All posts by admin5

22-0102 Yakini

Ujume: 62-1230m Yakini

PDF

pakua

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi arusi wa Ujumbe wa Mtu Mmoja,

 Huu Umekuwa mwaka Mkuu jinsi gani kwa Bibi-arusi.  Ametuunganisha kutoka ulimwenguni kote kwa kitu pekee kinachoweza kuleta Bibi-arusi Wake pamoja, Ujumbe wa wakati huu, Sauti yenyewe ya Mungu ikimwita Bibi-arusi Wake atoke .

 Na sasa, naamini uko tayari kugonga kilele kile cha mwisho kule kuleta imani ambayo italinyakua Kanisa hata Utukufuni; na lipo katika hizo Jumbe!

 Ufunuo wa Ujumbe huu sasa umetia nanga ndani kabisa ya mioyo yetu.  Matendo yetu yanaambatana kabisa na Neno.  Tunajua fundisho letu ni kamilifu na Neno, haliongezi chochote Kwake wala kuondoa lolote Kwake.  Kwetu sisi, si kingine ila Neno kwenye kanda.

 Amekuwa akitutayarisha kwa ajili ya kilele cha mwisho kwa kutupa Imani tunayohitaji kwa ajili ya Unyakuo.  Imani hiyo, iko ndani yetu SASA.  Uhai wa Kristo umezalishwa karibu katika njia ya kufanyika mwili, kupitia sisi, kama ilivyokuwa ndani ya Kristo.

 Tunaweza kuona maisha yake.  “Kazi nizifanyazo mimi nanyi mtazifanya, yeye aaminiye.”  Si yeye ajifanyaye anaamini, si yeye ajidhaniaye kuwa anaamini, bali, “Yeye aaminiye.”  “Yeye aniaminiye Mimi, kazi nizifanyazo Mimi yeye naye atazifanya.”  Kwa nini?  Ametiwa nanga kwenye Mwamba uleule.  Mwamba ulikuwa nini?  Neno, daima.  Umetiwa nanga hapo.  Ni Nyota yako ya kaskazini unapopotea baharini .

 Tumetia nanga sana kwenye Mwamba huo.  Tuna hakika nalo.  Tumeyakinika nalo.  Hatuchukui Neno la mtu mwingine, tunadumu na Bwana Asema hivi.  Tumekuja kwenye Yakini Yetu.

 Tumeridhika kabisa na tumetosheka. Hakuna kushangaa tena kama ilivyokuwa katika siku za Waamuzi, na kwa walio wengi sana leo, ambapo kila mtu alifanya lililo sawa machoni pake mwenyewe, ambapo kila mtu alikuwa na yakini yake mwenyewe na kufanya yale tu aliyotaka kufanya.  Mungu habadilishi kanuni zake, hawezi na awe Mungu.  Ikiwa Mungu atawahi kusema lolote au kufanya jambo lolote, ni lazima afanye vivyo hivyo kila wakati.

 Mungu daima hutuma nabii kuwaongoza watu wake.  Alitutumia Nabii Wake malaika wa 7 ;  Mwana wa Adamu akijifunua Mwenyewe katika mwili wa mwanadamu, kumwita Bibi-arusi Wake atoke na kumwongoza .  Kanda ni Sauti ya Mungu kwa Bibi-arusi Wake.  HIYO NDIO YAKINI YETU.

 Akapanda akaenda kule…Alijua…Nami napenda hilo, jinsi alivyokuja; alifikia kwenye yakini yake, nguzo yake ya kujishikilia.

 Mungu anamwita Bibi-arusi Wake pamoja. Yeye Hatabadilisha mpango Wake. Yeye Hatatuma kundi la watu kumkusanya Bibi-arusi Wake.  Bibi-arusi Wake ataungana tu kwenye Neno safi, hiyo ni Sauti ya Mungu kwenye hizo Kanda.  Ni huduma ya kweli ya Mungu kwa ajili  ya siku hii .

Hakuna njia bora ya kuanza Mwaka Mpya kuliko kukusanyika pamoja na kusikia nguzo yetu yakushikilia , Yakini yetu, ikizungumza nasi. Ningependa kuwaalika kila mmoja kuja kusikiliza pamoja nasi Jumapili saa 4:00 nne Asubuhi ., saa za Jeffersonville,( ni Saa kumi na mbili jioni ya Tanzania), ili kusikia Ujumbe: Yakini 62-1230M.

 Kama hamwezi kuungana nasi, ninawatia moyo kuchagua Ujumbe wa kucheza katika nyumba zenu, au mtie moyo mchungaji wenu kuchagua Ujumbe ambao ninyi pia mnaweza kuketi  pamoja, chini ya upako huu mkuu uliopo, na kusikia yakini ya Bibi-arusi iliyothibitishwa.

 Ndugu.  Joseph Branham

21-1226 Kwa Nini Bethlehemu Mdogo

Ujume: 63-1214 Kwa Nini Bethlehemu Mdogo

PDF

pakua

BranhamTabernacle.org

Wapendwa darasa,

Ningependa kuwahubiria na kuwafundisha leo kwa njia ya barua yangu. Hebu kwanza tupitie yale tuliyojifunza Jumapili iliyopita.

Je, unawezaje kuupata ule uzao wa Mungu uliochaguliwa tangu zamani? BONYEZA PLAY .

Yoshua aliwaambia wahudumu wake wafanye nini? Ingieni Yeriko, wahudumieni watu kwa KUBONYEZA PLAY, na yako na nyumba yako itaokolewa.

Wajumbe wake walirudi, wakasema, “Nimezitii amri zako. Nasi tulimpata mwanamke kule, tulipozicheza kanda.

Hatuonei haya. Hatujali ni nani anayeiona. Tulitaka kila mtu aione na kuisikia. Tumeiweka majumbani mwetu, katika makanisa yetu, kila mahali tunapoenda, ili kila mtu anayepita ajue ya kwamba tunatambulishwa na Ishara yetu; Yesu Kristo, Neno Lake, Roho Mtakatifu, Ujumbe wa saa hii, hizi Kanda, Sauti ya Mungu.

Tunaweza kuona ya kwamba hasira iko tayari kupitia juu ya uso wa nchi, na cho chote kisicho chini ya hiyo Ishara kitaangamia.
Bali atakapoiona Ishara, atapita juu yetu. Ndiyo masharti ya Mungu ya wakati huu. Ujumbe wa wakati wa jioni, ni kupaka Ishara.

Je, darasa alituambia ingefanana sana kiasi gani?

. Kusema tu ninaamini… hakutoshi.

. Kutembea mahali ilipo… hakutoshi, inakufanya kuwa mbaya zaidi.

. Siibi.

. Ninauzuria kwenye Maskani ya Branham.

. NAAMINI UJUMBE.

. NINAAMINI KILA NENO ULILOSEMA NDUGU BRANHAM…WOW !!!

Hilo ni sawa, bali hiyo ni uwezo tu wa kusoma

Usifikie tu umbali huu, ukasema, “Naamini Ujumbe.” Tii Mjumbe! Ingia katika Kristo!
Chukua Ujumbe, uingize moyoni mwako, ya kwamba huna budi kupata ile Ishara, Uhai ule ule uliokuwemo katika Kristo uwe ndani yako. “Nitakapoiona hiyo, nitapita juu yenu.”

Mungu amekuwa akimwambia nini Bibi-arusi wake Ujumbe baada ya Ujumbe? KANDA , KANDA, KANDA. kuhubiri Ujumbe na kufundisha Ujumbe ni sawa, lakini ni lazima UCHEZE UJUMBE.

Je, mtu anawezaje kusema anaupenda Ujumbe na hataki kuucheza Ujumbe mbele ya watu? Hawana uhusiano wa upendo ule nilio nao kwa ujumbe huu, kama ni pendavyo kila mmoja kuja pamoja na kusikia hilo likithibitishwa na sauti ya Nguzo ya Moto.

Tuna IMANI isiyotikisika katika Neno lake. Sisi sio Hawa. Sisi sio mabwana mashaka au kuridhiana na Shetani. Tunashikilia kila Neno la Mungu katika Biblia, na kila Neno kwenye Kanda. Kwa maana hizi kanda ni hasa mawazo yenyewe ya Mungu, yaliyonenwa na kufunuliwa kwa Bibi-arusi Wake, na haihitaji kufasiriwa kokote. Ndipo mahali pekee tunajuapo tunapoweza kusema AMINA kwa kila Neno.

Ujumbe huu ni mkate mpya unaoshuka kutoka Mbinguni, kwa ajili ya safari yetu. Ni Mkate wa Uzima, na kila siku tunapokea upya kutoka kwa Kristo, kutoka Mbinguni, Roho Mtakatifu, akija na kujaza nafsi zetu.

Tumeketi pamoja tukiwa na lengo moja, Neno la Mungu, nasi tunakula Neno Hilo. Tuko katika Bethlehemu ya kiroho ya Mungu, tukila Mkate wa kiroho wa Mungu, na nafsi zetu zinaitikia kila Neno alilosema, kwa “Amina!” Tunafurahia Chakula hiki cha malaika wa Mbinguni ambacho kimehifadhiwa kwa ajili yetu ili tukile.

Njoo uungane nasi Mezani Pake na kula pamoja nasi kile chakula cha malaika wa Mbinguni Jumapili hii saa 4:00 nne Asubuhi ., saa za Jeffersonville.( ni saa 12:00 Kumi na mbili jioni ya Tanzania).

Kama nyinyi watu wa kanda hapa, mnaosikiliza kanda, ningewatakeni msikilize huo: Ni Kwa Nini Ilibidi Yesu Kuja Bethlehemu. Ni kwa nini ilimbidi kufanya hivyo?

Baba amekwishanena nasi kupitia nabii Wake kwa mara nyingine tena na kuwaalika ninyi nyote Watu wa kanda kuja kusikiliza Ujumbe: Kwa nini Bethlehemu Mdogo 63-1214.

Mahubiri yangu na kufundisha kwangu sasa kumekwisha, sasa hebu na TUBONYEZE PLAY .

Ndugu. Joseph Branham

21-1219 Ile Ishara

UJUMBE: 63-0901M Ile Ishara

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi wa Ishara,

Haijawahi kutokea wakati kama huu hapo awali katika historia ya ulimwengu. Ulimwengu wote ulilazimika kushuhudia jambo hilo, kwani sayari tano zilijipanga zenyewe pamoja. Kuna jambo lililokuwa likitukia mnamo Desemba 12, 2021 katika mbingu, huku jambo fulani likiendelea duniani. Bibi-arusi waliungana wenyewe pamoja kutoka ulimwenguni kote kama vile Mungu alivyonena kupitia kwa nabii Wake, na Bibi-arusi Wake alikuwa na Ushirika na Kutawazana Miguu kwa pamoja katika nyumba zao.

Ni hali na uwepo wa Bwana ulioje uliokuwa ndani ya nyumba zetu. Baadhi ya vijana wa kanda waliingia ndani ya nyumba zetu nasi tukaifanya nyumba yetu kuwa kanisa la Bwana. Tuliweka Ishara kwa nyumba zetu na kwa familia zetu. Roho Mtakatifu aliijaza nyumba yetu, mioyo yetu, na nafsi zetu kwa uwepo wake. Ilikuwa kana kwamba sisi ni wana wa Israeli tukijiandaa kwa safari yetu ya kutoka.

Neno lilikuwa likisema nasi kupitia malaika wake na lilitumika kwenye nyumba zetu. Mauti ilikuwa imetuzunguka, lakini tulijua tulikuwa salama na ingepita juu ya nyumba zetu. Tulikuwa tunajiandaa kuondoka kuelekea Nchi YETU ya Ahadi.

Hatujawahi kamwe kuhisi ukaribu kama tulivyohisi usiku ule. Tulijua jambo fulani Lilikuwa likitendeka. Tulijua alikuwa anatutayarisha kwa ajili ya Kuja Kwake, lakini ilibidi iwe wakati huu, siku hii, mwezi huu, mwaka huu. Kila kitu kilikuwa kikamilifu na mahali pake. Ilikuwa na maana. Ilikuwa inatokea kama ishara kwa ulimwengu.

Kila tukio la kiroho ni ishara kutoka kwa Mungu. Iweni waangalifu. Tazameni hilo, mnaona. Tazameni, kila tukio la kiroho, kila kitu kinachotendeka, ni ishara. Hatuko hapa kwa bahati. Mambo haya hayatendeki kwa bahati. Ni ishara. Ni ishara, kuingia—ingieni mahali pa salama, upesi. Nuhu alikuwa ishara kwa kizazi chake; Elija alikuwa ishara kwa chake; Yohana alikuwa ishara kwa chake. Mnaona? Kila kitu, Ujumbe wa wakati huu, ni ishara. Uchunguze, tazama unachofanya. Unaona? Ni ishara. Kila kitu kina maana yake.

Musa alipoanza huduma yake katika Israeli, kwa ishara kuu, waona, Israeli walikusanyika upesi toka kila sehemu ya Misri kuenda Gosheni, wakirudi nyumbani kwao, kwa maana walijua kitu fulani kilikuwa karibu kutukia. Lo, ni mfano jinsi gani!

Ni mfano mkamilifu jinsi gani leo hii, Bibi-arusi anapokusanyika kwenye Neno safi lisiloghoshiwa la wakati huu; kwa sababu sisi pia tunajua, kuna jambo linakaribia kutukia.

wanakuja kutoka Mashariki na Magharibi, Wanatoka nchi za mbali; Kula karamu pamoja na Mfalme, kula kama wageni Wake, kwenye Chakula Chake Kilichohifadhiwa MEZANI PAKE.

Alimtuma malaika Wake nabii akiwa na Ujumbe kumwita atoke na kumwongoza Bibi-arusi Wake kwenye Nchi ya Ahadi. Amejitambulisha Mwenyewe miongoni mwetu kwa Nguzo ya Moto. Kisha, Yeye ametuma Ishara Yake ili Bibi-arusi Wake akae chini ya hiyo, kwa maana Yeye anaitambua Ishara hiyo Pekee.

Ishara ni nini leo hii?

Yeye hutambua tu I—Ishara. Huo ndio Ujumbe wa wakati huu! Huo ndio Ujumbe wa siku hizi! Huo ndio Ujumbe wa wakati huu! Katika Jina la Yesu Kristo, upokeeni !

Bibi-arusi na Kristo wanakuwa Mmoja. Huduma ya Bibi-arusi, na huduma ya Kristo, ni sawa. Mungu Mwenyewe Anatambua Ujumbe wa mjumbe Wake. Amemtambua Bibi-arusi Wake. Hasi inakuwa chanya. Kila ahadi katika Neno Lake ni YETU. Ni lazima itutii.

Tunakuwa Bibi-arusi Neno mkamilifu kwa njia iliyoandaliwa na Mungu kwa siku ya leo: Sauti Yake, Neno Lake, kwenye Kanda. Mungu kamwe habadilishi mpango Wake. Daima amemtuma nabii kuwaongoza watu wake. Alikuwa na wengine walioitwa na kutiwa mafuta, bali wao wangeweza kusema TU yale nabii aliyosema, kwa maana Maneno yake yalikuwa BWANA ASEMA HIVI kwa watu.

Unawezaje kuwa na UHAKIKA asilimia 100% kwamba unalosikia ni Neno KAMILIFU la Mungu? Kuna njia moja tu kwangu mimi: Bonyeza Play.

Hakika kuna wengine ambao wameitwa kuhubiri Neno, kwa maana limo ndani ya Neno na haliwezi kupingwa, lakini wanaweza tu kuhubiri Neno ambalo wamesikia kwenye Kanda kutoka kwa mjumbe wa Mungu. Hawawezi kuhubiri, kufundisha, kufasiri, kuondoa au KUONGEZA CHOCHOTE KWAKE kwani ni NENO KAMILIFU LA MUNGU. Hivyo ndivyo Neno lisemavyo.

Si vibaya kumsikia mhudumu, kama wengine wasemavyo, wala si vibaya kwenda kanisani. Unapaswa kwenda kanisani, Lakini Bibi-arusi anataka kusikia chakula cha kondoo, na wengi wanaamini njia pekee ya kusikia Neno safi ni Kubonyeza Play.

Mungu awabariki na huduma yao Mungu aliyowaitia. Kwa maana mimi siko kinyume chao na ninawapenda nakuamini nitatumia Umilele pamoja na Bibi-arusi Wake wote aliyechaguliwa tangu awali. Mimi niko tu kwa ajili ya huduma ya kanda.

Wengi husema ni lazima uwe na mhudumu ili uwe Bibi-arusi. Ninakubali , ninaye , William Marrion Branham, kwa maana yeye ndiye mhudumu mkuu sana aliye na huduma kuu sana kuliko zote ulimwenguni. Kwa maana si neno lake, ujumbe wake, mawazo yake, wala si fasiri yake. Ndilo Neno pekee la Mungu lililothibitishwa kwa ajili ya Wakati wetu. Na ndiyo, ndio HUDUMA kuu sana HAI iliyopo .

Maswali yangu ni: Je! Unaweza tu kusikiliza Kanda na kuwa Bibi-arusi wa Kristo, au je, inanibidi kuwa na kitu zaidi ya Sauti ya Mungu kwenye kanda?

Mimi na nyumba yangu, sisi ni NYUMBA YA KANDA, na tunaamini sisi ni Bibi-arusi Wake na Kila TUNACHOHITAJI ni Sauti ya Mungu kwenye kanda.

Ikiwa ungependa kuungana nasi nyumbani kwako, kanisani, garini au popote pale ambapo Bwana yuko nawe, ili kusikia Bwana Asema hivi, uungana nasi Jumapili saa 3:00 Tatu asubuhi, saa za Jeffersonville, ( ni saa 11:00 kumi na moja jioni ya Tanzania), kusikia Neno la Mungu likimkamilisha Bibi-arusi Wake na kutuletea Ujumbe: Ile Ishara 63-0901M

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya kusikia Ujumbe:

Mwanzo 4:10

Kutoka sura ya 12 yote

Yoshua sura ya 12 yote

Matendo 16:31 / 19:1-7

Warumi 8:1

1 Wakorintho 12:13

Waefeso 2:12 / 4:30

Waebrania 6:4 / 9:11-14 / 10:26-29 / 11:37 / 12:24 / 13:8,10-20

Yohana Mtakatifu 14:12

21-1204 Unyakuo

Ujume: 65-1204 Unyakuo

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi wa Sauti,

Ninaamini ninaweza kunena kwa niaba ya kila mmoja wetu ninaposema, tumekuwa na wikendi kuu sana ya Shukrani ya maishani mwetu. UTUKUFU!!

Tulisikia Neno juu ya Neno, Ufunuo juu ya Ufunuo. Kiu Yetu ilitulizwa na kitu pekee kinachoweza: Neno Lake, Ujumbe wa wakati huu, Kristo Mwenyewe akinena na Bibi-arusi Wake.

Sasa tunaona Neno lile lile lililoahidiwa, la Luka, la Malaki, ahadi hizi nyingine zote za siku ya leo, zikifanyika mwili, zikikaa kati yetu, ambazo tulisikia kwa masikio yetu; sasa tunamwona Yeye (kwa macho yetu) akifasiri Neno Lake Mwenyewe, hatuhitaji Fasiri yo yote ya mwanadamu. Ee kanisa la Mungu Aliye Hai! mlio hapa na kwenye simu! amkeni upesi, kabla hamjachelewa sana! Mungu awabariki.

Je! tunaweza kuwazia Hilo ya kwamba tungeweza kuwa tunatazama kwa macho yetu wenyewe, Neno lililo hai la Mungu lililodhihirishwa? Tukilitazama Neno lililo hai lililofasiriwa katika umbo la mwili, Mungu kati yetu! Si ajabu wahenga wote wa kale waliitazamia siku hii, lakini SASA, tunaishi katika siku hizo zilizoahidiwa, tukiona na kusikia jambo Hilo likiwa limedhihirishwa kwa masikio na macho yetu wenyewe.

Tumesikia habari Zako, ya kwamba Wewe ungeweza kuumba kuchakuro; Tumesikia habari Zako, ya kwamba Wewe ungeweza kuumba kondoo dume; lakini sasa Tunakuona Wewe, kwa jicho letu Wenyewe! Dhihirisho hilo, ono kufanywa lionekane.

Yeye ni nini basi? Neno lililofasiriwa ni dhihirisho la Jina la Mungu .

Haijalishi wakosoaji wanasema nini, Sisi tuko katika Mapenzi Yake Makamilifu kwa kukusanyika katika nyumba zetu, katika makanisa yetu, au popote tunapokusanyika, tukisikiliza Sauti Yake.

Kama mimi siamini kwenda kanisani, basi kwa nini niwe na makanisa? Tulikuwa nayo kila mahali nchini, yameunganishwa hivi majuzi usiku, kila maili mia mbili mraba kulikuwapo na kanisa langu .

Makanisa YAKE yameunganishwa kote ulimwenguni ili kusikia Sauti ya Mungu ikinena, na kumwita Bibi-arusi Wake atoke. Hakuna chachu miongoni mwetu, jambo Hilo linaleta utimilifu wote wa Uungu kwa jinsi ya mwili miongoni mwetu. Mwana wa Adamu anadhihirishwa, anafunuliwa, akilirudisha Kanisa pamoja na Uungu wote wa Mungu miongoni mwetu. Anatuonyesha ishara zile zile zionekanazo na Dhihirisho la Yeye Mwenyewe kama alivyofanya hapo mwanzo alipodhihirishwa duniani katika umbo la Mungu-Nabii.

Aliahidiwa na Malaki 4, aliahidiwa na Maandiko hayo mengine. Unaabudia wapi? Nyumba ya Mungu, umeketi (katika wakati uliopo).

Ninamshukuru sana Bwana kwa yote anayomfanyia Bibi-arusi Wake katika siku hizi za mwisho. Amekuwa akitutia moyo, akituhakikishia, kwamba sisi ni Wateule Wake waliokuwa ndani Yake kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu. Ni wakati wa ajabu jinsi gani kwa Bibi-arusi Wake.

Bwana ameweka moyoni mwangu kuendelea na Jumbe hizi za mwisho ambazo zilizohifadhiwa kwa ajili ya Bibi-arusi Wake. Ninahisi kubarikiwa sana kufikiria, Baba alitoa njia ambayo sote tungeweza kuungana pamoja, kutoka kote ulimwenguni, kusikia Jumbe hizi. Huu hakika ni, Muungano Usioonekana wa Bibi-arusi wa Kristo.

Tangu wakati hatukuweza kuwa na ibada pamoja ya mahali, kwa sababu ya Corona na ujenzi wa patakatifu papya, kuna mambo mawili ambayo sisi sote tunayakosa na tunatamani kuyafanya. Ni mambo hayo mawili ambayo Bwana aliamuru kwa Bibi-arusi Wake kufanya hadi kurudi Kwake: Ushirika na Kutawazana Miguu.

Nilipokuwa nikiomba na kumtafuta Bwana, Aliweka moyoni mwangu tuwe na vyote viwili Ushirika na Kutatawazana Miguu pamoja na familia zetu. Nilibarikiwa sana na kufurahishwa sana Alipoweka Jambo hilo moyoni mwangu, na jinsi tunavyoweza kulifanya. Tutakuwa tukiufanya katika tarehe kamili ya ibada ya mwisho ya Ushirika ambayo Ndugu Branham aliyokuwa nayo alipokuwa hapa pamoja nasi, tarehe 12 Desemba 1965. Pia tutabarikiwa kwa yeye kutuongozea ibada ya Ushirika na kutawazana Miguu kwa mara nyingine tena.

Nitakuwa nikikutumia barua, na kuchapisha kwenye tovuti ya Branham Tabernacle, maelezo yote katika siku chache. Ninaweza kukuahidi utakuwa ni wakati ambao Bibi-arusi hatasahau. Niko chini ya matarajio Haya ya baraka zake kuu ambazo atakuwa akitupatia.

Kuanzia Jumamosi hii, tutakuwa tukisikiliza Sauti yetu ikituletea Ujumbe: Unyakuo 65-1204 , saa 3:00 Tatu Asubuhi., saa za Jeffersonville( ni Saa 11:00 Kumi na Moja jioni ya Tanzania) . Itakuwa ni miaka 56 hadi siku hii ambapo Mungu alinena kupitia kwa mjumbe Wake na kuweka Sauti Yake kwenye kanda ya sumaku, ili Bibi-arusi apate kula kwenye Hiyo na kuiva Mwenyewe, akijifanya Mwenyewe tayari kwa ajili ya Unyakuo unaokuja hivi karibuni.

Tutaendeleza ratiba kwa kukusanyika Jumapili saa 8:00 Nane mchana, saa za Jeffersonville, ( ni Saa 4:00 nne usiku ya Tanzania) ili kusikia: Mambo Yatakayokuwapo 65-1205 .

Kisha Jumatatu tutasikia: Matukio ya Sasa Yakidhihirishwa Na Unabii 65-1206 , na

Jumanne : Uongozi 65-1207. Unaweza kuusikiliza siku hiyo wakati wowote unaofaa kwako na familia yako.

Kama tu wiki iliyopita, tutakuwa tukiweka jumbe hizi kwenye Voice Radio( iliyo kwenye app ya Lifeline ya vgr) saa 3:00 Tatu Asubuhi za Jeffersonville ( ni Saa 11:00 kumi na Moja jioni ya Tanzania)

na saa 1:00 Moja jioni ya Jeffersonville ( ni Saa 9:00 Tisa Usiku ya Tanzania) .

Ilioambatishwa hapa ni kalenda yenye siku, majira na Jumbe ambazo tutakazosikia. Katika siku chache zijazo, nitakuwa nikikutumia barua na kuchapisha ratiba ya Ibada yetu ijayo ya Ushirika.

Nikitazamia kuwa pamoja nawe, Bibi-arusi Wake Asiyeonekana, kwenye Kiti Chake cha Enzi.

Bwana na akubariki,

Ndugu. Joseph Branham