23-0521 Wakati Wa Kanisa La Thiatira

Ujume: 60-1208 Wakati Wa Kanisa La Thiatira

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Nyota Katika Taji Yake,

Furahi Bibi-arusi. Tunakuwa mmoja na Yeye. Kila siku, Anatupa Ufunuo zaidi wa yeye Mwenyewe na wetu sisi. Tunazidi kufahamu zaidi ile Nguvu ya Kuhuisha inayoishi na kukaa ndani yetu.

Hatuwezi hata kueleza jinsi tunavyojisikia. Tumemezwa na Roho wake. Ndio yote tuwazayo. Hakuna kitu kingine muhimu kwetu. Tunaona Neno Lake likifanyika Neno ndani yetu. Linalisha nafsi zetu. Tunaishi kila siku kumwabudu yeye, kumsifu, na kumshukuru kwamba tunaweza kusikia Sauti yake ikinena nasi.

Tunaposoma Kitabu chetu cha nyakati za Kanisa, ni vigumu kwetu kukiweka chini; mioyo yetu inalipuka. Kila siku huleta Ufunuo zaidi. Tunataka kuruka juu na kupaza sauti, kukimbia huku na huku chumbani na kupiga kelele: “Utukufu, Haleluya, Bwana apewe sifa.” “je, umelisoma hili?” “Nimeliwekea alama kwenye marejeo yangu pendwa, lakini sijawahi, KAMWE, kulisoma kama hivi hapo awali.” Yeye anatufunulia Biblia nzima kutoka Mwanzo hadi Ufunuo, nami najiona SISI WENYEWE KATIKA NENO LAKE.

Tunamwona Bibi-arusi huyo wa Kweli ambaye aliyedumu na Neno katika nyakati zote na hakudanganywa na udanganyifu mkuu wa Shetani. Alitaka kuabudiwa kama Mungu. Lakini wakati wote kulikuwa na yule BIBI-ARUSI WA KWELI, akidumu mwaminifu kwa Neno Lake. Hilo kundi dogo teule lililokaa na mjumbe Wake. Kama sisi tu, hawakuweza, na wasingeweza, kupatana. Walijua kulikuwa na NJIA MOJA PEKEE ya kuwa na hakika: kudumu na Njia Yake aliyoiandaa, Neno Lake, malaika Wake.

Jinsi gani Shetani amekuwa akidanganya wakati wote. Amefanya kazi katika Nyakati mbalimbali za Kanisa mpaka ametimiza malengo yake. Yeye Sasa amefanana sana na YULE ALIYE MKAMILIFU ili aweze kuwapoteza walio wateule kama yamkini….lakini Mungu apewe sifa, HAIWEZEKANI, HATUDANGANYIKI. Kwa nini? TULIKAA NA SAUTI YA MUNGU, NENO LAKE LILILOFANYIKA MWILI.

Hakuna njia ya mkato. Sauti ya Mungu ndiyo Njia Yake aliyoiandaa kwa ajili ya wakati huu. Tumeendelea kufanya kazi zake kwa uaminifu hadi mwisho. Tumepewa mamlaka juu ya mataifa, na ni watawala wenye nguvu, wenye uwezo, wasiokunjika ambao wanaoweza kukabiliana na hali yoyote kwa nguvu sana. Hata adui yetu aliyedhikika sana amevunjika. Udhihirisho wetu wa utawala, kwa Nguvu zake, ni kama ule wa Mwana.

Loo, jinsi tulivyotamani tungeweza kueleza kwa maneno jinsi tunavyojisikia. Siku moja tutafanya hivyo enyi marafiki. Tutaishi Milele na Bwana wetu, Malaika Wake, na sisi kwa sisi.

Kama yule bibi mzee mweusi huko Memphis, nasi tulijua alikuwa ndiye tulipomsikia. Kwa nini? Loo, sisi ni MMOJA WAO.

Je, ungependa Roho Mtakatifu azungumze nawe na kukuambia wewe ni nani? Njoo ujionee uwepo wa Bwana pamoja nasi Jumapili hii saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,( ni saa MOJA JIONI ya Afrika Mashariki ) tunaposikia: Wakati wa Kanisa la Thiatira 60-1208 . Itabadilisha maisha yako.

Ndugu. Joseph Branham