25-1201
62-0621E – Thibitisho Na Ushahidi
Kumbukeni, ya kwamba haitupasi kamwe kuja kanisani kuigiza dini. Haitupasi kuja, kuninii tu, kujivalisha tendo la kidini tupate kwenda kanisani, hatuna budi kuja kuabudu katika Roho na katika kweli, hatuna budi kuwa waaminifu sana, lazima kweli tumaanishe kile kilichotuleta hapa. Siku zinazidi kuwa ovu, wakati ni mwovu, nasi tunataka—tunataka kutumia kila dakika, na hasa sana tunapokuwa katika nyumba ya Bwana.
MKATE WA KILA SIKU
Ndipo Yesu alipomwambia, Nenda zako, Shetani; kwa maana imeandikwa, Msujudie Bwana Mungu wako, umwabudu yeye peke yake. Mathayo 4:10
25-1130
53-0508 – Mungu Akimpa Agizo Musa
Akasema, “Loo, loo, nili—nilifikiri nina Roho Mtakatifu nilipoamini.” wangali wanafundisha hilo, lakini ni makosa. Imani ni sawa. Imani ni nzuri sana. Imani ina…Ibrahimu alimwamini Mungu, nayo ikahesabiwa kwake kwa, ama, kuwa haki, bali Mungu alimpa muhuri wa tohara kama muhuri wa imani yake.
Ndugu, unapokuwa na imani halisi ya kweli kwa Mungu, Mungu atakupa ubatizo wa Roho Mtakatifu kama muhuri wa ahadi, ambao ni muhuri, kwamba unayo imani. Unaweza kufanya—a—aina fulani ya hisi, ama kuwafanya watu waamini, ama unaweza kusema una imani, lakini unapokuwa na imani halisi isiyoghoshiwa, Mungu atakupa ubatizo wa Roho Mtakatifu kama muhuri wa ahadi. Amina. Hayo sio maziwa ya mtindi sasa, enyi watoto.
Sasa kumbukeni, lichukueni, liaminini. Weka imani yako na uifungue huko na Mungu, naye Roho Mtakatifu atakuja juu yako. Aliahidi jambo hilo. Halafu, ndugu, ibilisi alionekana kama jamaa mdogo.
MKATE WA KILA SIKU
Naye aliipokea dalili hii ya kutahiriwa, muhuri ya ile haki ya imani aliyokuwa nayo kabla hajatahiriwa; apate kuwa baba yao wote waaminio, ijapokuwa hawakutahiriwa, ili na wao pia wahesabiwe haki;
Warumi 4:11
25-1129
65-1205 – Mambo Yatakayokuwapo
Sasa kumbukeni, tunautukuza sana mwili huu. Tunauvalisha nguo nyingi sana. Tunafanya mambo mengi, ambayo, si ya lazima, kubadili nguo baada ya nguo baada ya nguo, takataka zote hizo. Na—na, loo, kila mtu tu!
Hebu acha tu mtu fulani anaanza kitu fulani. Mtu paka vipandio vyako rangi nyekundu basi waone akina Jones wakivipaka vyao rangi nyekundu. Hebu badilisha kutoka Chevrolet ununue Ford, nao kamwe hawawezi kuvumilia jambo hilo. Ni wakati wa watu kujilinganisha na wengine. Hebu ninii…Acha mwanamke fulani aje kanisani, amevaa namna fulani ya kofia, waangalie wanawake wote wakiinunua hiyo; hasa mke wa mchungaji, unaona, hebu angalia tu jambo linalotukia. Sasa, hilo ni kweli. Huo ni ukweli kabisa. Ni wakati wa watu kujilinganisha. Ndugu, unapaswa kuwa ni wakati wa kujilinganisha. Na hao wote—mambo hayo yote ni—ni kwa kusudi fulani.
Sijali kama koti langu linafanana na suruali yangu ndefu. Nami nina wakati mgumu. Mke wangu ama mkaza mwana, mtu fulani, aniambie ni—nivae tai ya namna gani nayo. Si—sijali kama zinafanana, hata hivyo. Ninataka kupasika kwangu kulingane na Neno la Mungu. Hilo ndilo lipaswalo, maana hapa ndipo mahali ninapokusudia kuishi; si kule chini pembeni pamoja na akina Jones, bali huko ng’ambo Utukufuni aliko Yesu, aliyeenda kutuandalia mahali. Naam, tunataka jambo hilo. Naam, bwana.
MKATE WA KILA SIKU
Na mavazi, ya nini kuyasumbukia? Fikirini maua ya mashamba, jinsi yameavyo… Mathayo 6:28
25-1128
64-1221 – Kwa Nini Ilibidi Iwe Ni Mchungaji Wa Kondoo
Naam, hiyo ndiyo sababu Musa alijua Sauti hii iliyokuwa imesema naye, ilikuwa ni Sauti ya Neno. Yeye alijua ya kwamba Mungu alikuwa amemwambia Ibrahimu, “Uzao wako utakuwa mgeni kwa muda wa miaka mia nne, bali nitawakomboa.” Naye alijua hiyo miaka mia nne ilikuwa imekwisha na alikuwa ameitwa kufanya hivyo.
Enyi wanaume kwa wanawake, Mungu aliahidi katika siku hizi za mwisho ya kwamba Yeye angewamwagia watu wote Roho Yake. Aliahidi angetuma Ubatizo wa Roho Mtakatifu, Naye angemwita Bibi-arusi bila waa wala kunyanzi. Aliahidi kufanya hivyo, Yeye atafanya. Usiwasikilize hawa wachungaji wa kukodishwa, watakupoteza. Roho Mtakatifu ndiye Mchungaji wa kukulisha chakula cha kondoo kutoka kwenye Neno hili. Daima linakuja kwa Mchungaji. Yeye ndiye Mchungaji wetu. Msikieni, ninyi ni kondoo wa zizi Lake; kama ndivyo mlivyo, mnaisikia Sauti Yake. Si yale mtu mwingine yeyote asemayo, mnasikia yale asemayo. Sauti ngeni, hamna habari nayo.
MKATE WA KILA SIKU
Maneno yako yalionekana, nami nikayala; na maneno yako yalikuwa ni furaha kwangu, na shangwe ya moyo wangu; maana nimeitwa kwa jina lako, Ee Bwana, Mungu wa majeshi. Yeremia 15:16
25-1127
61-1231M – Huna Budi Kuzaliwa Mara Ya Pili
Na kukukaribia kuzaliwa huku, inakubidi kupitia hatua fulani. Ni kama tu vile chochote kilicho hai, chochote kinachoishi tena, hakina budi kufa kwanza. Wala huwezi kudumisha roho yako ile ile. Huwezi kudumisha tabia zako zile zile. Huwezi kudumisha mawazo yako yale yale. Huna budi kufa. Huna budi kufa kama Yeye alivyokufa! Huna budi kufa madhabahuni Pake, kama Habili alivyofanya na mwana-kondoo wake. Huna budi kufa pamoja na Mwana-kondoo wako. Huna budi kufa. Kufia mawazo yako mwenyewe, upate kuzaliwa kwenye mawazo Yake, kuacha nia iliyokuwa ndani ya Kristo iwe ndani yako. Huna budi kuyawaza mawazo Yake. Na sasa, ndugu, dada, hebu niseme hili kwa akili kadiri nijuavyo kulisema. Unawezaje kuyawaza mawazo Yake kisha ulikane Neno Lake, na hata hivyo udai umezaliwa mara ya pili? Hebu jiulize tu swali hilo. Unawezaje? Huwezi. Kama umezaliwa mara ya pili, unayo mawazo Yake. Endapo nia ya Kristo iko ndani yako, basi wewe ni kiumbe kipya.
MKATE WA KILA SIKU
Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya. 2 Wakorintho 5:17
25-1126
53-0729 – Maswali na Majibu Juu ya Kitabu Cha Mwanzo
Kama nilienda mezani kwako na kuketi pale, nawe ukasema, “Mhubiri karibu ule pamoja nami,” naamini unanipenda. Na una maharagwe na viazi na karati na kuku iliyokaangwa na sambusa ya boga na maziwa ya mtindi, kila kitu kimewekwa pale. Basi, naamini ningekaribishwa tu viazi jinsi ningalikaribishwa maharagwe. Jambo ni kwamba, naamini ningekaribishwa kuku kama nilivyokaribishwa sambusa. Vyote viko mezani. Na kitu pekee kinipasacho kufanya ni kusema, “Waweza nisogezea sambusa tafadhali?” Nami naamini kwa moyo mzuri na mkunjufu, upendo wako kwangu, ungesema, “Naam, ndugu yangu, chakua kipande kikubwa kitamu.” Sivyo? Kama ningesema, “Tafadhali nisogezee viazi?” “Naam, hakika, ndugu yangu, hivi hapa”
Na kila baraka ya ukombozi ambayo Yesu Kristo aliifia na kuinunua katika utakaso Wake Kalvari, iko mezani na kila mwamini anaketi mbele yake. Haleluya! Kama nahitaji uponyaji, nitasema, “Baba, nisogezee uponyaji,” nami naumwaga kwenye sahani yangu na kula kikubwa…Naam, ukitaka kufa kwa njaa, endelea.
MKATE WA KILA SIKU
Basi ikiwa ninyi, mlio waovu, mnajua kuwapa watoto wenu vipawa vyema, je! Si zaidi sana Baba yenu aliye mbinguni atawapa mema wao wamwombao? Mathayo 7:11
25-1125
53-0507 – Matarajio
Sikilizeni hili enyi watoto. Neno la Mungu lita-litamshinda Shetani popote pale, mahali popote, kwa hali yoyote, wakati wowote.
Wakati Yesu alipokuwa hapa Yeye alikuwa Mungu. Mungu alikuwa ndani ya Kristo akiupatanisha ulimwengu na nafsi Yake, lakini Yeye hakutumia kamwe mojawapo ya karama Zake. Alipokutana na Shetani, aliushusha sana Ufalme wa Mungu, hata Mkristo aliye dhaifu sana anaweza kuutumia. Wakati Shetani alipomjia Yeye na kusema, “Ikiwa wewe ni Mwana wa Mungu, yaamuru mawe haya…”
Yeye akasema, “Imeandikwa.” Neno. Akamchukua, akajaribu kulipiga msasa Neno. Naye Yesu akasema, “Na pia imeandikwa.”
Akampeleka juu ya kilele cha mlima, akasema, ilimbidi azitazame falme hizi zote, “Nitakupa wewe hizo kama utaniabudu.”
Yeye akasema, “Imeandikwa.” Hilo hapo.
Na imeandikwa, “Yo yote myaombayo mkisali, aminini kwamba mnayapokea; yatakuwa yenu.” Basi mshinde Shetani kwa Neno la Mungu.
MKATE WA KILA SIKU
Amin, nawaambieni, Ye yote asiyeukubali ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo hatauingia kabisa. Marko 10:15
25-1124
61-0903 – Vivyo Hivyo Nuru Yenu na Iangaze Mbele ya Watu
Nina mtoto mchanga Utukufuni, ambaye aliwekwa wakfu tu, hakubatizwa.
Kwa sababu, ubatizo ni kwa ajili ya ondoleo la dhambi, unaona, kuonyesha ya kwamba wewe umetubu. Mtoto huyo mchanga hajafanya jambo lo lote la kutubia. Ni mtoto mchanga, ndiyo kwanza tu azaliwe hapa ulimwenguni. Hana nguvu za kujia hapa, unaona, na wala hana dhambi. Kristo alipokufa Msalabani, alikufa apate kuondoa dhambi ya ulimwengu. Mpaka mtoto huyu mchanga atakapofanya jambo fulani la kutubia, Damu ya Yesu Kristo inamfanyia upatanisho.
Lakini sasa mama na baba, wazazi, wana haki ya kumleta huyo mtoto mdogo, na kumtoa kwa Mungu, huyo mtoto mchanga waliyepewa na Mungu.
MKATE WA KILA SIKU
Kilichozaliwa kwa mwili ni mwili; na kilichozaliwa kwa Roho ni roho.
Yohana 3:6
25-1123
63-0901M – Ile Ishara
Na katika Yeye hamna mauti. Katika Yeye hamna huzuni. Katika Yeye hamna uchovu. Katika Yeye hamna dhambi. Katika Yeye hamna magonjwa. Katika Yeye hamna mauti. Tumo ndani Yake! Shetani akijaribu kukupa kitu fulani, kama magonjwa, chukua Ishara yako na kuipaka. Jamani! Chukua Ishara yako na kuipaka, ya kwamba wewe ni mali iliyonunuliwa ya Yesu Kristo. Ishara inaonyesha ya kwamba nauli yako imelipwa.
Asemapo, “Unapokufa, umepotea.”
Sema, “Umekosea. Nina mali iliyonunuliwa. Mimi ni mali iliyokwisha nunuliwa. Nina Ishara.”
“Ishara ni nini?”
Yeye anajua ni nini. Usi-, usicheze naye. Anajua ni nini. Naam, huenda ukanena na baadhi ya hawa wahubiri, nao wangebishana nawe. Si shetani; yeye anajua vema zaidi. Unaona? Ndivyo, hasa. Yeye aliipinga, mara mbili tatu, mwajua, na kufanya kosa, kwa yale majaribio. Shetani anajua unayonena. Mwonyeshe tu hiyo Ishara, ataruka aende. Naam.
Kwa sababu, ni nini? Ni mali iliyotiwa muhuri. Hawezi kuvunja huo, na kutoa kitu mle ambacho ni kizuri. Sema, “Ondoa mikono yako! Mimi nimetiwa muhuri.” Lo, jamani! Mali iliyotiwa muhuri! Naam, bwana! Umekwisha kununuliwa. Shikilia Ishara juu ya imani yako isiyotikisika katika ahadi Yake. Mwangalie akiondoka.
MKATE WA KILA SIKU
Akatufufua pamoja naye, akatuketisha pamoja naye katika ulimwengu wa roho, katika Kristo Yesu; Waefeso 2:6
25-1122
64-1227 – Mnasema Huyu Eti Kuwa Ni Nani?
Sasa kumbukeni, watu hawa walifurahia hizo baraka. Walifurahia mahubiri ya nabii huyu, huyu mtiwa mafuta. Walimwamini. Walimfuata. Lakini kulitokea huko jangwani, mtu jina la—lake Dathani, na mwingine jina lake Kora. Nao wakasema, “Hii haina budi kuwa ni kazi ya mtu mmoja. Musa anafikiri yeye ndiye pekee aliyeitwa na Mungu.”
Huo Ujumbe wa mtu mmoja, hawakuutaka. La, hawakuutaka. Wala Mungu kamwe hakushughulika ila na mtu mmoja kwa wakati mmoja. Daima ni Ujumbe wa mtu mmoja. Ni wakati gani alipopata kushughulika na watu, nje ya mtu mmoja tu? Ni mtu binafsi. Si kundi. Wewe unawajibika kwa Mungu, kila mmoja wenu. Unasema, “Loo, ninaamini jambo Hilo.” Unaninii tu…Unachofanya, unalifurahia tu. Unafurahia wazo fulani.
MKATE WA KILA SIKU
Yule mwanamke akamwambia, Bwana, naona ya kuwa u nabii!
Yohana 4:19
25-1121
56-1207 – Vipawa
Sasa, Mungu akikaa ndani ya Kristo alitumia sauti yake kunena kwayo. Yesu alisema katika muujiza wake, “Amin, amin, nawaambia, Mwana hawezi kutenda neno mwenyewe, ila lile ambalo amwona Baba analitenda, ndilo atendalo Mwana vile vile. Je, hiyo ni kweli? Yohana Mtakatifu 5:19.
Kisha Hakutenda jambo lolote kwa nafsi yake. Hakuna nabii aliyewahi kutenda lolote kwa nafsi yake, mpaka kwanza Mungu alipoonyesha la kufanya. Ni kosa la namna gani Musa alilofanya wakati alipotoka bila ono la Mungu na kumpiga yule Mmisri, akafikiri angewakomboa kwa mikono yake, kwa maana alifikiri alikuwa na imani nyingi na angeweza kufanya jambo hilo, kwa kuwa alikuwa ameitiwa kazi hiyo.
Haijalishi umeitiwa kazi hiyo jinsi gani, inapaswa Mungu kuongoza. Unaona? Alishindwa na elimu yake yote na akili yake ya kijeshi na mafunzo yake kama kiongozi mkuu wa Misri. Lakini hata hivyo ilishindikana, kwa sababu Mungu alikuwa anao mpango nasi hatuna budi kutenda kulingana na mpango wa Mungu. Haijalishi nini tunafanya, sisi ni werevu kiasi gani, hatuna budi kujinyenyekeza na kutenda kulingana na mpango wa Mungu. Amina.
MKATE WA KILA SIKU
Neno niwaagizalo lo lote liangalieni kulifanya; usiliongeze, wala usilipunguze. Kumbukumbu 12:32
25-1120
56-1207 – Vipawa
Sasa, Mungu akikaa ndani ya Kristo alitumia sauti yake kunena kwayo. Yesu alisema katika muujiza wake, “Amin, amin, nawaambia, Mwana hawezi kutenda neno mwenyewe, ila lile ambalo amwona Baba analitenda, ndilo atendalo Mwana vile vile. Je, hiyo ni kweli? Yohana Mtakatifu 5:19.
Kisha Hakutenda jambo lolote kwa nafsi yake. Hakuna nabii aliyewahi kutenda lolote kwa nafsi yake, mpaka kwanza Mungu alipoonyesha la kufanya. Ni kosa la namna gani Musa alilofanya wakati alipotoka bila ono la Mungu na kumpiga yule Mmisri, akafikiri angewakomboa kwa mikono yake, kwa maana alifikiri alikuwa na imani nyingi na angeweza kufanya jambo hilo, kwa kuwa alikuwa ameitiwa kazi hiyo.
Haijalishi umeitiwa kazi hiyo jinsi gani, inapaswa Mungu kuongoza. Unaona? Alishindwa na elimu yake yote na akili yake ya kijeshi na mafunzo yake kama kiongozi mkuu wa Misri. Lakini hata hivyo ilishindikana, kwa sababu Mungu alikuwa anao mpango nasi hatuna budi kutenda kulingana na mpango wa Mungu. Haijalishi nini tunafanya, sisi ni werevu kiasi gani, hatuna budi kujinyenyekeza na kutenda kulingana na mpango wa Mungu. Amina.
MKATE WA KILA SIKU
Neno niwaagizalo lo lote liangalieni kulifanya; usiliongeze, wala usilipunguze. Kumbukumbu 12:32
25-1119
57-0126B – Ripoti ya Safari ya India
Lakini ninayo matumaini zaidi kwenu ninyi ndugu hapa asubuhi ya leo, kwamba mtakuwa watu wa Mungu mnaodumu na Neno la Mungu. Na kuacha kila kitu kingine kianguke kulia na kushoto, lakini mdumu sawa na Neno hilo. Usisogee. Haijalishi kama wewe ni janvi la mlangoni nje hapo, kuwa janvi zuri la mlangoni. Usijaribu kushindana na mtu mwingine ama kufanya hivi. Wewe ingia tu moja kwa moja katika Neno, na ukae papo hapo, Naye Mungu atakuweka mahali pako katika Ufalme Wake, mahali unapoweza kuwa bora zaidi.
Vipi kama kidole changu kingewazia tofauti, kwa sababu hakikuwa jicho, Je! kisingekuwa kidole tena? Ningechukia kukipoteza kidole hicho. Ingawa jicho langu laweza kuwa na thamani zaidi, lakini akipenda hicho kidole. Ni sehemu yangu. Mnaelewa kile ninachomaanisha? Nina hakika mnaelewa. Kwa hivyo ofisi yoyote, chochote kile, kuwa chochote ulicho. Na mahali pako ambapo Mungu amekuweka, kaa hapo na uwe mwaminifu kwa Neno hilo kadri ujuavyo. Mungu atalibariki hilo. Kama akiwazia kitu kingine, Yeye atakuweka mahali anapohitaji.
MKATE WA KILA SIKU
Lakini kama vyote vingekuwa kiungo kimoja, mwili ungekuwa wapi?
Lakini sasa viungo ni vingi, ila mwili ni mmoja.
1 Wakorintho 12:19-20
25-1118
63-0428 – Tazama
Imani imenuiwa kuona mapenzi na matakwa ya Mungu. Hakuna maarifa yanayoweza kufanya hivyo. Imani pekee imenuiwa, na ikapewa jamii ya wanadamu, kutambua kuwa mapenzi ya Mungu ni nini.
Nawe ukiichukua imani yako uliyo nayo, nayo hailengi kwenye Neno, basi achana nayo. Una imani isiyo sawa.
Lakini wakati imani yako uliyopewa na Mungu inapokulenga kwenye Neno la Mungu, wewe uko moja kwa moja mstarini na umelengwa kikamilifu. Loo, jamani! Mungu na atusaidie kwenye saa hii, saa kuu tunayoishi. Imani, iliyonuiwa kuona anachotaka Mungu! Unakiona vipi? Kupitia kwa kamera ya Neno Lake, ahadi Yake. Huu ni ufunuo mkamilifu wa Yesu Kristo.
MKATE WA KILA SIKU
Mwishindanie imani waliyokabidhiwa watakatifu mara moja tu.
Yuda 1:3
25-1117
50-0115 – Je! Unasadiki Hayo?
Kuzaliwa kwake, wakati Yesu alipozaliwa duniani, alikuwa na alama nyeusi kwa kuanzia. Daima alipokelewa na watu wa kawaida, na alidharauliwa zaidi na—madhehebu ya kidini ya watu katika siku hizo, na—na watu wakuu wa tabaka la juu na wenye kiburi. Na ni kama jinsi iyo hiyo leo hii pia. Ni jambo lile lile.
Si kwamba ninajaribu kusema kwamba watu matajiri ama wa tabaka la juu hawawezi kuokolewa; wanaweza, ikiwa watajinyenyekeza na kuja kama hao wengine wote. Lakini lazima sote tuje kwa njia moja: hiyo nikuja, tukijua kwamba sisi si kitu na Yeye ndiye yote; na kuwa tayari kujisalimisha Kwake ili tupate manufaa kutoka Kwake.
Ikiwa utawahi kupata kitu chochote kutoka kwa Mungu, huna budi kujinyenyekeza na kuwa si kitu mbele Zake, na usijue lolote, bali kusudi moja; yaani, unajaribu kumpata Yesu. Ndipo unapojinyenyekeza, Mungu atakuinua. Lakini unapojiinua, Mungu hana budi kukushusha. Hiyo ni kweli. Alisema hivyo katika Neno lake.
MKATE WA KILA SIKU
Kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa. Luka 14:11
25-1116
54-0103E – Maswali na Majibu #2
Naam! Pia, nataka kujua nini maana ya “yasiyo na maana.” “Yasiyo na maana—jiepushe na maneno yasiyo na maana, kwa kuwa wataendelea zaidi katika maovu.”
Sasa, jambo la kwanza ni “maneno yasiyo na maana kwa kuwa wataendelea.” Sasa, cho chote kilicho cha kale—kinaendelea tu kupayuka. Biblia ilisema—Yesu alisema, “Bali ‘ndiyo’ yetu iwe ‘ndiyo’ na ‘siyo’ yetu iwe ‘siyo’ kwa kuwa yazidiyo hayo yataleta dhambi.” Haiwapasi hata kufanya mizaha na kuchekeshana ninyi kwa ninyi. Mungu atakuhukumia kila neno lisilo maana unalonena. Mwajua hilo? Biblia ilisema kuwa itakupasa uhukumiwe kwa kila neno lisilo maana. Kwa hivyo yatupasa tuwe watu wa jinsi gani? Watu wanyofu, thabiti, wanaopendana, wakarimu, na wala si kundi la wapumbavu, kila mara kuendelea…
MKATE WA KILA SIKU
Jiepushe na maneno yasiyo na maana, ambayo si ya dini; kwa kuwa wataendelea zaidi katika maovu. 2 Timotheo 2:16
25-1115
55-0817 – Yehova-Yire
Na ndugu yangu, Ambaye tayari amemtoa katika Yesu Kristo, Mwana-Kondoo aliyechinjwa tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu, ametolewa kwa ajili ya ugonjwa wako usiku wa leo. Ameliandika jambo hilo Kitabuni. Amemtuma Roho Mtakatifu. Ameziweka karama Kanisani. Sasa, si kosa la Mungu; itakuwa ni kutokuamini kwetu wenyewe. Je, hiyo si ni kweli? Tusipolipokea, si kosa la Mungu. Je, unaliamini hilo kwa moyo wako wote, kwamba Yesu Kristo ametolewa kama Mwana-Kondoo aliyechinjwa tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu kwa ajili ya—kwa ajili ya wokovu wako na uponyaji. unaliamini hilo? Inua mkono wako.
MKATE WA KILA SIKU
Hakuna aliye na upendo mwingi kuliko huu, wa mtu kuutoa uhai wake kwa ajili ya rafiki zake. Yohana 15:13
25-1114
64-0307 – Ushuhuda Baharini
Kama ulikuwa na mvulana mdogo aliyeketi kule nje barabarani, nawe ukasema, “Kadogoo, kipenzi, afadhali uingie, kipenzi. Huenda ikawa, sijui, labda watakukanya-kanyaga.” Humpendi mtoto huyo. Hiyo ni kweli. Utatoka uende kule umpige kwelikweli, ama umlazimishe aingie. Hiyo ni kweli. Unampenda.
Hivyo ndivyo Injili ilivyo. Mungu anakupenda. “Na hao ambao anawapenda, Yeye huwarudi na humpiga kila mwana amkubaliye.” Kama hamwezi kuvumilia marudio, mnaondoka na kukasirikia jambo hilo, basi ninyi ni watoto haramu, ninyi si watoto wa Mungu. Kwa hiyo kumbukeni tu, ni Maandiko tu.
Sasa neno moja kutoka Kwake, neno moja, litamaanisha zaidi ya yale ningeweza kusema, nyakati milioni moja za muda wa uhai. Ni Yeye. Tunajua ahadi Yake. Tunajua alichoahidi kufanya.
MKATE WA KILA SIKU
Tazama, yu heri mtu yule Mungu amwadhibuye; Kwa hiyo usidharau kurudiwa na huyo Mwenyezi: Ayubu 5:17
25-1113
63-0803E – Ushawishi
Naamini ilikuwa Paulo aliyesema “Sisi ni barua zilizoandikwa za Mungu, zinazosomwa na watu wote.” Unapokuwa barabarani, unapokuwa kazini mwako, na popote ulipo, mtu fulani yu akutazama.
Na zaidi sana baada ya kusema na kukiri ya kwamba wewe ni Mkristo, wao watakuchunguza kwa makini zaidi, na hilo hutoa ushawishi kwa—kwa watu walio karibu nawe. Na inatubidi kuchunguza tunayofanya. Kwa maana, kama tukitoa ushawishi mbaya, basi tunasababisha shutuma, si sana kwetu sisi, bali juu ya yale tunayodai kuwa, Wakristo, tunaileta juu ya Kristo. Na hamna ye yote, ikiwa tungaliwazia, hangalitaka kuleta shutuma juu ya Kristo. Bali tendo baya, wakati usiofaa, bila shaka litasababisha sifa baya kwa mtu anayekutazama. Na kila mtu huchunguzwa, unapokiri kuwa Mkristo.
MKATE WA KILA SIKU
Nami nawaambia, kila atakayenikiri mbele ya watu, Mwana wa Adamu naye atamkiri yeye mbele ya malaika wa Mungu:
Luka 12:8
25-1112
63-1128E – Ile Ishara
..popote ulipo, saa imewadia. Na kila mtu anaweza kuona ubutu wa kanisa leo hii. Kila mtu anaweza kuona kupooza kwa wengi, wengi sana wa washiriki. Ni kwa sababu kwamba mmecheza, mmechukua misisimko na mmechukua mambo mengine. Pia mmetumaini juu ya hekima ya mwanadamu fulani, juu ya theolojia ya dhehebu fulani, juu ya kuwa mshiriki wa kanisa la mama yako, na juu ya mchungaji fulani mwaminifu. Lakini yote ni mambo mazuri, sina kitu dhidi yao, si zaidi ya jinsi tohara ilivyokuwa kwa Myahudi, bali hiyo haikuwa ni mpango wa Mungu. “Nionapo damu,” na hiyo pekee!
Basi leo hii Roho Mtakatifu ni agano la Mungu na watu wa Mungu wa agano. Roho Mtakatifu, Uhai wa Kristo aliyefufuka, hauna budi kuwekwa hadharani kanisani miongoni mwa watu, ukimfanya Yeye “yule yule jana, leo, na hata milele.”
MKATE WA KILA SIKU
Amewapelekea watu wake ukombozi, Ameamuru agano lake liwe la milele, Jina lake ni takatifu la kuogopwa. Zaburi 111:9
25-1111
54-1114 – Ukombozi Kwa Hukumu
Majaribu yanakuja, hakutakuwa na jaribu isipokuwa Yeye atakupa neema ya kulistahimili. Naye ameahidi kukutana nawe kwenye kila uwanja wa vita, papo hapo, na kusimama mahali pako. Hivyo basi, hapo ndipo tumaini lako lilipo.
Unafikia mahali, unasema, “Vema, Ndugu Bill, yako…Nina majaribu mengi sana.”
Niambie Mkristo mmoja ambaye hana majaribu. Hatuji kwenye pikiniki, tumekuja kwenye uwanja wa vita, tuko hapa kupigana na adui. Mbona hakika, hatuzivai silaha zetu ili tu kutazamwa. Kama unakuwa Mkristo, ili tu kutazamwa, basi wewe, naam, mbona, ninaofia umeingia mahali pasipofaa.
MKATE WA KILA SIKU
Jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu; ila Mungu ni mwaminifu; ambaye hatawaacha mjaribiwe kupita mwezavyo; lakini pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea, ili mweze kustahimili. 1 Wakorintho 10:13
25-1110
59-1128 – Mlango wa Moyo
Sasa, hebu tuangalie ndani ya moyo wa mwanadamu, ikiwa una milango ndani ya mlango. Sasa, watu husema, “Yesu, njoo moyoni mwangu, kwa sababu sitaki kwenda kuzimuni ninapokufa. Ninataka kukukubali Wewe kama Mwokozi wangu, lakini sitaki Wewe uwe Bwana wangu.”
Sasa, hapo kuna tofauti kabisa. Anaweza kuwa Mwokozi wako na bado asiwe Bwana wako. Wakati Yeye ni Bwana, Yeye ni Bwana juu ya yote. Kila sehemu yako, Yeye ni Bwana, amekaribishwa mahali popote moyoni mwako.
MKATE WA KILA SIKU
Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami. Ufunuo 3:20
25-1109
65-0718E – Chakula Cha Kiroho Kwa Wakati Wake
Yule mjumbe, ule Ujumbe—Ujumbe, na Neno, walikuwa mmoja kabisa. Nabii, Neno, Ujumbe; mjumbe, Ujumbe, na Ujumbe, walikuwa mmoja. Yesu alisema, “Kama sizitendi kazi nilizoandikiwa, basi msiniamini.” Hilo ni zuri. Mtu ye yote na ujumbe wake ni mmoja.
Hiyo ndiyo sababu ya kwamba leo wao hawaamini katika kuzitenda kazi za Mungu, kwa sababu wao hawaukubali Ujumbe wa Mungu. Wao hawaumini Ujumbe.
Lakini wale wanaoamini saa ya Mungu tunayoishi, mambo haya ni Chakula kilichofichwa. Hebu wazieni tu, Mungu ameficha Hilo kiasi kwamba ingawa wao wanaliangalia moja kwa moja hata hivyo hawalioni. Jinsi ile ile Eliya alivyolipofusha jeshi la Shamu. Jinsi ile ile Mungu anavyompofusha asiyeamini asione Chakula halisi cha mtoto, mwamini.
MKATE WA KILA SIKU
Lakini yule asiyeamini akiondoka, na aondoke. 1 Wakorintho 7:15
25-1108
53-0508 – Mungu Akimwagiza Musa
Mtu fulani siku ile, akifundisha, alisema, akizungumza kuhusu Apolo, Juu pale, yule mhubiri mzuri wa Kibaptisti. Paulo alimwendea akasema, “Loo, ndiyo, wewe ni jamaa mzuri, lakini je, umempokea Roho Mtakatifu tangu ulipoamini?”
Akasema, “Loo, loo, mimi—nilidhani nilimpokea Roho Mtakatifu nilipoamini.” Bado wangali wanafundisha hilo, lakini ni makosa. Imani ni sawa. Imani ni nzuri sana. Imani ina… Ibrahimu alimwamini Mungu, na ikahesabiwa kwake kwa, au, kwa ajili ya haki, lakini Mungu akampa muhuri wa tohara kama muhuri wa imani yake.
Ndugu, unapokuwa na imani halisi na ya kweli katika Mungu, Mungu atakupa ubatizo wa Roho Mtakatifu kama muhuri wa ahadi, ambayo ni muhuri, kwamba unayo imani. Unaweza kufanya—a—aina fulani ya hisia, au kuwafanya watu waamini, au unaweza kusema una imani, lakini unapokuwa kweli na imani halisi isiyoghoshiwa, Mungu atakupa ubatizo wa Roho Mtakatifu kama muhuri wa ahadi. Amina. Hilo si maziwa ya mtindi, enyi watoto.
Sasa kumbukeni, lichukueni, liaminini. Wekeni imani yenu na muifungie huko pamoja na Mungu, naye Roho Mtakatifu atawashukia. Yeye aliliahidi hilo. Basi, ndugu, ibilisi alionekana kama kajamaa kadogo mno.
MKATE WA KILA SIKU
Naye aliipokea dalili hii ya kutahiriwa, muhuri ya ile haki ya imani aliyokuwa nayo kabla hajatahiriwa; apate kuwa baba yao wote waaminio, ijapokuwa hawakutahiriwa, ili na wao pia wahesabiwe haki;
Warumi 4:11
25-1107
61-1224 – Mabwana, Sisi Tunataka Kumwona Yesu
Kama ukimgusia mwanafunzi, “Ningependa kumjua Bwana Yesu.”
“Vema, sasa angalia, sisi ni wafuasi wa kanisa fulani-fulani, shuka ukaungane na hilo, uungane nasi.” Mnaona? Ama, “Tulikuwa…Sisi ni wanachama wa shirika fulani hili, basi njoo ukajiunge na hilo.” Na hayo ndiyo unayosikia.
Lakini Kristo Mwenyewe aliwaelekeza watu kwa mauti Yake, na akasema, “Punje ya ngano isipoanguka ardhini, inakaa peke yake.”
Loo, jinsi ilivyo tofauti! Naam, bwana. Jinsi ilivyo tofauti! Bali maisha yako na Uzima Wake hupatana, sio kanisani, sio katika jengo, sio katika kanuni ya imani, sio katika matendo mema, bali msalabani ambapo unasulubiwa pamoja na Yeye. Hapo ndipo unapompata Kristo. Humpati Yeye kwa kufanya vema zaidi, kufungua ukurasa mpya. Kuanza maisha mapya, humpati Kristo. Unampata Kristo katika mauti pekee; sio katika hori, sio katika kuungama. Kuamini katika kanuni fulani za imani na hekaya, humpati Kristo huko.
Mtumishi wa kweli hukupeleka Kwake, na Yeye ni Neno.
MKATE WA KILA SIKU
Amin, amin, nawaambia, Chembe ya ngano isipoanguka katika nchi, ikafa, hukaa hali iyo hiyo peke yake; bali ikifa, hutoa mazao mengi.
Yohana 12:24
25-1106
61-0903 – Vivyo Hivyo Nuru Yenu na Iangaze Mbele ya Watu
Lakini ni kama vile mtu ungalikuwa na gari kuu kuu na ulikuwa unapanda mlima, nami nilijua wakati ulipoanza kuteremka upande wa pili hukuwa na breki. Mimi nisingekuwa na kitu dhidi ya mtu huyo, ninayapigia makelele. Si yeye. Ni lile gari alilopanda. Ataumia.
Na hivyo ndivyo ilivyo kuhusu madhehebu. Ninafikiri watu wanaoshikilia madhehebu hayo, kana kwamba yalikuwa ni Mungu Mwenyewe, nao wanaliacha Neno la Mungu, wapate tu kushikilia madhehebu. Vema, wanapofanya jambo hilo, ninasikitika watafanya kosa baya sana. Na si kwamba mimi nina jambo lo lote dhidi ya mtu huyo, bali ni huo mtumbwi aliopanda, unaona, nina hakika hatamaliza safari. Madhehebu hayatafaulu kamwe, bali Kristo atafaulu. Kwa hiyo toka tu kwenye—kwenye huo mtumbwi unaovuja wa umadhehebu, uingie kwenye Meli ya salama ya Sayuni, ile Meli ya kale ambayo bado haijashindwa kamwe kutua pwani mapema, Kristo.
MKATE WA KILA SIKU
kwa sababu nimesema nao, wasinisikilize; nimewaita, wala hawakuniitikia. Yeremia 35:17
25-1105
52-0713A – Uzoefu Wa Awali Wa Kiroho
Mungu wa Agano la Kale alikuwa Yesu wa lile Jipya, na Roho Mtakatifu wa leo hii. Mnajua hilo. Huamini hilo? Kumkufuru Roho Mtakatifu leo, ni adhabu ile ile, au mbaya zaidi, kuliko kumkufuru Yesu Kristo, au Mungu Baba. Je, Huamini hilo?
Sasa, nini zaidi? Sasa, tazameni. Ikiwa ulimwengu unatuita wazimu. Ikiwa ulimwengu unadhani kwamba tuna ufahamu nusu juu hapa…Tazama. Kwa sababu ishara hizo zilionekana mahali nilipo, naye Malaika huyu wa Bwana, na kadhalika, hiyo haimaanishi kwamba ni mimi tu, enyi marafiki. Hilo lina maana gani? Mungu anajaribu kuwafikishia kitu gani? Anajaribu kuwafikishia jambo hili, kwamba ninawaambieni kweli.
MKATE WA KILA SIKU
Kisha akawaambia,Sikizeni basi maneno yangu;Akiwapo nabii kati yenu,Mimi,Bwana,nitajifunua kwake katika maono,Nitasema naye katika ndoto. Hesabu 12:6
25-1104
61-0521 – Utuonyeshe Baba
Nami ninawapenda tai, kwa sababu Mungu huwafananisha watoto Wake, urithi Wake, na tai, naye Mungu, Mwenyewe, anajiita Tai, Yeye ni Yehova Tai, Bapa Tai, sisi ni vifaranga vya tai Wake.
Tai anaweza kuruka juu zaidi kuliko ndege mwingine yeyote aliyepo. Kama mwewe angejaribu kumfuata, angechanganukia hewani, kwa hiyo ukijaribu kuiga Ukristo, unajipasua tu wazi, hivyo tu, haikufai chochote. Kuwa tai, uzaliwe mara ya pili, maumbile yabadilishwe, ndipo unaweza kupanda ngazi ya Yakobo, ndipo unaweza kupanda hadi mahali pa juu sana ambapo mambo yote yanawezekana kwa hao waaminio, bali huna budi kuwa tai, mwaminio.
Usijaribu…Waebrania walipovuka, kama tai, wakavuka Bahari ya Shamu, kule kupima, wakifuatilia, Wamisri wasiotahiriwa walijaribu kufanya hivyo nao wakapoteza maisha yao. Huwezi kuiga Ukristo, huna budi kuwa Mkristo. Hiyo ni kweli.
MKATE WA KILA SIKU
Maana yeye asiyekuwa na hayo ni kipofu, hawezi kuona vitu vilivyo mbali, amesahau kule kutakaswa dhambi zake za zamani.
2 Petro 1:9
25-1029
63-0901E – Kudhikika
Pia, angalia, yeye hakuwa mchoyo. Wakati Mungu alipomsikia, na akajibu maombi yake, na kumpa mwana, yeye alimrudishia Mungu mtoto huyo. Na kwa kuwa alikuwa tayari kutokuwa mchoyo baada ya Mungu kuyajibu maombi yake, Yeye alimpa nabii. Loo, hiyo ilikuwa ni baraka ya ziada. Loo, Yeye anavyo vingi, vitu hivyo vya ziada anavyotoa. Si mwana tu, lakini nabii. Wala hakukuwako na ono wazi kwa muda wa miaka mingi, mingi sana, katika Israeli. Samweli, nabii wa kwanza, kwa muda wa miaka mingi, mingi sana, kwa sababau mama fulani alidhikika; kwamba hangeweza kupata watoto, naye alikuwa amepita umri wa kuzaa, labda mwenye umri wa miaka sitini, sabini. Naye akaomba kwa kudhikika, hana budi kumpata mtoto huyu! Ilikuwa ni nini? Mungu alikuwa amenena naye, hapa na shaka.
Huwezi kudhikika mpaka Mungu anene nawe. Loo, Kanisa, amka na ujitikise! Finya dhamira yako, amka katika saa hii! Hatuna budi Kudhikika ama tutaangamia! Kuna jambo linalokuja kutoka kwa Bwana! Ninajua jambo hilo kwamba ni BWANA ASEMA HIVI. Kuna jambo linalokuja, na ni afadhali tudhikike. Ni kati ya uzima na mauti. Litapita katikati yetu wala hatutaliona.
MKATE WA KILA SIKU
Kwa maana wakati umefika wa hukumu kuanza katika nyumba ya Mungu; na ikianza kwetu sisi, mwisho wao wasioitii injili ya Mungu utakuwaje? 1 Petro 4:17
25-1028
63-0120E – Mara Nyingine Moja Tu, Bwana
Mungu aliliinua kanisa lipate kuwa ni mnara wa taa, kuziachilia nguvu Zake, kuwaponya wagonjwa, kuwafufua wafu, kuwatoa pepo, kuishi kitakatifu, kuihubiri Injili yote, kuidhihirisha, bali tunaanza kujipenyeza ndani na kushusha viwango.
Tulichukua mifano mibaya. Wanawake walimwiga mke wa mchungaji. Yeye alimwachilia aingie wazimu, kukata nywele zake, kuvaa namna yoyote ya nguo za kizinifu, kamwe hakumkemea. Nao hao wanawake wengine wanasema, “Kama Dada Nanii anaweza kufanya hivyo, mimi pia ningeweza.” Usimfanye huyo mfano wako. Unaona? Mungu alikwambia jambo la kufanya, dumu na Hilo.
MKATE WA KILA SIKU
Maana Mungu hakutuitia uchafu, bali tuwe katika utakaso.
1 Wathesalonike 4:7
25-1027
57-0825E – Waebrania, Mlango Wa Pili #2
Ninawatakeni mshuhudie. Biblia ilisema, “Kama akiinuka mmoja miongoni mwenu, naye aseme hivi na vile, wala halitimii, msisikilize, kwa kuwa sijanena. Lakini kama akinena kwa Jina Langu, na asemayo yaje kutimia, basi lisikieni.” Amina. “Kwa kuwa niko pamoja na nabii huyo, ama mhubiri, yeyote yule. Kama asemayo yakitimia, basi msikieni.”
Sasa, enyi wapendwa, hebu na tumsikie Yeye, Roho Mtakatifu akinena katikati yetu, akionyesha miujiza ya namna nyingi, na ishara, na maajabu. Hebu na tusiyapuuze kama tu mambo ya kawaida yanayotukia. Hebu na tukumbuke ya kwamba ni Yesu Kristo, yeye yule jana, leo, na hata milele; akithibitisha Neno Lake. Hatuna budi kufanya jambo hilo. Loo, nawasihi mfanye hivyo. Iweni waangalifu. Acheni kila kitu kingine kiwe ni cha pili, hata makazi yako, mumeo, mkeo, watoto wako. Chochote kile, kiweke nafasi ya pili. Mweke Mungu wa kwanza. Unasema, “Ndugu Branham, ati juu ya watoto wangu?” Juu ya kitu chochote kile. Mweke Mungu awe ni wa kwanza. Acha awe wa kwanza.
MKATE WA KILA SIKU
Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa. Mathayo 6:33
25-1026
58-0406S – Najua Mkombozi Wangu Yu Hai
Ni kusudi la Mungu kutupa Roho Mtakatifu aliyebarikiwa. Ni kusudi la Mungu kutuonyesha ishara na maajabu na miujiza. Ni kusudi la Mungu, na hakuna kinachoweza kuliharibu. Nguvu zote za kuzimu zinaweza kupigana nayo, lakini itashinda. Tuna ahadi ya Milele ya Mungu. Kunaweza kuwa na walimu, kunaweza kuwa na itikadi kuinuka, kunaweza kuwa na mipango mikubwa kuinuka, kunaweza kuwa na mambo ambayo yanaonekana kama kwamba ingeharibiwa, lakini haiwezi kuharibiwa kamwe. Ni kusudi la Mungu kuona kwamba itashinda. Kisha, sio juu yangu, na sio juu yako, ikiwa itaharibiwa au la. Ni juu ya Mungu. Nasi tunaweza kuwa na uhakika juu yake, ya kwamba Mungu hataacha urithi wetu uharibiwe, kwa maana ni kusudi Lake kutupa sisi.
MKATE WA KILA SIKU
Ndiye BWANA; na afanye alionalo kuwa ni jema. 1 Samweli 3:18
25-1025
50-0227 – Mungu Katika Watu Wake
Kuna chemchemi iliyo wazi, inayotiririka bure kila mahali. Kunywa tu mpaka utosheke kabisa. Mti, kama ukinywa tu kile ulichogawiwa, mbona, ungekuwa tu daima, ungali kwenye ukame. Hiyo ndiyo shida ya Wakristo. Hawanywi vya kutosha. Unatakiwa kunywa hadi uenee tu na kuruhusu mtu mwingine alione hilo. Unaona? Sukuma. Pata ushuhuda. Likabidhi kwa Mungu. Liamini. Lichukulie hatua. Dai ahadi ya Mungu. Likabidhi tu—likabidhi kwa Mungu. Liamini. “Umkabidhi Bwana njia zako.” Atalitimiza lolote utakalo.
Lakini Yeye hawezi kufanya hivyo mpaka…mradi tu umelishikilia. Kusema, “Sasa, nitaona kama mimi nina nafuu yoyote, na nione kama hili litatenda kazi.” Wewe likabidhi jambo hilo Kwake; sahau mengineyo kulihusu. Nenda ukishuhudia mambo hata usiyoyaona. Unaliamini. Si kile unachokiona; ni kile unachoamini. Si jinsi unavyohisi. Hakuwahi kusema, “Je! ulilihisi?” Yeye alisema, “Je, uliliamini?”
MKATE WA KILA SIKU
Umkabidhi BWANA njia yako, Pia umtumaini, naye atafanya.
Zaburi 37:5
25-1024
57-0901M – Waebrania, Mlango Wa Tatu
Kuna kitu fulani kuhusu ninii…mahali unakoenda, kanisa gani unalohudhuria, na mwalimu gani anayekufundisha. Je! ulijua jambo hilo? Hilo, kuna jambo fulani kwake. Kwa hiyo inatupasa kutafuta yaliyo bora sana tunayoweza kupata, ili kwamba tuwe tunapata yaliyo bora sana; si kwa sababu eti ni mambo yanayopendwa na watu wengi na kadhalika, bali ni mafundisho halisi la Biblia.
Angalia, wakati mmoja wakati Israeli walipokuwa wametoka wakaenda jangwani pamoja na majeshi yao, nao walikuwa wamepiga kambi siku saba, ndipo wakaishiwa na maji. Nao walikuwa karibu kuangamia, wakasema, “Loo, laiti kungalikuwa na nabii karibu!”
Ndipo mmoja wao akasema, “Tuna Elisha, hapa chini. Alimimina maji kwenye mikono ya Eliya.” Unaona wenzake? Kwa maneno mengine, “Huyu hapa Elisha ambaye amekuwa na uhusiano na Eliya. Neno la Bwana liko pamoja naye.” Unalipata? Alikuwa amefundishwa vizuri.
MKATE WA KILA SIKU
Niletewe nuru yako na kweli yako ziniongoze.
Zaburi 43:3
25-1023
56-0121 Ndani ya Pazia
Wakati upandwapo katika Kristo Yesu, kila kitu unachokihitaji katika safari ya duniani kiko ndani yako unapompokea Roho Mtakatifu. Na jambo pekee unalopaswa kufanya ni kunywa, kunywa, na kusukuma kutoka, kusukuma kutoka. Kunywa tu mpaka basi. Kama unauhitaji uponyaji wa Kiungu, nenda kwenye Neno la Mungu na unywe kutoka Kwake, mpaka utokeze. Ikiwa unamhitaji Mungu zaidi, wewe endelea tu kunywa, sukuma utokeze. Naye Kristo ndiye Chemchemi ya Uzima isiyokauka. Na kama umepandwa ndani Yake, jambo pekee unalopaswa kufanya, ni kuunywa wema Wake na kusukuma utokeze chochote unachokihitaji katika safari ya hapa duniani. Yote ni kunywa tu, kupumzika, amani. Sio kile unachohangaikia na kujitahidi na kuvuta, wewe-unashindana na kusudi hasa ambalo unaloliwakilisha unapofanya hivyo.
Ukristo si kitu fulani, Mungu si Mtu wa kumwomba kwa huruma, na kulia, na kusihi, na kufunga, na kufa njaa, na kila kitu kama hicho ili kumfikia.
MKATE WA KILA SIKU
Naye atakuwa kama mti uliopandwa Kandokando ya vijito vya maji, Uzaao matunda yake kwa majira yake, Wala jani lake halinyauki; Na kila alitendalo litafanikiwa.
Zaburi 1:3
25-1022
55-1120 – Ni Nini Hiyo Uliyo Nayo Mkononi Mwako?
Biblia hii ni Barua ya Mungu. Na kila ahadi iliyomo ndani Yake ni yako, kama unaweza kuiamini na kuikubali katika namna sahihi ya mtazamo. Iko ndani yako, tumaini lenye utukufu, Kristo.
Angalia. Sasa tunaingiaje ndani ya Kristo? Kwanza, tunampokea Yeye kwa imani, tukiamini. Pili, “kwa Roho mmoja, basi, sisi sote tulibatizwa kuwa Mwili mmoja,” Wakorintho wa Kwanza 12; kwa uanachama mmoja? kwa Roho mmoja sisi sote tulibatizwa kuwa Mwili mmoja. Hao ni waamini, ambao tayari wamemwamini Bwana Yesu Kristo wanabatizwa katika Mwili wa Kristo kwa Roho Mtakatifu mmoja. Hiyo ni kinyume kidogo na mafundisho ya Baptisti yangu, lakini hiyo ni Biblia.
Mimi ni Mbaptisti mradi tu inadumu katika Biblia; baada ya hapo mimi ni Biblia.
MKATE WA KILA SIKU
Akawauliza, Je! Mlipokea Roho Mtakatifu mlipoamini?
Matendo 19:2
25-1021
59-0823 – Tunutu, Nzige, Parare, Madumadu
Kwa hiyo, kama kuna shida kanisani siku hizi, kwamba haliendelei jinsi ipaswavyo, ni maoni yangu kwamba tunapaswa kurejea kwenye yale Maagizo, tujue shida iko wapi hasa, hata kanisa hili ni wagonjwa sana kwamba kuna ugonjwa kanisani mwetu, ugonjwa wa dhambi. Kisha inatupasa kujua ni nini Daktari aliagiza, na tuone kama wauza dawa wachungaji wetu wanatupa Maagizo sahihi.
Pia, kumbuka, unaweza kuongeza kitu fulani kwenye Maandiko yaliyobainiwa vizuri sana, na kumwua mgonjwa. Na labda, sisemi tumeongeza, lakini vipi kama baadhi ya wauza dawa wetu wameongeza kitu fulani kwenye Maagizo ya Mungu? Endapo wameongeza, wanamuua mgonjwa, wakiwaacha wafe katika dhambi.
MKATE WA KILA SIKU
Ndugu zangu wapenzi, msidanganyike. Yakobo 1:16
25-1020
56-0404 – Kutokosea Kwa Neno Lililonenwa la Mungu
Unajua, ni—nilikuwa nikiwaambia wavulana muda mfupi uliopita nikija, nilisema kuhusu jinsi ambavyo hatuna budi kuwa na furaha kila wakati. Mungu hataki uwe na huzuni. Unajua hasira mbaya hufanya nini? Na hiyo hasira ya kale, hiyo ni moja ya mambo ya kale ya kutisha. Na ni—ni kama asilimia sitini ya chanzo cha magonjwa yote ni hasira. Naam, bwana, hizo hasi—ghadhabu unazoachilia, kumbuka, unatengeneza tu kansa, kidonda, ama kitu kama hicho, unapofanya hivyo. Unapofura kuhusu mtu fulani, “Sitarudi kule tena. Ngoja niwaonyeshe.” Sawa. Kumbuka, wewe ndiye utakayelilipia hilo. Dumu mwenye furaha tu.
Hadithi ndogo, ilisema kulikuwa na robini mdogo asubuhi moja, ameketi juu ya kingo, akimpigia mluzi mwenzake mdogo. Yule mwenzake mdogo akaruka karibu yake na kusema, “Unajua, nina—ninayo wasiwasi sana asubuhi ya leo kuhusu jambo moja.”
Kasema, “Nini?” Kasema, “Sisi akina robini hatuwi kamwe na wasiwasi.”
“Lakini ninashangaa tu ikiwa wale viumbe maskini, wanadamu, ambao wamekunja nyuso zao, wanatembea, nashangaa, huenda hawana Baba wa mbinguni anayewaangalia kama sisi, akina robini.”
Hiyo ni kuhusu hilo. Hujawahi kumsikia mmoja wao ana shinikizo la damu, sivyo?
MKATE WA KILA SIKU
Furahini katika Bwana sikuzote; tena nasema, Furahini.
Wafilipi 4:4
25-1019
60-0712 – Msikieni Yeye
Mwanadamu hapimwi kwa misuli, huyo ni mnyama, mwanamume hupimwa kwa tabia. Nimewaona wanaume waliokuwa na uzito wa ratili mia mbili, na misuli yote, na hawakuwa na hata chembe ya uwanaume ndani yake, wakimtoa mtoto mchanga kutoka mikononi mwa mama yake na kumlawiti. Huyo si mwanamume, huyo ni mnyama, huyo ni mkatili, mwanamume ni tabia.
Kamwe hakukuwa na mwanamume kama Yesu Kristo, lakini Biblia ilisema hakuwa na uzuri hata tumtamani. Pengine ni Jamaa mdogo, aliyeinama mabega, ama cho chote kile, “na kama mtu ambaye watu humficha nyuso zao.” Lakini Yeye…hakukuwa na tabia kama hiyo, hivyo ndivyo mwanamume halisi alivyo. Humpimi mwanamume kwa misuli, bali kwa michubuko ya magoti katika suruali yake kwamba amekuwa akiomba, ndivyo unavyompima mwanamume, kwa tabia. Ni kweli.
MKATE WA KILA SIKU
Kwa sababu upumbavu wa Mungu una hekima zaidi ya wanadamu, na udhaifu wa Mungu una nguvu zaidi ya wanadamu.
1 Wakorintho 1:25
25-1018
55-0403 Gufatanya kubwo gucungurwa
Igikoko ntikigira ubugingo.
Ariko umuntu arafise ubugingo. Kandi naho bimeze gutyo, ubwo bugingo cari igice c’Imana. Ikiremwa gihambaye mu biremwa vyose vyo kw’isi, naho ari mu gihagararo c’uwaguye, ni umuntu. Kandi, igihe yashiraho ugufatanya hamwe n’Umuremyi wiWe, yaciye aba nk’umuntu wo hejuru kurushiriza, kubera ari umwana w’Imana. Yariko ariga ingene yomenya umuremyi wiwe, Umuremyi w’ibintu vyose. Hanyuma igihe uwo muntu ng’aho yamenya Umuremyi wiWe, yaciye aba igice c’umuremyi wiWe. Aca aronka ugufatanya n’Umuremyi wiWe. Kuva ubwo, Ijambo ryose ry’Imana ryaciye riba kuri we, Irinyakuri, rizima, kandi akanaryizera.
Ntibitangaje ko abantu badashobora kwizera ugukiza indwara kw’Imana uyu munsi. N’uko atakiri muri bo cobatuma bizera. Mu gihe Imana Itarinjira mu mutima w’Umuntu, umuntu ntaco amaze na gatoya kurya kw’igikoko. Kubwo ubwenge bwiwe, azokwiyumvira ati ; « Ni gute ibi vyoshoboka ? » Hanyuma ace arondera insiguro zose zishoboka zo kuRihakana.
Ariko igihe Imana Ironse ikibanza caYo mu mutima w’umuntu, ukwiyumvira kwose kurazimangana. Imana Ikaza imbere ya vyose. Amen.
Umutsima wa Buri Munsi
Ku musi Imana yaremeyek’ umuntu, mw ishusho yayo ni ho yamuremye;
Itanguriro 5:1
25-1017
61-0207 – Matarajio
Lakini mtakapokuja pamoja, loo, jamani, hilo ndilo jambo lenyewe, unapomtii Mungu kikamilifu, “ Hivyo watu wote watatambua ya kuwa ninyi mmekuwa wanafunzi wangu, mkiwa na upendo ninyi kwa ninyi.” Unapopata sehemu ya theolojia na kupata upendo mdogo mle, itafanya kazi, na maajabu, na—na miujiza, bali hatuna budi kuwa nao. Kwa nani? Kwa kila mtu.
“Loo, ati kwa kundi hilo la kale la Assemblies of God, ama hilo kundi la kale la Church of God, ama la kale la Umoja, au Utatu, au Utano, ama cho chote kile walicho nacho? Ati mimi niwapende? Siwezi kuwapenda, wao ni wapinga Kristo.” Umejipoteza mwenyewe, ndugu, unapowazia hivyo, hiyo ni kweli, haupo sawa na Mungu.
Kama huwezi kuunyosha mkono kwa yule adui mkali zaidi uliye naye, na kujaribu kumvuta kwa Kristo, basi Roho wa Kristo hayumo ndani yako. “Kwa maana Yeye alikuja kwa Walio Wake, na Walio Wake hawakumpokea,” hata hivyo alitoa uhai Wake kwa ajili ya adui Yake, aliutoa. Ni kweli jinsi gani!
Na huyo Roho wa Mungu ndani yako hukufanya ujisikie vivyo hivyo juu ya kila mtu.
MKATE WA KILA SIKU
Mkiisha kujitakasa roho zenu kwa kuitii kweli, hata kuufikilia upendano wa ndugu usio na unafiki, basi jitahidini kupendana kwa moyo.
1 Petro 1:22
25-1016
60-0723 – Nena Na Mwamba Nao Utatoa Maji Yake
Kanisa ni kiti cha hukumu, ambapo Mbingu ndio Kiti kikuu cha Hukumu cha Mungu, na vile visima vidogo vinawakilisha makanisa madogo yote nje. Nayo hukumu huanzia katika nyumba ya Mungu. Unaona? Hapa ndipo hukumu inapoanzia.
Ndio maana sioni ni kwa nini wengi sana wanalalamika kwamba ninazungumza kwa nguvu sana, na kujaribu kuwafanya watu wanyooke, na kuwaambia jinsi wanavyoishi, jinsi wanavyovaa, na kuniambia ninaiharibu huduma yangu, wakati kiti cha hukumu ni nyumba ya Mungu. Hiyo ni kweli. Hapa ndipo inapopaswa kuanzia, papa hapa, ambapo haki, na unyofu, na hukumu ya Mungu yabidi kutoka mimbarani.
MKATE WA KILA SIKU
Kwa maana wakati umefika wa hukumu kuanza katika nyumba ya Mungu. 1 Petro 4:17
25-1015
60-0522E – Kufanywa Wana Wenye Mamlaka #4
Mara nikaanza kujirudia. Nikatazama, nimelala pale kitandani, nami nikaona mwili wangu mzee hapa ukizeeka na una makunyanzi, na umejikunyata na—na umejaa magonjwa na mateso, kisha nikaona mkono wangu nyuma ya kichwa changu, ndipo nikawaza, “Jamani, itanibidi kurudi kwenye kitu kile tena?”
Nami nikaendelea kuisikia Sauti ile, “Endelea kukaza mwendo! Endelea kukaza mwendo!”
Nikasema, “Bwana, daima nimeamini katika kuponya Kiungu, nitaendelea kuamini hilo. Lakini nitajitahidi sana kwa ajili ya hao watu, hivyo basi nisaidie. Nitakuwa na wengi sana kule nita-…Jalia niishi, Bwana, nami nitaingiza milioni nyingine mle, iwapo utaniruhusu tu kuishi.”
Sijali ni wa rangi gani, ni wa imani gani, ni wa taifa gani, hao ni nani, wote ni mmoja wanapofika kule, na mipaka hiyo imepita.
MKATE WA KILA SIKU
Vile vile kama mimi niwapendezavyo watu wote katika mambo yote, nisitake faida yangu mwenyewe, ila faida yao walio wengi, wapate kuokolewa. 1Wakorintho 10:33
25-1014
57-0303A – Kwa Nini Wakristo Wengi Hupata Ugumu Sana Kuishi Maisha Ya Kikristo?
Angalia, sasa, “Nami Nitawapa roho mpya, nami nitatia Roho Yangu…” Angalia, moyo mpya unawekwa moja kwa moja katikati yako. Na roho mpya inawekwa katikati ya moyo wako mpya. Na Roho wake anawekwa katikati kabisa ya hiyo roho mpya.
Ni kama springi kuu katika saa maarufu. Wakati hiyo…Wakati hiyo springi kuu inapowekwa katikati ya saa, inadhibiti kila mwendo wa saa hiyo. Na hilo ndilo jambo lenyewe, enyi marafiki. Sasa, natumai mnaona jambo hili. Nami sisemi hili ku-jaribu kupindisha ama kuwa tofauti; Ninasema jambo hilo tu kwa sababu najua kwamba siku moja nitasimama kwenye hukumu pamoja nanyi.
Unaona, ikiwa Roho Mtakatifu yuko katikati ya roho yako…Na hiyo springi ya saa hufanya mienendo mingine yote ielekee kabisa mahali pake, kudumisha wakati mkamilifu. Roho Mtakatifu anapokuwa katikati ya roho yako, hufanya kila tendo la Roho Mtakatifu ndani yako litimie sawasawa kabisa na Saa ya Mungu, Biblia. Kweli.
MKATE WA KILA SIKU
Nami nitawapa ninyi moyo mpya, nami nitatia roho mpya ndani yenu, nami nitatoa moyo wa jiwe uliomo ndani ya mwili wenu, nami nitawapa moyo wa nyama.
Nami nitatia roho yangu ndani yenu, na kuwaendesha katika sheria zangu, nanyi mtazishika hukumu zangu, na kuzitenda.
Ezekieli 36:26
25-1013
61-0108 – Ufunuo, Mlango Wa Nne Sehemu Ya III
Nanyi mkiona karama na kadhalika zikinyemelea kanisani, na kutenda kazi kwa karama hizi. Kabla hamjaruhusu zianze kutumika na kadhalika, kwanza…Ukizisikia zikikusukuma moyoni mwako…Sasa, adui ni mjanja sana. Mnaona? Na hilo ndilo tu linaloyararua makanisa vipande-vipande kila wakati, ni karama ya kweli ikitumiwa vibaya. Mnaona? Jambo fulani ambalo Mungu anajaribu kufanya, nalo linatumiwa vibaya, lita—kwa urahisi tu litaninii…Sio tu kuwadhuru, bali litalirarua kanisa lote. Mnaona? Shaurianeni, lipitishieni katika Biblia tena na tena, kisha mlijaribu muone kama ni Mungu ama siye. Endeleeni tu kulijaribu na kulichunguza, muone kama ni kamilifu kote kote na linalingana na Neno kikamilifu. Ndipo mko sawa, mnaona.
Maadamu Neno limesema zitakuwa hapa, na zingetenda kazi kwa njia fulani hii, dumuni moja kwa moja nalo. Kamwe msiende kombo, haidhuru mtu yeyote anafanya nini, jinsi linavyoonekana ni halisi. Endapo haliakisi katika Maandiko kutoka Mwanzo hadi Ufunuo, achaneni nalo. Msibahatishe hata kidogo, tuko katika siku za mwisho wakati Shetani ni mdanganyifu kabisa awezavyo kuwa.
MKATE WA KILA SIKU
Maana Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Manabii walio kati yenu, na wabashiri wenu, wasiwadanganye ninyi, wala msisikilize ndoto zenu, mnazootesha. Yeremia 29:8
25-1012
57-0901E – Waebrania, Mlango Wa Nne
Hampaswi kumhoji kitu chochote, Mungu. “Kwa kuwa hatua za mwenye haki zinaongozwa na Bwana.” Na kila jaribio linawekwa juu yako, kukuthibitisha. Na Biblia ilisema, “Yana thamani zaidi kwako kuliko dhahabu.” Kwa hiyo kama Mungu aliruhusu mateso machache mepesi yakupate, kumbuka, ni kwa ajili ya kukurudi wewe. “Kila mwana amjiaye Mungu hana budi kurudiwa na Mungu kwanza, na kujaribiwa, apate mafunzo ya mtoto.” Hakuna asiyerudiwa. “Kila mwana ajaye.” Mateso haya yanafanywa ama kusababishwa—kusababishwa, kuona utachukua msimamo gani. Unaona? Ni Mungu, kwenye mahali hapa pa kujaribia. Hiyo ni dunia nzima, ni mahali pa kujaribiwa, na mahali Yeye anapojaribu kukujaribu.
MKATE WA KILA SIKU.
Pande zote twadhikika, bali hatusongwi; twaona shaka, bali hatukati tamaa; 2 Wakorintho 4:8
25-1011
61-0427 – Amini Tu
Ninataka kuwaulizeni jambo fulani. Je, kanisa la Kipentekoste liko afadhali zaidi usiku wa leo kwa sababu lilijigawa katika madhehebu thelathini mbalimbali, au wakati lilipoanza hapo mwanzo? Mnaona? Uliza tu hilo. Tunazidi kuwa wabaya zaidi na zaidi. Je, wanawake na wanaume katika makanisa yetu ya Kipentekoste wanaonekana zaidi kama watakatifu, wakiomba? Niambie mahali fulani mjini ambapo wanafanya mkutano wa maombi usiku kucha, siku baada ya siku, kwa ajili ya dhambi zinazotendwa mjini, kama walivyokuwa wakifanya. Je, sisi ni bora zaidi? Tunakuwa wabaya zaidi.
“Loo, majengo yetu yanakuwa mazuri zaidi.” “Loo, tunakuwa bora zaidi katika ushirikiano na makanisa mengine.” Lakini ni nani anayetaka kuwa kama wao? Ninataka kuwa kama Yesu. Na hapo ndipo kila mtu anapaswa kutaka kuwa, kama Kristo, hebu na tumlete jukwaani. Mnaona? Nasi ni…Ma—ma—makanisa yanakufa, kwa hiyo hatuna budi kufanya jambo fulani, hatuna budi kuharakisha. Hatuna ninii yote…Hatupaswi kungojea mpaka—mpaka kwenye ule Utawala wa Miaka Elfu kufanya hivyo. Kama tutafanya hivyo, hatuna budi kufanya sasa, la sivyo litakufa. Jambo fulani litatukia.
MKATE WA KILA SIKU
…Mtu awaye yote aliye upande wa Bwana, na aje kwangu…
Kutoka 32:26
25-1010
56-0223 – Agano la Mungu Kwa Ibrahimu na Uzao Wake
Sasa, katika bustani ya Edeni kulikuwa na miti miwili, mmoja wao, tuseme upande wa kuume, ulikuwa ni Mti wa Uzima, upande wa kushoto ulikuwa ni mti wa ujuzi. Na mradi tu mtu anakula kutoka kwenye Mti wa Uzima, ambao ni imani, anaishi. Lakini mego ya kwanza alioimba kutoka kwenye mti wa ujuzi, alijitenga mwenyewe na ushirika wake na Mungu. Unaliona?
Na angalia basi, katika kujitenga kwake, yeye daima anauma kutoka kwenye mti huo, akiendelea kula kutoka kwenye mti huo, kisha analileta ndani mpaka anajaribu kuyachanganya maarifa hayo na ushirika na Mungu. Naye Mungu kamwe hakumfanya mtu, kwa maarifa yake, amjue Yeye.
Na maarifa yote tuliyo nayo kamwe hayatamwelewa Mungu. Mungu anajulikana kwa kipengele kimoja, hicho ni imani.
MKATE WA KILA SIKU
Walakini matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile:
Mwanzo 2:17
25-1009
64-0125 – Washa Taa
Mng’ao ni nuru danganyifu.
Ni kama tu mazigazi barabarani. Tunashuka kwenda barabarani na kuona mazigazi. Ni picha ya bandia ya jua. Na unapofika pale, haijadhihirisha kitu ila kitu cha uongo. Kwa sababu, huwezi kutembea katika mmweko wa jua, kwa sababu ni mazigazi, daima yakikuonyesha kitu fulani ambacho ni uongo mtupu.
Na wakati watu wanapojaribu kukwambia ya kwamba Yesu Kristo si yeye yule jana, leo, na hata milele, wanakuongoza kukuingiza katika mazigazi. Hivyo tu. Na wakati unapoingia katika kanisa na kujiunga na kanisa, kanuni fulani baridi ama kitu kama hicho, hakuna kitu hapo, si zaidi ya yale uliyokuwa nayo duniani.
Hebu nikwambie. Usiikatae Nuru ya Injili ya Yesu Kristo, ambayo inaleta miali inayotia joto ya Roho Mtakatifu juu yako, inakufanya kiumbe kipya katika Kristo Yesu. Usijaribu kutembea katika mng’ao fulani wa wakati mwingine.
MKATE WA KILA SIKU
Hawa ni visima visivyo na maji, na mawingu yachukuliwayo na tufani, ambao weusi wa giza ni akiba waliyowekewa. 2 Petro 2:17
25-1008
53-0906A – Unayasadiki Hayo?
Na kama wanawake, kama mngetambua tu ni mamia mangapi ya mabilioni ya dola kila mwaka ambayo wanawake hutumia huko Amerika kwa ajili ya vipodozi, kila unachoweka mapajani— kwenye midomo yako. Sivijui vitu hivyo ni vitu gani. Hata hivyo, ni mamilioni mangapi ya dola wanazotengeneza watu hawa kwa vitu hivyo wanajipaka usoni na kujipodoa namna hiyo…
Na wakati watoto wadogo maskini kule nao wamishenari wanaoketi hapa wamelala kwa sababu hawawezi kwenda. Hawana pesa za kutosha kuendelea. Mungu atakuwajibisha kwenye siku ya hukumu. Hiyo ni kweli. Ni kweli.
Naam, Wakristo, mnajiita wenyewe Wakristo, mkija mkiwa mmejipamba na kujirembesha. Kulikuwa na mwanamke mmoja tu katika Biblia ambaye aliwahi kujipaka rangi usoni na huyo alikuwa Yezebeli. Unajua Mungu alimfanya nini? Alimlisha kwa mbwa. Hiyo ni kweli.
Nawe unapomwona mwanamke akitenda Jinsi hiyo na kujiita mwenyewe Mkristo, sema, “Unaendeleaje, bibi nyama ya mbwa?” Hivyo ndivyo alivyo: nyama ya mbwa. Mungu alimlisha kwa mbwa. Ndiyo, bwana.
Loo, tunachohitaji leo ni Roho Mtakatifu wa mtindo wa kale akitaharikisha miongoni mwa watu kuwarudisha wanaume na wanawake kwa Mungu aliye hai tena.
*lMKATE WA KILA SIKU
Kwa kuwa nia ya mwili ni mauti; bali nia ya roho ni uzima na amani.
Warumi 8:6
25-1007
61-1119 – Uweza Mkamilifu Kwa Udhaifu Mkamilifu
Hapo, jambo ndilo hilo, tu—tunamsonga anatoka. Tunamfukuza kwa ninii yetu…Kutoka kwa maskini kuliko wote kwetu mpaka aliye tajiri kuliko wote kwetu, kutoka kwa mdogo kuliko wote hata aliye mkuu kuliko wote, tunamweka Mungu nje ya maisha yetu kwa sababu ya nafsi zetu.
Nimesema mara nyingi, “Adui mkubwa kuliko wote niliye naye ni William Branham.” Huyo ndiye anayemzuia Mungu. Ndiye mwenye kuzembea. Yeye ndiye anayefikia mahali wakati mwingine ambapo anawazia anaweza kufanya jambo fulani kulihusu, na, anapofanya hivyo, hilo linamsukumia Mungu moja kwa moja nje ya picha. Lakini ninapoweza kumwondosha jamaa huyo, ninapoweza kufikia mahali ambapo yeye ameondoka, basi Mungu anaweza kuja na kufanya mambo ambayo William Branham hajui kitu kuyahusu.
Hapo ndipo Mungu anapoweza kukutumia. Hapo ndipo anapoweza kumtumia yeyote wenu. Anaweza kumtumia mtu yeyote tunapoondoka njiani. Lakini mradi tumejiweka njiani, basi hatuwezi.
MKATE WA KILA SIKU
Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami. Ufunuo 3:20
25-1006
60-1126 – Kwa nini?
Loo, jamani! Tumeingiliwa sana na kila kitu, na tumefadhaika sana na tunaogopa. Msiogope. Juzi usiku nilihubiri juu ya jambo hilo, Msiogope, Ni Mimi. Kitu pekee ambacho kingeweza kuwasaidia, walikuwa wanakufa, wakizama, Shetani alikuwa anawachukua, nao walifikiri Yeye alikuwa ni mzuka, roho, Kitu pekee ambacho kingeweza kuwasaidia.
Na hivyo ndivyo ilivyo leo, Kitu pekee kinachoweza kukukomboa kutokana na kansa, Kitu pekee kinachoweza kukuokoa kutoka kwenye shida ya moyo, madawa hayana tiba ya hiyo, Kitu pekee kinachoweza kukusaidia ni Kitu ambacho wewe unachokiogopa, unaogopa ni roho ya namna fulani, Ni Roho, Roho Mtakatifu, Kristo akidhihirishwa maishani mwetu. Mwamini Yeye sasa.
MKATE WA KILA SIKU
Mara Yesu alinena, akawaambia, Jipeni moyo ni mimi; msiogope.
Mathayo 14:27
25-1005
64-0403 – Yehova-Yire #2
Lakini Mungu hahitaji mtu yeyote kumfasiri. Yeye hujifasiria Mwenyewe. Yeye huweka ahadi, halafu anaitimiza, na hiyo ndiyo fasiri yake. Hakuna mtu anayepaswa kulifasiri. Mungu hamwambii mtu yeyote aifasiri. “Biblia si ya kufasiriwa apendavyo mtu yeyote.” Kila mtu akijaribu kusema inamaanisha hivi, vile. Acha Mungu ajinenee Mwenyewe. Yeye Ndiye anayejifasiria. Aliweka ahadi; anasimama nyuma yake. Anafanya hivyo, kwa waaminio.
Lakini wasioamini hawapokei chochote. Si kwa ajili yao. Wamekufa, kwanza. Hata hawakupata kuwakilishwa kamwe. Hamna kitu ndani yao. Wao ni maganda yaliyokufa. Hutaki kuwa namna hiyo.
“Jazweni na Roho!”
MKATE WA KILA SIKU
Nao watatanga-tanga toka bahari hata bahari; na toka upande wa kaskazi hata upande wa mashariki; watapiga mbio, wakienda huko na huko, kulitafuta neno la Bwana, wasilione. Amosi 8:12
25-1004
61-0124 – Kipofu Bartimayo
Huamini kuwa Roho Mtakatifu ni halisi, shikilia ahadi ya Mungu, na udumu nayo tu, ishikilie, usiiachie. Kama huamini kuwa Yeye ni Mponyaji, ugonjwa wo wote ama shida uliyo nayo, sasa hivi, usisubiri mstari wa uponyaji, wewe ishikilie tu sasa hivi, na useme, “Mungu, niko mikononi Mwako.”
Na Shetani atasema: “Huna nafuu yoyote.”
Hivyo ndivyo alivyoniambia, nikasema, “Angalia hapa, ewe mguu wa kale uliyechinjwa, kama hutaki…ukitaka…ukipenda kunisikia nikishuhudia juu ya utukufu wa Mungu, endelea kukaa karibu, lakini hutanitikisa kwenye hilo. Kama unapenda kusikia shuhuda za Mungu, na sifa za uponyaji wa Kiungu, simama karibu, nitalitangaza kadiri tu niwezavyo, dumu nalo moja kwa moja. Endelea kukaa karibu, lisikilize, ninakualika ulisikilize, kaa karibu.”
Siku ya kwanza, hakuna unafuu; siku inayofuata, hakuna unafuu; siku iliyofuata, hakuna unafuu, niliendelea kudumu tu, nikishuhudia, nikimsifu Mungu, nikipenya katika mawingu meusi, Yeye alitoa ahadi, hatimaye, hilo hapo. Yeye alichoka baada ya kitambo kidogo na kukimbia.
MKATE WA KILA SIKU
Basi mtiini Mungu. Mpingeni Shetani, naye atawakimbia.
Yakobo 4:7
25-1003
65-0718M – Kumtendea Mungu Kazi Bila Mapenzi Yake
Msianzishe au kujaribu kuunda dhehebu kamwe. Msijaribu kujenga juu ya kitu cho chote kingine, lakini dumuni wanyenyekevu mbele za Bwana Mungu wenu, kwani yaonekana kama malango huenda yakafunguliwa ya kuingia katika nchi ya ahadi hivi karibuni. Basi natuingie kwa kuimba kwa kweli na shangwe, wakati Bibi na Bwana Arusi wanapochukua mahali pao kwenye kiti cha enzi.
Ishini wanyenyekevu; ishini wenye kupendana. Pendaneni. Msiingize kamwe kitu kati yenu. Ukiona kitu kinakuja moyoni mwako dhidi ya mtu fulani, kitoe papo hapo. Usimuachie…Na Shetani atafanya awezavyo kuingia kati yenu. Mnaona? Msiache hilo litokee. Mtu fulani mwenye ulimi laini huenda akaja akakutoa katika hilo. Unafikiri waliweza kumshawishi Musa atoke katika uwepo wa Mungu ambapo alikuwa amesimama pale na kuliona? La, bwana! La, hatulipunguzi au kuliongeza! Liwekeni tu vile ambavyo Bwana alisema. Hatutaki dhehebu; hatutaki vyama. Hatutaki uovu; hatutaki fitina; twamtaka Mungu; naye ni Neno.
MKATE WA KILA SIKU
Jaribuni mambo yote; lishikeni lililo jema. 1 Wathesalonike 5:21
25-1002
62-0621E – Thibitisho Na Ushahidi
Kumbukeni, ya kwamba haitupasi kamwe kuja kanisani kuigiza dini. Haitupasi kuja, kuninii tu, kujivalisha tendo la kidini tupate kwenda kanisani, hatuna budi kuja kuabudu katika Roho na katika kweli, hatuna budi kuwa waaminifu sana, lazima kweli tumaanishe kile kilichotuleta hapa. Siku zinazidi kuwa ovu, wakati ni mwovu, nasi tunataka—tunataka kutumia kila dakika, na hasa sana tunapokuwa katika nyumba ya Bwana.
MKATE WA KILA SIKU
Ndipo Yesu alipomwambia, Nenda zako, Shetani; kwa maana imeandikwa, Msujudie Bwana Mungu wako, umwabudu yeye peke yake.
Mathayo 4:10
25-1001
55-0223 – Ayubu
Wajua, wakati mmoja ilisemekana; Sijui kama hii ni kweli au la, ambapo mmishenari aliniambia kule—katika Palestina. Hata hivyo, alisema alimwona m—mchungaji akija na kondoo. Na kusema, “Kondoo mmoja, ilimbidi ambebe, naye alikuwa na gango kwenye mguu wake. Naye akasema, “Je, huyo kondoo alianguka, bwana, na kuumiza mguu wake?”
Akasema, Hapana.
Akasema, “Mguu wake umepatwa na nini?”
Akasema, “Niliuvunja.”
Akasema, “Umeuvunja?” Kasema, “Wewe utakuwa ni mchungaji mkatili sana kufanya tendo hilo.”
Akasema, Hapana. Alisema, “Unaona, kondoo huyu hakunijali, aliendelea tu kupotea, nami nilijua angeuawa. Kwa hiyo ilinibidi niuvunje mguu wake ili nimsogezekaribu yangu, na kumfanyia matibabu maalum kidogo, nimlishe kwa mkono wangu. Na hilo lingemfanya anipende zaidi.”
Kwa hiyo labda Mungu, wakati mwingine, inambidi tu kuruhusu jambo dogo litokee kwako, ili Aweze kukuleta tu karibu kidogo Naye, kukupenda zaidi kidogo, na kisha akupe matibabu maalum kidogo, uponyaji, nawe utasema, “Ndiyo, Bwana, ninaamini wewe ndiye.” Unaona? Ndivyo ilivyo. Unaona jinsi Mungu anavyofanya jambo hilo? Yeye si ni wa ajabu? Tunamwamini Yeye tu.
MKATE WA KILA SIKU
Kwa kuwa Bwana ampendaye humrudi. Mithali 3:12