RATIBA YA KRISMASI!

Ndugu na Dada Wapendwa,

Kwa sababu ya Krismasi kuwa kwenye siku ya Jumapili mwaka huu, nimejisikia moyoni mwangu kutokuwa na wakati maalum wa sisi kusikiliza Ujumbe siku hiyo. Familia nyingi zina watoto wadogo ambao huchangamka sana kufungua zawadi zao asubuhi ya Krismasi, na itakuwa vigumu sana kwao kutulia kusikiliza Ujumbe au kuwafanya wangoje hadi wakati fulani baadaye.

Na, hata hivyo, kwenye Krismasi, mwajua, watoto wadogo, huwezi kuwaambia vinginevyo. Wao, ninii tu, ni wakati wa Krismasi kwao. Nao wasingetaka maskini soksi zao zitundikwe, kungekuwa na kitu fulani. Ni desturi, hata katika taifa letu, kwamba wanatundika soksi, na kitu kingine. Mbona, nilifanya hivyo, nilipokuwa mtoto, na—na ingawa liko mba—mbali sana na Maandiko, njia iliyowekwa kama lilivyo. Hata hivyo, watoto ni ninii, wanasikia watoto wengine wakisema, “Vema, nilipata hiki kwa ajili ya Krismasi. Nilipata hiki.” Jamaa hao wadogo wanasimama huku, wanaangalia, mwajua. Huwezi, huwezi kuwafanya waelewe. Unaona? Kwa hiyo, kwamba tu, Krismasi itadumu. Naam.

Pia kunaweza kuwe na wengine ambao wangependelea kuamka mapema na kusikiliza Ujumbe, kama walivyopanga na washiriki wengine wa familia zao baadaye siku hiyo. Kwa hiyo nimeamua kwa kila familia kuchagua wakati ambao ungelingana vyema na ratiba yao ya kusikiliza Ujumbe. Tutatangaza Ujumbe huo kwenye Lifeline mara tatu tofauti Siku ya Krismasi:  Saa 3:00 Tatu Asubuhi . – Saa 06:00 Sita Mchana. – Saa 11:00 Kumi na moja Jioni. Tafadhali usijisikie kuwa ni lazima usikilize wakati mmojawapo wa nyakati hizi, lakini chagua wakati unaofaa zaidi kwako au kwa familia yako. Jambo muhimu zaidi ni, KUBONYEZA PLAY.

Inaweza ionekane kwa namna fulani inachekesha, asubuhi hii, kuvaa kabuti langu jukwaani, bali nilifurahia sana ku—kuonyesha hilo kabuti zuri nililopewa na kanisa hili. Nilimuona Ndugu Neville hapa juzijuzi, amevaa ile suti ya kupendeza, jinsi ilivyomkaa vizuri mno, na nikawaza, vema, ni…Ilionekana nzuri mno, na kusanyiko langu linazungumzia habari zake, nikafikiri, “Nitavaa tu kabuti jukwaani.”

Unajua, ninaamini kamwe hatukui. Sikuzote tu…Nami sitaki kukua. Unalionaje hilo, Ndugu Luther? La, kamwe hatutaki kukua, tunapenda siku zote tu kudumu tukali watoto.

Bwana na awape Sikukuu yakupendeza iliyojaa Uwepo Wake.

Ndugu. Joseph Branham