Swali: Je! tuko katika Mapenzi Yake makamilifu kwa kuzicheza Kanda? Jibu: NDIYO.
Swali: Je! Bibi-arusi anahitaji zaidi ya yale yaliyosemwa kwenye Kanda? Jibu: HAPANA.
Swali: Je! tunakosa kitu kwa sisi kusikiliza Kanda TU? Jibu: HAPANA.
Swali: Je! tunaweza kuwa Bibi-arusi kwa kusikiliza Kanda TU? Jibu: NDIYO, KWA MSISITIZO ZAIDI!
Sasa kumbukeni, “Hakuna lo lote linaloweza kufunuliwa; Mungu hatafanya neno lo lote, hata kidogo, mpaka kwanza alifunue kwa watumishi Wake, manabii.”
Hivyo, YOTE tunayohitaji yamekwisha nenwa na yako kwenye kanda; au, wakati malaika Wake wa saba atakaporudi duniani, YEYE atatuambia basi.
Loo! Bibi-arusi, hebu na tuwazie kile kinachotendeka miongoni mwa Bibi-arusi wa Kristo ulimwenguni kote. Baba anamkusanya Bibi-arusi Wake pamoja kwa Sauti Yake Naye Ananguruma, “Bwana Asema Hivi.”
Kumbukeni, alituambia zile Ngurumo zilikuwa kitu gani: “sauti kuu ya kishindo cha Ngurumo ni Sauti ya Mungu”. Nayo Sauti ya Mungu kwa Bibi-arusi ni nini? Malaika-mjumbe wa saba wa Mungu, William Marrion Branham.
Yeye alisema kunakuja Ngurumo saba za siri ambazo hata hazijaandikwa kamwe. Na ya kwamba kupitia Ngurumo hizo Saba, zitamkusanya Bibi-arusi pamoja kwa ajili ya kupata imani ya kunyakuliwa.
Neno la Bwana huwajia manabii Wake. Kama angekuwa na utaratibu bora zaidi, angeliutumia. Yeye alichagua utaratibu bora zaidi ya wote hapo mwanzo Naye hawezi, na hatabadilika.
Kwa hiyo, Sauti ya Mungu, inayonena kupitia malaika Wake wa saba, inamkusanya Bibi-arusi Wake pamoja na kutupa Imani ya Kunyakuliwa.
Kanisa halijashangaa tangu mwaka wa 1933, kule chini mtoni siku ile, ya kwamba William Marrion Branham ndiye Sauti ya Mungu, Inayonguruma, “Bwana Asema Hivi,” naye alitumwa kumwita, kumkusanya, na kumwongoza Bibi-arusi.
Ningependa kuwaalika mje msikilize pamoja nasi Jumapili saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville, (Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) wakati Bwana wetu Yesu anapokifungua kile Kitabu, kuuvunja huo Muhuri, na kuutuma duniani, kwa malaika Wake wa saba, atufunulie huo SISI!
Ndugu. Joseph Branham
Tarehe: Jumapili, 23 Machi, 2025
Ujumbe: Muhuri wa Pili 63-0319
Muda: Saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville (Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki)
Ninayo mengi sana kwa ajili yako Jumapili hii. Kwanza, utasikia kishindo cha Ngurumo. Itakuwa Sauti Yangu, Sauti ya Mungu ikinena nawe, Bibi-arusi Wangu. Nitakuwa nikikufunulia wewe Neno Langu zaidi ya hapo awali. Utaniona Mimi, yule Mwana-Kondoo aliyelowa damu ambaye aliyechinjwa tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu, nikikitwaa na kukifungua kile Kitabu, na kuichana ile Mihuri, na kukituma duniani, kwa malaika-mjumbe Wangu wa saba, William Marrion Branham, kuwafunulia NINYI siri ambazo zimefichwa tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu!
Kutakuwa na vigelegele, vifijo, na zile haleluya kutoka kote ulimwenguni wakati nizungumzapo nawe. Simba atakuwa akinguruma; watiwa mafuta, nguvu, utukufu, dhihirisho haitaelezeka. Wewe, Malkia Wangu, utakuwa umeketi pamoja katika ulimwengu wa roho Nikisema nawe na kukupa Imani ya kunyakuliwa.
Kumbuka, huna budi kuwa na hiyo Imani waliokabidhiwa watakatifu mara moja. Nilikuambia, lazima umsikilize malaika Wangu Niliyekutumia.
Yeye “atairudisha Imani ya watoto ielekee baba zao.” Ile imani asili ya Biblia itarudishwa na malaika wa saba.
Neno Langu linakuambia, katika siku za Sauti ya malaika wa saba, kupiga kwake baragumu, kupiga baragumu ya Injili; anapaswa kumaliza siri zote za Mungu. Hakuwezi kuwa na kitu hata kimoja chakuongezwa na hakuna kitu chakuondolewa kutoka kwenye yale niliyosema kwenye kanda; wewe sema tu kile Nilichosema Mimi kupitia malaika-mjumbe Wangu. Ndio maana niliirekodi, ili uweze tu KUBONYEZA PLAY na kusikia hasa kile nilichosema, na jinsi Nilivyosema. Itakupa Imani ya Kunyakuliwa.
Malkia Wangu kipenzi, Machoni Pangu, wewe ni mkamilifu, huna dhambi kabisa mbele Zangu. Usijali, HUTAPITIA katika ile dhiki; kwa kuwa umeikubali Damu Yangu, Neno Langu, malaika Wangu, Sauti Yangu, hivyo huna dhambi kabisa mbele Zangu.
Ninayo mambo makubwa sana niliyokutunzia. Unaliona Neno Langu likifunuliwa mbele ya macho yako kila siku. Nimekuwa nikiziweka ishara angani kukuambia wewe jambo fulani liko karibu kutukia. Ninakuja, jiandae. Liweke Neno Langu, Sauti Yangu, kuwa ya kwanza katika maisha yako.
Weka kila kitu kando, hakuna kitu kilicho muhimu zaidi kuliko Neno Langu. Najua adui anajaribu kukuangusha chini, lakini nilikuahidi nitakuinua. Mimi nipo pamoja nawe, hata NDANI YAKO. Wewe na Mimi tunakuwa Mmoja ninapokufunulia Neno Langu. Unajua moyoni mwako, wewe ndiwe Bibi-arusi Malkia Wangu. Unajua nilikuchagua tangu awali. Unajua Nakupenda. Unajua Niko pamoja nawe kila sekunde ya kila siku. Unajua SITAKUACHA KAMWE.
Tutakuwa na wakati mzuri sana pindi Ninapokufunulia zaidi kila Jumapili, kila siku, unaponisikia Mimi nikinena kila Jumapili, Nikinena nawe kupitia malaika Wangu. Huenda wengine wasielewe au kuona kile wewe unachokiona, lakini Imetia nanga ndani ya moyo wako kwamba hii ndiyo Njia Yangu niliyoiandaa.
Ni kimbilio lililoje nililokuwekea. Unaweza kwa urahisi tu Bonyeza Play wakati wowote, mchana au usiku, kunisikia Mimi nikinena nawe. Nitailetea faraja nafsi yako wakati ninapolifunua Neno Langu na kukuambia wewe ni nani. Kila Ujumbe ni kwa ajili yako, na kwa ajili yako peke yako. Tunaweza kushiriki na kuabudu pamoja wakati wowote unapotaka.
Jumapili saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville, (Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) sehemu ya Bibi-arusi itakusanyika kutoka ulimwenguni kote kuzisikia siri hizi kuu zikifunuliwa. Ninawaalika mje mkaungane nasi tunaposikia, 63-0318 – “Muhuri Wa Kwanza”.
Ndugu. Joseph
Maandiko ya kusoma kwa ajili ya maandalizi ya kusikiliza Ujumbe:
Sichoki kamwe kuisikia Sauti ya Mungu ikituambia sisi ni nani, wapi tunatoka, wapi tunakwenda, sisi ni warithi wa nini, na jinsi gani Yeye anavyotupenda.
Ukuhani wa kiroho, taifa la kifalme, wanaomtolea Mungu dhabihu za kiroho, matunda ya midomo yao, wakilisifu Jina Lake.” Ni watu wa—wa ajabu jinsi gani! Yeye anao.
Faraja na amani yetu pekee huja kwa kuisikia Sauti ya Mungu ikinena nasi, kisha tunamjibu Baba kwa kutoa dhabihu za kiroho kwa matunda ya midomo yetu, tukilisifu Jina Lake.
Ulimwengu wote huu unaugua. Maumbile yanaugua. Tunaugua na kungojea kule kuja kwa Bwana. Dunia hii haina kitu kwetu sisi. Tuko tayari kuondoka na kwenda kwenye Karamu yetu ya Arusi na Makao ya Baadaye pamoja Naye na wale wote ambao tayari wako Huko, ng’ambo tu ya pazia la wakati, wakitungojea.
Hebu na tuamke na tujitikise! Tufinye dhamiri zetu, tuamke kwa kile kinachoendelea sasa hivi na kile kinachoenda kutukia katika dakika moja kufumba na kufumbua jicho.
Kamwe katika historia ya ulimwengu haijawahi kuwezekana kwa Bibi-arusi wa Kristo kuungana kutoka ulimwenguni kote, wote kwa wakati ule ule mmoja, kuisikia Sauti ya Mungu ikinena na kulifunua Neno Lake kwa Bibi-arusi Wake.
Enyi Waaminio, jiulizeni wenyewe, ni sauti gani, mhudumu gani, ni mtu gani anayeweza kumuunganisha na kumkusanya Bibi-arusi wa Kristo wote pamoja? Kama wewe ni Bibi-arusi wa Kristo, unajua kwa urahisi hakuna kabisa Sauti nyingine ila Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda.
Ndiyo, Roho Mtakatifu yu ndani ya kila mmoja wetu, kila ofisi ya kanisa, lakini Mungu Mwenyewe alituambia angeuhukumu ulimwengu kwa Neno Lake. Bibi-arusi anajua Neno Lake huja kwa nabii Wake. Nabii Wake ndiye mfasiri PEKEE wa Kiungu wa Neno Lake. Kile asemacho hakiwezi kuongezewa lolote wala kuondolewa kitu. Ni Neno, lililo kwenye kanda, ndilo sisi sote tutakalohukumiwa kwalo, na wala si neno lingine ama fasiri ya Neno hilo.
Haiwezekani kwa sauti nyingine yoyote kumuunganisha Bibi-arusi. Ni Sauti ya Mungu peke yake iliyo kwenye kanda ndio inayoweza kumuunganisha Bibi-arusi Wake. Ndilo Neno pekee ambalo Bibi-arusi wanaloweza kukubaliana kwalo. Ndio Sauti pekee ambayo Mungu Mwenyewe aliithibitisha kuwa Sauti Yake kwa Bibi-arusi Wake. Bibi-arusi Wake lazima awe katika Nia Moja na Moyo Mmoja ili kuwa pamoja Naye.
Wahudumu wanaweza kuhudumu, waalimu wanaweza kufundisha, wachungaji wanaweza kuchunga, lakini Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda lazima iwe ndio Sauti iliyo muhimu zaidi wanayopaswa kuiweka mbele ya watu. Ndio Yakini ya Bibi-arusi.
Ikiwa unao Ufunuo wa jambo hilo, basi hiki ndicho kitakachoenda kutukia.
Neno linatuambia Adamu alipoteza urithi wake, dunia. Ulitoka mkononi mwake ukaenda kwa yule aliyemwuzia, Shetani. Aliuza imani yake katika Mungu, akachukua hoja za Shetani. Akapoteza kila kitu kikaenda kwenye mikono ya Shetani. Aliutoa mkononi mwake akampa Shetani.
Mungu ni Mungu wa ulimwengu, kila mahali. Lakini mwanawe alikuwa na mamlaka juu ya dunia hii. Angeweza kunena, aliweza kutoa majina, aliweza kusema, aliweza kusimamisha maumbile, aliweza kufanya lo lote alilotaka kufanya. Alikuwa na mamlaka makamilifu juu ya dunia.
Adamu alipoteza yote, lakini utukufu kwa Mungu, yote yeye aliyopoteza na kuachilia yamekombolewa na Mkombozi wetu aliye Jamaa wa Karibu, si mwingine ila Mungu Mwenyezi, ambaye alifanyika Imanueli, mmoja wetu. SASA, NI YETU.
Sisi ni wana na binti Zake watakaotawala na kuwa wafalme na makuhani pamoja Naye. Tunao uzima wa milele pamoja Naye na wale wote tuwapendao. Hakuna magonjwa tena, hakuna huzuni tena, hakuna kifo tena, yote ni milele tu pamoja.
Tunapoliwazia hilo, tunawezaje kumwacha shetani atushushe? Ni YETU, huko ndiko tunakoelekea hivi karibuni. Yeye ametupa jambo lililo kuu zaidi awezalo kutupa. Siku hizi chache za mitihani na majaribu hapa duniani zinamezwa kwa haraka na USHINDI wetu MKUU ULIO SIKU CHACHE TU ZIJAZO MBELE YETU.
IMANI yetu haijawahi kuwa kubwa jinsi hii. Furaha yetu haijawahi kuwa juu jinsi hii. Tunajua sisi ni nani na ni wapi tunakoenda. Tunajua tuko katika Mapenzi Yake makamilifu kwa kudumu na Neno Lake. Yote tunayohitaji kufanya ni kudumu na kanda na kuamini kila Neno; si kulielewa lote, BALI KUAMINI KILA NENO…nasi TUNAAMINI!
Imani huja kwa kusikia, kulisikia Neno. Neno huja kwa nabii. Mungu alilinena Hilo. Mungu alilirekodi Hilo. Mungu alilifunua Hilo. Tunalisikia Hilo. Tunaliamini Hilo.
Unaweza tu kuupata Ufunuo huu kwa kuisikia Sauti ya Mungu kwenye kanda.
“Yote yale ambayo Kristo atafanya wakati wa mwisho yatafunuliwa kwetu juma hili, katika ile Mihuri Saba, kama Mungu ataturuhusu. Unaona? Vema. Yatafunuliwa. Na kufunuliwa, wakati Mihuri hii inapovunjwa na kufunguliwa kwetu, ndipo tunaweza kuona mpango huu mkubwa wa ukombozi ulivyo, na ni lini na ni vipi utafanyika. Yote yamefichwa katika Kitabu hiki cha siri hapa. Kimetiwa muhuri, kimefungwa kwa Mihuri Saba, na kwa hiyo Mwana-Kondoo Ndiye pekee Ambaye anaweza kuivunja.
Jumapili hii saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville, (Ni Saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) sehemu ya Bibi-arusi kutoka ulimwenguni kote watakuwa wakiisikiliza Sauti ya Mungu wote kwa wakati mmoja. Tutakuwa tukiivumisha mbingu kwa maombi yetu na kumwabudu. Ninawaalika mje muungane nasi tunaposikia: Pengo Kati ya Nyakati Saba za Kanisa na ile Mihuri Saba 63-0317E.
Tafadhali msisahau kuhusu mabadiliko ya masaa huko Jeffersonville wikendi hii.
Mnamo tarehe 28, mwezi Februari, 1963, Ilinguruma. Whiu-whiiiu, Malaika Saba walikuja kutoka umilele nao wakamtokea Malaika-mjumbe wa Saba wa Mungu. Alinyakuliwa katika piramidi ya lile kundi. Kisha, wingu la kimbinguni likatokea angani juu ya Arizona. Ilikuwa ni ishara, Mungu alikuwa akimtuma malaika Wake wa saba arudi Jeffersonville ili kuifungua ile Mihuri Saba.
Tarehe 28 mwezi Februari, 2025, sayari saba zajipanga mstari angani. Bibi-arusi anajiweka mwenyewe tayari kukusanyika na kuisikia ile Mihuri Saba.
Unaalikwa, na Bwana Mwenyewe, kukusanyika pamoja na Bibi-arusi kutoka ulimwenguni kote, kuisikia Sauti ya Mungu ikifunua Ufunuo wa ile Mihuri Saba.
Ile siku ambayo manabii na wenye hekima waliitamani na kuingojea tangu mwanzo wa wakati, inatukia. Yule malaika mwenye nguvu ambaye Mungu alisema angemtuma duniani katika siku za mwisho amekuja kufungua na kuzifunua siri za Mungu zilizofichwa, ili Bwana wetu Yesu aweze kurudi kwa ajili ya Bibi-arusi Wake mwaminifu na kutupeleka kwenye Karamu yetu ya Arusi.
Wajibu wangu wa kwanza, nilipokuwa ninakuja kwenye kanisa hili jipya, niliwaunganisha katika ndoa kijana mwanamume na mwanamke wakiwa wamesimama ofisini. Na iwe ni mfano, ya kwamba nitakuwa mhudumu mwaminifu kwa Kristo, kumtayarishia Bibi-arusi kwa ajili ya sherehe ya Siku hiyo.
Leo hii, Neno hili limetimia. Mungu ananena kupitia malaika Wake, akimtayarisha Bibi-arusi Wake kwa ajili ya sherehe ya Siku hiyo. Tunafuata maagizo yake vilivyo kabisa. Bibi-arusi amejiweka mwenyewe tayari kwa KUDUMU NA SAUTI YA MUNGU ILIYO KWENYE KANDA.
Tumesikia kitu gani kwa ndoto na maono? Kile Chakula, HIKI HAPA, mahali penyewe ni hapa. Sauti ikamwambia, “Lete Chakula. Kihifadhi mle ndani. Hiyo ndiyo njia pekee ya kuwaweka hapa, ni kuwapa Chakula.”
Wengi wanaamini kwamba yeye anamaanisha tu, “dumuni tu na Neno,” na hiyo NI KWELI, anasema hivyo; lakini Bibi-arusi pia atasoma katikati ya mistari wakati Bwana-arusi anazungumza na Bibi-arusi Wake.
Hata yale maono ambayo Mungu anayaonyesha hapa mahali hapa, yanafahamika vibaya sana. Hiyo ndiyo sababu mnanisikia mimi kwenye kanda, nikisema, “Sema vile kanda zinavyosema. Sema vile maono yanavyosema.” Sasa, kama mko macho kabisa, mtaona kitu fulani. Mnaona? Natumaini si lazima nikishike mkononi mwangu na kuwaonyesheni.”
Hata maono yalieleweka vibaya, hata baada ya yeye kuwapa fasiri. Hilo ndilo yeye alilokuwa akituambia, ikiwa hutaki kupata mkanganyiko, au kuelewa vibaya, Bonyeza Play na usikie kile hasa Sauti ya Mungu inachosema.
Najua Neno lina maana zaidi ya moja, lakini hii ndiyo fasiri yangu: Ndoto na maono yote yalisema kitu kile kile; dumuni na kanda. Kama una swali, nenda kwenye kanda. Kanda hizo ni Chakula cha Mungu kilichohifadhiwa. Sema tu kile kilicho kwenye kanda; usiongeze chochote Kwake. Kanda hizo ni Bwana Asema Hivi kwa Bibi-arusi. Neno humjia nabii, peke yake. Nabii ndiye mfasiri PEKEE wa Kiungu wa Neno. Nabii alikuwa ndiye wa kumwita Bibi-arusi atoke na kumwongoza. Nitahukumiwa kwa kile kilichonenwa kwenye KANDA.
Kila kitu kinanielekeza kwenye KANDA.
Wapendwa wangu Mayungiyungi ya Kidimbwi, kwangu mimi, KUBONYEZA PLAY NDIO MUNGU KWA URAHISI KWA AJILI YA LEO HII.
Kila wiki napata changamko sana; ni kitu gani kinachoenda kufunuliwa leo wakati Bibi-arusi Wake atakapokusanyika ili kuusikia Ujumbe? Ninajua Roho Mtakatifu atakuwa akimtia mafuta kila mmoja wetu anapolifunua Neno Lake kuliko hapo awali. Ninahisi, wakati wowote tu, Yeye atakuja na kututwaa kwenda kwenye Karamu yetu ya Arusi.
Sisi ni, wana na binti za Mungu. Sisi ni, uzao uliotoka kwa Mungu. Sisi ni, urithi wa dunia. Tutatawala maumbile. Tutanena na iwe. Sisi ni Bibi-arusi!
Hebu na tujiweke wakfu upya kwa ajili ya kazi, na tujiweke wakfu kwa Kristo.”
Ndugu. Joseph Branham
Tarehe: 2 Machi, 2025
Ujumbe: Mungu Akijificha Kwa Urahisi, Halafu Akijifunua Kwa Jinsi Hiyo 63-0317M
Muda: saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville.(Ni saa 2 MBILI USIKU ya Afrika Mashariki)
Hii ndiyo, Ishara. Huu ndio, wakati wenyewe. Huu ndio, Ujumbe. Hili ndilo, Neno. Hii ndio, Sauti ya Mungu. Huyu ndiye, Mwana wa Adamu. Hii ndio, njia ya Mungu iliyoandaliwa. Huu ndio, mwisho wa wakati.
Hakuna nabii, hakuna mtume, kamwe, katika wakati wowote, aliyewahi kuishi katika wakati kama huu tunaoishi sasa. Imeandikwa mbinguni. Imeandikwa juu ya uso wa dunia. Imeandikwa katika kila gazeti. Huu ndio mwisho, ikiwa unaweza kusoma maandishi ya mkono.
Yeye aliye na sikio, na asikie yale Mungu aliyonena, na aliyorekodi, ili lisiwe neno langu, mawazo yangu, wazo langu, bali Sauti ya Mungu yenyewe ikimuelekeza Bibi-arusi Wake ni ipi njia Yake PEKEE kamilifu iliyoandaliwa kwa ajili ya siku hii.
Njoo usikilize anapotuambia na kutufunulia kwa maandiko, kwa maono, kwa fasiri ya ndoto, kudumu na Ujumbe, kudumu na kanda. Sema TU kilicho kwenye kanda.
Hakuna njia iliyo bora, wala njia iliyo ya hakika, kuliko kuisikia Sauti ya Mungu kutoka kwa Mungu Mwenyewe. Mungu alimwamuru Bibi-arusi Wake kwa kunena kupitia nabii Wake na kutuambia, BONYEZA PLAY, kwisha.
Linene Hilo, lihubiri Hilo, lishuhudie Hilo, na uuambie ulimwengu kuhusu Hilo, bali Yeye anatuambia kuna njia moja tu kamilifu iliyoandaliwa ya kumkamilisha Bibi-arusi: sikilizeni Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda. Ikiwa jambo fulani linakutatiza, cheza kanda. Ni lazima iwe ndio ya KWANZA, na Sauti iliyo muhimu zaidi ikupasayo kuisikia. Ndilo Neno Lake kamilifu aliloliweka kwenye kanda.
“Sasa linganisha hilo na zile nyingine, zile ndoto. Hili lilikuwa ono. Kile Chakula; Hiki hapa. Mahali penyewe ni hapa.
Sikiliza, kwa ndoto na maono, Chakula cha Bibi-arusi kiko wapi? Mahali penyewe ni wapi? Ujumbe wa Bibi-arusi uko kwenye kanda.
“Ninajisikia nyumbani hapa. Hapa ndipo panapofaa. Na kama ukiangalia, ndoto ile ilizungumzia jambo lile lile. Unaona, kilipo Chakula.
Ili kuhakikisha tumelipata, anatuambia kwa mara nyingine tena, kanda hizo ndicho Chakula cha Bibi-arusi.
“Wakati umekwisha.” Kama ndivyo ilivyo, hebu na tujiandae, marafiki, kumlaki Mungu wetu.
Naam, Bwana, hiyo ndiyo shauku ya mioyo yetu, ni kuwa tayari kukulaki Wewe, kuwa Bibi-arusi Wako. Tufanye nini Bwana? Njia Yako iliyoandaliwa ni ipi? Mpango Wako ni upi? Njia Yako kamilifu ni ipi? Ulitutumia nabii ambaye Ungeweza kunena kupitia yeye kutuambia sisi. Tafadhali tuelekeze.
“Kumekwisha wekwa chakula kingi sana sasa; hebu na tukitumie. Hebu na tukitumie sasa.
Mtu anawezaje kuwa kipofu? Yeye anatuambia nini cha kufanya: kuna chakula kingi sana kilichohifadhiwa kwenye kanda; kitumieni SASA. Haya ndio maagizo ya Mungu kwa Bibi-arusi Wake.
Ikiwa unadai unauamini Ujumbe huu, amini William Marrion Branham ndiye nabii-mjumbe wa Mungu aliyetumwa kumwita Bibi-arusi atoke; maisha yake yanatimiza maandiko yote yaliyonenwa kumhusu yeye; amini ndio Sauti ya Mungu ya siku hii, basi YEYE; Mungu, akinena kupitia nabii Wake, anamwambia Bibi-arusi kwa Kiingereza kilicho wazi nini cha kufanya.
Ingawa tunadhihakiwa, tunateswa, na kudharauliwa kwa sababu tu tunasikiliza kanda, tunafanya yale hasa Yeye aliyotuambia sisi tufanye. Asante Bwana kwa Ufunuo.
Ninataka kuualika ulimwengu mzima kuungana nasi Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni saa 2 MBILI USIKU ya Afrika Mashariki), wakati tunaposikia: “Hii Ndiyo Ishara ya Mwisho, Bwana?” Tutasikia kila kitu kuhusu:
Ngurumo, Mihuri Saba, Mwamba wa Piramidi, Chakula cha Kiroho, Umilele, Kundi la Malaika, Makao Makuu Yangu, Ono, Ndoto, Unabii, Siri Zilizofichwa, Andiko baada ya Andiko.
Hakuna jambo lililo kuu katika maisha haya kuliko kuisikia na kuitii Sauti ya Mungu.
Ndugu. Joseph Branham
Maandiko:
Malaki Sura ya 4 Mathayo 13:3-50 Warumi 9:33 / 11:25 / 16:25 1 Wakorintho 14:8 / Sura ya 15 Wagalatia 2:20 Waefeso 3:1-11 / 6:19/ 5:28-32 Wakolosai 4:3 1 Wathesalonike 4:14-17 1 Timotheo 3:16 Waebrania 13:8 2 Petro 2:6 Ufunuo 1:20 / 3:14 / 5:1 / 6:1 / 10:1-7 / Sura ya 17
Kuna msisimko mkubwa miongoni mwa Bibi-arusi zaidi ya hapo kabla. Tuko chini ya matarajio makubwa; mwaka wetu wa yubile unakaribia kutimia. Bibi-arusi amengoja kwa muda mrefu sana siku hii ifike. Mwisho wa kipindi cha Mataifa umefika nao mwanzo wa umilele na Bwana wetu utaanza hivi karibuni.
Tunauelewa wakati tunaoishi kwa kulisikia Neno. Muda umeisha. Wakati wa Kunyakuliwa umekaribia. Tumewasili. Roho Mtakatifu amekuja na kumfunulia Bibi-arusi Wake mambo yote makuu, ya siri, yenye kilindi.
Tuko katika hali ya kudhikika, tukimtafuta Mungu; tukijiweka tayari. Tumetupilia mbali mambo yote ya ulimwengu huu. Masumbuko ya maisha haya hayamaanishi kitu kwetu. Imani yetu imefikia viwango vikuu kuliko hapo awali. Roho Mtakatifu anampa Bibi mteule Wake Imani ya kunyakuliwa, ili aweze kuja na kumchukua.
“Haya majuma sitini na tisa yametimia kikamilifu; kule kuondoka kwa Wayahudi kulitimia kikamilifu; wakati wa kanisa ulitimia kikamilifu. Tuko katika wakati wa mwisho, wakati wa kanisa la Laodikia, mwisho wake. Wale wajumbe nyota wote wamehubiri ujumbe wao. Umetangazwa. Tuko tu karibu na ukingoni.”_
Ni wakati wa kitendawili jinsi gani tunaoishi. Ni nyakati ngumu kuliko kwani adui anamshambulia kila mmoja kuliko hapo awali. Anatutupia yote aliyo nayo. Yuko katika hali ya kudhikika, kwa maana anajua wakati wake umefika mwisho.
Lakini wakati huo huo, hatukuwahi kuwa wenye furaha maishani mwetu.
° Hatukuwahi kuwa karibu zaidi na Bwana.
° Roho Mtakatifu anajaza kila kiungo cha mwili wetu.
° Upendo wetu kwa Neno Lake haujawahi kuwa mkuu zaidi.
° Ufunuo wetu wa Neno Lake hujaza nafsi zetu.
° Tunamshinda kila adui kwa Neno.
NA, hatukuwahi kuwa na hakika ya kuwa sisi ni nani:
° ALIYECHAGULIWA TANGU ZAMANI
° MTEULE
° ALIYECHAGULIWA
° UZAO WA KIFALME
° KIPENZI,
WA MILELE, ALIYEVIKWA MAVAZI MEUPE, BI. JÉZU, MSIKILIZA KANDA, ALIYEANGAZWA, BIKIRA SAFI, ALIYEJAZWA NA ROHO, ASIYESHINDWA, MWANA MWENYE MAMLAKA, ASIYEGHOSHIWA, BIBI-ARUSI NENO BIKIRA.
Kitu gani kinachofuata? Lile Jiwe linakuja. Tunakesha, tukingoja na kuomba kila dakika ya kila siku. Hakuna kitu kingine kilicho muhimu ila sisi kujitayarisha kwa ajili ya kuja Kwake.
Sio, “Tunatumai hivyo”, TUNAJUA. Hakuna mashaka tena. Katika dakika moja, katika kufumba na kufumbua jicho itakwisha, nasi tutakuwa ng’ambo ya pili pamoja na wapendwa wetu wote na YEYE kwenye Karamu yetu ya Arusi.
NA HUO NI MWANZO TU…NA HAKUNA MWISHO!!
Njoo ujitayarishe kwa ajili ya Karamu hiyo ya Arusi pamoja nasi Jumapili hii saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni saa 2 MBILI USIKU ya Afrika Mashariki) wakati Mungu anaponena kupitia malaika Wake mwenye nguvu, yule aliyemtuma kumwongoza Bibi-arusi Wake, wakati aelezapo, na kufunua, siri zote za Mungu.
Tumeelekeza nyuso zetu Mbinguni katika maombi na kusihi ili kupata siku na saa hasa tunayoishi.
Zaidi ya hapo awali, tumeketi pamoja katika ulimwengu wa roho, kutoka ulimwenguni kote, tukimsikiliza Mungu akinena na kulifunua Neno Lake kwetu kupitia malaika-mjumbe Wake mwenye nguvu. Malaika-mjumbe wa duniani ambaye Baba alimtuma kwa Bibi-arusi Wake katika siku hii ya mwisho kulifunua Neno Lake.
Gabrieli ndiye malaika kwa watu waliochaguliwa na Mungu, Wayahudi. Lakini kwa Bibi-arusi Wake Mmataifa, Melkizedeki Mwenyewe alikuja na kunena kupitia mwili wa mwanadamu katika malaika wa duniani aitwaye William Marrion Branham, ili apate kunena na kulifunua Neno Lake LOTE kwa Bibi-arusi Wake kipenzi wa moyoni.
Alilifanya lirekodiwe, lihifadhiwe, na litunzwe, ili Bibi-arusi apate Chakula Chake cha kiroho, Mana iliyofichwa, kwenye ncha ya vidole vyao kila dakika ya kila siku mpaka mwisho wa wakati.
Utu wetu wa ndani umejawa na upako kama nini wakati tunaiposikia Sauti ya Mungu ikilifunua Neno Lake kwetu. Jinsi gani Yeye anavyolifunua Neno Lake ili tuweze kuona waziwazi na kuelewa maana Yake. Linafunua saa yenyewe hasa tunayoishi, linatuambia sisi ni nani na ni nini kinachoenda kutukia hivi karibuni; Unyakuo wetu unaokuja hivi karibuni.
Yeye hata anamfunulia Bibi-arusi Wake kile kitakachokuwa kikitendeka hapa duniani wakati tuwapo pamoja Naye kwenye Karamu ya Arusi. Jinsi ambavyo Yeye atakavyoyafungua macho yaliyopofushwa ya wateule Wake; wale aliowapofusha kwa ajili ya Bibi-arusi Wake Mmataifa.
Enyi marafiki, najua jinsi tulivyochoshwa na ulimwengu huu na tukitamani kuja kwake kutuchukua, lakini pia hebu na tufurahi na kushukuru kwa yale yanayotukia hivi sasa mbele ya yaya haya macho yetu.
Hebu na tuinue mikono yetu, mioyo yetu, sauti zetu, na kufurahi. Sio tu kwamba tunatazamia yale ambayo anayoenda kututendea hivi karibuni, lakini hebu na tufurahi juu ya yale anayotufunulia na kututendea hivi SASA.
Yeye anatuambia sisi ni Bibi-arusi Wake aliyechaguliwa tangu asili tukiungana pamoja Naye na Neno Lake. Anatuhakikishia tena na tena, tuko katika Mapenzi Yake makamilifu kwa sisi kukaa na Sauti Yake, Neno Lake, malaika Wake. Ametupa IMANI ya kujua na kujitambua sisi ni nani: NENO LAKE LIISHILO KATIKA MWILI.
Hatuna cha kuogopa; Hakuna cha kuhofia, hakuna cha kujihuzunisha nacho; Ninalijuaje hilo? MUNGU ALISEMA HIVYO! KWA HIYO HEBU NA TUSHANGILIE, TUFURAHI, TUWE NA SHUKRANI; NENO LILILO HAI LINAISHI NA KUKAA NDANI YETU. SISI NDIO UZAO WAKE MKUU WA KIFALME.
Ninaamini kweli Bwana lazima atakuwa pia amechangamshwa sana kujua kwamba wakati umefika nasi tumejiweka wenyewe tayari kwa kudumu wa kweli na waaminifu kwa Neno Lake.
Kama yule mvulana mdogo aliyejitazama kwenye kioo kwa mara yake ya kwanza, tunatazama katika Neno Lake, tukiona sisi NI NANI. Bwana…NI MIMI. Mimi ndiye Bibi-arusi Neno lililo hai Wako. Mimi ndiye uliyemchagua WEWE. Mimi niko ndani Yako, Wewe U ndani yangu, sisi ni Mmoja.
Tunawezaje kutosherehekea na kuwa watu wenye furaha kuliko wote waliowahi kuishi kwenye uso wa dunia? Watakatifu na manabii wote waliotutangulia walitaka kuishi katika siku hii na kuziona ahadi hizi zikishika kasi. Lakini kwa NEEMA ya Mungu,Yeye alituweka SISI hapa.
Tunasubiri kwa hamu:
Brrrr! Loo, jamani! Whiu! Kwa maneno mengine, wakati adui atakapokuwa ameondolewa, mwisho wa dhambi umekuja, kuletwa kwa haki ya milele kumekuja, Shetani amefungiwa kuzimuni, na maarifa ya Bwana yataijaza dunia kama maji yaifunikavyo bahari. Amina! Mungu atukuzwe! Linakuja, ndugu, linakuja!
Ni upako wa namna gani utakaotendeka Jumapili saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni saa 2 MBILI USIKU ya Afrika Mashariki) tunapokusanyika pamoja kutoka ulimwenguni kote kumsikia malaika wa Mungu, Sauti ya Mungu kwa Bibi-arusi, akituletea Ujumbe: Sababu Sita Za Kusudi La Gabrieli Kumzuru Danieli 61-0730E.
Ni Majira ya baridi ya ajabu vipi tumekuwa nayo tulipojifunza Nyakati Saba za Kanisa, na kisha Mungu akitufunulia hata na zaidi katika Kitabu cha Ufunuo wa Yesu Kristo. Jinsi zile sura tatu za kwanza za Ufunuo zilivyokuwa Nyakati za Kanisa, halafu jinsi ambavyo Yohana alivyotwaliwa juu katika mlango wa 4 na wa 5 kutuonyesha mambo ambayo yangekuja.
Katika sura ya 6, Yeye alifunua jinsi Yohana alivyoshushwa duniani tena ili kuyaona mambo yakitukia ambayo yatakayoanzia sura ya 6 hadi sura ya 19 ya Ufunuo.
Jinsi gani Bibi-arusi atakavyobarikiwa Jumapili tunapoisikia Sauti ya Mungu ikinena kupitia malaika Wake wa saba mwenye nguvu na kutuambia kile kinachoenda kufunuliwa.
Ninayo furaha sana kutangaza kwamba sasa tutaanza lile somo kuu la Yale Majuma Sabini Ya Danieli. Nabii alisema ya kwamba itaunganisha ile sehemu nyingine ya Ujumbe kabla hatujaingia kwenye ile Mihuri Saba; Baragumu Saba; Ole Tatu; yule mwanamke katika jua; kutupwa nje kwa yule pepo mwekundu; wale mia na arobaini na nne elfu waliotiwa muhuri; yote yanatukia katikati ya wakati huu.
Kitabu cha Danieli ndicho kalenda halisi kwa ajili ya kizazi na wakati tunaoishi, na haijalishi linaweza kuonekana gumu kiasi gani, Mungu atalivunja-vunja na kulifanya rahisi kwa ajili yetu.
Na Mungu anajua hayo ndiyo ninayotafuta sasa, nipate kuwafariji watu Wake na kuwaambia mambo yaliyo karibu kutimia, hapa asubuhi ya leo, na pia huko nje katika nchi ambako kanda hizi zitakwenda, kila mahali ulimwenguni, ya kwamba tuko katika wakati wa mwisho.
Sisi ndio wateule wa Mungu ambao tunaotamani na kuomba kwa ajili ya siku hiyo na saa hiyo. Na macho yetu yameelekezwa Mbinguni, nasi tunakutazamia Kuja Kwake.
Hebu sote tuwe kama Danieli na tuzielekeze nyuso zetu Mbinguni, katika maombi na kusihi, kama tujuavyo kwa kusoma Neno na kuisikia Sauti Yake, kuja kwa Bwana kunakaribia upesi; tuko mwisho.
Tusaidie Baba kuweka kando kila mzigo, kila dhambi, kila kutokuamini kudogo ambako kungetuzinga kwa upesi. Hebu sasa na tukaze mwendo kuelekea mede ya wito mkuu, tukijua ya kwamba wakati wetu ni mdogo.
Ujumbe umetoka. Kila kitu kiko tayari sasa; tunangojea na kupumzika. Kanisa limetiwa muhuri. Walio waovu wanazidi kutenda maovu. Makanisa yanazidi kuwa baridi, lakini watakatifu Wako wanakukaribia Wewe zaidi.
Tunayo Sauti inayolia kutoka nyikani, ikiwaita watu waurudie Ujumbe wa asili; wayarudie mambo ya Mungu. Tunafahamu kwa Ufunuo mambo haya yanatukia.
Njoo uungane nasi Jumapili hii saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni saa 2 MBILI USIKU ya Afrika Mashariki) Wakati Mungu anapotufunulia Neno Lake, tunapolianza somo letu kuu la Kitabu cha Danieli.
Hakika haya ni Majira ya baridi yaliyo bora maishani mwetu. Kuja kwa Bwana kumekaribia. Tumetiwa muhuri na Roho Mtakatifu; Muhuri wa kibali cha Mungu kwamba kila kitu alichokifia Kristo ni mali yetu.
Sasa tunayo arabuni ya urithi wetu, Roho Mtakatifu. Ni hakikisho, yale malipo ya kwanza, ya kwamba tumepokelewa katika Kristo. Tunapumzika katika ahadi za Mungu, tukilala katika joto la Mwangaza Wake wa Jua; Neno Lake lililothibitishwa, tukiisikiliza Sauti Yake.
Ni arabuni ya wokovu wetu. Hatuna wasiwasi kama tunaenda kule ama hatuendi, TUNAENDA! Tunalijuaje hilo? Mungu alisema hivyo! Mungu aliliahidi nasi tunayo arabuni. Tayari tumeipokea na Kristo ametukubali.
Hakuna njia ya kuliondokea…kwa kweli, tupo hapo! Yote itupasayo kufanya ni kungojea tu; Yeye anafanya kazi ya Mkombozi wa Jamaa wa Karibu sasa hivi. Tunayo Arabuni yake sasa hivi. Tunangojea tu wakati ambapo Yeye atakaporudi kutuchukua. Kisha, katika dakika moja, katika kufumba na kufumbua jicho, sote tutakuwa tumekwenda kwenye Karamu ya Arusi.
Kuwazia tu yale yote yaliyo mbele yetu. Akili zetu haziwezi kuyaingiza yote ndani. Siku baada ya siku Yeye analifunua zaidi Neno Lake, akihakikisha kwamba ahadi hizi kuu ni zetu.
Ulimwengu Unaporomoka; mioto, matetemeko ya ardhi, na machafuko kila mahali, lakini wao wanaamini kuwa wanaye mwokozi mpya ambaye atauokoa ulimwengu, na kuwaletea wakati wao wa heri na furaha kuu. Tayari sisi tumekwishampokea Mwokozi wetu nasi tumekuwa tukiishi katika Wakati wetu wa Heri na Furaha Kuu.
Sasa Yeye anatutayarisha kwa Ufunuo hata na zaidi wakati tunapoingia katika mlango wa 5 wa Ufunuo. Anaandaa tukio hapa kwa ajili ya kufunguliwa kwa ile Mihuri Saba. Kama tu vile alivyofanya katika mlango wa 1 wa Ufunuo, akiifungua njia kwa ajili ya Nyakati Saba za Kanisa.
Je! Majira mengine yaliyosalia ya baridi yatakuwaje kwa Bibi-arusi? Hebu tuangalie muhtasari mdogo:
Sasa, sina wakati. Nimeiandika, muktadha fulani juu yake hapa, bali mkutano wetu ujao kabla hatujaliingilia hili…Labda nitakapotoka kwenye likizo yangu ama wakati mwingine, ninataka kuyachukua haya majuma sabini ya Danieli na kuyafunganisha mumu humu, na kuonyesha mahali yanapolipeleka kwenye Yubile ya Pentekoste, na kuyarejesha moja kwa moja pamoja na vile ninii saba…hiyo mihuri saba itakayofunguliwa hapa kabla tu hatujaenda, na kuonyesha kwamba ni wakati wa mwisho, hii…
Ni wakati wa ajabu jinsi gani Bwana aliomwekea Bibi-arusi Wake. Akijifunua Mwenyewe katika Neno Lake kwetu zaidi ya hapo awali. Akitutia moyo kwamba sisi ndio wateule Wake anaowajia Yeye. Akituambia tuko katika mapenzi Yake Makamilifu kwa kukaa na Sauti Yake, na Neno Lake.
Tunafanya nini? Si hata jambo moja, tunapumzika tu! Tunangojea! Hakuna kutenda kazi tena, hakuna masumbuko tena, TUNAPUMZIKA KWENYE HILO!
Njoo upumzike pamoja nasi Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville, (Ni saa 2:00 MBILI USIKU ya Afrika Mashariki) tunapoisikia Sauti ya Mungu ILIYOTHIBITISHWA ikituletea Ujumbe:
Ni wakati wa sisi kuvua kofia yetu ya vita na mvae mawazo yenu ya kiroho, maana Mungu anajitayarisha kumpa Bibi-arusi Wake Ufunuo zaidi wa Neno Lake.
Yeye atakuwa akitufunulia siri zote za wakati uliopita. Atatuambia yale yatakayotukia wakati ujao. Yale ambayo wengine wote katika Biblia waliyoyaona au kusikia, Yeye atafunua kila jambo dogo la Neno Lake na maana Yake kwetu.
Tutasikia na kuelewa maana ya alama za Biblia: Viumbe Hai, Bahari ya Kioo, Simba, Ndama, Mwanadamu, Tai, Kiti cha Rehema, Walinzi, Wazee, Sauti, Therion, Zoon.
Tutasikia na kuelewa yote kuhusu walinzi wa Agano la Kale. Yuda: Mlinzi wa Mashariki; Efraimu: Mlinzi wa Magharibi; Rubeni: Mlinzi wa Kusini; na Dani: Mlinzi wa Kaskazini.
Hakuna kitu kingaliweza kuja popote karibu na hicho kiti cha rehema pasipo kuyapitia makabila hayo. Simba, akili ya mwanadamu; Maksai: farasi mtenda-kazi; Tai: Wepesi wake.
Jinsi Mbingu, nchi, katikati, na kote kote huku, walikuwa ni walinzi. Na juu yake ilikuwa ile Nguzo ya Moto. Hakuna kitu kilichogusa kiti hicho cha rehema pasipo kuyapitia makabila hayo.
Sasa kuna walinzi wa Agano Jipya: Mathayo, Marko, Luka na Yohana, wakienda mbele moja kwa moja. Lango la mashariki limelindwa na simba, lango la kaskazini limelindwa na tai arukaye, Yohana, yule mwinjilisti. Halafu tabibu upande huu, Luka, mwanadamu.
Zile Injili nne zinalinda Baraka za Kipentekoste pamoja na kila Andiko kuunga mkono yale hasa waliyosema. Na sasa Matendo ya mitume yanathibitisha leo hii pamoja na zile Injili nne ya kwamba Yesu Kristo ni yeye yule jana, leo, na hata milele.
Wakati mpakwa mafuta wa kweli wa Mungu anaponena, ni Sauti ya Mungu! Tunataka tu kupaza sauti, “Mtakatifu, mtakatifu, mtakatifu kwa Bwana!”
Hakuna njia ya kumwacha Huyo. Kwa kweli, Hatuwezi kumwacha, kwa kuwa Yeye hatatuacha. Tumetiwa muhuri hata Siku ya ukombozi wetu. Hakuna cha usoni, hakuna cha wakati uliopo, hatari, njaa, kiu, mauti, wala CHOCHOTE KILE, kinachoweza kututenganisha na upendo wa Mungu ulio ndani ya Kristo.
Kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu majina yetu yaliwekwa kwenye Kitabu cha Uzima cha Mwana-Kondoo ili kuiona Nuru HII, kuipokea Sauti Hii, kuuamini Ujumbe Huu, kumpokea Roho Mtakatifu wa wakati wetu na kutembea ndani Yake. Wakati Mwana-Kondoo alipochinjwa, MAJINA YETU yaliwekwa kwenye Kitabu wakati ule ule Jina la Mwana-Kondoo lilipowekwa mle. UTUKUFU!!
Hivyo, hakuna kinachoweza kututenganisha na Ujumbe huu. Hakuna kinachoweza kututenganisha na Sauti hiyo. Hakuna kinachoweza kuuondoa Ufunuo wa Neno Hili kutoka kwetu. Ni wetu. Mungu alituita na akatuchagua na kutuchagua tangu awali. Kila kitu ni chetu, ni yetu.
Kuna njia moja tu ya kuyapata haya yote. Ni lazima uoshwe kwa maji ya Neno. Huna budi kulisikia Neno kabla hujaingia Mle. Na kuna njia moja tu unayoweza kumkaribia Mungu, hiyo ni kwa Imani. Na Imani huja kwa kusikia, kusikia Neno la Mungu, ambalo linaakisiwa kutoka Patakatifu pa Patakatifu ndani ya mjumbe wa wakati.
Kwa hiyo, hapa, malaika wa wakati wa kanisa anaakisi kuingia kwenye maji hayo kwamba Jamaa huyu ni nani hapa, akiakisi rehema Zake, Maneno Yake, hukumu Yake, Jina Lake. Yote yanaakisiwa humu ndani ambako unatenganishwa kwa kuliamini. Unalipata?
Usiache kuzisikiliza kanda, wewe dumu nalo tu. Lichunguze kwa Neno na uone kama ni kweli. Ni Njia iliyoandaliwa na Mungu kwa ajili ya siku hii.
Njoo uungane nasi Majira haya ya baridi wakati tunapoungana pamoja kutoka kote ulimwenguni na kuisikia Sauti ya Mungu ikilifunua Neno Lake kwa Bibi-arusi Wake kuliko hapo awali. Hakuna upako mkuu kuliko kubonyeza play na kusikiliza Sauti Yake.
Kutoka katika kilindi cha moyo wangu, Naweza kusema: Nina furaha sana naweza kusema Mimi ni Mmoja Wao pamoja na kila mmoja wenu.
Ndugu. Joseph Branham
Ujumbe: 61-0108 – “Ufunuo, Mlango Wa Nne Sehemu ya III”
Muda: saa 6:00 SITA MCHANA Saa za Jeffersonville ( ni Saa 2:00 MBILI USIKU ya Afrika Mashariki )