Ningependa tuwe na Ibada nyingine ya Ushirika na Kutawadhana Miguu Jumapili hii, tarehe 29 Septemba, Bwana akipenda. Kama tulivyofanya wakati uliyopita, ningewahimiza muanze saa 11:00 KUMI NA MOJA JIONI. kwa masaa ya nchi zenu. Ingawa Ndugu Branham alisema mitume wao walifanya Ushirika kila wakati walipokutana pamoja, Yeye alipendelea kuufanya wakati wa jioni, naye akautaja kama Meza ya Bwana.
Ujumbe na ibada ya Ushirika itakuwa kwenye Redio ya Sauti, na pia kutakuwa na anuani ya faili la kupakuliwa kwa wale ambao hawawezi kuipata Redio ya Sauti Jumapili asubuhi.
Kwa waamini wa eneo la Jeffersonville, tutakuwa na divai ya Ushirika tena itakayopatikana kwa ajili ya kuja kuchukua. Tangazo litatoka hivi karibuni kueleza mahali, siku na saa.
Hakika niko chini ya matarajio kwa sisi kushika agizo hili la thamani ambalo Bwana alilotuachia. Ni fursa ilioje kwetu sisi kuandaa nyumba zetu na kuifungua mioyo yetu kwa ajili ya Mfalme wa Wafalme aingie na kula pamoja nasi Mezani Pake.
Sisi ndio sifa halisi ya Baba yetu wa Mbinguni; kwa maana tulikuwa ndani yake hapo mwanzo. Hatukumbuki hilo sasa, lakini tulikuwa pamoja Naye, na Yeye alitujua. Alitupenda sana hata akatufanya kuwa mwili, ili aweze kuwasiliana nasi, kuzungumza nasi, kutupenda, hata kutushika mikono.
Lakini Shetani alikuja na kupotosha Neno la asili la Mungu, Ufalme Wake, na mpango Wake kwa ajili yetu. Aliwapotosha wanaume na wanawake na kufanikiwa katika kupotosha na kuuteka ulimwengu huu tunaoishi. Ameufanya ulimwengu kuwa ufalme wake, bustani yake ya Edeni.
Ni saa danganyifu na yenye hila iliyowahi kuwako. Ibilisi ameweka kila mtego wa ujunja awezao; maana yeye ni mdanganyifu mkuu. Mkristo hana budi kuwa mwangalifu zaidi leo kuliko alivyowahi kuwa katika wakati wowote.
Lakini wakati huohuo, ndio wakati uliyo mzuri zaidi ya nyakati zote, kwa sababu tunaelekea kwenye ule Utawala wa Miaka Elfu mkuu. Bustani yetu ya Edeni inakuja hivi karibuni, ambamo tutakuwa na upendo mkamilifu na ufahamu mkamilifu wa upendo wa Mungu. Tutakuwa hai na salama pamoja Naye katika Edeni yetu Milele yote.
Yesu alituambia katika Mathayo 24 tunapaswa kuwa waangalifu jinsi gani katika siku hii. Alituonya kwamba ingekuwa ni siku ya udanganyifu sana iliyowahi kuwepo, “inafanana sana hata ingewadanganya wale Walioteuliwa na Mungu kama yamkini”; kwa kuwa ujanja wa Ibilisi utawafanya watu waamini ya kwamba wao ni Wakristo, wakati wao sio.
Lakini wakati huu pia ungemtoa Bibi-arusi Neno safi wake ambaye hangedanganyika na asingeweza kudanganywa; kwa maana wangedumu na Neno Lake la asili.
Kama Yoshua na Kalebu, Nchi yetu ya ahadi imeanza kuonekana kama vile yao ilivyoanza kuonekana. Nabii wetu alisema Yoshua maana yake ni, “Yehova-Mwokozi”. Alimwakilisha kiongozi wa wakati wa mwisho ambaye atakuja kwa kanisa, kama vile Paulo alivyokuja kama kiongozi wa kwanza.
Kalebu aliwakilisha wale waliomtii Yoshua. Kama vile wana wa Israeli, Mungu alikuwa amewaanzisha kama bikira kwa Neno Lake; bali wao walitaka kitu tofauti. Nabii wetu alisema, “vivyo hivyo na kanisa hili la siku za mwisho nalo.” Kwa hiyo, Mungu hakuwaacha Waisraeli waingie katika nchi ya ahadi mpaka wakati Wake Mwenyewe uliokusudiwa ulipowadia.
Watu walimsonga Yoshua, kiongozi wao waliyepewa na Mungu, na kusema, “Hiyo nchi ni yetu, hebu na twende tukaitwae. Yoshua, umeshindwa, lazima umepoteza agizo lako. Huna ile nguvu uliyokuwa nayo. Ulikuwa ukisikia kutoka kwa Mungu na kujua mapenzi ya Mungu, na kutenda kwa haraka. Una kasoro fulani wewe.”
Yoshua alikuwa nabii aliyetumwa na Mungu, naye alijua ahadi za Mungu. Nabii wetu alituambia:
“Mungu aliuweka uongozi mzima katika mikono ya Yoshua kwa sababu alikuwa amedumu na Neno. Mungu aliweza kumwamini Yoshua lakini si hao wengine. Kwa hiyo itajirudia katika siku hizi za mwisho. Shida ile ile, usumbufu ule ule.”
Kama vile Mungu alivyofanya na Yoshua, Yeye aliuweka UONGOZI MZIMA mikononi mwa malaika-nabii Wake, William Marrion Branham; kwa maana alijua angeweza kumwamini yeye, lakini si hao wengine. Ilibidi kuwe na Sauti Moja, Kiongozi Mmoja, Neno Moja la mwisho, wakati huo, na SASA HVI.
Ninapenda jinsi nabii alivyotuambia kutakuwa na maelfu mara maelfu ambao watakaozisikia kanda. Alisema kuwa hizo kanda NI HUDUMA. Kutakuwa na baadhi yetu tutakaoingia kwa siri Majumbani na makanisani tukiwa na kanda (huduma yake) ili kuupata Uzao wa Mungu uliochaguliwa tangu awali.
Tuliporudi na kusema, Bwana, tumetii maagizo yako, nako kulikuwa na watu tuliowapata tulipozicheza kanda walioamini. Sasa tumehubiri jambo hilo, kote ulimwenguni, Je, utatimiza hilo?
Yeye atasema: “Hilo ndilo Mimi nililowatuma kufanya.”
Mungu atalitimiza hilo. Nyumba yako kamwe haitaporomoka. Wakati Mungu atakapotoa ishara ya kukiangamiza kitu hicho chote, familia yako yote, mali zako zote, zitakuwa salama nyumbani mwako. Unaweza kusimama humo. Haikulazimu kuchungulia dirishani, wewe Bonyeza Play tu huku vita vikiendelea.
Maneno yako yalionekana, nami nikayala; na maneno yako yalikuwa ni furaha kwangu, na shangwe ya moyo wangu; maana nimeitwa kwa jina lako, Ee Bwana, Mungu wa majeshi.
Ninakualika uje uungane nasi wakati tunapokula huduma kuu ya Mungu, hai, ya wakati wa mwisho, Jumapili hii saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni saa 1:00 Jioni ya Afrika mashariki) tunaposikia yote yanayohusu: Edeni ya Shetani 65-0829.
Hebu tuishi mpaka kuja Kwake Bwana kama ikiwezekana. Hebu na tutende kila kitu kilicho katika uwezo wetu kwa upendo, na uelewano—kuelewa kwamba Mungu anauchunguza ulimwengu, siku hii ya leo, kutafuta kila kondoo aliyepotea. Hebu tuzungumze nao kwa maombi ya upendo yaliyokolea chumvi na Neno la Mungu, ili tuweze kumpata huyo wa mwisho kusudi tupate kwenda nyumbani, na tutoke katika Edeni hii ya kale ya Shetani hapa, Bwana.
Roho wa Mungu aliye hai, tupulizie. Hebu tuchukue Chujio lako nasi tuishi chini ya Hilo, Bwana. Tupulizie hewa safi ya Roho Mtakatifu ndani ya mapafu yetu na ndani ya nafsi zetu kila siku. Tunaweza tu kuishi kwa Neno Lako; kila Neno litokalo katika kinywa Chako kwa ajili ya wakati huu tunaoishi.
Sisi tumeonja mambo Yako ya Mbinguni nasi tuna Neno Lako mioyoni mwetu. Tumeliona Neno Lako likidhihirishwa mbele yetu, na nafsi yetu yote imesitiriwa ndani Yake. Ulimwengu huu, na mambo yote ya Ulimwengu yamekufa kwetu.
Sisi ni chembechembe iliyo hai, mbegu Neno ambayo iliyokuwa ndani Yako tangu mwanzo Tukisimama hapa tukiivuta ile mbegu yako ya Uzima. Mbegu yako imo mioyoni mwetu kwa kujua kwako tangu awali. Ulituchagua tangu awali tusivute kupitia chochote kile, ila Neno Lako, Sauti Yako, kwenye kanda.
Ule wakati wa jicho umefika; hakuna kilichosalia ila Kuja Kwako kumjia Bibi-arusi Wako. Chujio letu ni Neno Lako, Malaki 4, Bwana Asema Hivi.
Hebu tulipande Neno Lako mioyoni mwetu, na tuazimie ya kwamba hatutageuka mkono wa kulia ama wa kushoto, bali tuishi tukiwa waaminifu Kwake siku zote za maisha yetu. Baba, tutumie juu yetu Roho Mtakatifu wa Uzima, na alihuishe Neno Lako kwetu, ili tupate kukudhihirisha Wewe.
Shauku ya mioyo yetu ni kuwa wana na binti wa kweli Kwako. Tumeketi katika uwepo wa Sauti Yako, tukiivishwa, tukijifanya wenyewe tayari kwa ajili ya Karamu yetu ya Harusi pamoja nawe hivi karibuni.
Mataifa yanavunjika. Ulimwengu unavurugika. Matetemeko ya ardhi yanaitikisa California kama vile Wewe ulivyotuambia ingefanya. Tunajua hivi karibuni Kipande kinene cha maili elfu moja na mia tano, upana wa maili mia tatu ama mia nne kitazama, labda maili arobaini ndani ya ule ufa kule. Mawimbi yataruka mpaka mkoa wa Kentucky, Na wakati kitakapozama, kitaitikisa dunia sana mpaka kila kitu juu yake kitaanguka chini.
Onyo lako la mwisho linaendelea. Ulimwengu uko katika machafuko kamili, lakini wakati wote Bibi-arusi Wako anapumzika ndani Yako na Neno Lako, ameketi pamoja katika ulimwengu wa roho unapozungumza nasi, na kutufariji njiani.
Jinsi gani tunavyoshukuru, Baba, kwamba tunaweza kwa urahisi “Kubonyeza Play” na kuisikia Sauti Yako ikizungumza nasi, kututia moyo na kutuambia:
Msiogope, enyi kundi dogo. Yote niliyo Mimi, ninyi ni warithi wake. Nguvu Zangu zote ni zenu. Uwezo Wangu ni wenu ninaposimama katikati yenu. Sikuja kuleta hofu na kushindwa, bali upendo na ujasiri na uwezo. Nimepewa mamlaka yote nanyi mnaweza kuitumia. Ninyi neneni Neno Nami nitalitimiza. Hilo ni agano Langu wala haliwezi kushindwa kamwe.”
Ee Baba, hatuna cha kuogopa. Unatupa upendo wako, ujasiri na uwezo wako. Neno Lako liko ndani yetu kulitumia tunapolihitaji. Tunalinena, na Wewe Utalitimiza. Ni agano Lako, nalo haliwezi KUSHINDWA KAMWE.
Maneno yapatikayo na mauti hayawezi kueleza jinsi gani tunavyojisikia, Baba, lakini tunajua Wewe unaona ndani ya mioyo na roho zetu; kwa maana sisi ni sehemu Yako.
Jinsi gani tunavyoshukuru kwamba Umeiandaa njia kwa ulimwengu kuisikia Sauti Yako katika wakati huu wa mwisho. Kila wiki, Wewe unaualika ulimwengu mzima uje kuungana kumsikia malaika-mjumbe wako wakati Wewe unapotulisha Chakula cha Kondoo ambacho kimehifadhiwa ili kutudumisha hadi Utakaporudi kutuchukua.
Tunakupenda Baba.
Ndugu. Joseph Branham
Ujumbe: 65-0822E Chujio La Mtu Mwenye Busara
Muda: Saa 06:00 SITA MCHANA, Saa za Jeffersonville(Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika mashariki)
Jinsi gani macho yetu yalivyobarikiwa; maana yanaona. Jinsi gani masikio yetu yalivyobarikiwa; maana yanasikia. Manabii na watu wenye haki walitamani kuona na kusikia yale tuliyoyaona na kuyasikia, lakini hawakuyaona. Sisi vyote viwili TUMEONA NA KUISIKIA SAUTI YA MUNGU.
Mungu Mwenyewe alichagua kuiandika Biblia Yake kupitia manabii Wake. Mungu Mwenyewe pia alichagua kufunua siri Zake zote katika wakati huu wa mwisho kwa Bibi-arusi Wake kupitia nabii Wake. Ni sifa Zake, Neno Lake lililodhihirishwa, likifanya jambo hilo lote kuwa sehemu Yake.
Pindi wakati wetu ulipowadia, Yeye alimwasilisha nabii Wake akawasili wakati uo huo. Alimvuvia na kunena kupitia yeye. Ilikuwa ndiyo njia Yake iliyokusudiwa tangu zamani na iliyoandaliwa ya kufanya jambo hilo. Kama vile Biblia, Ni Neno la Mungu, na si neno la mwanadamu.
Ni lazima tuwe na Yakini, mkataa; Neno la mwisho. Baadhi ya watu husema Biblia ndio Yakini yao, si yale yanayosemwa kwenye kanda; kana kwamba zinasema kitu tofauti. Ni ajabu sana jinsi Mungu ameuficha Ufunuo wa kweli wa Neno Lake kwa wengi sana, lakini ameufunua na kuuweka wazi sana kwa Bibi-arusi Wake. Wengine hawawezi kujizuia, wamepofushwa na hawana Ufunuo kamili wa Neno la Mungu lililofunuliwa.
Mungu alisema katika Neno Lake (Biblia) kupitia nabii Wake na kutuambia, “Mungu, ambaye alisema zamani na baba zetu katika manabii kwa sehemu nyingi na kwa njia nyingi”. Hivyo, manabii wa Mungu waliiandika Biblia. Haikuwa wao, bali Mungu akinena kupitia wao.
Alisema katika siku yetu Yeye angemtuma Roho wake wa kweli ili atuongoze katika kweli zote. Yeye hatanena kwa shauri lake mwenyewe; lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atatuonyesha.
Ujumbe uliyo kwenye kanda ndio kweli za Mungu zilizofunuliwa. Haihitaji fasiri yoyote. Ni Mungu akilifasiri Neno Lake Mwenyewe wakati anapolinena kwenye kanda.
Hakuna mwendeleo katika yale watu wengine wanachozungumza, Ila tu kile Mungu anenacho. Kile kinachosemwa kwenye kanda ndio Sauti pekee ambayo HAITABADILIKA KAMWE. Watu hubadilika, mawazo hubadilika, fasiri hubadilika; Neno la Mungu halibadiliki kamwe. Ndio Yakini ya Bibi-arusi.
Nabii anatupa mfano wa rifarii kuwa ndio yakini katika mchezo wa mpira. Neno lake ndilo la mwisho. Huwezi kulihoji. Kile anachosema, ndivyo hivyo, Mwisho wa maneno. Sasa rifarii ana kitabu cha sheria ambacho lazima akipitie. Kinamwambia mahali yalipo maeneo ya mpira kawaida au goli, ni wakati gani salama kwako na wakati gani uko nje; sheria ni zipi kwa mchezo wa mpira.
Anasoma na kukisoma kitabu hicho ili anaponena, na kufanya uamuzi wake, hiyo ndiyo sheria, hilo ndilo neno la mwisho. Hamna budi kudumu na kile anachosema, hakuna swali, hakuna mabishano, chochote anachosema, hivyo ndivyo kinavyopaswa kuwa nacho hakiwezi kubadilishwa. Utukufu.
Ndugu Branham hakusema hupaswi kuhubiri, au kufundisha; kinyume chake, yeye alisema muhubiri, na kuwasikiliza wachungaji wenu, lakini Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda haina budi kuwa Yakini yenu.
Kunapaswa kuwe na nguzo ya kushikilia; kwa maneno mengine, mkataa. Kila mtu hana budi kuwa na mkataa huo. Ni neno la mwisho. Mungu ametoa mahali pamoja tu pa kulipata hilo, Sauti ya Mungu kwenye kanda. Ndio fasiri ya kiungu ya Neno la Mungu. NDILO NENO LA MWISHO, ILE AMINA, ILE BWANA ASEMA HIVI.
Yesu Mwenyewe alisema tunawaita “miungu,” walionena Neno Lake; nao walikuwa miungu. Alisema wakati manabii walipotiwa mafuta na Roho wa Mungu, walilileta Neno la Mungu sawasawa. Ilikuwa ni Neno la Mungu likinena kupitia kwao.
Hiyo ndiyo sababu nabii wetu alikuwa jasiri sana. Aliongozwa na Roho Mtakatifu kunena Neno la Mungu lisilokosea. Mungu alikuwa amemchagua kwa ajili ya wakati wetu. Akauchagua Ujumbe ambao angeunena, hata tabia ya nabii wetu na kile kingetukia katika wakati wetu.
Maneno aliyonena, vile alivyotenda, imewapofusha wengine, lakini imeyafungua macho yetu. Yeye hata alimvalisha kwa namna ya mavazi aliyovaa; tabia yake, shauku yake, kila kitu jinsi tu ilivyompasa kuwa, alichaguliwa tu kikamilifu kwa ajili yetu sisi, Bibi-arusi wa Mungu.
Ndiyo maana, wakati TUNAPOKUSANYIKA PAMOJA, Ni Sauti ndio tunayotaka kuiweka KUWA YA KWANZA kuisikia. Tunaamini kwamba tunalisikia Neno Safi lililonenwa kutoka kwa mjumbe mteule na aliyechaguliwa wa Mungu.
Tunajua wengine hawawezi kuliona au kulielewa hilo, lakini yeye alisema alikuwa akilizungumzia kusanyiko lake peke yake. Yeye hakuwajibika na wale ambao Mungu aliowapa wengine kuwachunga; yeye aliwajibika tu na aina ya Chakula anachotulisha sisi.
Ndiyo maana tunasema sisi ni Maskani ya Branham, kwa sababu yeye alisema Ujumbe ulikuwa kwa ajili ya watu wake tu katika Maskani, lile kundi dogo lililotaka kuzipata na kuzisikiliza kanda. Alikuwa anawazungumzia wale Mungu aliyompa kuwaongoza.
Yeye alisema, “kama watu wanataka kutengeneza chakula cha kisasa na kadhalika huko nje, wewe pata ufunuo kutoka kwa Mungu kisha ufanye yale ambayo Mungu anakwambia ufanye. Nitafanya jambo lilo hilo. Bali Jumbe hizi, kwenye kanda, ni kwa ajili ya kanisa hili peke yake.”
Jinsi gani alivyolifanya Hilo rahisi kweli kweli kwa Bibi-arusi Wake kuliona na kuisikia Sauti ya Mungu na kufuata maagizo Yake.
Iwapo ungependa kuungana nasi kuisikia Sauti hiyo, tutakuwa tukisikiliza sote kwa wakati mmoja Jumapili hii saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni saa 1:00 MOJA JIONI masaa ya Afrika mashariki): 65-0822M – “Kristo Amefunuliwa Katika Neno Lake Mwenyewe”.
Ikiwa huwezi kuungana nasi, nakuhimiza usikilize Ujumbe huu wakati wowote uwezapo.
Kaeni karibu na Kristo. Hebu niwaonye sasa, kama mhudumu wa Injili, juu ya jambo hili. Msichukue upumbavu wo wote. Msiwazie cho chote. Kaeni moja kwa moja pale mpaka huu wa ndani wa ndani umetiwa nanga kwenye Neno, mpaka uwe ndani ya Kristo kabisa, kwa maana hicho ndicho kitu pekee ambacho kitaninino…Kwa maana, tuko katika wakati wa udanganyifu sana tuliopata kuishi ndani yake. “Utawapoteza walio Wateule kama yamkini,” kwa maana wana upako, wanaweza kufanya cho chote kama wengine wao.
Baba, Ulituonya kwamba tunaishi katika wakati wa udanganyifu zaidi ya nyakati zote. Roho hizo mbili ulimwenguni zingefanana sana, ingewadanganya walio wateule, kama yamkini. Lakini Bwana asifiwe, isingewezekana kutudanganya sisi, Bibi-arusi Wako; tutakaa na Neno Lako.
Sisi ni Uumbaji Wako Mpya, nasi hatuwezi kudanganywa. Tutakaa na Sauti Yako. Tutaitikia na kushikilia kila Neno, bila kujali mtu yeyote anasema nini. Hakuna njia nyingine isipokuwa Njia Yako iliyoandaliwa; Bwana Asema Hivi kwenye kanda.
Wakati nabii Wako alipokuwa hapa duniani, yeye alijua jinsi gani ilivyokuwa muhimu kwa Bibi-arusi kusikia kila Neno lililonenwa, kwa sababu hiyo yeye alimuunganisha Bibi-arusi Wako kwa mawasiliano ya simu. Alituunganisha pamoja kwenye Sauti Yako iliyothibitishwa ya Neno Lililonenwa.
Yeye alijua hapakuwepo na upako mkuu kuliko Sauti Yako.
Huko nje kwenye mawimbi ya simu hii, naomba Roho Mtakatifu aliye mkuu aingie katika kila kusanyiko. Jalia Nuru ile ile Takatifu tunayoiangalia papa hapa kanisani, jalia imwangukie kila mmoja, na kila mtu.
Kila kitu ambacho Bibi-rusi Wako anachohitaji kwa ajili ya kule Kuja Kwako kilinenwa, kikahifadhiwa na kufunuliwa kwa Bibi-arusi Wako na malaika Wako; hilo ni Neno Lako. Ulituambia ikiwa tuna maswali yoyote, twende kwenye kanda. Ulituambia William Marrion Branham alikuwa ndiye Sauti Yako kwetu. Kunawezaje kuwa na swali niani mwa Bibi-arusi Wako jinsi gani ilivyo muhimu kuiweka Sauti Yako kama Sauti iliyo muhimu zaidi Anayoweza kuisikia? Hakuna swali Bwana, kwa Bibi-arusi Wako.
Nabii wako alituambia juu ya ndoto ambapo alisema, “Nitapanda farasi kupitia njia hii tena.” Hatujui hilo linamaanisha nini, lakini kwa hakika Bwana, Sauti Yako imepanda farasi kwa njia ya mawimbi ya hewa leo tena, ikinena, na kumwita Bibi-arusi Wako atoke kutoka kote ulimwenguni.
Unaalikwa uje uungane nasi, Maskani ya Branham, Jumapili saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika mashariki) tunaposikiliza Sauti ya Mungu kupitia mawimbi ya hewa ikituletea Ujumbe: 65-0815 – “Nawe Hujui”.
Palipo na Mzoga, tai wanakusanyika. Ni wakati wa jioni, na unabii umetimizwa mbele ya macho yetu. Mioyo yetu inawaka ndani yetu tunapomwalika katika makanisa yetu, nyumba zetu, na vibanda vyetu vya udongo huko msituni. Atazungumza nasi na kulifunua Neno Lake. Tunaona njaa na kiu ya Mungu zaidi.
Yeye amechagua njia ile Neno lake lingetujia; ni kwa nabii Wake, ambaye Yeye alimchagua tangu zamani na kumtenga tangu zamani. Alimchagua William Marrion Branham kuwa mtu wa wakati huu kuwashika wateule Wake wa wakati huu, SISI, Bibi-arusi Wake.
Hakuna mtu mwingine anayeweza kupachukua mahali pake. Tunapenda jinsi anavyojieleza; ii, siho, iyo, pepa, dafuta, ni Mungu akizungumza masikioni mwetu. Mungu, akinena kupitia midomo ya mwanadamu, akifanya yale hasa Yeye aliyosema angefanya. Hilo latosha!
Mungu aliongoza mikono na macho yake katika maono. Yeye hakuweza kusema kitu chochote ila kile alichokuwa akikiangalia. Mungu alitawala kabisa ulimi wake, kidole, hata kila kiungo cha mwili wake kilikuwa katika utawala mkamilifu wa Mungu. Alikuwa ndiye kinywa chenyewe cha Mungu.
Mungu alijua kimbele katika wakati huu kanisa lingeingia kwenye mchafuko. Kwa hiyo, Yeye alikuwa na nabii Wake tayari kwa ajili ya wakati wetu, kumwita na kumwongoza Bibi-arusi Wake aliyechaguliwa kwa Neno Lake lililothibitishwa.
Katika mpango Wake mkuu, Yeye pia alijua angempeleka nabii Wake Nyumbani kabla ya Kuja Kwake, kwa hiyo Alihakikisha ameirekodi Sauti Yake na kuihifadhi, ili Bibi-arusi Wake mteule daima wangeweza kuwa na Bwana Asema Hivi kiganjani. Basi wasingekuwa na swali kamwe. Hakukuwa na fasiri iliyohitajiwa, Neno safi na bikira tu waliloweza kulisikia wakati wote.
Alijua kungekuwa na sauti nyingi na machafuko mengi katika siku za mwisho. Wiki tatu zilizopita amezungumza nasi na kuweka saa tunayoishi. Alituambia kuhusu manabii wa uongo ambao wangetokea na kuwadanganya wateule, kama yamkini.
Jinsi gani huyu mungu wa kizazi hiki alivyoipofusha mioyo ya watu. Na jinsi ambavyo Mungu Mwenyewe alisema kupitia kwa nabii Zake ya kwamba mambo haya yangetukia katika Wakati huu wa Laodikia. Alituambia hakuna kitu ambacho kimeachwa bila kutimia.
Amejitambulisha Mwenyewe mbele zetu kwa mambo yale yaliyotabiriwa kumhusu Yeye kuyafanya katika siku hii. Matendo yake yenyewe yametuthibitishia Yeye ni yeye yule jana, leo, na hata milele. Ni Sauti ya Mungu, ikizungumza na, na kuishi ndani ya, Bibi-arusi Wake.
Je! unaamini Ujumbe huu ni Waebrania 13:8? Kuwa ni Neno lililo hai? Kuwa ni Mwana wa Adamu akijifunua Mwenyewe katika mwili? Basi unabii utatendeka Jumapili hii ikiwa utaamini na kutii.
Kitu fulani kitakuwa kikitendeka ulimwenguni kote ambacho hakijawahi kutokea katika historia ya dunia. Mungu atakuwa akinena kupitia midomo ya mwanadamu, akizungumza na Bibi-arusi Wake kila mahali ulimwengu mzima wote kwa wakati mmoja. Atatufanya tuwekeane mikono na kuombeana mmoja kwa mwingine wakati yeye anapotuombea sisi wote.
Ninyi mlio huko nje kwenye simu, kama mmekwisha amini kwa moyo wenu wote, wahudumu wakiwa wanawawekea mikono, na wapendwa wenu wakiwawekea mikono, kama mnaamini kwa moyo wenu wote ya kwamba imekwisha, imekwisha.
Chochote tunachohitaji, Mungu atatupa ikiwa tu tutaamini… NASI TUNAAMINI. SISI NDIO BIBI-ARUSI WAKE MWAMINIFU. Itatendeka. Nguzo ya Moto itakuwa popote tutakapokusanyika na kumpa kila mmoja wetu chochote tunachohitaji, ni BWANA ASEMA HIVI.
Jalia Nuru ile ile Takatifu tunayoiangalia papa hapa kanisani, jalia imwangukie kila mmoja, na kila mtu, na jalia waponywe wakati huu. Tunamkemea adui, Ibilisi, katika Uwepo wa Kristo; tunamwambia huyo adui, ya kwamba ameshindwa na—na mateso yaliyompata badala yetu, yale mauti ya Bwana Yesu na ushindi wa ufufuo katika siku ya tatu; na ushuhuda Wake uliothibitishwa ya kwamba Yeye yuko hapa kati yetu usiku wa leo, akiwa hai, baada ya miaka elfu moja mia tisa. Jalia Roho wa Mungu aliye hai aujaze kila moyo kwa imani na nguvu, na nguvu za kuponya kutokana na kufufuka kwa Yesu Kristo, Ambaye ametambulikana sasa kwa Nuru hii kuu inayolizunguka kanisa, katika Uwepo Wake. Katika Jina la Yesu Kristo, tujalie kwa ajili ya utukufu wa Mungu.
Wewe ni Bibi-arusi Wake. Hakuna kinachoweza kuliondoa hilo kutoka kwako, HAKUNA CHOCHOTE. Shetani ameshindwa. Unaweza kuhisi una kijiko tu kilichojaa Yeye, hicho ndicho tu unachohitaji, NI HALISI. NI YEYE. WEWE NI WAKE. NENO LAKE HALIWEZI KUSHINDWA.
Liamini, likubali, lishikilie, haliwezi kushindwa. Huna nguvu lakini una mamlaka yake. Sema, “Nimeichukua Bwana, ni yangu, Wewe umenipa hiyo nami sitamwacha Shetani aichukue.”
Tutakuwa na wakati ulioje. Hakuna mahali pengine ningependa kuwa. Roho Mtakatifu atatuzunguka sote. Tumepewa Ufunuo zaidi. Mioyo iliyovunjika. Kila mtu aliponywa. Hatuwezije kusema, “Je! Mioyo yetu haikuwaka ndani yetu, nayo haiwaki sasa, kujua kwamba sasa tuko katika uwepo wa Yesu Kristo aliyefufuka, utukufu na sifa vina yeye milele.
Ndugu. Joseph Branham.
Tunaalika ulimwengu wote uje kuungana nasi:
Muda: saa 06:00 SITA MCHANA masaa ya Jeffersonville(ni saa 1:00 MOJA JIONI masaa ya Afrika mashariki) Ujumbe: 65-0801E Matukio Yakidhihirishwa Na Unabii
Maandiko ya kusoma kabla ya kusikiliza Ujumbe:
Mwanzo: 22:17-18 Zaburi: 16:10 / Sura ya 22 / 35:11 / 41:9 Zekaria 11:12 / 13:7 Isaya: 9:6 / 40: 3-5 / 50:6 / 53:7-12 Malaki: 3:1 / sura ya 4 Yohana 15:26 Luka Mt: 17:30 / 24:12-35 Warumi: 8:5-13 Waebrania: 1:1 / 13:8 Ufunuo: 1:1-3 / Sura ya 10
Sauti tunayosikia kwenye kanda ndio Sauti ile ile iliyolitangaza Neno Lake katika Bustani ya Edeni, juu ya Mlima Sinai, na kwenye Mlima wa Kugeuzwa Sura. Inasikika leo kwa Ufunuo kamili na wa mwisho wa Yesu Kristo. Inamwita Bibi-arusi Wake atoke, ikimtayarisha kwa ajili ya Kunyakuliwa. Bibi-arusi analisikia, analikubali, analiishi, naye amejiweka mwenyewe tayari kwa kuliamini.
Hakuna mtu anayeweza kuliondoa Hilo kutoka kwetu. Maisha yetu hayawezi kuchezewa. Roho wake anawaka na kuangaza ndani yetu. Yeye ametupa Uzima Wake, Roho Wake, naye Anaudhihirisha Uzima Wake ndani yetu. Tumefichwa ndani ya Mungu nasi Tunalishwa kwa Neno lake. Shetani hawezi kutugusa. Sisi hatuwezi kuondoshwa. Hakuna kinachoweza kutubadilisha. Kwa Ufunuo, sisi tumekuwa BIBI-ARUSI NENO.
Wakati Shetani anapojaribu kutuangusha, tunamkumbusha tu jinsi Mungu anavyotuona. Anapotutazama, anachokiona tu ni dhahabu SAFI. Haki yetu ni haki YAKE. Sifa zetu ni sifa ZAKE mwenyewe zenye utukufu. Utambulisho wetu unapatikana katika Yeye. Kile alicho Yeye, sasa tunakionyesha. Kile alicho nacho Yeye, TUNAKIDHIHIRISHA SASA.
Jinsi gani Yeye anavyopenda kumwambia Shetani, “Sioni dosari yoyote ndani Yake; Yeye ni MKAMILIFU. Kwangu mimi, Yeye ni Bibi-arusi Wangu, amejaa utukufu ndani na nje. Tangu mwanzo hata mwisho, Yeye ni Kazi Yangu, na Kazi Zangu zote ni kamilifu. Kwa kweli, ndani Yake kumejumlishwa na kudhihirishwa hekima na kusudi Langu la milele”.
“Nimemwona Bibi-arusi Wangu anayependeza anastahili. Kama vile dhahabu inavyofulika, Yeye amestahimili mateso kwa ajili Yangu. Yeye hajapatana, kukunjwa, au kuvunjwa, bali amefanywa kitu chenye uzuri. Majaribu na majaribio yake ya maisha haya yamemfanya Yeye kuwa Bibi-arusi wangu kipenzi”.
Je! hivyo si kama tu Bwana? Anajua jinsi ya kututia moyo. Anatuambia, “Msivunjike moyo kamwe, bali jipeni moyo”. Anaona kazi zetu za upendo Kwake. Anaona kile kinachotulazimu kupitia. Anaona vita vya kila siku tunavyovivumilia. Kwa vile anavyotupenda sisi kupitia kila moja ya hayo.
Machoni pake sisi ni wakamilifu. Ametungojea sisi tangu mwanzo wa wakati. Hataruhusu lolote litutokee isipokuwa ni kwa manufaa yetu. Anajua tutashinda kila kizuizi ambacho Shetani anachoweka mbele yetu. Anapenda kumthibitishia kwamba sisi ni Bibi-arusi Wake. Hatuwezi kuondoshwa. Sisi ndio Wale ambao amekuwa akingojea tangu mwanzo. Hakuna kinachoweza kututenganisha Naye na Neno Lake.
Alitutumia malaika-mjumbe wake mwenye nguvu ili aweze kusema nasi mdomo kwa sikio. Aliirekodi ili kusiwe na maswali yale aliyosema. Alikuwa ameihifadhi ili Bibi-arusi Wake awe na kitu cha kula mpaka Yeye ajapo kumchukua.
Haijalishi ikiwa wengine wanatuelewa vibaya na wanatutesa kwa kusema sisi ni “Watu wa Kanda”, tunafurahi, kwa kuwa hili ndilo Yeye alilotufunulia sisi tufanye. Wengine hawana budi kufanya kama wanavyohisi kuongozwa kufanya, lakini kwetu sisi, hatuna budi kuungana pamoja chini ya Sauti moja, Sauti ya Mungu iliyothibitishwa kwenye kanda.
Hatuwezi kufahamu kitu kingine chochote. Hatuwezi kuelewa kitu kingine chochote. Hatuwezi kufanya kitu kingine chochote. Hatuwezi KUKUBALI kitu kingine chochote. Sisi hatupingani na kile waamini wengine wanachohisi wanaongozwa na Bwana kufanya, lakini hiki ndicho Mungu AMETUONGOZA SISI KUFANYA, nasi ni lazima TUDUMU hapa.
Tumeridhika. Tunalishwa na Sauti ya Mungu. Tunaweza kusema “amina” kwa KILA NENO tunalosikia. Hii ndiyo Njia Mungu aliyotuandalia. Hatuwezi kufanya kitu kingine chochote.
Ninapenda tu kuwaalika kila mmoja kuja kuungana nasi. Tunazifanya ibada jinsi vile tu Ndugu Branham alivyozifanya wakati yeye alipokuwa hapa duniani. Ingawa yeye hayuko hapa katika mwili, jambo kuu ni kile Mungu alichomwambia Bibi-arusi Wake kwenye kanda.
Yeye aliualika ulimwengu kuwa sehemu ya MAWASILIANO ya simu, lakini tu ikiwa wao WALITAKA KUFANYA HIVYO. Aliwafanya wakusanyike popote walipoweza kuisikia Sauti ya Mungu ikizungumza nao wote kwa wakati mmoja. Hivyo ndivyo nabii wa Mungu alivyofanya wakati huo, kwa hiyo mimi ninajaribu tu kufanya yale yeye aliyofanya kama mfano wangu.
Hivyo, unaalikwa kuja kuungana nasi Jumapili saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville, (ni Saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) tunapomsikiliza mjumbe wa Mungu akituletea Ujumbe: Mungu Wa Wakati Huu Mwovu 65-0801M.
Ndugu. Joseph Branham
Maandiko ya kusoma kabla ya kusikiliza Ujumbe:
Mathayo Mt. sura ya 24/27:15-23 Mtakatifu Luka 17:30 Yohana Mtakatifu 1:1 / 14:12 Matendo 10:47-48 1 Wakorintho 4:1-5 / sura ya 14 2 Wakorintho 4:1-6 Wagalatia 1:1-4 Waefeso 2:1-2 / 4:30 2 Wathesalonike 2:2-4 / 2:11 Waebrania sura ya 7 1 Yohana Sura ya 1 / 3:10 / 4:4-5 Ufunuo 3:14 / 13:4 / Sura ya 6-8 na 11-12 / 18:1-5 Mithali 3:5 Isaya 14:12-14
Tuko chini ya matarajio na matazamio makubwa. Twaweza kulihisi jambo hilo, jambo fulani linaenda kutukia. Tunataka kuungana pamoja ili kuisikia Sauti Yako; kupata cho chote na kila kitu unachosema. Tunalitaka. Tunataka kuwa sehemu Yake. Tunaamini kila Neno.
Nini kinatendeka? Mungu anafanya historia. Mungu anatimiza unabii. Hiyo Daima husababisha kuvutia macho. Huwakusanya wapinzani wote, wale nderi wa Ujumbe tuliousikia Jumapili iliyopita, lakini pia linawakusanya Tai Wake pamoja. Kwa maana palipo Mzoga, hapo Tai watakusanyika.
Ni jibu la unabii wa nabii, angalieni, nitawapelekea Eliya nabii. Mungu anamthibitisha nabii Wake. Ni Mungu akitimiza unabii. Mungu akifanya historia, akilitimiza Neno Lake. Ni ule Mvuto wa Tatu ukitimia.
Najua yaonekana kama yote Nifanyayo tu ni kutokukubaliana na viongozi wote wa makanisa, naonekana kulaumu chochote wanachofanya, lakini ninaamini sisi ndio lile kundi fulani la watu ambao wamechaguliwa tangu asili Kubonyeza Play na kuusikia Ujumbe huo, Sauti hiyo, na kuufuata.
Sisi hatujali umati wa watu. Hatujali lawama za asiyeamini. Hatubishani nao. Tuna wajibu mmoja, huo ni kuamini na kupata kila sehemu Yake tuwezayo; tuiingize ndani kama Mariamu aliyeketi miguuni pa Yesu.
Hatuvutiwi na kitu kingine chochote. Hatuhitaji kitu kingine chochote. Tunaamini kwamba kila kitu tunachohitaji kusikia kiko kwenye kanda. Neno la Mungu halihitaji fasiri yoyote.
Ile ahadi imetimizwa. Ni wakati gani, bwana, na mvuto huu ni wa nini? Mungu akitimiza Neno Lake! Ni yeye yule jana, leo, na hata milele.
Ni mvuto gani? Mungu, kwa mara nyingine tena, akilitimiza Neno Lake, akiwakusanya watu Wake pamoja makanisani, vituo vya mafuta, majumbani, wamekusanyika kuzunguka vipaza sauti vidogo kutoka kote nchini, kote kote hata kwenye Pwani ya Magharibi, kule juu kwenye milima ya Arizona, chini kwenye mabonde ya Texas, mbali sana hata Pwani ya Mashariki; kote nchini na ulimwenguni kote.
Tuko umbali wa masaa mengi katika wakati, lakini Bwana, tuko pamoja kama jamii moja, waamini, tukingojea Kuja kwa Masihi. Ninajaribu kufuata na kufanya vile tu nabii Wako alivyofanya ili kumuunganisha Bibi-arusi Wako wakati yeye alipokuwa hapa. Kile yeye alichokifanya ndio mfano wangu.
Hatuna nafasi ya kumketisha kila mmoja hapa kwenye Maskani ya Branham, kwa hivyo inatulazimu tu kuwatumia Neno kwa njia ya simu, kama vile yeye alivyofanya wakati huo. Tumekusanyika hapa, Jeffersonville, katika makanisa yetu ya nyumbani, tukingojea Kuja kwa Bwana.
Umetoka kutuambia kutakuwa na wengi katika siku hizi za mwisho ambao watajaribu kukufanyia wewe kazi bila ya kuwa mapenzi Yako makamilifu. Kutakuwa na wengi ambao watatiwa mafuta na Roho Mtakatifu wa kweli, lakini watakuwa waalimu wa uongo. Bwana, njia pekee tunayojua KUWA NA HAKIKA ni kudumu na Neno, kudumu na mafundisho ya kanda, kudumu na Sauti Yako iliyothibitishwa.
Tunaamini sisi ndio Uzao Wako uliochaguliwa tangu asili ambao hatuwezi kutenda chochote bali kulifuata; ni zaidi ya maisha kwetu. Twaa maisha yetu, bali usichukue Hilo.
Nini kitatendeka Jumapili hii? Mungu atakuwa akitimiza Neno lake. Kote nchini, kwa njia ya simu, mamia ya watu watawekeleana mikono wao kwa wao kote taifani, pwani kwa pwani, kutoka Kaskazini hata Kusini, Mashariki hata Magharibi.
Hata kutoka nchi za ng’ambo ulimwenguni kote, sote tutawekeana mikono . Ulituambia, “hatuhitaji kadi ya maombi, si lazima kupitia kwenye mstari, tunahitaji tu IMANI.”
Tutainua mikono yetu na kusema, “Mimi ni mwamini.” Yapi yatatendeka?
Shetani, umeshindwa. Wewe u muongo. Na, kama mtumishi wa Mungu, na kama watumishi, tunakuamuru ya kwamba katika Jina la Yesu Kristo, ya kwamba utii Neno la Mungu na utoke ndani ya watu, kwa maana imeandikwa, “Katika Jina Langu watatoa pepo.”
Mungu mpendwa. Wewe ndiye Mungu wa Mbinguni uliyeshinda, siku hiyo kwa mvuto juu ya Mlima Kalvari, magonjwa yote na maradhi na kazi zote za Ibilisi. Wewe ni Mungu! Na watu wameponywa kwa mapigo Yako. Wao ni huru. Katika Jina la Yesu Kristo. Amina.
Mungu ATATIMIZA Neno Lake!
Ningependa kukualika uje kusikiliza pamoja nasi, sehemu ya Bibi-arusi Wake, tunapousikia Ujumbe: 65-0725E Nini Kinachovutia Kule Mlimani? Tutakusanyika Jumapili saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville.(Ni Saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki).
Wengine wanaweza kuhisi sisi tu madhehebu kwa kukusanyika pamoja, kusikiliza Ujumbe uleule kwa wakati mmoja, lakini naamini kama Ndugu Branham angekuwepo hapa, angekuwa anafanya kile hasa tutakachokifanya, kumkusanya Bibi-arusi pamoja, kutoka ulimwenguni kote, kusikiliza kwa wakati mmoja KUMSIKIA YEYE.
Ndugu. Joseph Branham
Maandiko:
Mathayo 21:1-4 Zekaria 9:9 / 14:4-9 Isaya 29:6 Ufunuo 16:9 Malaki 3:1 / Sura ya 4 Yohana Mt 14:12 / 15:1-8 Luka Mt 17:22-30
Mungu alimtuma malaika-mjumbe wake wa saba amwongoze Bibi-arusi Wake; si mtu mwingine, si kundi la watu, bali MTU MMOJA, kwa maana Ujumbe na mjumbe Wake ni kitu kile kile. Neno la Mungu halihitaji kufasiriwa. Alilinena kwa Bibi-arusi Wake kupitia midomo ya mwanadamu nasi tunaliamini Hilo jinsi vile tu Yeye alivyolisema.
Ni lazima tuwe waangalifu sana leo ni sauti gani inayotuongoza, na inatuambia nini. Kikomo chetu cha milele kinategemea uamuzi huo hasa; kwa hiyo ni lazima tuamue ni sauti gani ndio sauti iliyo muhimu zaidi ambayo tunayopaswa kuisikia. Ni Sauti gani ambayo imethibitishwa na Mungu? Ni Sauti gani iliyo na Bwana Asema Hivi? Haiwezi kuwa sauti yangu, maneno yangu, fundisho langu, lakini lazima liwe Neno, kwa hiyo ni lazima tuende kwenye Neno kuona kile Linachotuambia.
Je! linatuambia kwamba Yeye atainua huduma tano ituongoze mwishoni? Tunaweza kuona waziwazi katika Neno wao wana mahali pao; mahali muhimu sana, lakini Je, Neno linasema MAHALI POPOTE kuwa wao ndio watakaokuwa na sauti zilizo muhimu zaidi TUNAZOPASWA kuzisikia ili kuwa Bibi-arusi?
Nabii alituambia kutainuka watu wengi katika siku za mwisho watakaojaribu kumtendea Mungu kazi bila ya kuwa Mapenzi Yake. Ataibariki huduma yao, lakini sio njia Yake kamilifu ya kumwongoza Bibi-arusi Wake. Alisema Mapenzi yake makamilifu ni, na daima yamekuwa, ni kuisikia na kuiamini Sauti ya nabii wake aliyethibitishwa; kwa maana ni Hiyo, na hiyo peke yake ndio iliyo na Bwana Asema Hivi. Ndioamana alimtuma malaika Wake. Ndiomaana alimchagua yeye. ndiomaana Yeye aliirekodi. Ni Chakula Cha Kiroho Kwa Wakati Wake, Mana Iliyofichwa, kwa Bibi-arusi Wake.
Kwa kuwa saba kati ya nyakati saba, sijaona kitu ila watu wakiliheshimu neno lao wenyewe kuliko Langu. Kwa hiyo mwishoni mwa wakati huu ninawatapika mtoke katika kinywa Changu. Yote yamekwisha. Nitazungumza basi. Naam, niko hapa katikati ya Kanisa. Amina wa Mungu, aliye mwaminifu na wa kweli atajifunua Mwenyewe na itakuwa KWA NJIA YA NABII WANGU.” Loo! ndiyo, hivyo ndivyo ilivyo.
Saba kati ya nyakati saba watu wanaliheshimu neno lao wenyewe kuliko Langu. Unatakiwa kujiuliza mwenyewe, Je, jambo hili halifanyiki kati yetu hivi sasa? “Usicheze kanda kanisani, bali lazima umsikie mchungaji wako, zicheze tu kanda nyumbani kwako”. Wao hawaiweki Sauti Yake iliyo kwenye kanda kuwa ndio Sauti iliyo muhimu zaidi, bali sauti yao.
Wanawaelekeza watu kwao wenyewe, na umuhimu wa huduma YAO; Wito WAO kulileta Neno, kumwongoza Bibi-arusi; Lakini Bibi-arusi hawezi kulivumilia hilo. Hawatalikubali. Hawatalifanya jambo hilo. Hawatapatana kuhusu Hilo; ni Sauti ya Mungu na si kitu kingine. Hivyo ndivyo Neno linavyosema.
Swali lililo niani mwa watu siku hizi ni: Ni nani ambaye Mungu alimchagua kumuongoza Bibi-arusi Wake, Je, ni kanda au ni huduma tano? Je, wahudumu watamkamilisha Bibi-arusi? Je, wahudumu watamwongoza Bibi-arusi? Kulingana na Neno la Mungu, hiyo haijawahi kamwe kuwa Njia Yake.
Kuna watu wengi sana leo wanaosema wameufuata na kuuamini Ujumbe huu kwa miaka na miaka, lakini sasa wanaiweka huduma YAO kuwa ndio sauti iliyo muhimu zaidi unayopaswa kuisikia.
Utaifuata huduma ipi basi? Utaweka kikomo chako cha Milele kwenye huduma ipi? Wote wanasema wameitwa na Mungu kuhubiri Ujumbe. Sikatai ama kulihoji hilo, lakini baadhi ya wahudumu wenye ushawishi mkubwa katika vyeo vya huduma tano wanasema, “Hiyo siyo Sauti ya Mungu, ni sauti ya William Branham tu”. Wengine wanasema, “siku za Ujumbe wa mtu mmoja zimepita”. “Ujumbe huu sio Yakini”. Je, Huyo ndiye anayekuongoza?
Wanaume ambao wamehubiri katika mamia ya makusanyiko yao, viongozi wakubwa wa huduma tano, SASA wanaukana Ujumbe na KUSEMA “Ujumbe huu ni wa uongo”.
Nyingi kati ya huduma zote husema, “Hampaswi kusikiliza Sauti ya malaika wa Mungu kanisani, isipokuwa tu majumbani mwenu.” “Ndugu Branham hakusema kamwe kuzicheza kanda kanisani.”
Hilo halisadikiki. Siamini ndugu ama dada wanaosema wanaamini Ujumbe huu; kwamba Ndugu Branham ndiye malaika-mjumbe wa saba wa Mungu, ni Mwana wa Adamu anayezungumza, angeangukia kwenye kauli ya udanganyifu kama hiyo. Hilo lingepaswa kukuchefua tumbo. Ikiwa wewe ni Bibi-arusi, LITAKUCHEFUA.
Mungu hajawahi kamwe kubadilisha Nia Yake kuhusu Neno Lake. Daima Yeye amemchagua mtu mmoja kuwaongoza watu wake. Wengine wana mahali pao, lakini wao wanapaswa kuwaongoza watu kwa yule mmoja ambaye YEYE amemchagua kuwaongoza watu. Amkeni, enyi watu. Hebu jaribuni kusikiliza kile hawa wahudumu wanachowaambia, Nukuu hizo wanazotumia kuiweka huduma yao mbele ya ile ya nabii. Inawezaje huduma ya mtu ye yote kuwa ndio muhimu zaidi kuisikia kuliko Sauti ya Mungu iliyothibitishwa ambayo Yeye ameihakikisha na kuithibitisha kuwa Bwana Asema Hivi?
Yeye ametuambia, na kutuambia, kunaweza kuwa na watu waliotiwa mafuta kweli, na Roho Mtakatifu wa kweli juu yao, ambao ni wa uongo. Kuna NJIA MOJA tu ya kuwa na hakika, KUKAA NA NENO LA ASILI, kwa maana Ujumbe huu na mjumbe ni kitu kile kile. Kuna Sauti moja tu ambayo Mungu aliichagua kuwa Bwana Asema Hivi…MOJA.
Huduma ya kweli itakuambia kwamba HAKUNA KITU kilicho muhimu zaidi kuliko kulisikia Neno la Mungu kutoka kwenye Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda. Wao wanaweza kuhubiri, kufundisha, au chochote walichoitiwa kufanya, LAKINI LAZIMA WAIWEKE SAUTI YA MUNGU KUWA NAFASI YA KWANZA; LAKINI WAO HAWAFANYI HIVYO, BALI WANAIWEKA HUDUMA YAO KUWA NDIO NAFASI YA KWANZA. Matendo yao yenyewe yanathibitisha kile wanachoamini.
Wanakwepa kujibu swali kuhusu kuiweka Sauti ya Mungu kwenye mimbara zao kwa kusema, “Ndugu Joseph haamini katika wahudumu. Haamini katika kwenda kanisani. Wao wanamwabudu mtu. Wanafuata fundisho hilo la Joseph. Yeye anatengeneza dhehebu kwa kucheza na kusikiliza wote kanda ileile.” Wakiwakengeusha tu watu kutoka kwenye swali kuu hasa, lakini matendo yao yanathibitisha kile wanachoamini kwa kile wanachowafundisha watu wao: HUDUMA YAO NDIO NAFASI YA KWANZA.
Wanasema, kuwafanya watu wasikilize wote kanda ile ile kwa wakati mmoja ni dhehebu. Je! Hivyo sivyo hasa alivyofanya Ndugu Branham Wakati yeye alipokuwa hapa; kuwaunganisha watu kwa simu ili wasikie Ujumbe wote kwa wakati mmoja?
Wewe jiulize, kama Ndugu Branham angekuwepo hapa leo katika mwili, Je! hangewafanya Bibi-arusi wote KUJIUNGANISHA KWA SIMU ili wamsikie yeye wote kwa wakati mmoja? Je! asingejaribu kuwakusanya Bibi-arusi pamoja katika HUDUMA YAKE kama vile yeye alivyofanya kabla Mungu hajampeleka nyumbani?
Hebu niingize kitu fulani hapa. Wakosoaji watasema, unaona, anafanya yale yale, kumsifia huyo mtu sana; wao wanamfuata mtu, William Marrion Branham!! Hebu tu tuone kile Neno linachosema kuhusu hilo pia:
Katika siku za mjumbe wa saba, katika siku za wakati wa Laodikia, mjumbe wake atafunua siri za Mungu kama zilivyofunuliwa kwa Paulo. Yeye atanena, na hao watakaompokea nabii huyo katika jina lake mwenyewe watapokea matokeo mema ya huduma ya nabii huyo.
Hili litamkasirisha shetani zaidi ya chochote kile naye atanishambulia hata na zaidi, lakini enyi watu, afadhali mlichunguze hili kwa Neno. Si kwa sababu mimi nimelisema, hapana, basi ningekuwa kama mtu yeyote yule; bali ifungueni mioyo yenu na nia zenu na mlichunguze hilo kwa Neno. Si kile mtu mwingine ye yote anachosema au anachowafasiria, bali kile nabii wa Mungu alichosema.
Baada ya barua hii wao watawapa nukuu baada ya nukuu baada ya nukuu, nami nasema AMINA kwa kila nukuu, LAKINI VIPI KUHUSU JAMBO LILILO KUU? Je! wanazitumia nukuu kuwaambia kuwa kumsikia nabii ndilo jambo mnalopaswa kufanya, au HUDUMA YAO? Wakisema Ujumbe, nabii, basi waambieni waiweke hiyo Sauti KUWA NAFASI YA KWANZA katika kanisa lenu.
Juu ya msingi wa tabia za wanadamu peke yake, mtu ye yote anajua ya kwamba palipo na watu wengi kuna hata na maoni yasiyopatana juu ya mambo madogo-madogo ya fundisho muhimu ambalo wote wanashikilia pamoja.
Hilo hapo. Hii nukuu moja tu inawaambia haiwezi na HAITAKUWA kundi la watu. Si wahudumu watakaowaunganisha watu kwa sababu ya tabia za wanadamu peke yake; wamegawanyika juu ya maoni ya mambo madogo-madogo ya mafundisho muhimu. Wote hawawezi kukubaliana, kwa hivyo mnapaswa kurudi kwenye NENO LA ASILI.
Ni nani basi atakayekuwa na mamlaka ya kutokosea ambayo itarudishwa katika wakati huu wa mwisho, kwa kuwa wakati huu wa mwisho utarudi kwenye kumdhihirisha Bibi-arusi wa Neno Halisi?
NI NANI atakayetuongoza? SAUTI MOJA, iliyo na mamlaka ya kutokosea ndio itamwongoza Bibi-arusi.
Hiyo inamaanisha tutakuwa na Neno tena kama lilivyotolewa kikamilifu, na kueleweka kikamilifu katika siku za Paulo.
Utukufu… Limetolewa kikamilifu na kueleweka kikamilifu. Halihitaji fasiri, kwa vile lilivyotolewa kikamilifu, na sisi, Bibi-arusi, tunalielewa kikamilifu na kuamini kila Neno.
Hilo hapo. Yeye anamtuma nabii aliyethibitishwa.
Anatuma nabii baada ya karibu miaka elfu mbili.
Yeye anamtuma mtu fulani aliye mbali sana na madhehebu, elimu, na ulimwengu wa dini hivi kwamba kama vile Yohana Mbatizaji na Eliya wa kale,
Yeye ata-sikia tu kutoka kwa Mungu
Ata-kuwa na “Bwana asema hivi” na kunena kwa niaba ya Mungu.
Yeye atakuwa kinywa cha Mungu
NAYE, KAMA INAVYOTANGAZWA KATIKA MAL. 4:6, ATAIGEUZA MIOYO WA WATOTO IWAELEKEE BABA ZAO.
Atawarudisha wateule wa siku za mwisho nao watamsikiliza nabii aliyethibitishwa akitoa kweli halisi kama vile ilivyokuwa kwa Paulo.
Atairudisha kweli kama walivyokuwa nayo.
Na hao wateule walio pamoja naye katika siku hiyo watakuwa ndio wanaomdhihirisha Bwana kwa kweli na watakuwa ndio Mwili Wake na kuwa sauti Yake na kutenda kazi Zake. Haleluya! Unaliona hilo?
Umealikwa kuja kuungana nasi wakati tunapokisikia kinywa cha Mungu, Sauti ile itakayo muunganisha Bibi-arusi wa Yesu Kristo, Nabii wake aliyethibitishwa, anapotupa ukweli halisi, saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki)
Mpendwa Bibi-arusi wa Kristo, hebu na tukusanyike pamoja Jumapili saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni Saa 1 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) ili kusikia 65-0718E Chakula cha Kiroho Kwa Wakati Wake.