21-1226 Kwa Nini Bethlehemu Mdogo

Ujume: 63-1214 Kwa Nini Bethlehemu Mdogo

PDF

pakua

BranhamTabernacle.org

Wapendwa darasa,

Ningependa kuwahubiria na kuwafundisha leo kwa njia ya barua yangu. Hebu kwanza tupitie yale tuliyojifunza Jumapili iliyopita.

Je, unawezaje kuupata ule uzao wa Mungu uliochaguliwa tangu zamani? BONYEZA PLAY .

Yoshua aliwaambia wahudumu wake wafanye nini? Ingieni Yeriko, wahudumieni watu kwa KUBONYEZA PLAY, na yako na nyumba yako itaokolewa.

Wajumbe wake walirudi, wakasema, “Nimezitii amri zako. Nasi tulimpata mwanamke kule, tulipozicheza kanda.

Hatuonei haya. Hatujali ni nani anayeiona. Tulitaka kila mtu aione na kuisikia. Tumeiweka majumbani mwetu, katika makanisa yetu, kila mahali tunapoenda, ili kila mtu anayepita ajue ya kwamba tunatambulishwa na Ishara yetu; Yesu Kristo, Neno Lake, Roho Mtakatifu, Ujumbe wa saa hii, hizi Kanda, Sauti ya Mungu.

Tunaweza kuona ya kwamba hasira iko tayari kupitia juu ya uso wa nchi, na cho chote kisicho chini ya hiyo Ishara kitaangamia.
Bali atakapoiona Ishara, atapita juu yetu. Ndiyo masharti ya Mungu ya wakati huu. Ujumbe wa wakati wa jioni, ni kupaka Ishara.

Je, darasa alituambia ingefanana sana kiasi gani?

. Kusema tu ninaamini… hakutoshi.

. Kutembea mahali ilipo… hakutoshi, inakufanya kuwa mbaya zaidi.

. Siibi.

. Ninauzuria kwenye Maskani ya Branham.

. NAAMINI UJUMBE.

. NINAAMINI KILA NENO ULILOSEMA NDUGU BRANHAM…WOW !!!

Hilo ni sawa, bali hiyo ni uwezo tu wa kusoma

Usifikie tu umbali huu, ukasema, “Naamini Ujumbe.” Tii Mjumbe! Ingia katika Kristo!
Chukua Ujumbe, uingize moyoni mwako, ya kwamba huna budi kupata ile Ishara, Uhai ule ule uliokuwemo katika Kristo uwe ndani yako. “Nitakapoiona hiyo, nitapita juu yenu.”

Mungu amekuwa akimwambia nini Bibi-arusi wake Ujumbe baada ya Ujumbe? KANDA , KANDA, KANDA. kuhubiri Ujumbe na kufundisha Ujumbe ni sawa, lakini ni lazima UCHEZE UJUMBE.

Je, mtu anawezaje kusema anaupenda Ujumbe na hataki kuucheza Ujumbe mbele ya watu? Hawana uhusiano wa upendo ule nilio nao kwa ujumbe huu, kama ni pendavyo kila mmoja kuja pamoja na kusikia hilo likithibitishwa na sauti ya Nguzo ya Moto.

Tuna IMANI isiyotikisika katika Neno lake. Sisi sio Hawa. Sisi sio mabwana mashaka au kuridhiana na Shetani. Tunashikilia kila Neno la Mungu katika Biblia, na kila Neno kwenye Kanda. Kwa maana hizi kanda ni hasa mawazo yenyewe ya Mungu, yaliyonenwa na kufunuliwa kwa Bibi-arusi Wake, na haihitaji kufasiriwa kokote. Ndipo mahali pekee tunajuapo tunapoweza kusema AMINA kwa kila Neno.

Ujumbe huu ni mkate mpya unaoshuka kutoka Mbinguni, kwa ajili ya safari yetu. Ni Mkate wa Uzima, na kila siku tunapokea upya kutoka kwa Kristo, kutoka Mbinguni, Roho Mtakatifu, akija na kujaza nafsi zetu.

Tumeketi pamoja tukiwa na lengo moja, Neno la Mungu, nasi tunakula Neno Hilo. Tuko katika Bethlehemu ya kiroho ya Mungu, tukila Mkate wa kiroho wa Mungu, na nafsi zetu zinaitikia kila Neno alilosema, kwa “Amina!” Tunafurahia Chakula hiki cha malaika wa Mbinguni ambacho kimehifadhiwa kwa ajili yetu ili tukile.

Njoo uungane nasi Mezani Pake na kula pamoja nasi kile chakula cha malaika wa Mbinguni Jumapili hii saa 4:00 nne Asubuhi ., saa za Jeffersonville.( ni saa 12:00 Kumi na mbili jioni ya Tanzania).

Kama nyinyi watu wa kanda hapa, mnaosikiliza kanda, ningewatakeni msikilize huo: Ni Kwa Nini Ilibidi Yesu Kuja Bethlehemu. Ni kwa nini ilimbidi kufanya hivyo?

Baba amekwishanena nasi kupitia nabii Wake kwa mara nyingine tena na kuwaalika ninyi nyote Watu wa kanda kuja kusikiliza Ujumbe: Kwa nini Bethlehemu Mdogo 63-1214.

Mahubiri yangu na kufundisha kwangu sasa kumekwisha, sasa hebu na TUBONYEZE PLAY .

Ndugu. Joseph Branham