23-0917 Anɔ Tsitre Le Gbagbãƒe La Me

Gbedasi: 63-0623m Anɔ Tsitre Le Gbagbãƒe La Me


BranhamTabernacle.org

Wapendwa Wateule,

Bwana wetu Yesu anatupenda sana, hata ikampendeza Yeye kututumia nabii katika siku yetu. Mmoja yule ambaye alimwamini asilimia mia moja. Mmoja yule Yeye angeweza kuja na kuishi ndani yake, ili aweze kujifunua Mwenyewe kupitia ule mwili wa mwanadamu kumwita Bibi-arusi Wake.

Nabii wake alitupenda sana hata akatuahidi, sisi, na Mungu, ya kwamba Ujumbe wo wote mpya ungetoka kwenye maskani yake ndogo. Angeurekodi, kuuhifadhi, ili Bibi-arusi wa Mungu apate Chakula cha Kiroho cha kufanyia karamu, hata alipokuwa ameondoka.

Mungu alimpenda malaika-nabii Wake sana Yeye alimsaidia nabii Wake kulitimiza neno lake kwetu.

Baada ya Mungu kunena kupitia malaika Wake mwenye nguvu na kuifunua kikamilifu na kutufasiria sisi Biblia nzima, ndipo akakifungua kilele cha Mwamba ulio kama piramidi, ambao hata haukuandikwa, na kulifunua hilo kwa malaika Wake, ili aweze kutupa sisi siri Zake zote zilizofichwa, Bibi-arusi Wake.

Mungu hata alitoa ono kwa Ndugu Roberson, ambapo aliona Nguzo ya Moto ikimtwaa nabii Wake na kumpeleka Magharibi, kisha ikamrudisha na kumweka mbele ya Meza ambapo alikuwa amekwisha badilishwa.

Ndipo Roho Mtakatifu akanena na kumwambia,
“Huyu ni mtumishi Wangu. Nami nimemwita kuwa nabii kwa wakati huu, kuwaongoza watu kama tu Musa alivyofanya. Naye amepewa mamlaka, angeweza kunena kitu kiwepo.”

Wito wa Musa ulikuwa ni upi? Yeye alipaswa kufanya kitu gani? Mungu alikuwa amemwagiza Musa kuwaongoza watu hadi nchi ya ahadi. Lakini waliinuka watu waliokuwa wameamua kwamba wangeingilia agizo ambalo Mungu alimpa Musa, wakisema, “Umejitwalia madaraka mengi mno wewe. Wewe, ukijaribu kujifanya mtu wa pekee katika kundi hili ambaye ana mamlaka yote.”

Tendo hili lilimuudhi Mungu sana mpaka akamwambia Musa, “Jitenge ukaondoke miongoni mwao. Nitaliua tu kundi hilo lote, na kuanza kizazi kipya kwako.” Naye Musa akaanguka mbele za Mungu na kusema yeye itambidi kuja juu yake.

Kama Mungu angeamua kuwaangamiza watu katika siku yetu, ni nani angesimama kama Musa kwa ajili ya watu? Tungempata wapi mtu ambaye angesimama, au angeweza kusimama, ambaye Mungu angemkubali kama Yeye alivyomkubali Musa? Kuna maisha ya mtu mmoja tu duniani yaliyo muhimu sana kwa Mungu kuizuia hasira yake, malaika wake wa saba mwenye nguvu.

Mungu daima amekuwa na mpango. Bibi-arusi Wake atautambua mpango huo naye atadumu nao Neno kwa Neno. Wao wanajua inawabidi wadumu na Sauti hiyo ambayo Mungu ameichagua kuwaongoza kufika kwenye Nchi ya Ahadi.

Mungu alinena kupitia nabii wake naye akatoa nafasi ya kutosha ya kwenda mwelekeo tofauti upendao, kama vile Nuhu alivyowafanyia yule njiwa na kunguru ndani ya safina. Lakini kama tu vile njiwa ambaye daima alirudi ndani ya Safina, Bibi-arusi daima atarudi kwenye Ujumbe, Sauti hiyo, KANDA.

Nabii wa Siku yetu alikuwa nani? Kumekuwa na manabii wenye nguvu hapo awali ambao Mungu alikuwa amewaita na kuwatuma kuongoza watu wake kote katika nyakati: Ibrahimu, Musa, Eliya, Elisha, lakini hakuna hata mmoja wao aliyekuwa kama huyu nabii mwenye nguvu wa siku yetu. Yeye Aliitwa kuwepo kwenye huduma ya juu zaidi kuliko hao wote. Yeye ndiye ambaye Mungu alimchagua kufunua siri zake zote. Yeye ndiye ambaye Mungu alimchagua kunena kitu fulani kiwepo pasipo na kitu. Yeye ndiye aliyechaguliwa kufunua Mvuto wa Tatu. Yeye ndiye ambaye Mungu alimchagua kumwongoza Bibi-arusi Wake.

Sisi ni watu waliobarikiwa jinsi gani, Bibi-arusi mteule wa Mungu. Tunawezaje kushushwa chini? Tunawezaje kuwa na huzuni? Shetani anajaribu kutukatisha tamaa, lakini tunao ushindi, tuko ndani tumetiwa muhuri, salama ndani ya Safina. Milango imefungwa. Hakuna kinachoweza kutudhuru. Sisi ni Adamu Wake aliyerejeshwa.

Anakuja kwa ajili yetu, Bibi-arusi Wake mteule. Kutakuwa na baadhi yetu ambao haitawalazimu kuonja kifo, lakini watabadilishwa mara moja, kufumba na kufumbua. UTUKUFU!!

Kama vile kila mmoja wenu, nimechangamshwa sana, wakati kila siku, Neno Lake, Ufunuo wangu aliyonipa, unazidi kuwa mkuu zaidi na zaidi. Niko chini ya matarajio makubwa. Ikiwa Yeye hatakuja leo, huenda kesho, lakini najua Yeye yuaja hivi karibuni sana na Anakuja KWA AJILI YANGU NA KWA AJILI YAKO.

Njoo uungane nasi Jumapili saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,( ni saa MOJA JIONI ya Afrika Mashariki ), tunaposikia Chakula ambacho kimehifadhiwa mahali pamoja padogo tunapotazama na kusikia: Kusimama Katika Pengo 63-0623M. Tutauanza Ujumbe huu kwenye namba ndogo ya 27.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya Kusoma Kabla ya Kusikiliza Ujumbe:

Hesabu 16:3-4