All posts by admin5

24-1110 Wakati Wa Kanisa La Thiatira

UJUMBE: 60-1208 Wakati Wa Kanisa La Thiatira

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi Aliyeangaziwa,

Jinsi ambavyo Bwana anavyotufunulia kwamba katika nyakati zote kumekuwa na kundi dogo sana ambalo lilidumu na Neno Lake. Wao hawakuanguka katika mtego wa udanganyifu wa adui, bali walibaki wa kweli na waaminifu kwa Neno la siku yao.

Lakini hakujawahi kuwa na wakati, au kundi la watu, ambalo Bwana amekuwa akijivunia, au kuwa na imani zaidi nalo, kuliko sisi. Sisi ndio Bibi-arusi Bibi Mteule Wake ambaye hatadanganywa, na hata muhimu zaidi HATUWEZI, kudanganywa; kwa maana sisi tunaisikia Sauti ya Mchungaji na kumfuata.

Yeye anatuonyesha kwamba katika nyakati zote kumekuwa na makundi mawili ya watu, yote yakidai ufunuo wao kutoka kwa Mungu na uhusiano wao na Mungu. Lakini alituambia, Bwana awajua walio Wake. Anafuatilia mawazo yetu. Yeye anajua kilicho mioyoni mwetu. Yeye anaziona kazi zetu kwa kudumu na nabii na Neno Lake, ambayo ni madhihirisho dhahiri ya yale yaliyo ndani yetu. Madhumuni yetu, makusudi yetu yanajulikana Kwake kwa kuwa Yeye hulichunguza kila tendo letu.

Yeye anatuambia kwamba ahadi zote alizozitoa kwa kila wakati, ni ZETU. Anatuona sisi tunaoendelea kutenda kazi Zake kwa uaminifu hata mwisho. Yeye AMETUPA SISI mamlaka juu ya mataifa. Anatuambia sisi ni viongozi wenye nguvu, hodari, shupavu ambao wanaweza kukabiliana vizuri sana na hali yo yote. Hata adui aliye mbaya sana atavunjwa kama kukiweko na haja. Dhihirisho letu la kutawala kwa mamlaka Yake litakuwa kama lile lile la Mwanawe. UTUKUFU!!

Tumepata ujuzi wa kina cha Mungu katika maisha yetu. Ni tukio la kibinafsi la Roho wa Mungu akiishi ndani yetu. Nia zetu zinaangazwa na hekima na maarifa ya Mungu kwa kupitia Neno Lake.

Sisi tunaenda po pote Bwana-arusi alipo. Hatutaachwa Naye kamwe. Hatutaondoka ubavuni Mwake. Tutashiriki kiti cha enzi pamoja Naye. Tutatiwa taji kwa utukufu na sifa Zake.

Yeye ametufunulia jinsi gani ambavyo adui amekuwa mdanganyifu katika kila wakati na jinsi ilivyo muhimu KUDUMU NA NENO LAKE LA ASILI. Hakuna Neno moja linaloweza kubadilishwa. Kila wakati waliongeza kwake na kuondoa kutoka kwake, wakiweka fasiri yao wenyewe kwenye Neno la asili; nao wanapotea milele kwa kufanya hivyo.

Katika Wakati wa Kanisa la Thiatira, hiyo roho ya udanganyifu ilinena kupitia papa wa Rumi na kulibadilisha Neno Lake. Alilifanya kuwa “mpatanishi mmoja kati ya Mungu na mwanadamu (si wanadamu).” Kwa hiyo sasa yeye anapatanisha kati ya mpatanishi na wanadamu. Hivyo, mpango wote wa Mungu ulibadilishwa; si kwa kubadili neno, bali kwa kubadili HERUFI MOJA. Shetani alikuwa amebadilisha “E” kuwa “A”.

Kila Neno litahukumiwa kwa Neno Lake la Asili lililonenwa kwenye kanda. Kwa hiyo, Bibi-arusi Wake LAZIMA adumu na kanda. Wakati adui anajaribu kuwakatisha tamaa watu kwa kuwapa mpango tofauti, wazo tofauti, herufi tofauti, Bibi-arusi ATADUMU NA NENO LA ASILI.

Katika kila wakati Yesu anajitambulisha Mwenyewe na mjumbe wa wakati huo. Wao wanapokea kutoka Kwake ufunuo juu ya Neno kwa ajili ya wakati wao. Ufunuo huu wa Neno huwaleta wateule wa Mungu kutoka katika ulimwengu na waingie katika muungano mkamilifu na Yesu Kristo.

Yeye amewaita na kuwaweka wakfu watu wengi ili wawe baraka kwa kanisa, lakini Yeye ana ila MJUMBE MMOJA TU ambaye Yeye alimuita ili KULIONGOZA kanisa Lake kwa Roho Wake Mtakatifu. Kuna SAUTI MOJA yenye Bwana Asema Hivi. Kuna SAUTI MOJA ambayo Yeye alisema atatuhukumu kwayo. Kuna SAUTI MOJA ambayo Bibi-arusi Wake wameweka kikomo chao cha Milele. SAUTI HIYO NI SAUTI YA MUNGU ILIYO KWENYE KANDA.

Bibi-arusi, Mapenzi ya Mungu kwetu ni Ukamilifu, na mbele zake, sisi NI WAKAMILIFU. Na huo ukamilifu ni subira, kumngojea Mungu… na kumngoja Mungu. Anatuambia ni njia ya kuumba tabia zetu. Tunaweza kuwa na mitihani, majaribu na dhiki nyingi, lakini uaminifu wako kwa Neno Lake unafanya subira ndani yetu ili tuwe wakamilifu na watimilifu, bila kupungukiwa na neno.

Hatutasahau kamwe IMANI huja kwa kusikia, kusikia Neno, nalo Neno huja kwa nabii.

Njoo ujionee furaha kuu ya maisha yako unapoketi pamoja nasi katika Mahali pa Mbinguni tunapoisikia Sauti ya Mungu ikituletea Neno juu ya: Wakati wa Kanisa la Thiatira 60-1208, saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville.(Ni Saa 2:00 MBILI USIKU ya Afrika Mashariki)

Ndugu. Joseph Branham

24-1103 Wakati Wa Kanisa La Pergamo

UJUMBE: 60-1207 Wakati Wa Kanisa La Pergamo

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi Bikira Safi,

Je! Mmekuwa mkifurahia Nyakati Saba za Kanisa? Mungu anampa Bibi-arusi Wake ufufuo kuliko hapo awali. Yeye anatupa Ufunuo zaidi, Imani zaidi, na hakikisho zaidi kujua sisi ni nani, na kile tunachofanya kwa kukaa na Neno, Njia Yake aliyoiandaa kwa ajili ya siku hii.

Sasa Yeye anatuambia: “Kuanzia ibada ya Jumapili na kuendelea, vaeni mawazo yenu ya kiroho. Acha Roho Mtakatifu alizamishe Hilo ndani na myashike matumizi ya kiroho katika yote nitakayofanya. Ni Neno Langu lililohuishwa na Roho lililonenwa na nabii Wangu wa Malaki 4.”

Hebu na tusome na tuyapate machache ya Maneno Yake nasi tutumie mawazo yetu ya kiroho kuyahusu.

Mungu alimweka kiongozi Wake aliyejazwa Roho kwa ajili ya kundi Lake lililojazwa na Roho; malaika Wake; Naye akatia juu yake muhuri wa jina, bali haimpasi kulifunua. Hapaswi kumwambia mtu, mnaona. “Hakuna mtu ajuaye ila yeye mwenyewe.”

Kwa hiyo Mungu alimpa Bibi-arusi Wake kiongozi aliyejazwa na Roho kwa ajili ya kundi Lake lililojazwa na Roho. KIONGOZI, SIO VIONGOZI kwa ajili ya kundi Lake lililojazwa na Roho.

Anayekuja ulimwenguni hivi karibuni, yule malaika mkuu wa Nuru atakayetujia, atakayetuongoza tutoke, Roho Mtakatifu mkuu, akija mamlakani, naye atatuongoza kwa Bwana Yesu Kristo.

Malaika mkuu wa Nuru. Malaika mkuu wa Nuru ni nani kwa wakati huu wa mwisho? William Marrion Branham. Yeye hazungumzi juu ya Roho Mtakatifu. Yeye tayari amekwishakuja naye anasema atakayekuja.

Atakaye TUONGOZA TUTOKE. Kwa kweli tunajua na kuamini kwamba ni Roho Mtakatifu anayetuongoza, lakini Yeye ameweka wazi malaika Wake na Roho Mtakatifu pamoja na kusema Yeye (Roho Mtakatifu Wake) atakuwa akituongoza (KUPITIA) malaika Wake mkuu wa Nuru.

Yeye anaendelea kuwaunganisha pamoja kwa kusema:

Labda hatajua hilo,

Yeye hasemi Roho Mtakatifu hatamjua ni nani, bali malaika-mjumbe Wake wa duniani yule ambaye Yeye amemchagua KUTUONGOZA TUTOKE.

Bali atakuwa hapa moja ya siku hizi. Atafanya… Mungu atamtambulisha. Haitambidi kujitambulisha mwenyewe, Mungu atamtambulisha. Mungu atamthibitisha aliye Wake.

Tena, Yeye hasemi Roho Mtakatifu atakuwa hapa MOJA YA SIKU HIZI, bali malaika Wake mkuu wa Nuru ili kumwongoza Bibi-arusi Wake. Haitambidi kujitambulisha mwenyewe, Mungu atamtambulisha kiongozi Wake mkuu kwa Bibi-arusi Wake Mwenyewe kwa UFUNUO.

Je, umeyashika matumizi ya kiroho? Je! unaona malaika wa Nuru ni nani ambaye Mungu alimchagua kumwongoza Bibi-arusi Wake? Je! Inasema hapa ati kijiti kimepokezwa viongozi wengine?

Kamwe hutaweza kuishi juu zaidi ya mchungaji wako. Kumbuka hilo tu, unaona.

Ingawa wengine wanaweza wasituelewe na kutudhihaki, jinsi sisi tunavyofurahi na tunavyoshukuru kweli kwa Ufunuo kusema, WILLIAM MARRION BRANHAM NDIYE MCHUNGAJI WETU.

Sasa kwa kuwa kila moja ya jumbe hizi umeelekezwa kwa ‘malaika’—(mjumbe wa kibinadamu) wajibu mkubwa sana na pia majaliwa makuu sana ni fungu lake.

Ujumbe ulielekezwa kwa malaika Wake, kisha malaika Wake anampa huo Bibi-arusi; si wahudumu tu, bali kwa BIBI-ARUSI WAKE WOTE Nao upo kwenye kanda kwa wote kuusikia. Hauwezi kuongezwa kwake au kuondolewa kitu kwake, Nao HAUHITAJI FASIRI YO YOTE.

“Hivi karibuni Yeye atakuja. Na atakapokuja, Yeye atakuja kwako kwanza. Nawe utahukumiwa kulingana na Injili uliyohubiri, nasi tutakuwa raia wako.” Nikasema, “Wataka kusema ninawajibika kwa hawa wote?” Akasema, “Sisi sote. Wewe ulizaliwa kiongozi.”

Wakati siku ile kuu ya hukumu itakapokuja, Yeye anakuja kwanza kwa malaika Wake wa Nuru naye atamhukumu yeye kwanza kulingana na injili aliyohubiri. Sisi ni RAIA WAKE. Yeye anawajibika kwa kila mmoja wetu kwa kuwa yeye alikuwa KIONGOZI aliyechaguliwa na Mungu.

Weka matumizi yako ya kiroho kwenye jambo hilo. Tutahukumiwa kwa yale ambayo malaika wa Mungu aliyosema. Kwa hiyo, unataka kubahatisha kuhusu uzima wako wa milele kwa kile mtu fulani anachosema ALISEMA wakati wewe unaweza kusikia moja kwa moja kutoka KWAKE?

Anawezaje mtu yeyote kuamini kuwa kuna HUDUMA MUHIMU KULIKO ILE ILIYO KWENYE KANDA. Ikiwa unaamini hivyo, au umeshawishiwa hivyo kwa hoja, ni afadhali urudi kwenye NENO LA ASILI; kwa maana utahukumiwa kwa maneno yaliyo kwenye kanda. Dumu na Neno kama vile Lilivyonenwa.

Lakini huyu nabii atakuja, na kama vile yule mtangulizi wa kule kuja kwa kwanza alivyopaza sauti, “Tazama Mwana-Kondoo wa Mungu aichukuaye dhambi ya ulimwengu,” vivyo hivyo bila shaka naye atapaza sauti, “Tazama Mwana-Kondoo wa Mungu anayekuja katika utukufu.” Atafanya jambo hili, kwa maana kama vile Yohana alivyokuwa mjumbe wa ile kweli kwa wateule, ndivyo alivyo na huyu mjumbe wa mwisho kwa wateule na kwa bibi-arusi aliyezaliwa kwa Neno.

Ni nani atakayetutambulisha kwa Bwana Yesu? Malaika Wake mkuu wa Nuru, William Marrion Branham.

Njoo uwe Bibi-arusi Bikira Safi pamoja nasi tunapomsikia malaika-mjumbe Wake mkuu akituletea Ufunuo zaidi, Jumapili saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni saa 2:00 MBILI USIKU ya Afrika Mashariki) tunaposikia Ujumbe 60-1207 – “Wakati wa Kanisa la Pergamo.”

Ndugu. Joseph Branham

24-1027 Wakati Wa Kanisa La Smirna

UJUMBE: 60-1206 Wakati Wa Kanisa La Smirna

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi Aliyejazwa Roho,

Kuna kundi moja tu la watu; kundi maalum sana la watu, ambao wanaweza kusikia yale Roho anayosema katika wakati huu wa mwisho. Ni kundi maalum ambalo limeupokea Ufunuo wa wakati huu. Kundi hilo ni la Mungu. Kundi lile ambalo haliwezi kusikia, si la Mungu.

Kundi ambalo linaweza, na linasikia yale Roho anayosema, linapokea Ufunuo wa Kweli. Sisi ndio hao walio na Roho wa Mungu. Sisi ndio hao waliozaliwa na Mungu na kubatizwa kwa Roho Mtakatifu. Sisi ndio Bibi-arusi Wake Aliyejazwa Roho ambaye ameupokea Ufunuo kwa ajili ya wakati wetu.

Inamaanisha nini kwetu sisi Kubonyeza Play? UFUNUO! Ni kusikia, kupokea na kukaa na Njia ya Mungu iliyoandaliwa kwa ajili ya siku hii. Sauti ya Mungu mwenyewe ikinena mdomo kwa sikio na Bibi-arusi Wake. Ni Roho Mtakatifu akizungumza na mioyo na nafsi zetu.

Tunajua Mungu huwatumia watu waliotiwa mafuta na Roho wake kunena, lakini hakuna mahali pengine pa kuisikia Bwana Asema Hivi isipokuwa kwa Kubonyeza Play na kuisikia SAUTI ya malaika wake wa saba, William Marrion Branham. Ndiyo Sauti pekee iliyothibitishwa na Roho Mtakatifu Mwenyewe. Yeye ndiye Sauti ya Mungu, nabii wa Mungu, mchungaji wa Mungu, kwetu sisi, na kwa ulimwengu mzima.

Wakati Yeye anaponena, sisi tunasema AMINA kwa kila Neno; kwa maana ni Mungu mwenyewe anayesema nasi. Neno Lake ndilo Neno pekee lisilohitaji kufasiriwa. Ni Mungu akitumia sauti yake kuongea na Bibi-arusi Wake.

Ni Mungu mwenyewe anayetuambia, “Watoto wangu, si ninyi mlionichagua mimi, bali ni mimi niliyewachagua ninyi. Kabla hakujawa na chembe ya vumbi ya nyota; kabla hata sijajulikana kwako kuwa Mungu wako, Nilikujua. Ulikuwa Niani Mwangu, ukiwa katika Mawazo Yangu ya milele. Wewe ni Bibi-arusi Wangu halisi wa Uzao Wa Neno Lililonenwa.

Ingawa mlikuwa katika Mawazo Yangu ya milele, Sikuwadhihirisha hadi majira Yangu niliyoyakusudia na yaliyoamriwa. Kwa maana nilijua NINYI mngekuwa kundi langu maalum ambalo lingedumu na Neno Langu. Wengine wote wameshindwa, lakini Nilijua ninyi hamgeshindwa.

Ninajua ya kwamba unateswa na kudhihakiwa kwa sababu umedumu na nabii Wangu, lakini wewe ndiye Mzabibu Wangu wa Kweli ambao haujakengeuka kutoka kwenye Neno Langu, bali umedumu kuwa mkweli na mwaminifu kwa nabii Wangu ambaye hunena Maneno Yangu.

Kuna wengine wengi ambao wamefundishwa kwa uaminifu, lakini wao daima hawajifunzi jinsi ilivyo jambo muhimu kusema yale tu Mimi Niliyoyanena kupitia mjumbe Wangu.”

Jinsi tunavyopaswa kuwa waangalifu kusikia sauti MOJA, kwa kuwa Roho hana ila sauti moja ambayo ni sauti ya Mungu.

Loo! jinsi ilivyo muhimu kusikia sauti ya Mungu kwa njia ya wajumbe Wake, halafu kusema yale waliyopewa kuyaambia makanisa.

“Neno Langu daima limemjia nabii Wangu, lakini katika siku hii, Ilinibidi niirekodi Sauti Yangu ili KUSIWEKO NA MAKOSA kwa yale niliyomwambia Bibi-arusi. Kuna timazi moja tu, fimbo moja tu, na hiyo ni NENO nililolinena Mimi kupitia malaika Wangu. Kama ilivyo katika kila wakati, nabii Wangu ndiye Neno la siku hiyo.”

Kanda, Sauti Yake, ni barua ya mahaba kwetu sisi. Wakati adui anapotupiga mara kwa mara kupitia majaribio na dhiki na shida zetu, Yeye alimtuma malaika Wake mwenye nguvu kutuambia kwamba si chochote ila upendo wa kuchagua wa Mungu kwetu sisi, akituthibitishia kwamba ametuchagua sisi kwani hatutaondoshwa.

Kusudi Lake kuu ni kwamba baada ya sisi kuteseka kwa muda kidogo, angetufanya wakamilifu, atuimarishe na kututia nguvu. Alituambia kwamba hata Bwana wetu Yesu alikamilishwa kwa mateso Yake. Ni baraka iliyoje ambayo Yeye ametuachia. Kwa maana kwa mateso yetu, Yeye angetufikisha katika ukamilifu pia.

Anatujenga tabia kupitia majaribio na dhiki zetu. Maana tabia yetu haiumbiki bila mateso. Hivyo, mateso yetu ni USHINDI kwetu, na si karama.

Tunawezaje kuuthibitisha upendo wetu Kwake?

¶ Kwa kuamini yale aliyosema.

¶ Kukaa na Neno Lake.

¶ Kuenenda kwa furaha katikati ya majaribio na dhiki zetu, ambayo Yeye, katika hekima Yake kuu, anayaruhusu yatimie.

Jinsi anavyoinua roho zetu kwa kulisikia Neno Lake. Sauti Yake hufariji nafsi zetu. Tunapobonyeza Play na kumsikia Yeye akinena, mizigo yetu yote inainuliwa. Hatuwezi hata kuanza kufikiria ni hazina gani ambazo zimewekwa kwa ajili yetu kupitia dhiki zetu zote.

Loo, Bibi-arusi wa Yesu Kristo, ninayo furaha jinsi gani kuwa Mmoja Wao pamoja na kila mmoja wenu. Ni furaha iliyoje moyoni mwangu kujua Yeye ametupa Ufunuo wa Neno Lake. Wakati anapotuambia zitafanana sana ingewapoteza walio wateule kama yamkini, Yeye ametupa UFUNUO WA KWELI.

Njoo, uingie katika Roho pamoja nasi Jumapili hii saa 06:00 sita MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni saa 1:00 moja JIONI ya Afrika Mashariki) tunapolisikia Neno kamilifu: 60-1206 – Wakati wa Kanisa la Smirna.

Ndugu. Joseph Branham

24-1020 Wakati Wa Kanisa La Efeso

UJUMBE: 60-1205 Wakati Wa Kanisa La Efeso

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi Wa Kweli,

Ni wakati mzuri sana jinsi gani tulio nao huku Uzima Wake ukitiririka na kudundadunda ndani na kupitia kwetu, ukitupa uzima. Bila ya Yeye, hakungekuwa na uzima wo wote. Neno Lake ndilo pumzi yetu.

Katika siku hii kuu ya giza, sisi ndio kundi Lake la mwisho ambalo limeinuka; Bibi-arusi Wake wa kweli wa siku ya mwisho ambaye atamsikiliza Roho peke yake, Sauti ya Mungu kwa ajili ya siku yetu. 

Jinsi tunavyopenda kumsikia Yeye akituambia, “Kwangu Mimi, umefananishwa na dhahabu safi iliyofuliwa. Haki yako ni haki Yangu. Sifa zako ndio sifa Zangu zenye utukufu. Wewe ndiye Bibi-arusi Wangu wa Kweli wa kupendeza.”

Kama vile vita vyetu vinavyoonekana kuwa vigumu zaidi na zaidi kila wiki, sisi Tunabonyeza Play tu ili kumsikia Yeye akizungumza nasi kwa utamu sana na kutuambia, “Usijali, wewe unaistahili injili Yangu. Wewe ni kitu cha uzuri na furaha. Ninapenda kukutazama pindi unapomshinda adui kwa majaribu na majaribio ya maisha haya.”

Ninaiona taabu yako ya upendo; ni wito mkuu maishani mwako kunitumikia Mimi. Nilijua kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu ya kwamba wewe ungemtambua malaika Wangu mwenye nguvu ambaye ningemtuma awe Sauti Yangu kwako; jinsi ambavyo usingedanganyika wakati ambapo wale mbwa-mwitu wakali wakija huku wakijaribu kudai ufunuo sawasawa. Wewe Hungetoka kwenye Neno Langu, hata kidogo, HATA KWA NUKTA MOJA. Wewe ungekaa na Neno Langu, Sauti Yangu.

Ungeona wakati ninapokufunulia Neno Langu jinsi gani ule Mzabibu wa Kweli na mzabibu wa uongo ile iliyoanza katika Bustani ya Edeni jinsi ingekua pamoja kote katika nyakati zote. 

Kile kilichoanza katika kanisa la kwanza kingeendelea katika kila wakati. Jinsi ambavyo katika wakati wa kwanza wa kanisa, ule mzabibu wa uongo wa Shetani ungeanza kujiingiza ndani, na kuwashinda washirika kwa roho yake ya unikolai. Lakini jinsi gani ninavyolipenda hili kwamba wewe tu, Bibi-arusi Wangu mteule, hutadanganywa. 

Wiki hii, Nitaliangazia Neno Langu ndani yenu kwa kuifichua ile siri kuu ya ule uzao wa nyoka. Nitawafunulia kwa undani yote yaliyotukia katika bustani ya Edeni; jinsi ambavyo Shetani alivyojichanganya katika jamii ya binadamu. 

Litakuwa wazo la kufurahisha sana wakati mtakapotambua kwamba Mimi, Ule Mti wa Uzima katika Bustani ya Edeni, ambao usingeweza kukaribiwa hadi sasa kwa sababu ya kuanguka kwa Adamu, sasa mmepewa ninyi, washindi Wangu. 

Hii ndiyo itakuwa thawabu yako. Nitakupa haki ya bustani ya Mungu; ushirika wa daima na Mimi. Kamwe hautatengana na Mimi. Po pote Niendapo, wewe, Bibi-arusi Wangu utakwenda. Kile kilicho Changu Mimi, Nitakishiriki na wewe, Mpendwa Wangu.

Jinsi gani mioyo yetu inavyoenda mbio ndani yetu wakati tunapoyasoma maneno haya. Tunajua ule utimilifu wa ahadi zake unakaribia upesi, na ni vigumu kwetu kusubiri. Na hebu tuharakishe kulitii Neno Lake na hapo tuthibitishe kustahili kwetu kushiriki utukufu Wake.

Ningependa kuwaalika mje kuungana nasi wakati tunapoendelea na somo letu kuu la Nyakati Saba za Kanisa, ambapo Mungu anapotufunulia Neno Lake kwa njia Yake aliyoiandaa, malaika-mjumbe Wake wa saba. 

Ndugu. Joseph Branham

Jumapili saa 6:00 sita MCHANA, saa za Jeffersonville. (Ni Saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki)
60-1205 Wakati Wa Kanisa La Efeso

24-1013 Ono La Patimo

UJUMBE: 60-1204E Ono La Patimo

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi Neno Mkamilifu, 

Ni kitu gani kinachotukia ndani ya Bibi-arusi kote ulimwenguni? Tunaingia katika Roho, tukiinuka na kupaza sauti, “Utukufu! Haleluya! Bwana asifiwe!” Mungu anatusafirisha na kulifunua Neno Lake kwa Bibi-arusi Wake.

Mambo ambayo tumeyasoma na kuyasikia maisha yetu yote sasa yanadhihirika. Uhuishaji mkuu unatendeka. Tumeangaziwa na Neno kuliko wakati wowote. 

Tunalihisi ndani kabisa ya nafsi zetu. Kuna kitu fulani cha tofauti, kuna kitu kinatendeka. Tunamhisi Roho Mtakatifu akitutia mafuta, akiijaza mioyo na akili zetu kwa Neno Lake. 

Tunaweza kumsikia Yeye akisema nasi: Najua adui anapigana nanyi kuliko hapo awali, lakini msiogope enyi watoto wadogo, NINYI NI WANGU. Ninawapa upendo Wangu, ujasiri na uwezo. Mnene tu Neno, nami nitalitimiza. Mimi ni pamoja nanyi siku zote.

Katika somo letu kuu la Ufunuo wa Yesu Kristo, tuko chini ya matazamio makubwa kila wiki nini kifuatacho Atakachotufunulia. Neno lake ndilo kimbilio letu pekee, amani na faraja yetu. Tunasikiliza kwa makini tena na tena na tena. Kila aya ndogo tunayosoma, tunataka kupiga kelele na kupaza sauti wakati Neno linapofunuliwa mbele ya macho yetu. Imani ya Kunyakuliwa inakuja juu ya Bibi-arusi, ikizijaza nafsi zetu.

Hebu wazia, hakuna mahali pengine ulimwenguni unapoweza kwenda, ila papo hapo kwenye vidole vyako, kuisikia Sauti ya Mungu ikisema nawe na kulifunua Neno Lake. 

Jinsi ambavyo Mungu alivyoliondoa lile pazia, akalivuta, na kumruhusu Yohana atazame ndani na kuona kile ambacho kila wakati wa kanisa ungefanya, na kuyaandika katika Kitabu na kututumia sisi. Ndipo, wakati utimilifu wa wakati ulipotimia, Mungu alitutumia sisi malaika Wake wa saba mwenye nguvu kukinena, na kufunua yote Ilichomaanisha. 

Yohana aliandika kile alichokiona, lakini hakujua maana yake. Yesu hata hakulijua hilo wakati alipokuwa hapa duniani. Hakuna mtu katika nyakati zote aliyejua, mpaka siku hii, wakati huu, watu hawa, SISI, Bibi-arusi Wake.

Jinsi ambavyo ametufunulia kwamba hizo taa saba zilikuwa zikifyonza uhai na nuru kutoka kwenye hazina ya hilo bakuli kuu. Alitueleza jinsi ambavyo kila mmoja walivyokuwa wametumbikiza tambi zao mle. Kila mjumbe wa wakati wa kanisa alikuwa amewashwa moto na Roho Mtakatifu na utambi wake ukiwa umetumbukizwa ndani ya Kristo, akifyonza uzima halisi wa Kristo na kuitoa Nuru hiyo kwa kanisa. Na sasa, mjumbe wetu wa siku ya mwisho, aliye mkuu kuliko wajumbe wote, alikuwa na maisha yale yale na Nuru ile ile iliyodhihirishwa na maisha yaliyofichwa pamoja na Kristo katika Mungu.

Kisha malaika wetu mwenye nguvu anatuambia kuwa si tu kwamba kila mjumbe alionyeshwa hapo, BALI KILA MMOJA WETU NASI PIA, waamini wa kweli wa Mungu. Kila mmoja wetu pia anawakilishwa wazi wazi hapo. Kila mmoja wetu anafyonza kutoka kwenye chemchemi ile ile kama wale wajumbe. Sote tumetumbukizwa kwenye bakuli lile lile. Tumekufa kwa nafsi zetu na maisha YETU yamefichwa pamoja na, na ndani ya, Kristo Yesu Bwana wetu. 

Jinsi Yeye anavyotutia moyo kwa kusema hakuna mtu anayeweza kututoa sisi kutoka katika Mkono wa Mungu. Maisha yetu hayawezi kuchezewa. Maisha yetu yanayoonekana yanawaka moto na kuangaza, yakitoa nuru na madhihirisho ya Roho Mtakatifu. Maisha yetu ya ndani, yasiyoonekana yamefichwa ndani ya Mungu na kulishwa kwa Neno la Bwana. 

Vita ni vikali. Adui anashambulia kwa hasira kuliko hapo awali, akijaribu awezavyo kutuvunja moyo, kutupiga kabisa, lakini hawezi kulifanya hilo.  Mungu Mwenyewe ananena nasi kupitia midomo ya mwanadamu naye anatuambia, SISI NI BIBI-ARUSI WAKE, ALIYEMCHAGUA, na hilo linamshinda shetani KILA WAKATI. 

Bwana wetu Mkamilifu, akinena Neno Lake Kamilifu, akitoa Amani Kamilifu, kwa Bibi-arusi Wake Mkamilifu.

Kama kawaida, tunaualika ulimwengu mzima uje kuchovya utambi wao ndani ya BAKULI KUU, Ujumbe huu, ambao umehifadhiwa na kutunzwa kwa ajili ya Bibi-arusi. Tutakuwa tukipiga mayowe na kupaza sauti saa 6:00 Sita MCHANA, saa za Jeffersonville, (Ni saa 1:00 Moja JIONI ya Afrika Mashariki) tunapoisikia Sauti ya Mungu ikinena na kufunua yaliyotukia katika: Ono la Patimo 60-1204E.

Ndugu. Joseph Branham 

24-1006 Ufunuo Wa Yesu Kristo

UJUMBE: 60-1204M Ufunuo Wa Yesu Kristo

PDF

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Jeshi la Mungu Lisiloweza Kushindwa,

Sisi ndio wale ambao Baba aliyowachagua na kuwapa UFUNUO WA KWELI wa Yeye Mwenyewe; KANISA Lake la KWELI na pekee. Wale aliowachagua watende KAZI Yake KUBWA ZAIDI. Kwa maana kwa Roho Wake, tunaweza kuitambua na kuipinga roho ya mpinga-Kristo ya Shetani. Yeye HANA NGUVU mbele ZETU, kwa sababu sisi ni Jeshi Lake Lisiloweza Kushindwa.

Shetani anachukia ufunuo wote. LAKINI SISI TUNAUPENDA. kwa maana sisi ni wapenzi wa Neno la Mungu lililofunuliwa. Tukiwa na ufunuo wa kweli maishani mwetu, milango ya kuzimu haiwezi kutushinda, tunamshinda adui. Kila pepo yuko chini ya miguu yetu. Sisi ni Mmoja na Yeye nasi tunaweza kunena Neno, kwa maana sisi ni Neno Lake.

Bwana ameliweka hilo moyoni mwangu kwamba tujifunze na kuzisikia Nyakati Saba za Kanisa. Zitakuwa Wiki kuu sana kwa kila mmoja wetu. Atakuwa akitufunulia Neno Lake kuliko hapo awali, kwa nguvu zake za ushindi.

Huu sasa ndio wakati. Haya ndio majira yake. Atakuwa akituhuisha, akitutia moyo, kwa kutupa Changamko kwa Ufunuo, nalo Litaiwasha moto mioyo yetu!!

Ufunuo wa Yesu Kristo ni Kitabu cha kinabii ambacho kinaweza tu kueleweka na tabaka fulani la watu walio na ono la kinabii, SISI, Bibi-arusi Wake. Inahitaji Ufunuo wa KWELI kujua kwamba unasoma na kuisikia Sauti ya Mungu inayotoka kwa malaika-mjumbe Wake aliyemchagua, akitupa mafundisho ya kimbinguni.

Ni Ufunuo wa Yesu Kristo aliopewa Yohana kwa ajili ya Wakristo wa nyakati zote. Ndicho kitabu pekee katika Biblia nzima ambacho kimeandikwa na Yesu Mwenyewe, kwa kumtokea mwandishi Yeye Mwenyewe.

Ufunuo 1:1-2, “Ufunuo wa Yesu Kristo, aliopewa na Mungu awaonyeshe watumwa wake mambo ambayo kwamba hayana budi kuwako upesi; naye akatuma kwa mkono wa malaika Wake na kumwonyesha mtumwa Wake Yohana: aliyelishuhudia Neno la Mungu, na ushuhuda wa Yesu Kristo, yaani, mambo yote aliyoyaona.

Kitabu cha Ufunuo ni mawazo ya Mungu kabisa yaliyoandikwa na Mungu Mwenyewe. Lakini Yeye alituma na kumwonyesha mtumwa Wake Yohana kupitia malaika Wake. Yohana hakujua maana Yake; aliandika tu kile alichokiona na kusikia.

Lakini leo, Mungu alimtuma malaika Wake mwenye nguvu duniani kufunua Ufunuo huu Mkuu kwa Bibi-arusi Wake, ili tuweze kusoma na kusikia yale yaliyokuwa yametukia katika nyakati zote za kanisa. Tunaweza kuliona lile kundi Lake dogo lile lililodumu mwaminifu na wa kweli kwa Neno katika kila Wakati.

Mungu alinena kupitia malaika Wake na kusema ya kwamba katika siku hizi za mwisho, wakati Sauti ya mjumbe Wake wa wakati wa saba wa kanisa itakapoanza kupiga baragumu, Yeye atafunua siri za Mungu kama zilivyofunuliwa kwa Paulo. Wale wanaompokea nabii huyo katika jina lake mwenyewe watapokea matokeo mema ya huduma ya nabii huyo.

Utukufu, sisi ni Bibi-arusi wa Kubonyeza Play wa Mungu ambaye tumempokea nabii huyo katika jina lake mwenyewe, nasi tunapokea matokeo mema. Tunaamini ni Sauti ya Mungu inayonena na kumwongoza Bibi-arusi Wake.

Lo, Kanisa, kile tutakachosoma na kukisikia katika wiki zijazo. Kwake Yeye, sisi tunafananishwa na dhahabu SAFI. Kile alicho Yeye, ndicho tulicho. Sisi ndio Mzabibu Wake wa Kweli. Tumeshinda. Tumefanywa wakamilifu, tumeimarishwa, tumetiwa nguvu. Tumechaguliwa kwa Upendo Wake wa Kuchagua. Hakuna cha kuogopa. Sisi ndio kundi lile lililomsikia mjumbe na Ujumbe wake na Kuutwaa na Kuuishi.

Kila wiki tutakuwa tunasema, “Je, mioyo yetu haiwaki ndani yetu wakati Yeye anaponena na kutufunulia Neno lake njiani”.

Ukitaka kuuhisi upako wa Roho Wake Mtakatifu, kupokea Ufunuo zaidi wa Neno la Mungu, na unataka kuketi katika uwepo wa Mwana kuivishwa, na kupokea Imani ya Kunyakuliwa, njoo uungane nasi Jumapili saa 6:00 Sita MCHANA, saa za Jeffersonville.(Ni saa 1:00 Moja JIONI ya Afrika Mashariki), tunapoanza somo letu kuu juu ya: Ufunuo Wa Yesu Kristo 60-1204M.

Ndugu. Joseph Branham

Ningependa kukuhimiza usikie, au kusoma, kila wiki Kitabu cha Maelezo ya nyakati za Kanisa, sura tuliyomaliza kusikiliza kila Jumapili.

24-0929 Ufunguo Wa Mlango

UJUMBE: 62-1007 Ufunguo Wa Mlango

PDF

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Wenye Ufunguo wa Imani,

“Mimi ndiye Mlango wa zizi la kondoo. Mimi ndimi Njia, Njia pekee, Kweli, na Uzima, na mtu haji kwa Baba ila kwa njia ya Mimi. Mimi ndimi Mlango wa vitu vyote, na imani ndiyo ufunguo unaofungua mlango ili uweze kuingia.”

Kuna mkono mmoja tu unaoweza kuushikilia ufunguo huu, na huo ni mkono wa IMANI. IMANI ndiyo ufunguo pekee unaofungua ahadi zote za Mungu. IMANI katika kazi yake iliyokwisha kumalizika inaufungua kila mlango kwa kila hazina iliyo ndani ya Ufalme wa Mungu. IMANI ni Ufunguo malaya mkuu wa Mungu ambao unaufungua KILA MLANGO KWA BIBI-ARUSI WAKE nasi tunaushikilia huo Ufunguo katika MKONO wetu wa IMANI.

Ufunguo huo wa imani uko mioyoni mwetu, nasi tunasema, “Ni Neno la Mungu; Ni ahadi za Mungu kwa ajili yetu, nasi tunaushikilia ufunguo.” Na kisha, kwa kila sehemu ya imani tuliyo nayo, bila kutilia shaka hata chembe moja, tunaufungua kila mlango unaosimama kati yetu na baraka ambazo Mungu alizonazo kwa ajili yetu. Inazima jeuri ya moto. Inaufungua uponyaji kwa wagonjwa. Inaufungua wokovu wetu. Tumefika kwenye Mlango na lolote tunalofanya kwa neno au kwa tendo, tunayafanya yote katika Jina Lake, tukijua kwamba tunao ufunguo wa imani; nao ni ufunguo uliotengenezwa kwa Maandiko.

Sisi hatujali kile mtu yeyote anachowazia, kuna jambo moja la hakika: Mungu alituita SISI, alituchagua SISI tangu awali, alitufunulia SISI Neno Lake, alituambia sisi ni nani, nasi tumeyakinia kulifuata Neno Lake, kwa sababu Yeye ametuita sisi tuwe Bibi-arusi Wake.

Baba alizishikilia nyota Zake saba, wajumbe Wake saba, kwa zile nyakati saba mkononi Mwake. Amewashika mkononi Mwake, hivyo wanahusishwa na nguvu Zake. Hicho ndicho mkono unachomaanisha. Unamaanisha nguvu za Mungu! Na mamlaka ya Mungu.

Tumelishika Neno lake katika mikono yetu ya Imani, ikimaanisha uweza na mamlaka ya Mungu vipo MIKONONI MWETU naye ametupa UFUNGUO wa kuufungua kila mlango kwa kila jambo tunalohitaji. Ni Ufunguo Maalum ambao utaufungua KILA MLANGO.

Sasa ninajua kwa nini Mungu alitupa vidole 5 katika kila mkono; sio 4, sio 6, lakini 5, kwa hivyo kila wakati tunapoitazama mikono yetu tutakumbuka, tunayo ILE IMANI ya kuufungua kila mlango.

Ni ishara ya milele kwa jamii ya binadamu kwa hivyo sisi hatutasahau kamwe; daima tutakumbuka na kujipa moyo, kwamba tunaishikilia IMANI hiyo mikononi mwetu. Naye ataiinua imani yetu ya mbegu ya haradali na kutupa ILE IMANI YAKE KUU KATIKA NENO LAKE LISILOWEZA KUSHINDWA KAMWE, LA MILELE LISILOSHINDWA KAMWE!!!

Tunaweza kuinua mikono yetu Mbinguni, kuvinyoosha vidole vyetu 5 kwa kila mkono na kumwambia, “Baba, tunaamini na tunayo IMANI katika kila Neno ulilonena. Ni Ahadi Yako, Neno Lako, nawe Utatupatia Ile IMANI TUNAYOHITAJI ikiwa tu tutaamini….nasi TUNAAMINI.”

Kwa vile tutakuwa na ibada yetu ya Ushirika hadi ifikapo Jumapili jioni, ningependa kuwahimiza mchague Ujumbe wa kusikiliza pamoja na Kanisa lako, familia, au mtu binafsi, Jumapili asubuhi, kwa wakati unaofaa kwako. Hakika hakuna njia bora ya kuitathmini Imani yetu kuliko kusikia Neno; kwa maana IMANI huja kwa kusikia, kulisikia Neno, nalo Neno huja kwa nabii.

Hebu Basi tuungane wote kwa pamoja saa 11:00 kumi na moja JIONI. (kwa masaa ya nchi yako) ili kusikiliza Ujumbe, 62-1007 Ufunguo wa Mlango. Kama ilivyotangazwa, ningependa kuifanya hii kuwa Ibada Maalum ya Ushirika, ambayo itakuwa ikicheza kwenye Redio ya Sauti (Voice Radio) saa 11:00 kumi na moja JIONI. (Masaa ya Jeffersonville). Mnaweza kupakua na kucheza ibada kwa Kiingereza au lugha zingine kwa kubofya hapa: BOFYA HAPA.

Sawa na ibada zingine za Ushirika wa Nyumbani katika wakati uliyopita, mwishoni mwa kanda Ndugu Branham ataombea mkate na divai. Kutakuwa na muziki wa piano kwa dakika kadhaa ili mkamilishe sehemu ya ibada ya Ushirika. Kisha, Ndugu Branham atasoma Maandiko yanayohusu kutawadhana miguu, na Nyimbo za Injili zitafuata usomaji wake kwa dakika kadhaa, ili muweze kukamilisha sehemu ya ibada ya kutawadhana miguu.

Ni fursa iliyoje tuliyo nayo kumwalika Bwana wetu Yesu kula pamoja na kila mmoja wetu katika nyumba zetu, makanisani, au popote ulipo. Niombeeni wakati mnapozungumza Naye, kama ilivyo hakika nitakuwa nikiwaombea.

Mungu awabariki,

Ndugu Joseph Branham

TANGAZO LA IBADA YA USHIRIKA WIKI HII

Ilitumwa jana: Jumatatu, tarehe 23 Septemba, 2024

Ndugu na dada,

Ningependa tuwe na Ibada nyingine ya Ushirika na Kutawadhana Miguu Jumapili hii, tarehe 29 Septemba, Bwana akipenda. Kama tulivyofanya wakati uliyopita, ningewahimiza muanze saa 11:00 KUMI NA MOJA JIONI. kwa masaa ya nchi zenu. Ingawa Ndugu Branham alisema mitume wao walifanya Ushirika kila wakati walipokutana pamoja, Yeye alipendelea kuufanya wakati wa jioni, naye akautaja kama Meza ya Bwana.

Ujumbe na ibada ya Ushirika itakuwa kwenye Redio ya Sauti, na pia kutakuwa na anuani ya faili la kupakuliwa kwa wale ambao hawawezi kuipata Redio ya Sauti Jumapili asubuhi.

Kwa waamini wa eneo la Jeffersonville, tutakuwa na divai ya Ushirika tena itakayopatikana kwa ajili ya kuja kuchukua. Tangazo litatoka hivi karibuni kueleza mahali, siku na saa.

Hakika niko chini ya matarajio kwa sisi kushika agizo hili la thamani ambalo Bwana alilotuachia. Ni fursa ilioje kwetu sisi kuandaa nyumba zetu na kuifungua mioyo yetu kwa ajili ya Mfalme wa Wafalme aingie na kula pamoja nasi Mezani Pake.

Mungu awabariki,

Ndugu Joseph

https://branhamtabernacle.org/en/bt/A9/109403

24-0922 Edeni Ya Shetani

UJUMBE: 65-0829 Edeni Ya Shetani

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa sifa ya Mungu,

Sisi ndio sifa halisi ya Baba yetu wa Mbinguni; kwa maana tulikuwa ndani yake hapo mwanzo. Hatukumbuki hilo sasa, lakini tulikuwa pamoja Naye, na Yeye alitujua. Alitupenda sana hata akatufanya kuwa mwili, ili aweze kuwasiliana nasi, kuzungumza nasi, kutupenda, hata kutushika mikono.

Lakini Shetani alikuja na kupotosha Neno la asili la Mungu, Ufalme Wake, na mpango Wake kwa ajili yetu. Aliwapotosha wanaume na wanawake na kufanikiwa katika kupotosha na kuuteka ulimwengu huu tunaoishi. Ameufanya ulimwengu kuwa ufalme wake, bustani yake ya Edeni.

Ni saa danganyifu na yenye hila iliyowahi kuwako. Ibilisi ameweka kila mtego wa ujunja awezao; maana yeye ni mdanganyifu mkuu. Mkristo hana budi kuwa mwangalifu zaidi leo kuliko alivyowahi kuwa katika wakati wowote.

Lakini wakati huohuo, ndio wakati uliyo mzuri zaidi ya nyakati zote, kwa sababu tunaelekea kwenye ule Utawala wa Miaka Elfu mkuu. Bustani yetu ya Edeni inakuja hivi karibuni, ambamo tutakuwa na upendo mkamilifu na ufahamu mkamilifu wa upendo wa Mungu. Tutakuwa hai na salama pamoja Naye katika Edeni yetu Milele yote.

Yesu alituambia katika Mathayo 24 tunapaswa kuwa waangalifu jinsi gani katika siku hii. Alituonya kwamba ingekuwa ni siku ya udanganyifu sana iliyowahi kuwepo, “inafanana sana hata ingewadanganya wale Walioteuliwa na Mungu kama yamkini”; kwa kuwa ujanja wa Ibilisi utawafanya watu waamini ya kwamba wao ni Wakristo, wakati wao sio.

Lakini wakati huu pia ungemtoa Bibi-arusi Neno safi wake ambaye hangedanganyika na asingeweza kudanganywa; kwa maana wangedumu na Neno Lake la asili.

Kama Yoshua na Kalebu, Nchi yetu ya ahadi imeanza kuonekana kama vile yao ilivyoanza kuonekana. Nabii wetu alisema Yoshua maana yake ni, “Yehova-Mwokozi”. Alimwakilisha kiongozi wa wakati wa mwisho ambaye atakuja kwa kanisa, kama vile Paulo alivyokuja kama kiongozi wa kwanza.

Kalebu aliwakilisha wale waliomtii Yoshua. Kama vile wana wa Israeli, Mungu alikuwa amewaanzisha kama bikira kwa Neno Lake; bali wao walitaka kitu tofauti. Nabii wetu alisema, “vivyo hivyo na kanisa hili la siku za mwisho nalo.” Kwa hiyo, Mungu hakuwaacha Waisraeli waingie katika nchi ya ahadi mpaka wakati Wake Mwenyewe uliokusudiwa ulipowadia.

Watu walimsonga Yoshua, kiongozi wao waliyepewa na Mungu, na kusema, “Hiyo nchi ni yetu, hebu na twende tukaitwae. Yoshua, umeshindwa, lazima umepoteza agizo lako. Huna ile nguvu uliyokuwa nayo. Ulikuwa ukisikia kutoka kwa Mungu na kujua mapenzi ya Mungu, na kutenda kwa haraka. Una kasoro fulani wewe.”

Yoshua alikuwa nabii aliyetumwa na Mungu, naye alijua ahadi za Mungu. Nabii wetu alituambia:

“Mungu aliuweka uongozi mzima katika mikono ya Yoshua kwa sababu alikuwa amedumu na Neno. Mungu aliweza kumwamini Yoshua lakini si hao wengine. Kwa hiyo itajirudia katika siku hizi za mwisho. Shida ile ile, usumbufu ule ule.”

Kama vile Mungu alivyofanya na Yoshua, Yeye aliuweka UONGOZI MZIMA mikononi mwa malaika-nabii Wake, William Marrion Branham; kwa maana alijua angeweza kumwamini yeye, lakini si hao wengine. Ilibidi kuwe na Sauti Moja, Kiongozi Mmoja, Neno Moja la mwisho, wakati huo, na SASA HVI.

Ninapenda jinsi nabii alivyotuambia kutakuwa na maelfu mara maelfu ambao watakaozisikia kanda. Alisema kuwa hizo kanda NI HUDUMA. Kutakuwa na baadhi yetu tutakaoingia kwa siri Majumbani na makanisani tukiwa na kanda (huduma yake) ili kuupata Uzao wa Mungu uliochaguliwa tangu awali.

Tuliporudi na kusema, Bwana, tumetii maagizo yako, nako kulikuwa na watu tuliowapata tulipozicheza kanda walioamini. Sasa tumehubiri jambo hilo, kote ulimwenguni, Je, utatimiza hilo?

Yeye atasema: “Hilo ndilo Mimi nililowatuma kufanya.”

Mungu atalitimiza hilo. Nyumba yako kamwe haitaporomoka. Wakati Mungu atakapotoa ishara ya kukiangamiza kitu hicho chote, familia yako yote, mali zako zote, zitakuwa salama nyumbani mwako. Unaweza kusimama humo. Haikulazimu kuchungulia dirishani, wewe Bonyeza Play tu huku vita vikiendelea.

Maneno yako yalionekana, nami nikayala; na maneno yako yalikuwa ni furaha kwangu, na shangwe ya moyo wangu; maana nimeitwa kwa jina lako, Ee Bwana, Mungu wa majeshi.

Ninakualika uje uungane nasi wakati tunapokula huduma kuu ya Mungu, hai, ya wakati wa mwisho, Jumapili hii saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni saa 1:00 Jioni ya Afrika mashariki) tunaposikia yote yanayohusu: Edeni ya Shetani 65-0829.

Hebu tuishi mpaka kuja Kwake Bwana kama ikiwezekana. Hebu na tutende kila kitu kilicho katika uwezo wetu kwa upendo, na uelewano—kuelewa kwamba Mungu anauchunguza ulimwengu, siku hii ya leo, kutafuta kila kondoo aliyepotea. Hebu tuzungumze nao kwa maombi ya upendo yaliyokolea chumvi na Neno la Mungu, ili tuweze kumpata huyo wa mwisho kusudi tupate kwenda nyumbani, na tutoke katika Edeni hii ya kale ya Shetani hapa, Bwana.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya kusikiliza Ujumbe:

2 Timotheo 3:1-9
Ufunuo 3:14
2 Wathesalonike 2:1-4
Isaya 14:12-14
Mathayo 24:24

24-0915 Chujio La Mtu Mwenye Busara

UJUMBE: 65-0822E Chujio La Mtu Mwenye Busara

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bi. Yesu Kristo,

Roho wa Mungu aliye hai, tupulizie. Hebu tuchukue Chujio lako nasi tuishi chini ya Hilo, Bwana. Tupulizie hewa safi ya Roho Mtakatifu ndani ya mapafu yetu na ndani ya nafsi zetu kila siku. Tunaweza tu kuishi kwa Neno Lako; kila Neno litokalo katika kinywa Chako kwa ajili ya wakati huu tunaoishi.

Sisi tumeonja mambo Yako ya Mbinguni nasi tuna Neno Lako mioyoni mwetu. Tumeliona Neno Lako likidhihirishwa mbele yetu, na nafsi yetu yote imesitiriwa ndani Yake. Ulimwengu huu, na mambo yote ya Ulimwengu yamekufa kwetu.

Sisi ni chembechembe iliyo hai, mbegu Neno ambayo iliyokuwa ndani Yako tangu mwanzo Tukisimama hapa tukiivuta ile mbegu yako ya Uzima. Mbegu yako imo mioyoni mwetu kwa kujua kwako tangu awali. Ulituchagua tangu awali tusivute kupitia chochote kile, ila Neno Lako, Sauti Yako, kwenye kanda.

Ule wakati wa jicho umefika; hakuna kilichosalia ila Kuja Kwako kumjia Bibi-arusi Wako. Chujio letu ni Neno Lako, Malaki 4, Bwana Asema Hivi.

Hebu tulipande Neno Lako mioyoni mwetu, na tuazimie ya kwamba hatutageuka mkono wa kulia ama wa kushoto, bali tuishi tukiwa waaminifu Kwake siku zote za maisha yetu. Baba, tutumie juu yetu Roho Mtakatifu wa Uzima, na alihuishe Neno Lako kwetu, ili tupate kukudhihirisha Wewe.

Shauku ya mioyo yetu ni kuwa wana na binti wa kweli Kwako. Tumeketi katika uwepo wa Sauti Yako, tukiivishwa, tukijifanya wenyewe tayari kwa ajili ya Karamu yetu ya Harusi pamoja nawe hivi karibuni.

Mataifa yanavunjika. Ulimwengu unavurugika. Matetemeko ya ardhi yanaitikisa California kama vile Wewe ulivyotuambia ingefanya. Tunajua hivi karibuni Kipande kinene cha maili elfu moja na mia tano, upana wa maili mia tatu ama mia nne kitazama, labda maili arobaini ndani ya ule ufa kule. Mawimbi yataruka mpaka mkoa wa Kentucky, Na wakati kitakapozama, kitaitikisa dunia sana mpaka kila kitu juu yake kitaanguka chini.

Onyo lako la mwisho linaendelea. Ulimwengu uko katika machafuko kamili, lakini wakati wote Bibi-arusi Wako anapumzika ndani Yako na Neno Lako, ameketi pamoja katika ulimwengu wa roho unapozungumza nasi, na kutufariji njiani.

Jinsi gani tunavyoshukuru, Baba, kwamba tunaweza kwa urahisi “Kubonyeza Play” na kuisikia Sauti Yako ikizungumza nasi, kututia moyo na kutuambia:

Msiogope, enyi kundi dogo. Yote niliyo Mimi, ninyi ni warithi wake. Nguvu Zangu zote ni zenu. Uwezo Wangu ni wenu ninaposimama katikati yenu. Sikuja kuleta hofu na kushindwa, bali upendo na ujasiri na uwezo. Nimepewa mamlaka yote nanyi mnaweza kuitumia. Ninyi neneni Neno Nami nitalitimiza. Hilo ni agano Langu wala haliwezi kushindwa kamwe.”

Ee Baba, hatuna cha kuogopa. Unatupa upendo wako, ujasiri na uwezo wako. Neno Lako liko ndani yetu kulitumia tunapolihitaji. Tunalinena, na Wewe Utalitimiza. Ni agano Lako, nalo haliwezi KUSHINDWA KAMWE.

Maneno yapatikayo na mauti hayawezi kueleza jinsi gani tunavyojisikia, Baba, lakini tunajua Wewe unaona ndani ya mioyo na roho zetu; kwa maana sisi ni sehemu Yako.

Jinsi gani tunavyoshukuru kwamba Umeiandaa njia kwa ulimwengu kuisikia Sauti Yako katika wakati huu wa mwisho. Kila wiki, Wewe unaualika ulimwengu mzima uje kuungana kumsikia malaika-mjumbe wako wakati Wewe unapotulisha Chakula cha Kondoo ambacho kimehifadhiwa ili kutudumisha hadi Utakaporudi kutuchukua.

Tunakupenda Baba.

Ndugu. Joseph Branham

Ujumbe: 65-0822E Chujio La Mtu Mwenye Busara

Muda: Saa 06:00 SITA MCHANA, Saa za Jeffersonville(Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika mashariki)

Maandiko: Hesabu 19:9 / Waefeso 5:22-26