malkia Wangu. Unajua nilikuchagua tangu awali. Unajua Nakupenda. Unajua Niko pamoja nawe kila sekunde ya kila siku. Unajua SITAKUACHA KAMWE.

Tutakuwa na wakati mzuri sana pindi Ninapokufunulia zaidi kila Jumapili, kila siku, unaponisikia Mimi nikinena kila Jumapili, Nikinena nawe kupitia malaika Wangu. Huenda wengine wasielewe au kuona kile wewe unachokiona, lakini Imetia nanga ndani ya moyo wako kwamba hii ndiyo Njia Yangu niliyoiandaa.

Ni kimbilio lililoje nililokuwekea. Unaweza kwa urahisi tu Bonyeza Play wakati wowote, mchana au usiku, kunisikia Mimi nikinena nawe. Nitailetea faraja nafsi yako wakati ninapolifunua Neno Langu na kukuambia wewe ni nani. Kila Ujumbe ni kwa ajili yako, na kwa ajili yako peke yako. Tunaweza kushiriki na kuabudu pamoja wakati wowote unapotaka.

Jumapili saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville, (Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) sehemu ya Bibi-arusi itakusanyika kutoka ulimwenguni kote kuzisikia siri hizi kuu zikifunuliwa. Ninawaalika mje mkaungane nasi tunaposikia, 63-0318 – “Muhuri Wa Kwanza”.

Ndugu. Joseph

Maandiko ya kusoma kwa ajili ya maandalizi ya kusikiliza Ujumbe:

Mathayo Mt 10:1 / 11:1-14 / 24:6 / 28:19
Yohana 12:23-28
Matendo 2:38
2 Wathesalonike 2:3-12
Waebrania 4:12
Ufunuo 6:1-2 / 10:1-7 / 12:7-9 / 13:16 / 19:11-16
Malaki Sura ya 3 na 4
Danieli 8:23-25 ​​/ 11:21 / 9:25-27

25-0309 Pengo Kati Ya Nyakati Saba Za Kanisa Na Ile Mihuri Saba

UJUMBE: 63-0317E Pengo Kati Ya Nyakati Saba Za Kanisa Na Ile Mihuri Saba

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Waliorejeshwa,

Sichoki kamwe kuisikia Sauti ya Mungu ikituambia sisi ni nani, wapi tunatoka, wapi tunakwenda, sisi ni warithi wa nini, na jinsi gani Yeye anavyotupenda.

Ukuhani wa kiroho, taifa la kifalme, wanaomtolea Mungu dhabihu za kiroho, matunda ya midomo yao, wakilisifu Jina Lake.” Ni watu wa—wa ajabu jinsi gani! Yeye anao.

Faraja na amani yetu pekee huja kwa kuisikia Sauti ya Mungu ikinena nasi, kisha tunamjibu Baba kwa kutoa dhabihu za kiroho kwa matunda ya midomo yetu, tukilisifu Jina Lake.

Ulimwengu wote huu unaugua. Maumbile yanaugua. Tunaugua na kungojea kule kuja kwa Bwana. Dunia hii haina kitu kwetu sisi. Tuko tayari kuondoka na kwenda kwenye Karamu yetu ya Arusi na Makao ya Baadaye pamoja Naye na wale wote ambao tayari wako Huko, ng’ambo tu ya pazia la wakati, wakitungojea.

Hebu na tuamke na tujitikise! Tufinye dhamiri zetu, tuamke kwa kile kinachoendelea sasa hivi na kile kinachoenda kutukia katika dakika moja kufumba na kufumbua jicho.

Kamwe katika historia ya ulimwengu haijawahi kuwezekana kwa Bibi-arusi wa Kristo kuungana kutoka ulimwenguni kote, wote kwa wakati ule ule mmoja, kuisikia Sauti ya Mungu ikinena na kulifunua Neno Lake kwa Bibi-arusi Wake.

Enyi Waaminio, jiulizeni wenyewe, ni sauti gani, mhudumu gani, ni mtu gani anayeweza kumuunganisha na kumkusanya Bibi-arusi wa Kristo wote pamoja? Kama wewe ni Bibi-arusi wa Kristo, unajua kwa urahisi hakuna kabisa Sauti nyingine ila Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda.

Ndiyo, Roho Mtakatifu yu ndani ya kila mmoja wetu, kila ofisi ya kanisa, lakini Mungu Mwenyewe alituambia angeuhukumu ulimwengu kwa Neno Lake. Bibi-arusi anajua Neno Lake huja kwa nabii Wake. Nabii Wake ndiye mfasiri PEKEE wa Kiungu wa Neno Lake. Kile asemacho hakiwezi kuongezewa lolote wala kuondolewa kitu. Ni Neno, lililo kwenye kanda, ndilo sisi sote tutakalohukumiwa kwalo, na wala si neno lingine ama fasiri ya Neno hilo.

Haiwezekani kwa sauti nyingine yoyote kumuunganisha Bibi-arusi. Ni Sauti ya Mungu peke yake iliyo kwenye kanda ndio inayoweza kumuunganisha Bibi-arusi Wake. Ndilo Neno pekee ambalo Bibi-arusi wanaloweza kukubaliana kwalo. Ndio Sauti pekee ambayo Mungu Mwenyewe aliithibitisha kuwa Sauti Yake kwa Bibi-arusi Wake. Bibi-arusi Wake lazima awe katika Nia Moja na Moyo Mmoja ili kuwa pamoja Naye.

Wahudumu wanaweza kuhudumu, waalimu wanaweza kufundisha, wachungaji wanaweza kuchunga, lakini Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda lazima iwe ndio Sauti iliyo muhimu zaidi wanayopaswa kuiweka mbele ya watu. Ndio Yakini ya Bibi-arusi.

Ikiwa unao Ufunuo wa jambo hilo, basi hiki ndicho kitakachoenda kutukia.

Neno linatuambia Adamu alipoteza urithi wake, dunia. Ulitoka mkononi mwake ukaenda kwa yule aliyemwuzia, Shetani. Aliuza imani yake katika Mungu, akachukua hoja za Shetani. Akapoteza kila kitu kikaenda kwenye mikono ya Shetani. Aliutoa mkononi mwake akampa Shetani.

Mungu ni Mungu wa ulimwengu, kila mahali. Lakini mwanawe alikuwa na mamlaka juu ya dunia hii. Angeweza kunena, aliweza kutoa majina, aliweza kusema, aliweza kusimamisha maumbile, aliweza kufanya lo lote alilotaka kufanya. Alikuwa na mamlaka makamilifu juu ya dunia.

Adamu alipoteza yote, lakini utukufu kwa Mungu, yote yeye aliyopoteza na kuachilia yamekombolewa na Mkombozi wetu aliye Jamaa wa Karibu, si mwingine ila Mungu Mwenyezi, ambaye alifanyika Imanueli, mmoja wetu. SASA, NI YETU.

Sisi ni wana na binti Zake watakaotawala na kuwa wafalme na makuhani pamoja Naye. Tunao uzima wa milele pamoja Naye na wale wote tuwapendao. Hakuna magonjwa tena, hakuna huzuni tena, hakuna kifo tena, yote ni milele tu pamoja.

Tunapoliwazia hilo, tunawezaje kumwacha shetani atushushe? Ni YETU, huko ndiko tunakoelekea hivi karibuni. Yeye ametupa jambo lililo kuu zaidi awezalo kutupa. Siku hizi chache za mitihani na majaribu hapa duniani zinamezwa kwa haraka na USHINDI wetu MKUU ULIO SIKU CHACHE TU ZIJAZO MBELE YETU.

IMANI yetu haijawahi kuwa kubwa jinsi hii. Furaha yetu haijawahi kuwa juu jinsi hii. Tunajua sisi ni nani na ni wapi tunakoenda. Tunajua tuko katika Mapenzi Yake makamilifu kwa kudumu na Neno Lake. Yote tunayohitaji kufanya ni kudumu na kanda na kuamini kila Neno; si kulielewa lote, BALI KUAMINI KILA NENO…nasi TUNAAMINI!

Imani huja kwa kusikia, kulisikia Neno. Neno huja kwa nabii. Mungu alilinena Hilo. Mungu alilirekodi Hilo. Mungu alilifunua Hilo. Tunalisikia Hilo. Tunaliamini Hilo.

Unaweza tu kuupata Ufunuo huu kwa kuisikia Sauti ya Mungu kwenye kanda.

“Yote yale ambayo Kristo atafanya wakati wa mwisho yatafunuliwa kwetu juma hili, katika ile Mihuri Saba, kama Mungu ataturuhusu. Unaona? Vema. Yatafunuliwa. Na kufunuliwa, wakati Mihuri hii inapovunjwa na kufunguliwa kwetu, ndipo tunaweza kuona mpango huu mkubwa wa ukombozi ulivyo, na ni lini na ni vipi utafanyika. Yote yamefichwa katika Kitabu hiki cha siri hapa. Kimetiwa muhuri, kimefungwa kwa Mihuri Saba, na kwa hiyo Mwana-Kondoo Ndiye pekee Ambaye anaweza kuivunja.

Jumapili hii saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville, (Ni Saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) sehemu ya Bibi-arusi kutoka ulimwenguni kote watakuwa wakiisikiliza Sauti ya Mungu wote kwa wakati mmoja. Tutakuwa tukiivumisha mbingu kwa maombi yetu na kumwabudu. Ninawaalika mje muungane nasi tunaposikia: Pengo Kati ya Nyakati Saba za Kanisa na ile Mihuri Saba 63-0317E.

Tafadhali msisahau kuhusu mabadiliko ya masaa huko Jeffersonville wikendi hii.

Ndugu. Joseph Branham