Tumewasili. Tumefika. Kule Kuthibitishwa kwa Neno kumethibitisha ya kwamba Ufunuo wetu wa Ujumbe Huu unatoka kwa Mungu. Tuko katika MAPENZI Yake MAKAMILIFU kwa kudumu na Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda.
Kubonyeza Play ni muhimu jinsi gani? Maneno tunayosikia kwenye kanda ni muhimu sana, matakatifu sana, hivi Mungu Mwenyewe hata asingeweza kumwamini kumpa hayo Malaika…hata kwa mmoja wa Malaika Wake wa Mbinguni. Ilibidi yafunuliwe na kuletwa kwa Bibi-arusi Wake na nabii Wake, kwa maana huyo ndiye Neno la Mungu humjia, nabii Wake, PEKE YAKE.
Mungu aliichana ile Mihuri, akaikabidhi kwa malaika-mjumbe Wake wa saba wa duniani, na kumfunulia Kitabu chote cha Ufunuo. Kisha, Mungu akanena kupitia malaika Wake wa duniani na kufunua KILA KITU kwa Bibi-arusi Wake.
Kila maelezo madogo yamenenwa na kufunuliwa kwetu. Mungu ametujali sana hivi kwamba Yeye hakutuambia tu mambo ambayo yametukia hapa duniani tangu mwanzo wa wakati, bali alinena kupitia malaika Wake na kutuambia mambo yanayoendelea katika mahali kama paradiso sasa hivi.
Yeye hakutaka tuhangaike, ama tusiwe na hakika juu ya kile wakati ujao unachoshikilia kwa ajili yetu wakati tuiachapo maskani hii ya kidunia. Kwa hiyo, Mungu Mwenyewe alimchukua malaika Wake wa saba mwenye nguvu ng’ambo ya pazia la wakati, kusudi aweze kuliona, kulihisi, hata azungumze nao kule ng’ambo. Haikuwa ono, alikuwepo KULE.
Mungu alimpeleka huko ili yeye aweze kurudi na kutuambia: “Nilikuwa huko, nililiona. Linatukia SASA HIVI… Mama zetu, baba zetu, kaka zetu, dada zetu, wanetu, mabinti zetu, wake, waume, babu, Musa, Eliya, WATAKATIFU WOTE ambao waliotangulia huko wamevalia mavazi meupe, wakipumzika na wakitungojea SISI”.
Hatutalia tena, maana Itakuwa ni furaha tupu. Hatutakuwa na huzuni tena, maana itakuwa furaha tupu. Hatutakufa kamwe, maana yote ni Uzima mtupu. Hatuwezi kuzeeka, maana sote tutakuwa vijana milele.
Ni ukamilifu…kuongeza ukamilifu…kuongeza ukamilifu, nasi tunakwenda huko!! Na kama vile Musa, hatutaacha hata ukwato, SOTE TUNAKWENDA…FAMILIA YETU YOTE.
Ni muhimu jinsi gani KUMPENDA huyo malaika wa saba mwenye nguvu?
Nayo ikalia, ikasema, “Vyote ulivyowahi kupenda…” thawabu ya huduma yangu. Sihitaji thawabu yo yote. Akasema,“Vyote ulivyowahi kupenda, na wote waliowahi kukupenda,Mungu amekupa.”
Hebu tulisome hilo tena tafadhali: Amesema nini?….Mungu amekupa WEWE!!
Nasi tutaungana nao na kupaza sauti, “Tunategemea Jambo Hilo”
Tumekitegemeza kikomo chetu cha milele juu ya nini? KILA NENO LILILONENWA KWENYE KANDA. Ninamshukuru sana Bwana kuwa ametupa Ufunuo wa Kweli kwamba Kubonyeza Play ndilo jambo lililo MUHIMU SANA ambalo Bibi-arusi analopaswa kufanya.
Je! ungependa kupumzika pamoja nasi? Njoo uungane nasi Jumapili hii saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) tunaposikia yote yahusuyo wakati ujao unachoshikilia, wapi tunakoenda, na jinsi ya kufika huko, tunaposikia Sauti ya Mungu ikinena na kuufungua: Muhuri Wa Tano 63-0322.
Baba anatukusanya pamoja kwa Neno Lake, na kule kuthibitishwa kwa Ufunuo huo kunatupa changamko. Yeye alituchagua kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu, kwa maana Yeye alijua tungekuwa waaminifu kwa Neno Lake kwa uchaguzi wetu wenyewe.
Hebu niliseme hilo tena ili liweze kuzama ndani kabisa. Yeye Alitazama kote katika wakati, hadi mwisho kabisa wa nyakati zote, na KUTUONA SISI… hivi unalisikia hilo? ALIKUONA WEWE, ALINIONA MIMI, na akatupenda, kwa sababu kwa uchaguzi wetu wenyewe, sisi tungedumu NA NENO LAKE.
Wakati huohuo, huenda aliwaita pamoja malaika Zake wote na makerubi na kutuelekezea sisi kidole na kusema: “HUYO NDIYE MWANAMKE MWENYEWE,” “HUYO NDIYE BIBI-ARUSI WANGU,” “HAO NDIO AMBAO NIMEKUWA NIKIWASUBIRI!”
Kama vile Yohana, hiyo ndiyo sababu tunapiga makelele haya yote na kupaza sauti, na kumsifu Bwana, tumechangamshwa na Divai Mpya na tunajua, BILA SHAKA HATA CHEMBE, SISI NI Bibi-arusi Wake.
Ni kama mvua na mvua za ngurumo zote ambazo tumekuwa nazo hapa Jeffersonville wiki hii…Sisi pia tunatuma ONYO kwa ulimwengu.
Bibi-arusi anapokea MVUA YA NGURUMO YA UFUNUO, NAYO INATOA MAFURIKO YA UFUNUO. BIBI-ARUSI AMEJIWEKA TAYARI NAO WAMEJITAMBUA WAO NI NANI. NENDA MAHALI SALAMA UPESI. BONYEZA PLAY AMA UANGAMIE.
Hatuishi katika wakati wa Simba, au wakati wa Ndama, wala Wakati wa Mwanadamu; tunaishi katika WAKATI WA TAI, Naye Mungu ametutumia tai mwenye nguvu, Malaki 4, kumwita Bibi-arusi Wake atoke na kumwongoza.
Litakuwa jambo lenye manufaa jinsi gani Jumapili hii, tutakapokuwa tumeungana pamoja tukiusikiliza Muhuri wa Nne. Itakuwa ni Siku ya Kuzaliwa ya nabii-tai mwenye nguvu wa Mungu.
Hebu na tuisherehekee siku hii ya ajabu na tumshukuru Bwana kwa kututumia mjumbe-tai Wake, ambaye aliyemtuma kutuita tutoke na kilifunua Neno Lake.
Ndugu. Joseph Branham
Ujumbe: Muhuri wa Nne 63-0321
Muda: saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville (Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki)
Hebu niianze barua yangu leo na bomu la atomiki la Mungu; si bunduki aina ya 22, BOMU LA ATOMIKI kwa Bibi-arusi wa Yesu Kristo.
Sasa, kama unataka kuandika mambo hayo; bila shaka, nyote mnayajua: Yesu, Yohana 14:12; na Yoeli, Yoeli 2:38; Paulo, Timotheo wa Pili 3; Malaki, mlango wa 4; na Yohana mfunuzi, Ufunuo 10, kumi na saba, moja hadi kumi na saba. Unaona, ni vile vile ambavyo ingetukia sasa!
Notisi na onyo: Nukuu ifuatayo si kwa ajili yako ikiwa wewe unaamini.
“Tunamwelezea sana nabii wa Mungu.” “Huwezi kuwa Bibi-arusi ikiwa tu unamsikiliza nabii.” “Kuzicheza kanda kanisani ni kosa.” “Mwenge umepitishwa; jambo lililo muhimu zaidi leo ni kuwasikiliza wahudumu.” “Kubonyeza play wote kwa wakati mmoja ni dhehebu.”
Kwa kanisa, ni Kitu gani? Neno lililofanyika mwili likifanywa mwili miongoni mwa watu Wake tena! Unaona?
KABUUM…Kwa hivyo kwa kubonyeza play, tunaweza kulisikia Neno lililofanyika mwili, likinena nasi mdomo kwa sikio anapolifunua Neno Lake.
Na mtu fulani anaweza kusema ati Sio SAUTI ILIYO MUHIMU ZAIDI UNAYOPASWA KUISIKIA? Sehemu hii ya nukuu ni kwa ajili yako.
Nao hawaliamini Hilo kamwe.
Kadiri Bwana anavyozidi kutupa sisi Ufunuo zaidi wa Neno Lake, na sisi ni nani, ndivyo kila mtu aliye nje ya Ufunuo huo anavyozidi kuwa mbali zaidi.
Hebu niseme jambo hilo, vizuri hasa, ili mninii… litadidimia ndani sana. Ninataka hili lilipatie hasa. Hiyo ndiyo shida yenu leo, mnaona, hamlijui Neno! Mnaona?
Mungu anao watu waliotiwa mafuta kuhubiri Ujumbe Huu, lakini kuna Yakini moja tu: Neno. Unapomsikia mhudumu, au mtu ye yote akinena, ni lazima uwe na imani ya kuamini kuwa anachokisema ndicho HASA ambacho nabii wa Mungu alichokwisha sema. Neno lao, ufunuo wao, fasiri yao inaweza kushindwa; Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda HAIWEZI KUSHINDWA KAMWE.
Nena kuhusu Mungu katika urahisi kwa kubonyeza play…Yeye analisema TENA.
Wanapitwa Naye, Neno lililo hai lililodhihirishwa katika mwili, kwa Neno lililoahidiwa. Neno liliahidi kufanya mambo haya. Ahadi ilifanywa, ya kwamba itakuwa hivi katika siku za mwisho.
Sikiliza Ngurumo Yake. Ngurumo ni Sauti ya Mungu. William Marrion Branham ndiye Sauti ya Mungu kwa kizazi hiki.
Bi-Bibi arusi hajawa na uamsho bado. Mnaona? Hakujakuwako na uamsho humo, hakujakuwako na madhihirisho ya Mungu kumwamsha Bibi-arusi bado. Mnaona? Tunautarajia huo sasa. Itahitaji hizo Ngurumo Saba zisizojulikana kule nyuma, kumwamsha Yeye tena, unaona. Naam. Yeye atazituma. Aliliahidi. Sasa angalia.
Unaweza kulipindisha hilo ukipenda, lakini zile Ngurumo Saba zitampa Bibi-arusi changamko kwa Ufunuo na imani ya kunyakuliwa, ambayo huja tu kwa Roho Mtakatifu akizungumza kupitia nabii wa Mungu. Hilo linatendeka SASA HIVI ulimwenguni kote. Mungu amemchangamsha Bibi-arusi Wake na Neno Lake.
Si hivyo tu, bali tayari Yeye amekwisha mwambia adui yetu la kufanya.
Usiwaguse. Wao wanajua wanakoenda, kwa maana wametiwa Mafuta Yangu. Na kwa kutiwa kwa Mafuta Yangu, wao wana divai ya furaha, maana wanajua Neno Langu la ahadi, ‘Nitawafufua tena.’ Usidhuru Hao! Usiende ukajaribu kuwachafua.
Yeye amemwambia adui yetu aiondoe mikono yake michafu mbali nasi. Lakini je! ugonjwa bado ungali unaweza kutushambulia? Ndiyo. Je! bado tungali tunayo matatizo? Ndiyo. Lakini Yeye pia alituambia la kufanya.
Ni la kilindi. Lisome polepole na mara tena na tena.
Kabla ya kuwa Neno, ni wazo. Nalo wazo halina budi kuumbwa. Vema. Kwa hiyo, mawazo ya Mungu yakawa uumbaji wakati yaliponenwa, kwa Neno. Hapo ndipo wakati anapoyaleta kwa—kwako kama wazo, wazo Lake, nalo linafunuliwa kwako. Halafu, lingali ni wazo mpaka wewe utakapolinena.
Mawazo Yake yakawa uumbaji wakati yaliponenwa. Kisha, mawazo Yake yaliletwa na kufunuliwa kwetu kama Neno. Sasa lingali ni wazo kwetu mpaka tutakapolinena. KWA HIYO TUNAYANENA… NA KUYAAMINI.
Mimi ni Uzao wa Kifalme wa Ibrahimu. Mimi ni Bibi-arusi wa Kristo. Niliteuliwa na kuchaguliwa tangu zamani kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu kuwa Bibi-arusi Wake, na hakuna kitu kinachoweza kulibadili hilo. Kila ahadi katika Biblia ni yangu. Ni Neno Lake kwangu. Mimi ni mrithi wa Ahadi yenyewe. Yeye ndiye Bwana Mungu aniponyaye magonjwa yangu yote. Chochote ninachokihitaji ni changu, Mungu alisema hivyo.
Mungu katika Urahisi: Imani huja kwa kusikia, kulisikia Neno. Neno huja kwa nabii.
Kila mtu anataka kuzitumia “NUKUU” kuthibitisha mawazo yao, mafikara yao, ujumbe wao. Nao wako sahihi, nafanya vivyo hivyo na mimi, ndio maana yote niwapayo ni nukuu za kuwaambia: Dumuni na Kanda. Isikilizeni hiyo Sauti. Sauti hiyo ni Sauti ya Mungu. Hamna budi kuamini kila Neno lililo kwenye Kanda, si yale mtu mwingine yeyote asemayo. Hiyo Sauti NDIO SAUTI ILIYO MUHIMU ZAIDI MNAYOPASWA KUISIKIA.
Wengine huzitumia nukuu kuwaleta ninyi kwenye huduma yao, kwenye kanisa lao, kwenye fasiri zao, ufunuo wao. “Dumuni na mchungaji wenu.” (Vema, ninaipenda hiyo pia, kwa sababu sisi tunadumu naye, ila tu mchungaji tofauti.) “Yeye siye changarawe pekee ufukoni.” “Yeye hakusema kamwe kuzicheza kanda kanisani.”
Usiweke fasiri yo yote ya kibinafsi Kwake. Yeye anataka Neno lililo safi, lisiloghoshiwa, hata ubembe wo wote usiwepo. Singetaka mke wangu afanye ubembe na mwanamume mwingine. Na unapoanza kusikiliza hoja za namna yo yote, zaidi ya Hilo, unasikiliza, unafanya ubembe na Shetani. Amina! Hilo halikufanyi ujisikie kubarikiwa? Mungu anakutaka ubakie msafi kabisa. Udumu daima hapo na Neno hilo. Dumu Nalo. Vema.
Mimi na nyumba yangu, tutabonyeza play na kulifuata Neno la Mungu lililofanyika Mwili linenalo kupitia malaika-mjumbe Wake wa saba. Hatutaongeza fasiri yetu ya kibinafsi Kwake; hatutabembana au kusikiliza hoja yoyote. TUTADUMU NA NENO HILO KAMA LILIVYONENWA KWENYE KANDA. Ni Mungu katika Urahisi.
Ni wakati mtukufu jinsi gani tutakaokuwa nao Jumapili hii saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) Tusikiapo: Muhuri Wa Tatu 63-0320. Ningependa kuwaalika mje mkaungane nasi tunapoungana katika Neno la leo.
Ndugu. Joseph Branham
Maandiko ya kusoma kabla ya kusikiliza Ujumbe:
Mathayo mt. 25:3-4 Yohana Mt. 1:1, 1:14, 14:12, 17:17 Matendo Sura ya 2 I Timotheo 3:16 Waebrania 4:12, 13:8 1 Yohana 5:7 Mambo ya Walawi 8:12 Yeremia Sura ya 32 Yoeli 2:28 Zekaria 4:12
Hebu nichukue fursa hii kuliweka wazi kwa mara nyingine tena. Mimi sipingani na huduma tano. Ninaamini katika huduma tano. Sioni ni vibaya kumsikiliza mhudumu. Naamini unapaswa kumsikiliza mchungaji wako pale ambapo Mungu amekuweka. Nisemalo ni kwamba, Ninaamini Mungu alimtuma nabii katika siku yetu. Mungu alilifunua Neno Lake kwa nabii Wake. Mimi naweza kukosea, mchungaji wako anaweza kukosea, lakini LAZIMA tukubaliane (tukisema tunauamini UJUMBE HUU ni kweli na Ndugu Branham ni nabii wa Mungu) yale yaliyosemwa kwenye kanda ni Bwana Asema Hivi. Kama huamini hilo, basi wewe huamini Ujumbe huu. Hivyo, Mimi ninaamini ndio SAUTI ILIYO MUHIMU ZAIDI UNAYOPASWA KUISIKIA. Huhitaji kunisikia mimi, huhitaji kumsikia mtu mwingine yeyote, lakini LAZIMA UISIKIE SAUTI HIYO ILIYO KWENYE KANDA.
Swali: Je! tuko katika Mapenzi Yake makamilifu kwa kuzicheza Kanda? Jibu: NDIYO.
Swali: Je! Bibi-arusi anahitaji zaidi ya yale yaliyosemwa kwenye Kanda? Jibu: HAPANA.
Swali: Je! tunakosa kitu kwa sisi kusikiliza Kanda TU? Jibu: HAPANA.
Swali: Je! tunaweza kuwa Bibi-arusi kwa kusikiliza Kanda TU? Jibu: NDIYO, KWA MSISITIZO ZAIDI!
Sasa kumbukeni, “Hakuna lo lote linaloweza kufunuliwa; Mungu hatafanya neno lo lote, hata kidogo, mpaka kwanza alifunue kwa watumishi Wake, manabii.”
Hivyo, YOTE tunayohitaji yamekwisha nenwa na yako kwenye kanda; au, wakati malaika Wake wa saba atakaporudi duniani, YEYE atatuambia basi.
Loo! Bibi-arusi, hebu na tuwazie kile kinachotendeka miongoni mwa Bibi-arusi wa Kristo ulimwenguni kote. Baba anamkusanya Bibi-arusi Wake pamoja kwa Sauti Yake Naye Ananguruma, “Bwana Asema Hivi.”
Kumbukeni, alituambia zile Ngurumo zilikuwa kitu gani: “sauti kuu ya kishindo cha Ngurumo ni Sauti ya Mungu”. Nayo Sauti ya Mungu kwa Bibi-arusi ni nini? Malaika-mjumbe wa saba wa Mungu, William Marrion Branham.
Yeye alisema kunakuja Ngurumo saba za siri ambazo hata hazijaandikwa kamwe. Na ya kwamba kupitia Ngurumo hizo Saba, zitamkusanya Bibi-arusi pamoja kwa ajili ya kupata imani ya kunyakuliwa.
Neno la Bwana huwajia manabii Wake. Kama angekuwa na utaratibu bora zaidi, angeliutumia. Yeye alichagua utaratibu bora zaidi ya wote hapo mwanzo Naye hawezi, na hatabadilika.
Kwa hiyo, Sauti ya Mungu, inayonena kupitia malaika Wake wa saba, inamkusanya Bibi-arusi Wake pamoja na kutupa Imani ya Kunyakuliwa.
Kanisa halijashangaa tangu mwaka wa 1933, kule chini mtoni siku ile, ya kwamba William Marrion Branham ndiye Sauti ya Mungu, Inayonguruma, “Bwana Asema Hivi,” naye alitumwa kumwita, kumkusanya, na kumwongoza Bibi-arusi.
Ningependa kuwaalika mje msikilize pamoja nasi Jumapili saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville, (Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) wakati Bwana wetu Yesu anapokifungua kile Kitabu, kuuvunja huo Muhuri, na kuutuma duniani, kwa malaika Wake wa saba, atufunulie huo SISI!
Ndugu. Joseph Branham
Tarehe: Jumapili, 23 Machi, 2025
Ujumbe: Muhuri wa Pili 63-0319
Muda: Saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville (Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki)
Ninayo mengi sana kwa ajili yako Jumapili hii. Kwanza, utasikia kishindo cha Ngurumo. Itakuwa Sauti Yangu, Sauti ya Mungu ikinena nawe, Bibi-arusi Wangu. Nitakuwa nikikufunulia wewe Neno Langu zaidi ya hapo awali. Utaniona Mimi, yule Mwana-Kondoo aliyelowa damu ambaye aliyechinjwa tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu, nikikitwaa na kukifungua kile Kitabu, na kuichana ile Mihuri, na kukituma duniani, kwa malaika-mjumbe Wangu wa saba, William Marrion Branham, kuwafunulia NINYI siri ambazo zimefichwa tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu!
Kutakuwa na vigelegele, vifijo, na zile haleluya kutoka kote ulimwenguni wakati nizungumzapo nawe. Simba atakuwa akinguruma; watiwa mafuta, nguvu, utukufu, dhihirisho haitaelezeka. Wewe, Malkia Wangu, utakuwa umeketi pamoja katika ulimwengu wa roho Nikisema nawe na kukupa Imani ya kunyakuliwa.
Kumbuka, huna budi kuwa na hiyo Imani waliokabidhiwa watakatifu mara moja. Nilikuambia, lazima umsikilize malaika Wangu Niliyekutumia.
Yeye “atairudisha Imani ya watoto ielekee baba zao.” Ile imani asili ya Biblia itarudishwa na malaika wa saba.
Neno Langu linakuambia, katika siku za Sauti ya malaika wa saba, kupiga kwake baragumu, kupiga baragumu ya Injili; anapaswa kumaliza siri zote za Mungu. Hakuwezi kuwa na kitu hata kimoja chakuongezwa na hakuna kitu chakuondolewa kutoka kwenye yale niliyosema kwenye kanda; wewe sema tu kile Nilichosema Mimi kupitia malaika-mjumbe Wangu. Ndio maana niliirekodi, ili uweze tu KUBONYEZA PLAY na kusikia hasa kile nilichosema, na jinsi Nilivyosema. Itakupa Imani ya Kunyakuliwa.
Malkia Wangu kipenzi, Machoni Pangu, wewe ni mkamilifu, huna dhambi kabisa mbele Zangu. Usijali, HUTAPITIA katika ile dhiki; kwa kuwa umeikubali Damu Yangu, Neno Langu, malaika Wangu, Sauti Yangu, hivyo huna dhambi kabisa mbele Zangu.
Ninayo mambo makubwa sana niliyokutunzia. Unaliona Neno Langu likifunuliwa mbele ya macho yako kila siku. Nimekuwa nikiziweka ishara angani kukuambia wewe jambo fulani liko karibu kutukia. Ninakuja, jiandae. Liweke Neno Langu, Sauti Yangu, kuwa ya kwanza katika maisha yako.
Weka kila kitu kando, hakuna kitu kilicho muhimu zaidi kuliko Neno Langu. Najua adui anajaribu kukuangusha chini, lakini nilikuahidi nitakuinua. Mimi nipo pamoja nawe, hata NDANI YAKO. Wewe na Mimi tunakuwa Mmoja ninapokufunulia Neno Langu. Unajua moyoni mwako, wewe ndiwe Bibi-arusi Malkia Wangu. Unajua nilikuchagua tangu awali. Unajua Nakupenda. Unajua Niko pamoja nawe kila sekunde ya kila siku. Unajua SITAKUACHA KAMWE.
Tutakuwa na wakati mzuri sana pindi Ninapokufunulia zaidi kila Jumapili, kila siku, unaponisikia Mimi nikinena kila Jumapili, Nikinena nawe kupitia malaika Wangu. Huenda wengine wasielewe au kuona kile wewe unachokiona, lakini Imetia nanga ndani ya moyo wako kwamba hii ndiyo Njia Yangu niliyoiandaa.
Ni kimbilio lililoje nililokuwekea. Unaweza kwa urahisi tu Bonyeza Play wakati wowote, mchana au usiku, kunisikia Mimi nikinena nawe. Nitailetea faraja nafsi yako wakati ninapolifunua Neno Langu na kukuambia wewe ni nani. Kila Ujumbe ni kwa ajili yako, na kwa ajili yako peke yako. Tunaweza kushiriki na kuabudu pamoja wakati wowote unapotaka.
Jumapili saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville, (Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) sehemu ya Bibi-arusi itakusanyika kutoka ulimwenguni kote kuzisikia siri hizi kuu zikifunuliwa. Ninawaalika mje mkaungane nasi tunaposikia, 63-0318 – “Muhuri Wa Kwanza”.
Ndugu. Joseph
Maandiko ya kusoma kwa ajili ya maandalizi ya kusikiliza Ujumbe:
Sichoki kamwe kuisikia Sauti ya Mungu ikituambia sisi ni nani, wapi tunatoka, wapi tunakwenda, sisi ni warithi wa nini, na jinsi gani Yeye anavyotupenda.
Ukuhani wa kiroho, taifa la kifalme, wanaomtolea Mungu dhabihu za kiroho, matunda ya midomo yao, wakilisifu Jina Lake.” Ni watu wa—wa ajabu jinsi gani! Yeye anao.
Faraja na amani yetu pekee huja kwa kuisikia Sauti ya Mungu ikinena nasi, kisha tunamjibu Baba kwa kutoa dhabihu za kiroho kwa matunda ya midomo yetu, tukilisifu Jina Lake.
Ulimwengu wote huu unaugua. Maumbile yanaugua. Tunaugua na kungojea kule kuja kwa Bwana. Dunia hii haina kitu kwetu sisi. Tuko tayari kuondoka na kwenda kwenye Karamu yetu ya Arusi na Makao ya Baadaye pamoja Naye na wale wote ambao tayari wako Huko, ng’ambo tu ya pazia la wakati, wakitungojea.
Hebu na tuamke na tujitikise! Tufinye dhamiri zetu, tuamke kwa kile kinachoendelea sasa hivi na kile kinachoenda kutukia katika dakika moja kufumba na kufumbua jicho.
Kamwe katika historia ya ulimwengu haijawahi kuwezekana kwa Bibi-arusi wa Kristo kuungana kutoka ulimwenguni kote, wote kwa wakati ule ule mmoja, kuisikia Sauti ya Mungu ikinena na kulifunua Neno Lake kwa Bibi-arusi Wake.
Enyi Waaminio, jiulizeni wenyewe, ni sauti gani, mhudumu gani, ni mtu gani anayeweza kumuunganisha na kumkusanya Bibi-arusi wa Kristo wote pamoja? Kama wewe ni Bibi-arusi wa Kristo, unajua kwa urahisi hakuna kabisa Sauti nyingine ila Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda.
Ndiyo, Roho Mtakatifu yu ndani ya kila mmoja wetu, kila ofisi ya kanisa, lakini Mungu Mwenyewe alituambia angeuhukumu ulimwengu kwa Neno Lake. Bibi-arusi anajua Neno Lake huja kwa nabii Wake. Nabii Wake ndiye mfasiri PEKEE wa Kiungu wa Neno Lake. Kile asemacho hakiwezi kuongezewa lolote wala kuondolewa kitu. Ni Neno, lililo kwenye kanda, ndilo sisi sote tutakalohukumiwa kwalo, na wala si neno lingine ama fasiri ya Neno hilo.
Haiwezekani kwa sauti nyingine yoyote kumuunganisha Bibi-arusi. Ni Sauti ya Mungu peke yake iliyo kwenye kanda ndio inayoweza kumuunganisha Bibi-arusi Wake. Ndilo Neno pekee ambalo Bibi-arusi wanaloweza kukubaliana kwalo. Ndio Sauti pekee ambayo Mungu Mwenyewe aliithibitisha kuwa Sauti Yake kwa Bibi-arusi Wake. Bibi-arusi Wake lazima awe katika Nia Moja na Moyo Mmoja ili kuwa pamoja Naye.
Wahudumu wanaweza kuhudumu, waalimu wanaweza kufundisha, wachungaji wanaweza kuchunga, lakini Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda lazima iwe ndio Sauti iliyo muhimu zaidi wanayopaswa kuiweka mbele ya watu. Ndio Yakini ya Bibi-arusi.
Ikiwa unao Ufunuo wa jambo hilo, basi hiki ndicho kitakachoenda kutukia.
Neno linatuambia Adamu alipoteza urithi wake, dunia. Ulitoka mkononi mwake ukaenda kwa yule aliyemwuzia, Shetani. Aliuza imani yake katika Mungu, akachukua hoja za Shetani. Akapoteza kila kitu kikaenda kwenye mikono ya Shetani. Aliutoa mkononi mwake akampa Shetani.
Mungu ni Mungu wa ulimwengu, kila mahali. Lakini mwanawe alikuwa na mamlaka juu ya dunia hii. Angeweza kunena, aliweza kutoa majina, aliweza kusema, aliweza kusimamisha maumbile, aliweza kufanya lo lote alilotaka kufanya. Alikuwa na mamlaka makamilifu juu ya dunia.
Adamu alipoteza yote, lakini utukufu kwa Mungu, yote yeye aliyopoteza na kuachilia yamekombolewa na Mkombozi wetu aliye Jamaa wa Karibu, si mwingine ila Mungu Mwenyezi, ambaye alifanyika Imanueli, mmoja wetu. SASA, NI YETU.
Sisi ni wana na binti Zake watakaotawala na kuwa wafalme na makuhani pamoja Naye. Tunao uzima wa milele pamoja Naye na wale wote tuwapendao. Hakuna magonjwa tena, hakuna huzuni tena, hakuna kifo tena, yote ni milele tu pamoja.
Tunapoliwazia hilo, tunawezaje kumwacha shetani atushushe? Ni YETU, huko ndiko tunakoelekea hivi karibuni. Yeye ametupa jambo lililo kuu zaidi awezalo kutupa. Siku hizi chache za mitihani na majaribu hapa duniani zinamezwa kwa haraka na USHINDI wetu MKUU ULIO SIKU CHACHE TU ZIJAZO MBELE YETU.
IMANI yetu haijawahi kuwa kubwa jinsi hii. Furaha yetu haijawahi kuwa juu jinsi hii. Tunajua sisi ni nani na ni wapi tunakoenda. Tunajua tuko katika Mapenzi Yake makamilifu kwa kudumu na Neno Lake. Yote tunayohitaji kufanya ni kudumu na kanda na kuamini kila Neno; si kulielewa lote, BALI KUAMINI KILA NENO…nasi TUNAAMINI!
Imani huja kwa kusikia, kulisikia Neno. Neno huja kwa nabii. Mungu alilinena Hilo. Mungu alilirekodi Hilo. Mungu alilifunua Hilo. Tunalisikia Hilo. Tunaliamini Hilo.
Unaweza tu kuupata Ufunuo huu kwa kuisikia Sauti ya Mungu kwenye kanda.
“Yote yale ambayo Kristo atafanya wakati wa mwisho yatafunuliwa kwetu juma hili, katika ile Mihuri Saba, kama Mungu ataturuhusu. Unaona? Vema. Yatafunuliwa. Na kufunuliwa, wakati Mihuri hii inapovunjwa na kufunguliwa kwetu, ndipo tunaweza kuona mpango huu mkubwa wa ukombozi ulivyo, na ni lini na ni vipi utafanyika. Yote yamefichwa katika Kitabu hiki cha siri hapa. Kimetiwa muhuri, kimefungwa kwa Mihuri Saba, na kwa hiyo Mwana-Kondoo Ndiye pekee Ambaye anaweza kuivunja.
Jumapili hii saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville, (Ni Saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki) sehemu ya Bibi-arusi kutoka ulimwenguni kote watakuwa wakiisikiliza Sauti ya Mungu wote kwa wakati mmoja. Tutakuwa tukiivumisha mbingu kwa maombi yetu na kumwabudu. Ninawaalika mje muungane nasi tunaposikia: Pengo Kati ya Nyakati Saba za Kanisa na ile Mihuri Saba 63-0317E.
Tafadhali msisahau kuhusu mabadiliko ya masaa huko Jeffersonville wikendi hii.
Mnamo tarehe 28, mwezi Februari, 1963, Ilinguruma. Whiu-whiiiu, Malaika Saba walikuja kutoka umilele nao wakamtokea Malaika-mjumbe wa Saba wa Mungu. Alinyakuliwa katika piramidi ya lile kundi. Kisha, wingu la kimbinguni likatokea angani juu ya Arizona. Ilikuwa ni ishara, Mungu alikuwa akimtuma malaika Wake wa saba arudi Jeffersonville ili kuifungua ile Mihuri Saba.
Tarehe 28 mwezi Februari, 2025, sayari saba zajipanga mstari angani. Bibi-arusi anajiweka mwenyewe tayari kukusanyika na kuisikia ile Mihuri Saba.
Unaalikwa, na Bwana Mwenyewe, kukusanyika pamoja na Bibi-arusi kutoka ulimwenguni kote, kuisikia Sauti ya Mungu ikifunua Ufunuo wa ile Mihuri Saba.
Ile siku ambayo manabii na wenye hekima waliitamani na kuingojea tangu mwanzo wa wakati, inatukia. Yule malaika mwenye nguvu ambaye Mungu alisema angemtuma duniani katika siku za mwisho amekuja kufungua na kuzifunua siri za Mungu zilizofichwa, ili Bwana wetu Yesu aweze kurudi kwa ajili ya Bibi-arusi Wake mwaminifu na kutupeleka kwenye Karamu yetu ya Arusi.
Wajibu wangu wa kwanza, nilipokuwa ninakuja kwenye kanisa hili jipya, niliwaunganisha katika ndoa kijana mwanamume na mwanamke wakiwa wamesimama ofisini. Na iwe ni mfano, ya kwamba nitakuwa mhudumu mwaminifu kwa Kristo, kumtayarishia Bibi-arusi kwa ajili ya sherehe ya Siku hiyo.
Leo hii, Neno hili limetimia. Mungu ananena kupitia malaika Wake, akimtayarisha Bibi-arusi Wake kwa ajili ya sherehe ya Siku hiyo. Tunafuata maagizo yake vilivyo kabisa. Bibi-arusi amejiweka mwenyewe tayari kwa KUDUMU NA SAUTI YA MUNGU ILIYO KWENYE KANDA.
Tumesikia kitu gani kwa ndoto na maono? Kile Chakula, HIKI HAPA, mahali penyewe ni hapa. Sauti ikamwambia, “Lete Chakula. Kihifadhi mle ndani. Hiyo ndiyo njia pekee ya kuwaweka hapa, ni kuwapa Chakula.”
Wengi wanaamini kwamba yeye anamaanisha tu, “dumuni tu na Neno,” na hiyo NI KWELI, anasema hivyo; lakini Bibi-arusi pia atasoma katikati ya mistari wakati Bwana-arusi anazungumza na Bibi-arusi Wake.
Hata yale maono ambayo Mungu anayaonyesha hapa mahali hapa, yanafahamika vibaya sana. Hiyo ndiyo sababu mnanisikia mimi kwenye kanda, nikisema, “Sema vile kanda zinavyosema. Sema vile maono yanavyosema.” Sasa, kama mko macho kabisa, mtaona kitu fulani. Mnaona? Natumaini si lazima nikishike mkononi mwangu na kuwaonyesheni.”
Hata maono yalieleweka vibaya, hata baada ya yeye kuwapa fasiri. Hilo ndilo yeye alilokuwa akituambia, ikiwa hutaki kupata mkanganyiko, au kuelewa vibaya, Bonyeza Play na usikie kile hasa Sauti ya Mungu inachosema.
Najua Neno lina maana zaidi ya moja, lakini hii ndiyo fasiri yangu: Ndoto na maono yote yalisema kitu kile kile; dumuni na kanda. Kama una swali, nenda kwenye kanda. Kanda hizo ni Chakula cha Mungu kilichohifadhiwa. Sema tu kile kilicho kwenye kanda; usiongeze chochote Kwake. Kanda hizo ni Bwana Asema Hivi kwa Bibi-arusi. Neno humjia nabii, peke yake. Nabii ndiye mfasiri PEKEE wa Kiungu wa Neno. Nabii alikuwa ndiye wa kumwita Bibi-arusi atoke na kumwongoza. Nitahukumiwa kwa kile kilichonenwa kwenye KANDA.
Kila kitu kinanielekeza kwenye KANDA.
Wapendwa wangu Mayungiyungi ya Kidimbwi, kwangu mimi, KUBONYEZA PLAY NDIO MUNGU KWA URAHISI KWA AJILI YA LEO HII.
Kila wiki napata changamko sana; ni kitu gani kinachoenda kufunuliwa leo wakati Bibi-arusi Wake atakapokusanyika ili kuusikia Ujumbe? Ninajua Roho Mtakatifu atakuwa akimtia mafuta kila mmoja wetu anapolifunua Neno Lake kuliko hapo awali. Ninahisi, wakati wowote tu, Yeye atakuja na kututwaa kwenda kwenye Karamu yetu ya Arusi.
Sisi ni, wana na binti za Mungu. Sisi ni, uzao uliotoka kwa Mungu. Sisi ni, urithi wa dunia. Tutatawala maumbile. Tutanena na iwe. Sisi ni Bibi-arusi!
Hebu na tujiweke wakfu upya kwa ajili ya kazi, na tujiweke wakfu kwa Kristo.”
Ndugu. Joseph Branham
Tarehe: 2 Machi, 2025
Ujumbe: Mungu Akijificha Kwa Urahisi, Halafu Akijifunua Kwa Jinsi Hiyo 63-0317M
Muda: saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville.(Ni saa 2 MBILI USIKU ya Afrika Mashariki)
Hii ndiyo, Ishara. Huu ndio, wakati wenyewe. Huu ndio, Ujumbe. Hili ndilo, Neno. Hii ndio, Sauti ya Mungu. Huyu ndiye, Mwana wa Adamu. Hii ndio, njia ya Mungu iliyoandaliwa. Huu ndio, mwisho wa wakati.
Hakuna nabii, hakuna mtume, kamwe, katika wakati wowote, aliyewahi kuishi katika wakati kama huu tunaoishi sasa. Imeandikwa mbinguni. Imeandikwa juu ya uso wa dunia. Imeandikwa katika kila gazeti. Huu ndio mwisho, ikiwa unaweza kusoma maandishi ya mkono.
Yeye aliye na sikio, na asikie yale Mungu aliyonena, na aliyorekodi, ili lisiwe neno langu, mawazo yangu, wazo langu, bali Sauti ya Mungu yenyewe ikimuelekeza Bibi-arusi Wake ni ipi njia Yake PEKEE kamilifu iliyoandaliwa kwa ajili ya siku hii.
Njoo usikilize anapotuambia na kutufunulia kwa maandiko, kwa maono, kwa fasiri ya ndoto, kudumu na Ujumbe, kudumu na kanda. Sema TU kilicho kwenye kanda.
Hakuna njia iliyo bora, wala njia iliyo ya hakika, kuliko kuisikia Sauti ya Mungu kutoka kwa Mungu Mwenyewe. Mungu alimwamuru Bibi-arusi Wake kwa kunena kupitia nabii Wake na kutuambia, BONYEZA PLAY, kwisha.
Linene Hilo, lihubiri Hilo, lishuhudie Hilo, na uuambie ulimwengu kuhusu Hilo, bali Yeye anatuambia kuna njia moja tu kamilifu iliyoandaliwa ya kumkamilisha Bibi-arusi: sikilizeni Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda. Ikiwa jambo fulani linakutatiza, cheza kanda. Ni lazima iwe ndio ya KWANZA, na Sauti iliyo muhimu zaidi ikupasayo kuisikia. Ndilo Neno Lake kamilifu aliloliweka kwenye kanda.
“Sasa linganisha hilo na zile nyingine, zile ndoto. Hili lilikuwa ono. Kile Chakula; Hiki hapa. Mahali penyewe ni hapa.
Sikiliza, kwa ndoto na maono, Chakula cha Bibi-arusi kiko wapi? Mahali penyewe ni wapi? Ujumbe wa Bibi-arusi uko kwenye kanda.
“Ninajisikia nyumbani hapa. Hapa ndipo panapofaa. Na kama ukiangalia, ndoto ile ilizungumzia jambo lile lile. Unaona, kilipo Chakula.
Ili kuhakikisha tumelipata, anatuambia kwa mara nyingine tena, kanda hizo ndicho Chakula cha Bibi-arusi.
“Wakati umekwisha.” Kama ndivyo ilivyo, hebu na tujiandae, marafiki, kumlaki Mungu wetu.
Naam, Bwana, hiyo ndiyo shauku ya mioyo yetu, ni kuwa tayari kukulaki Wewe, kuwa Bibi-arusi Wako. Tufanye nini Bwana? Njia Yako iliyoandaliwa ni ipi? Mpango Wako ni upi? Njia Yako kamilifu ni ipi? Ulitutumia nabii ambaye Ungeweza kunena kupitia yeye kutuambia sisi. Tafadhali tuelekeze.
“Kumekwisha wekwa chakula kingi sana sasa; hebu na tukitumie. Hebu na tukitumie sasa.
Mtu anawezaje kuwa kipofu? Yeye anatuambia nini cha kufanya: kuna chakula kingi sana kilichohifadhiwa kwenye kanda; kitumieni SASA. Haya ndio maagizo ya Mungu kwa Bibi-arusi Wake.
Ikiwa unadai unauamini Ujumbe huu, amini William Marrion Branham ndiye nabii-mjumbe wa Mungu aliyetumwa kumwita Bibi-arusi atoke; maisha yake yanatimiza maandiko yote yaliyonenwa kumhusu yeye; amini ndio Sauti ya Mungu ya siku hii, basi YEYE; Mungu, akinena kupitia nabii Wake, anamwambia Bibi-arusi kwa Kiingereza kilicho wazi nini cha kufanya.
Ingawa tunadhihakiwa, tunateswa, na kudharauliwa kwa sababu tu tunasikiliza kanda, tunafanya yale hasa Yeye aliyotuambia sisi tufanye. Asante Bwana kwa Ufunuo.
Ninataka kuualika ulimwengu mzima kuungana nasi Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni saa 2 MBILI USIKU ya Afrika Mashariki), wakati tunaposikia: “Hii Ndiyo Ishara ya Mwisho, Bwana?” Tutasikia kila kitu kuhusu:
Ngurumo, Mihuri Saba, Mwamba wa Piramidi, Chakula cha Kiroho, Umilele, Kundi la Malaika, Makao Makuu Yangu, Ono, Ndoto, Unabii, Siri Zilizofichwa, Andiko baada ya Andiko.
Hakuna jambo lililo kuu katika maisha haya kuliko kuisikia na kuitii Sauti ya Mungu.
Ndugu. Joseph Branham
Maandiko:
Malaki Sura ya 4 Mathayo 13:3-50 Warumi 9:33 / 11:25 / 16:25 1 Wakorintho 14:8 / Sura ya 15 Wagalatia 2:20 Waefeso 3:1-11 / 6:19/ 5:28-32 Wakolosai 4:3 1 Wathesalonike 4:14-17 1 Timotheo 3:16 Waebrania 13:8 2 Petro 2:6 Ufunuo 1:20 / 3:14 / 5:1 / 6:1 / 10:1-7 / Sura ya 17
Kuna msisimko mkubwa miongoni mwa Bibi-arusi zaidi ya hapo kabla. Tuko chini ya matarajio makubwa; mwaka wetu wa yubile unakaribia kutimia. Bibi-arusi amengoja kwa muda mrefu sana siku hii ifike. Mwisho wa kipindi cha Mataifa umefika nao mwanzo wa umilele na Bwana wetu utaanza hivi karibuni.
Tunauelewa wakati tunaoishi kwa kulisikia Neno. Muda umeisha. Wakati wa Kunyakuliwa umekaribia. Tumewasili. Roho Mtakatifu amekuja na kumfunulia Bibi-arusi Wake mambo yote makuu, ya siri, yenye kilindi.
Tuko katika hali ya kudhikika, tukimtafuta Mungu; tukijiweka tayari. Tumetupilia mbali mambo yote ya ulimwengu huu. Masumbuko ya maisha haya hayamaanishi kitu kwetu. Imani yetu imefikia viwango vikuu kuliko hapo awali. Roho Mtakatifu anampa Bibi mteule Wake Imani ya kunyakuliwa, ili aweze kuja na kumchukua.
“Haya majuma sitini na tisa yametimia kikamilifu; kule kuondoka kwa Wayahudi kulitimia kikamilifu; wakati wa kanisa ulitimia kikamilifu. Tuko katika wakati wa mwisho, wakati wa kanisa la Laodikia, mwisho wake. Wale wajumbe nyota wote wamehubiri ujumbe wao. Umetangazwa. Tuko tu karibu na ukingoni.”_
Ni wakati wa kitendawili jinsi gani tunaoishi. Ni nyakati ngumu kuliko kwani adui anamshambulia kila mmoja kuliko hapo awali. Anatutupia yote aliyo nayo. Yuko katika hali ya kudhikika, kwa maana anajua wakati wake umefika mwisho.
Lakini wakati huo huo, hatukuwahi kuwa wenye furaha maishani mwetu.
° Hatukuwahi kuwa karibu zaidi na Bwana.
° Roho Mtakatifu anajaza kila kiungo cha mwili wetu.
° Upendo wetu kwa Neno Lake haujawahi kuwa mkuu zaidi.
° Ufunuo wetu wa Neno Lake hujaza nafsi zetu.
° Tunamshinda kila adui kwa Neno.
NA, hatukuwahi kuwa na hakika ya kuwa sisi ni nani:
° ALIYECHAGULIWA TANGU ZAMANI
° MTEULE
° ALIYECHAGULIWA
° UZAO WA KIFALME
° KIPENZI,
WA MILELE, ALIYEVIKWA MAVAZI MEUPE, BI. JÉZU, MSIKILIZA KANDA, ALIYEANGAZWA, BIKIRA SAFI, ALIYEJAZWA NA ROHO, ASIYESHINDWA, MWANA MWENYE MAMLAKA, ASIYEGHOSHIWA, BIBI-ARUSI NENO BIKIRA.
Kitu gani kinachofuata? Lile Jiwe linakuja. Tunakesha, tukingoja na kuomba kila dakika ya kila siku. Hakuna kitu kingine kilicho muhimu ila sisi kujitayarisha kwa ajili ya kuja Kwake.
Sio, “Tunatumai hivyo”, TUNAJUA. Hakuna mashaka tena. Katika dakika moja, katika kufumba na kufumbua jicho itakwisha, nasi tutakuwa ng’ambo ya pili pamoja na wapendwa wetu wote na YEYE kwenye Karamu yetu ya Arusi.
NA HUO NI MWANZO TU…NA HAKUNA MWISHO!!
Njoo ujitayarishe kwa ajili ya Karamu hiyo ya Arusi pamoja nasi Jumapili hii saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni saa 2 MBILI USIKU ya Afrika Mashariki) wakati Mungu anaponena kupitia malaika Wake mwenye nguvu, yule aliyemtuma kumwongoza Bibi-arusi Wake, wakati aelezapo, na kufunua, siri zote za Mungu.
Tumeelekeza nyuso zetu Mbinguni katika maombi na kusihi ili kupata siku na saa hasa tunayoishi.
Zaidi ya hapo awali, tumeketi pamoja katika ulimwengu wa roho, kutoka ulimwenguni kote, tukimsikiliza Mungu akinena na kulifunua Neno Lake kwetu kupitia malaika-mjumbe Wake mwenye nguvu. Malaika-mjumbe wa duniani ambaye Baba alimtuma kwa Bibi-arusi Wake katika siku hii ya mwisho kulifunua Neno Lake.
Gabrieli ndiye malaika kwa watu waliochaguliwa na Mungu, Wayahudi. Lakini kwa Bibi-arusi Wake Mmataifa, Melkizedeki Mwenyewe alikuja na kunena kupitia mwili wa mwanadamu katika malaika wa duniani aitwaye William Marrion Branham, ili apate kunena na kulifunua Neno Lake LOTE kwa Bibi-arusi Wake kipenzi wa moyoni.
Alilifanya lirekodiwe, lihifadhiwe, na litunzwe, ili Bibi-arusi apate Chakula Chake cha kiroho, Mana iliyofichwa, kwenye ncha ya vidole vyao kila dakika ya kila siku mpaka mwisho wa wakati.
Utu wetu wa ndani umejawa na upako kama nini wakati tunaiposikia Sauti ya Mungu ikilifunua Neno Lake kwetu. Jinsi gani Yeye anavyolifunua Neno Lake ili tuweze kuona waziwazi na kuelewa maana Yake. Linafunua saa yenyewe hasa tunayoishi, linatuambia sisi ni nani na ni nini kinachoenda kutukia hivi karibuni; Unyakuo wetu unaokuja hivi karibuni.
Yeye hata anamfunulia Bibi-arusi Wake kile kitakachokuwa kikitendeka hapa duniani wakati tuwapo pamoja Naye kwenye Karamu ya Arusi. Jinsi ambavyo Yeye atakavyoyafungua macho yaliyopofushwa ya wateule Wake; wale aliowapofusha kwa ajili ya Bibi-arusi Wake Mmataifa.
Enyi marafiki, najua jinsi tulivyochoshwa na ulimwengu huu na tukitamani kuja kwake kutuchukua, lakini pia hebu na tufurahi na kushukuru kwa yale yanayotukia hivi sasa mbele ya yaya haya macho yetu.
Hebu na tuinue mikono yetu, mioyo yetu, sauti zetu, na kufurahi. Sio tu kwamba tunatazamia yale ambayo anayoenda kututendea hivi karibuni, lakini hebu na tufurahi juu ya yale anayotufunulia na kututendea hivi SASA.
Yeye anatuambia sisi ni Bibi-arusi Wake aliyechaguliwa tangu asili tukiungana pamoja Naye na Neno Lake. Anatuhakikishia tena na tena, tuko katika Mapenzi Yake makamilifu kwa sisi kukaa na Sauti Yake, Neno Lake, malaika Wake. Ametupa IMANI ya kujua na kujitambua sisi ni nani: NENO LAKE LIISHILO KATIKA MWILI.
Hatuna cha kuogopa; Hakuna cha kuhofia, hakuna cha kujihuzunisha nacho; Ninalijuaje hilo? MUNGU ALISEMA HIVYO! KWA HIYO HEBU NA TUSHANGILIE, TUFURAHI, TUWE NA SHUKRANI; NENO LILILO HAI LINAISHI NA KUKAA NDANI YETU. SISI NDIO UZAO WAKE MKUU WA KIFALME.
Ninaamini kweli Bwana lazima atakuwa pia amechangamshwa sana kujua kwamba wakati umefika nasi tumejiweka wenyewe tayari kwa kudumu wa kweli na waaminifu kwa Neno Lake.
Kama yule mvulana mdogo aliyejitazama kwenye kioo kwa mara yake ya kwanza, tunatazama katika Neno Lake, tukiona sisi NI NANI. Bwana…NI MIMI. Mimi ndiye Bibi-arusi Neno lililo hai Wako. Mimi ndiye uliyemchagua WEWE. Mimi niko ndani Yako, Wewe U ndani yangu, sisi ni Mmoja.
Tunawezaje kutosherehekea na kuwa watu wenye furaha kuliko wote waliowahi kuishi kwenye uso wa dunia? Watakatifu na manabii wote waliotutangulia walitaka kuishi katika siku hii na kuziona ahadi hizi zikishika kasi. Lakini kwa NEEMA ya Mungu,Yeye alituweka SISI hapa.
Tunasubiri kwa hamu:
Brrrr! Loo, jamani! Whiu! Kwa maneno mengine, wakati adui atakapokuwa ameondolewa, mwisho wa dhambi umekuja, kuletwa kwa haki ya milele kumekuja, Shetani amefungiwa kuzimuni, na maarifa ya Bwana yataijaza dunia kama maji yaifunikavyo bahari. Amina! Mungu atukuzwe! Linakuja, ndugu, linakuja!
Ni upako wa namna gani utakaotendeka Jumapili saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni saa 2 MBILI USIKU ya Afrika Mashariki) tunapokusanyika pamoja kutoka ulimwenguni kote kumsikia malaika wa Mungu, Sauti ya Mungu kwa Bibi-arusi, akituletea Ujumbe: Sababu Sita Za Kusudi La Gabrieli Kumzuru Danieli 61-0730E.