24-1027 Wakati Wa Kanisa La Smirna

UJUMBE: 60-1206 Wakati Wa Kanisa La Smirna

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi Aliyejazwa Roho,

Kuna kundi moja tu la watu; kundi maalum sana la watu, ambao wanaweza kusikia yale Roho anayosema katika wakati huu wa mwisho. Ni kundi maalum ambalo limeupokea Ufunuo wa wakati huu. Kundi hilo ni la Mungu. Kundi lile ambalo haliwezi kusikia, si la Mungu.

Kundi ambalo linaweza, na linasikia yale Roho anayosema, linapokea Ufunuo wa Kweli. Sisi ndio hao walio na Roho wa Mungu. Sisi ndio hao waliozaliwa na Mungu na kubatizwa kwa Roho Mtakatifu. Sisi ndio Bibi-arusi Wake Aliyejazwa Roho ambaye ameupokea Ufunuo kwa ajili ya wakati wetu.

Inamaanisha nini kwetu sisi Kubonyeza Play? UFUNUO! Ni kusikia, kupokea na kukaa na Njia ya Mungu iliyoandaliwa kwa ajili ya siku hii. Sauti ya Mungu mwenyewe ikinena mdomo kwa sikio na Bibi-arusi Wake. Ni Roho Mtakatifu akizungumza na mioyo na nafsi zetu.

Tunajua Mungu huwatumia watu waliotiwa mafuta na Roho wake kunena, lakini hakuna mahali pengine pa kuisikia Bwana Asema Hivi isipokuwa kwa Kubonyeza Play na kuisikia SAUTI ya malaika wake wa saba, William Marrion Branham. Ndiyo Sauti pekee iliyothibitishwa na Roho Mtakatifu Mwenyewe. Yeye ndiye Sauti ya Mungu, nabii wa Mungu, mchungaji wa Mungu, kwetu sisi, na kwa ulimwengu mzima.

Wakati Yeye anaponena, sisi tunasema AMINA kwa kila Neno; kwa maana ni Mungu mwenyewe anayesema nasi. Neno Lake ndilo Neno pekee lisilohitaji kufasiriwa. Ni Mungu akitumia sauti yake kuongea na Bibi-arusi Wake.

Ni Mungu mwenyewe anayetuambia, “Watoto wangu, si ninyi mlionichagua mimi, bali ni mimi niliyewachagua ninyi. Kabla hakujawa na chembe ya vumbi ya nyota; kabla hata sijajulikana kwako kuwa Mungu wako, Nilikujua. Ulikuwa Niani Mwangu, ukiwa katika Mawazo Yangu ya milele. Wewe ni Bibi-arusi Wangu halisi wa Uzao Wa Neno Lililonenwa.

Ingawa mlikuwa katika Mawazo Yangu ya milele, Sikuwadhihirisha hadi majira Yangu niliyoyakusudia na yaliyoamriwa. Kwa maana nilijua NINYI mngekuwa kundi langu maalum ambalo lingedumu na Neno Langu. Wengine wote wameshindwa, lakini Nilijua ninyi hamgeshindwa.

Ninajua ya kwamba unateswa na kudhihakiwa kwa sababu umedumu na nabii Wangu, lakini wewe ndiye Mzabibu Wangu wa Kweli ambao haujakengeuka kutoka kwenye Neno Langu, bali umedumu kuwa mkweli na mwaminifu kwa nabii Wangu ambaye hunena Maneno Yangu.

Kuna wengine wengi ambao wamefundishwa kwa uaminifu, lakini wao daima hawajifunzi jinsi ilivyo jambo muhimu kusema yale tu Mimi Niliyoyanena kupitia mjumbe Wangu.”

Jinsi tunavyopaswa kuwa waangalifu kusikia sauti MOJA, kwa kuwa Roho hana ila sauti moja ambayo ni sauti ya Mungu.

Loo! jinsi ilivyo muhimu kusikia sauti ya Mungu kwa njia ya wajumbe Wake, halafu kusema yale waliyopewa kuyaambia makanisa.

“Neno Langu daima limemjia nabii Wangu, lakini katika siku hii, Ilinibidi niirekodi Sauti Yangu ili KUSIWEKO NA MAKOSA kwa yale niliyomwambia Bibi-arusi. Kuna timazi moja tu, fimbo moja tu, na hiyo ni NENO nililolinena Mimi kupitia malaika Wangu. Kama ilivyo katika kila wakati, nabii Wangu ndiye Neno la siku hiyo.”

Kanda, Sauti Yake, ni barua ya mahaba kwetu sisi. Wakati adui anapotupiga mara kwa mara kupitia majaribio na dhiki na shida zetu, Yeye alimtuma malaika Wake mwenye nguvu kutuambia kwamba si chochote ila upendo wa kuchagua wa Mungu kwetu sisi, akituthibitishia kwamba ametuchagua sisi kwani hatutaondoshwa.

Kusudi Lake kuu ni kwamba baada ya sisi kuteseka kwa muda kidogo, angetufanya wakamilifu, atuimarishe na kututia nguvu. Alituambia kwamba hata Bwana wetu Yesu alikamilishwa kwa mateso Yake. Ni baraka iliyoje ambayo Yeye ametuachia. Kwa maana kwa mateso yetu, Yeye angetufikisha katika ukamilifu pia.

Anatujenga tabia kupitia majaribio na dhiki zetu. Maana tabia yetu haiumbiki bila mateso. Hivyo, mateso yetu ni USHINDI kwetu, na si karama.

Tunawezaje kuuthibitisha upendo wetu Kwake?

¶ Kwa kuamini yale aliyosema.

¶ Kukaa na Neno Lake.

¶ Kuenenda kwa furaha katikati ya majaribio na dhiki zetu, ambayo Yeye, katika hekima Yake kuu, anayaruhusu yatimie.

Jinsi anavyoinua roho zetu kwa kulisikia Neno Lake. Sauti Yake hufariji nafsi zetu. Tunapobonyeza Play na kumsikia Yeye akinena, mizigo yetu yote inainuliwa. Hatuwezi hata kuanza kufikiria ni hazina gani ambazo zimewekwa kwa ajili yetu kupitia dhiki zetu zote.

Loo, Bibi-arusi wa Yesu Kristo, ninayo furaha jinsi gani kuwa Mmoja Wao pamoja na kila mmoja wenu. Ni furaha iliyoje moyoni mwangu kujua Yeye ametupa Ufunuo wa Neno Lake. Wakati anapotuambia zitafanana sana ingewapoteza walio wateule kama yamkini, Yeye ametupa UFUNUO WA KWELI.

Njoo, uingie katika Roho pamoja nasi Jumapili hii saa 06:00 sita MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni saa 1:00 moja JIONI ya Afrika Mashariki) tunapolisikia Neno kamilifu: 60-1206 – Wakati wa Kanisa la Smirna.

Ndugu. Joseph Branham