25-1015
60-0522E – Kufanywa Wana Wenye Mamlaka #4
Mara nikaanza kujirudia. Nikatazama, nimelala pale kitandani, nami nikaona mwili wangu mzee hapa ukizeeka na una makunyanzi, na umejikunyata na—na umejaa magonjwa na mateso, kisha nikaona mkono wangu nyuma ya kichwa changu, ndipo nikawaza, “Jamani, itanibidi kurudi kwenye kitu kile tena?”
Nami nikaendelea kuisikia Sauti ile, “Endelea kukaza mwendo! Endelea kukaza mwendo!”
Nikasema, “Bwana, daima nimeamini katika kuponya Kiungu, nitaendelea kuamini hilo. Lakini nitajitahidi sana kwa ajili ya hao watu, hivyo basi nisaidie. Nitakuwa na wengi sana kule nita-…Jalia niishi, Bwana, nami nitaingiza milioni nyingine mle, iwapo utaniruhusu tu kuishi.”
Sijali ni wa rangi gani, ni wa imani gani, ni wa taifa gani, hao ni nani, wote ni mmoja wanapofika kule, na mipaka hiyo imepita.
MKATE WA KILA SIKU
Vile vile kama mimi niwapendezavyo watu wote katika mambo yote, nisitake faida yangu mwenyewe, ila faida yao walio wengi, wapate kuokolewa. 1Wakorintho 10:33
25-1014
57-0303A – Kwa Nini Wakristo Wengi Hupata Ugumu Sana Kuishi Maisha Ya Kikristo?
Angalia, sasa, “Nami Nitawapa roho mpya, nami nitatia Roho Yangu…” Angalia, moyo mpya unawekwa moja kwa moja katikati yako. Na roho mpya inawekwa katikati ya moyo wako mpya. Na Roho wake anawekwa katikati kabisa ya hiyo roho mpya.
Ni kama springi kuu katika saa maarufu. Wakati hiyo…Wakati hiyo springi kuu inapowekwa katikati ya saa, inadhibiti kila mwendo wa saa hiyo. Na hilo ndilo jambo lenyewe, enyi marafiki. Sasa, natumai mnaona jambo hili. Nami sisemi hili ku-jaribu kupindisha ama kuwa tofauti; Ninasema jambo hilo tu kwa sababu najua kwamba siku moja nitasimama kwenye hukumu pamoja nanyi.
Unaona, ikiwa Roho Mtakatifu yuko katikati ya roho yako…Na hiyo springi ya saa hufanya mienendo mingine yote ielekee kabisa mahali pake, kudumisha wakati mkamilifu. Roho Mtakatifu anapokuwa katikati ya roho yako, hufanya kila tendo la Roho Mtakatifu ndani yako litimie sawasawa kabisa na Saa ya Mungu, Biblia. Kweli.
MKATE WA KILA SIKU
Nami nitawapa ninyi moyo mpya, nami nitatia roho mpya ndani yenu, nami nitatoa moyo wa jiwe uliomo ndani ya mwili wenu, nami nitawapa moyo wa nyama.
Nami nitatia roho yangu ndani yenu, na kuwaendesha katika sheria zangu, nanyi mtazishika hukumu zangu, na kuzitenda.
Ezekieli 36:26
25-1013
61-0108 – Ufunuo, Mlango Wa Nne Sehemu Ya III
Nanyi mkiona karama na kadhalika zikinyemelea kanisani, na kutenda kazi kwa karama hizi. Kabla hamjaruhusu zianze kutumika na kadhalika, kwanza…Ukizisikia zikikusukuma moyoni mwako…Sasa, adui ni mjanja sana. Mnaona? Na hilo ndilo tu linaloyararua makanisa vipande-vipande kila wakati, ni karama ya kweli ikitumiwa vibaya. Mnaona? Jambo fulani ambalo Mungu anajaribu kufanya, nalo linatumiwa vibaya, lita—kwa urahisi tu litaninii…Sio tu kuwadhuru, bali litalirarua kanisa lote. Mnaona? Shaurianeni, lipitishieni katika Biblia tena na tena, kisha mlijaribu muone kama ni Mungu ama siye. Endeleeni tu kulijaribu na kulichunguza, muone kama ni kamilifu kote kote na linalingana na Neno kikamilifu. Ndipo mko sawa, mnaona.
Maadamu Neno limesema zitakuwa hapa, na zingetenda kazi kwa njia fulani hii, dumuni moja kwa moja nalo. Kamwe msiende kombo, haidhuru mtu yeyote anafanya nini, jinsi linavyoonekana ni halisi. Endapo haliakisi katika Maandiko kutoka Mwanzo hadi Ufunuo, achaneni nalo. Msibahatishe hata kidogo, tuko katika siku za mwisho wakati Shetani ni mdanganyifu kabisa awezavyo kuwa.
MKATE WA KILA SIKU
Maana Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Manabii walio kati yenu, na wabashiri wenu, wasiwadanganye ninyi, wala msisikilize ndoto zenu, mnazootesha. Yeremia 29:8
25-1012
57-0901E – Waebrania, Mlango Wa Nne
Hampaswi kumhoji kitu chochote, Mungu. “Kwa kuwa hatua za mwenye haki zinaongozwa na Bwana.” Na kila jaribio linawekwa juu yako, kukuthibitisha. Na Biblia ilisema, “Yana thamani zaidi kwako kuliko dhahabu.” Kwa hiyo kama Mungu aliruhusu mateso machache mepesi yakupate, kumbuka, ni kwa ajili ya kukurudi wewe. “Kila mwana amjiaye Mungu hana budi kurudiwa na Mungu kwanza, na kujaribiwa, apate mafunzo ya mtoto.” Hakuna asiyerudiwa. “Kila mwana ajaye.” Mateso haya yanafanywa ama kusababishwa—kusababishwa, kuona utachukua msimamo gani. Unaona? Ni Mungu, kwenye mahali hapa pa kujaribia. Hiyo ni dunia nzima, ni mahali pa kujaribiwa, na mahali Yeye anapojaribu kukujaribu.
MKATE WA KILA SIKU.
Pande zote twadhikika, bali hatusongwi; twaona shaka, bali hatukati tamaa; 2 Wakorintho 4:8
25-1011
61-0427 – Amini Tu
Ninataka kuwaulizeni jambo fulani. Je, kanisa la Kipentekoste liko afadhali zaidi usiku wa leo kwa sababu lilijigawa katika madhehebu thelathini mbalimbali, au wakati lilipoanza hapo mwanzo? Mnaona? Uliza tu hilo. Tunazidi kuwa wabaya zaidi na zaidi. Je, wanawake na wanaume katika makanisa yetu ya Kipentekoste wanaonekana zaidi kama watakatifu, wakiomba? Niambie mahali fulani mjini ambapo wanafanya mkutano wa maombi usiku kucha, siku baada ya siku, kwa ajili ya dhambi zinazotendwa mjini, kama walivyokuwa wakifanya. Je, sisi ni bora zaidi? Tunakuwa wabaya zaidi.
“Loo, majengo yetu yanakuwa mazuri zaidi.” “Loo, tunakuwa bora zaidi katika ushirikiano na makanisa mengine.” Lakini ni nani anayetaka kuwa kama wao? Ninataka kuwa kama Yesu. Na hapo ndipo kila mtu anapaswa kutaka kuwa, kama Kristo, hebu na tumlete jukwaani. Mnaona? Nasi ni…Ma—ma—makanisa yanakufa, kwa hiyo hatuna budi kufanya jambo fulani, hatuna budi kuharakisha. Hatuna ninii yote…Hatupaswi kungojea mpaka—mpaka kwenye ule Utawala wa Miaka Elfu kufanya hivyo. Kama tutafanya hivyo, hatuna budi kufanya sasa, la sivyo litakufa. Jambo fulani litatukia.
MKATE WA KILA SIKU
…Mtu awaye yote aliye upande wa Bwana, na aje kwangu…
Kutoka 32:26
25-1010
56-0223 – Agano la Mungu Kwa Ibrahimu na Uzao Wake
Sasa, katika bustani ya Edeni kulikuwa na miti miwili, mmoja wao, tuseme upande wa kuume, ulikuwa ni Mti wa Uzima, upande wa kushoto ulikuwa ni mti wa ujuzi. Na mradi tu mtu anakula kutoka kwenye Mti wa Uzima, ambao ni imani, anaishi. Lakini mego ya kwanza alioimba kutoka kwenye mti wa ujuzi, alijitenga mwenyewe na ushirika wake na Mungu. Unaliona?
Na angalia basi, katika kujitenga kwake, yeye daima anauma kutoka kwenye mti huo, akiendelea kula kutoka kwenye mti huo, kisha analileta ndani mpaka anajaribu kuyachanganya maarifa hayo na ushirika na Mungu. Naye Mungu kamwe hakumfanya mtu, kwa maarifa yake, amjue Yeye.
Na maarifa yote tuliyo nayo kamwe hayatamwelewa Mungu. Mungu anajulikana kwa kipengele kimoja, hicho ni imani.
MKATE WA KILA SIKU
Walakini matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile:
Mwanzo 2:17
25-1009
64-0125 – Washa Taa
Mng’ao ni nuru danganyifu.
Ni kama tu mazigazi barabarani. Tunashuka kwenda barabarani na kuona mazigazi. Ni picha ya bandia ya jua. Na unapofika pale, haijadhihirisha kitu ila kitu cha uongo. Kwa sababu, huwezi kutembea katika mmweko wa jua, kwa sababu ni mazigazi, daima yakikuonyesha kitu fulani ambacho ni uongo mtupu.
Na wakati watu wanapojaribu kukwambia ya kwamba Yesu Kristo si yeye yule jana, leo, na hata milele, wanakuongoza kukuingiza katika mazigazi. Hivyo tu. Na wakati unapoingia katika kanisa na kujiunga na kanisa, kanuni fulani baridi ama kitu kama hicho, hakuna kitu hapo, si zaidi ya yale uliyokuwa nayo duniani.
Hebu nikwambie. Usiikatae Nuru ya Injili ya Yesu Kristo, ambayo inaleta miali inayotia joto ya Roho Mtakatifu juu yako, inakufanya kiumbe kipya katika Kristo Yesu. Usijaribu kutembea katika mng’ao fulani wa wakati mwingine.
MKATE WA KILA SIKU
Hawa ni visima visivyo na maji, na mawingu yachukuliwayo na tufani, ambao weusi wa giza ni akiba waliyowekewa. 2 Petro 2:17
25-1008
53-0906A – Unayasadiki Hayo?
Na kama wanawake, kama mngetambua tu ni mamia mangapi ya mabilioni ya dola kila mwaka ambayo wanawake hutumia huko Amerika kwa ajili ya vipodozi, kila unachoweka mapajani— kwenye midomo yako. Sivijui vitu hivyo ni vitu gani. Hata hivyo, ni mamilioni mangapi ya dola wanazotengeneza watu hawa kwa vitu hivyo wanajipaka usoni na kujipodoa namna hiyo…
Na wakati watoto wadogo maskini kule nao wamishenari wanaoketi hapa wamelala kwa sababu hawawezi kwenda. Hawana pesa za kutosha kuendelea. Mungu atakuwajibisha kwenye siku ya hukumu. Hiyo ni kweli. Ni kweli.
Naam, Wakristo, mnajiita wenyewe Wakristo, mkija mkiwa mmejipamba na kujirembesha. Kulikuwa na mwanamke mmoja tu katika Biblia ambaye aliwahi kujipaka rangi usoni na huyo alikuwa Yezebeli. Unajua Mungu alimfanya nini? Alimlisha kwa mbwa. Hiyo ni kweli.
Nawe unapomwona mwanamke akitenda Jinsi hiyo na kujiita mwenyewe Mkristo, sema, “Unaendeleaje, bibi nyama ya mbwa?” Hivyo ndivyo alivyo: nyama ya mbwa. Mungu alimlisha kwa mbwa. Ndiyo, bwana.
Loo, tunachohitaji leo ni Roho Mtakatifu wa mtindo wa kale akitaharikisha miongoni mwa watu kuwarudisha wanaume na wanawake kwa Mungu aliye hai tena.
*lMKATE WA KILA SIKU
Kwa kuwa nia ya mwili ni mauti; bali nia ya roho ni uzima na amani.
Warumi 8:6
25-1007
61-1119 – Uweza Mkamilifu Kwa Udhaifu Mkamilifu
Hapo, jambo ndilo hilo, tu—tunamsonga anatoka. Tunamfukuza kwa ninii yetu…Kutoka kwa maskini kuliko wote kwetu mpaka aliye tajiri kuliko wote kwetu, kutoka kwa mdogo kuliko wote hata aliye mkuu kuliko wote, tunamweka Mungu nje ya maisha yetu kwa sababu ya nafsi zetu.
Nimesema mara nyingi, “Adui mkubwa kuliko wote niliye naye ni William Branham.” Huyo ndiye anayemzuia Mungu. Ndiye mwenye kuzembea. Yeye ndiye anayefikia mahali wakati mwingine ambapo anawazia anaweza kufanya jambo fulani kulihusu, na, anapofanya hivyo, hilo linamsukumia Mungu moja kwa moja nje ya picha. Lakini ninapoweza kumwondosha jamaa huyo, ninapoweza kufikia mahali ambapo yeye ameondoka, basi Mungu anaweza kuja na kufanya mambo ambayo William Branham hajui kitu kuyahusu.
Hapo ndipo Mungu anapoweza kukutumia. Hapo ndipo anapoweza kumtumia yeyote wenu. Anaweza kumtumia mtu yeyote tunapoondoka njiani. Lakini mradi tumejiweka njiani, basi hatuwezi.
MKATE WA KILA SIKU
Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami. Ufunuo 3:20
25-1006
60-1126 – Kwa nini?
Loo, jamani! Tumeingiliwa sana na kila kitu, na tumefadhaika sana na tunaogopa. Msiogope. Juzi usiku nilihubiri juu ya jambo hilo, Msiogope, Ni Mimi. Kitu pekee ambacho kingeweza kuwasaidia, walikuwa wanakufa, wakizama, Shetani alikuwa anawachukua, nao walifikiri Yeye alikuwa ni mzuka, roho, Kitu pekee ambacho kingeweza kuwasaidia.
Na hivyo ndivyo ilivyo leo, Kitu pekee kinachoweza kukukomboa kutokana na kansa, Kitu pekee kinachoweza kukuokoa kutoka kwenye shida ya moyo, madawa hayana tiba ya hiyo, Kitu pekee kinachoweza kukusaidia ni Kitu ambacho wewe unachokiogopa, unaogopa ni roho ya namna fulani, Ni Roho, Roho Mtakatifu, Kristo akidhihirishwa maishani mwetu. Mwamini Yeye sasa.
MKATE WA KILA SIKU
Mara Yesu alinena, akawaambia, Jipeni moyo ni mimi; msiogope.
Mathayo 14:27
25-1005
64-0403 – Yehova-Yire #2
Lakini Mungu hahitaji mtu yeyote kumfasiri. Yeye hujifasiria Mwenyewe. Yeye huweka ahadi, halafu anaitimiza, na hiyo ndiyo fasiri yake. Hakuna mtu anayepaswa kulifasiri. Mungu hamwambii mtu yeyote aifasiri. “Biblia si ya kufasiriwa apendavyo mtu yeyote.” Kila mtu akijaribu kusema inamaanisha hivi, vile. Acha Mungu ajinenee Mwenyewe. Yeye Ndiye anayejifasiria. Aliweka ahadi; anasimama nyuma yake. Anafanya hivyo, kwa waaminio.
Lakini wasioamini hawapokei chochote. Si kwa ajili yao. Wamekufa, kwanza. Hata hawakupata kuwakilishwa kamwe. Hamna kitu ndani yao. Wao ni maganda yaliyokufa. Hutaki kuwa namna hiyo.
“Jazweni na Roho!”
MKATE WA KILA SIKU
Nao watatanga-tanga toka bahari hata bahari; na toka upande wa kaskazi hata upande wa mashariki; watapiga mbio, wakienda huko na huko, kulitafuta neno la Bwana, wasilione. Amosi 8:12
25-1004
61-0124 – Kipofu Bartimayo
Huamini kuwa Roho Mtakatifu ni halisi, shikilia ahadi ya Mungu, na udumu nayo tu, ishikilie, usiiachie. Kama huamini kuwa Yeye ni Mponyaji, ugonjwa wo wote ama shida uliyo nayo, sasa hivi, usisubiri mstari wa uponyaji, wewe ishikilie tu sasa hivi, na useme, “Mungu, niko mikononi Mwako.”
Na Shetani atasema: “Huna nafuu yoyote.”
Hivyo ndivyo alivyoniambia, nikasema, “Angalia hapa, ewe mguu wa kale uliyechinjwa, kama hutaki…ukitaka…ukipenda kunisikia nikishuhudia juu ya utukufu wa Mungu, endelea kukaa karibu, lakini hutanitikisa kwenye hilo. Kama unapenda kusikia shuhuda za Mungu, na sifa za uponyaji wa Kiungu, simama karibu, nitalitangaza kadiri tu niwezavyo, dumu nalo moja kwa moja. Endelea kukaa karibu, lisikilize, ninakualika ulisikilize, kaa karibu.”
Siku ya kwanza, hakuna unafuu; siku inayofuata, hakuna unafuu; siku iliyofuata, hakuna unafuu, niliendelea kudumu tu, nikishuhudia, nikimsifu Mungu, nikipenya katika mawingu meusi, Yeye alitoa ahadi, hatimaye, hilo hapo. Yeye alichoka baada ya kitambo kidogo na kukimbia.
MKATE WA KILA SIKU
Basi mtiini Mungu. Mpingeni Shetani, naye atawakimbia.
Yakobo 4:7
25-1003
65-0718M – Kumtendea Mungu Kazi Bila Mapenzi Yake
Msianzishe au kujaribu kuunda dhehebu kamwe. Msijaribu kujenga juu ya kitu cho chote kingine, lakini dumuni wanyenyekevu mbele za Bwana Mungu wenu, kwani yaonekana kama malango huenda yakafunguliwa ya kuingia katika nchi ya ahadi hivi karibuni. Basi natuingie kwa kuimba kwa kweli na shangwe, wakati Bibi na Bwana Arusi wanapochukua mahali pao kwenye kiti cha enzi.
Ishini wanyenyekevu; ishini wenye kupendana. Pendaneni. Msiingize kamwe kitu kati yenu. Ukiona kitu kinakuja moyoni mwako dhidi ya mtu fulani, kitoe papo hapo. Usimuachie…Na Shetani atafanya awezavyo kuingia kati yenu. Mnaona? Msiache hilo litokee. Mtu fulani mwenye ulimi laini huenda akaja akakutoa katika hilo. Unafikiri waliweza kumshawishi Musa atoke katika uwepo wa Mungu ambapo alikuwa amesimama pale na kuliona? La, bwana! La, hatulipunguzi au kuliongeza! Liwekeni tu vile ambavyo Bwana alisema. Hatutaki dhehebu; hatutaki vyama. Hatutaki uovu; hatutaki fitina; twamtaka Mungu; naye ni Neno.
MKATE WA KILA SIKU
Jaribuni mambo yote; lishikeni lililo jema. 1 Wathesalonike 5:21
25-1002
62-0621E – Thibitisho Na Ushahidi
Kumbukeni, ya kwamba haitupasi kamwe kuja kanisani kuigiza dini. Haitupasi kuja, kuninii tu, kujivalisha tendo la kidini tupate kwenda kanisani, hatuna budi kuja kuabudu katika Roho na katika kweli, hatuna budi kuwa waaminifu sana, lazima kweli tumaanishe kile kilichotuleta hapa. Siku zinazidi kuwa ovu, wakati ni mwovu, nasi tunataka—tunataka kutumia kila dakika, na hasa sana tunapokuwa katika nyumba ya Bwana.
MKATE WA KILA SIKU
Ndipo Yesu alipomwambia, Nenda zako, Shetani; kwa maana imeandikwa, Msujudie Bwana Mungu wako, umwabudu yeye peke yake.
Mathayo 4:10
25-1001
55-0223 – Ayubu
Wajua, wakati mmoja ilisemekana; Sijui kama hii ni kweli au la, ambapo mmishenari aliniambia kule—katika Palestina. Hata hivyo, alisema alimwona m—mchungaji akija na kondoo. Na kusema, “Kondoo mmoja, ilimbidi ambebe, naye alikuwa na gango kwenye mguu wake. Naye akasema, “Je, huyo kondoo alianguka, bwana, na kuumiza mguu wake?”
Akasema, Hapana.
Akasema, “Mguu wake umepatwa na nini?”
Akasema, “Niliuvunja.”
Akasema, “Umeuvunja?” Kasema, “Wewe utakuwa ni mchungaji mkatili sana kufanya tendo hilo.”
Akasema, Hapana. Alisema, “Unaona, kondoo huyu hakunijali, aliendelea tu kupotea, nami nilijua angeuawa. Kwa hiyo ilinibidi niuvunje mguu wake ili nimsogezekaribu yangu, na kumfanyia matibabu maalum kidogo, nimlishe kwa mkono wangu. Na hilo lingemfanya anipende zaidi.”
Kwa hiyo labda Mungu, wakati mwingine, inambidi tu kuruhusu jambo dogo litokee kwako, ili Aweze kukuleta tu karibu kidogo Naye, kukupenda zaidi kidogo, na kisha akupe matibabu maalum kidogo, uponyaji, nawe utasema, “Ndiyo, Bwana, ninaamini wewe ndiye.” Unaona? Ndivyo ilivyo. Unaona jinsi Mungu anavyofanya jambo hilo? Yeye si ni wa ajabu? Tunamwamini Yeye tu.
MKATE WA KILA SIKU
Kwa kuwa Bwana ampendaye humrudi. Mithali 3:12
25-0930
59-1227M – Ishara Kuu
Ndugu, ninapomwona Mungu, Mungu wa Mbinguni, alivyokiacha kiti Chake cha enzi, uzuri Wake, na yote aliyokuwa; apate kuzaliwa juu ya lundo la samadi, afunikwe nguo za kitoto, adhihakiwe kwa ishara Zake na maajabu Yake, aitwe ibilisi; je, ati nimwonee aibu? La, bwana. Acha huu ulimwengu maarufu ufanye yale wanayotaka kufanya. Kwangu mimi, Yeye ni ishara kuu. Roho Mtakatifu ndani yangu anapaza sauti. Huenda akanifanya nitende kiajabu na niwe mwenye kichaa, kwa ulimwengu huu, bali siwezi kumkataa Yeye Yule aliyenifanyia mengi sana. Alipachukua mahali pangu katika mauti. Alipachukua mahali pangu pale Kalvari. Alifanya mambo haya yote. Alijidhili kutoka Mbinguni, kutoka kwenye viti vyeupe vya enzi vya lulu, ili kuwa mwanadamu; apate kuonja mateso yangu, kupitia kwenye majaribu yangu, kujua jinsi ya kuwa mpatanishi anayefaa ndani yangu, kuniongoza na kunielekeza kwenye Uzima wa Milele. Na kupitia kwenye umaskini Wake, ninafanywa tajiri. Kupitia mauti Yake, ninapewa Uzima, Uzima wa Milele.
Usimkatae. Usimwonee aibu. Usimwonee aibu. Lakini mkumbatie, na kusema, “Naam, Mpendwa Bwana wangu, nipe kama walivyofanya kwenye Siku ya Pentekoste, Bwana. Nipe Roho Mtakatifu. Mmwage moyoni mwangu. Sijali matineja wanasema nini. Sijali walimwengu wanasema nini. Siwaangalii wao. Ninakuangalia Wewe.” Ni kitu gani? Kujiunga na kanisa? La. Ishara kuu, Imanueli, Mungu pamoja nasi.
MKATE WA KILA SIKU
Kwa hiyo Bwana mwenyewe atawapa ishara. Tazama, bikira atachukua mimba, atazaa mtoto mwanamume, naye atamwita jina lake Imanueli.
Isaya 7:14
25-0929
61-0122 – Kama Tai Ataharikishavyo Kiota Chake
Unajua, yeye ni ndege wa mbinguni. Akarudi kwenye kizimba namna hiyo, huyu hapa akakutana na kizimba hicho kwa nguvu awezavyo, akapiga mbawa hizo kubwa, na kugonga kichwa chake kwenye hicho kizimba tena, kikimwangusha chali sakafuni, naye, damu ikimtoka kwenye mbawa zake ambapo alijaribu kuzipiga kwenye hicho kizimba ili atoke nje. Kilimuumiza vikali sana wakati huo, hata akalala pale, na macho yake yaliyochoka yakitazama angani.
Niliwaza, “Ee Mungu, hilo si ni jambo la kusikitisha!” Ndipo jambo fulani likagonga moyoni mwangu, nikawazia, “La, hilo si jambo la kusikitisha sana nililopata kuona, mnyama ndani ya kizimba, jambo la kusikitisha sana nililopata kuona ni mtu aliyezaliwa kuwa mwana wa Mungu,” haleluya. “amebanwa na madhehebu fulani, ama kanuni fulani ya imani inayomwambia, ‘Siku za miujiza zimepita. Hakuna kitu kama ubatizo wa Roho Mtakatifu.’” Wakati akilala katika kanuni hizo za imani za kale za kimadhehebu na kuangalia huku na huku namna hiyo!
Alizaliwa ili awe mwana wa Mungu, kanuni za imani zilimweka kwenye kizimba, Mungu anataka atoke. Amina. Toka huko, ulizaliwa…Hiyo ilikuwa ni kazi ya mwanadamu kumweka huyo tai mle ndani, ni kazi ya mwanadamu inayowaweka ninyi watu katika kanuni za imani na madhehebu, yote ni ya ibilisi. Ndiyo, bwana. Kumfungia mtu chini kwa kanuni ya Imani, “Siku za miujiza zimepita, hakuna kitu kama furaha ya Roho Mtakatifu, hakuna kitu kama kupiga makelele, hakuna kitu kama kunena kwa lugha, hakuna uponyaji wa Kiungu.” Loo, jamani! Inasikitisha! Wana wa Mungu, waliozaliwa ili wawe huru, kisha wanatiwa kizimbani.
MKATE WA KILA SIKU
Kwa maana viumbe vyote pia vinatazamia kwa shauku nyingi kufunuliwa kwa wana wa Mungu. Warumi 8:19
25-0928
62-0128M – Kutokuamini hakumzuii Mungu
Na kama tungekuwa na ufunuo wowote, ambao ungetambulishwa kwetu, ambao ni kinyume cha Neno lililoandikwa, basi hatupaswi kamwe kuupokea, kwa maana hivyo ndivyo hasa Shetani alivyomfanyia Hawa. Hawa yeye alikuwa na Neno, bali alikuwa akiwinda Nuru fulani mpya, naye Shetani alihakikisha kwamba ameipata. Kwa hiyo hatutaki kamwe kuongeza cho chote kwenye Neno, ama kuondoa lolote kwenye Neno, bali kuliacha tu jinsi Lilivyo. Dumu sawasawa na Neno, kwa maana chochote kilicho kinyume ni kutokuamini.
MKATE WA KILA SIKU
Ulisawazishe pito la mguu wako, Na njia zako zote zithibitike.
Mithali 4:26
25-0927
56-0404 – Kutokushindwa Kwa Neno Lililonenwa la Mungu
Neema ni yale Mungu anayokutendea; matendo ni yale wewe unayomfanyia Mungu. Unaona? Ni neema inayokuleta wewe kwa Mungu; matendo ni yale ambayo—ambayo unamfanyia Mungu. Unaona?
Basi, kama vile Ibrahimu alivyohesabiwa haki kwa imani, kwa sababu alimwamini Mungu. Paulo alimhesabia haki kwa imani; yakobo anageuka na kumhesabia haki kwa matendo. Lakini Paulo alikuwa anazungumza yale ambayo Mungu aliona, na Yakobo alikuwa akisema yale ambayo mwanadamu aliona. Ukisema wewe ni mwamini, na kisha utende kinyume na kile unachosema, basi wewe si mwamini. Unaona? Ukimwambia Mungu, “Ndiyo, sasa ninaamini kabisa.” Ndugu, huwezi kufanya lolote ila kutenda jinsi ile unavyoamini. Hiyo ni kweli.
MKATE WA KILA SIKU
Njia ni hii, ifuateni,… Isaya 30:21
25-0926
62-0607 – Kuvaa Silaha Zote za Mungu
Sasa, walimpata mtu anayezunguka angani. Wote wanalipigia kelele hilo mwajua, “Tunaye mtu angani.” Mbona, hilo si lolote, sisi Wakristo tumekuwa na mmoja angani kwa miaka elfu mbili, mwajua. Hiyo ni kweli. Hiyo ni kweli. Wanapiga kelele kuhusu hilo, hilo si jambo jipya, hilo ni la kale kwetu sisi, tulijua hilo wakati wote. Kwa hiyo, unaona? Unaona, hivyo ndivyo tulivyo mbele, ni kwamba tu hawatambui.
Ndiyo, kujenga barabara kuu kubwa na vitu vya ajabu kama hivyo na kujaribu kuifanya dunia kuwa mahali pazuri na kadhalika, hawatambui ya kwamba wapole watairithi, haya basi. Kwa hiyo tu—ni nii tu…Unaona, Mungu alikwisha tupangia yote. Ndilo, jambo pekee tunalopaswa kufanya, ni kushikilia tu Kwake na kuendelea tu mbele. Unaona? Ndilo, kuamini tu, hilo ndilo tu alilotuomba tufanye, Yeye atatuvusha moja kwa moja.
MKATE WA KILA SIKU
Hawa wanataja magari na hawa farasi, Bali sisi tutalitaja jina la BWANA, Mungu wetu. Zaburi 20:7
25-0925
57-0922E – Waebrania, Mlango Wa Saba #2
Lakini, sasa, ninaamini ya kwamba Biblia inafundisha habari za jehanamu halisi inayowaka moto. Biblia inafundisha jambo hilo, ya kwamba dhambi na uovu hayo yataadhibiwa, milele na milele. Hiyo si Umilele, sasa. Hiyo huenda ikawa ni kwa miaka bilioni kumi. Huenda ikawa ni kwa miaka bilioni mia moja, lakini wakati fulani haina budi kukoma. Kwa kuwa, kila kitu kilichokuwa na mwanzo, kina mwisho. Ni vitu vile visivyo na mwanzo, havina mwisho.
Mnakumbuka somo hilo sasa? [Kusanyiko linasema, “Amina.”—Mh.] Jinsi tulivyorudi nyuma na kupata ya kwamba kila kitu kilichokuwa na mwanzo kilikuwa kimepotoshwa, unaona, kupotoshwa kutokana na kitu chenyewe cha kwanza. Na, hatimaye, ni jambo linaloishia katika Umilele. Ndipo basi kuzimu yote, mateso yote, na kumbukumbu lote la hayo, vitatoweka Milele. Kila kitu kinachoanza, hukoma.
MKATE WA KILA SIKU
Mauti na Kuzimu zikatupwa katika lile ziwa la moto. Hii ndiyo mauti ya pili. Ufunuo 20:14
25-0924
63-0115 – Kuikubali Njia Ya Mungu Iliyowekwa Katika Wakati Wa Mwisho
Hivi uliwahi kuona maskini kifaranga anapotoka kwenye ganda? Anacho cha ziada, maskini kidomo kwenye ganda lake, kikwaruzio kidogo cheupe. Naye jamaa huyo mdogo humo ndani, mara uhai unapoanza kuja, anaanza kukitikisa maskini kichwa chake. Huko kunafanya nini? Kikwaruzio hicho kidogo hulikwaruza hilo ganda, na kulifanya jembamba. Anapopata uhai mwingi zaidi kidogo, anaanza kugonga kwa kitu hicho kidogo. Basi akiisha kutoka kwenye ganda, hakihitaji tena, kwa hiyo kinaanguka tu chini.
Nacho kitu kinachosababisha hilo, ni kinga ya ncha ya kidomo chake. Isingalikuwa hivyo, angekuwa na kidomo kilichoumbuka, wala asingeweza kuidonoa nafaka yake. Loo, jamani! Njia ya Mungu iliyowekwa ya kuishi! Mungu humwandaa, njia tu ya kutoka humo. Hakuna njia iliyo bora zaidi. Kitu kingine chochote kingemwua. Hana budi kupitia kwenye njia ya Mungu iliyowekwa. Sasa, kama ukijaribu kutengeneza njia nyingine ama kuwazia njia nyingine, utamwua.
Hiyo ndiyo shida ya kanisa la Kikristo siku hizi. Limejaribu kukubali njia fulani iliyotengenezwa, badala ya kupiga na kutoboa njia yake, kuingia kwenye Ufalme wa Mungu.
MKATE WA KILA SIKU
Mungu njia yake ni kamilifu; Ahadi ya Bwana imehakikishwa; Yeye ndiye ngao yao Wote wanaomkimbilia. 2 Samweli 22:31
25-0923
55-1116 – Kuitwa kwa Ibrahimu
Ungeweza kuwazia kwenda hapa na kumwambia nguruwe, kusema, “Sasa, tazama hapa, bwana Nguruwe, nitakuambia, umekosea.” Mbona, ungeweza kumwosha na kumvika suti rasmi, kama ungetaka. Hilo lisingefaa kitu; angerudi moja kwa moja kwenye dimbwi la matope na kugaagaa tena. Ni asili yake. Yeye ni nguruwe kwa kuanzia. Na kila mtu, kila mtu ambaye hajazaliwa upya, haidhuru unajaribu kuwa mzuri jinsi gani, unafikiri wewe ni mzuri jinsi gani, wewe ni mwenye dhambi kwa asili, mpaka Mungu aibadilishe asili yako. Amina.
Sasa, hiyo ni kweli. Hatupendi kulisema hilo. “Loo,” unasema, “Mimi huvaa nguo iliyo bora katika ujirani wangu. Nina gari bora zaidi. Nina ninii bora zaidi…” Hilo halihusiani na jambo hilo. Kama asili sio…“Sijawahi kusema uwongo. Sijawahi…” Hilo bado halina uhusiano wowote nalo. Si kustahili kwako mwenyewe, bali ni uchaguzi na wito usio na masharti wa Mungu. Na wokovu ni kustahili kwa Yesu Kristo, na hakuna kitu ambacho mtu ye yote angeweza kufanya. Mungu, kwa upendo Wake alimwokoa mwanadamu.
MKATE WA KILA SIKU
Lakini kwa neema ya Mungu nimekuwa hivi nilivyo.
1 Wakorintho 15:10
25-0922
55-1111 – Pale Ninapodhani Wapentekoste Waliposhindwa
Musa aliwaongoza watu milioni mbili jangwani. Naye akawaongoza kwa muda wa miaka arobaini, na alipofika kule ng’ambo ya pili, hapakuwa na mtu aliye dhaifu kati yao.
Je! ninyi madaktari hapa usiku wa leo, ama baadhi yenu, mngependa kujua daktari Musa alikuwa na maagizo gani ya daktari? Yeye aliwapa nini watu hao? Ni watoto wangapi waliyozaliwa kila usiku? Ni wazee wangapi na kadhalika? Ni walemavu wangapi na wachechemeao ? Na ni maradhi mangapi, na kila kitu kingine, alichowapatia usiku kucha? Naye Daktari Musa aliyashughulikia kila moja ya hayo.
Je! ungependa kuangalia mkoba wake wa dawa na kujua ni aina gani ya dawa atoayo? Je, ungependa kujua ni kitu gani? Hebu tuone ilikuwa nini. Hii hapa: “Mimi ndimi Bwana nikuponyaye magonjwa yako yote.” Amina. Hiyo ndiyo tiba pekee aliyokuwa nayo, na ilifanya kazi kwa watu milioni mbili.
MKATE WA KILA SIKU
… kama yule nabii angalikuambia kutenda jambo kubwa, usingalilitenda?
2Wafalme 5:13
25-0921
53-0405S – Nendeni, Mkawaambie Wanafunzi Wangu
Ilikuwa mapema asubuhi moja. Waliuweka mwili Wake ardhini, siku ya Sabato, ambayo ilikuwa ni desturi kwamba hawakufanya lolote siku ya Sabato. Kwa hiyo alikufa Ijumaa alasiri, saa tisa, akafufuka mapema Jumapili asubuhi.
Sasa nataka kutatua swali hili, wakati mkiwa hapa asubuhi hii katika ibada hii ya mapambazuko. Watu wengi wanasema, “Imekuwaje basi kwamba Yeye alisema ya kwamba angelala…Alikuwa kaburini, siku tatu mchana na usiku?” Kamwe hakusema angefanya hivyo.
Alisema, “Katika siku hizi tatu nitaufufua mwili Wangu.” Mnaona? Sasa, sababu ya Yeye kufanya hivyo ni kwa sababu Daudi alikuwa amesema, mahali pamoja katika Maandiko, “Sitaiacha nafsi Yake katika kuzimu, wala sitamwacha Mtakatifu Wangu aone uharibifu.” Naye alijua ya kwamba uharibifu huingia katika mwili wa mwanadamu baada ya saa sabini na mbili, siku tatu usiku na mchana. Na wakati fulani ndani ya hizo siku tatu mchana na usiku, Mungu alikuwa amfufue. Kwa hiyo alikufa Ijumaa alasiri saa tisa, na kufufuka mapema Jumapili asubuhi.
MKATE WA KILA SIKU
Maana hutakuachia kuzimu nafsi yangu, Wala hutamtoa mtakatifu wako aone uharibifu. Zaburi 16:10
25-0920
61-1231M – Huna Budi Kuzaliwa Mara Ya Pili
Sasa, ninyi watu mnaozungumza kuhusu kumpokea Roho Mtakatifu na jinsi inavyowapasa kungojea muda mrefu, haya basi. Mpaka Mungu atakapoipokea dhabihu hiyo, mpaka itakapowekwa juu ya hukumu Zake kule, mpaka hukumu Zake zitakapoziua hisi zako kweli! Huenda ukasema, “Vema, nitafungua ukurasa mpya.” Hivyo sivyo. “Vema, ninajua nilikuwa nikivuta sigara, nitaacha kuvuta sigara.” Hilo bado silo. Mpaka Mungu atakapoipokea dhabihu hiyo kwenye madhabahu Yake ya shaba, madhabahu Yake ni hukumu. Hukumu Yake ni nini? Mauti. Hiyo ndiyo adhabu.
“Nafsi inayotenda dhambi,” inabaki humo, “itakufa.” Sijali yale umefanya.
Yesu alisema, “Wengi watakuja Kwangu siku hiyo, na kusema, ‘Bwana, si nimefanya hili na kufanya lile?’ Yeye aseme, ‘Ondokeni Kwangu, ninyi mtendao uovu.’” Mnaona?
Wakati dhabihu hiyo inapopokelewa na moto, nao unapanda juu namna hiyo, nao moshi unapanda juu, unainuka pamoja na dhabihu yako ukaingia mbinguni, nawe umetiwa muhuri kutoka kwa mambo ya ulimwengu basi. Nafsi yetu iko madhabahuni Mwake.
MKATE WA KILA SIKU
Msikitendee kazi chakula chenye kuharibika, bali chakula kidumucho hata uzima wa milele; ambacho Mwana wa Adamu atawapa, kwa sababu huyo ndiye aliyetiwa muhuri na Baba, yaani, Mungu. Yohana 6:27
25-0919
62-0909E – Katika Uwepo Wake
Mwangalie maskini yule kahaba kule chini Samaria siku ile, mwanamke huyo. Alikuwa katika hali mbaya kiakili na kimwili. Tunajua jambo hilo. Lakini mara alipoiona hiyo ishara ikifanywa, ya Masihi, alisema, “Tunajua Masihi yuaja kufanya jambo hili. Huna budi kuwa ni nabii Wake.”
Akasema, “Mimi Ndimi huyo Masihi aliyeandikiwa atakuja.”
Alitambua jambo hilo. Kamwe hakuuliza swali lingine zaidi. Alianza jukumu mara moja, kujua ya kwamba kama alikuwa amepata jambo hilo na akaja katika Uwepo wa Mungu, alikuwa anawajibika kumwambia mtu mwingine kuhusu jambo hilo. Haleluya! Kweli. Mtu yeyote anayekuja katika Uwepo wa Mungu anawajibika mbele za Mungu, tangu dakika hiyo na kuendelea, kumwambia mtu mwingine. Hebu mwangalie Ibrahimu, mwangalie Musa, mwangalie Petro, mwangalie Paulo. Mara walipokuja katika Uwepo wa Mungu, walijitambua ni “wenye dhambi,” na kuutia muhuri ushuhuda wao kwa maisha yao. Hebu mwangalie maskini mama huyo, asingeweza kukaa zaidi, alienda mjini na kuwaambia wanaume, “Njoni, mwone Mtu aliyeniambia mambo ambayo nimefanya. Yamkini huyu siye yule Masihi?” Wasingeweza kukanusha jambo Hilo, kwa sababu lilikuwa ni la Kimaandiko. Hakika. Naam, hawana budi kufanya jambo hilo, mtu, wakati tukiwa na jukumu la kuwaambia wengine kama vile Musa alivyofanya, kama vile Petro alivyofanya, kama vile Paulo alivyofanya. Baada ya mambo haya, umeliona na ukaja katika Uwepo Wake, wewe unawajibika kwa Ujumbe kumfikia mtu mwingine. Kamwe huwezi tu kuketi kitako nao. Huna budi kumpelekea mtu mwingine.
MKATE WA KILA SIKU
Akawaambia, Enendeni ulimwenguni mwote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe. Marko 16:15
25-0918
65-0217 – Mtu Anayejiepusha Na Uso Wa Bwana
Bali ni rahisi kuipitia njia ambayo ulimwengu unaipitia. Ni rahisi kufuata mkondo.
Unaondoka unaenda kule na kuketi mtoni, na mashua yako. Unachukua makasia yako na kuanza kuyapiga dhidi ya mkondo; huachilii makasia, nayo inakuwa ngumu. Bali achilia makasia mara moja na utaona vile utakavyoipita miti haraka, ukitelemka, bali angalia unakoelekea!
Wakati mambo yanaelea kwa urahisi, kumbuka, unaelekea kwenye—kwenye maporomoko makubwa sana kule chini, ya namna fulani. Unaelekea kwenye maporomoko, na haitachukua muda mrefu nawe utatumbukia kwenye maporomoko hayo. Unaelea tu na ulimwengu, kwa urahisi, jinsi unavyoenda, hutaki jambo hilo. La, bwana. Bali huna budi ku-…kukubali jukumu lako.
Sasa, unaliamini, nawe una-…Unafikiri ni Kweli.
Na jukumu ambalo Mungu ametupa katika siku hii, kuuleta ujumbe huu! Na ninapozeeka, na kujua kwamba siku zangu zinakuwa fupi, ninasikia jukumu hilo likiwa kubwa kuliko nilivyowahi kusikia. Tunakaza mwendo, hatuna budi kufanya hivyo! Lazima tuanze kuutekeleza, kila mahala tuendapo, na kuuhubiri Ujumbe; na—na kuwaambia watu ya kwamba Yesu Kristo anakuja, ya kwamba Yeye ni Mungu na yuaja hivi karibuni. Hakuna tu—tumaini lililobakia ulimwenguni ila Kuja kwa Bwana.
MKATE WA KILA SIKU
Ndugu, sijidhanii nafsi yangu kwamba nimekwisha kushika; ila natenda neno moja tu; nikiyasahau yaliyo nyuma, nikiyachuchumilia yaliyo mbele;
Nakaza mwendo, niifikilie mede ya thawabu ya mwito mkuu wa Mungu katika Kristo Yesu.
Wafilipi 3:13-14
25-0917
55-1009 – Njia ya Kuwa na Ushirika
Kuna nguvu mbili tu zinazomtawala mwanadamu, na mojawapo ni—ni imani, ambayo huleta matokeo; na nyingine ni hofu, ambayo haina faida ndani yake hata kidogo. Imani ni ya Mungu. Hofu ni ya shetani. Hofu hukuchosha; hofu hukufanya kuzubaa.
Na kama ningalikuwa naenda kufa asubuhi, ingefaa nini kwangu kuhangaishwa na jambo hilo? Vipi kama naenda kuawa kwa umeme asubuhi, na maisha yangu yatakoma kesho asubuhi, ingenisaidia nini kuyahofia?
“Vema,” unasema, “ingekuwa na faida gani kuwa na imani?” Imani inaweza kusaini msamaha wangu, hakika; kuna faida katika imani. Usichoke; usiogope; usifadhaike; wewe kuwa tu na imani na uamini. Na njia pekee unayoweza kuwa na imani, huna budi kuwa na upendo kwanza, kwa maana upendo huzaa imani. Kwa maana upendo mkamilifu…Lipate. Upendo mkamilifu huondolea mbali hofu yote.
MKATE WA KILA SIKU
Akawaambia, Mbona mmekuwa waoga, enyi wa imani haba?…
Mathayo 8:26
25-0916
53-0405E – Mashahidi
Nawazia, usiku kucha kulikuwa na mkutano wa maombi ukiendelea. Unajua, ikiwa unakuja kwenye jaribio…
Hili hapa. Hiyo ndiyo shida ya kanisa siku hizi; unategemea hisia na uwezo wako mwenyewe, badala ya kulipeleka kwa Bwana katika maombi. Hiyo ni kweli. Siku hizi tunaanza kumtuma mtu fulani mahali fulani, vema, unasema, tunashuka na kuwa na mashauri kidogo, na kukutana na kusema, “Tunapaswa kufanya hivi, au kwenda hapa, au kufanya vile.”
Lakini Biblia, katika zile siku kabla hawajawatuma mitume, walikusanyika pamoja na kufunga na kuomba. Ndipo Roho Mtakatifu akasema, “Nitengeeni Paulo na Barnaba.” Roho Mtakatifu! Mnaona, si maoni ya mwanadamu; bali Roho Mtakatifu akiongoza, akiongoza. Amina. Tazama.
Sasa, mkutano wa maombi, usiku kucha, kwa hiyo iliwabidi waonyeshe walichoumbwa kwacho. Na, ndugu, kila mtu anayedai kuwa Mkristo, wakati mmoja ama mwingine huna budi kuonyesha umeumbwa kwa kitu gani. Ibilisi atakupa changamoto.
MKATE WA KILA SIKU
Nami maombi yangu nakuomba Wewe, Bwana, Wakati ukupendezao; Ee Mungu, Kwa wingi wa fadhili zako unijibu, Katika kweli ya wokovu wako.
Zaburi 69:13
25-0915
65-1128E – Juu Ya Mbawa Za Hua Mweupe Kama Theluji
Je! ulijua ya kwamba Mkristo halisi hana hata dhambi yo yote iliyohesabiwa kwake? Daudi alisema, “Heri mtu yule ambaye Bwana hamhesabii dhambi.” Unapooshwa kwa Damu ya Mwana-kondoo (si kwa kujifanya mwamini bali hasa kwa—kwa Damu ya Mwana-kondoo), Mungu hakuhesabii cho chote kilichotendwa, kwa maana uko chini ya Damu, Naye hakioni. Kuna toleo la Damu; kitu pekee anachoweza kukuona ndani yake, ni jinsi alivyokuona kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu yeye alipoweka jina lako katika Kitabu cha Uzima cha Mwana-kondoo. Hiyo ndiyo tu anayoweza kutazama, kwa maana umekuombolewa kutoka kwa kila kitu ambacho kilipata kufanywa, umeoshwa katika Damu ya Mwana-Kondoo. Kwa hivyo hamna nyongo ndani yako, hamna tabia chafu ndani yako, kwa sababu damu ya Mwana-kondoo imetenda haya;siku na Mungu hawezi kukuhesabia dhambi baada ya kuwa na toleo la dhambi pale likikungoja.
“Vema,” mnasema, “hiyo inanipa nafasi kubwa sana basi, Ndugu Branham, naweza kufanya cho chote ninachotaka.” Mimi hufanya hivyo daima; kila mara. Lakini mtu awezapo kuona yale Yesu amemtendea, na akageuka na kufanya kitu dhidi yake, inaonyesha yeye hakumpokea Kristo kamwe.
MKATE WA KILA SIKU
Na damu yake Yesu, Mwana wake, yatusafisha dhambi yote. 1 Yohana 1:7
25-0914
65-0427 – Je! Mungu Hubadilisha Nia Yake?
Sasa, ninaamini ya kwamba Yesu Kristo anadumisha kila Neno. Maandiko yote yana pumzi ya Mungu. Siamini tuna haki hata moja, nasi tutahukumiwa kwa hilo, kama tukiongeza neno moja Kwake au kuondoa Neno moja Kwake. Ufunuo 22 inasema hivyo. Ninaamini ni yeye yule jana, leo, na hata milele.
Kwa kweli ninafurahiwa na Walutheri kwa ajili ya msimamamo wao katika siku yao, Wamethodisti kwa ajili ya utakaso katika siku yao, na Wapentekoste kwa ajili ya msimamo wao katika siku yao, bali tunaishi katika siku nyingine. Tunaishi wakati kumekuwa na shina, kishada, kapi, linalofanana sana na Ngano, bali Ngano iko ndani ya kapi. Kapi ndio kwanza limesaidia tu Ngano, limezuia jua kali lisiichome. Na sasa madhehebu yanajiondoa Kwake, kusudi ipate kujianika Mbele za Mwana, ipate kuiva. Kwa hiyo tuko—tuko ndani…Hakutakuwako na madhehebu mengine yatakayoinuka. Huu ndio mwisho wake. Tumekuwa, daima yapata miaka mitatu, wakati ujumbe unapoanza, wao wanauundia madhehebu.
Huu umekuwa ukiendelea kwa karibu miaka ishirini, wala hakuna madhehebu. Haiwezekani. Tuko katika wakati wa Ngano, wakati wa mavuno. Ninaweza kusikia kombaini havesta kubwa ikija. Tunaenda Nyumbani siku moja. “Ni yeye yule jana, leo, na hata milele.”
MKATE WA KILA SIKU
Viacheni vyote vikue hata wakati wa mavuno; na wakati wa mavuno nitawaambia wavunao, Yakusanyeni kwanza magugu, myafunge matita matita mkayachome; bali ngano ikusanyeni ghalani mwangu. Mathayo 13:30
25-0913
55-0312 – Muhuri Wa Kristo
Watu wengine huja kanisani kwa ajili ya sehemu ya kihisia tu. Watu wengine huja kanisani ili kuimba tu. Baadhi ya watu huja kanisani kufurahia tu uimbaji mzuri, hiyo ni sawa. Baadhi ya watu huja kanisani, na kujiunga na kanisa ili tu kuficha ubaya wao, kujitengenezea jina bora zaidi katika ujirani. Wengine huja kanisani kwa uaminifu, lakini hawana mguso wowote kutoka kwa Mungu. Lakini Mungu anapomwita mtu, “Hakuna mtu awezaye kuja Kwangu asipovutwa na Baba Yangu kwanza. Na kila ajaye nitampa Uzima wa milele, nitamfufua siku ya mwisho.”
Loo, natumai unaliona. Ndugu, ni kazi ya Roho Mtakatifu kumfunulia mtu huyo binafsi, si kwa hisia fulani, si juu ya jambo fulani unalopaswa kufanya, ama usilopaswa kufanya, ama hili, lile, ama linginelo. Mambo hayo yote ni sawa, mienendo na vitendo, na kupiga kelele na kucheza, na kunena kwa lugha; mambo hayo yote ni sawa. Lakini jambo la kwanza, haina budi kuwa ufunuo wa kiroho ambao Mungu amempa mtu binafsi, ya kwamba Yesu Kristo ni Mwana wa Mungu, anayeita. Hiyo ni kweli. Bila hivyo, ndugu, unaiga tu, unajifanya tu.
MKATE WA KILA SIKU
Yeye aliye wa Mungu huyasikia maneno ya Mungu. Yohana 8:47
25-0912
50-0227 – Mungu Katika Watu Wake
Mungu hayashukii madhehebu. Mungu haishukii mitambo. Mungu, Roho Mtakatifu, aliwashukia wanadamu. Mwanadamu ndiye wakala wa Mungu, na jambo lililo gumu zaidi ambalo Mungu amewahi kufanya ni kupata mwanadamu mmoja kumwamini mwingine. Je, mnaamini hilo?
Wao hawakuweza kumwamini Musa, na Mungu akampa ishara mbili ili kuwathibitishia watu kwamba alitumwa kutoka kwa Mungu kwa ajili ya ukombozi wao. Mnaamini hilo? Vema, hivi si ni Yeye yule jana, leo na hata milele?
Je! Mnaamini kuwa Malaika aliyenena naye kwenye kichaka kinachowaka moto ni Malaika wa Agano? Hiyo ilikuwa ni kweli? Vema. Ni yeye yule jana, leo na hata milele. Yuko hapa sasa hivi. Naye anafanya mambo yale yale leo aliyoyafanya wakati huo. Na bado angali anafanya miujiza na ishara. Yeye ni Mungu wa miujiza. Na daima Yeye hufanya kazi kwa njia ya miujiza kwa ishara na maajabu. Naye aliyaahidi katika siku hizi za mwisho. Nasi tunaishi katika hizo siku za mwisho. Tunayo haki ya kuyatarajia sasa (hiyo ni kweli) ili kuwaleta watu Wake pamoja.
MKATE WA KILA SIKU
Ishara zake ni kubwa kama nini! Na maajabu yake yana uweza kama nini! Ufalme wake ni ufalme wa milele; na mamlaka yake ni ya kizazi hata kizazi. Danieli 4:3
25-0911
64-0312 – Macho Yao Yalipofumbuliwa,
Mungu hahitaji mfasiri yeyote. Siwezi kulifasiri Neno Lake, wala mtu yeyote kufasiri Neno Lake. Yeye hujifasiria Mwenyewe. Wakati aliposema kuwa angefanya lolote, Yeye analifanya, na hilo latosha. Ni hayo tu. Alisema angelifanya, Naye akalifanya. Hilo latosha. Hamhitaji mtu yeyote kusema hili ni Lile, ama hilo ni Lile. Yeye hulifanya, Mwenyewe. Fasiri zetu si kitu kwa Maandiko. Yeye hunena, Mwenyewe, na hivyo ndivyo lilivyo.
Wakati wa mwanzo, Yeye aliposema, “Iwe nuru,” na ikawa nuru. Hiyo haihitaji fasiri yoyote. “Bikira atachukua mimba,” alichukua! “Nitamwaga Roho Yangu juu ya wote wenye mwili,” akafanya hivyo. Haihitaji fasiri yoyote.
Lile alilosema kuwa angefanya katika siku hii, Yeye amelifanya. Halihitaji kufasiriwa; hujifasiri lenyewe. Yeye Ndiye anayejifasiria Mwenyewe.
MKATE WA KILA SIKU
Mimi, Bwana, nimenena neno hili, nalo litakuwa; nami nitalifanya. Ezekieli 24:14
25-0910
65-0829 – Edeni Ya Shetani
Basi kama Hawa alitamani maarifa, ilikuwa dhambi.
Nasi tunapotamani maarifa (tunataka Ph.D, LL.D.) ni dhambi kufanya hivyo. Huo ni msemo mzito, lakini hiyo ni Ukweli. Haidhuru ni mzito kiasi gani, bado ni Ukweli, mnaona. Kutamani maarifa, ufahamu…
Jambo lenyewe ni kwamba, ni leo hatujaribu kuliimarisha Neno la Mungu katika mioyo ya watu. Tunajaribu kujiimarisha sisi wenyewe! Makanisa yanajaribu kuweka fundisho la kanisa katika moyo wa mtu.
Tumeamriwa kuliimarisha Neno la Mungu. Paulo alisema, “Sikuwajia kwa maneno ya hekima yenye kushawishi akili za watu ili imani yenu isiwe katika hekima ya wanadamu, lakini naja kwenu kwa nguvu; katika madhihirisho ya Roho Mtakatifu ili imani yenu ikae katika Mungu.”
Haya basi.
MKATE WA KILA SIKU
Je! Hamkujua? Hamkusikia? Hamkuambiwa tokea mwanzo? Hamkufahamu tangu kuwekwa misingi ya dunia? Isaya 40:21
25-0909
55-1110 – Maisha Yaliyofichwa Katika Kristo
Sasa, tutazungumza usiku wa leo kuhusu Patakatifu pa patakatifu, mahali pa kukaa ambapo Mungu Mwenyewe alipokaa.
Siku hizo, Yeye alikaa katika maskani Yake. Na leo Yeye anakaa ndani yako kama maskani Yake. Lakini ni lazima tupafanye mahali hapa kuwa makao, si mahali pa ua wa nje, au mahali patakatifu pa kwanza. Lakini ni lazima tuishi pamoja na Mungu katika Patakatifu pa patakatifu, maisha yaliyowekwa wakfu, yaliyofichwa, peke yako, tulivu na Mungu.
Tunachangamka sana, tunakasirika, kuhusu mambo mengi sana. Inaonyesha kuna kitu fulani kinakosekana. Kanisa linapaswa kuwa maili milioni moja juu ya jinsi lilivyo hivi sasa. Bado tumerudi chini katika enzi za utoto, tukizozana, na kupigana, na kugombana, na kuchukizana, wakati inatupasa kujiweka wakfu, tumefichwa katika Patakatifu pa patakatifu pamoja na Mungu.
MKATE WA KILA SIKU
Bali kama yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, ninyi nanyi iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote; 1 Petro 1:15
25-0908
65-0718E – Chakula Cha Kiroho Kwa Wakati Wake
Mnasema, “Hivi kwa nini Ujumbe huu hauendi huko nje kwenye sehemu hizi maarufu kubwa kubwa, mikutano hii mikubwa, kama vile miongoni mwa madhehebu?”
Si Chakula chao. Si Chakula cha linalojiita kanisa. Ni Chakula cha Bibi-arusi. Ni Chakula cha rohoni kwa wakati wake. Kingewachefua tumbo. Ni kinono mno kwao. Mnaona? Mnaona? Hu—hu—huwezi kufanya jambo hilo. Lakini, kwa watoto, Hicho ni Mkate, Hicho ni Uzima, Hicho ni Yesu Kristo yeye yule jana, leo, na hata milele.
MKATE WA KILA SIKU
Yesu akawaambia, Njoni mfungue kinywa. Yohana 21:12
25-0907
61-0122 – Kama Vile Tai Ataharikishavyo Kiota Chake
“Kama mtu aliyetoka,” Yeye alisema, “Ufalme wa Mungu, alitupa jarife baharini, na alipolivuta, alikuwa na kasa, kamba, mijusi, na kila kitu kingine. Akawavuta ufuoni. Hiyo ndiyo kazi ya mhubiri, hatujui yupi ni yupi. Baadhi yao ni samaki, baadhi yao ni mijusi, baadhi yao ni nyoka, baadhi yao kamba.
Mwangalie maskini kamba anapokuwa pale, mtu fulani anasema, “Utukufu! Haleluya!*
*Kasema, “Butu, butu, butu, butu, butu, butu! Siwezi kuamini jambo hilo,” huyo anarudi moja kwa moja majini.
Maskini nyoka anakiinua tu kichwa chake, kusema, “Nilifikiri nilikuwa kanisani, kumbe ni watakatifu wanaojifingirisha,” naye huyu hapa anaondoka.
Yeye alikuwa nini? nyoka tangu mwanzo, kamba tangu mwanzo.
Maskini bibi buibui, dubwiii, anarudi moja kwa moja kwenye shimo la matope tena, akirudi moja kwa moja, akiwa amevalia kaptula, akizikata nywele zake. Ndiyo. Sawa. “Kama nguruwe aendavyo kwenye kugaagaa kwake, na mbwa kwenye matapishi yake,” haya basi. Usikasirike, wewe tulia tu.
MKATE WA KILA SIKU
Kama vile mbwa arudiavyo matapiko yake; Kadhalika mpumbavu afanya upumbavu tena. Mithali 26:11
25-0906
63-0126 – Uwekezaji
Danieli alikusudia moyoni mwake ya kwamba hatajichafua na ulimwengu. Alikuwa anaenda kudumisha utaratibu ambao Mungu alikuwa ameandaa, zile amri za Mungu.
Kwa nini ninyi wanawake na wanaume msiweze kufanya jambo lile lile? Lakini Marilyn Monroe ama mtu fulani walizikata nywele zao, halafu mke wa mhubiri fulani akafanya jambo lile lile, nanyi mnafikiri mna haki ya kufanya hivyo. Hilo haliwaachilii kutoka kwa Neno la Mungu.
Nanyi wahubiri mnawaacha wake zenu wawaongoze. Ni aibu jinsi gani! Ni—ni—ni neno la jinsi gani, la kuwa mwanamume. “Mtumishi wa Kristo asiyeweza kuiongoza nyumba yake mwenyewe, ataongozaje nyumba ya Mungu?”
“Vema,” mnasema, “Ndugu Branham, hayo, hayo ni mambo madogo tu.” Vema.
Hebu na tuyanyoshe mambo yaliyo madogo, ndipo tuliendee jambo kubwa. Mnaona? Ndipo tutazungumza juu ya Roho Mtakatifu, na ma—na mambo ya jinsi ya kupokea karama za Kiungu.
MKATE WA KILA SIKU
Jitakaseni basi, iweni watakatifu, kwa kuwa mimi ndimi Bwana, Mungu wenu. Walawi 20:7
25-0905
57-0818 – Kumbukumbu Za Mungu Zilizojaribiwa Na Wakati
Ninaamini, moja ya siku hizi wakati Kanisa hilo kuu…
Wakati, sayansi inaposema, “Inawezaje kuachilia? Nguvu za uvutano zinakushikilia duniani.”
Sasa ninajisikia kubarikiwa. Hebu niwaambie. Kanisa hilo lililojaribiwa na wakati litakuwepo siku moja. Huenda ikawa nusu yao wamelala katika mavumbi ya ardhi. Sijui walipo, lakini Mungu amezijaribu nyenzo Zake zote. Siku moja Yeye anakuja kuchukua mstari wa mbele: “Nifuateni!” Moja kwa moja kupitia angahewa na anga za juu, na nyanja na nyanja, hadi kwenye Uwepo wa Mwenyezi Mungu atakwenda, pamoja na Kanisa lililojaribiwa na wakati.
MKATE WA KILA SIKU
Umenijaribu moyo wangu, umenijilia usiku, Umenihakikisha usione neno; Nimenuia kinywa changu kisikose. Zaburi 17:3
25-0904
59-1220M – Kongamano Pamoja Na Mungu
Labda wewe ni mwenye dhambi, na umetenda dhambi nyingi sana. Labda ulivuta sigara mpaka huwezi kuzivuta tena, wala huwezi kuachana nazo. Labda umekunywa pombe hata huwezi kuinywa tena, wala huwezi kuiacha. Labda umefikia mahali ambapo umejaa dhambi sana na tamaa mbaya, mpaka inakubidi kumtazama kila mwanamke unayemwona, vibaya. Ama, labda hata umepotosha asili yako mwenyewe. Labda umefika mwisho. Sijali mahali ulipo, Mungu angali yuko tayari kuja kwako, katika kongamano, na kulizungumzia pamoja nawe.
MKATE WA KILA SIKU
Haya, njoni, tusemezane, asema Bwana. Dhambi zenu zijapokuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama theluji; zijapokuwa nyekundu kama bendera, zitakuwa kama sufu. Isaya 1:18
25-0903
64-0125 – Washa Taa
Na leo kuna Mti wa Bibi-arusi; ulianza huko nyuma hapo mwanzo, huko nyuma kabisa katika Siku ya Pentekoste.
Sikilizeni, ninyi watu ambao ni washiriki wa kanisa! Kanisa kamwe halikuanzia huko Nikea, Rumi. Lilianzia huko Yerusalemu, kwenye Siku ya Pentekoste, kanisa lilianza. Ndipo walifanya nini? Waliendelea tu kuunda madhehebu; na Mungu anaendelea kukata matawi. Ndipo wakaunda la Kilutheri; akakata matawi. Wesley; akakata matawi. Pentekoste; akakata matawi. Mpaka imefikia…
Lakini Mungu atakuwa na Mti wa Bibi-arusi! “Yote yaliyoliwa na parare na madumadu wamekula, nitayarudisha,” asema Bwana. Malaki 4 inatwambia tutarudishwa kwenye Imani ya mwanzoni kama ilivyokuwa kwenye Siku ya Pentekoste, “Imani ya baba.” Tunaamini kwamba itakuja. Ninaamini wakati wake umewadia sasa. Matawi yamenyauka na kukauka.
MKATE WA KILA SIKU
…Enyi wanafiki, mwajua kuutambua uso wa mbingu; lakini, je! Ishara za zamani hizi hamwezi kuzitambua? Mathayo 16:3
25-0902
59-0412E – Unasikia Nini, Eliya?
Mara zote si mambo yenye kelele yaliyo mambo makuu. Sio mambo yenye kelele. Gari la mizigo laweza kwenda shambani; linapopakuliwa litadunda, na kunguruma, na kutoa kelele nyingi, linaweza kurudi moja kwa moja juu ya matuta yale yale likiwa limesheheni vitu vizuri, na hata halitatoa mlio. Kwa nini? Limepakiwa. Kile kanisa linachohitaji usiku wa leo ni kupakiwa, kujazwa na upendo wa Mungu.
Jua linaweza kuvuta galoni milioni za maji kwa kelele kidogo kuliko tunavyoweza kusukuma glasi iliyojaa kutoka kwenye pampu. Hiyo ni kweli. M—mbingu zinaweza kunyunyiza umande duniani kote kwa kelele kidogo kuliko unavyoweza kunyunyizia nyasi zako za upande wa mbele. Hakika. Je, umewahi kusikia sayari zikizunguka? Mambo makuu ni mambo ya kimya kimya.
Mwangalie Roho Mtakatifu anapoingia usiku wa leo, jinsi Anavyopata kila kitu kwa ukimya. Lakini sisi tunaendea misisimko, tukikimbilia mambo madogo, tukishindwa kuisikia Sauti hiyo.
MKATE WA KILA SIKU
Lakini BWANA yumo ndani ya hekalu lake takatifu; dunia yote na inyamaze kimya mbele zake. Habakuki 2:20
25-0901
62-0318 – Lile Neno Lililonenwa Ndio Mbegu ya Asili
Billy Graham aweza kuhubiri kila mahali. Oral Roberts, hao watu wacha Mungu, waweza kuhubiri kila mahali. Bwana aweza kunituma kupanda Mbegu mahali pengine, shamba fulani. Lakini naamini taifa letu limepandwa mbegu. Ninaamini iko tayari kwa mavuno sasa.
Roho anaposhuka, na kunakuwa na msukumo kati ya watu, hayo madhehebu yatajikusanya pamoja kwa hakika kama vile ninavyosimama hapa mimbarani, nalo Kanisa la Mungu litafukuzwa. Nao wataifanya njama hiyo, mpaka wataliunda shirikisho, na kususia mtu yeyote asiyekuwa wao.
Rumi itatawala ulimwengu kwa saa moja tu. Itatawala kwa kipande kidogo. Si ukomunisti. Urumi ndio utakaotawala ulimwengu, kwa ushirikiano wa Uprotestanti, katika mfumo wa kimadhehebu wa kanisa ambao Mungu ameukataa. Hiyo ni karibu kama nijuavyo Neno la Mungu.
MKATE WA KILA SIKU
Kisha nikaona mnyama akitoka katika bahari, mwenye pembe kumi, na vichwa saba, na juu ya pembe zake ana vilemba kumi, na juu ya vichwa vyake majina ya makufuru. Ufunuo 13:1
25-0831
62-0513M – Mwenendo Wa Nabii Wa Kweli Wa Mungu
Ee Simba, wa kabila la Yuda, simama na ungurume! Wewe unanguruma katika siku hii ya mwisho. Macho yako yamefinyaa. Unaangalia chini. Unaona dhambi za taifa hili na ulimwengu unaojiita wa Kikristo. Unaona dhambi ya taifa hili, wakati limenunuliwa kwa Damu ya thamani. Unaona jinsi madhehebu yanavyogaagaa juu ya Neno Lako. Unaona jinsi manabii wa uongo wanavyosema uongo. Wanaukana Ukweli wa Mungu.
Nguruma, Ee Simba wa Yuda! Jalia manabii wako wapaze sauti. “Mungu anaponena, ni nani awezaye neno ila kutabiri?” Ni Neno la Mungu likitoka katika Biblia, likipitia kwa nabii. Anawezaje kutulia? Kama angetulia, angepasuka vipande-vipande. Ee Mungu, jalia nabii Wako angurume, Bwana. Nguruma Ujumbe Wako, Mungu, na jalia kila kiumbe cha Ufalme Wako kisikilize.
Jalia wakome. Jalia wanawake wasimame na kujichunguza wenyewe. Jalia wanaume wasimame na wajichunguze wenyewe. Jalia kila mhubiri anayesikiliza kanda hii, asimame na kujichunguza mwenyewe, kwa maana Simba wa kabila la Yuda ananguruma. Na Neno la kweli linawajia manabii, wanene, waseme kwa sauti kuu, “Tubuni mkageuke kabla ya kuchelewa sana.”
MKATE WA KILA SIKU
Simba amekwisha kunguruma, ni nani asiyeogopa? Bwana MUNGU amenena, ni nani awezaye neno ila kutabiri? Amosi 3:8
25-0830
65-1031M – Nguvu Za Kugeuzwa
Unaweza kuuvuka mstari huo. Kama vile wana wa Israeli walivyofanya katika safari yao, wakija kupitia nyikani, Israeli walifanya vivyo hivyo. Baada ya kuusikia ujumbe wa Musa na kuuona ukithibitishwa; wakamsikiliza nabii wa uongo aliyesema, “Loo, sasa angalieni, enyi watoto, sisi sote ni sawa. Tunapaswa kuoana sisi kwa sisi, na tunapasa kufanya hivi.” Naye Musa alikwishawaambia vinginevyo, na wakaona Mungu akilithibitisha. Kwa sababu, Balaamu alionekana kuwa mtu mwenye kuelezea mambo vizuri zaidi kuliko vile Musa alivyokuwa, unaona. Yeye alikuwa ametoka katika taifa kuu ambako kulikuwa na watu mashuhuri, nao wote walikuwa wamejiratibu pamoja katika utaratibu, ile nchi ya Moabu, majeshi makubwa, na mambo makubwa ambayo watu katika siku hizo wangeyaogopa. Na huyu hapa nabii anakuja, nabii, aliyepakwa mafuta, nabii wa uongo aliyetiwa mafuta, unaona, akashuka akaja kwa aliyetiwa mafuta (angalia jinsi walivyofanana), na akawafundisha watu, na wengi wao wakamfuata huyo. Kamwe msisahau jambo hilo. Unaona, wakafuata jambo lile ambalo halikuwa ni Neno, Neno lililothibitishwa na kuhakikishwa!
Msiruhusu mtu fulani aje aingie hapa na kuwaambia jambo la tofauti. Angalia yale Mungu anayothibitisha na kuhakikisha.
MKATE WA KILA SIKU
Msidanganyike, Mungu hadhihakiwi; kwa kuwa cho chote apandacho mtu, ndicho atakachovuna. Wagalatia 6:7
25-0829
60-0925 – Siku Hiyo Pale Kalvari
Gharama iliyolipwa, na utumwa wa Shetani ukavunjiliwa mbali.
Mungu akairudisha mkononi mwa mwanadamu, njia ya kurudia kile alichokuwa akitafuta. Haikumpasa kulia tena. Wakati Yeye alipouvunja uti wa mgongo wa Shetani Kule Kalvari—uti wa mgongo wa dhambi, wa magonjwa—na hiyo ikamrudisha kila mwanadamu duniani katika uwepo wa Mungu huku dhambi zimesamehewa.
Haleluya! Dhambi zetu zimesamehewa! Shetani hawezi tena kututia giza akatuondoa kwa Mungu. Kuna njia kuu iliyotengenezwa. Kuna simu pale. Kuna simu inayoelekea Utukufuni. Inamleta kila mtu karibu na simu hiyo.
Kama mtu amejaa dhambi, inamuunganisha na “makao makuu ya kale.” Anaweza kusamehewa hiyo dhambi. Si hivyo tu, bali dhambi hiyo imekwisha lipiwa tayari. Utukufu! Haikupasi kusema, “Mimi sistahili.” Hakika hustahili. Haungaliweza kamwe kustahili. Bali Mtu aliyestahili alipachukua mahali pako. Uko huru. Haikupasi kutangatanga tena. Haikupasi kuwa mtafuta anasa tena huku nje duniani. Kwa kuwa:
“Damu imebubujika,
Ni ya Imanweli;
Wakioga wenye taka,
Husafiwa kweli.”
Haikupasi kupotea; kuna njia kuu na njia. Nayo inaitwa, “Njia ya utakatifu.” Mwenye taka haipitii, kwa kuwa yeye huja kwenye chemchemi kwanza; kisha anaingia katika njia kuu.
MKATE WA KILA SIKU
Ataniita nami nitamwitikia; Nitakuwa pamoja naye taabuni, Nitamwokoa na kumtukuza Zaburi 91:15
25-0828
55-1110 – Maisha Yaliyofichwa Katika Kristo
Mnaogopa. Watu leo wanaogopa. Mnaogopa nini? Mbona, hata kifo chenyewe hakimtishi Mkristo. “Mauti, u wapi uchungu wako?”
Mawazo yenyewe ya watu yanaogopa. “Loo, Ndugu Branham, daktari aliniambia siwezi kupona.” Unaogopa nini? Kuna upatanisho ulio kwa ajili yako huko ng’ambo. Hakika. “Vema Ndugu Branham, nimefanya dhambi nyingi sana. Nime…” Unaogopa nini? Kuna upatanisho unaokungojea. Kuna Mtu Anayekupenda. Usiogope.
Maneno ya mara kwa mara ya Yesu, “Msiogope. Mimi ndiye niliyekuwa nimekufa, na ni hai tena, na ni hai hata milele na milele. Msiogope.” IPate hali hiyo karibu nawe. IPate hiyo hali.
MKATE WA KILA SIKU
Bwana ni nuru yangu na wokovu wangu, Nimwogope nani? Zaburi 27:1
25-0827
55-1006E – Nguvu za Mungu
Lakini usipoikubali Nuru, itakuwa giza kwako. Utalishutumu, na kuliita mtakatifu anayejifingirisha, nawe unaweza vilevile kufungiwa jiwe la kusagia shingoni mwako, na kuzamishwa katika kilindi cha bahari. Unamkufuru Roho Mtakatifu. Hakuna msamaha.
Alisema, “Yeye anenaye neno juu ya Mwana wa Adamu atasamehewa.
Lakini ukinena dhidi ya Roho Mtakatifu, hilo kamwe halitasamehewa. “
Lakini, loo, ulijua mengi sana. Kwa hivyo ukawadhihaki watu waliokuwa katika Roho wa Mungu, wanaoamini katika uponyaji wa Kiungu, na kukufuka kwa Kristo, na nguvu za Mungu. Ulilifanyia hilo mzaha, ukainua pua yako juu na kutoka nje ya kanisa.
Ninawatakeni muone kitakachotokea usimamapo mbele za yule Mfalme Aliyeutuma Ujumbe huu. Uh-ha. Loo, unafikiri umelipatia, lakini wewe ngoja tu hadi siku hiyo ifike. Hii ni siku ya mwanadamu, siku ya Bwana inakuja. Hiyo ni kweli.
MKATE WA KILA SIKU
Angalia basi, mwanga ulio ndani yako usije ukawa giza. Luka 11:35
25-0826
57-0114 – Uthibitisho Usiokosea wa Ufufuo
Na sasa, wakati Mungu alipoahidi Mzao wa kifalme ambaye angetokea kama Mwokozi, imekuwa ni kazi ya adui—wa Mungu wetu, Ibilisi, kujaribu kumuangamiza huyo Mzao kote kote. Jambo la kwanza, wakati mwana mwenye haki alipozaliwa, Habili, na yule asiye haki alipozaliwa, Kaini, kwanza, alimwua Habili akifikiri alikuwa akimpata yule Mzao mwenye haki.
Kwa maana yeye alikuwa amesimama pale wakati Mungu alipotangaza hukumu za milele za kidunia juu ya watu, na juu yule nyoka, na juu ya nchi, naye aliahidi kupitia kwa mwanamke ungekuja Uzao. Nao Uzao huu ungekiponda kichwa cha nyoka. Naye nyoka alipigana na Uzao huo kotekote katika nyakati, naye angali anapigana nao.
MKATE WA KILA SIKU
Nao watapigana nawe; lakini hawatakushinda; Yeremia 1:19
25-0825
62-0601 – Kuchagua Upande wa Yesu
Mnakumbuka ile ndoto niliyopata tafsiri yake ilivyokuwa. “Rudi ukakihifadhi chakula.” Ghala lilikuwa wapi?—maskani haya. Ni mahali gani nchini palipo kama hapa ambapo pangelinganishwa na ujumbe tulio nao? (Sasa, bila shaka, ndugu zetu hapa walio karibu hapa, makanisa haya mengine madogo, ni sisi. Sisi ni mmoja). Ungeenda wapi, kuupata? Onyesha mahali po pote panapoweza kulinganishwa napo. Ukienda moja kwa moja katika kanuni za kidhehebu, utaenda mbali sana na Jina la Bwana Yesu; utaenda mbali na mambo haya mengine. Ona? Na hapa ndipo chakula kimehifadhiwa.
Vema Ujumbe mmoja niliowahubiria ninyi nyote…Tazama, nimekuwa nikiwahubiria kutoka saa moja hata masaa sita kwa Ujumbe mmoja. Vema, kama ingalinipasa kutumia mmoja wa Jumbe hizo, ningechukua juma moja kuchukua kidogo hapa na kidogo pale (ona?) kwa sababu umehifadhiwa.
Uko kwenye kanda; utaenda ulimwengu mzima katika kanda ambapo watu manyumbani mwao…Hizo kanda zitaangukia mikononi mwa wale waliochaguliwa tangu awali wa Mungu. Yeye anaweza kuliongoza Neno; yeye ataelekeza kila kitu kuelekea njia yake hasa. Hiyo ndiyo sababu Yeye alinituma nirudi nikafanye hivi. “Kihifadhi chakula hapa.” Alinikataza kwenda nchi za ng’ambo.
MKATE WA KILA SIKU
Na hicho chakula kitakuwa akiba ya nchi kwa ajili ya miaka hiyo saba ya njaa, itakayokuwa katika nchi ya Misri, nchi isiharibike kwa njaa. Mwanzo 41:36
25-0824
62-0622B – Kutoa Presha
Wazia jambo hilo, Mungu, katika Siku ya Pentekoste, ile Nguzo ya Moto ilitengana na Ndimi za Moto zikatua juu ya kila mmoja wao, Mungu akijitenga Mwenyewe, akijigawanya Mwenyewe, miongoni mwa watu Wake. Tunakuwa Uzima wa Mungu Mwenyewe ndani yetu, kisha tumekufa kwa mambo ya ulimwengu, na tumefufuka pamoja na Kristo na tumeketi katika ulimwengu wa Roho, tukitazama nyuma tulikotoka.
Inatosha kwamba tungeweza kuliwazia jambo hilo, nalo linaondoa presha, linaondoa presha, tunapotambua nafasi ambayo sasa tunashikilia katika Kristo kwa kupokea Roho Mtakatifu, Uhai wa Mungu Mwenyewe, neno la Kiyunani, Zoe, ambalo linamaanisha Uzima wa Mungu Mwenyewe, ukikaa ndani yako nawe huwezi kufa kama vile Mungu asivyoweza kufa. Sisi ni wa Milele pamoja na wa Milele, amina, tukingojea ule wakati mtukufu wa kukombolewa kwa mwili.
Na sasa tumekufa tayari, nayo maisha yetu yamefichwa ndani ya Mungu kupitia Kristo na kutiwa muhuri na Roho Mtakatifu. Ibilisi yuko nje ya picha kabisa.
MKATE WA KILA SIKU
Lakini Mungu na ashukuriwe atupaye kushinda kwa Bwana wetu Yesu Kristo. 1 Wakorintho 15:57
25-0823
61-0224 – Msiogope
Sasa, kama ungemwendea, Naye alikuwa amevaa suti hii aliyonipa, Naye angesema…ungesema, “Yesu, utaniponya?”
Unajua kile Yeye angekwambia? “Vema, mwanangu, nilifanya hivyo.” Hawezi kufanya hivyo tena. Kama umekombolewa kutoka kwenye duka la rehani, unawezaje kukombolewa mara ya pili? Alikutoa, “Alijeruhiwa kwa makosa yako, na kwa kupigwa Kwake wewe uliponywa.” Mnaona ninalomaanisha? Uponyaji wako tayari umekamilika, wokovu wako umekamilika, jambo pekee unalopaswa kufanya ni kuupokea tu.
Inaleta tofauti gani ni nani anayekuwekea mikono, ni kitu nani kinachofanya hiki, kile, au kinginecho? Popote ulipo, amini tu, hivyo tu, lipokee. Ni, Mungu hana budi kukupa wewe.
MKATE WA KILA SIKU
Yeye mwenyewe alizichukua dhambi zetu katika mwili wake juu ya mti, tukiwa wafu kwa mambo ya dhambi, tuwe hai kwa mambo ya haki; na kwa kupigwa kwake mliponywa. 1 Petro 2:24
25-0822
63-0630M – Kutoka Kwa Tatu
Mungu alimwambia Ibrahimu kabla halijatukia. Lipateni, enyi kanisa linalolala! Mungu alimwambia Ibrahimu kabla halijatukia, “Uzao wako utakuwa mgeni katika—katika Misri, kwa muda wa miaka mia nne, na Mimi nitawatoa.” Hiyo ndiyo sababu waliliona, kwa kuwa waliteuliwa wapate kuliona. Hao ni wateule. Israeli iliteuliwa kuiona ahadi ya Mungu, nao wakatoka Misri, ambako wasioamini waliangamia.
Na, leo hii, Mungu anawaita wateule Wake, Uzao wa kiroho wa Ibrahimu, kwa imani aliyokuwa nayo katika Neno la Mungu. Hivi hamwoni ule Uzao wa kiroho, leo? [Kusanyiko linasema, “Amina.”—Mh.] Ambao haulioni kanisa la kimwili. Unaliona Neno. Nao unaitwa kutoka kwenye hayo madhehebu makubwa, waingie Uweponi mwa Yesu Kristo.
MKATE WA KILA SIKU
… maana nimekukomboa; nimekuita kwa jina lako, wewe u wangu. Isaya 43:1
25-0821
47-0412 – Imani Ni Kuwa Na Hakika
Musa, yule mkombozi mwenyewe, karama ya Mungu kwa watu, hawakumwelewa. Mnaona ninalomaanisha? Hawakumwelewa Musa. Naye Musa alifikiri, kwa hakika, kwamba wangeelewa kwamba yeye alikuwa Ndiye karama yao ya kuwakomboa. Lakini hawakuelewa.
Na sasa, enyi marafiki, msinielewe vibaya. Naomba niseme haya kwa uchaji moyoni mwangu, nikijua ya kwamba mimi ni mtu Niliyefungwa kwa umilele ambaye nitasimama mbele ya hukumu siku moja.
Maelfu ya watu wanaikosa karama yao. Unaona? Hawawezi kuielewa. Nao wataangalia na kusema, “Loo, yeye ni mtu tu.”
Hiyo ni kweli. Je! Ilikuwa ni Mungu au Musa ndiye aliyewakomboa wale watu? Ilikuwa ni Mungu ndani ya Musa. Unaona? Walimlilia mkombozi. Na wakati Mungu alipowatumia mkombozi, wao walishindwa kuliona hilo, kwa maana ilikuwa kupitia mtu. Lakini haikuwa ni mtu; alikuwa ni Mungu ndani ya mtu.
MKATE WA KILA SIKU
Basi ijulikane kwenu ya kwamba wokovu huu wa Mungu umepelekwa kwa Mataifa, nao watasikia! Matendo 28:28
25-0820
55-0225 – Yesu Aliyetukuzwa
Kaini na Habili, wote wa wavulana hao, walitambua ya kwamba walikuwa wapatikanao na mauti, walikuwa wakifa, na kuteketea kama mshumaa, na siku moja lazima warudi mavumbini na kwa yule Muumba aliyewaleta. Na walitaka kupata kibali kwa Mungu. Basi wote wawili wakaja kuabudu.
Hili hapa ni jambo dogo ambalo tunaweza kuliangazia sasa hivi, ili mpate kweli kuelewa…Sasa, nadhani kila mtu anapaswa kuwa mfuasi wa kanisa mahali fulani. Huo ni wajibu wako; unapaswa kuwa mshiriki wa kanisa. Lakini kuwa mshiriki wa kanisa peke yake hakutafaulu. Unaona?
Nafikiri kila mtu anapaswa kuabudu, anapaswa kumwabudu Bwana Yesu Kristo kwa moyo mmoja, usafi wa moyo, lakini hilo tu halitoshi. Ninaamini kila mtu anapaswa kumwamini Mungu, imani thabiti katika Mungu. Lakini bado, hilo silo. Unaona?
Kama kwenda kanisani, kuwa mfuasi wa kanisa, kulipa zaka, kumwabudu Mungu, na mambo haya yote tunayofanya leo yaitwayo dini, Mungu angekuwa dhalimu kumhukumu Kaini, maana alifanya kila moja ya hayo.
MKATE WA KILA SIKU
Kwa imani Habili alimtolea Mungu dhabihu iliyo bora kuliko Kaini; kwa hiyo alishuhudiwa kuwa ana haki; Mungu akazishuhudia sadaka zake. Waebrania 11:4
25-0819
60-0925 – Siku Hiyo Pale Kalvari
Sasa tazama, Yesu alisema…Tazama jinsi alivyolielezea! “Kazi nizifanyazo Mimi…” (Anazifanya hizo sasa hivi.) “Kazi ninazofanya sasa—kuwaponya wagonjwa, kuwafufua wafu, kuyafungua macho ya vipofu—kazi hizi mtazifanya nyinyi pia. Mtazifanya hizi kama mnaniamini Mimi. Mtazifanya hizi kazi, halafu kubwa kuliko hizi mtazifanya. Kwa kuwa naenda kwa Baba Yangu. Bado kitambo kidogo na ulimwengu hautaniona tena. Bali ninyi mtaniona. Nitakuwa pamoja nanyi, hata ndani yenu hata ukamilifu wa dahari. Sitawaacha ninyi bila faraja. Nitamwomba Baba. Naye atawapelekea Msaidizi mwingine, ambaye ni Roho Mtakatifu, ambaye ulimwengu hauwezi kumpokea, bali ninyi mnaweza kumpokea Huyo.”
Sasa tazama zile kazi kubwa zaidi zilikuwa kupata nguvu kanisani, si kuwaponya tu wagonjwa kwa maombi, kuwatoa pepo kwa maombi, bali kuwapa waamini uzima wa milele. Roho Mtakatifu alikuwa yuaja na aliwekwa mikononi mwa kanisa apate kuwapa uzima. Lo! hiyo ndiyo maana ya Kalvari.
Alichukua wanaume na wanawake waliodhiliwa na walioshushwa vyeo naye akawainua mpaka mahali ambapo wamekuwa wana na binti za Mungu, kuwaponya wagonjwa na kuwapa uzima wa milele. Kwa kuwapa Roho Mtakatifu waaminio watiifu. Watu ambao siku moja walikuwa wasioamini kuwafanya waamini na kuwapa uzima wa milele.
MKATE WA KILA SIKU
Amin, amin, nawaambieni, Yeye aniaminiye mimi, kazi nizifanyazo mimi, yeye naye atazifanya; naam, na kubwa kuliko hizo atafanya, kwa kuwa mimi naenda kwa Baba. Yohana 14:12
25-0818
57-0306 – Mungu Hutimiza Neno Lake #1
Jichanganyeni pamoja, na muwe na uamsho wa muungano; pateni wahubiri wadumuo na Neno la Mungu, na sio kutawanyika hapa. Soma Neno. Baadhi yenu hamlisomi Neno ila mara moja kwa wiki. Unapaswa kusoma sura baada ya sura kila siku. Tafakari; kama mngeviondoa vichwa vyenu kutoka kwenye hayo magazeti ya kale na mambo mnayoyasoma, na kutoka kwenye haya ya kale, makaratasi mengi sana, na yale yanayoitwa fasihi ya kidini ambayo hayafai kamwe kuwa sokoni… Hayo ni mabaya tu kama kusoma baadhi ya yale magazeti mengine, mambo yaliyo mafundisho ya uongo, na kila namna ya kanuni za imani, na kuliwekea msingi hilo kwenye_kwenye kweli. Mbona, fundisho haliwezi kutegemea uzoefu fulani. Fundisho linategemea Neno la Mungu, si uzoefu. Watu wanaweza kuwa na uzoefu wa kila kitu.
MKATE WA KILA SIKU
Hata nitakapokuja, ufanye bidii katika kusoma na kuonya na kufundisha. 1 Timotheo 4:13
25-0817
63-0120M – Sauti Ya Mungu Katika Siku Hizi Za Mwisho
Kama wewe ni mwaminio vuguvugu tu, Sauti ya Mungu inapaza sauti moyoni mwako asubuhi ya leo, “wewe ni mwaminio vuguvugu,” afadhali utubu!
Wewe mwanaume, wanawake, wavulana ama msichana, ambao hammwishii Kristo, na Sauti ya Mungu inasema nanyi kupitia kwenye Neno Lake na kusema “acha kufanya jambo hilo,” afadhali ufanye hivyo. Kwa sababu utaisikia tena siku moja, Nayo itakuhukumu. Huwezi kuikana, inazungumza nawe sasa. Na, kumbuka, inarekodiwa.
Na wale wanaotenda mema na kuisikia Sauti Yake, watafufuka katika haki, kwa Utukufu, waende Mbinguni.
MKATE WA KILA SIKU
Mwenye masikio, na asikie. Mathayo 11:15
25-0816
65-1127E – Nimesikia, Bali Sasa Ninaona
Sasa wakati tunapokwenda kuombewa, kwa ajili ya magonjwa yetu, sijui kama tumefanya kila kitu Mungu anachotutaka tufanye. Je! tumefuata kila yodi ya Maandiko? Je! tumempa mioyo yetu na maisha yetu kwa utumishi? Ni kwa nini unataka kuponywa? Hiyo ndiyo sababu huwezi kupata imani ya kutosha, unaona, kwa maana labda hujafanya jambo hili kwa Mungu kwa uaminifu kutoka moyoni mwako. Kama vile Hezekia alivyofanya, alivyompa Mungu sababu, alitaka kuweka ufalme wa—wake sawa. Ndipo Mungu akamtuma nabii Wake arudi na kumwambia, na kwamba angepona. Unaona? Lakini, huna budi kuweka mambo hayo sawa, kwanza.
Ndipo mara unapofikia hali hizi na kujua ya kwamba imefunuliwa kwako kwa Neno la Mungu, kwa ufunuo, kwa Neno ambalo Mungu anakutaka ufanye, basi una imani, imani halisi.
MKATE WA KILA SIKU
Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi. Itakaseni mikono yenu, enyi wenye dhambi, na kuisafisha mioyo yenu, enyi wenye nia mbili. Yakobo 4:8
25-0815
61-0217 – Alama Ya Mnyama Na Muhuri Wa Mungu #2
Angalia, “Mtu asipozaliwa mara ya pili, hawezi kamwe kuingia katika ule Ufalme.” Hiyo ni kweli. Huna budi kuja, haidhuru wewe ni wa kidini jinsi gani, yote ufanyayo, hayo hayana uhusiano wowote. Hayo yanakufanya raia mwema sana, bali si raia wa Ufalme huo kule, labda wa ufalme huu hapa. Lakini Ufalme wa Mungu uko ndani yako, umezaliwa katika Ufalme. Ufalme huja katika…Ufalme wa Mungu ni Roho Mtakatifu, wewe ni wa Ufalme huo.
Hiyo ndiyo sababu wanawake hawakati nywele zao, hawavai kaptura; hiyo ndiyo sababu wanaume hawavuti sigara, na mambo kama hayo, wanatoka Juu, Roho wao huwafundisha haki, utakatifu. Hawa—hawaapi, hawa—hawatumii lugha mbaya, na kadhalika. Kwa nini? Wamezaliwa kutoka Juu, wao ni tofauti, wanatoka, raia kutoka Juu.
MKATE WA KILA SIKU
Wala hawatasema, Tazama, upo huku, au, kule, kwa maana, tazama, ufalme wa Mungu umo ndani yenu. Luka 17:21
25-0814
63-0707M – Lile Shtaka
Walimshtakije? Kwa sababu kanuni zao za imani hazingalimkubali. Na ndani mioyoni mwao walijua tofauti. Je, si Nikodemo, katika sura ya 3 ya Injili ya Yohana, alieleza vema? “Rabi, sisi, Mafarisayo, wahubiri, waalimu, twajua ya kuwa Wewe u mwalimu, kutoka kwa Mungu; kwa maana hakuna mtu awezaye kufanya ishara hizi uzifanyazo Wewe, isipokuwa Mungu yu pamoja naye.” Mwaona? Wao waliishuhudia hadharani kupitia kwa mmoja kati ya watu wao mashuhuri. Ingawaje, kwa ajili ya kanuni za imani zao wao walimsulubisha Kristo.
Na leo hakuna msomaji ambaye hawezi kusoma Matendo 2:38 kama vile mimi niwezavyo kuisoma, na mengineyo jinsi mimi niwezavyo kuyasoma. Lakini kwa ajili ya kanuni za imani zao na kwa ajili ya—ya tikiti zao za kidhehebu walizo nazo mifukoni mwao (ile chapa ya mnyama wanayoibeba kama kadi ya ushirika)…Na kwa kuchukua mambo hayo, wao humsulubisha Yesu Kristo upya kwao wenyewe, na kumsulubisha kwa umma; na kukufuru Mungu yule yule aliyeahidi kutenda hili, wakileta laana juu ya kizazi hiki.
MKATE WA KILA SIKU
Alikuja kwake, wala walio wake hawakumpokea. Yohana 1:11
25-0813
63-0112 – Ushawishi
Sasa angalia. Sikuzote sikilizeni. Tambua udogo wako.
U nani wewe? Ingiza kidole chako kwenye ndoo ya maji na kukitoa, kisha tafuta shimo ulimoingiza kidole chako. Kisha useme, “Huyo alikuwa ni mimi.” Wewe si kitu. Hutakumbukwa baada ya, muda mfupi baada ya wewe kuondoka. Wana msafara wa mazishi hapa nje, na ni hayo tu. Lakini ushawishi wako utaendelea kuishi, na kuendelea, na kuendelea.
Hiyo ndiyo sababu leo hii, katikati ya makafiri, kamwe hawajawahi kuelezea na kupata njia ya kuuondokea ushawishi wa Mtu mmoja, Yesu Kristo, Yule aliyekuwa ni Mungu aliyefanyika mwili. Wakati alipoutoa uhai Wake huku chini duniani, ulifanya mahali pa kufyonza ambapo huwavuta watu wote Kwake, katika ule mzunguko mkuu wa maisha Yake yaliyokuwa duniani wakati mmoja. Huwezi kuukaribia pasipo kuingizwa ndani yake.
178 Lakini, mimi na wewe, sisi si kitu. Sisi si kitu.
MKATE WA KILA SIKU
Lakini hutujalia sisi neema iliyozidi; kwa hiyo husema, Mungu huwapinga wajikuzao, bali huwapa neema wanyenyekevu. Yakobo 4:6
25-0812
60-0925 – Siku Hiyo Pale Kalvari
Hatimaye siku moja—hiyo ni ile siku pale Kalvari—Mtu mmoja akashuka akaja kutoka Utukufuni— Mtu mmoja aliyeitwa Yesu Kristo, Mwana wa Mungu Yeye aliyetoka Utukufuni, kisha Kalvari ikatengenezwa. Hiyo ndiyo siku ambayo ile gharama ililipwa, na swali la dhambi likatatuliwa milele, naye akafungua njia ya kitu hiki tunachokionea njaa na kukionea kiu. Ilileta mahali pa utoshelevu.
Hakuna mtu aliyepata kutembelea Kalvari na kuona jinsi ilivyokuwa, anayeweza kubaki alivyokuwa. Kila alichoonea shauku au kutamani sana kinapatikana anapofika mahali hapo. Ilikuwa siku muhimu sana na jambo muhimu sana, hata ikaitikisa dunia. Iliitikisa dunia jinsi ambavyo haijatikiswa hapo awali, Yesu alipokufa pale Kalvari naye akalilipia swali la dhambi.
Dunia hii yenye dhambi ilitiwa giza kabisa. Jua lilitua mchana nalo likazimia roho kwa wasiwasi. Miamba ikatikisika. Milima ikapasuka. Miili ya waliokufa ikafufuka ghafla kutoka kaburini.
MKATE WA KILA SIKU
Siku ya pili yake amwona Yesu anakuja kwake, akasema, Tazama, Mwana-kondoo wa Mungu, aichukuaye dhambi ya ulimwengu! Yohana 1:29
25-0811
54-0624 – Kilindi Kikiita Kilindi
Kilindi kikiita kilindi: kama kilindi kinaita, kuna kilindi cha kuitika. Kwa maneno mengine, kabla hapajakuwa na mti unaokua duniani, ilibidi kuwe na ardhi ya kukulia kwanza. Mungu kwanza hakuumba mti kwa ajili ya ardhi, aliiumba ardhi kwa ajili ya mti. Aliiumba ardhi kisha akaiamuru ardhi izae mti. Nayo ardhi ilikuwa ikiita, mpaka mti ukatokea. Kabla hakujakuwa na pezi kwenye mgongo wa samaki, hapakuwa na maji apate kuogelea. Kusudi la yeye kuwa na pezi, ni kwa sababu kulikuwa na maji apate kuogelea kuitumia. Kila kitu tulicho nacho kina kusudi na sababu fulani.
MKATE WA KILA SIKU
Kilindi chapigia kelele kilindi kwa sauti ya maboromoko ya maji yako, Gharika zako zote na mawimbi yako yote yamepita juu yangu. Zaburi 42:7
25-0810
59-0823 – Tunutu, Nzige, Parare, Madumadu
Na kama Mungu hana kikomo, hana kikomo, wala hawezi kubadilika, Kanisa Lake halina budi kubaki kama lilivyokuwa hapo mwanzo. Je, mnakubali hilo? Kanisa halina budi kubaki kama lilivyokuwa.
Bali mwanadamu ameliingilia ovyoovyo, wakaweka tafsiri zao wenyewe ndani Yake. Kamwe usijaribu kulifasiri Neno la Mungu. Sema tu kile Hilo lisemacho. Haijalishi jinsi lilivyo, kwa hiyo ambatana tu na Hilo, hivyo tu. Usilibadilishe Neno. Biblia ilisema, kwamba, “Maandiko si ya kutafsiriwa apendavyo mtu kibinafsi.” Hatuna haki ya kusema mambo haya; inatubidi tu kulisoma na kusema jinsi tu lisemavyo, na kuliamini vivyo hivyo. Sijali jinsi linavyoonekana la kijinga; liamini, kwa vyovyote vile.
MKATE WA KILA SIKU
Likiwa jema, au likiwa baya, sisi tutaitii sauti ya Bwana, Mungu wetu. Yeremia 42:6
25-0809
56-0814 – Upendo wa Kiungu na Neema kuu
Nimeingia…nilikuwa nikiendesha kwelikweli. Nimepanda miaka mingi katika mzunguko na kadhalika; na nimetembea maeneo ya farasi wa mwituni, na kwa namna fulani katika dakika chache, angeweka kichwa chake juu ya bega langu. Ningemvika tu blanketi, na kumwendesha kwa muda kidogo akiwa na blanketi juu yake, kisha nikamtupia tandiko, na muda si muda wajua, ningekuwa nimempanda kote. Unaona? Yeye—anakupenda. Na ikiwa kweli unampenda, yeye anajua.
Sasa, sikilizeni, nataka kuwaambia jambo fulani. Wanadamu wana akili zaidi kuliko wanyama, na huwezi kuwaambia watu unawapenda…Hawataamini, isipokuwa kuwe na jambo halisi kuthibitisha hilo. Kwa hiyo unasema, “Loo, ndugu, unajua tuna ushirika mkubwa sana.” Na chini ya moyo wako kinyongo? Anajua tofauti. Mungu anajua hilo. Jirani yako anajua hilo. Unapaswa kuwa safi na mkweli, na kusema, “Bwana Mungu, umba ndani yangu moyo safi wa kupenda.”
MKATE WA KILA SIKU
Wapenzi, na mpendane; kwa kuwa pendo latoka kwa Mungu, na kila apendaye amezaliwa na Mungu, naye anamjua Mungu. 1 Yohana 4:7
25-0808
54-0513 – Alama Ya Mnyama
Lakini, katika kila kanisa, tuna fundisho.
Mara nyingi, katika mashirika, madhehebu, wana kanuni ya imani. Nao wanadumu katika kanuni hiyo ya imani, “Hii ndiyo kanuni yetu ya imani.” Haidhuru mhudumu anawazia jambo gani, hana budi kufundisha hiyo kanuni ya imani, kwa maana yeye yumo katika hayo madhehebu.
Basi humu ndani, hatuna kanuni ya imani ila Kristo, huyo ndiye kanuni ya imani; na hakuna sheria ila upendo; hatuna kitabu ila Biblia. Naye Kristo ndiye Kichwa; nayo Biblia ndiyo kitabu chetu cha mafundisho; dunia ndiyo uwanja wangu. Kwa hiyo napenda—napenda kuhubiri tu jinsi ninavyojisikia ninaongozwa kuhubiri, na jinsi tu ninavyoliona.
MKATE WA KILA SIKU
Mwenye masikio, na asikie. Mathayo 11:15
25-0807
63-1222 – Karama Za Mungu Daima Hupata Mahali Pao
Mariamu, mama wa Yesu, katika mji wa Nazareti, mji duni kuliko yote uliokuwapo nchini, bali kutoka pale Mungu alichagua mama mdogo kumzaa Mwana Wake; kiangulio, tumbo la uzazi ambalo ilibidi…ilibidi Mtoto azaliwe kwalo. Alimchukua mtu kama huyo kufanya hivyo. Mungu hufanya kazi kupitia wanadamu kuwakomboa wanadamu. Anaweza kukuchukua, afanye kazi kupitia wewe ili kukomboa wanadamu, iwapo utasalimisha kabisa kila kitu ulicho.
Kama wewe ni msichana, salimisha maadili yako. Wewe ni kijana mwanamume, salimisha maadili yako, salimisha nia yako, salimisha mawazo yako, salimisha moyo wako, salimisha nafsi yako, salimisha yote uliyo! Na umwache Kristo afanye kazi kupitia hayo. Ni jambo tukufu jinsi gani!
MKATE WA KILA SIKU
…simameni imara katika Bwana, wapenzi wangu. Wafilipi 4:1
25-0806
62-0211 – Umoja
Shetani ni mwerevu zaidi kuliko Hawa. Yeye hakuninii…hata hakuwa kwenye picha. Bali hakupaswa kuwa mwerevu, alipaswa kuwa mtiifu. Hatupaswi kuwa werevu. Yesu alisema wana wa ulimwengu huu, ama, ufalme wa ulimwengu huu ni mwerevu zaidi, watoto wa giza kuliko watoto wa Nuru. Tunafananishwa na kondoo. Kondoo hawawezi hata kujiongoza wenyewe, hawana budi kuwa na mchungaji. Mungu hatutaki tuwe werevu, Yeye anatutaka kuzitegemea akili Zake, amina, mahali tu Yeye aongozapo. Amina. Mnaiona hiyo picha? Usizitegemee akili zako mwenyewe. Methali 5, 3. Usizitegemee akili zako mwenyewe, tegemea akili Zake. Haijalishi inaonekana ni kinyume namna gani, na jinsi nuru kubwa zinavyoonekana angavu hapa nje, usizijali. Tegemea tu akili Zake, yale Yeye aliyosema ni Kweli.
MKATE WA KILA SIKU
Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote, Wala usizitegemee akili zako mwenyewe. Mithali 3:5
25-0805
50-0115 – Je! Unasadiki Hayo?
Si muda mrefu uliopita, nilikuwa nimesimama karibu na jumba la makumbusho. Kuna picha ya mtu hapo, ratili mia na hamsini. Nayo-inatoa uchambuzi wa kemikali za mwili wake. Ana thamani ya senti themanini na nne. Hiyo ndio thamani yote ya mtu mwenye ratili mia na hamsini, ni senti themanini na nne. Lakini atahakikisha anaweka kofia ya dola kumi kwenye senti hiyo themanini na nne na kufikiri yeye ni kitu fulani kikubwa. Hiyo ni kweli. Mwanamke ataivika senti hiyo themanini na nne kanzu ya manyoya ya dola mia moja naye hatazungumza na nusu ya majirani zake.
Kuna nini? Upendo wa Mungu unakupeleka mahali fulani. Hiyo ni kweli. Ni kitu gani? Bado ni ile senti themanini na nne. Utaishughulikia hiyo sawa. Lakini nafsi hiyo iliyo na thamani ya dunia elfu kumi, utaacha chochote kidumbukizwe ndani yake. Hiyo ni kweli. Huo ndio ukweli.
MKATE WA KILA SIKU
Vivyo hivyo wanawake na wajipambe kwa mavazi ya kujisitiri, pamoja na adabu nzuri, na moyo wa kiasi; si kwa kusuka nywele, wala kwa dhahabu na lulu, wala kwa nguo za thamani; 1 Timotheo 2:9
25-0804
61-0827 – Ujumbe Wa Neema
Wazieni juu yake: Upendo na neema ni dada, dada mapacha. Huwezi kuwa na neema pasipokuwa na upendo. Hao ni dada mapacha. Kweli kabisa. Kabla hujaweza kupata neema, huna budi kuwa na upendo. Kabla kweli hujamwonyesha mtu fadhili, unawapenda; sahihi ama makosani, huna budi kuwapenda, kwa vyovyote vile, la sivyo huwezi. Unaona? Kwa hiyo upendo na neema ni kitu kile kile. Hao ni dada mapacha tu, hivyo tu, upendo na neema. Wao, sisi tulikuwa…Hatuwezi kumwona mmoja bila huyo mwingine. “Mungu aliupenda ulimwengu, akamtoa Mwanawe pekee,” Yeye alitoa neema Yake, na kuileta mioyoni mwetu kupitia Roho Mtakatifu. Mnaona? Hakuna kabisa kitu unachoweza kufanya bila ya kutenda kazi na moja kwa nyingine. Neema, neema ya Mungu ndiyo inayotuokoa.
MKATE WA KILA SIKU
Neema na iwe pamoja na wote wampendao Bwana wetu Yesu Kristo katika hali ya kutokuharibika. Waefeso 6:24
25-0803
64-0614M – Kufunuliwa Kwa Mungu
Neno Lake linafunuliwa kwa mmoja. Daima imekuwa hivyo, nabii alikuja na Neno la Bwana, kila kipindi cha wakati, kila wakati, kote katika Maandiko. Neno humjia mmoja. Katika kila wakati, vivyo hivyo, hata katika nyakati za kanisa, tangu wa kwanza hadi wa mwisho. Wengine wana mahali pao, hiyo ni kweli, angalia, lakini kaeni mbali na hiyo Nguzo ya Moto. Unaona? Ni somo la jinsi gani tunalosoma hapa! Unaona, kila mtu akitaka kuwa Musa, na kila mtu…
Mnakumbuka yale Dathani na hao wengine waliyosema kule njiani? Walisema, “Sasa, Musa, hebu ngoja hapa kidogo tu! Unajitukuza sana, unaona. Sasa, wapo watu wengine hapa ambao Mungu amewaita.”
Hiyo ni kweli. Wao, kila mmoja, walikuwa wakifuata vizuri mradi tu waliendelea mbele, lakini wakati mmoja alipojaribu kuinuka na kuchukua nafasi ya Mungu ambayo alikuwa amempa Musa, ambaye alikuwa amekusudiwa tangu zamani na kuchagulia kwa ajili ya kazi hiyo, alipojaribu kupachukua, moto ulishuka na ukaifunua nchi na kuwameza moja kwa moja ndani yake. Unaona? Unaona? Kuwa mwangalifu. Unaona? Kuwa mwema tu, Mkristo wa Mungu mcha Mungu, ukiliamini Neno. Unaona? Kaa mbali na hiyo Nguzo. Ni somo la jinsi gani!
MKATE WA KILA SIKU
Kwake nitanena mdomo kwa mdomo, Maana, waziwazi wala si kwa mafumbo; Na umbo la Bwana yeye ataliona. Mbona basi ninyi hamkuogopa Kumnenea mtumishi wangu, huyo Musa? Hesabu 12:8
25-0802
53-0609A – Elimu Juu ya Pepo, Milki ya Kidini
Mnajua, kuna—kuna wa uongo. Kuna cha kweli na cha uongo kwa kila kitu. Kama nikikupa dola, nami niseme, “Je! hii ni dola nzuri?” Nawe ungeiangalia, na ingebidi ionekane zaidi sana kama dola halisi la sivyo hungeiamini. Hiyo ni kweli? Kwa hiyo haina budi kuwa ni bandia nzuri kweli.
Na kama Yesu alisema roho hizo mbili katika siku za mwisho zingefanana sana hata zingewadanganya walio Wateule kama yamkini, watu wa kidini. Sasa kumbuka. Sasa, hakuna kitu huko nje kwa ajili ya hayo ninii ba-…kide-…ninii baridi, ya kidesturi. Kwa nje wao wana mfano tu wa utauwa, mnaona. Lakini roho hizi mbili, roho halisi, zingefanana sana hata zingewapoteza walio Wateule, jinsi zilivyokuwa zikitenda kazi sambamba katika siku za mwisho. Je! Yesu hakusema jambo hilo? Alisema.
MKATE WA KILA SIKU
Mtu asiwadanganye kwa maneno yasiyo na maana… Waefeso 5:6
25-0801
47-1123 – Wana wa Israeli
Tuko katika hatua yetu ya tatu na ya mwisho. Na kumbukeni, wakati wa Kipentekoste ni wakati uliokataliwa. Sipendi kusema hilo, kwa maana sijawahi kuona imani katika kanisa lolote kama kanisa la Kipentekoste. Lakini limekataliwa, kwa sababu ni wakati wa mwisho wa kanisa la Laodikia, vuguvugu. Umetapikwa kutoka katika kinywa cha Kristo. Lakini Mungu mle ndani atawatoa watu Wake, kutoka katika wakati huo wa Kipentekoste.
Unasema, “Vema, ninatazamia wakati mkuu.” Ninajua, wengi wenu ninyi watu…Kunalo fundisho, shule za manabii. Nao wangesema ni wakati uliyo mkuu wa kanisa unaokuja. Usiamini jambo hilo. Kitu kinachofuata ni Kristo kuja kwa ajili ya Kanisa Lake. Hiyo ni kweli. Kwa…Kwa hiyo kumbuka, wakati wa mwisho wa kanisa ni wakati wa kanisa la Laodikia, uliyo vuguvugu ambao umetapikwa kutoka katika kinywa cha Mungu. Ni kweli. Nanyi mnajua jambo hilo.
MKATE WA KILA SIKU
Alikuja kwake, wala walio wake hawakumpokea. Yohana 1:11
25-0731
55-0223 – Ayubu
Kuna habari za kukaribisha kwako usiku wa leo. Wakati Mungu, akijivua Mwenyewe, akitoka katika majumba ya kifalme, akijitwalia yeye mwenyewe umbo la mwili wenye dhambi, kujinyenyekeza ili ashuke, kuwa Jamaa wa karibu wa maskini ombaomba aliyeko ulimwenguni usiku wa leo, apate kuwa Jamaa yake. Yehova Mwenyewe, alijifanya wa jamaa aliye wa karibu kwa ombaomba. “Mbweha wana mapango, na ndege wana viota, lakini Mwana wa Adamu hana mahali pa kulaza kichwa chake.” Amezaliwa horini, amevikwa nguo za kitoto, hata hivyo ndiye Mkuu wa Utukufu, Mapambazuko kutoka juu. Akijinyenyekeza, kujishusha mwenyewe, akishuka, kuja kufanywa Jamaa wa karibu wa mwenye dhambi. Wazieni hilo, enyi watu. Unawezaje kukataa upendo huo usio na kifani?
Ilikuwa ni kitu gani? Wakati Mungu alipofanyika mwenye dhambi, kuzichukua dhambi zetu. Yesu alifanyika mimi, ili mimi nipate kuwa Yeye. Mwana-Kondoo wa Mungu asiye na hatia, Asiyejua dhambi, alifanyika mwenye dhambi, ili mimi nifanywe mwana wa Mungu.
MKATE WA KILA SIKU
Alikuwako ulimwenguni, hata kwa yeye ulimwengu ulipata kuwako, wala ulimwengu haukumtambua. Yohana 1:10
25-0730
52-0713E – Mungu Akizishuhudia Karama Zake
Unapochukua msimamo wako kwa ajili ya Yesu Kristo, kaa hapo na ulifie jambo hilo. Yale asemayo Mungu ni kweli, nawe usiogope kile…Shetani hana lo lote la kufanya juu ya jambo hilo. Wewe usihojiane naye; usibishane naye. Wewe mpuuze tu na uondoke zako. Endapo ukibishana naye, atakufanya ubishane mchana na usiku. Unaona? “Vema,” yeye atasema, “Unajua hujaponywa.”
Utasema, “Vema, sasa, tazama, Shetani, nataka kukuambia jambo fulani.” Usiliseme. Wewe Sema tu, “Ondoka, sitaki kusikia lo lote kukuhusu.” Na uendelee kwenda, na useme, “Asante, Bwana.” Endelea. Unaona? Usivutie usikivu wo wote kwa jambo hilo.
MKATE WA KILA SIKU
Nimemweka BWANA mbele yangu daima, Kwa kuwa yuko kuumeni kwangu, sitaondoshwa. Zaburi 16:8
25-0729
64-1221 – Kwa Nini Ilibidi Iwe Ni Mchungaji Wa Kondoo
Sasa hebu na tufunge tu macho yetu, tuwazie juu ya Yehova. Hakuna mtu aliyestahili, hakuna mtu angaliweza kufanya jambo hilo ila Yeye. Naye alishuka akaja, na akawa mtoto mchanga. Yeye alikuja, tineja. Akawa seremala, mfanyakazi. Alifanyika Mwana-Kondoo, alifanyika dhabihu. Alifufuka kwa shangwe ya ushindi, Yehova. Na kama vile Musa alivyoutoa mkono wake kutoka kifuani mwake juu ya moyo wake, Mungu aliutoa mkono Wake kutoka kifuani Mwake (siri Yake) Mwanawe aliyepigwa na ugonjwa wa dhambi, isiyotibika; kisha akaurudisha kifuani tena, na kuutoa na kuuweka kwako na kwangu mimi: “Yesu Kristo yeye yule jana, leo, na hata milele.”
Mwangalieni Yeye sasa.
MKATE WA KILA SIKU
Kwa maana Baba mwenyewe awapenda kwa kuwa ninyi mmenipenda mimi, na kusadiki ya kwamba mimi nalitoka kwa Baba.
Nalitoka kwa Baba, nami nimekuja hapa ulimwenguni; tena nauacha ulimwengu; na kwenda kwa Baba. Yohana 16:27-28
25-0728
53-0405E – Mashahidi
Mnajua, nafikiri, siku hizi, tunawazika watu wengi kupita kiasi walio hai.
Mnazika watu wakiisha kufa. Hiyo ni kweli? Naaam, bwana. Sikiliza, ndugu, mtu aliyekufa hatabishana nawe. Unaweza kumwambia chochote unachotaka, umwite majina ya kila namna, hatasema neno. Kwa nini? Amekufa.
Na mtu ambaye amekufa katika Kristo, unaweza kumpa pombe, unaweza kumpa hiki, kile, ama kinginecho, lakini amekufa. Naye amefichwa ndani ya Kristo, kwa njia ya Mungu, ametiwa muhuri na Roho Mtakatifu. Amina. Ndiyo hiyo. Sasa, basi, hawezi kufanya mambo hayo, kwa sababu ha—hawezi tu kufanya hivyo. Ni kinyume na asili yake. Anakuwa kiumbe kipya.
Hebu mchukue nguruwe mzee na kumwosha, na kumsugua, na kuzipodoa kucha za vidole vyake vya miguu, na kumpa rangi ya mdomo, na kumvika, nailoni zote utakazo; mfungulie, ataenda moja kwa moja kwenye kugaagaa na kugaagaa. Kusugua hakufai kitu. Angali ana asili ya nguruwe.
Na kisha mchukue mwana-kondoo na kumtia kwenye shimo la matope, atapiga kelele mpaka umtoe nje. Kwa nini? Yeye ni asili ya mwana-kondoo.
Sasa, njia pekee ya kumzuia nguruwe asiingie kwenye matope ni kuibadilisha asili yake. Hiyo ni kweli.
Hiyo ndiyo njia pekee ya kumfanya Mkristo. Asili yake ibadilishwe, kutoka mwenye dhambi kuwa mtakatifu. Unaona? Na kuna dawa moja tu, hiyo ni Roho Mtakatifu. Ndipo wewe ni shahidi. Amina.
MKATE WA KILA SIKU
Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya. 2 Wakorintho 5:17
25-0727
60-0805 – Mwana-Kondoo Na Hua
Wakati Mungu alipomuumba mtu kwanza, alimuumba akiwa vyote mwanamume na mwanamke katika Roho; Alimfanya kwa mfano Wake Mwenyewe, na Mungu ni Roho. Wakati Alipomtenga na kumweka katika mwili, Aliiweka roho ya kiume ndani ya mwanamume, na roho ya kike ndani ya mwanamke, na kama kitu chochote ni kinyume na hilo, kuna upotovu kidogo hapo. Kabisa.
Unamwona mwanamke anajaribu kujifanya mwanamume, kuna kasoro fulani kidogo pale, seli imevuka mahali fulani. Hiyo ni kweli. Unamwona mwanamume dondoa dume kiasi kwamba hatahubiri dhidi ya dhambi ama kitu kingine kama hicho, kuumiza hisia za mtu fulani, kuna mchanganyo hapo mahali fulani, pia, si tu kuzaliwa kwake kwa kawaida, bali kuzaliwa kiroho. Loo, tunachohitaji leo hii ni kwamba mwanamume awe mwanamume, mwanamke, Mwanamke. Mungu amekusudia wawe jinsi hiyo, wavae tofauti.
Unasema, “Unatupiga nyundo sisi wanawake.”
Sasa nitawaambieni kuhusu wanaume. Mwanamume ye yote ambaye atamruhusu mke wake avute sigara, na kuvaa hizo kaptura, na kutenda jinsi hiyo, kuna uwanaume mdogo sana ndani yake, nionavyo mimi.
MKATE WA KILA SIKU
Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba. Mwanzo 1:27
25-0726
58-0128 – Umoja Wa Muungano
Yesu hangewaruhusu wanafunzi Wake kuhubiri Injili mpaka walipompokea Roho Mtakatifu. Hata hivyo, walikuwa wamepewa heshima ya kutembea pamoja Naye, miaka mitatu na nusu. Ingawa walikuwa watu watakatifu, waliokubalika machoni Pake, lakini Yeye hakuwaacha waende kuhubiri mpaka walipongoja kule juu na kujiondolea tofauti zote, ndipo Roho Mtakatifu akaja.
Kile ambacho ulimwengu unahitaji siku hizi ni ujazo uo huo. Kufanywa tupu kunapokuja, kujazwa kunahitajika. Ujazo huo hufanya nini unapoingia? Mahali ulipo na shaka, huleta imani. Mahali ulipo na kutokujali, huleta upendo. Mahali ulipokuwa na chuki, huleta ushirika.
Na halafu, wakati, Kanisa la Mungu aliye hai siku moja litaunganishwa chini ya Kichwa kimoja kikuu, na hicho kitakuwa ni—ni Kichwa cha Mungu. Mungu, na katika umoja wa Mwili wa Kristo, atakuwa Gavana na Mfalme na Bwana, juu ya Kanisa zima, chini ya udhibiti Wake. Kisha litapokelewa juu.
MKATE WA KILA SIKU
Naye akiisha kusema hayo, akawavuvia, akawaambia, Pokeeni Roho Mtakatifu. Yohana 20:22
25-0725
61-0125 – Kwa Nini?
Sote tumezaliwa katika dhambi, tusingeweza kujiokoa. Hatungeweza kujiokoa wenyewe, kuliko tungeweza kuchukua kamba zetu za buti na kujinyanyulia mwezini. Tusingeweza kufanya hivyo, hatujiwezi kabisa. Na kwa hiyo Mungu asingekuhukumu kwa misingi hiyo kwa sababu wewe ni mwenye dhambi, Atakuhukumu kwa sababu unakataa kuchukua njia ya kuepukia. Kwa hiyo basi si Mungu, ni wewe mwenyewe, unajihukumu mwenyewe. Na unapojihukumu mwenyewe, hakuna mtu wa kukuhurumia ila wewe mwenyewe. Hivyo tu. Sisi ni…Hu—huna budi kujihurumia mwenyewe, kwa sababu hujakubali njia iliyowekwa na Mungu ya kuepukia.
Sasa, Mungu anapoweka njia Zake, sijui tu ni kwa nini Yeye hujisikia anapotuwekea njia, kwa ajili ya uponyaji wetu, kwa ajili ya wokovu wetu, kwa ajili ya faraja yetu, kwa ajili ya amani yetu, na mambo haya yote, nasi tunaondoka tu na kuziacha. Hapana shaka tunamfanya ajisikie vibaya sana.
MKATE WA KILA SIKU
Kwa maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani; ambayo hiyo haikutokana na nafsi zenu, ni kipawa cha Mungu; Waefeso 2:8
25-0724
56-0406 – Neno La Mungu Lisiloweza Kukosea
Mungu, kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu, alitazama chini katika mkondo wa wakati naye akaona kila kitu kitakachokuwepo. Na kwa hiyo, Yeye angeweza kuwaita na kuwachagua wale ambao Yeye alijua kwamba angewaweka katika jengo Lake. Hiyo ni kweli. Na kama umeitwa usiku wa leo na Roho Mtakatifu na kupewa nafasi ya kuingia katika Ufalme wa Mungu, unapaswa kuwa na furaha. Amina.
Ikiwa uko katika Ufalme wa Mungu, na wewe ni sehemu ya mwili wa Kristo, Mungu ashukuriwe. Unaishi maisha hayo. Unafanya mambo yaliyo sahihi. Na kumbukeni, hili laweza kuzama kwa ukali kidogo tu linaposhuka, lakini liache limeng’enye kwa muda. Ikiwa uko katika mwili wa Kristo, Yeye hana kukata viungo kokote. Hapana, mwili Wake ni mkamilifu, hauhitaji kukatwa viungo vyovyote. Amina. Whew. Hiyo ni kweli.
MKATE WA KILA SIKU
Kristo atakapofunuliwa, aliye uhai wetu, ndipo na ninyi mtafunuliwa pamoja naye katika utukufu. Wakolosai 3:4
25-0723
58-0209A – Msikieni Yeye
Katika shughuli zako za biashara, neno lako ndilo kifungo chako, ushuhuda wako unapaswa kuwa wa kweli. Mungu ajalie siku, ambapo watu watakuwa kile walicho, kile wanachosema walicho. Kama mimi nisingekuwa wa Kristo alasiri hii, ningekuwa kinyume Naye. Ningekuwa nikienda huku na huku nikiharibu mambo. Bali ninamwamini Yeye, nami ni—niko tayari ku—hata kutoa maisha yangu kwa ajili Yake, kwa maana ninamwamini Yeye, ya kwamba ni kweli. Na kama Neno Lake si sahihi, basi Yeye hayuko sahihi. Na kama Neno Lake haliwezi kuaminiwa, Yeye hawezi kuaminiwa. Lakini ninayo furaha sana kujua ya kwamba mimi…Unaweza kuning’iniza nafsi yako kwenye Neno fulani katika Biblia hiyo, nalo ni kweli, kila Neno Lake ni kweli. Mungu anaishi katika Neno Lake.
MKATE WA KILA SIKU
Bwana ni mwema, ni ngome siku ya taabu; naye huwajua hao wamkimbiliao.
Nahumu 1:7
25-0722
62-0422 – Kurudishwa Kwa Mti Wa Bibi-Arusi
Kwa hiyo, unaona, kanisa la Kiprotestanti lisilolichukua Neno la Mungu ni binti kwa kanisa la Kirumi. Mungu kamwe, katika wakati wowote, hakuliundia kanisa dhehebu. Kanisa Katoliki la Kirumi ndilo lililokuwa dhehebu la kwanza. Na kila mmoja wao, aliyeunda dhehebu, ni binti kwake.
Wanakufa pamoja naye. Biblia ilisema, ya kwamba, “Atawateketeza watoto wake kwa moto.” Ni wangapi wanaojua jambo hilo? [Kusanyiko linasema, “Amina.”—Mh.] Biblia ilisema hivyo. Vema, Biblia ilisema ya kwamba ngano na magugu vitakua pamoja mpaka siku ya mwisho, ndipo atayafunga magugu (hiyo ni kweli?), kwanza, na kuyateketeza kwa moto. [“Amina.”] Na ngano itawekwa ghalani. Hiyo ni kweli? [“Amina.”] Magugu yanajifunga pamoja katika dhehebu, Muungano wa Makanisa, kwa ajili ya kuchomwa na atomu. Kweli kabisa. Bali Kanisa linajiandaa tayari kwenda kwenye ghala, hakika kabisa, katika Unyakuo, kwa maana mwanamke huru hatarithi pamoja na mjakazi.
MKATE WA KILA SIKU
Nao watajua ya kuwa mimi ndimi Bwana; sikusema bure kama nitawatenda mabaya hayo. Ezekieli 6:10
25-0721
53-1205 – Ufufuo
Hakuna kitu kama Imani ya Mitume. Kama kuna Imani yo yote ya Mitume katika Biblia, inapatikana katika Matendo ambapo Yeye alisema, “Tubuni kila mmoja wenu, mkabatizwe katika Jina la Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu. Nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na watoto wa watoto wenu, kwa hao walio mbali, na wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie.”
Hiyo inasikika zaidi kama Imani ya Mitume, si, “Ninaamini katika Kanisa takatifu la Kikatoliki la Kirumi. Ye yote anayeamini katika ushirika wa watakatifu ni mwabudu mizimu. Hiyo ni kweli kabisa. Watakatifu wamekufa; wako katika Uwepo wa Mungu. Hakuna mpatanishi kati ya Mungu na mwanadamu ila Yesu Kristo. Amina. Hiyo ni kweli. Lo, jinsi unavyojipotosha. Jamani, ni aibu…
Unaona, sitaki kuwalaumu ninyi watu; hilo lilianzia kwenye Mimbara. Si ajabu huko ndiko kuangamia kwa nchi, wakati Shetani alipoingia mimbarani. Ni ukweli. Kushindwa kuhubiri Neno la Mungu lisiloghoshiwa, nalo Neno la Mungu litazaa kile hasa lilichosema lingefanya.
MKATE WA KILA SIKU
Wanakiri ya kwamba wanamjua Mungu, bali kwa matendo yao wanamkana. Tito 1:16
25-0720
53-0405S – Nendeni, Mkawaambie Wanafunzi Wangu
Mariamu Magdalene, alikuwa amejua nguvu Zake. Alijua kulikuwa na kitu juu Yake kilichokuwa tofauti na mtu mwingine yeyote. Alikuwa ametolewa pepo saba.
Kila mtu ambaye amewahi kuwa huru na ibilisi, kwa nguvu za Yesu Kristo, anajua mahali wanaposimama. Hakuna mtu awezaye kuja, na katika Uwepo Wake mkuu wa Kiungu, na awe mtu yule yule tena. U—umebadilishwa. Kuna jambo linalokupata. Loo, unaweza kusimama mbali, na saikolojia, na kuwazia hili, na kukubali hili, jambo fulani, na nadharia fulani, au kitu kama hicho. Lakini hatuamini katika theolojia. Tunaamini katika nguvu za kufufuka kwake Yesu Kristo. Nawe unapokuja Mbele Zake, kuna jambo fulani linalotukia maishani mwako, ambalo linakubadilisha. Nawe si yeye yule tena, mtu aliyepata kuwa katika Uwepo wa Kristo.
MKATE WA KILA SIKU
Kwa maana mlikuwa mnapotea kama kondoo; lakini sasa mmemrudia Mchungaji na Mwangalizi wa roho zenu. 1Petro 2:25
25-0719
59-0813 – Kwa nini?
Ikiwa kuna dhambi maishani mwako, iondoe. Ikiwa kuna hukumu, iondoe. Ikiwa kuna shaka, iondoe. Mpaka uweze kuona kikamilifu kwamba ni mapenzi ya Mungu, ni mpango wa Mungu, nawe umejumuishwa katika hilo, kisha useme, “Ugonjwa, katika Jina la Yesu Kristo, ondoka kwangu.” Na kumbuka, unaweza usijisikie vizuri wiki nzima. Lakini mara tu uliposema neno hilo, jambo fulani lilitukia. Mungu hana budi kulitimiza Neno Lake. Ugonjwa huo unatetemeka, naye anaanza kuachia. Ataondoka ikiwa tu utaamini hilo. Usitie shaka.
Kama Petro akitembea juu ya maji, alisema, “Kwa nini uliona shaka? Lo, Enyi wa imani haba.” Kwa sababu tu alikuwa anazama, hilo halikuwa na uhusiano wowote nalo. Kristo alikuwa amemwamuru, na Neno Lake lilitosha. Hivyo ndivyo tunavyopaswa kuliwazia pia.
MKATE WA KILA SIKU
Na mlishike sana ungamo la tumaini letu, lisigeuke;…
Waebrania 10:23
25-0718
56-0805 – Kanisa Na Hali Yake
Unajua, mahali wanapokwenda kuwachinjia kondoo, unajua anayewaongoza kondoo machinjioni, ni mbuzi. Bali mbuzi atamwongoza kondoo moja kwa moja hadi kwenye maporomoko ya machinjioni, na, mara akimfikisha kondoo kwenye maporomoko, basi ataruka nje. Lakini, loo, wao husema, wanapotaka kumchinja mbuzi, basi anaanza matata kwelikweli. Unaona?
Na hivyo ndivyo Ibilisi atatenda. Atajaribu kuongoza wana wa Mungu moja kwa moja hatarini, bali ufikapo wakati wake wa kufa, atafanya matata kwelikweli wakati huo. Hivyo ndivyo Ibilisi hutenda. Na hivyo ndivyo wakati mwingine, maskini msichana aliyejirembesha kipumbavu au maskini mvulana mhuni, akiwa na paketi ya sigara au chupa ya wiske, angemwongoza msichana mdogo vibaya, mwana-kondoo, akiwa na kitoto cha mtu, kwenye mambo mabaya. “Loo, yote ni sawa. Mambo hayo ya kujifanya mwema ya kanisa hayafai kitu.” Lakini acha kifo kimpige maskini mvulana huyo wakati mmoja, utamsikia akilia kama paka na kupiga mayowe nchini kote. Na hivyo ndivyo Ibilisi anavyotenda.
MKATE WA KILA SIKU
Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani. Waefeso 6:11
25-0717
65-0718E – Chakula Cha Kiroho Kwa Wakati Wake
Tunaona ya kwamba mtu anapokuja, ametumwa kutoka kwa Mungu, amechaguliwa na Mungu, akiwa na BWANA ASEMA HIVI ya kweli, ujumbe huo na mjumbe huyo ni mmoja na kitu kimoja. Kwa sababu yeye ametumwa kuwakilisha BWANA ASEMA HIVI, Neno kwa Neno, kwa hiyo yeye pamoja na ujumbe wake ni mmoja.
Mtu wa kimadhehebu chini ya uongozi wa kimadhehebu, yeye na kanisa hilo ni “mmoja.” Mwanatheolojia chini ya theolojia, iliyobuniwa na madhehebu fulani, yeye na ujumbe wake ni mmoja; kanisa la theolojia, mwanatheolojia. Ni kweli.
Basi wakati mtu anapokuja na BWANA ASEMA HIVI, yeye na Ujumbe huo ni mmoja. Na wakati Eliya alipokuja na BWANA ASEMA HIVI, yeye na ujumbe wake wakawa kitu kimoja. Kama tu vile Yesu, wakati alipokuja, Yeye alikuwa ni Neno, Yohana Mtakatifu 1. Kwa hiyo Neno la Mungu na mjumbe wa wakati ule walikuwa ni kitu kile kile, daima.
MKATE WA KILA SIKU
Kama Bwana, Mungu wa Israeli, aishivyo, ambaye ninasimama mbele zake, hakutakuwa na umande wala mvua miaka hii, ila kwa neno langu. 1 Wafalme 17:1
25-0716
55-0114 – Daktari Musa
Jambo lile lile kuhusu Roho Mtakatifu. Unasema, “Nimekuwa nikimtafuta Roho Mtakatifu kwa miaka mingi.” Sikukemei. Aidha umefundishwa isivyo, au kuna jambo fulani kasoro, au huelewi.
Mungu anawajibika kwa Neno Lake. Petro alisema katika Siku ya Pentekoste, “Tubuni mkabatizwe kila mmoja wenu katika Jina la Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.” Hayo ni Maandiko, wazi kabisa kama nijuavyo kuyasoma.
Kama ulitubu na kubatizwa, basi Mungu anawajibika, kama imani yako iko sahihi kwa Mungu kukupa Roho Mtakatifu dakika ile unapolitii Neno Lake. Amini hilo. Mungu atalithibitisha kwako.
Kama moyo wako kweli uko sahihi mbele za Mungu, nawe umefundishwa sahihi, na kuliamini, na uende kule ukiwa na hakikisho, jambo fulani litatukia, maana Mungu yuko tayari kukupa Roho Mtakatifu kuliko vile wewe ulivyo tayari kumkubali.
MKATE WA KILA SIKU
Heri wazifuao nguo zao, wawe na amri kuuendea huo mti wa uzima, na kuingia mjini kwa milango yake. Ufunuo 22:14
25-0715
65-0418M – Ni Kuchomoza Kwa Jua
Kama kungekuwa na sherehe yo yote takatifu, ingepaswa kutokea kwenye siku ya Sabato, ambayo ilikuwa siku ya saba ya juma, ambayo ni Jumamosi. Bali mliona, katika kumbukumbu hii, utatikiswa siku ya kwanza ya juma?
“Mganda, ambao ulikuwa ni malimbuko ya kwanza ya nafaka yenu mliyopanda, wakati inapochipusha na kuiva, unakata mganda huu na kumpelekea kuhani. Na kumwacha auchukue na kuutikisa mbele za Bwana, upate kibali, ya kwamba umekubalika. Umekuja na mganda wako, naye anapaswa kuutikisa mbele za Bwana, kwenye…”
Si katika sabato, siku ya saba; bali kwenye siku ya kwanza, ambayo tunaita Jumapili, J-u-m-a-p-i-l-i.
MKATE WA KILA SIKU
Akawaambia, Sabato ilifanyika kwa ajili ya mwanadamu, si mwanadamu kwa ajili ya sabato. Marko 2:27
25-0714
62-1013 – Ushawishi Wa Mwingine
Luka 24:49 ilisema, “Tazama, nawaletea juu yenu ahadi ya Baba Yangu; lakini ngojeni humu mjini Yerusalemu, hata mvikwe uwezo utokao juu.” Muda gani? Saa moja, masaa mawili, siku kumi, miezi minne, miezi sita, haikuleta tofauti yo yote. Hata! Ni muda gani huo? Hata tu. Ukimwomba Mungu cho chote, kaa papo hapo hata. Amina! Najisikia vizuri. Kaa hata. Mpaka nini? Hata itimie. Idai! Iamini! Ishikilie! Tenda kitendo! Shuhudia juu yake! Shuhudia! Usiwe na hofu. Tenda kitendo.
Walikuwa orofani kwa nini? Wakisifu na kumbariki Mungu. Kwa nini? Walijua ahadi ingetimia. Ndiyo hiyo; anza kitendo. Endelea kumsifu Mungu hata hiyo Ahadi itakapotimizwa. Una ahadi.
MKATE WA KILA SIKU
… bali waingoje ahadi ya Baba. Matendo 1:4
25-0713
61-0415B – Tangu Wakati Huo
Nguvu kuu kuliko zote ulimwenguni si kunena kwa lugha, wala kufasiri lugha, ama kupewa heshima na Mungu kuwa mhudumu, ama kuwa mwinjilisti, ama kuwa nabii, silaha yenye nguvu kuliko zote ambayo nimewahi kupata maishani mwangu, ni upendo. Utaninii…Upendo wa fileo, ambapo hilo neno la Kiyunani linatokana na urafiki, kama vile ulivyo nao kwa mkeo. Kuna tofauti. Itamfanya mama kwa ajili ya mtoto huyo mchanga, apitie kwenye ndimi za moto, maisha yake hayana maana, huo ni fileo. Agapao utafanya nini? Mnaona? Upendo wa kiungu.
Hatuna budi kupendana, kupendana Kiungu sisi kwa sisi, ndipo huoni kosa la ndugu yako. Kama akifanya kosa, wewe kamwe, angalia juu yake, nawe unampenda kwa vyovyote vile. Unaona? Jambo ndilo hilo. Ukiwapenda wale wanaokupenda, basi si mwenye dhambi hufanya jambo lile lile? Lakini wapende wale wasiokupenda, hilo ndilo linaloonyesha Roho wa Mungu yuko ndani yako, maana Yeye alikupenda ulipokuwa adui Yake, Naye akakupenda. Na ikiwa Roho huyo yuko ndani yako, atakufanya umpende adui yako, kama unavyompenda rafiki yako.
MKATE WA KILA SIKU
Tumikianeni kwa upendo. Wagalatia 5:13
25-0712
59-0510E – Ni Nani Huyu?
Ufunuo mmoja juu ya mchanga huo mtakatifu, wakati mmoja juu ya mahali hapo, mtu hawezi kuwa vile vile. Mtu, kabla hajajiita Mkristo, kabla hajaweza kujitambulisha, kwanza anapaswa kuwa na tukio hilo la upande-wa-nyuma-ya-jangwa, ambapo alikutana na Mungu, uso kwa uso.
Kwa kuwa, siku hizi, unaweza kuwa na aina yoyote ya jibu. Unaweza kumwona Bwana akifanya vile hasa Yeye alivyosema ufanye, na wanatheolojia werevu watalielezea vinginevyo. Watasema, “Hiyo ilikuwa ni kwa ajili ya siku nyingine. Ilikuwa kwa ajili ya hii. Ama, ni kwa ajili ya wakati mwingine. Au, ni makosa.” Kama walivyosema juu ya Yesu, “Yeye ni Beelzebuli, ibilisi. Yeye ni mpiga ramli.” Na mambo hayo yote, wana jibu.
Lakini wakati mtu amewahi kamwe kukutana na Kristo, na kumwona kama Paulo alivyomwona, ama kupata tukio Naye, hakuna wanatheolojia wa kutosha ulimwenguni kuweza kuelezea tukio hilo vinginevyo kwa mtu.
Hiyo ndiyo sababu, siku hizi, hawana tukio. Hiyo ndiyo sababu hawawezi kusema…wote wanasema, “Ni nani Huyu? Ni nini Hii? Inatoka wapi?” Hawana jibu. Kwa nini? Kwa sababu, yote wajuayo ni thiolojia ambayo kanisa fulani limeunda. Sio “kuijua thiolojia” ni Uzima. Sio “kuijua Biblia” ni Uzima.
Bali “kumjua Yeye” ni Uzima. “Kumjua Yeye” kama Mwokozi wako binafsi, kama Yule ambaye amekujaza na Uwepo Wake. Ulikuwepo wakati ilipototendeka. Hakuna mtu anayeweza kuliondoa kwako. Hakuna mtu anayeweza kukuelezea Hilo vinginevyo. Wakati tukio hilo linapokutokea, unajua Yeye ni Nani. Kwangu mimi, Yeye ni Yesu Kristo yeye
yule jana, leo, na hata milele.
MKATE WA KILA SIKU
Kwa kuwa nia ya mwili ni mauti; bali nia ya roho ni uzima na amani. Warumi 8:6
25-0711
64-0315 – Ushawishi
Saa huja na kuenda. Kitu cha kwanza unajua, utakuwa unasema, “Vema, ni—nilidhani kulipaswa kuwa na hili likitukia kabla ya Unyakuo.”
Huenda kukawa na Sauti itakayorudi kama ilivyofanya wakati mmoja, “Imetendeka tayari wala hamkujua.”
Utafungwa kabisa kwenye kanisa mahali fulani, ukisema, “Mimi ni salama tu niwezavyo kuwa,” na, muda si muda wajua, Unyakuo utakuwa umekwisha. Utakuwa ni kuondoka upesi, kisiri, hakuna mtu anayejua chochote kuuhusu. Ulimwengu utaendelea tu moja kwa moja.
Kama Nuhu alivyoingia kwenye safina. Mnakumbuka, baada ya Nuhu kuingia kwenye safina, alikaa humo siku saba baada ya Mungu kufunga mlango. Mungu alifunga mlango, ndipo Nuhu akakaa ndani ya safina siku saba kabla ya chochote kutokea.
Nao mlango wa rehema utafungwa machoni pako, na huenda umefungwa tayari.
MKATE WA KILA SIKU
… Uniongoze juu ya mwamba nisioweza kuupanda. Zaburi 61:2
25-0710
49-1225 – Uungu Wa Yesu Kristo
Na halafu, tena, nawatakeni muone jambo lingine, mojawapo ya yanayotimia. Watu hawa ambao ni baridi katika makanisa haya baridi, wanainuka dhidi ya hii Huduma. Nayo Biblia ilisema, “Wangekuwa na mfano wa utauwa, lakini wakikana Nguvu zake; hao nao mjiepushe nao.” Na wanachukua msimamo wao.
Ukomunisti unachukua msimamo wake.
Mungu asifiwe, Roho Mtakatifu anachukua msimamo Wake. Naam. “Adui atakapokuja kama mafuriko, basi nitainua bendera dhidi yake.” Hiyo ni kweli. Nalo Kanisa limechukua msimamo Wake, ninamaanisha Kanisa la Roho Mtakatifu.
Sasa hayo ndiyo tu yanayonivutia, enyi marafiki, nami niko hapa. Huko nje, nitawaombea wagonjwa. Lakini hapa ndani ninavutiwa na jambo moja, na hilo ni Kanisa la Mungu lililozaliwa mara ya pili. Hiyo ni kweli. Hilo ndilo linalonivutia, kwa vyovyote vile. Sivutiwi na sheria ndogo, na mashemasi, na kadhalika, namna hiyo, ama taratibu za makanisa. Ninavutiwa na ubatizo wa Roho Mtakatifu juu ya Kanisa, kwa siku hizi tunazoishi. Hiyo ndiyo sehemu ya kimsingi, na hiyo ndiyo tunayotafuta.
MKATE WA KILA SIKU
Basi, wataliogopa jina la BWANA toka magharibi, na utukufu wake toka maawio ya jua; maana yeye atakuja kama mkondo wa mto ufurikao, uendeshwao kwa pumzi ya BWANA. Isaya 59:19
25-0709
61-0723M – Maji Yaliyopo Daima Yatokayo Mwambani
Mnaona, mara nyingi, watu wanafikiri ya kwamba karama ya unabii, kwamba Mungu husema tu “Nitakuchukua papa hapa, na kukuweka hapa chini. Sasa wewe nenda moja kwa moja hapa.” Naye hakwambii mambo hayo yote. Kama angekwambia, basi wewe ulikuwa na imani gani ya ushindi? Unaona? Unaona, wewe, Yeye hukuacha usimame peke yako kuliko mtu mwingine yeyote. Unaona? Ninyi nyote mnaweza kunijia na kuniomba mambo fulani, na Yeye kamwe hajashindwa bado ila amewapa jibu. Hiyo ni kweli. Naam. Lakini mimi ninaweza kumwomba mambo yangu ya binafsi, na mara nyingi Yeye huniacha tu peke yangu, mnaona, ananiacha tu niendelee na kuingia humo.
Nina mambo sasa ambayo inanibidi kuyatatua mwenyewe, na maamuzi yanayonibidi kufanya. Na hili ni muhimu sana, mpaka siwezi kulifanya mpaka niwe na hakika ya kwamba ni Yeye anayesema na mimi. Na mimi—mimi…Yeye hatanipa ono. Ananiacha tu peke yangu. Kwa hiyo nimekaa tu kama yatima, kitu kama hicho, asubuhi ya leo, si—sijui nielekee wapi. Kwa hiyo, nimelikabidhi kwa Bwana.
MKATE WA KILA SIKU
Nimemngoja Bwana, roho yangu imengoja, Na neno lake nimelitumainia. Zaburi 130:5
25-0708
65-0725M – Watiwa Mafuta Katika Wakati Wa Mwisho
Lakini angalia. Yesu alisema, ya kwamba, katika wakati huu wa mwisho, tena, hizo roho mbili zingefanana sana tena. Hiyo ni kweli? [Kusanyiko linasema, “Amina.”—Mh.] Sasa angalia. Zitafanana sana kuliko hizo zilivyokuwa. Huu ni wakati wa mwisho. Loo, enyi watoto! Mungu na aturehemu! Mpaka, “Hata ingefanana sana hata ingewapoteza hata Walioteuliwa kama yamkini.” Sasa utalitambuaje, tulilitambuaje katika siku hizo? Utalitambuaje leo? Namna ile ile, dumu na Neno. “Yesu Kristo yeye yule jana, leo, na hata milele.”
Sasa ujali Ujumbe huu wote. Na unapoisikiza kanda, hata labda nitakuwa nimeondoka siku moja hapo Bwana atakapomaliza nami hapa duniani, mtarejea kwenye huu. Isikizeni sauti yangu, yale ninayowaambia. Kama akinichukua kabla ya Kuja Kwake, kumbukeni tu, nimenena nanyi katika Jina la Bwana, kwa Neno la Bwana. Naam.
MKATE WA KILA SIKU
Majani yakauka, ua lanyauka; Bali neno la Mungu wetu litasimama milele. Isaya 40:8
25-0707
65-1206 – Matukio Ya Sasa Yanadhihirishwa Na Unabii
Kama watu katika siku za Bwana Yesu wangalimtafuta tu Mungu na kujua yale yaliyokuwa tu karibu kutimia, wasingemhukumu Yesu kifo. Lakini sababu ya hayo kufanyika, ni kwamba Maandiko yalipaswa kutimizwa, kwa sababu ilibidi Wayahudi wapofushwe. Sote tunajua hilo.
Je! mnatambua ya kwamba hilo limeahidiwa tena katika wakati uu huu tunaoishi? Wakati wa Kanisa la Laodikia, wakati huu wa saba wa kanisa tulio ndani yake sasa, ni uchi, wenye mashaka, ni mpofu, wala haujui. Jinsi vile vile alivyowapofusha kule nyuma kwa ajili ya kuupeleka Ujumbe Wake kwa watu walioteuliwa, ameahidi kufanya jambo lilo hilo leo.
Na kama ningesema jambo hilo kwa heshima, na kwa ndugu zangu wote na dada katika Kristo, moja ya siku hizi mtu fulani atasema, “Hivi haijaandikwa ya kwamba mambo haya yanapaswa kutukia kwanza?”
Na itakuwa vile vile jinsi ilivyokuwa wakati huo, “Amini, nawaambia, amekuja tayari, nao wakamtendea yale waliyotaka.”
MKATE WA KILA SIKU
Mwayachunguza maandiko, kwa sababu mnadhani kwamba ninyi mna uzima wa milele ndani yake; na hayo ndiyo yanayonishuhudia. Yohana 5:39
25-0706
56-0405 – Kufufuka Kwa Yesu
Mungu hataki ukunje uso. Mungu anataka uwe na furaha. Moyo wa mwanadamu ulifanywa kuwa na furaha. Hofu itasababisha kansa. Hasira itasababisha kansa. Usikasirike kamwe. Tembea tu katika upendo Wake. Amina. Ukijua kwamba unatembea ndani Yake, na hakuna kitu kinachoweza kukudhuru. Hakuna kitu kinachoweza kukudhuru. Hakuna nguvu, mambo yaliyopo, mambo yajayo, hakuna kinachoweza kututenganisha naye. Tuko ndani Yake. Na kamwe hatuingii kwa mapenzi yetu wenyewe. Yeye, kwa hiari yake, alituchagua sisi na kutuleta kwake. Amina. Kwa hiyo ni kazi Yake kushughulikia kile alichojichukulia Mwenyewe. “Hakuna mtu awezaye kuwatoa katika mikono ya Baba Yangu, maana Yeye ndiye mkuu kuliko wote.” Amina. Ni Baba Anayelishughulikia. Ni nani aliye na nguvu zaidi ya Mungu? Kwa hivyo wewe una nguvu ya aina gani juu yako ya kukushughulikia? Nguvu zote zilizoumba ulimwengu. Amina.
MKATE WA KILA SIKU
Enyi watu wote, pigeni makofi, Mpigieni Mungu kelele kwa Sauti ya shangwe. Zaburi 47:1
25-0705
63-0126 – Uwekezaji
Waaminio hawapaswi kucheza kamari kamwe. “Loo, vema, hii ni sawa. Nitabahatisha kwa hii.” Usifanye hivyo.
Kuna kielelezo kilichowekwa, kitu halisi, na Hicho si cha kundi lolote lile la watu. Ni Neno la Mungu. Usibahatishe kwa Hilo. Sasa, usibahatishe.
Pia jambo lingine nilionalo miongoni mwa watu, wakati mwingine, hususan. Mtu anapata pesa kidogo, halafu atajaribu kuiwekeza katika namna fulani ya lala maskini-amka tajiri, biashara isiyotambulikana. Utapoteza shati kutoka mgongoni mwako, nawe unajua hilo. Unaona? Usijaribu hilo. Naye mfanyabiashara mzuri, mwenye akili timamu hatafanya hivyo. Mtu asiye na uzoefu wa kazi ndiye atakayebahatisha hivyo. Kamwe haina faida.
MKATE WA KILA SIKU
Heri mtu yule aonaye hekima, Na mtu yule apataye ufahamu. Mithali 3:13
25-0704
53-0405S – Nendeni, Mkawaambie Wanafunzi Wangu
Nilikuwa nikisema juu ya, nikizungumza hapa chini, kuhusu chemchemi ya kale niliyozoea kuinywea. Ilikuwa ikibubujika na kuruka, na kuruka na kuruka, huko chini karibu na Milltown. Nilikuwa nikishangaa ni kwa nini chemchemi hiyo iliruka, kwa hiyo siku moja niliketi pale chini nami nilikuwa nikizungumza nayo. Waweza kuwazia mtu akizungumza na chemchemi? Lakini nilikuwa nikizungumza na Asili Yule aliyeiumba hiyo chemchemi. Nami nikashangaa, “Ni nini kinachokufanya ububujike hivi, mwenye kurukaruka hivi? Ni kwa sababu ati—ati watoto huja hapa na kunywa kwako, ama mimi hunywa kwako, ama chochote kile?”
Kama hiyo chemchemi ingeweza kujibu, ingesema, “La, Billy, si kwa sababu unakunywa humo. Si kwa sababu mtu yeyote anakunywa kwangu. Ni kitu fulani chini yangu hapa, kinachonisukuma na kunifanya nibubujike na kuruka-ruka, na kupiga makelele hivi.”
Hivyo ndivyo, kila mwanamume ama mwanamke aliyezaliwa kwa Roho wa Mungu. Si wewe. Sio mhemko wa kibinadamu. Ni kwa sababu ufufuo, ama Nguvu za Mungu, zimo katika maisha hayo ya mwanadamu, nazo zinasukuma juu kuingia katika Uzima wa Milele, kuingia katika Uzima wa Milele. Kitu fulani humu ndani! Usingeweza kunyamaza hata ufanye nini. Kuna kitu fulani ndani yako.
MKATE WA KILA SIKU
Yule mwanamke akamwambia, Bwana, huna kitu cha kutekea, na kisima ni kirefu; basi umeyapata wapi hayo maji yaliyo hai? Yohana 4:11
25-0703
58-0609 – Ujumbe kwa Kanisa la Laodikia
Nami kwa kweli ninawazia jambo hili, ya kwamba mara nyingi kanisa katika ulegevu wake huanza kufanya mambo, na kuwaza mambo, na—na kuchukua mambo jinsi tu yalivyo, wakati inatupasa kupima kile tunachofanya na kusema. Tunapaswa kulitafakari kabla ya kulizungumza.
Mama yangu mzee wa kusini alizoea kuniambia, “Fikiria mara mbili na uzungumze mara moja.” Ni mambo madogo, wakati mwingine, ambayo tunaacha bila kufanywa, ambayo yana maana sana kwetu. Tunakuwa na haraka sana ya kushindana na mambo katika wakati huu wa msongo tunaoishi. Ingetupasa sisi, kama kanisa la Mungu usiku wa leo, kusimama na kungoja kidogo, tuone tulipo.
MKATE WA KILA SIKU
Basi, jiangalieni, mioyo yenu isije ikalemewa na ulafi, na ulevi, na masumbufu ya maisha haya; siku ile ikawajia ghafula, kama mtego unasavyo Luka 21:34
25-0702
61-1224 – Mabwana, Sisi Tunataka Kumwona Yesu
Loo, Isaya alisema Yeye alikuwa ni wa Ajabu. Hebu tuwazie baadhi ya mambo aliyosema, yaliyomfanya Yeye wa Ajabu. Ni kitu gani kilichomfanya Yeye wa Ajabu? Wakati aliposema jambo hili, “Mimi na Baba Yangu ni Mmoja,” wa Ajabu.
Niambie ni Farisayo gani angaliweza kusema hilo. Niambie ni kuhani gani mkuu angaliweza kusema hilo, huku Mungu akimuunga mkono. Mnaona?
Kasema, “Nisipozifanya zile kazi sasa, msiamini lolote ninalosema. Bali nikilihubiri hili, basi inaonyesha ya kwamba Mungu alinituma kulifanya.”
Kasema sasa, ndipo Yeye akasema, “Mimi na Baba Yangu ni Mmoja.” Sio, “Mimi na Baba Yangu ni watatu.” Yesu alisema. Sasa, kanuni ya imani inasema, “Mimi na Baba Yangu ni watatu.” Bali Biblia ilisema, naye Yesu akasema, “Mimi na Baba Yangu ni Mmoja.” Hiyo ni Ajabu.
MKATE WA KILA SIKU
…Naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa Amani. Isaya 9:6
25-0701
62-0117 – Kudhania
Mtu fulani alisema, hivi majuzi, kasema, “Ndugu Branham, watu wanakuthamini wewe kama nabii. Kwa nini sana sana huwafundishi watu hao jinsi ya kupata karama za kiroho? Uachane na vile hao wanawake wanavyovaa nguo na jinsi hao wanaume wanavyotenda. Achana nao. Si kazi yako kuyasema hayo. Wafundishe mambo makuu, ya kiroho, yenye kilindi.”
Nikasema, “Ninawezaje kuwafundisha aljebra, wakati hawajui ABC?” Unawezaje kuwapa elimu ya chuoni; hata hawajatoka kwenye shule ya chekechea? Hata hamna adabu ya kawaida kujisafisha na kutenda kama Wakristo, na kuvaa kama Wakristo, na kuishi kama Wakristo, na halafu kuzungumza juu ya karama za kiroho. Tokeni kwenye shule ya chekechea. Wanadhani hayo ni sawa, bali ni makosa. Hampaswi kufanya jambo hilo. Mama zenu hawakufanya jambo hilo, hilo lilikuwa katika miaka ya Kipentekoste. Bali wanalifanya.
Na ninyi wanaume, jinsi mnavyoishi, mnawaacha wake zenu kufanya hivyo? Mngali mko katika shule ya chekechea. Mnaona? Hiyo ni kweli. Mnadhani ni sawa, bali si sawa.
MKATE WA KILA SIKU
…wawe na mwenendo wa utakatifu. Tito 2:3
25-0630
65-0429E – Kuchagua Bibi-Arusi
Sasa, huna budi kuomba juu ya kanisa unamoshiriki. Kumbuka, makanisa huwa na roho.
Sasa, sitaki kukosoa. Bali natambua kuwa mimi ni mzee, na sina budi kuondoka hapa, mojawapo ya siku hizi. Nami sina budi kuwajibika kwenye Siku ya Hukumu kwa yale ninayosema usiku wa leo ama wakati wowote mwingine. Nami, kwa hivyo, sina budi kuwa mkweli kabisa na kushawishika kabisa.
Bali, hebu nenda kanisani, na kama utachunguza tabia ya hilo kanisa, hebu mwangalie tu mchungaji kwa muda mfupi, na mara nyingi utaona ya kwamba kanisa hutenda kama mchungaji wake. Wakati mwingine, mimi hushangaa iwapo hatupati roho ya sisi kwa sisi badala ya Roho Mtakatifu.
MKATE WA KILA SIKU
Kama vile Baba anijuavyo, nami nimjuavyo Baba. Nami nautoa uhai wangu kwa ajili ya kondoo. Yohana 10:15
25-0629
65-1205 – Mambo Yatakayokuwapo
Yesu Kristo ni kwa imani; si yale unayoweza kuthibitisha kisayansi, bali ni yale unayoamini. Siwezi kukuthibitishia kisayansi, usiku huu, katika jengo hili, ya kwamba kuna Mungu, lakini hata hivyo ninajua Yeye yuko hapa. Lakini, kwa imani yangu, ninathibitisha hilo.
Ibrahimu asingeweza kukuthibitishia kisayansi ya kwamba atampata mtoto kwa mwanamke huyo, naye akiwa na umri wa karibu miaka mia moja. Bali imani yake ilithibitisha jambo hilo. Unaona? Hakuhitaji thibitisho lolote la kisayansi.
Mbona, ninii…Mbona, daktari angalisema, “Huyo mzee ana kichaa, amekuja hapa akisema ya kwamba atampata m—mtoto kwa mwanamke yule; yeye akiwa na umri wa miaka mia moja; na mkewe tisini.” Lakini, unaona, Mungu alisema hivyo, kwa hivyo halihitaji sayansi. Inahitaji imani, kuliamini Neno la Mungu, si sayansi.
MKATE WA KILA SIKU
…tukiisha kuhesabiwa haki itokayo katika imani, na mwe na amani kwa Mungu, kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo: Warumi 5:1
25-0628
60-0310 – Eliya Na Sadaka Ya Unga
Loo, hilo hapo! Na walipoingia katika tanuru ya moto, chini ya majaribio, chini ya majaribu, walibaki waaminifu hadi mwisho. Lakini Mungu alikuwepo kwa muda mfupi tu, na akawaokoa. Walijua kuwa walikuwa wameomba vya kutosha, dhambi zao ziliungamwa. Walijua walikuwa wametimiza kila hitaji, na bado Yeye alionekana kuwa kimya. Yeye yuko kimya tu kukujaribu, kuona kweli wewe ni nini, ni nini kilicho ndani yako, kuona ikiwa kweli unamaanisha kutoka moyoni mwako kile unachosema kwa midomo yako. Acha hiyo iingie kwa kilindi. Tunaweza kusema kwa midomo yetu, lakini je, moyo wetu unasema hivyo?
MKATE WA KILA SIKU
Nimemtumaini Mungu, sitaogopa; Mwanadamu atanitenda nini Zaburi 56:11
25-0627
62-0204 – Ushirika
Sasa, tunataka kufikiria kumhusu Yesu na kumhusisha Yeye, kile alichokuwa Yeye. Mwili Wake ni nini? Mwili wa Kristo ni nini? Ni kundi la waamini ambao wanashirikiana na Yeye katika Roho Mtakatifu. Si sanamu, si kipande cha mkate, bali Roho ambaye yuko ndani ya moyo wa mwamini, nao wanashirikiana pamoja, kwamba wakati mwanadamu na Mungu wanaweza kuzungumza mmoja kwa mwingine, wana na binti za Mungu. Binadamu asiyedumu, kwa kumwaga Damu ilileta ondoleo la dhambi, na mtu huyu na mwanamke huyu, mvulana au msichana, ambaye ana ushirika pamoja na Kristo, anashirikiana Naye, mwili.
MKATE WA KILA SIKU
Vivyo hivyo na sisi tulio wengi tu mwili mmoja katika Kristo, na viungo, kila mmoja kwa mwenzake. Warumi 12:5
25-0626
47-0412 – Imani Ni Hakika
Siku hii tunayoishi, ni siku yenye mahangaiko na masumbuko kila mahali. Watu wanakimbia huku na huku wakizungumza chochote wanachoweza kusema. Wengi mtu yeyote awezaye kupata ufuasi. Haijalishi wanafundisha nini ama wanafikiri nini, mtu fulani atawasikiliza. Na ndio siku Ile ambayo manabii waliinena.
Watu, wanapokuwa na njaa, watakula kutoka mahali popote. Ikiwa watoto na watu wanakufa kwa njaa, watakula kutoka kwenye pipa la takataka, ambao hula mara moja kutoka kwenye meza nzuri. Lakini ikiwa wana njaa, watakula mahali fulani. Kwa hiyo nadhani wahudumu wa kweli wa Injili wanapaswa kuamka na kuondoka, wanapaswa kuwapa watu mambo yanayofaa: nyama katika majira yake.
MKATE WA KILA SIKU
Lichungeni kundi la Mungu lililo kwenu 1 Petro 5:2
25-0625
56-0218E – Mwenye Dhambi Kuliko Wote Katika mji
Natamani ningesimama pale aliposimama. Nilitamani ningesimama mahali pale alipokuwa amesimama. Unajua ningefanya nini? Loo, nisingevutiwa na mambo lukuki ya kanisa; Ningepomoka kifudifudi na kusema, “Mpendwa Bwana Yesu, Bwana wa Uzima, nipe neema Yako ya msamaha,” kama ningekuwa na nafasi ya kusimama mbele Zake.
Naamini hivyo ndivyo kila mtu hapa usiku wa leo anavyojisikia. Tungefanya jambo lile lile. Mimi…Lakini leo ni kama tu ilivyokuwa wakati huo. Tumechukuliwa sana na mambo mengi sana kanisani ya sisi kufanya, mambo mengi sana kanisa linatutaka tufanye, na sehemu nyingi sana za kwenda, mpaka kweli, tunashindwa mara nyingi kuipokea ile fursa. Na labda, usiku fulani ilitubidi kwenda kufanya mazoezi kwa ajili ya ibada ya nyimbo. Ilitubidi kufanya jambo lingine.
Jambo fulani, huenda, asili ya kidini, lakini wakati Roho Mtakatifu anazungumza moyoni mwako, jambo bora unaloweza kufanya ni kujibu kila wakati, haijalishi ni kitu gani, ni wakati gani wa usiku, ama ni aina gani ya kazi unayofanya; kwa sababu huenda asiongee tena kwa muda mrefu, na labda hatawahi kamwe.
MKATE WA KILA SIKU
Acheni, mjue ya kuwa Mimi ni Mungu… Zaburi 46:10
25-0624
55-1006A – Maisha Yaliyofichwa
Je! ninamtazama Henry Groat. Mungu akubariki, Ndugu Henry, sijakuona kwa muda mrefu na ndugu. Nilitokea tu kutazama nyuma na kumuona baba nami nikamtambua.
Nilipopata shida kubwa ama nilipotoka kazini kwa takriban miezi minane, wao walikuwa ndugu na baba halisi kwangu mimi. Walikaa moja kwa moja nami wakati wote. Sitasahau kamwe siku ambayo Ndugu Groat pale, tulienda kwenye shamba la mahindi kuomba. Nilikuwa na wasiwasi sana; Nilikaa katika ono muda mrefu sana nisingeweza kujua kama nilikuwa ndani au nje. Sitasahau kamwe Ndugu Groat alipopiga magoti kuomba pamoja nami. Alinikumbatia, kirahisi kama kusema, “Sasa, Baba Mungu, utakuja kumsaidia Ndugu Branham? Baba Mungu, utakuja kumsaidia Ndugu Branham? Hilo limedumu nami daima, Ndugu Groat.
Loo, itakuwaje, Ndugu Groat, siku moja natumai kukukumbatia kwa mkono wangu na kuketi karibu na miti ya kijani kibichi ambapo chemchemi za maji ya Uzima zinatiririka kutoka chini ya kile kiti cha enzi. Tutakuwa katika Uwepo wa Baba yetu Mungu basi milele na milele kuishi katika Uwepo Wake.
MKATE WA KILA SIKU
Kwa maana huyo Mwana-Kondoo, aliye katikati ya kiti cha enzi, atawachunga, naye atawaongoza kwenye chemchemi za maji yenye uhai, na Mungu atayafuta machozi yote katika macho yao. Ufunuo 7:17
25-0623
56-0527 – Huko Kadesh Barnea
Naye Roho Mtakatifu ni Roho wa Bwana Yesu Kristo aliyelishukia Kanisa, kuendeleza kazi za Bwana Yesu, katika kuondoka Kwake. Ni kutoa Nuru ya Injili, kwa nuru ndogo zaidi, kuliko ilivyokuwa wakati Kristo alipokuwa hapa.
Kama mwezi na jua. Mwezi hujitokeza, kutoa mwanga wakati jua halipo, mpaka linapoweza kuchomoza tena, ndipo mwezi unatoweka. Na jua ni nuru angavu zaidi, hata huzima mwanga wa mwezi. Lakini mwanga wa mwezi ni nini? Ni uakisi wa jua kwenye mwezi.
Na hiyo ni kama Kristo. Alipokuwa hapa, Yeye alikuwa Nuru ya ulimwengu. Akaenda zake, na kuliangazia Kanisa Lake tena, lipate kuiakisi Nuru Yake ulimwenguni leo hii, tupate Nuru ya kutembelea mpaka atakaporudi. Ndipo basi yote-kwa-yote atapewa Yeye. Naye ataketi kwenye kiti cha enzi cha Mfalme Daudi, na kutawala milele na milele.
MKATE WA KILA SIKU
Nami nitamwomba Baba, naye atawapa Msaidizi mwingine, ili akae nanyi hata milele; Yohana 14:16
25-0622
55-1111 – Pale Ninapodhani Wapentekoste Waliposhindwa
Musa aliwaongoza watu milioni mbili jangwani. Naye akawaongoza kwa muda wa miaka arobaini, na alipofika kule ng’ambo ya pili, hapakuwa na mtu aliye dhaifu kati yao.
Je! ninyi madaktari hapa usiku wa leo, ama baadhi yenu, mngependa kujua daktari Musa alikuwa na maagizo gani ya daktari? Yeye aliwapa nini watu hao? Ni watoto wangapi waliyozaliwa kila usiku? Ni wazee wangapi na kadhalika? Ni walemavu wangapi na wachechemeao ? Na ni maradhi mangapi, na kila kitu kingine, alichowapatia usiku kucha? Naye Daktari Musa aliyashughulikia kila moja ya hayo.
Je! ungependa kuangalia mkoba wake wa dawa na kujua ni aina gani ya dawa atoayo? Je, ungependa kujua ni kitu gani? Hebu tuone ilikuwa nini. Hii hapa: “Mimi ndimi Bwana nikuponyaye magonjwa yako yote.” Amina. Hiyo ndiyo tiba pekee aliyokuwa nayo, na ilifanya kazi kwa watu milioni mbili.
MKATE WA KILA SIKU
… kama yule nabii angalikuambia kutenda jambo kubwa, usingalilitenda? 2Wafalme 5:13
25-0621
60-0304 – Kuonea Kiu Uzima
Mara nyingi nimesema kama ningeweza kuwa kijana wa umri wa miaka ishirini na mitano, kama Mungu angetokea jukwaani usiku wa leo, na kusema, “Nitakugeuza uwe na umri wa miaka ishirini na mitano, utabaki hivyo kwa miaka milioni moja, nami nitakufanya uwe mfalme juu ya ulimwengu wote, kila kitu kitakuwa chini ya amri yako; ama nitakupa miaka mia ya taabu na ole, na shida, na huzuni, lakini mwisho wa hiyo miaka mia moja, nitakupa Uzima wa Milele, lakini mwisho wa hiyo miaka milioni moja, upotee.”
Loo, ningesema, “Bwana Mungu, sihitaji kungoja zaidi kufanya chaguo langu: Acha niwe na miaka mia ya taabu na ole, aina yo yote ya kifo utakachonichagulia nife, Bwana, nipe tu Uzima wa Milele. Kwa maana ingawa ninamiliki ulimwengu wote na nilikuwa mfalme kwa miaka milioni moja, mwisho wa hiyo miaka milioni moja, ninakuwa kiumbe wa kuzimu kwa Milele yote. Bali haidhuru hali yangu ni mbaya jinsi gani hapa, mwishoni mwa maisha yangu, kama nina Uzima wa Milele, nitaendelea kuishi katika Uwepo uliobarikiwa wa Mungu milele na milele.”
MKATE WA KILA SIKU
Yeye aipendaye nafsi yake ataiangamiza; naye aichukiaye nafsi yake katika ulimwengu huu ataisalimisha hata uzima wa milele. Yohana 12:25
25-0620
62-0318 – Neno Lililonenwa Ndilo Mbegu Ya Asili
Mungu alikuwa amewaambia Adamu na Hawa, “Zaeni mkaijaze nchi.” Lilikuwa ni jambo linalokuja, ahadi. Yeye hakuwa mke wake, bado, kwa sababu kamwe hakuwa ameishi naye.
Bibi-arusi wa Kristo si mke Wake bado. Ile Karamu ya Arusi itafanyika. Mnalipata? Angalieni, loo, hili limekolea.
Alikuwa na haraka, ndipo akafanya nini? Akachanganya mbegu yake. Aliichanganya na mbegu ya nyoka. Basi alipofanya hivyo, alileta ni—ninii…Alileta nini? Alileta mtoto wa mauti. Mtoto, ambaye, alimpotosha kila mtoto baada yake.
Ndipo wakati kanisa la Yesu Kristo lilipopotoshwa katika wakati wa Rumi, baada ya kuzaliwa kwake na bikira, kisha likatolewa kwa Kristo pale Pentekoste, lilininii…Lilifanya nini? Lilichanganyana na fundisho la sharti la Kirumi. Nalo kanisa la Kiprotestanti limefanya jambo lile lile. Haliwezi kungojea.
MKATE WA KILA SIKU
Hekima yako, na maarifa yako yamekupotosha; Isaya 47:10
25-0619
58-0510 – Uwe na Imani na Mungu
Dhambi iko kwenye maandamano.
Huwezi kuwaambia, kwa sababu shetani amelitwaa taifa. Ilitujia miaka michache iliyopita, yeye aliishi Paris, Ibilisi na malaika zake, nao walikuwa na vita vya kwanza vya dunia, nayo Ujerumani ingelilizamisha taifa hilo chini ya nchi, lakini sisi tulienda kuwasaidia, na mara vilipokwisha, hilo lilirudi tena katika mvinyo, wanawake, na wakati wakujifurahisha. Ndipo Shetani akatuma mitindo yake hapa, akawavua nguo wanawake wetu, akaleta fedheha kwa taifa letu, kupitia mitindo na fasheni, ndipo akalichukua tu jeshi lake na kutua Hollywood.
Wengi wenu ninyi watu hamngewaruhusu watoto wenu kwenda kwenye maonyesho ya sinema na kuyaona mambo kama hayo, ibilisi ni mtu mwerevu, yeye huyaingiza moja kwa moja kwenye televisheni, ili mhakikishe mnalipata.
MKATE WA KILA SIKU
Wala msiifuatishe namna ya dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu. Warumi 12:2
25-0618
55-0109E – Mwanzo Na Mwisho Wa Kipindi Cha Mataifa
Ni nini? Nimetembea na kuitazama nyota hiyo kuu ya asubuhi, inapoanza kusogea huko nga’mbo. Je, nyota ya asubuhi inasema nini? Nyota ya asubuhi inaakisi tu nuru kuu ya jua linalokuja. Hiyo ni kweli? Nyota ya asubuhi, sababu ya kuwa yenye kung’aa sana hivi (mnajua ni kwa nini?), jua liko karibu nayo zaidi sana. Linasukuma. Nayo nyota ya asubuhi inakukaribisha kuja kwa jua.
Vema, enyi nyota za asubuhi, wakati wa kuanza kumkaribisha Yeye akija umewadia! Angazeni, enyi Nyota za asubuhi! Amkeni mapema! Inasema, “Mwana atakuwa hapa hivi karibuni!”
Tunapotazama na kuiona ile nyota ya asubuhi, ikimetameta angani, ina maana kwamba jua litawaka hivi karibuni sana.
Basi tunapoziona Nyota za asubuhi za Mungu, zikisimama na kuangaza kwa utukufu wa kufufuka kwa Yesu Kristo, inaonyesha kwamba yule aliye Mkuu anakaza mwendo. Taa zinakusanyika, lakini Nyota ya asubuhi inapiga kelele, “Shikilia! Sio muda mrefu hadi mapambazuko.” Shikilia! Si muda mrefu hadi mapambazuko. Endelea tu kushikilia.
MKATE WA KILA SIKU
Msistaajabie maneno hayo; kwa maana saa yaja, ambayo watu wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake. Yohana 5:28
25-0617
54-0301 – Malaika wa Agano
Sasa, ninapoingia kwenye duka la vitu vya aina mbalimbali, napenda kutazama pande zote kidogo, sivyo nyote, hasa ikiwa lilikuwa langu? Nami nikiona kitu fulani kilicho juu, nitajitafutia ngazi, na kwenda kupanda juu, kukitazama, kukichunguza, kuona jinsi kinavyoonekana.
Ndivyo ilivyo katika Kristo Yesu. Kwa Roho mmoja, sote tumebatizwa katika duka kubwa la Mungu la vitu vya aina mbalimbali, Yesu Kristo, ambapo tuna amani, furaha, shangwe, uvumilivu, fadhili,utu wema, upole, Roho Mtakatifu, nguvu za Mungu, kunena kwa lugha, fasiri za lugha, uponyaji wa Kiungu, utukufu, vifijo, hekima. Haleluya. Mambo haya yote ni yetu, kila Mwaminio: ni mali yako.
Mimi ni Bwana, nikusamehaye maovu yako yote, na kukuponya magonjwa yako yote. Yote ni yangu. Kama uponyaji wa Kiungu unaonekana uko juu kidogo, umo katika duka langu la vitu vya aina mbalimbali, maana uko papa hapa. Na hili ndilo duka letu la vitu vya aina mbalimbali. Amina.
Basi ninapokuwa mle ndani, nitapanda juu na kuchukua hili. Ni yangu. Huenda ikanibidi nipande juu kidogo, naweza kulazimika kujivuta kidogo, bali nitakipata. Ni mali yangu. Nimeazimia kukipata.
MKATE WA KILA SIKU
Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu. Wafilipi 4:13
25-0616
64-0719M – Sikukuu Ya Baragumu
Ishara ya mwisho ambayo Ibrahimu…Nasi ni Uzao wa kifalme wa Ibrahimu; Bibi-arusi. Ishara ya mwisho ambayo Ibrahimu aliwahi kuona kabla ya ile ishara iliyoahidiwa kuja…mwana aliyeahidiwa akaja, alikuwa nani? Mungu, katika umbo la mwanadamu, ambaye aliweza kuyatambua mawazo ya watu; mtu mmoja, si dazani; mtu mmoja, haidhuru kuna miigo mingapi. Wao walikuwa na Mmoja, Naye akatambua mawazo yaliyokuwa mle ndani. Nini? Na, jambo la pili lililotukia, Ibrahimu na Sara wakageuka wakawa kijana mwanamume na mwanamke.
MKATE WA KILA SIKU
Bwana akanena, Je! Nimfiche Ibrahimu jambo nilifanyalo, Mwanzo 18:17
25-0615
50-0115 – Je!
Sasa, nataka uangalie tofauti kati ya Mariamu na Zakaria. Zakaria, yule mhudumu, mhudumu wa Injili, ama mhubiri, kama ilivyokuwa katika siku hiyo, kuhani katika hekalu, alikuwa amejua kila namna ya mambo ambayo yalikuwa yametukia hapo awali ya nguvu za miujiza ya Mungu, lakini alimtilia shaka Malaika katika suala lake, ambapo Mariamu alisema, “Tazama, mimi ni mjakazi wa Bwana.” Yeye hakuswali itakuaje ama kadhalika.
Na angalia ni kiasi gani yeye Mariamu alipaswa kuamini zaidi ya kile Zakaria alipaswa kuamini. Hana alikuwa amepata mtoto hapo awali, wakati alipokuwa amepita umri. Sara alipata mtoto kabla, baada ya yeye kupita umri. Na hilo lilikuwa tayari limekwishatokea mara nyingi. Lakini Mariamu alipaswa kuamini jambo ambalo halikuwahi kutokea. Hakuna mwanamke aliyewahi kumleta mtoto namna hiyo duniani kwa kutokumjua mwanamume.
Lakini yeye alikuwa na mengi ya kuamini zaidi ya yale Zakaria alipaswa. Hivyo basi, yeye hakumhoji Mungu; alimchukua tu Mungu kwenye Neno Lake. Amina. Nalipenda hilo. Mchukue Mungu kwenye Neno Lake. Liamini hata hivyo. Haijalishi jinsi linavyoonekana kuwa haiwezekani, mwamini Mungu, Naye atalitimiza.
MKATE WA KILA SIKU
Akasema, Naamini, Bwana. Akamsujudia. Yohana 9:38
25-0614
58-0309M – Yale Maandiko Ya Mkono Kwenye Ukuta
Taifa hili likiepuka hukumu, Mungu atawajibika kufufua Sodoma na Gomora, na kuomba msamaha kwa kuwazamisha na kuwateketeza, kwa maana sisi ni waovu tu kama vile Sodoma na Gomora ilivyowahi kuwa. Na ikiwa aliizamisha Sodoma na Gomora, na kuwateketeza, kwa sababu ya dhambi yao, na asitutende sisi vivyo hivyo, basi atakuwa amewadhulumu na anastahili kuwaomba msamaha.
Haimbidi Mungu kumwomba msamaha mtu yeyote, au chochote. Dhambi itahukumiwa. Na itaadhibiwa, hakika tu kama vile kulivyo na Mungu Yule awezaye kufanya hukumu. Na hukumu ya Mungu ni takatifu. Mungu ni mtakatifu.
MKATE WA KILA SIKU
Ni makuu, na ya ajabu, matendo yako, Ee Bwana Mungu Mwenyezi; Ni za haki, na za kweli, njia zako, Ee Mfalme wa mataifa. Ufunuo 15:3
25-0613
53-0831 – Mungu Alinena na Musa
Kidogo kidogo, mnapoua kundi hili la Waamori, nitawaruhusu kuingia ndani yake na kuiteka. Mkiua kundi hili la Wahivi, nitawaruhusu muingie, kuteka.”
Mtu fulani alisema, “Vema, nina…niliombewa jana usiku. Nilikuwa na mkono uliolemaa na kitu pekee ninachoweza kufanya ni kutikisa kidole changu.” Vema, huo ndio umbali tu ulioeneza. Ndugu, vema, ikiwa utaenea mbali zaidi utausogeza mkono wako. Unapoieneza imani yako, Mungu atakuruhusu uliteke eneo hilo. Ni lako. Mungu alikuahidi afya yako tena. Haleluya. Whew. Jamani, najisikia vizuri. Ee Mungu, nieneze. Amina.
MKATE WA KILA SIKU
Kila mahali zitakapopakanyaga nyayo za miguu yenu, nimewapa ninyi, kama nilivyomwapia Musa. Yoshua 1:3
25-0612
56-1230 – Yusufu Akikutana Na Nduguze
Sasa, hapo mwanzo, wakati Mungu aliponena, naye Shetani alikuwa amesimama pale naye akasikia.
Nao watu wanajaribu kutafuta kiungo hiki kisichopatikana. Nitawaambia, kwa ufunuo, mkitaka kuupokea. Mtu huyo asiyepatikana, kati ya mnyama na mwanadamu, ni nyoka, kabla hajanyang’anywa miguu yake. Biblia ilisema, “Alikuwa mwerevu kuliko hayawani wote,” sio mtambaaji, “wote wa mwituni.” Yeye ndiye aliyemdanganya mwanamke, kwa urembo wake, naye akapata mimba.
Na sasa, kwa kufanya hivyo, na kuona dhambi ilikuwa inakuja, Mungu aliweka laana kubwa sana juu yake mpaka sayansi haitapata uhusiano wowote kati ya nyoka huyu, kama anavyojulikana siku hizi, na binadamu. Lakini huyo hapo mtu wako aliyeanguka, aliyeshushwa hadhi, katikati, aliyeunganisha maisha ya hao wanyama pamoja. Haya basi.
“Mungu amelificha wenye hekima na busara, lakini atawafunulia watoto wachanga watakaojifunza.” Mnaona?
Huyo hapo mtu wako aliyeanguka…
MKATE WA KILA SIKU
Basi nyoka alikuwa mwerevu kuliko wanyama wote wa mwitu aliowafanya Bwana Mungu. Akamwambia mwanamke, Ati! Hivi ndivyo alivyosema Mungu, Msile matunda ya miti yote ya bustani?
Mwanzo 3:1
25-0611
53-0512 – Uambie Mwamba
Sasa, Injili si Neno tu. Hili ni Neno la Mungu, na mambo yote lazima yaelekezwe kwenye Neno hili. Ikiwa sivyo lilivyo, si kweli. Hili ni…Lakini Yesu alisema, “Enendeni ulimwenguni mwote mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe.” Sasa, Yeye hakusema “Lifundisheni Neno,” Yeye alisema, “Ihubirini Injili.”
Kwa hiyo Injili inajumuisha zaidi ya kufundisha Neno, kwa maana Paulo, akithibitisha hilo, alisema, “Injili ilitujia, si kwa Neno tu, bali kwa nguvu.” Madhihirisho ya Roho Mtakatifu yangekuja na kuidhihirisha Injili, kulileta Neno kwenye uhalisia ulio hai.
Ukilipokea tu Neno kwa kulijua Neno, hilo halikufanyii jema lolote. “Andiko huua; Roho huuisha.” Basi huna budi kuzaliwa mara ya pili, na ndipo Roho Mtakatifu hulihuisha Neno kwako.
MKATE WA KILA SIKU
Si wa andiko, bali wa roho; kwa maana andiko huua, bali roho huhuisha.
2 Wakorintho 3:6
25-0610
56-0115 – Njia Panda Ya Wakati
Usingekunywa supu iliyo na nzi ndani yake. La, bwana. U—usingeinywa. Usingekuwa…Ungeogopa kula chakula ambacho hakikuonekana sawa kabisa, na kilikuwa kimechafuliwa. Kwa sababu, unajua, kinaweza kukupa sumu ya chakula ama chochote kile, na kingekuua baada ya muda mfupi. Na wewe unautunza mwili huu. Lakini, hiyo nafsi, unaiacha ijifurahishe na mambo ya ulimwengu, ambayo unajua yamechafuka na yanaweza tu kufanya jambo moja, kukupeleka kwenye maangamizi. Haijalishi jinsi unavyoutendea vizuri mwili huu, na jinsi chakula kilivyo kizuri, ama jinsi unavyoishi, hauna budi kuingia katika mavumbi ya nchi. Lakini nafsi hiyo itaishi milele, mahali fulani. Afadhali ninywe supu iliyochafuliwa kuliko kuichafua nafsi yangu na mambo ya ulimwengu, wakati wowote.
MKATE WA KILA SIKU
Maana Mungu hakutuitia uchafu, bali tuwe katika utakaso.
1 Wathesalonike 4:7
25-0609
58-0928E – Uzao Wa Nyoka
Ni nani aliye na nguvu zaidi ya wote, nimesema, Mwokozi ama mwenye dhambi? Ni nani aliye na nguvu nyingi kupita wote? Basi, ilimbidi aliye na nguvu zaidi amruhusu asiye na nguvu sana, Naye hufanya jambo hilo tu kwa ajili ya utukufu Wake. Alipomfanya Lusifa, Yeye alijua angekuwa ibilisi. Ilimbidi kumwacha aweko kuonyesha ya kwamba Yeye alikuwa Mwokozi, yule Kristo. Ilimbidi kuacha jambo hilo litukie namna hiyo.
Naam, hivi Biblia haisemi, ya kwamba, “Mambo yote hutendeka kwa manufaa ya hao wampendao Mungu”? [Kusanyiko, “Amina.”—Mh.] Basi mnaogopa nini?
Na tuamke tukatende kazi,
Tujitie moyo katika mzozo wo wote.
Msiwe kama ng’ombe bubu wanaosukumwa, hawana budi waombwe na kubembelezwa!
Na mwe shujaa!
Ninapenda hilo. Simameni!
MKATE WA KILA SIKU
Nasi twajua ya kuwa katika mambo yote Mungu hufanya kazi pamoja na wale wampendao katika kuwapatia mema, yaani, wale walioitwa kwa kusudi lake. Warumi 8:28
25-0608
63-0117 – Kumwamsha Yesu
Sasa, ndani ya Yesu mlikuwamo Mungu. “Mungu alikuwa ndani ya Kristo, akiupatanisha ulimwengu kwa nafsi Yake.” Nao hawa watu waliamini ushuhuda Wake. Na wale ambao kweli waliuamini, wangeweza kuvuta baraka za Mungu kutoka Kwake.
Basi walipofanya hivyo, Yeye alisema, “Nguvu zilimtoka.” Nguvu ni “uweza.” Yeye…Kwa maneno mengine, kama tungeweza kulisema leo hii: Yeye alidhoofika wakati watu walipovuta kutoka Kwake. Vema, kama ilitenda kazi hivyo katika mwili huo wa binadamu, itatenda kazi katika mwili mwingine wa binadamu.
Nasi tunajiumbia mazingira yetu kutuzunguka, kila mmoja wetu. Umekuwa na watu waliokuwa ni watu wazuri, bali ni vigumu tu kwako kuwa karibu nao. Halafu umekuwa na watu wengine ambao unapenda tu kuwa karibu nao. Unaumba mazingira hayo.
Na, loo, hivi si ungalipenda kuwa karibu na Yesu kidogo tu? Ajabu! Uone jinsi hayo mazingira aliyoumba yangalikuwa, nakisia lilikuwa ni lundo moja kubwa tu la upendo, heshima, na kicho cha kitauwa.
MKATE WA KILA SIKU
Njia ya Bwana ni kimbilio lake mtu mkamilifu:
Mithali 10:29
25-0607
56-0613 – Yehova-Yire
Kama ningekuwa mrithi wa nyumba, hakika nisingependa kuhamia humo hadi nipate na kuangalia kila kitu humo. Nataka kuona kilicho changu. Nataka kuona ninachomiliki. Nami niliporithi Ufalme wa Mungu, kwa haki ya Yesu Kristo, kubatizwa katika ukumbi huu mkuu wa baraka za milele za Mungu, napenda kuzunguka na kuona yaliyo yangu (Amina.),
Niangalie kwenye safu nione hiki ni kitu gani. Hili hapa, kila ahadi katika Kitabu ni ya kila Mwamini. Usisimame kimya ili mtu fulani akusukumie kwenye kona, akupe viazi baridi kidogo, na kukuambia usubiri. Usisikilize mambo hayo. Ahadi ya Mungu ni sasa hivi. Kukusukuma mbali katika Utawala wa Miaka Elfu mahali fulani…Biblia ilisema, “Sisi ni wana wa Mungu sasa hivi.” si tutakuwa, tuko sasa hivi, wakati uliopo.
MKATE WA KILA SIKU
na kama tu watoto, basi, tu warithi; warithi wa Mungu, warithio pamoja na Kristo… Warumi 8:17
25-0606
61-0117 – Masihi
Je, mmewahi kuwazia hili? Hebu niwaulizeni jambo fulani. Niangalieni kwa dakika moja. Huu ni mkono wangu, hiki ni kidole changu, hili ni sikio langu, hili ni pua langu, lakini mimi ni nani? Huyo si mimi, hicho ni kitu kilicho changu. Unaona? Huu ni mkono wangu, lakini huyo mimi ni nani anayeumiliki mkono? Huh? Unaona, hii ni nyumba tu ninayoishi ndani yake. Ambayo ni aina ya…?
Vema, lazima kuwe na kitu fulani humo ndani kinachoitwa mimi. Huyo mimi haina budi awe mahali fulani, kwa sababu hii ni mali yangu. Unaliona hilo? Huyo Mimi ni mtu fulani, kwa sababu ninamiliki kitu fulani. Ninao mkono, ni wangu. Vema, huyo mimi ni mali ya nani? Huyo ni roho yako. Vema, inategemea ni kwa roho ya aina gani. Yule unakabidhi viungo vyako kwake huyo ndiye uliye mtumishi wake.
MKATE WA KILA SIKU
Maana mlinunuliwa kwa thamani. Sasa basi, mtukuzeni Mungu katika miili yenu. 1 Wakorintho 6:20
25-0605
53-0607A – Huduma Ya Kristo
Petro alisema…Wakati walipoanza kuyumbayumba na kupiga mayowe, ulimwengu wa nje wa kimsingi wa kikanisa wa Injili yote, ama ulimwengu wa kishupavu ulimjia na kusema, “Watu hawa wamelewa.”
Waweza kuwazia? Na sikilizeni, enyi marafiki Wakatoliki, na ninyi wengine. Bikira Mariamu aliyebarikiwa alikuwa miongoni mwao. Na kama Mungu hata asingemruhusu mama wa Mungu Mwana, aingie katika Ufalme wa Mungu mpaka ajazwe kabisa Roho Mtakatifu hata akatenda kama mwanamke mlevi, mtaingiaje, kwa chochote pungufu? Hilo litakuwaje? Liwazie jambo hilo wewe mwenyewe. Biblia ilisema Mariamu alikuwa mle ndani. Mama mwenyewe wa Kristo ilimbidi kwenda Pentekoste na kukaa kule katika mji wa Yerusalemu mpaka alipokuwa amejawa Roho Mtakatifu hata akayumbayumba kama vile alikuwa amelewa. Amina. Hiyo ni kweli. Hiyo ni Biblia.
MKATE WA KILA SIKU
Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu. Matendo 2:38
25-0604
58-1005M – Isikie Sauti Yake
Mungu ana Kuzaliwa upya kwa ajili yako.
Lakini isikieni Sauti Yake ndogo tulivu. Kila mmoja wenu ninyi watu mnaokiri kuwa Wakristo, tulieni mbele Zake. Msiruhusu kufua nguo kuzuie. Msiruhusu kazi izuie. Msiruhusu chochote kizuie. Usiruhusu mtu yeyote kujua unachofanya. Nenda tu mbele Zake.
Ingia msituni mahali fulani. Nenda kando ya barabara. Ingia kwenye chumba cha siri na ufunge mlango. Watoto wanapoenda shuleni, hapo piga magoti. Umesikia kila aina ya sauti kila mahali, lakini piga magoti tu na ukae hapo mpaka hizo sauti zimenyamazishwa na umeanza kuinuliwa juu.
Itakubadilisha. Itakufanya kuwa tofauti, kama ilivyomfanyia huyu mtoto Samweli. Itakufanyia kitu ikiwa utafanya tu. Sasa, itakufanya kile unachopaswa kuwa. Itakufanya aina ya Mkristo unayepaswa kuwa.
MKATE WA KILA SIKU
Nena, Bwana; kwa kuwa mtumishi wako anasikia. 1 Samweli 3:9
25-0603
61-0426 – Nabii Mikaya
Sasa, ilikuwa ni muda mrefu tangu Eliya alipotoa unabii huu. Alikuwa Utukufuni kwa muda mrefu. Lakini angeweza, alikuwa ametoa unabii huu, naye alijua ulikuwa unakuja kutimia. Halafu basi Mikaya alijua ya kwamba Eliya alikuwa ni mtu wa Mungu, na huyu hapa Mungu juu Mbinguni akifanya baraza Kule juu, jinsi ya kulifanya Neno la Eliya litimie.
Na kama una Neno la Bwana, na utanena Neno la Bwana, wala usilitilie shaka Neno la Bwana, Mungu atafanya mkutano wa baraza kulifanya Neno lako litimie, kwa sababu si neno lako, ni Neno Lake. Ni Neno Lake, kama ni BWANA ASEMA HIVI, kama kweli ni BWANA ASEMA HIVI.
MKATE WA KILA SIKU
Mbingu na nchi zitapita; lakini maneno yangu hayatapita kamwe. Mathayo 24:35
25-0602
51-0508 – Imani Ni Kuwa na Uhakika
Si muda mrefu uliopita, msichana wangu mdogo aliniita, nilipokuwa hapa wakati ule. Namna fulani ya kunipa wazo. Alisema, “Baba, ninakutaka urudi nyumbani.”
Nami nikasema, “Kipenzi, kutoka Texas nilikutumia m—mdoli mdogo.” Alisema-yeye ana umri wa miaka minne tu. Nikasema, “Nimekutumia mdoli mdogo, kipenzi.”
Akasema, “Nimeupokea baba.” Nami nikasema—Akasema, “Nakutaka urudi nyumbani, baba.”
Nami nikasema, “Vema, kipenzi, nilikutumia sungura mdogo kutoka Chattanooga.”
Akasema, “Nimempata, baba.” Lakini akasema, “Nakutaka wewe urudi nyumbani.” Unaona?
Nami nikasema, “Vema, kipenzi, mimi—baba…”
Akasema, “Baba, ninakupenda, nami nazipenda zawadi unazonipa, lakini Mimi namtaka baba.”
Hilo ndilo. Karama zake zote ni zakupendeza, lakini namtaka Baba. Nazipenda karama Zake, kumsikia Yeye katika madhihirisho, kule kumsifu Mungu, na kupiga makelele, na uponyaji, na kunena kwa lugha, na kufasiri lugha, na karama zote mbalimbali. Ninapenda kuketi na kuzitazama. Sina hizo, lakini ninapenda kuzitazama zikitenda kazi Kanisani. Lakini baada ya hayo yote, namtaka Yesu. Ni—ninataka jambo hilo. Karama zake ni nzuri, lakini namtaka Mpaji wake ndani humu. Unaona? Hiyo ni kweli.
MKATE WA KILA SIKU
Sitawaacha ninyi yatima; naja kwenu. Yohana 14:18
25-0601
60-1125 – Kongamano
Hebu wazia tu. Ninaweza kumwona Gabrieli akishuka, upanga Wake mkuu ukiwa ubavuni Mwake. Ninaweza kumwona pakanga. Ninaweza kuwaona Malaika wengine wakuu wakiangaza juu ya mawe yaliyozunguka kando. Ilikuwa ni kitu gani? Meza ya kongamano ilikuwa imeandaliwa.
Kisha huyo Roho Mtakatifu wa Mungu, kama tuonavyo kwenye picha ya Gethsemane, ile Nuru, ambayo Mungu ni Nuru, El Elohim, Yeye Aishie Peke Yake, wakati aliposhuka katika Uwepo Wake. “Je! Unataka kupitia jambo hili, Mwanangu?” Kitu gani? Malaika wakisikiliza. “Ni nini Matokeo yake? Ulimwengu wote uko begani Mwako. Je! Unataka kulipia gharama, ama unataka kufanya nini? Waweza kuja sasa hivi moja kwa moja bila ya mauti. Hiyo hapo Kalvari iko mbele Yako. Ambapo watakutemea mate usoni Mwako, nao watakupeleka Kalvari, mambo haya yote. Utakufa kwa uchungu na taji ya miiba juu ya kichwa chako, na Damu yako itamwagika. Je, uko tayari?”
Hebu tuone hilo kongamano. Mwitikio wake utakuwaje? Malaika wote wamesimama huku wakishangaa kinachotukia sasa. Uamuzi umefanywa. Ni upi? “Si mapenzi Yangu bali Yako yatimizwe.” lo, Malaika wakazimwaga baraka zao na kuanza kumtumikia wakati huo, wakimtayarisha kwa ajili ya saa ile kuu. Kongamano lilifanywa. Uamuzi ukafanywa. Ninayo furaha kweli kwa uamuzi huo.
MKATE WA KILA SIKU
Akisema, Ee Baba, ikiwa ni mapenzi yako, uniondolee kikombe hiki; walakini si mapenzi yangu, bali yako yatendeke Luka 22:42
25-0531
60-0805 – Mwana-Kondoo Na Hua
Wakati Mungu alipomuumba mtu kwanza, alimuumba akiwa vyote mwanamume na mwanamke katika Roho; Alimfanya kwa mfano Wake Mwenyewe, na Mungu ni Roho. Wakati Alipomtenga na kumweka katika mwili, Aliiweka roho ya kiume ndani ya mwanamume, na roho ya kike ndani ya mwanamke, na kama kitu chochote ni kinyume na hilo, kuna upotovu kidogo hapo. Kabisa.
Unamwona mwanamke anajaribu kujifanya mwanamume, kuna kasoro fulani kidogo pale, seli imevuka mahali fulani. Hiyo ni kweli. Unamwona mwanamume dondoa dume kiasi kwamba hatahubiri dhidi ya dhambi ama kitu kingine kama hicho, kuumiza hisia za mtu fulani, kuna mchanganyo hapo mahali fulani, pia, si tu kuzaliwa kwake kwa kawaida, bali kuzaliwa kiroho. Loo, tunachohitaji leo hii ni kwamba mwanamume awe mwanamume, mwanamke, Mwanamke. Mungu amekusudia wawe jinsi hiyo, wavae tofauti.
Unasema, “Unatupiga nyundo sisi wanawake.”
Sasa nitawaambieni kuhusu wanaume. Mwanamume ye yote ambaye atamruhusu mke wake avute sigara, na kuvaa hizo kaptura, na kutenda jinsi hiyo, kuna uwanaume mdogo sana ndani yake, nionavyo mimi.
MKATE WA KILA SIKU
Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba. Mwanzo 1:27
25-0530
65-0718M – Kumtendea Mungu Kazi Bila Mapenzi Yake
Huyu alikuwa Musa akinena na Israeli baada ya yeye kuthibitishwa na Mungu kwa Nguzo ya Moto na kujua alithibitishwa kuwa mtumishi wa Mungu kuwaongoza watoke. Na kabla hawajakwenda katika nchi ile, kabla hawajaingia, Musa alisema, “Sasa maneno niliyonena kwenu, naita mbingu na nchi kushuhudia dhidi yenu. Mkiongeza kitu kimoja kwake au kuondoa neno moja toka kwake, hamtadumu katika nchi awapayo Bwana Mungu.”
Nasema vivyo hivyo katika Jina la Yesu Kristo. Usiongeze kitu. Usiondoe—kuliwekea mawazo yako. Wewe sema tu yaliyosemwa katika kanda hizo. Tenda sawasawa kabisa na vile Bwana Mungu amekuamuru kutenda. Usiongezee Kwake.
Yeye kama kawaida, hutimiza ahadi Yake kwetu. Kila ahadi aliyotoa ameitimiza. Aliwaambieni yatakayotendeka, na je, yalitendeka? Nazileta mbingu na nchi mbele yenu leo kuwahimiza, Mungu aliwahi kusema cho chote ambacho hakutimiza na kutenda sawasawa na alivyosema angetutendea? Ametenda sawasawa hasa na alivyosema angetenda? Hilo ni sawa hasa! Ataendelea kufanya vivyo hivyo. Usiliongezee. Usilipunguzie. Liamini tu nawe utembee kwa unyenyekevu mbele ya Bwana Mungu wako…
MKATE WA KILA SIKU
Na mtu ye yote akiondoa lo lote katika maneno ya unabii wa kitabu hiki, Mungu atamwondolea sehemu yake katika ule mti wa uzima, na katika ule mji mtakatifu, ambao habari zake zimeandikwa katika kitabu hiki. Ufunuo 22:19
25-0529
60-1206 – Wakati Wa Kanisa La Smirna
Haiwezekani kuwa na kuzimu ya Milele. Maana kama kuliwahi kuwa na kuzimu ya Milele, basi daima kulikuwako na kuzimu ya Milele, maana Milele…Kuna aina moja tu ya Uzima wa Milele, na huo ndio sisi sote tunashindania.
Na endapo utateketezwa daima na Milele, basi itakubidi kuwa na Uzima wa Milele ukiteketezwa, ndipo ingekuwa ni Mungu anayeteketea.
Huwezi kuwa na kuzimu ya Milele, na Biblia inasema dhahiri ya kwamba “kuzimu iliumbwa.” Na ikiwa imeumbwa, si ya Milele. Kitu chochote kilicho cha Milele kamwe hakikuumbwa; kilikuwako daima, ni cha Milele.
Nayo Biblia inasema ya kwamba “Kuzimu iliumbiwa ibilisi pamoja na malaika wake.” Kuzimu iliumbwa, si ya Milele. Wala siamini ya kwamba mtu ataadhibiwa Milele.
MKATE WA KILA SIKU
Kisha atawaambia na wale walioko mkono wake wa kushoto, Ondokeni kwangu, mliolaaniwa, mwende katika moto wa milele, aliowekewa tayari Ibilisi na malaika zake. Mathayo 25:41
25-0528
56-1207 – Karama
Haijalishi wana mabomu mangapi ya atomiki, ni mabomu mangapi ya haidrojeni, na wanazungumza kiasi gani juu ya hili na lile litatokea. Msiogope. Mungu yuko kwenye gurudumu. Yeye anajua kabisa jinsi ya kuongoza. Anajua jinsi inavyoenda kuwa. Kwa hivyo hatuna jambo moja la kuogopa, lakini hebu na nikuwa tu mtoto mzuri, asiye na hofu, ambaye anamtazama Baba kila dakika, na kumtegemea Yeye atuongoze, atuelekeze, na kutupeleka kwenye kikomo chetu kwa neema Yake.
Na kwa kumpenda Yeye jinsi hiyo, hungefanya lolote la kumuumiza Yeye. Mbona, kama ungefanya jambo lolote la kumuumiza, ama usiku kucha, machozi yako yenye ya moto yangetiririka mashavuni mwako kwa toba. Kwa sababu haungemuumiza Baba kwa lolote. Je! unge…Hungemuumiza mtoto wako mchanga; ungechukia kufanya hivyo. Ungechukia kuumiza hisia za mke wako au mume wako. Je! ni zaidi sana jinsi gani Bwana na Mwokozi wako? Ungefanya hivyo kama unampenda…
MKATE WA KILA SIKU
Mungu ni upendo, naye akaaye katika pendo, hukaa ndani ya Mungu, na Mungu hukaa ndani yake. 1 Yohana 4:16
25-0527
54-1219M – Uponyaji Wa Kiungu
Sasa, unaona, hakuna haja ya kupigana. Mungu hushughulikia mambo yote, unaona. Usifanye hivyo. Upendo tu. Rudisheni wema kwa ubaya kila wakati. Je, hiyo ni kweli? Mtu yeyote anaposema mema juu yako; vizuri, shukuru. Ikiwa mtu yeyote anazungumza mabaya juu yako; wabariki hata hivyo. Hakika. Hiyo ni kweli. Hebu…Mungu hushughulikia mengine. Yeye Ndiye. Hiyo si ni kweli? Yeye Ndiye. Kwa hiyo, hata hivyo, sote hatuna budi kujibu Kwake.
Na haijalishi ni nini, ikiwa adui yako mkuu…Ikiwa una hisia yoyote, na adui mbaya zaidi uliye naye, ambaye unajua alikuwa anaenda mahali kama kuzimu, ingekufanya ujisikie vibaya.
Sijui mtu, sijui…siwezi kuwazia mtu wa chini kabisa duniani, leo, kwamba alikuwa Stalin kule juu, yeyote yule, ningechukia kujua kwamba mtu huyo alikuwa anateseka katika mateso ya kuzimu asubuhi ya leo. Ningechukia kujua hilo. Hakika ningechukia. Ninaomba Mungu airehemu nafsi yake iliyopotea, alipokuwa akifa, unaona, kwamba Mungu hatamwacha ateseke hivyo,…?…Mwazie mwanadamu katika mateso ya kuzimu, ambayo Biblia inaonyesha hapa kwa asiyeamini.
MKATE WA KILA SIKU
Lakini nawaambia ninyi mnaosikia, Wapendeni adui zenu, watendeeni mema wale ambao wawachukia ninyi Luka 6:27
25-0526
59-0920 – Kupanda Mzabibu Na Mahali Pa Kuupandia
Yale ibilisi afanyayo ni hadithi ya uongo. Yale Mungu afanyayo ni halisi. Kwa hiyo, ninapenda hili lizame ndani kabisa mioyoni. Mungu anapomwokoa mtu, yeye ameokoka. Usiwe na wasiwasi juu ya kurudi nyuma kamwe; huwezi. Kile Mungu afanyacho ni cha Milele. Ibilisi anaweza kukuchochea na kukufanya uamini umeokoka. Lakini wakati Mungu anapokuokoa kweli, unao milele, kwa sababu unao Uzima wa Milele. Yesu alisema hivyo.
“Yeye ayasikiaye Maneno Yangu, na kumwamini Yeye aliyenipeleka yuna Uzima wa Milele, wala hataingia hukumuni, bali amepita kutoka mautini kuingia Uzimani.” Huo ni wa Milele kama Mungu Mwenyewe alivyo, kwa sababu ni Neno Lake.
MKATE WA KILA SIKU
…bali wokovu wangu utakuwa wa milele, na haki yangu haitatanguka.
Isaya 51:6
25-0525
56-0728 – Kufanya Bonde Lijae Mahandaki
Nionyeshe marafiki zako, nitakuambia wewe ni nani. Hebu niingie nyumbani mwako. Hebu acha nione kile kilichowekwa wazi mezani. Hebu nione jinsi Biblia hiyo ilivyowekwa alama. Hebu nione ziko wapi hizo Hadithi za Kweli. Hebu nisikilize ni aina gani ya muziki unauoleta kwenye redio yako. Hebu nione ni aina gani ya picha ulizonazo nyumbani mwako. Nitakuambia umefanywa kwa kitu gani. Ndiyo, bwana. Hayo ndiyo roho yako inakula. Bila kujali ushuhuda wako ukoje, matunda yako yanathibitisha ulivyo. Kweli.
Lo, ni ukweli. Nafsi yako inalishwa kwa kitu fulani. Na vyovyote tabia ya nafsi yako ilivyo, hivyo ndivyo itakavyo—itajidhihirisha. Hiyo ndiyo sababu Yesu alisema, “Kwa matunda yao mtawatambua.”
MKATE WA KILA SIKU
Ndiposa kwa matunda yao mtawatambua. Mathayo 7:20
25-0524
60-0109 – Mabwana, Sisi Tunataka kumwona Yesu
Hapo ndipo imani yangu imejengwa juu yake, si chochote pungufu ya Neno la Milele la Mungu wa Milele.
Na Mungu si bora kuliko Neno lake; Mimi si bora kuliko neno langu; na wewe si bora kuliko neno lako. Kama siwezi kulikubali neno lako, basi mimi…Hakuna haja ya mimi kusema nina imani nawe, kwa maana singeweza. Na kama huwezi kulikubali neno langu, hakuna haja ya wewe kuniambia kuwa unaniamini, kwa sababu huwezi. Basi kama hatuwezi kuchukua Neno la Mungu, hatuwezi kuwa na ujasiri. Lakini wakati Mungu amesema jambo hilo, nawe unaliamini kwa moyo wako wote, kwamba limetumiwa kwako, halina budi kutukia.
Hebu naomba ifahamike sasa hivi nikisema: Kwamba ninaamini kwamba mtazamo sahihi wa kiakili kuhusu ahadi yo yote ya Kiungu ya Mungu utaitimiza.
MKATE WA KILA SIKU
Basi msiutupe ujasiri wenu, kwa maana una thawabu kuu. Waebrania 10:35
25-0523
63-1114 – Ushawishi
Tunapaswa kuheshimiana mmoja na mwenzake, kuheshimiana mmoja na mwenzake, kama ndugu, dada. Na kupendana mmoja na mwenzake, kwa upendo usiopungua. Unasema, “Vema, siwezi kabisa.” Vema, bakia tu hapa muda mrefu kidogo, na ndipo utawapenda watu, pia. Utawapenda wale wasiokupenda. Hiyo kweli ni ishara nzuri ya Ukristo: wakati unapoweza, kutoka moyoni mwako, kuwapenda wale ambao hawakupendi. Wapende wasiopendeka.
Yesu alisema, “Ukiwafanyia fadhili wale tu ambao hukufadhili, vema, watoza ushuru hufanya jambo lilo hilo.” Bali, unaona, lazima uwahurumie wale wasiokuhurumia. Watendee wema wale ambao wangekutendea uovu. Daima kumbuka hilo. Weka hilo mbele zako, kwamba Mungu anakutazama. Kumbuka, Mungu alikuwa mwema kwako wakati ulipokuwa mwovu Kwake. “Wakati mlipokuwa mngali wenye dhambi, Kristo alikufa kwa ajili yenu.”
MKATE WA KILA SIKU
Maana, hii ndiyo habari mliyoisikia tangu mwanzo, kwamba tupendane sisi kwa sisi; 1 Yohana 3:11
25-0522
63-0428 – Tazama
Wakati mwingine hatuwezi kungoja kutoka usiku mmoja hadi mwingine. Wakati mwingine hatuwezi kungoja kutoka uamsho mmoja hadi mwingine. Inatubidi kutoka nje na kujitatanisha na mambo ya ulimwengu. Jinsi inavyotupasa kujionea aibu.
Kabla hatujaja hapa kukiri na kuingia ndani ya hiyo Damu ya Yesu inayotusafisha na dhambi yote, inatupasa kujilenga kikamilifu, tupate kumwona yule Mungu mmoja aliye hai amesimama pale, Yeye aliyefanya ahadi, ya kwamba, “Mbingu na nchi zitapita, bali Neno Lake haliwezi kushindwa.” Kaa papo hapo juu ya Hilo, ndipo hutatupwa huku na huko kwa pepo za mafundisho, ukichukuliwa mahali mahali, huku na huku.
Lakini, unajua mahali unaposimama, kwa maana umelengwa shabaha pamoja na Mungu. Unayaona maisha yako mwenyewe yakipiga ile shabaha, kama tu wale mitume walivyofanya. Unaishi jinsi walivyoishi. Ulibatizwa jinsi walivyobatizwa. Unaona matokeo yale yale waliyoona. Unaona likitenda kazi ndani yako. Umelengwa kikamilifu. Sijali yale kampuni isemayo na yale madhehebu yasemayo. Umelengwa kikamilifu, kwa sababu unajua ya kwamba unapiga shabaha. Amina.
MKATE WA KILA SIKU
Mwe na kiasi na kukesha; kwa kuwa mshitaki wenu Ibilisi, kama simba angurumaye, huzunguka-zunguka, akitafuta mtu ammeze. 1 Petro 5:8
25-0521
56-0726 – Upendo
Huwaoni kunguru na hua wakikaa pamoja, kwa sababu hawana ushirika. Hawana mambo ya pamoja. Kunguru anaweza kuruka juu ya mzoga uliokufa na kuula. Na…Lakini hua atakwenda kwenye shamba la ngano na kula nafaka. Sasa, nataka mwone kile shetani anachoweza kufanya. Sasa, hua yeye hawezi kuketi juu ya mzoga uliokufa na kuula. Lakini kunguru anaweza kula mzoga uliokufa na pia kula ngano. Yeye ni mnafiki. Unaona? Hua hawezi kufanya hivyo, kwa sababu yeye ameumbwa tofauti.
Sasa, mtu anaweza kuuiga Ukristo, lakini Mkristo hawezi kuiga dhambi. Roho aliye ndani yake hatamruhusu yeye kufanya hivyo. Yeye ana…Hua, sababu ya yeye kutoweza kuula huo, ungemuua. Yeye Hana nyongo, kama tulivyozungumza usiku uliopita. Hana nyongo. Kama angeula, ungemuua; ile sumu ingemuua. Hawezi kufanya jambo hilo.
Lakini kunguru yeye anaweza kula mzoga uliokufa na ngano pia. Hivyo ndivyo mwigaji anavyoweza kufanya. Lakini Mkristo halisi wa kweli hawezi kuwa kitu kingine kile ila waraka halisi wa Mungu.
MKATE WA KILA SIKU
Kwani tumaini la mpotovu ni nini, ingawa ajipatia faida, Hapo Mungu amwondoleapo roho yake? Ayubu 27:8
25-0520
56-0902 – Yale Maandiko Kwenye Ukuta
Kuna kitu kimoja tu, na mahali pamoja tu katika Biblia, palipowahi kufanywa, ambacho kilimfanya mtu wavue nguo zao, nao walikuwa wamepagawa na ibilisi. Hiyo ni kweli. Ni Ukweli. Na hakuna pongezi juu ya hilo, kupatana. Ni Ukweli. Ni ibilisi ndiye anayewaingia watu hao, anayewafanya kuvua nguo zao. Ni shetani. Humaanishi kukosea, lakini, Ewe mwanamke, ni ibilisi anayefanya jambo hilo.
Ilikuwa ni makosa kwa wanawake wa holiness kuvaa rangi kwenye nyuso zao. Na sasa, wanaliendeleza hilo tu, hata hivyo, na kuimba na kupaza sauti, na kumsifu Bwana, kana kwamba hakuna jambo lolote kwake.
Loo, ndugu, Je!unatambua ya kwamba huyo ni ibilisi anayefanya jambo hilo? Kusudia moyoni mwako, kwamba utaishi, kama ni mtindo wa kale, uishi mtindo wa kale, na umtumikie Bwana Mungu wa mbingu na nchi. Kusudia moyoni mwako.
MKATE WA KILA SIKU
Atendaye dhambi ni wa Ibilisi; kwa kuwa Ibilisi hutenda dhambi tangu mwanzo. 1 Yohana 3:8
25-0518
62-0607 – Kuvaa Silaha Zote Za Mungu
Sikilizeni, hivi mliwahi kuwazia hizo ofisi za Kanisa ni nini? Ni vazi la Mungu, vazi la ndani, mtume, nabii, mwonaji. Kuliona kabla Shetani hajalifikia, tayari amelisema. Ni kitu gani? Mungu amevaliwa Kanisani Mwake, ofisi hizi ni vazi la Mungu. Unapoona ofisi hizo, wachungaji, waalimu, wainjilisti, hizo ni nini? Hizo ni vazi la Mungu, Uwepo wa Mungu, Roho wa Mungu, na kama…akitenda kazi kupitia kwa mwanadamu.
Na kama ofisi hiyo ikikanusha lolote la Neno hili, basi hayo si mavazi ya Mungu, mnaona. Mnaona? La, siyo, huyo ni mbwa mwitu aliyevaa ngozi ya kondoo. Mwangalie jamaa huyo, jihadhari naye. Lakini anapochukua tu yale Neno lisemayo, kumbukeni, huyo ni Mungu, maana yeye ananena Neno Lake. Mnaona? Lakini kama akisema, “Vema, si…” Loo, loo, loo, loo, loo, loo, jamani! Ondokeni, enyi kondoo, ondokeni!
MKATE WA KILA SIKU
Jihadharini na manabii wa uongo, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini kwa ndani ni mbwa-mwitu wakali. Mathayo 7:15
25-0517
62-1122 – Kurudi Na Yubile
“Rudini. Rudini.” Roho Mtakatifu analia, “Rudini!” Ninaweza kuwazia wakati Yesu alipotazama nje juu ya Yerusalemu naye akalia, aliipenda, nao walikuwa wamemkataa. Na mtu ambaye amejazwa na Roho usiku wa leo anaweza kuangalia nje juu ya kanisa na kuwaona watu wanaopaswa kung’aa kwa uweza wa Mungu wenye utukufu, huku Roho Mtakatifu ndani ya moyo wako akilia machozi ya majuto. Tumefanya nini?
Mungu alituita sisi, baba zetu watoke miaka hamsini iliyopita, nasi tukarudi. Nanyi mnaona kilichotuletea: kundi la aibu chini ya jina la Pentekoste, watu wanaovuta sigara, kunywa pombe, waliooa mara tatu au nne, wanawake wanaokata nywele zao, kujipaka rangi, kutumia ninii zao…kaptura, wanavaa mavazi ya kizinifu, kila kitu, wanajiita dada wa Kipentekoste. Ni fedheha jinsi gani kwa Jina la Kristo! Ni fedheha jinsi gani juu ya Kanisa Lake! Si ajabu anasema majina yanayokufuru yalipatikana Babeli, dhehebu, machafuko, yote yamevurugika, kila aina ya hili, lile, na linginelo. Kristo yuko wapi katika jambo hilo lote? Rudini, enyi watu.
MKATE WA KILA SIKU
…itakuwa ni yubile kwenu, nanyi kila mtu atairudia milki yake mwenyewe, nanyi mtarejea kila mtu kwa jamaa yake. Walawi 25:10
25-0516
62-0607 – Kuvaa Silaha Zote Za Mungu
Sikilizeni, hivi mliwahi kuwazia hizo ofisi za Kanisa ni nini? Ni vazi la Mungu, vazi la ndani, mtume, nabii, mwonaji. Kuliona kabla Shetani hajalifikia, tayari amelisema. Ni kitu gani? Mungu amevaliwa Kanisani Mwake, ofisi hizi ni vazi la Mungu. Unapoona ofisi hizo, wachungaji, waalimu, wainjilisti, hizo ni nini? Hizo ni vazi la Mungu, Uwepo wa Mungu, Roho wa Mungu, na kama…akitenda kazi kupitia kwa mwanadamu.
Na kama ofisi hiyo ikikanusha lolote la Neno hili, basi hayo si mavazi ya Mungu, mnaona. Mnaona? La, siyo, huyo ni mbwa mwitu aliyevaa ngozi ya kondoo. Mwangalie jamaa huyo, jihadhari naye. Lakini anapochukua tu yale Neno lisemayo, kumbukeni, huyo ni Mungu, maana yeye ananena Neno Lake. Mnaona? Lakini kama akisema, “Vema, si…” Loo, loo, loo, loo, loo, loo, jamani! Ondokeni, enyi kondoo, ondokeni!
MKATE WA KILA SIKU
Jihadharini na manabii wa uongo, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini kwa ndani ni mbwa-mwitu wakali. Mathayo 7:15
25-0515
64-0305 – Kung’ang’ania
Sasa tunaamini Biblia kuwa ni Neno la Mungu lisilokosea. Tunaamini ya kwamba ndiyo ufunuo mkamilifu wa Yesu Kristo; akijifunua Mwenyewe katika Agano la Kale, kwa manabii; Mungu akijijulisha Mwenyewe kupitia kwa Mwanawe, Kristo Yesu, na katika Yeye ulikaa utimilifu wa Mungu, kwa jinsi ya mwili. Yeye alisulibishwa kwa ajili ya dhambi zetu; akafa, akazikwa, akafufuka katika siku ya tatu, akapaa Mbinguni, na amerudi hapa tena katika Jina la…Katika umbo la Roho Mtakatifu, Mungu akiishi…Wakati mmoja, Mungu juu yetu; katika Kristo, Mungu pamoja nasi; sasa Mungu ndani yetu. Ni Mungu akirudi katika mwanadamu, kuabudu, kuabudiwa katika mwanadamu, ajenti wa Mungu. Mungu hatendi jambo lo lote nje ya mwanadamu kuwa ajenti Wake, msaidizi Wake.
MKATE WA KILA SIKU
Njoni, tuabudu, tusujudu, Tupige magoti mbele za Bwana aliyetuumba. Zaburi 95:6
25-0514
61-0117 – Yule Masihi
Mko tayari? Yohana Mtakatifu 14:12, Yesu alisema, “Yeye aniaminiye Mimi, kazi nizifanyazo Mimi, yeye naye atazifanya,” Masihi wadogo, hiyo ni kweli, Masihi wadogo, uwakilishi wa Masihi duniani, bado…
Marko 16, Alisema, “Enendeni ulimwenguni mwote, mkaihubiri Injili. Ishara hizi zitafuatana,” na Masihi wadogo. “Aaminiye na kubatizwa ataokoka. Asiyeamini atahukumiwa, na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio.”
Umbali ngani? Kwa ulimwengu wote. Kwa akina nani? Kila kiumbe. Lo, ninayo furaha! Utaliondoaje jambo hilo?
Akasema, “Ni kwa wanafunzi peke yao.”
Ati Kwa wanafunzi? Alisema, “Kwa ulimwengu wote, na kwa kila kiumbe. Ishara hizi zitafuatana na hao waaminio.”
MKATE WA KILA SIKU
Amin, amin, nawaambieni, Yeye aniaminiye mimi, kazi nizifanyazo mimi, yeye naye atazifanya; naam, na kubwa kuliko hizo atafanya, kwa kuwa mimi naenda kwa Baba. Yohana 14:12
25-0513
62-0518 – Kutoa Presha
Naye Mwakilishi wa Mungu duniani siku hizi ni Roho Mtakatifu. Na unapokuwa Uweponi Mwake, umwone Yeye akikubariki, unawezaje kupandisha presha kama hiyo ya kumchukia jirani yako? Unawezaje kujenga tofauti ya kimadhehebu moyoni mwako? Unasema, “Kama hawakuwa Wapentekoste, kama alikuwa wa Umoja, ama kama alikuwa wa Utatu, kama alikuwa, alikuwa mfuasi wa Assemblies, kama alikuwa mfuasi wa Church of God, ningeweza kushiriki pamoja naye.” Unawezaje kufanya hivyo Mbele za Mwenyezi Mungu? Roho Mtakatifu anawezaje kuwa akishuka juu ya kusanyiko, na kisha kuleta tofauti za kimadhehebu? Anawezaje kufanya hivyo? Toeni presha.
Shida, tulipandisha presha yetu, kwa sababu tuna nia za kimadhehebu sana. Loo, Marekani imeoza nazo, madhehebu, wakijenga nyua, kanuni za imani. Unajali nini kuhusu hizo kanuni za imani na nyua? Ingia katika Uwepo wa Mungu, ingia katika Uwepo wa Roho Mtakatifu, toa presha basi.
MKATE WA KILA SIKU
Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu. Wagalatia 5:22
25-0512
61-0209 – Yehova-Yire
Moja ya mambo ya kusikitisha sana ambayo nimewahi kuona katika Biblia, Biblia ikitabiri, ilikuwa wakati huu wa kanisa. Huu ndio wakati wa kanisa ulio wa kutisha kuliko nyakati zote za kanisa. Kila wakati wa kanisa…Angalia Ufunuo, katika Ule wa Laodikia, wakati wa kanisa la Kipentekoste, ya kwamba Kristo alikuwa ametolewa nje ya Kanisa Lake Mwenyewe, akisimama nje, akibisha mlango, akijaribu kurudi katika Kanisa Lake Mwenyewe. [Ndugu Branham abisha hodi kwenye mimbara—Mh.]
Sasa, ilionekana kama wito kwa wenye dhambi, lakini huo ni wakati wa kanisa, wakati wa Laodikia. Alikuwa ametolewa nje na madhehebu, na kadhalika, walimweka nje, nao walikuwa wamechukua mambo ya kilimwengu, Naye akasema, “Nasimama mlangoni, nabisha.” Wa kanisa Lake Mwenyewe! Si wakati mwingine uliofanya hivyo, bali wakati huu, kwa hiyo unaona mahali tunaposimama. Nia yoyote ya kweli, nzuri, ya kiroho inaweza kulishika hilo, na kulinyakua, na kwenda nalo, unaona, kwa sababu unaona mahali lilipo.
Wachache sana wa wakati huu ndio watakaochukuliwa, kama tunavyolijua hilo. Watu wengi wanatazamia kuongezeka kukuu, kumwagwa kukuu, na kadhalika, kumbukeni tu, wekea hilo alama katika Biblia yako: Hutaliona hilo, hiyo ni BWANA ASEMA HIVI.
MKATE WA KILA SIKU
Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi. Ufunuo 3:17
25-0511
65-0220 – Mahali Alipopachagua Mungu Pa Kuabudia
Na sasa tunaona kwamba Yesu alisema, pia, “Mimi nilikuja katika Jina la Baba Yangu, nanyi hamkunipokea Mimi.” Basi, Jina la Baba lazima liwe ni Yesu. Hiyo ni kweli. Jina la Baba ni Yesu, sababu Yesu alisema hivyo. “Ninachukua Jina la Baba Yangu. Nimekuja katika Jina la Baba Yangu, wala ninyi hamkunipokea Mimi.” Basi Jina Lake lilikuwa ni Yesu.
Ndipo Gabrieli alimwita Yeye Yesu, manabii walimwita Yeye Yesu, na Yeye alikuwa Yesu hasa. Kabla ya kuzaliwa Kwake, hata nabii mtakatifu alimwita Jina Lake Imanueli, ambalo ni, “Mungu pamoja nasi.” Basi, “Mungu alidhihirishwa katika mwili, apate kuondoa dhambi ya ulimwengu,” na, katika kufanya hivyo, Yeye alipewa Jina la Yesu. Kwa hiyo, Jina hilo ni Yesu.
Na hilo Jina liliwekwa katika Mtu; si kanisa, si madhehebu, si kanuni ya imani, bali Mtu! Yeye alichagua kuweka Jina Lake katika Yesu Kristo. Sasa tunaona kwamba ndipo Yeye anakuwa mahali pa Mungu pa kuabudia, ambapo unamwabudu Yeye.
MKATE WA KILA SIKU
Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi. Yohana 14:6
25-0510
64-0306 – Aliye Mkuu Kuliko Sulemani Yupo Hapa Sasa
Mungu hahitaji mfasiri ye yote.
Sisi tunafasiri, tunasema, “Hili, hili ni lile, na hili ni lile,” na kadhalika.
Mungu hahitaji mfasiri ye yote. Yeye ndiye anayejifasiria. Mungu hatuhitaji sisi kulifasiri Neno Lake. Biblia, limeandikwa, Nalo linasema si la kufasiriwa anavyotaka mtu ye yote. Mungu alisema, hapo mwanzo, “iwe nuru,” ikawa nuru. Hiyo ndiyo fasiri yake. Mungu alisema, “bikira atachukua mimba,” naye akachukua mimba. Hiyo ndiyo fasiri yake. Haihitaji mtu ye yote kuifasiri.
Mungu alisema, katika siku hii, mambo haya yangetukia, nayo yanatukia. Hayahitaji kufasiriwa ko kote. Ni Mungu akijifasiria Mwenyewe. Yanatukia. Haidhuru tujaribu kulivuruga jinsi gani, na kusema, “Halimaanishi Hivi, wala halimaanishi Lile.” Linamaanisha jambo lilo hilo hasa, na Mungu ndiye anayejifasiria Mwenyewe. Yeye huthibitisha Neno Lake, na hiyo ndiyo fasiri Yake, kwa sababu linatimizwa.
MKATE WA KILA SIKU
Usiongeze neno katika maneno yake; Asije akakulaumu, ukaonekana u mwongo. Mithali 30:6
25-0509
61-0827 – Ujumbe Wa Neema
Kwa hiyo ilimbidi Mungu kufanyika mtu, Naye alikufa katika mwili wa binadamu, katika umbo la mtu aliyeitwa “Yesu Kristo,” na Huyo alikuwa Ndiye Masihi aliyeahidiwa aliyeinunua neema. Hapo ndipo unapoona ya kwamba Mungu na Kristo ni Mtu yule yule, Mungu akiishi katika Kristo. “Mimi na Baba Yangu ni Mmoja, Baba Yangu anaishi ndani Yangu; si Mimi ninayenena Neno, bali ni Baba Yangu anayeishi ndani Yangu.” Mungu katika Kristo! Hakika.
Neema iliahidiwa katika bustani ya Edeni, nayo neema ikaja, neema kwa Adamu na Hawa. Hakuna mahali pa kwenda, hakuna njia ya kugeukia na hata hivyo neema ilifanya njia!
Hebu niseme jambo hili, rafiki yangu mwenye dhambi. Huenda ukawa hapa asubuhi ya leo kahaba, huenda ukawa hapa asubuhi ya leo mwandama wanawake, huenda ukawa hapa mlevi ama mcheza kamari, ama mwuaji. Huenda ukawa hapa kama mume mchafu, mke mchafu. Huenda ukawa ndiye mwenye dhambi aliye mchafu kuliko wote. Unasema, “Nimepita kiwango hicho cha ukombozi.” La, hujapita, la sivyo usingekuwa kanisani asubuhi ya leo. Neema itakufanyia njia katika saa hii ya giza kama utaikubali. Ilimbidi Adamu kuwa radhi kuipokea, nawe pia. Ikubali.
MKATE WA KILA SIKU
Kwa maana dhambi haitawatawala ninyi, kwa sababu hamwi chini ya sheria, bali chini ya neema. Warumi 6:14
25-0508
62-1223 – Dhihaka Kwa Sababu Ya Neno
Na Mungu huweka wakati na ana kusudi kwa ajili ya kila kitu afanyacho. Hakuna kitu kinachotukia kwa bahati mbaya tu kwa wale wampendao Bwana na wameitwa kulingana na wito Wake. Mnaona? Tumechaguliwa tangu zamani. Na kila kitu hufanya kazi vizuri tu, kwa ajili ya jambo hilo, kwa kuwa Yeye hawezi kusema uongo. Naye alisema hiyo ilikuwa ndivyo, ya kwamba kila kitu kina wakati wake, majira yake, na kina njia yake. Na Mungu yuko nyuma ya kila msogeo. Na wakati mwingine unafikiri kwamba kila kitu kinaenda mrama. Ni juu yetu. Mambo hayo yanawekwa juu yetu, majaribu na fadhaa. Ni kujaribiwa, kuona vile tutakavyotenda kwa tukio fulani.
MKATE WA KILA SIKU
Kwa maana dhambi haitawatawala ninyi, kwa sababu hamwi chini ya sheria, bali chini ya neema. Warumi 6:14
25-0507
58-1221M – Yuko Wapi, Mfalme Wa Wayahudi?
Ni Krismasi. Mapambo yote, pilkapilka zote barabarani, za Baba Krismasi, hadithi ya kubuni ya Kijerumani, fundisho la sharti la Kikatoliki, hakuna hata sehemu moja yake iliyo kweli. Na inachukua mahali pa Yesu Kristo, katika mioyo ya Wamarekani wengi sana. Krismasi haimaanishi Baba Krismasi. Krismasi maana yake Kristo. Si mtu fulani aliye na kiko kinywani mwake, na akishuka kwenye dohani! Ukiwafundisha watoto wako vitu kama hivyo, unatarajia wakue wawe nini? Waambie Ukweli, sio kwenye hadithi fulani za uwongo. Waambie, “Kuna Mungu wa Mbinguni ambaye alimtuma Mwanawe, na hiyo ndiyo maana ya Krismasi. Naye yuko karibu kuja tena.”
Na shinikizo linapoanza kuja duniani, ibilisi ametoa vitu vyake, kwa macho, vile unavyoweza kuona, mapambo, na kadhalika. Mungu ametoa Yake, ambayo ni Roho, ambayo huwezi kuona, lakini unaamini.
MKATE WA KILA SIKU
Mungu ni Roho, nao wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli. Yohana 4:24
25-0506
64-0306 – Aliye Mkuu Kuliko Sulemani Yupo Hapa Sasa
Mungu, na daima katika nyakati zote, daima amewapa watu Wake karama za kiroho. Hivyo ndivyo anavyotambulishwa na kujulikana, kwa karama za kiroho. Na hapo Mungu anapotuma karama ya kiroho kwa watu Wake, na karama hiyo ya kiroho inakataliwa, basi hao—watu hao huingia katika giza la machafuko. Kila wakati, katika nyakati zote, wakati Mungu anapowatumia watu jambo fulani, karama, nao wanalikataa, watu hao wanakataliwa na Mungu kwa sababu wameikataa rehema ya Mungu.
Loo, ungekuwa ni usalama wa namna gani, usiku wa leo, jinsi lingekuwa ni jambo bora zaidi kuliko kinga zote za mabomu na—na mahali pote tungaliweza kuwazia, kama taifa hili, ambalo linaitwa taifa la Kikristo, lingeweza kukubali karama ya Mungu ambayo limepewa, Roho Mtakatifu aliye mkuu aliyemwagwa katika siku hizi za mwisho. Na jinsi ambavyo kama taifa hili lingekubali jambo Hilo, lingekuwa mahali pa salama zaidi kuliko kitu cho chote wangaliweza kuingia ndani yake. Lakini walimkataa, kwa hiyo hakuna kilichosalia ila machafuko na hukumu.
MKATE WA KILA SIKU
Ni nani aliye na hekima, naye atayafahamu mambo haya? Ni nani aliye na busara, naye atayajua? Kwa maana njia za Bwana zimenyoka, nao wenye haki watakwenda katika njia hizo; bali waasio wataanguka ndani yake. Hosea 14:9
25-0505
65-0424 – Mmoja Katika Milioni Moja
Yesu alisema, duniani, “Mtu hataishi kwa mkate tu, bali kwa kila Neno.” Kila Neno! Si tu mara kwa mara, Neno, bali kwa kila Neno.
Ilikuwa ni Neno moja lisiloaminiwa, na ninii ya Mungu…la amri za Mungu, lililosababisha mauti, huzuni, na kila maradhi na magonjwa ya moyo, kukosa Neno la Mungu, Neno moja! Kama aliipeleka jamii ya mwanadamu mautini, kwa kukosa, kutokuamini Neno moja, “hakika,” hakika. Bali Yeye alisema lingetukia. Shetani akasema, “Hakika halitatukia.” Lakini lilitukia.
Kwa hiyo, inatupasa kutimiza kila Neno la Mungu. Na kama mwanadamu na kuteseka huku kote na kadhalika kulikoingia kwenye jamii ya mwanadamu, kwa kuelewa vibaya, ama—ama kutokuamini Neno moja, tutarudi namna gani kwa kuacha Moja, kama liligharimu gharama hii yote, hata uhai wa Mwanawe?
MKATE WA KILA SIKU
Kwa maana ni amri juu ya amri, amri juu ya amri; kanuni juu ya kanuni, kanuni juu ya kanuni; huku kidogo na huku kidogo. Isaya 28:10
25-0504
54-0216 – Yairo na Uponyaji wa Kiungu
Sasa, nitawashtua kidogo. Hamjali, sivyo? Sawa. Kwa mfano, unakaanga nyama, na mara moja mafuta yanatona mkononi mwako. Sasa, ikiwa utayatikisa tu na uendelee kukaanga nyama, hilo halitakusumbua. Sasa, najua hamkulipata hilo sawasawa. Tazama. Jambo la kwanza, “Loo, Yuko wapi Yule Asiyejua?” Kitu fulani…Unaona, kiliushika mkono wako. Unaona, unaona? Inakuogopesha nusura kufa. Hilo ndilo linalofanya jambo hilo. Ni hofu.
Petro akitembea juu ya maji. Alikuwa akitembea vizuri, mpaka alipoona mawimbi ya mbisho naye akaogopa. Yesu akasema, “Kwa nini umeogopa?” Hiyo ndiyo shida ya watu wa Roho Mtakatifu leo. Wana hofu sana…
Ibilisi anajaribu tu kukutisha uondokane na jambo fulani. Anajaribu kuahirisha jambo fulani mahali pengine, kusema, “Moja ya siku hizi utakuwa hivi.” Uko hivyo sasa hivi. Sasa, sisi tu wana wa Mungu. Sasa, tumeketi pamoja katika mahali pa mbinguni. Sasa, tunayo mamlaka yote mbinguni na duniani. Unaona? Sasa, tunayo. Si katika Utawala wa Miaka Elfu, hatutayahitaji wakati huo. Tunayo sasa hivi. Sisi ni…Sasa hivi sisi tu wana wa Mungu.
MKATE WA KILA SIKU
Wapenzi, sasa tu wana wa Mungu, wala haijadhihirika bado tutakavyokuwa; lakini twajua ya kuwa atakapodhihirishwa, tutafanana naye; kwa maana tutamwona kama alivyo. 1 Yohana 3:2
25-0503
60-0109 – Mabwana, Tunataka kumwona Yesu
Njia pekee ya kumwona Mungu ni kumweka Yeye ndani yako, ili aweze kutumia macho yako. Utamuona Yeye. Lakini kama unajaribu kumwona katika dhana ya kiakili ya Neno Lake, ama kazi ya hisi fulani, haitafaa chochote; Anapaswa Yeye awe ndani yako.
Kisha utalia wakati wa machweo na mawio ya jua. Utatazama ukuu wa mwaka ujao. Kabla hata baridi au upepo wa baridi haujawahi kugonga dunia, utomvu utaiacha miti na kwenda chini kwenye mizizi, kujificha. Kwa sababu ukikaa huko, majira ya baridi kali yataua mti huo.
Kisha ninauliza swali hili, “Ni akili gani inayoendesha huo utomvu kutoka kwenye mti huo hadi kwenye mizizi ili kujificha kwa ajili ya majira ya baridi?” Loo, kafiri hana sababu. Lakini atakapoingia, utamwona katika kila kitu.
MKATE WA KILA SIKU
Ameiumba dunia kwa uweza wake, Ameuthibitisha ulimwengu kwa hekima yake, Yeremia 51:15
25-0502
52-0810E – Yesu Kristo Yeye Yule Jana, Leo, Na Milele
…katika bustani ya Edeni, kuna miti miwili; mmoja ulikuwa maarifa na mmoja imani. Mmoja ulikuwa Uzima. Mmoja ulikuwa mauti ya maarifa, huo mwingine ulikuwa uzima kwa imani. Na ilimradi tu wanakula kwa imani ya mti huu, vema, waliishi. Lakini alipofika kwenye mti huu, alikufa. Mego ya kwanza aliyokula, alijitenga mwenyewe na Mungu. Naye mwanadamu daima amekuwa akimega kutoka kwenye mti huo. Na kila wakati anapong’ata kwa maarifa, anajiangamiza mwenyewe. Mungu Yeye haangamizi chochote. Mwanadamu hujiangamiza mwenyewe kwa maarifa.
Angalia, alijing’atisha mwenyewe kwenye baruti, akawaua wenzake. Alijing’atisha kwenye gari kutoka kwenye ule mti, linaua zaidi ya vita vyote vikiwekwa pamoja. Je! hiyo ni kweli? Maarifa, maarifa, kula kutoka kwenye mti huo. Amejipatia bomu la hidrojeni sasa; Nashangaa kile atakachofanya na hilo. Unaona?
Lakini shida yake ni kwamba, watu hawa, wanawazia sana, kwenye mti huu wa maarifa, basi wakati hawawezi kulifjua hilo zaidi tena, wao husema, “yote ni upuuzi.”
Sikilizeni, katika Jina la Bwana, sikilizeni: Wakati huwezi kujua zaidi, huo ndio wakati wa kuamini.
MKATE WA KILA SIKU
…Msiyale wala msiyaguse, msije mkafa. Mwanzo 3:3
25-0501
63-1128E – Ile Ishara
Wakati Mungu alipoanzisha kutoka katika Misri, kuita Israeli watoke kutoka Misri, kuelekea nchi Yake ya ahadi, hakukuwa na udhuru. Kila mtu ilibidi aweke damu hadharani.
Basi, leo hii, kutoka, ni kuitwa kutoka katika mifumo, kuingia ndani ya Bibi-arusi. Haijalishi ni kiasi gani ulivyo ndani ya mfumo, bado inahitaji ile Ishara ya Uhai wa Yesu Kristo tena. Hakuna kitu kingine kitakachofanya kazi. Bado Ishara inahitajika.
Kila mtu, haijalishi kama alikuwa ni mtu mwaminifu. Huenda alikuwa ndiye Farao wa Misri, naye alikuwa ndiye mtu muhimu kuliko wote wa siku hiyo, lakini ishara ilibidi kuwekwa kwake, haijalishi jinsi alivyokuwa muhimu. Kama ni askofu, kasisi, chochote kile, rais, mfalme, mwenye hekima, mtawala, hiyo haikuwa na uhusiano wowote nalo. Mungu alitambua tu watu wa agano waliokuwa na ishara.
MKATE WA KILA SIKU
Likumbukeni agano lake milele, Neno lile aliloviamuru vizazi elfu. 1 Mambo ya Nyakati 16:15
25-0430
59-0525 – Sura Za Kristo
Nimeambiwa, na mabingwa, kwamba…kabla hawajakuwa na siku za kiyeyushi, kutoa ma—takataka katika dhahabu, kutoa chuma na kimbwi. Kimbwi inafanana sana, na dhahabu halisi, hata inaitwa “dhahabu ya mjinga.” Lakini jinsi walivyotoa hayo yote, waliipiga kwa nyundo. Wahindi walikuwa wakifanya hivyo. Na wafua dhahabu wa kale walikuwa wakifanya hivyo, kuipiga kwa nyundo, na kuigeuza tena na tena, na kuipiga mpaka takataka yote ikatoka ndani yake.
Na njia pekee waliyojua ya kwamba ilikuwa imebaki tu dhahabu, ilikuwa ni wakati mpigaji aliweza kuona uakisi wake ndani yake. Yule ambaye alikuwa akipiga angeweza kuendelea kutazama, hadi karibu aweze kujinyoa, kwa uakisi wake katika dhahabu aliyokuwa akipiga.
Basi Roho Mtakatifu wa Mungu anapoanza kutupiga, kwa nyundo ya Injili, mpaka mambo yote ya ulimwengu yametolewa, nasi tunaweza kuakisi sura ya Bwana Mungu, ndipo ninaamini tunakuwa Wakristo. Maana, neno Mkristo linamaanisha “kama Kristo, na kumwakisi Yeye.”
MKATE WA KILA SIKU
Nami nitalileta fungu lile la tatu na kulipitisha kati ya moto, nami nitawasafisha kama fedha isafishwavyo, nami nitawajaribu kama dhahabu ijaribiwavyo; wataliitia jina langu, nami nitawasikia; mimi nitasema, Watu hawa ndio wangu; nao watasema, Bwana ndiye Mungu wangu. Zekaria 13:9
25-0429
61-0108 – Ufunuo, Mlango Wa Nne Sehemu Ya III
Adamu na Hawa walishona nguo nzuri tu kama Mmethodisti, Mbaptisti, Mpresbiteri, ama Mpentekoste yeyote angeweza kushona, iliufunika uchi wao. Lakini Mungu angeweza kuona kupitia hiyo, kwa hiyo akaua kitu fulani na kuzichukua hizo ngozi zilizokufa za—ngozi za mnyama aliyekufa na kuufunika. Ilibidi damu ichukue mahali pake. Hiyo iliizuia hasira Yake, Yeye aliiona hiyo damu ndipo akarudi nyuma, kwa sababu kitu fulani kilikuwa kimeumwaga uhai wake. Ee Mungu!
Wazia hilo! Kitu pekee kitakachomzuia Mungu ni Damu. Na kuna Damu moja tu ambayo itamfanya arudi nyuma, na hiyo ni Mwana Wake Mwenyewe. Akiona hiyo ni Damu ya Mwana Wake Mwenyewe, atarudi nyuma. Maana hiyo ndiyo karama ambayo…Mungu amempa Mwanawe, kuwakomboa wale aliowajua tangu zamani, nayo inamrudisha Mungu kutoka kwenye hukumu Yake. Lakini hiyo Damu ikiondolewa, na wote waliojulikana tangu zamani wameletwa wakaingia kwenye huo Mwili wa thamani, Kanisa Lake limefanywa tayari na kunyakuliwa, basi hasira ya Mungu iko juu ya watu.
Loo, ndugu, kamwe usipende kusimama hapo!
MKATE WA KILA SIKU
Kwa ajili hii Yesu naye, ili awatakase watu kwa damu yake mwenyewe, aliteswa nje ya lango. Waebrania 13:12
25-0428
61-0414 – Msiogope, Ni Mimi
Kwa nini tunabatiza? Maji hayatakuokoa, bali ni kutii tendo fulani. Kula ushirika hakutakuokoa, bali ni kufuata amri. Unaninii tu…
Kupigapiga madhabahuni hakutakuponya, kupigapiga madhabahuni hakutakuokoa, ungeweza kupigapiga madhabahuni mpaka ukaishiwa tu na pumzi na—na kufia pale, ungali ungekuwa hujaokoka, mpaka utakapokubali na kuamini ya kwamba Yesu alikufa badala yako, nawe umkubali kama Mwokozi wako binafsi. Kila mhudumu hapa ndani angeweza kuweka mikono juu ya kila mgonjwa hapa ndani, na kuomba tangu sasa, mpaka kesho kutwa usiku, kamwe kusingetukia lolote, mpaka utakapokubali yale Yesu aliyokufanyia. Kwa hiyo, basi haliko juu ya wahudumu, katika mmoja kwa mwingine, bali liko katika imani yetu binafsi katika kazi iliyomalizika ambayo Kristo alitufanyia pale Kalvari.
MKATE WA KILA SIKU
Ambaye kwa yeye tumepata kwa njia ya imani kuifikia neema hii ambayo mnasimama ndani yake; na kufurahi katika tumaini la utukufu wa Mungu. Warumi 5:2
25-0427
64-0619 – Anayeng’ang’ania
Silaha zote za Mungu ni mambo ya kimbinguni. Silaha za Mungu ni nini? Upendo, upendo ni nini? Hebu nithibitishie kisayansi kwamba kuna kitu kama upendo. Uko wapi? Ninyi, ni wangapi wanaopenda, inua mkono wako; unampenda mke wako, unampenda ndugu yako, unawapenda marafiki zako? Vema, ninataka mtu fulani, sayansi fulani, inithibitishie ni sehemu gani ya wewe ambayo ni upendo. Unaununua wapi, ni duka gani la dawa? Ninataka fungu lake, upendo. Furaha, je! una furaha? Amani, uvumilivu, upole, subira, ni kitu gani? Yote ni mambo ya kimbinguni.
Mungu ni wa mbinguni. Humthibitishi Mungu kisayansi. Unamwamini Mungu. Unaliamini. Usipoliamini, basi, mtu anayesema “kila kitu ambacho si cha kisayansi, si cha halisi, si kweli,” basi mtu huyo hawezi kuwa Mkristo. Inambidi kuamini. Kwa imani tunamwamini Mungu; sio kwa elimu, sio kwa theolojia. “Bali kwa imani unaokolewa.”
MKATE WA KILA SIKU
… Na kila tendo lisilotoka katika imani ni dhambi. Warumi 14:23
25-0426
60-0802 – El-Shaddai
Ugonjwa ni nini? Ugonjwa ni sifa ya dhambi. Kabla hatujawa na ugonjwa wowote, hatukuwa na dhambi. Dhambi huja kama matokeo ya ugonjwa, labda, si dhambi yako wewe, lakini dhambi ya wazazi wako. Kama vile tu ulivyoipewa wewe ulipozaliwa, na kadhalika.
Sasa, si lazima ufanye tu…Kama joka kubwa ama—ama mnyama kama simba, alikuwa amenasa makucha yake ubavuni mwangu, hiyo ilikuwa ni uvimbe ama kansa, na inajaribu kuniua. Hakuna haja ya kujaribu tu kukata mguu wake kwa ajili ya uponyaji wa Kiungu. Ukimpiga tu kichwani, inaua kitu hicho chote.
Na Yesu alipokufa kwa ajili ya dhambi, alikufa kwa ajili ya kila sifa ambayo dhambi iliwahi kuzaa. Unaona? Kwa hiyo dhambi ilipokwisha, yote yalikuwa yamekwisha, ule mpango kamili wa ukombozi. Kwa hiyo sisi ni…Ukimpiga tu kichwani kwa kesi ya dhambi, ukiua dhambi unaua kila sifa yake. Unaona?
Dhambi ni nini? Kutokuamini. Kwa hiyo unapoua kutokuamini kote, mbona, unajua ya kwamba Neno la Mungu ni sahihi, ya kwamba ni yeye yule jana, na hata milele, kwa hiyo ahadi zote ni zako. Tembea katika nchi hiyo, yote ni yako. Ni mali yako. Ifurahie tu; ni yako. Mungu alikupa.
MKATE WA KILA SIKU
… kama wasio na kitu, bali tu wenye vitu vyote. 2 Wakorintho 6:10
25-0425
53-0405S – Nendeni, Mkawaambie Wanafunzi Wangu
Ndipo nabii huyu alipoingia katika Roho, Mungu alianza kumwonyesha yale yatakayotukia; ya kwamba kungekuwa na Mtu ambaye angeiondoa dhambi ya ulimwengu, na angefufuka tena. Aliona ufufuo wa Bwana. Halafu, ninapenda hilo, ninapowazia. Alisema alisimama. Akajitikisa.
Alikuwa ameketi kwenye lundo la majivu. Jamani! Kile tunachokiita, siku hizi, mkosi mbaya ulikuwa umeipiga nyumba yake. Watoto wake wote waliuawa. Utajiri wake wote ulikuwa umetoweka. Afya yake ilikuwa imezorota. Yeye ameketi, Mkristo, ama mwaminio, ameketi, aliyeachwa. Mtu, hata kanisa lake, lilikuwa limempa kisogo. Yeye ameketi pale, akiyakwangua majipu yake.
Ndipo Roho wa Bwana alipomjilia, naye akauona huu ufufuo asubuhi ya leo, mnajua, alisimama, akasema, “Najua Mkombozi wangu yu hai, na siku za mwisho atasimama juu ya nchi. Na ingawa mabuu ya ngozi watauharibu mwili huu, hata hivyo katika mwili wangu nitamwona Mungu; Ambaye nitamwona mimi mwe-…” Alijua angemwona katika siku za mwisho, kwa sababu kutakuwa na ufufuo, ufufuo wa kiama.
MKATE WA KILA SIKU
Lakini mimi najua ya kuwa Mteteaji wangu yu hai, Na ya kuwa hatimaye atasimama juu ya nchi.
Na baada ya ngozi yangu kuharibiwa hivi, Lakini, pasipokuwa na mwili wangu nitamwona Mungu: Ayubu 19:25-26
25-0424
62-0408 – Kudhania
Lazima uwe na vita. Ikiwa kila kitu kinakuja kirahisi, kivivu, Mbona, wewe ni, una-unashinda kitu gani? Wanashinda kwa Neno la Mungu na ushuhuda wao, Damu ya Kristo.
Hamna budi kushinda kitu fulani, na yawabidi muwe na vizuizi fulani. Na watu walio tofauti, na wabishanao nanyi, na kuwaambia ninyi ni watakatifu wanaojifingirisha, na kadhalika, ninyi, ambayo yamewekwa mbele yenu, ni jaribio. Ikiwa hujapata hayo, basi hata hauko vitani.
Unajiunga na Kanisa kwa…? Kwa nini ulijiunga na Jeshi na kupata mafunzo? Kujikalia, kujiinua juu-chini mitaani na kujionyesha? Hivyo ndivyo baadhi ya Wakristo wanavyofanya, ambao tunataka kutazamwa. Hutatazamwa, watakushusha, “Kwa maana wote wapendao kuishi maisha ya utauwa katika Kristo Yesu wataudhiwa.” Twaa Upanga, kata uondoe kila kitu kutoka kwako, na uendelee kusonga mbele.
MKATE WA KILA SIKU
Piga vita vile vizuri vya imani; shika uzima ule wa milele ulioitiwa… 1 Timotheo 6:12
25-0423
63-1226 – Utaratibu Wa Kanisa
Sasa, sijaribu kuchukua mamlaka au kitu kama hicho, lakini, mwaona, mtu au cho chote kilicho na vichwa viwili, haki—hakijui jinsi ya kuenenda. Mungu hajapata kuwa na vichwa viwili kamwe kwa Kanisa Lake, Yeye hakufanya hivyo kamwe, ni kichwa kimoja. Yeye kila mara alitenda hivyo katika kila kizazi vile tumesoma Maandiko kote, kila mara kuna mtu mmoja ambaye Yeye humshughulikia. Kwa sababu ukiwa na watu wawili, una maoni mawili. Yapasa kuwe na uamuzi mmoja thabiti na wa mwisho, na uamuzi wangu wa mwisho ni Neno, Biblia. Kama mchungaji hapa wa kanisa, uamuzi wangu wa mwisho ni Neno, nami nataka…Najua ninyi ni Ndugu, mnanichukua mimi kama uamuzi wenu mkamilifu kwa yale…mradi ninamfuata Mungu kama Paulo alivyosema katika Maandiko, “Mnifuate mimi kama ninavyomfuata Kristo.”
MKATE WA KILA SIKU
Basi, nawasihi mnifuate mimi. 1 Wakorintho 4:16
25-0422
54-1024 – Dhambi Isiyosameheka
…lakini siku imewadia ambapo Nuru ya Injili inaangaza. Theolojia ya ka-…Makanisa ya Kikristo yanakufa. Yameshindwa. Mungu anakuchukua sasa, ili ajifunue Mwenyewe tena, kupitia Kanisa Lake, Mwili uliofufuka wa Bwana Yesu Kristo. Uliofufuliwa kutoka kwa ukanisa; uliofufuka kutoka kwa makanisa rasmi baridi; uliofufuka kutokana na ulokole. Mungu analeta fungu la mifupa na kuitia ngozi, katika Uweza wa Roho Mtakatifu utakaoleta Injili katika siku hizi za mwisho, pamoja na ishara na maajabu, hata mwisho wa dunia. Watafundisha Biblia. Watasimama Nayo. Wataishi kwa Hiyo. Hawatapatana, kulia wala kushoto. Kweli. Watasimama moja kwa moja kwenye Neno, na kusonga mbele. Naye Mungu atakuwa pamoja nao, kila siku, akilithibitisha Neno, kwa ishara na maajabu yanayofuata. Haleluya! Enyi nyote nyota za asubuhi, amkeni mkaangaze! Haleluya!
MKATE WA KILA SIKU
Ninyi ni nuru ya ulimwengu. Mji hauwezi kusitirika ukiwa juu ya mlima. Mathayo 5:14
25-0421
62-0603 – Uinjilisti Wa Wakati Wa Mwisho
Kila wakati umekuwa na ujumbe wake na wajumbe wake. Kote katika nyakati, kila wakati umeubeba ujumbe wake na mjumbe. Mungu, katika kila kipindi cha wakati, amemtuma mtu fulani aliyetiwa mafuta na Roho Mtakatifu, kuuleta Ujumbe Wake kwa ajili ya wakati huo, kila wakati.
Sasa, tungeweza kuanzia nyuma, kuliunga mkono kidogo tu. Hata tangu mwanzo, Mungu alikuwa ndiye Mjumbe hapo mwanzo, kuwaambia Adamu na Hawa, “Mtakula hili, bali hamtafanya hili.” Huo ulikuwa ndio Ujumbe. Ndipo mwanadamu alipouvuka Ujumbe wa wakati, ilisababisha mauti na machafuko kwa jamii yote ya binadamu. Sasa, hivyo ndivyo Ujumbe unavyomaanisha. Pia kumbukeni kwamba haikuwa ni kukanusha kinaganaga yale Mungu aliyosema, ambayo Hawa aliamini, ilikuwa ni kuchukua yale Mungu aliyosema na kuyapaka chokaa, ama—ama kuyafasiri vibaya kidogo tu, kuongeza kidogo tu Kwake, ama kuondoa kidogo kutoka Kwake.
Hiyo ndiyo sababu ninaamini ya kwamba Neno ni Kweli.
MKATE WA KILA SIKU
Kwa kuwa yeye aliyetumwa na Mungu huyanena maneno ya Mungu; kwa sababu hamtoi Roho kwa kipimo. Yohana 3:34
25-0420
62-0610E – Kushawishika Kisha Kuhusika
Nimeshawishika kwamba Yeye ni yeye yule jana, leo, na hata milele. Nimeshawishika, katika hii huduma na huu Ujumbe, ninaohubiri, nimeshawishika kwamba ni Kweli. Nimeshawishika ya kwamba maono haya yanatoka kwa Mungu. Nimeshawishika tunaishi katika siku za mwisho. Nimeshawishika ya kwamba Roho yuyu huyu aliye juu yangu ni Roho Mtakatifu. Utukufu!
Nimeshawishika kabisa. Nimeshawishika kwamba njia ya Roho Mtakatifu ni ya kweli. Nimeshawishika ya kwamba njia ya Biblia ni ya Kweli. Nimeshawishika ya kwamba Huyu ni Yesu Kristo hapa sasa. Nimeshawishika. Kama tukimwamini dakika hii, nimeshawishika kwamba Yeye angeponya kila mtu mgonjwa katika dakika moja, kufumba na kufumbua jicho. Nimeshawishika Yeye angemwaga Roho Mtakatifu juu ya mahali hapa, mpaka kungekuwako na kelele kubwa mno, hata ingekuwa ni vigumu kujua yale yangetukia.
Nimeshawishika. Ninaliamini kwa moyo wangu wote…
MKATE WA KILA SIKU
Yeye tu ndiye mwamba wangu na wokovu wangu, Ngome yangu, sitatikisika sana. Zaburi 62:6
25-0419
62-0401 – Hekima Dhidi Ya Imani
Kanisa la Mungu aliye hai, hapa na kwenye kanda, pia, mnajua mahali mnaposimama? Mnajua ya kwamba mliitwa na Mungu, ya kwamba Roho Mtakatifu anatawala moyoni mwenu, na kila Neno la Mungu ni halisi kwenu? Loo, ndugu! Shetani atawezaje kusimama dhidi ya hilo? Atawezaje kukomesha hilo lisikue? Atawezaje kuzizuia ishara hizo zisilifuate Hilo?
Mbona, ungeweza kuwatupa gerezani. Wao, kama ungeweza, sijali kile ufanyacho, wamekwisha lijaribu. Waliozea gerezani. Walilishwa kwa simba. Walikatwa kwa misumeno. Waliraruliwa vipandevipande. Huwezi kuliua Hilo, kweli, Kanisa ambalo limekusudiwa tangu zamani. “Wale aliotangulia kuwajua,” kama alivyofanya Yesu, “Yeye amewaita. Hao aliowaita, amewahesabia haki. Na wale aliokuwa amewahesabia haki, Yeye amewatukuza, kuwakusudia tangu zamani.”
Na sasa, katika siku za mwisho, huku kila mbegu imepandwa; kila kitu katika utaratibu, ulimwengu katika utaratibu wake, wakati umejipanga, Kanisa liko katika utaratibu Wake, Mbegu, Nuru za jioni, ishara za kama alivyosema, “Kama ilivyokuwa katika siku za Sodoma.” Malaika wa Mungu, Roho Mtakatifu, akishuka, akitenda kazi, akifanya ishara ambazo alizifanya wakati huo. Malaki 4 iliahidi Yeye atatuma, katika siku za mwisho, kile alichoahidi. Nasi tunaona hayo yote papa hapa. Wapi? Wapi?
Amina! Amina! Amina! Amina! Amina!
MKATE WA KILA SIKU
Kwa maana viumbe vyote pia vinatazamia kwa shauku nyingi kufunuliwa kwa wana wa Mungu. Warumi 8:19
25-0418
57-0516 Tunataka Kumwona Yesu
Mtu anapoongoka, macho yake yanaelekezwa Kalvari. Ikiwa ana wasiwasi kidogo tu, usipomtazama, ataenda upande wa ushupavu. Ikiwa yeye ni msomi kidogo tu, ataenda upande mgumu. Lakini moja kwa moja katikati ya njia kuna walio na akili timamu, wanaojielewa, waliozaliwa mara ya pili, waongozwao na Roho, Kanisa lenye majaliwa la Mungu aliye hai, likishuka moja kwa moja njiani kwenda kwa Kristo. Hilo ndilo la kweli linalotoka pande zote mbili. Mmoja alienda njia moja, na mmoja akaenda nyingine, akionyesha ushupavu wa dini au aidha msomi na mgumu sana kukunjwa. Wao wanajua zaidi kuhusu Neno kuliko wanavyojua kuhusu Mwandishi wake. Kulijua Neno si Uzima, bali kumjua Yeye ndio Uzima: kumjua Yeye. Huhitaji kuwa msomi; unatakiwa kuwa mtu aliyejisalimisha.
MKATE WA KILA SIKU
…msipogeuzwa na kuliacha tumaini la Injili mliyosikia habari zake, iliyohubiriwa katika viumbe vyote vilivyo chini ya mbingu… Wakolosai 1:23
25-0417
61-0428 – Kuingia Katika Roho
Sijali kama mtu huyo amekosea. Kama amekosea na ni mwaminifu moyoni mwake, nawe uko sawa katika imani yako na—nawe umekosea katika kutenda jinsi unavyotenda, afadhali niwe mahali pake kuliko kuwa mahali pako. Hiyo ni kweli. Afadhali nikosee katika fundisho langu, na niwe sawa moyoni mwangu, Mungu ataliheshimu zaidi.
Kwa hiyo kama mtu amekosea, vipi kuhusu hilo? Msaidie, anahitaji usaidizi, mpende. Kama huwezi kumpenda adui yako kama vile unavyowapenda wale wanaokupenda, wewe si bora kuliko watoza ushuru. Sawa. Hilo ndilo kanisa limeshindwa kupata. Natumaini mnalipata usiku wa leo, natumaini mnaona kile ninachozungumzia. Ni kurudi kwenye upendo, upendo wa ukombozi, mambo mengine yote ni sawa, lakini hatuna budi kurudi kwenye ushirika sisi kwa sisi.
Nao watu wanasema ya kwamba ninayashambulia madhehebu, siyashambulii, ninashambulia mfumo huo humo ndani ambao unavunja udugu, daima nimefanya hivyo, na daima nitafanya hivyo, hiyo ni kweli.
MKATE WA KILA SIKU
Lakini mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi. Mathayo 5:44
25-0416
62-1125M – Kushawishika Na Kisha Kuhusika
Kazi yangu ni kupanda Mbegu. Sijui zinaangukia wapi, lakini ninazipanda tu. Mungu anathibitisha. Popote inapoangukia, na kugonga namna hiyo, upesi inakuwa Hai ikiwa kwenye udongo mzuri. Ikiwa kwenye mwamba, siwezi kuisaidia. Msingi fulani wa kimadhehebu, siwezi kuisaidia. Jambo pekee, nitaendelea tu kupanda Mbegu. Najua Yeye yuaja. Ninaamini. Nataka kuishia hilo. Nimeshawishika kwamba anakuja. Nimeshawishika kwamba anakuja hivi karibuni. Nimeshawishika.
MKATE WA KILA SIKU
Na uje, Bwana Yesu Ufunuo 22:20
25-0415
58-0130 – Maandiko Ya Mkono Kwenye Ukuta
Unafanya nini? Kutangatanga tu huku na huko kwenye baa, na kuzunguka mahali pengine, kisha unashuka kwenye karamu ya roki, na unaelekea kwenye maskini kanisa baridi; na kumsikia mchungaji akihubiri juu ya jambo fulani. Loo, anatekenya sikio lako, hakika, bila shaka, jambo fulani tu; kwa sababu ni kupata riziki.
Kamwe hamkunikodisha kuja hapa, msingeweza kunifuta kazi, kwa sababu nimekodishwa na Mungu. Kweli. Hakuna askofu, wala askofu mkuu, wala hakuna kanisa linaloniambia nihubiri nini; ninamsikiliza Mungu, nina Ujumbe Wake, hivyo tu. Sichukui pesa zenu, sikuja kwa ajili ya pesa zenu, sitaki zozote.
Nimekuja kuwaonya, katika Jina la Kristo, jitayarisheni, saa hiyo imekaribia, na inaweza kuwa kabla ya asubuhi: mwisho wa wakati wa kanisa.
MKATE WA KILA SIKU
Tokea wakati huo Yesu alianza kuhubiri, na kusema, Tubuni; kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia. Mathayo 4:17
25-0414
63-0630M – Kutoka Kwa Tatu
Ninatumaini mtu wa rohoni anaweza kulishika hilo. Nina hakika mnalishika. Lakini sijui, huko nje. Kwa vyovyote vile, huwezi kutembelea kila taifa. Unaweza kutuma kanda huko. Mungu atakuwa na njia fulani ya kumshika mtu huyo huko nje ambako mbegu hiyo inapandwa. Kweli. Na mara Nuru itakapoigusa [Ndugu Branham anapiga makofi yake mara moja—Mh.], imetoka, imepata Uzima. Kama vile yule mwanamke pale kisimani, alisema, “Hilo hapo.” Akaishika.
MKATE WA KILA SIKU
Tena habari njema ya ufalme itahubiriwa katika ulimwengu wote, kuwa ushuhuda kwa mataifa yote; hapo ndipo ule mwisho utakapokuja. Mathayo 24:14
25-0412
50-0716 – Je! Unasadiki Hayo?
Kama ungewahi kujua Yesu ni Nani hasa, basi unaweza kuithamini dhabihu Yake kuu zaidi sana. Huna budi kumjua Yeye ni Nani, kwanza.
Yeye hakuwa tu mtu mtakatifu, au mtu mwema. Alikuwa Mwana wa Mungu. Hakuna mtu, hakuna Malaika, hakuna kitu kingine chochote ambacho kingeweza kupachukua mahali hapo ila Yeye. Naye alikuwa tayari kushuka kwa ajili yetu.
Na alipozaliwa, alizaliwa duniani hapa, na akaja kwa njia ya zizi la ng’ombe, naye akaondoka katika njia ya adhabu ya kifo. Na bado, sisi tunalalamika wakati mwingine kwa sababu tunapata majaribu na shida chache. Vema, angalia kile Yeye—kilichompata.
Unajua kwa nini Yeye alizaliwa katika zizi la ng’ombe? Kwa sababu Yeye alikuwa Mwana-Kondoo. Wana-kondoo hawazaliwi katika nyumba; wanazaliwa mabandani. Naye alikuwa…Je! uliona mpaka Kalvari, walimpeleka machinjoni. Hivyo ndivyo wanavyowafanya wana-kondoo. Wanawaongoza mbali. Alikuwa Mwana-Kondoo wa Mungu, aliyetolewa, aliyetolewa kwa ajili yetu, ili sisi wenye dhambi tupate kumkaribia Mungu kupitia Yeye.
MKATE WA KILA SIKU
…Astahili Mwana-Kondoo aliyechinjwa, kuupokea uweza na utajiri na hekima na nguvu na heshima na utukufu na baraka. Ufunuo 5:12
25-0410
63-1216 – Tumeiona Nyota Yake Na Tumekuja Kumsujudia
Pia wakati mwingine tunafikiria kwamba, mizigo yetu. Huenda nikaingiza hii papa hapa, kwamba, tunafikiria mizigo yetu ni mizito sana wakati mwingine, kwamba hakuna kitu kama huo ulimwenguni. Je! unajua kwamba mambo hayo yote ni mazuri kwako? Yote ni ya kukufinyanga wewe, kukuumba wewe. Manabii na wenye hekima walifinyangwa upande wa nyuma ya jangwa, kwenye jua kali, linalowaka, kupitia dhiki na majaribu, na mateso. Na mambo haya tuliyo nayo leo hii, hakuna kitu kilichotendeka kwetu ambacho hakijawahi kuwatendekea Wakristo wengine, hapo kabla. Wakristo wengine imewabidi kustahimili katika wakati wa giza kama huu, na hata kulishwa simba, kwa ajili ya ushuhuda wao.
MKATE WA KILA SIKU
Ili kwamba kujaribiwa kwa imani yenu, ambayo ina thamani kuu kuliko dhahabu ipoteayo, ijapokuwa hiyo hujaribiwa kwa moto, kuonekane kuwa kwenye sifa na utukufu na heshima, katika kufunuliwa kwake Yesu Kristo. 1 Petro 1:7
25-0409
56-1208 – Ibrahimu
Mungu ni Mungu wa vitu vya aina mbalimbali. Ana vilima vikubwa na vilima vidogo. Ana nyanda, mito, milima, maeneo yenye nyasi. Ana miti midogo, miti mikubwa, maua meupe, maua ya buluu, maua mekundu. Yeye ana…Yeye ni wa vitu vya aina mbalimbali na kwa watu Wake kuna aina mbalimbali; naye hufanya yote kwa uradhi wa mapenzi yake. Angalia a—angalia dunia. Unaweza kuona kile ambacho Mungu anapenda, na hivyo ndivyo itakavyokuwa katika ufufuo. Lo, ninayo furaha sana kwa jambo hilo, sivyo? Kuwazia kwamba siku moja tutamwona Yeye kama alivyo.
Mtu fulani alisema si muda mrefu uliopita, kasema, “Ndugu Branham, tutajua—je nitamjua mama yangu?”i
“Hautamjua mama yako tu, lakini utamjua kila mama. Utajua kila mtu.”
“Loo,” akasema, “sasa, huo ni upuzi.”
“Loo, la, la. Kwenye Mlima wa Kugeuzwa Sura, Petro, Yakobo na Yohana hawakuwa wamewahi kumwona Musa wala Eliya, lakini walipokuwa chini ya uvuvio huo, waliwatambua mara tu walipotokea nao hawakuwahi kuwaona.” Je! hiyo ni kweli? Lakini tutajuana mmoja kwa mwingine. Usijali kuhusu hilo, utalijua.
MKATE WA KILA SIKU
Yeye aliyemfufua Yesu katika wafu anakaa ndani yenu, yeye aliyemfufua Kristo Yesu katika wafu ataihuisha na miili yenu iliyo katika hali ya kufa, kwa Roho wake anayekaa ndani yenu. Warumi 8:11
25-0408
62-0909M – Kuhesabu Kinyumenyume
Roho Mtakatifu ni nguvu kwa ajili ya huduma. Kwa hiyo tunapozungumza kuhusu wewe huna budi kuzaliwa mara ya pili, na kulitumia hilo kwa Roho Mtakatifu, wengi wa Wamethodisti na kadhalika wamekosea hapo. Haiwezi. Haitaendana na Maandiko hapa. Unalifanya jambo hilo kwenda kombo. Haina budi kulichukua jinsi Maandiko yalivyoliweka hapa. Unaona? Na Roho Mtakatifu ni…“Utapokea Kuzaliwa upya baada ya hili”? Nini? Hapana. “Mtapokea nguvu,” Matendo 1:8, “baada ya huyu Roho Mtakatifu kuja juu yenu.” Unaona? Nao walikuwa tayari wameamini hata Uzima wa Milele, na kadhalika, lakini iliwabidi kuwa na Roho Mtakatifu kwa ajili ya nguvu. “Mtakuwa mashahidi Wangu baada ya Roho Mtakatifu kuwajilia juu yenu,” kwa sababu Roho Mtakatifu ni shahidi wa ufufuo, akionyesha kwamba umekuwa mtu mzima katika Kristo.
MKATE WA KILA SIKU
Ya kwamba injili yetu haikuwafikia katika maneno tu, bali na katika nguvu, na katika Roho Mtakatifu, na uthibitifu mwingi; 1 Wathesalonike 1:5
25-0407
63-0113M – Kutoa Presha
Wakristo, kutoka dhehebu moja hadi lingine, inaonyesha kwamba kamwe hawajapata kuja kwenye kimbilio hilo. Mnaona?
Wanaenda wakati mwingine kwenye seminari. Hilo ni sawa. Nao wanajifunza Neno vizuri tu wawezavyo. Wanakuja nyumbani, na kujaribu kuzungumza Neno hilo vizuri kadiri tu dhehebu lao linavyowaruhusu kulizungumzia. Na hilo ni zuri. Bali hilo silo. Sio kulijua Neno Lake, bali ni kumjua Yeye. Yeye! Mbona, hakika! Sio kiasi cha Neno ukijuacho, jinsi ulivyo na kanisa zuri, yale dhehebu letu linayomaanisha kwa ulimwengu, ni maachilio mangapi tuliyo nayo kwa hili, na ni ushirika kiasi gani tulio nao pamoja na ulimwengu, ni umati wa namna gani unaokuja. Ni wewe. Je, uko chini ya damu? Endapo wewe, kama mtu binafsi, sijali kama kila mmoja wa kusanyiko amekosea, wewe ungali salama. Uko chini ya Damu.
MKATE WA KILA SIKU
Kuwaogopa wanadamu huleta mtego; Bali amtumainiye Bwana atakuwa salama. Mithali 29:25
25-0406
65-1125 – Muungano Usioonekana Wa Bibi-Arusi Wa Kristo
Mungu mpendwa, tumeketi kwa kicho sasa, kweli hii ni siku ya kutoa shukrani, Bwana. Ninashukuru, Bwana, kwamba ninaishi katika siku hii. Hii ndiyo siku iliyo kuu sana. Mtume Paulo alitamani kuiona siku hii. Wale watu mashuhuri wa zamani walitamani kuiona. Manabii walitamani kuiona. Waliitazamia siku hii. Ibrahimu aliitazamia siku hii, kwa kuwa aliutafuta Mji ambao Mwenye Kuujenga na Mwenye Kuubuni alikuwa ni Mungu; unaning’inia moja kwa moja juu yetu, usiku wa leo. Yohana aliona Roho wa Mungu akishuka kutoka Mbinguni, alishuhudia, alijua ya kwamba huyo alikuwa ni Mwana wa Mungu. Na, wazia sasa, Yeye anamchagua Bibi-arusi Wake.
Mungu mpendwa, kote huko nje nchini, nena na moyo wao. Wewe ndiwe tu unayeweza kuubadilisha moyo wao. Kama hiyo haikuwa ni Mbegu iliyowekwa humo ndani hapo mwanzo, kamwe hawataliona, Bwana. Wao ni ninii tu…“Kipofu atamwongoza kipofu mwenziwe. Wataanguka shimoni,” hakika kabisa, kwa kuwa Neno Lako linasema wataanguka.
MKATE WA KILA SIKU
Ingieni malangoni mwake kwa kushukuru; Nyuani mwake kwa kusifu; Mshukuruni, lihimidini jina lake. Zaburi 100:4
25-0405
53-0611 Utuonyeshe Baba Itatutosha
Vema, wakati mauti yanapolipiga maskini ua, unaona linainamisha kichwa chake kidogo, kwa uchaji tu. Petali huanguka, na majani huanguka, na mbegu ndogo nyeusi huanguka. Kisha wana msafara wa mazishi. Mvua zinakuja na kulia katika masika ya mwaka na kumzika huyo jamaa mdogo.
Na kisha jambo la kwanza wajua kuganda huja. Labda hiyo mbegu ndogo imelala kwenye kina kirefu chini ya ardhi mahali ambapo mvua ya masika iliizika, halafu baada ya kitambo kidogo, kuona-…hali halisi ya baridi kali inakuja nako kunaganda. Kisha maskini mbegu ya kale inaganda. Ganda linapasuka, inatoka ndani yake. Mbegu inapasuka na kufunguka na nyama yake inatoka. Na kisha majira ya baridi yanaendelea kupitia dhoruba za theluji na tufani baada ya kimbunga.
Kisha baada ya kitambo karibu na Februari, mwisho wa Februari, Machi mwanzoni, bua limekwisha, uoto umetoweka, mbegu imetoweka, umbo limekwisha, petali imetoweka, ua limetoweka. Kila kitu kilichopo kimepita. Je, huo ndio mwisho wa ua hilo? La, bwana; acha tu jua hilo lianze kuipa dunia hiyo joto tena na ua hilo litaishi tena. Kwa nini? Kuna chembechembe ya uhai katika ua hilo ambayo hakuna mwanadamu anayeweza kuipata au hakuna msimu wa baridi unaoweza kuigandisha. Mungu ameliumba kwa njia Yake Mwenyewe, na hiyo chembechembe ndogo ya uhai imehifadhiwa katika ardhi hiyo, na ua hilo litaishi tena.
Vema, ikiwa Mungu aliweka njia ya ua kuishi tena, vipi kuhusu mtu aliyeumbwa kwa mfano Wake? Kuna njia mahali fulani kwa huyo kuishi tena.
MKATE WA KILA SIKU
Mtu akifa, je! Atakuwa hai tena? Mimi ningengoja siku zote za vita vyangu, Hata kufunguliwa kwangu kunifikilie. Ayubu 14:14
25-0404
62-1123 – Njia Ya Kurudi
Mungu daima amekuwa na watu mahali fulani ambao anaweza kuwaelekezea na kusema, “Ndivyo hivyo.” Loo, nataka kuwa miongoni mwa idadi hiyo. Nina hakika sote tunataka kuwa hapo, ndiyo shauku ya kila moyo. Tunataka kuwa miongoni mwa idadi hiyo ambayo Mungu anaweza kusema, “Hawa ni watu Wangu. Waangalieni, wao ni mfano wa kile nilicho Mimi. Wanaakisi Maisha Yangu katika yao, wamesalimisha maisha yao, nami ninaakisi Yangu, Maisha, kupitia kwa yao.” Ni jambo zuri jinsi gani! Ni…Jinsi hapana shaka inamfanya Mungu ajisikie vizuri kujua kwamba ana mtu anayeweza kumwamini…
MKATE WA KILA SIKU
…lakini upepo utawachukua; uvuvio tu utawachukulia mbali; lakini yeye anayenitumaini ataimiliki nchi, na kuurithi mlima wangu mtakatifu. Isaya 57:13
25-0403
53-0508 – Mungu Akimpa Agizo Musa
Sasa, unataka kuzungumza kuhusu jambo la kipuuzi, hebu na tuangalie tukishuka kilimani hapa sasa. Asubuhi moja ya kupendeza, jua linachomoza, ndege wakipiga miluzi, huyu hapa anakuja mzee, mwenye umri wa miaka themanini, masharubu yakiruka namna hii, na nywele nyeupe zikipeperuka nyuma yake, akimwongoza nyumbu mzee akiwa na mke aliyeketi juu akihangaika na mtoto kwenye kila nyonga, fimbo iliyopinda mkononi mwake. Huyu hapa anaenda.
“Unaenda wapi Musa?”
“Nashuka kwenda Misri kuiteka!” Uvamizi wa mtu mmoja, kwenda Misri. Mbona, Misri ingekuwa kama kwenda kule na kuiteka Urusi.
‘Vikosi bora zaidi vyenye mitambo vilikuwepo huko, lakini Mungu akamwambia,“Nitakutuma kule chini kuteka.”
“Vema, unamaanisha kwamba unaenda kuteka?”
“Hakika.”
“Kwanini? Kwa ninii yako…”
Naam, Mungu alisema hivyo. Hiyo ni kweli.
Unasema, “Utaiteka?”
“Hakika, tutaiteka sasa. Ni hayo tu. Mungu alisema hivyo.” Hiyo ni kweli. Maadamu Mungu alisema hivyo, amina. Hilo—hilo latosha.
Kama Mungu alisema hivyo, unaweza kulifanya hilo. Je! hiyo ni kweli? Vema, basi hebu na tuteke sasa hivi, na kumwambia Shetani, ya kwamba hatakuwa na uhusiano wowote nasi. Kila aliye mgonjwa ataponywa; kila jicho lililopofuka litafunguliwa; kila aliye kiziwi atasikia; kila ulimi ulio bubu utanena; kila mwenye dhambi ataanguka jukwaani na kuitoa mioyo yao kwa Kristo. Tunakwenda kuteka. Mnaona? Mungu tupe jambo hilo. Endelea mbele ukateke.
MKATE WA KILA SIKU
Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru. Luka 10:19
25-0402
55-1116 – Kuitwa Kwa Ibrahimu
Sasa, hiki hapa Mungu alichotufanyia katika Kristo. Mungu aliyedhihirishwa katika mwili, akamchukua Mwanawe Mwenyewe hadi Kalvari, na hapo akamwua Mwanawe Mwenyewe juu ya msalaba wa Kalvari kufanya agano na jamii ya binadamu. Na alipofanya hivyo, Yeye alimsulubisha msalabani, dhabihu iliyokufa, ilikuwa hivyo, na kumchomoa kutoka Kwake Roho Mtakatifu. “Mikononi Mwako naiweka Roho Yangu,” Damu ikitoka ubavuni Mwake, na mikono na miguu. Naye Mungu akachomoa Roho kutoka Kwake, na kuusukuma mwili chini kaburini, akaufufua siku ya tatu, na kuuweka kwenye mkono Wake wa kuume, na kulirudisha agano lililosalia kwa Kanisa, ambaye alikuwa ni Roho Mtakatifu yule yule aliyekuwa juu ya Kristo, akalishukia Kanisa. Na njia pekee ulimwenguni tutakayoweza kufaulu kwenye Siku ya Hukumu ni kwa Roho Mtakatifu yeye yule, aliyekuwa juu ya Yesu Kristo itabidi ashikamane, kama Mkewe katika Mwili. Amina.
MKATE WA KILA SIKU
Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. Yohana 3:16
25-0401
50-0115 – Je, Unasadiki Hayo?
Siku moja nilipokuwa na mkutano wangu wa kwanza na watu holiness. Nilikuwa huko St. Louis, nami nikakutana na Kasisi Robert Daugherty. Naye alikuwa katika mkutano wa hema. Nami nilienda kule usiku huo, naye msichana wake mdogo alikuwa ametoka kuponywa. Ushuhuda wake ulionekana pale.
Naye akanipeleka kwenye mkutano walipokuwa wakiufanyia. Alifika kule, naye akaanza kuhubiri, na ndio mara ya kwanza nilipopata kumsikia mhubiri wa Kipentekoste akihubiri. Mvulana huyo alihubiri mpaka magoti yake yakagongana pamoja. Alienda mpaka sakafuni, na akavuta pumzi. Ungeweza kumsikia ukiwa huko miraba miwili. Akija kuhubiri.
Mtu fulani akasema, “Je! wewe ni mhubiri?”
Nikasema, “La, bwana.” La, la. Njia zangu za kale za polepole za Kibaptisti hazifikiri jambo hilo haraka jinsi hiyo. Ni hayo tu. Ninaninii tu…sikuwa mhubiri basi baada ya kusikia jambo hilo. Kwa hiyo nilinyamaza tangu wakati huo na kuendelea nikiwa karibu na watu wa Full Gospel kuhusu mimi kuwa mhubiri. Nililiacha tu. Nikasema, “La, nitawaombea wagonjwa.” hebu iwe hivyo.
Lakini ninafurahia kuja siku hii namna hii, kujaribu kusoma baadhi ya Neno na kulifafanua vizuri nijuavyo; kwa sababu yote…ninaamini ya kwamba ni Kweli. Kila Neno la Mungu ni kweli.
MKATE WA KILA SIKU
…bali kwa kuidhihirisha iliyo kweli twajionyesha kuwa na haki, dhamiri za watu zikitushuhudia mbele za Mungu. 2 Wakorintho 4:2
25-0331
61-0218 – Zeri Katika Gileadi
Lakini kumbuka, ndugu, Ujumbe huo unapaswa kulitikisa taifa, ama, kulitikisa Kanisa. Usitafute jambo fulani kuu litakaloshuka kwenye kila ushoroba, Ujumbe wa Mungu utakuwa hasa kwa Kanisa lililochaguliwa. Ishara hizi na maajabu hazitafanyika kamwe mbele za ulimwengu, hazipaswi kufanywa.
Rais wa Kampuni ya Four Rose Whisky, mke wake alikuwa, yeye ni wa Muungano wa Wamishenari, naye alikuwa katika mmoja wa mikutano hiyo, alimwita Ndugu Bosworth, ambaye ulikuwa wa Muungano wa Wamisionari, na kusema, “Jambo lenyewe ni kwamba, hamwachi karama hiyo ianze kazi.” Kasema, “Nilichoona jana usiku kingetendeka katika miji mikuu, na kadhalika, ya taifa, mbona,” kasema, “ingeongoa, kuuleta ulimwengu mzima katika Ukristo.” Lakini unaona, hailikutumwa kwenye miji mikuu ya mataifa, unaona, linatumwa kwa Kanisa lililochaguliwa. Unaona, hamninii…
“Loo,” wao husema, “liandike jina lako kwenye tangazo kubwa sana, na vifikie vituo vikubwa mno, nenda kwenye televisheni.” Hili halikukusudiwa jambo hilo, Mimi nilitumwa tu kwenu ninyi, Kanisa, unaona, ndivyo ilivyo. Sasa, liamini Hilo kwa moyo wako wote.
MKATE WA KILA SIKU
Apate kujiletea Kanisa tukufu, lisilo na ila wala kunyanzi wala lo lote kama hayo; bali liwe takatifu lisilo na mawaa. Waefeso 5:27
25-0330
62-0610E – Kushawishika Kisha Kuhusika
Sasa, Biblia ilisema, “Katika siku za mwisho, mpinga Kristo atakuwa wa kidini sana, na kufanana sana na kitu kilicho halisi, hata ingewadanganya walio Wateule kama yamkini.” Lakini, haiwezekani. Hiyo ni kweli. Na, “Wote.” “Angewadanganya wote, walio juu ya nchi, ambao majina yao hayakuandikwa katika Kitabu cha Uzima cha Mwana-kondoo.” Tangu ule uamsho wa mwisho? Hilo halisikiki kama Biblia, sivyo? [Kusanyiko linasema, “La.”—Mh.] “Tangu kuwekwa msingi wa ulimwengu.” Hutawadanganya, maana wao wamekaa moja kwa moja katika Neno hilo. Wanapoyaona mambo hayo yakitokea, [Ndugu Branham anadata vidole vyake.] Ni Uzima, wanaushika sasa hivi.
Wengine watatembea huku na huku, wakisema, “Aa, hakuna kitu katika Hilo. Huh!” Mnaona? Hawajashawishika. Hakuna kitu pale cha kuwashawishi. Hakuna kitu ndani yao, cha kuaminia.
Mama alizoea kusema, “Unawezaje kupata damu kutoka kwa mboga nyekundu wakati hamna damu yoyote mle?” Kweli.
“Kondoo Wangu huisikia Sauti Yangu.” Wanalijua Neno. Sauti Yake ni nini? Hii hapa. Kanuni hizi za imani hawazifuati. “Bali, wanaisikia Sauti Yangu, wanaifuata.”
MKATE WA KILA SIKU
…na hao walio pamoja naye ndio walioitwa, na wateule, na waaminifu. Ufunuo 17:14
25-0329
61-0224 – Msiogope
Sasa, kumbukeni, kama Mungu akipata kuitwa jukwaani kutenda kazi, basi jinsi anavyotenda kwanza, hana budi kutenda kila wakati, baadaye, vivyo hivyo, la sivyo alikosea alipotenda kwanza. Kwa hiyo kama hiyo ilikuwa ndiyo njia ya kujitambulisha Mwenyewe katika siku hiyo kwa Wayahudi, na kwa Wasamaria waliokuwa wakimtazamia Masihi…
Hakuna Mmataifa aliyekuwa akimtazamia Masihi, tulikuwa Warumi na Wayunani, huku tukiabudu miungu ya chuma, felesi, marumaru, kama vile wengi wao wangali wanafanya, na—na namna hiyo, tukiwa na rungu mgongoni mwetu. Lakini sasa, baada ya miaka elfu mbili ya theolojia na mafundisho, sasa Kanisa la Mataifa, Kanisa teule, linamtazamia Masihi. Sasa, itambidi kutenda wakati atakapokuja wakati huu, kama tu alivyofanya wakati huo, itambidi kufanya mambo yale yale, maana Neno lilisema angefanya.
MKATE WA KILA SIKU
Kwa kuwa mimi, Bwana, sina kigeugeu… Malaki 3:6
25-0328
57-0308 – Mchungaji Mwema Wa Kondoo
Unajua, kuna Chakula kingi cha kondoo, na kuna chakula kingi ambacho ungewapa kondoo wako, ungewaua. Nami nina furaha sana ya kwamba Mungu alikuwa mwangalifu vya kutosha juu ya kondoo Wake kumpata Mchungaji anayefaa, Bwana Yesu, Yeye anajua Chakula cha kondoo ni kipi. Na Je, unajua Chakula cha kondoo ni nini? Ni Neno la Mungu. “Mtu hataishi…” Naomba nibadilishe hilo kidogo tu: “Kondoo hawataishi kwa mkate tu, bali kwa kila Neno litokalo katika kinywa cha Mungu.”
Kondoo wa Mungu wanalishwa na Neno la Mungu. Roho Mtakatifu ndani yako, anayekufanya kuwa kondoo, hula Neno kwa uthabiti, na Yeye hujilisha Neno peke yake. Chochote unachorusha bandani nje ya Neno, Yeye ataking’oa na kukitupa upande huo mwingine na kukiacha kikae pale.
MKATE WA KILA SIKU
Bwana ndiye mchungaji wangu, Sitapungukiwa na kitu. Zaburi 23:1
25-0327
62-0117 – Kudhania
Siku ya Pentekoste, walingojea mpaka wakapata mamlaka ya Kimaandiko. Hiyo ni kweli, kabla hawajadai chochote, walijua walikuwa nayo. Hawakusema—kusema, “Vema, ni—nilisikia mhemuko mdogo.” Waliihisi, wakaiona, chochote kile. Walijua walikuwa nayo. Waliiona ikitenda kazi ndani yao, ikitenda kazi ndani yao, ikizungumza kupitia kwao, kila kitu. Ilikuwa pale. Haikuwabidi kudhania chochote. Ilikuwa pale, ikijielezea.
Na mtu, anapozaliwa mara ya pili kwa Roho wa Mungu, ni jambo lile lile leo. Hudhanii.
“Ni—ninaamini tunampokea Roho Mtakatifu tunapoamini.” La. Hamkumpokea. Hamumpo-…Wengine, mngeweza kumpokea. Lakini kwa sababu tu ati uliamini, kama Mungu hakukujaza na Roho Mtakatifu, basi Yeye hajakuthibitisha bado. Hujampata. Unaona? Hiyo ni kweli.
Usidhanie unaye. Kuwa na hakika na kitu hicho. Hutaki kubahatisha juu ya jambo hilo, la, maana utapotea. Usibahatishe tu. Kaa tu, nenda, kaa mpaka jambo hilo limetimizwa kwako.
MKATE WA KILA SIKU
Jijaribuni wenyewe kwamba mmekuwa katika imani; jithibitisheni wenyewe. 2 Wakorintho 13:5
25-0326
59-1220M – Kongamano Pamoja Na Mungu
Yeye akawaambia wanafunzi Wake, wachovu, walikuwa na mikutano mingi mikubwa, walikuwa wamechoka, labda kama mlivyo asubuhi ya leo. Lakini Yeye akasema, “Mtakesha nami tu yapata saa moja? Kwa kuwa inanibidi kwenda huko na kufanya kongamano. Inanibidi kwenda peke Yangu.” Ndipo wakati wao…
Kongamano liliwekwa. Naye Mwana-Kondoo, mdogo, maisha mazuri, kamwe hakuna maisha kama hayo. Kamwe hapakuwapo, kamwe hapatakuwapo, maisha kama hayo aliyokuwa nayo Mwana-Kondoo. Lakini sasa Baba alisema, “Uko tayari? Upendo Wako kwa ndugu Zako ni mkubwa vya kutosha? Je, upendo Wako kwa ulimwengu huo wenye dhambi ulimozaliwa, unaonuka, hivi unawapenda vya kutosha kuachilia maisha Yako? Unawapenda vya kutosha kupachukua mahali pao, kuzibeba dhambi zao, kwa mauti magumu sana, yaliyo muhimu sana?” Ninyi…Hakuna kitu kingaliweza kufa kifo cha namna hiyo ila Yeye.
Na katika kongamano hilo, uamuzi kama huo ulifanywa, mpaka Damu ikaanguka kutoka usoni Mwake. Alikuwa na majaribu. Dhambi za ulimwengu zilikuwa juu Yake. Halafu akaangalia usoni mwa Hua, na kusema, “Si mapenzi Yangu, bali mapenzi Yako yafanyike.”
MKATE WA KILA SIKU
Akaendelea mbele kidogo, akaanguka kifulifuli, akaomba, akisema, Baba yangu, ikiwezekana, kikombe hiki kiniepuke; walakini si kama nitakavyo mimi, bali kama utakavyo wewe. Mathayo 26:39
25-0325
61-0207 – Matarajio
Simeoni, huyu mtakatifu mkuu wa kale wa Mungu, alikuwa mtu mwenye sifa kuu.
Loo, leo hawana budi kusema, “Lakini ngoja kidogo, bwana, mimi ni mfanyabiashara. Mimi ni daktari. Mimi—mimi ni profesa.” Wewe si bora kuliko mtu mwingine yeyote. Na wakati wowote unapofikiri kuwa wewe ni bora kuliko mtu mwingine, basi wewe si chochote kile unachopaswa kuwa, Maandiko yanasema. Unaona?
Unapofika mahali…Huna budi…Mnawezaje kuwa na imani wakati mnatazamia kuheshimiwa, mmoja kwa mwingine? Unaona? Hamna budi kuwatanguliza wengine ninyi kwa ninyi, siku zote, hayo ndio maisha ya Kristo, kumtanguliza ndugu yako, dada. Na kama wamekosea, hiyo ni sawa, kamwe hutawafanya kuwa bora zaidi kwa kuwapiga teke kando,mkumbatie, mwinue.
Ninaipenda dini hii ya mtindo wa kale, ninawaambia kile hiyo itakalofanya, ita-itaifanya mwenye suti maridadi kuketi na wa ovaroli, na kupeana mkono, na kuitana ndugu, hiyo ni kweli; itafanya mwenye mavazi ya kaliki na hariri kuitana dada. Hakika itafanya hivyo. Ni pipa la mtutu wa bunduki moja kwa moja, na anga la bluu, nayo bila shaka itafanya hivyo.
MKATE WA KILA SIKU
Kwa pendo la udugu, mpendane ninyi kwa ninyi; kwa heshima mkiwatanguliza wenzenu; Warumi 12:10
25-0324
59-0628E – Maswali na Majibu
Ni…Mungu ana wakati mgumu kujaribu kumpata mtu fulani ambaye Yeye aweza kumshughulikia, atakayedumu mnyenyekevu, na mpole, na akae mahali pale hadi Mungu amwite akafanye kitu fulani (mwaamini hilo? Ona?), mtu ambaye Mungu aweza kumbariki naye bado atadumu mwenyewe mtu, si kuwa malaika wala Mungu. Mara tu mtu abarikiwapo na ana kitu fulani kidogo alichopewa, yeye ataka kuwa mungu; yeye ataka kuwa ma—malaika. Yeye ataka kuwa mtu mkuu. “Kile nifanyacho, kile…Mimi na mimi na vyangu…” hayo yote. Hiyo ni nia mbaya. Mungu anamtafuta mtu ambaye Yeye angembariki na kumumwagia baraka, na—na jinsi anavyombariki ndivyo mtu huyo anavyozidi kuwa mdogo.
Na hutapata zaidi ya Mungu hadi uwe si kitu. Yakubidi ujifanye mwenyewe mdogo. Yeye ajikwezaye, Mungu atamdhili. Yeye ajidhiliye, Mungu atamkweza. Huna budi kuwa mdogo kabla hujawa mkubwa. Na hutakuwa kamwe mkubwa kwa nafsi yako; utakuwa tu mkubwa kadiri Mungu atakavyokuwa mkubwa ndani yako. Ona?
MKATE WA KILA SIKU
Na ye yote atakayejikweza, atadhiliwa; na ye yote atakayejidhili, atakwezwa. Mathayo 23:12
25-0323
63-0119 – Mapito Ya Nabii Wa Kweli
Biblia ilisema, “Wakati Mungu…Simba akinguruma, ni nani asiyeweza kuogopa? Basi Mungu anaponena, tunawezaje kukosa kutabiri?” Tunaweza kujiepusha nako? Mungu anaponena, nabii hulitangaza Neno lililonenwa kwa sauti. Na kama ni Neno la Mungu…
Naye simba anaponguruma; mende, kila kitu, hutulia, kwa sababu wanaogopa. Mfalme wa—wa—wao a—anazungumza. Wanayo a—akili ya kutosha, ujasiri, na heshima ya kutosha, kumheshimu mfalme wao anaponena.
Kwa hiyo, Mungu hunena kwa Neno Lake, basi kila kiumbe cha uumbaji Wake na kitilie maanani. Yeye ananena katika siku hizi za mwisho.
MKATE WA KILA SIKU
Acheni, mjue ya kuwa Mimi ni Mungu, Nitakuzwa katika mataifa, nitakuzwa katika nchi. Zaburi 46
25-0322
63-0825E – Imani Kamilifu
Na tulipokuwa wenye dhambi, tumefarikishwa, bila Mungu; duniani, katika takataka za matope, kama nilivyonena asubuhi ya leo, Mungu akatujia! Mungu alikutafuta wewe, wewe haukumtafuta Mungu. “Hamna mtu awezaye kuja kwangu asipovutwa na Baba Yangu kwanza.” Naye Mungu akashuka katika takataka hiyo, jinsi ulivyokuwa, na kukutafuta hata akakutoa! Hiyo inapaswa kuumba Upendo Mkamilifu. Tazama ulivyokuwa, na tazama ulivyo. Nini ilisababisha hilo? Mtu fulani aliyekupenda! Je, huwezi kuwa na imani katika yale aliyokuahidi, basi? Upendo halisi na dhahiri utaumba matumaini katika Neno Lake.
MKATE WA KILA SIKU
Nami maombi yangu nakuomba Wewe, Bwana, Wakati ukupendezao; Ee Mungu, Kwa wingi wa fadhili zako unijibu, Katika kweli ya wokovu wako.
Uniponye kwa kunitoa matopeni, Wala usiniache nikazama. Na niponywe nao wanaonichukia, Na katika vilindi vya maji.
Zaburi 69:13-14
25-0321
63-1114 – Ushawishi
Jambo ni kwamba, watu, ndugu yangu, dada, na marafiki, ni kutambua udogo wako. Unaona? Usione jinsi ulivyo mkubwa. Tambua jinsi ulivyo mdogo. Wewe ni—wewe ni mdogo. Sote tuko hivyo. Mungu anaweza kufanya bila ya sisi, bali sisi hatuwezi bila Yeye. Unaona? Unaona? Sisi, sisi hatuwezi bila Yeye, lakini Yeye anaweza bila ya sisi.
Mungu anajaribu tu kumpata mtu mmoja ambaye Yeye anaweza kumshika mikononi Mwake. Daima amejaribu kufanya hivyo. Unatambua, kote katika Biblia, wakati Yeye alipompata Isaya, wakati Yeye alipompata Yeremia. Na Yeye alimpata—Yeye alimpata Samsoni, siku moja; bali Samsoni alimpatia Mungu nguvu zake, lakini akampa Delila moyo wake. Unaona, yeye…
Inakubidi kutoa yote uliyo nayo kwa Mungu; kicho chako, heshima zako, kila kitu ulicho wewe. Usiwe chochote, uone tu jinsi ulivyo mdogo, na hilo ndilo Mungu anatutaka tufanye.
MKATE WA KILA SIKU
Maana sijui sababu ya kujishitaki nafsi yangu… 1 Wakorintho 4:4
25-0320
57-1222 – Mwanga Mkuu Unaong’aa
Uliposema, “Mlima, ng’oka,” na ungali umesimama pale, unasema, “Vema, haikutukia”? Loo, kweli ilitendeka. Uliposema, “Ewe mlima, ng’oka,” labda chembe moja ya mchanga isiyo na maana iliachilia, toka kwa mamia ya mabilioni na mabilioni ya tani. Chembe moja ndogo ilisogea, lakini limeanza kutukia. Shikilia imani hiyo na uuangalie huo mlima ukitoweka. Hakika.
Utasema moyoni mwako, “Ewe ugonjwa, ondoka kwa mtoto wangu. Ewe ugonjwa, toka katika mwili wangu, katika Jina la Bwana Yesu,” na usione shaka. Papo hapo zile chembechembe zenye afya zinatwaa silaha na zana mpya za vita, na adui anaanza kurudi nyuma.
Yeye ameshindwa kwa sababu Kristo, katika kunywa manemane Yake pale Kalvari, alimshinda Ibilisi na kila moja ya nguvu zake. Kisha akamvua kila kitu alichokuwa nacho, naye si kitu ila ni laghai tu; anaweza kumaliza nayo, atafanya hivyo.
MKATE WA KILA SIKU
Wala halitakuwako neno lisilowezekana kwenu. Mathayo 17:20
25-0319
60-1211M – Wale Wanawali Kumi, Na Wayahudi Mia Na Arobaini Na Nne Elfu
Yeye hakumkasirisha. Yale Bwana alisema yatendwe, Henoko aliyatenda. Sasa, yeye alikuwa ni mfano, kumbukeni. Safina ni mfano wa Wayahudi, wale mia na arobaini na nne elfu waliobebwa, ambao ni Nuhu na kundi lake; bali Henoko alienda Nyumbani muda kidogo tu kabla ya ile gharika. Mnajua hilo. Kwa hiyo Henoko aliendelea tu kutembea Nuruni. Kwa hiyo siku moja aliihisi miguu yake ikiondoka ardhini, akaendelea tu kutembea, ndipo akatembea akaingia Utukufuni pasipo hata kufa. Hiyo ni kweli. Mungu alimchukua kwa sababu alikuwa akitembea katika Nuru, akiwa na ushuhuda ya kwamba “yeye alitembea katika Nuru ya Mungu.” Akaendelea kutembea, kutembea.
Hebu tuvae viatu vyetu vya kutembea, enyi Kanisa:
Tuendelee kutembea Nuruni, Nuru nzuri,
Huja ambapo matone ya umande wa rehema yanang’aa;
Tuangazie kote mchana na usiku,
Yesu, Nuru ya ulimwengu.
Hebu tuuimbe sasa:
Tutatembea Nuruni, Nuru nzuri,
Loo, njoo ambapo matone ya umande wa rehema yanang’aa;
Tuangazie kote mchana na usiku,
Yesu, Nuru ya ulimwengu.
Enyi watakatifu wote wa Nuru tangazeni,
Yesu, Nuru ya ulimwengu;
Ndipo kengele za Mbinguni zitalia,
Yesu, Nuru ya ulimwengu.
Tutatembea Nuruni, Nuru nzuri sana,
Loo, njoo ambapo matone ya umande wa neema yanang’aa;
Tuangazie kote mchana na usiku,
Loo, Yesu, Nuru ya ulimwengu.
MKATE WA KILA SIKU
Henoko akaenda pamoja na Mungu, naye akatoweka, maana Mungu alimtwaa. Mwanzo 5:24
25-0318
62-0128A – Kitendawili
Ni ajabu kwamba alichagua kundi la watu wasio na elimu, na kuwatuma huko juu pamoja na agizo huko Pentekoste, si kwenda kwenye seminari fulani, bali wangoje hata watakapovikwa Uwezo utokao Juu. Kama mtu huyo, Petro, na Yohana na hao wengine, walitaka kuhubiri nao walikuwa wasio na elimu wala maarifa, inaonekana kama angeninii, angesema, “Enyi vijana, kuna shule nzuri papa hapa, nendeni mpaka mtakapojifunza ABC zenu, ndipo baada ya kufanya hivyo, mtaingia shule yenu ya sekondari, mpate yote, hayo yote, ndipo mtachukua miaka minne ya shule ya upili, kisha miaka minne ya chuoni, halafu yapata miaka minne au mitano ya Shule ya Biblia, ndipo mnaweza kutoka nje.”
Lakini Yeye alisema, “Ngojeni katika mji wa Yerusalemu, kwa maana nitawaletea juu yenu ahadi ya Baba. Ndipo mtakuwa mashahidi Wangu,” Luka 24:49, “mashahidi Wangu katika Yerusalemu, Uyahudi, Samaria, na hata pande za mwisho za dunia.” Hayo yangali ndiyo matakwa Yake.
MKATE WA KILA SIKU
Na tazama, nawaletea juu yenu ahadi ya Baba yangu; lakini kaeni humu mjini, hata mvikwe uwezo utokao juu. Luka 24:49
25-0317
61-0205M – Tarajio
Dhehebu fulani, hivi majuzi, kwa sababu kwamba nilimruhusu mhudumu mwingine aketi jukwaani ambaye hakuwa mfuasi wa shirika lao, yeye alisema, “Tumechora mstari. Tumekuweka nje yake, Ndugu Branham, nje ya—nje ya kundi letu.”
Nikasema, “Ninachora mwingine, mkubwa sana, kuwarudisha ndani tena.” Nikasema, “Kwa hiyo ha—hamwezi kunilazimisha nitoke nje.” Hiyo ni kweli. “Nitachora mstari moja kwa moja juu ya huo wenu na kuwaingiza ndani moja kwa moja.” Mnaona?
Hiyo ni kwa ajili ya…Sisi ni ndugu. “Hatujagawanyika; sisi sote ni mwili mmoja.” Kweli. Sisi ni Wakristo, waliozaliwa kwa Roho Wake, tukaoshwa kwa Damu Yake. Sisi ni Wakristo. Inatupasa kutenda kama Wakristo; inatupasa kuenenda kama Wakristo. Wanaume na wanawake, hebu niwaambie hilo ni jambo moja sisi, kanisa limepungukiwa nalo siku hizi, ni kuenenda kama Wakristo.
MKATE WA KILA SIKU
Na kama mnavyotaka watu wawatendee ninyi, watendeeni vivyo hivyo. Luka 6:31
25-0316
57-0818 – Kumbukumbu Za Mungu Zilizojaribiwa Na Wakati
Naye Yesu Kristo alikuja kutoka Mbinguni, Utukufuni; kutoka Utukufuni, akashuka huku, kujenga Kanisa. Na nyenzo ambazo Yeye anaweka ndani Yake, ni nyenzo zilizojaribiwa na wakati. Unaweza kuja madhabahuni na kufanya maungamo, lakini Yeye anapopata mashimo yaliyotobolewa na hewa na kadhalika, unaona, ulimwengu—ulimwengu umekupulizia na kuingiza funza ndani yako, na kadhalika, huwezi kusimama. Anakusukuma tu upande mmoja. Mungu anataka Kanisa lililojaribiwa na wakati; si mtu
ambaye ni Mkristo leo na kesho amerudi nyuma, kuingia na kutoka, na huku na huko. Hawezi kukuweka popote.
Bali ana Kanisa lililojaribiwa, likapitia majaribuni, katika hasara, katika maradhi, katika huzuni, katika kifo, na bado linasimama na ushuhuda. Huyo ndiye mtu, naam, huyo ndiye mtu Yeye anamtafuta. Sijali kama wewe ni ombaomba. Sijali kama wewe ni mwombaji. Sijali kama wewe ni mwokota-matambara. Chochote ulicho, Mungu anakuwekea jaribio. Anatafuta nyenzo zilizojaribiwa na wakati.
MKATE WA KILA SIKU
Umenijaribu moyo wangu, umenijilia usiku, Umenihakikisha usione neno; Nimenuia kinywa changu kisikose, Zaburi 17:3
25-0313
25-0312
64-0312 – Macho Yao Yalipofumbuliwa, Walimtambua
…mabomu ya atomiki na makombora na kadhalika, kwa ajili ya ulimwengu wote.
Wachekeshaji kwenye televisheni, na kusema, na—na redio na kadhalika, wanapiga mbinja na kuimba, na kufanya mizaha michafu, na kutamka maneno machafu na mambo mabaya ambayo hata hayafai kuruhusiwa, na magazeti na kadhalika yamejazwa kabisa wanawake walio uchi, wazinifu, kila kitu, wakijaribu kuridhisha moyo, kujaribu kukutuliza. Inanikumbusha kuhusu mvulana mdogo akipiga mbinja gizani, akipitia makaburini, akijaribu kujifanya afikirie kuwa si mwoga. Umetishwa kabisa, na unajua hilo. Unajua hukumu inakungojea, na inakuja kwa sababu umemkufuru Roho Mtakatifu, nawe umemkataa Yesu Kristo aliyefufuka. Kweli kabisa. Macho yao yamefumbwa. Hawajui.
MKATE WA KILA SIKU
Mimi nalisema nawe wakati wa kufanikiwa kwako; lakini ulisema, Sitaki kusikia. Hii ndiyo iliyokuwa desturi yako tangu ujana wako, kutokuitii sauti yangu. Yeremia 22:21
25-0311
64-0306 – Aliye Mkuu Kuliko Sulemani Yupo Hapa Sasa
Na sasa tunaona ya kwamba yule mpinga-Kristo, katika siku ya mwisho, “atawadanganya wote wakaao juu ya nchi, ambao majina yao hayakuandikwa katika Kitabu cha Uzima cha Mwana-Kondoo tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu.” Jina lako liliwekwa katika Kitabu cha Mungu kabla Mwana-Kondoo hajachinjwa. Wakati mpango Wake ulipoamuriwa, kila kitu, wewe ulitambuliwa katika mpango huo kwa sababu una Uzima wa Milele. Neno Milele, haikuwa na mwanzo na wala haiwezi kukoma, nawe ni sifa za mawazo ya Mungu kabla ulimwengu haujaumbwa. Hiyo ndiyo njia ya pekee ya kupata Uzima wa Milele. Na Uzima huo, ambao Yeye alikuwa akikufikiria, umo ndani yako sasa. Hakuna njia ya kuutenganisha. Unakaa hapo ndani.
MKATE WA KILA SIKU
Nami nawapa uzima wa milele; wala hawatapotea kamwe; wala hakuna mtu atakayewapokonya katika mkono wangu. Yohana 10:28
25-0310
63-0803E – Ushawishi
Nikimwona mtu akitembea, kijana mwenye sura nzuri, katika miaka michache, tazama nywele zake zikigeuka kuwa mvi na kung’oka, mabega yake yanainama. Kijana mwanamke mrembo amesimama, mwenye uso wa kitawa, mcha Mungu, akisimama na kumsifu Mungu; nami narudi katika muda wa miaka michache na kumkuta ana mabega yaliyoinama, huku amebeba watoto wawili watatu. Vema, jamani, pale, inaonyesha ya kwamba katika mwili huo mna mauti. Haidhuru ni mzuri vipi na unaonekana mrembo vipi, ungali una mauti ndani yake.
Basi natazama kule hiyo roho mle ndani inakoegemea. Ikiwa daima inawakilisha Nuru, inanena kuhusu Nuru, inazungumza habari za Nuru, itaambatana na Nuru. Bali kama kila mara iko upande ule mwingine, wa dunia, wa mambo ya ulimwengu, inashawishiwa na ulimwengu, hamna lingine ila kwake kuingia gizani inapokufa, kuingia katika giza la nje. Kwa hivyo unaona, tulivyo sisi, hatuna budi kukumbuka ya kwamba sisi tuko jinsi tulivyo kwa neema ya Mungu, na hamna mmoja wetu anayeweza kujivunia hayo. Tunaweza tu kuinama katika kusujudu na kwa unyenyekevu, mbele za Mungu, na kumshukuru kwa wema Wake.
MKATE WA KILA SIKU
Na rehema zake hudumu vizazi hata vizazi Kwa hao wanaomcha. Luka 1:50
25-0309
57-0420 – Kuzikwa
Na kila kitu duniani, uzuri, utamu, uzuri wa dunia, si kitu kingine ulimwenguni ila ni jibu la kilicho bora kuliko hicho, ambacho kinatungojea tunapouacha ulimwengu huu.
Kwa maana, kila kitu duniani ni mfano tu wa kile kilicho Mbinguni. Kila kitu kizuri, kila kitu ambacho ni cha haki, kila kitu kinachovutia, miti, ndege, kila kitu, ni mfano tu wa kile kilicho Mbinguni.
Maisha yetu yenyewe ni mfano tu. Ni kivuli tu, wala sio kitu halisi. Ni upande hasi. Inahitaji kifo kuisafisha hiyo picha, kuturudisha katika thiofania tulimotoka.
Ndipo katika ufufuo tunakuja katika sura Yake, mwili uliofufuliwa. Ni mzuri jinsi gani; sio tu mzuri, bali ni halisi, Ukweli mnyofu wa Neno la Mungu la Milele, kwamba tutakuwa kama Yeye.
MKATE WA KILA SIKU
Basi, mtamlinganisha Mungu na nani? Au mtamfananisha na mfano wa namna gani? Isaya 40:18
25-0308
57-0908E – Waebrania, Mlango Wa Sita #2
Sasa, kama umeokolewa, umeokolewa. Kama Mungu akikuokoa usiku wa leo, akijua atakupoteza miaka kumi kuanzia leo hii, Yeye anavunja kusudi Lake Mwenyewe; asiye na kikomo, Mwenyezi, wa Milele, hekima ya milele, Mungu, hajui vya kutosha basi kujua kama wewe utashikilia ama kama hutashikilia. Basi, wakati anapokuokoa, unasema, “Vema, nitajaribu kumthibitisha. Nitaona atakachofanya,” basi Yeye hajui mwisho tokea mwanzo. Mungu anajua anachofanya, kamwe usiwe na wasiwasi juu ya jambo hilo. Ni wewe na mimi tunaoenda tukijikwaa-kwaa. Mungu anajua anachofanya. Naye alijua sisi…kama tungeweza kushikilia, ama kile tungalifanya.
Sasa, Biblia ilisema ya kwamba, Esau na Yakobo, kabla hata mmoja wa hao watoto kuzaliwa, Mungu alisema, “Ninampenda mmoja, na namchukia huyo mwingine,” kabla hata hawajapumua pumzi yao ya kwanza, kusudi uteule Wake ubakie kuwa ni wa kweli.
MKATE WA KILA SIKU
Si kwa sababu ya matendo ya haki tuliyoyatenda sisi; bali kwa rehema yake, kwa kuoshwa kwa kuzaliwa kwa pili na kufanywa upya na Roho Mtakatifu; Tito 3:5
25-0307
61-0217 – Alama Ya Mnyama Na Muhuri Wa Mungu #2
Loo, ni Muhuri wa Roho Mtakatifu, ndugu, huo ndio Muhuri wa Mungu. Hiyo ni kweli, kutia muhuri.
Sasa, Wayahudi ndio wanaofuata kuupokea. Wapentekoste wamekuwa nao, Wamethodisti, Wabaptisti, hao wote wametoka katika madhehebu mbalimbali wameketi papa hapa usiku wa leo. Mimi mwenyewe ni Mbaptisti, ama nilikuwa, ningali Mbaptisti, bali mimi ni Mpentekoste aliye Mbaptisti mwenye Roho Mtakatifu. Mimi ni Mnazarayo-Mpentekoste-Mpresbiteri-Mbaptisti. Loo, unajua ninachomaanisha, yote katika hilo. Ni kitu gani, ni Roho Mtakatifu, ndiye aliyeleta tofauti, huyo ndiye aliyenitia muhuri katika Ufalme wa Mungu.
Huyo ndiye aliyemtia muhuri kila Mmethodisti, kila Mkatoliki, kila Mpresbiteri. Sisi sote ni wanadamu, na kwa Roho mmoja, sisi sote hatujaungana katika kanisa moja, sote kupeana mkono kumoja tumeingizwa, maji moja, bali kwa Roho mmoja sisi sote tunabatizwa kuwa Mwili mmoja kwa Roho Mtakatifu, na kutiwa muhuri mpaka Siku ya ukombozi wetu. Amina. Huyo ndiye Roho Mtakatifu.
MKATE WA KILA SIKU
Kwa maana katika Roho mmoja sisi sote tulibatizwa kuwa mwili mmoja, kwamba tu Wayahudi, au kwamba tu Wayunani; ikiwa tu watumwa au ikiwa tu huru; nasi sote tulinyweshwa Roho mmoja. 1 Wakorintho 12:13
25-0306
55-1006A – Maisha Yaliyofichwa
Je! umewahi kufika mahali katika maisha ambapo Kristo alimaanisha mengi kwako kuliko mabishano yote unayoweza kufanya kuhusu kanisa lako? Je! Kristo anamaanisha zaidi kwako kuliko ulimwengu wote? Simaanishi kutoka kwenye mhemko au kazi ya kiakili; Ninamaanisha kutoka katika kilindi cha moyo wako, ya kwamba jambo fulani limetulia mle, kwamba jambo fulani limetukia, ambalo hujui jinsi lilivyokuja, bali umefichwa, na nia yako yote ni kumtumikia Yesu Kristo. Je! umeingia mahali hapo, ndugu yangu mpendwa? Je! umefika mahali hapo ambapo hujali mtu yeyote anasema nini, si kwenda nje na kutenda kwa busara, bali mpaka upendo wa Mungu umetiwa nanga ndani yako, hata huwezi kuona kitu kingine chochote, nia yako yote ni kufanya mapenzi ya Mungu, upendo kwa kila mtu, ukitiririka huru kutoka kila mahali? Ni mahali pa jinsi gani pa kuishi. Hapo ndipo mahali pa siri. Hapo ndipo mahali tulipopaswa kufika, ndugu zangu. Hapo ndipo mahali ambapo Mungu hufunua mambo Yake ya siri. Hapo ndipo mahali ambapo Mungu hufanya kazi ya kumweka mtu mahali pake na kuitia.
MKATE WA KILA SIKU
Kama ayala aioneavyo shauku mito ya maji. Vivyo hivyo nafsi yangu inakuonea shauku, Ee Mungu. Zaburi 42:1
25-0305
50-0716 – Je! Unasadiki Hayo?
Ukiipenda dunia, mambo ya dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yako. Hilo linaweza kuwa gumu kidogo kufundishwa hapa, lakini ni kweli; ngoja niwaambie. Sina vijiti vya kupimia kanisani. La, hata kidogo. La, bwana.
Mti wa mwaloni wa zamani mlio nao hapa unashikilia majani yake wakati wote wa majira ya baridi kali. Majira ya kuchipua ya mwaka yanakuja, huna haja ya kwenda kuyachuma majani ya kale, acha tu uhai mpya uingie, jani kuukuu huanguka. Ndivyo ilivyo. Hebu Kristo aingie moyoni; hayo mengine yatajishughulikia yenyewe. Hiyo ni kweli. Mwingize tu Kristo moyoni; itashughulikia hayo mengine.
MKATE WA KILA SIKU
Kwa kuwa kila mti hutambulikana kwa matunda yake. Luka 6:44
25-0304
61-0415E – Sauti Isiyojulikana
Musa alikuwa, labda, kamwe hajaisikia Sauti ya Mungu, bali alijua kwa akili, alijua kwa hisia iliyokuwa ndani yake, ya kwamba alikuwa ndiye mkombozi, bali alijaribu kufanya hivyo akashindwa, kwa hiyo akasema, “Labda nilifanya kosa.”
Huenda kukawa na wahubiri wanaoketi hapa nje vile vile, waliodhani mlifanya kosa, mlipoona kushindwa kwenu, kamwe hamkungojea muda mrefu vya kutosha. Biblia ilisema, “Wao wamngojeao Bwana watapata nguvu mpya, watapaa juu kwa mbawa kama tai.”
Musa alifikiri kwamba labda alikuwa ameukosa wito wake, lakini siku moja wakati Mungu aliponena naye uso kwa uso, naye akasikia Neno la Mungu, Malaika wangu akanena naye, nayo yakapatana na Neno, alipoona ya kwamba ile Sauti iliyonena naye ilikuwa ni kitu kile kile Neno lilichokuwa limeahidi, basi akawa na imani, naye akawa na hakika kwamba atashuka kwenda kule. Alikuwa na hakika Israeli itatoka chini ya utumwa, kwa sababu Mungu alifanya ahadi, ilikuwa ni ahadi ya Kimaandiko.
MKATE WA KILA SIKU
Ila na mfurahi katika dhiki pia; mkijua ya kuwa dhiki, kazi yake ni kuleta saburi;
Na kazi ya saburi ni uthabiti wa moyo; na kazi ya uthabiti wa moyo ni tumaini;
Warumi 5:3-4
25-0302
Vema, mlipata kuona mwana reli akipakia mabehewa? Yeye atatoka aende na ataweka kiasi fulani hapa, na kiasi fulani hapa. Mkaguzi anapita pale, anaangalia ndani; na iwapo hili limelegea kidogo, linatikisika, “La. Mimi sitalitia muhuri. Sina budi kulifungua na kulirudia tena.” Basi, atajaribu kulipakia tena; atakosea hili. Mkaguzi anapita pale, “Ni makosa. Fanya tena.”
Na hivyo ndivyo Mungu amekuwa akifanya na kanisa Lake kwa muda mrefu. Utapakiwa, nawe unaenda Mbinguni; unachukua kila kitu. Karata zako, a-ha, kila kitu kingine unachoweza kupakia kwenye kanisa, unajaribu kwenda nacho. Mungu anahukumu jambo hilo; huko tayari kwa kutiwa mhuri.
Lakini wakati Mungu anapomwona mtu, mwenye roho iliyopondeka, iliyovunjika, moyo mwaminifu, kwenye madhabahu, Mungu hufunga mlango wa ulimwengu kwake, na kumtia muhuri mle kwa ubatizo wa Roho Mtakatifu, na unadumu mpaka Yesu atakapokuja; si kutoka ufufuo mmoja hata mwingine, lakini, “hata siku ya ukombozi wako.”
MKATE WA KILA SIKU
Lakini msingi wa Mungu ulio imara umesimama, wenye muhuri hii, Bwana awajua walio wake. 2 Timotheo 2:19
25-0228
63-0601 – Njoo, Unifuate
Enyi watoto, ninyi, kila mmoja, mnaonekana kama wangu. Ninyi, kila mmoja, mnaonekana kama tu wana na binti zangu. Kwa njia moja, ndivyo mlivyo, mnaona, tukinena kiroho. Hiyo ni kweli. Bwana Mungu ame—ameziweka nafsi zenu katika ulinzi wangu, kwa sababu mnakuja, kunisikiliza. Mnaniamini mimi. Mnaona? Na katika maana moja ya neno hilo, ninyi ni wana na binti zangu. Hiyo ni kweli.
Daima kumbukeni, kuzishika amri za Mungu ni jambo kuu. Kulelewa katika nyumba nzuri ni urithi kutoka kwa Mungu. Na kuwa watoto wazuri wenye haiba kama mlivyo nazo, vema. Vizuri sana, kuwa na elimu. Ni vizuri sana hata kuishi katika nchi hii huru. Tuna mambo mengi ya kutolea shukrani.
Ila kuna kitu kimoja ambacho hukirithi. Inakubidi kukikubali. Hicho ni Uzima wa Milele. Nawe utafanya hivyo tu kwa kumfuata Yesu, kwa ujuzi wa kuzaliwa mara ya pili. Usipuuze hilo.
MKATE WA KILA SIKU
Yule kijana akamwambia, Haya yote nimeyashika; nimepungukiwa na nini tena? Mathayo 19:20
25-0227
58-1004 – Imani Ndiyo Ushindi Wetu
Jisalimishe! Kuwa sawa na Mungu! Ama uwe kile ulicho, au usiwe kabisa. Endapo Biblia ya Mungu hailifundishi, basi jiepushe nalo. Kama inalifundisha, dumu Nalo.
Inanikumbusha jambo hili. Kwa mfano, vipi kama tungefunga safari kidogo, katika siku thelathini tangu sasa, kwenda kwenye nchi nyingine? Na katika nchi hii, hali ya hewa ilikuwa nzuri sana, hata hatungerudi tena. Na huko isingetulazimu kufa wala kuzeeka, bali tungekuwa huko milele. Je, ningeweza kuwazia nikikuona ukienda kwenye duka la mali rahisi, ukinunua vikorokoro vingi kwenda navyo? Ungekuwa ukijaribu kuondoa vikorokoro ulivyo navyo.
Na unapojihangaisha tu, kwa kujiunga na kanisa moja na kisha lingine, utajikusanyia takataka zaidi. Lakini ikiwa utatafakari unakoenda, utaondoa mashaka hayo mengi na upuuzi huo. Utakuwa na imani halisi.
MKATE WA KILA SIKU
…Visivyoonekana. Kwa maana vinavyoonekana ni vya muda tu; bali visivyoonekana ni vya milele. 2 Wakorintho 4:18
25-0226
57-0915E – Waebrania, Mlango Wa Saba #1
Lakini wakati Mungu alipolinena hapa nyuma, kila Neno la Mungu ni imara. Halikubadilika. Haiwezekani. Haliwezi kushindwa. Na wakati Mungu alipomchinja Mwanawe kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu, Yeye alikuwa amechinjwa wakati huo kabisa kama alivyokuwa amechinjwa pale Kalvari. Ni kazi iliyomalizika, wakati Mungu anaposema hivyo. Pia kumbuka, wakati Mwana-Kondoo alipochinjwa, wokovu wako ulihesabiwa katika hiyo dhabihu, kwa maana Biblia ilisema ya kwamba jina lako lilikuwa “Limeandikwa katika Kitabu cha Uzima cha Mwana-Kondoo kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu.”
Na hilo je? Basi tutafanya nini? Mungu Ndiye arehemuye. Mungu Ndiye aliyekuita. Mungu Ndiye aliyekuchagua katika Kristo kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu. Yesu alisema, “Ha—hamkunichagua kabisa. Mimi niliwachagua. Nami niliwajua, kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu.” Haya basi.
MKATE WA KILA SIKU
Na sisi tumeona na kushuhudia ya kuwa Baba amemtuma Mwana kuwa Mwokozi wa ulimwengu. 1 Yohana 4:14
25-0225
60-1204E – Ono La Patimo
Si ni vizuri sana wakati unapoweza kweli kuitia nanga nafsi yako katika Kristo, kufikia mahali ambapo unaweza kutulia mbele Zake? Na kusikia Sauti Yake ikisema nawe, “Mimi ndimi Bwana nikuponyaye. Mimi ndimi Bwana nikupaye Uzima wa Milele. Ninakupenda. Nilikujua kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu. Niliandika jina lako kwenye Kitabu, wewe ni Wangu. Usiogope, ni Mimi. Usiogope, niko pamoja nawe.” Ndipo ninaimba:
Nimetia nanga nafsi yangu katika mahali pa raha,
Sitaabiri bahari zenye tufani tena;
Huenda tufani ikakipiga kilindi cha bahari yenye dhoruba;
Lakini katika Yesu mimi ni salama milele.
Kumbukeni, Sauti ile ile inayokuzungumzia kwa utamu, itamhukumu mwenye dhambi. Gharika ile ile iliyomwokoa Nuhu, ilimwangamiza mwenye dhambi. Mnaona ninalomaanisha?
MKATE WA KILA SIKU
Tuliyo nayo kama nanga ya roho, yenye salama, yenye nguvu,… Waebrania 6:19
25-0224
61-0416 – Ibrahimu Na Uzao Wake Baada Yake
Usijiangalie mwenyewe; iangalie Dhabihu yako. Mungu hakuangalii; Yeye anaiangalia Dhabihu yako ambayo ni Kristo. Usijiangalie mwenyewe. Mimi sistahili; wewe hustahili; hakuna mtu anayestahili; bali Yeye Ndiye. Sihesabu yale nimefanya, kile nilicho mimi, la sivyo ni—nisingefaulu. Lakini ninaangalia yale Yeye amefanya. Hipo ndipo ninapotumainia: Yale Yeye amefanya. Yeye ndiye Dhabihu yangu. Sistahili uponyaji. La, bwana. Bwana, nilipaswa kufa muda mrefu uliopita, kamwe sikustahili hata kuzaliwa. Ila ninaishi; ninao Uzima wa Milele; ninaenda Mbinguni. Kwa nini? Kwa maana Yeye alilifanya kwa ajili yangu. Alikuwa Ndiye. Alichukua mahali pangu. Nilikuwa na matege, mwenye makengeza katika hali ya kila namna, bali Yeye alipachukua mahali pangu. Tukinena kiroho, nilikuwa nimepindika kabisa, na kuvurugika kabisa; bali Yeye akapachukua mahali pangu; kwa hiyo Yeye ananifaya mwana mkamilifu wa Mungu, binti mkamilifu wa Mungu. Dhabihu Yake ilifanya hilo, si yangu. Sikuwa na uhusiano wowote nalo. Nilizaliwa nimeumbuka kabisa kwa vyovyote vile. Lakini si—situmaini katika yale nimefanya. Ninatumaini yale Yeye amefanya (Mnaona?), kile Yeye alichokuwa, hivyo ndivyo ilivyokuwa.
MKATE WA KILA SIKU
Kwa maana Mwana wa Adamu hakuja kuziangamiza roho za watu, bali kuziokoa. Wakaondoka wakaenda mpaka kijiji kingine. Luka 9:56
25-0223
61-0215 – Ewe Mwana Wa Daudi, Unirehemu
Mungu aliwaambia huko chini kabisa Misri, “Nimewapa nchi hiyo.” Bali Yeye hakusema, “Nitaenda huko nje na kuwafagilia mbali, na kuzipamba nyumba, na kuweka mapazia, na kila kitu. Nyote mwingie tu.” La, la. Iliwabidi kupigania kila inchi ya ardhi waliyoiteka. Hiyo ni kweli, kupiga vita, na kuiteka kwa kila…kupiga vita kila inchi. Bali Yeye alisema, “Kila mahali nyayo za miguu yenu zitakapokanyaga, huo ni umiliki.” Nyayo za miguu ni umiliki.
Hilo ndilo jambo lile lile siku hizi. Uponyaji wa Kiungu ni wetu. Roho Mtakatifu ni wetu. Ni mali yetu, bali itakubidi kupigania kila inchi yake. Naam, bwana. Lakini ndugu, nyayo za miguu ni umiliki. Endelea tu kupiga vita. Iteke. Ibilisi anasema, “Siku za miujiza zimepita.”
Sema, “Unadanganya. Mungu alisema Yeye ni yule yule jana, leo, na hata milele.” Iteke. Kila mahali mguu wako utakapokanyaga, huo ni umiliki. Hiyo ni kweli.
MKATE WA KILA SIKU
Yeye Bwana, Mungu wenu, atawatoa kwa nguvu mbele yenu, atawafukuza wasiwe mbele ya macho yenu tena; nanyi mtaimiliki nchi yao, kama Bwana Mungu wenu, alivyowaambia. Yoshua 23:5
25-0222
56-0223 – Agano la Mungu pamoja na Ibrahimu na Uzao Wake
Mungu hafanyi tofauti yo yote miongoni mwa watoto wake. Kila mwana amjiaye Mungu hana budi kwanza kujaribiwa ama kurudiwa. Mnalipata? Kwanza kujaribiwa, ama kurudiwa, kusahihishwa, kupewa mafunzo ya mwana, kufundishwa, kila mmoja, bila kubagua mmoja, kila mwana. Je, umepitia majaribu? Je, umepitia dhiki? Je, umepitia mateso? Basi, mkistahimili mambo haya, mmekuwa watoto halisi wa Mungu.
Lakini unaposhindwa kustahimili kurudiwa, fimbo ishukapo nzito, nawe ukimbie na kurudi ulimwenguni, Biblia ilisema ninyi ni watoto haramu, na si watoto wa Mungu. Kwa maana mtu anapozaliwa kwa Roho wa Mungu, yeye hutarajia mambo hayo, naye hupenda mambo hayo. Na Biblia ilisema ya kwamba majaribu yanayotujia, majaribu ya moto, ni ya thamani kuliko dhahabu kwetu. Liwazie jambo hilo.
MKATE WA KILA SIKU
Angalieni, twawaita heri wao waliosubiri. Yakobo 5:11
25-0221
61-0226 – Yehova-Yire
Usijiangalie ulivyo, mtazame Mwanakondoo wako. Mungu hakukubali wewe, Yeye alimkubali Mwana-Kondoo, naye Mwana-Kondoo akachukua mahali pako. Ee Mungu! Je, huwezi kuona jambo hilo? Si wewe, wewe haustahili, Mimi sistahili, hakuna hata mmoja wetu anayestahili. Lakini, unaona, je! Yeye anastahili? Mungu alisema hivyo, alimkubali Yeye, akasema, “Huyu ni Mwanangu mpendwa, ninayependezwa naye; huyu ni Mwanangu, msikieni Yeye,” siku ya kufanywa mwana mwenye Mamlaka, “huyu Ndiye.”
Usiseme, “Vema, daktari anasema sitapona kamwe.” Hayo ni asemayo daktari. Sasa, mtu huyo ni mwanasayansi, anaangalia jinsi maumbile yanavyoenenda, naye anaona huwezi kamwe kupona, hilo linamwonyesha jambo hilo kisayansi. Naam, hayo ndiyo yeye anayoangalia, ukiangalia kitu kile kile, hutapona. Lakini usiangalie kile alichosema, usiangalie kile wewe…jinsi unavyopungua, bali iangalie Sadaka yako. Hilo ndilo.
Na kumbukeni ninyi ni Uzao wa Ibrahimu na warithi pamoja naye, basi kama ndivyo ulivyo, dumu na ahadi, umkubali Yeye kama Mponyaji wako, na ukae tu papo hapo.
MKATE WA KILA SIKU
Siku ya pili yake amwona Yesu anakuja kwake, akasema, Tazama, Mwana-kondoo wa Mungu, aichukuaye dhambi ya ulimwengu. Yohana 1:29
25-0220
62-0120 – Mungu Asiyebadilika Akitenda Kazi Katika Njia Isiyotarajiwa
Yeye anajua haja zenu. Yeye anajua jinsi ya kuzileta kwenu. Lakini shida ni kwamba, kwa kuwa jambo haliji jinsi mnavyofikiri linapaswa kuja, basi mnakufa moyo kabisa, nanyi mnalirudisha Kwake. Hebu na tumwombe, na tuamini ya kwamba Yeye atalituma jinsi tu anavyotaka kulituma. Na tulikubali juu ya msingi huo. Hiyo ni kweli. Unaona?
Kama ukimwomba, usimfanye Yeye kuwa mwongo. Yeye hawezi kusema uongo. Aliahidi, “Mwombeni Baba lolote katika Jina Langu, nitalifanya.” Sasa, Mungu hawezi kusema uongo. Mwombe na litatimizwa. “Tafuteni, nanyi mtapata; bisheni, nanyi mtafunguliwa.” Tunaamini hilo. Hakika tunaamini.
MKATE WA KILA SIKU
Tena siku ile hamtaniuliza neno lo lote. Amin, amin, nawaambia, Mkimwomba Baba neno lo lote atawapa kwa jina langu. Yohana 16:23
25-0219
61-0213 – Na Uzao Wako Utamiliki Lango la Adui Zake
Wakati tu walipokuwa tayari, wakifanya hatua yao ya mwisho, ninaweza kumwona Yeye akisimama, mavazi Yake ya ukuhani yakishuka kumzunguka Yeye mahali anapoketi usiku wa leo. Wameloa Damu, wakifanya maombezi juu ya maungamo yetu, kwa kuwa Yeye alikufa ili kutimiza lo lote tuombalo. Imani yetu kwake iko wapi?
Huyo hapo anasimama, akisonga namna hiyo, na hili hapa linakuja wingu kubwa, jeupe karibu, anapanda juu yake, akiuita upepo wa mashariki, upepo wa kaskazini, upepo wa kusi, na upepo wa magharibi, kuuendesha kama farasi, kafika juu, akashika radi ya zigizaga, akazipasua anga kwayo. Kabla hawajaingia mle, Yeye alikuwa kwenye tanuru ya moto pamoja nao.
Alisimama mle ndani akiwa na feni kubwa ya mitende pale mahali fulani ya Mti wa Uzima, akiizima miale ya moto namna hiyo, Kasema, “Nilitaka tu kuzungumza nanyi enyi watoto. Ninajua ya kwamba ninyi ni Uzao wa Ibrahimu, Mimi ndiye niliyeitoa ahadi hii, nami niko hapa kujibu, njoo hapa,” akiizima miali ya moto, loo, naam.
Wakafungua, wakasema, “Mmeweka wangapi mle ndani?”
Kasema, “Watatu.”
Akasema, “Kuna Mmoja zaidi mle, Naye anafanana na Mwana wa Mungu.” Alikuwa. Kwa nini? Wao, baada ya kujaribiwa, walilimiliki lango la adui. Amina.
MKATE WA KILA SIKU
Mungu kwetu sisi ni kimbilio na nguvu, Msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso. Zaburi 46:1
25-0218
53-0405S – Nendeni, Mkawaambie Wanafunzi Wangu
Ninao watu, kila mahali nchini kote, wakati mwingine wakinishutumu kuhusu uponyaji wa Kiungu. Mbona, ndugu yangu, ningewezaje kujizuia kuamini katika uponyaji wa Kiungu, wakati ndiyo asili yenyewe ya Roho Mtakatifu. Kila mtu aliyezaliwa kwa Roho wa Mungu itambidi kuamini katika mambo ya kimbinguni, kwa sababu yeye ni sehemu ya Mungu, yeye ni mtoto wa Mungu.
Nasema, “Unafanana na baba yako.” Aisee, “Una pua kama…” Wananiambia nina pua kama ya baba; nina kinywa kama cha baba. Kwa nini? Yeye ni baba yangu. Nina haki ya kufanana naye.
Haleluya! Basi, kama Mungu ni Baba yangu, nina haki ya kuamini katika mambo ya kimbinguni, kwa sababu nimezaliwa kwa Roho wa kimbinguni. Hiyo inanifanya kiumbe cha kimbinguni. Kwa ndani, kwa nje, mimi ni—mimi ni mtu wa udongo; wewe ni mtu wa udongo. Lakini kwa ndani, unapozaliwa kwa Roho wa Mungu, unakuwa kiumbe cha kimbinguni humo ndani, nacho hicho kiumbe cha kimbinguni kinaona njaa na kiu kwa ajili ya Makao yake ya Mbinguni, huko ng’ambo. Hiyo ni kweli.
MKATE WA KILA SIKU
Kwa kuwa ninyi nyote mmekuwa wana wa Mungu kwa njia ya imani katika Kristo Yesu. Wagalatia 3:26
25-0217
58-0128 – Umoja Wa Muungano
Siku zote nilimhurumia kuku wa kiangulio. Kuku aliyezaliwa ndani ya kiangulio, hulia, wala hana mama wa kumwendea. Hilo linanikumbusha juu ya mhubiri wa seminari ambaye hajui zaidi kuhusu Neno la Mungu kuliko vile seminari ilisema; akilia, wala hana Mama wa kumwendea.
Lakini unapozaliwa kweli chini ya mbawa za neema na nguvu Zake, utakubaliana na kila Neno alilosema Yeye, ni Kweli. Ndipo Mungu anaposonga mbele katika mambo ya kimbinguni, moyo wako utakuwa na njaa moja kwa moja Kwake.
Hutaenda kando na kusema, “Telepathia ya akili! Ibilisi! Beelzebuli! Siamini Hilo. Kanisa langu halifundishi Hilo.”
Utasema, “Mungu asifiwe milele,” kwa kuwa umejazwa. Huwezi kukaa tupu.
MKATE WA KILA SIKU
Kwa manyoya yake atakufunika, Chini ya mbawa zake utapata kimbilio; Uaminifu wake ni ngao na kigao. Zaburi 91:4
25-0216
61-0429E – Sauti Isiyojulikana
Hebu—hebu tuonyeshe kilicho ndani yetu. Kama…Hebu tupate kitu fulani hapa ndani kuonyesha upendo na heshima, na kumheshimu mtu huyo mwingine na—na kumpenda, awe sahihi ama makosani.
Kama unaweza tu kuwapenda wale wanaokupenda, mbona, wenye dhambi hufanya jambo lile lile. Lakini sisi ni tofauti, wakati Kristo ameingia moyoni mwetu tunawapenda wale wasiotupenda; tunawapenda wasiopendeka. Nasi tulikuwa hatupendeki wakati mmoja, pia, mwajua, naye Kristo akatupenda mpaka tukamjia. Na basi kama sisi ni wa Kristo na Kristo yuko ndani yetu, tuna Roho yeye yule wa ushirika, na ushirikiano, na kusaidia kujaribu kuusogeza huo mzigo mkubwa, na kuyarahisisha maisha kidogo kwa ajili ya wenzetu.
MKATE WA KILA SIKU
Maana mkiwapenda wale wawapendao ninyi, mwaonyesha fadhili gani? Kwa kuwa hata wenye dhambi huwapenda wale wawapendao. Luka 6:32
25-0214
63-0630E – Je! Maisha Yako Yanaistahili Injili?
Mwangalieni Yesu. Nena kuhusu sisi kujinyenyekeza? Wakati Mungu Mwenyewe alipofanyika mtoto mchanga, badala ya kuja katika ki—kitanda kidogo cha mtoto mahali fulani katika nyumba nzuri, alizaliwa huko nje juu ya lundo la samadi horini, miongoni mwa ndama wa ng’ombe waliokuwa wakilia. Walimfunga nguo za kitoto, zilizotoka kwenye shingo ya nira ya maksai. Maskini kuliko maskini wote, na, hata hivyo, ni Muumba wa mbingu na nchi.
Usiku mmoja baridi, wenye mvua, walisema, “Bwana, tutaenda nyumbani pamoja na Wewe.”
Akasema, “Mbweha wana mapango, na ndege wana viota, bali sina hata mahali pa kulaza kichwa Changu.”
Mungu, Yehova, alijinyenyekeza na kuwa Mwanadamu; akawakilishwa katika mwili wa dhambi, kukukomboa wewe na mimi. Sisi ni akina nani basi? Yeye alikuwa ni mfano wetu. Mimi ni nani? Si kitu.
MKATE WA KILA SIKU
Mimi kati yenu ni kama atumikaye. Luke 22:27
25-0213
64-1212 – Wakati Wa Mavuno
…kuna aina moja tu ya Uzima wa Milele, na hiyo ni Mungu. Kwa hiyo kama tuna Uzima wa Milele, tulikuwako pamoja na Mungu wakati huo, sehemu ya Mungu. Tulikuwa ni sifa Yake. Sisi sasa ni sifa Yake. Na, kwa sababu, “Hapo mwanzo kulikuwako Neno.” Nalo neno ni wazo lililotamkwa. Kwa hiyo sisi tulikuwa ni mawazo Yake, kisha tukadhihirishwa katika neno na tukawa kile tulicho. Hiyo ndiyo sababu majina yetu, labda si yale tuliyo nayo sasa, lakini majina yetu yaliandikwa katika Kitabu cha Uzima cha Mwana-Kondoo kabla ya kuwekwa msingi wa ulimwengu. Unaona? Na kama halikuwa humo wakati huo, kamwe halitakuwapo. Unaona? Naye Yesu alikuja kuwakomboa hao wote, hiyo ni kusema, ambao majina yao yalikuwa kwenye Kitabu hicho.
MKATE WA KILA SIKU
… yeye afanyaye mapenzi ya Mungu adumu hata milele. 1 Yohana 2:17
25-0212
61-0413 – Kwa Nini?
“Ni yupi, akijisumbua, aweza kujiongeza kimo chake hata mkono mmoja?” alisema Yesu. Tuko kile tulicho.
Na hilo ndilo jambo moja ambalo limeathiri uamsho wetu wa Kipentekoste, na miamsho mingine, ni mtu fulani anayejaribu kuwa kitu ambacho wasicho, wanajaribu kumwiga mtu mwingine. Huwezi kufanya hivyo, uko tu kile ulicho, hivyo tu. Na unapofanya hivyo, Mungu atakutumia tu jinsi ulivyo.
Nawe ni muhimu tu kama mtu mwingine yeyote. Kama nilivyosema hivi majuzi usiku, ile springi iliyo ndogo sana katika saa hii ni muhimu tu kama ile springi kuu, maana zote zinahitajika kwa kupima wakati. Na hivyo…Tunapotambua mahali petu katika Kristo, na kisha kudumu hapo, kama ni maskini mke wa nyumbani, kaa papo hapo, hivyo ndivyo Mungu anavyokutaka ufanye. Unaona? Kuwa tu kile ulicho.
MKATE WA KILA SIKU
Lakini kama Bwana alivyomgawia kila mtu, kama Mungu alivyomwita kila mtu, na aenende vivyo hivyo. 1 Wakorintho 7:17
25-0211
59-0412E – Unasikia Nini, Eliya?
Kuna hakikisho moja ambalo mwamini alilonalo, ingawa ulimwengu ulimkataa, bado Mungu anampenda. Ulimwengu unaweza kukuita mtakatifu anayejifingirisha; wanaweza kukuita mshupavu wa dini; lakini kama wewe ni mkweli kwa Mungu kuna jambo moja la hakika: Mungu anakupenda, nao Malaika Zake wamepiga kambi kuwazunguka wale wamchao.
Ningewazia kwenye kila tawi, kote kote mahali pale, kulikuwa na makundi ya Malaika. Ndipo Mungu akashuka, Naye akasema, “Maskini mtumishi wangu aliyechoka. Ana wasiwasi sana naye amechoka, hajui la kufanya. Ninataka kumchagua Malaika aliyesimama hapa aliye na mikono myororo zaidi. Usimtishe; wewe tembea pale na umguse paji la uso wake taratibu. Nami nataka mpishi aliye bora kati yenu, nanyi nendeni kule, na kuchukua vitamini zote mnazoweza kupata, na kuweka kwenye unga huu wa mahindi. Ulimwengu umemkataa, lakini nitamtendea vizuri.” Haleluya. Hilo linamaanisha “msifuni Mungu wetu.” Msiogope hilo.
“Leteni yaliyo bora zaidi tuliyo nayo; mwokee keki ya unga wa mahindi na umwekee kiasi cha maji.” Naye Malaika huyu mwenye mikono myororo akasogea na kumgusa maskini yule mtumishi wa Mungu kwenye paji la uso.
Kumbuka, kama umefanya vizuri uwezavyo, Mungu angali anao hao Malaika katika utaratibu. Anakupenda vile vile tu kama alivyompenda Eliya.
MKATE WA KILA SIKU
Kwa kuwa atakuagizia malaika zake Wakulinde katika njia zako zote. Zaburi 91:11
25-0210
63-1130B – Ushawishi
Mungu humwagiza mtu Wake, na huwezi kuchukua mahali pa mwingine. Ukichukua, unafanya tu uigaji wa kimwili, na hatimaye utashindwa. Unaona, huwezi kufanya hivyo. Mungu hukuagiza mahali pako. Isaya aliona hili, kwamba asingeweza kuweka tumaini lake juu ya mtu yeyote. Hapo alikuwepo mtu mashuhuri kuliko wote waliokuweko duniani, wakati huo, mfalme ambaye ulimwengu wote ulikuwa ukimlipa kodi; lakini kwa sababu alitoka mahali pake, Isaya aliona basi kwamba asingeweza kuegemea mkono wowote wa mwanadamu, na hilo likampeleka nabii hekaluni, kuomba.
Ee Mungu! Laiti kanisa, laiti watu wanaojiita wenyewe Wakristo, wangeweza tu kuona hili leo hii, na lingewasukuma madhabahuni mahali fulani kuomba. Huwezi kuwa kitu usicho.
MKATE WA KILA SIKU
Kila mtu ana karama yake mwenyewe itokayo kwa Mungu, huyu hivi, na huyu hivi. 1 Wakorintho 7:7
25-0209
65-0801E – Matukio Yakidhihirishwa Na Unabii
Mnaona, Biblia haijipingi Yenyewe; Biblia ni Mungu. Hakuna kuhitilafiana kwa Mungu; Yeye ni mkamilifu.
Lakini watu, kwa ufasiri wao wenyewe! Sasa angalia, hebu niwaonyeshe, enyi marafiki. Makanisa hayawezi kukubaliana juu ya fasiri Yake. Mmethodisti hawezi kukubaliana na Mbatisti, Mbatisti hawezi kukubaliana na Mpresbiteri, Mpresbiteri na Wapentekoste. Na kukiwepo na kama madhehebu arobaini ya Wapentekoste, wao hawawezi kukubaliana wao kwa wao. Kwa hiyo unaona, hiyo ingekuwa ni Babeli tena, mchafuko.
Lakini Mungu hujifasiria Mwenyewe Neno Lake. Yeye aliahidi jambo hili, na halafu analifanya Mwenyewe. Hutoa, Yeye Mwenyewe, fasiri Yake, kwa maana Yeye hujitambulisha Mwenyewe katika saa hiyo. Ni mbali jinsi gani Mwi—Mwili wa Kristo umekwenda, kutoka miguuni mpaka kichwani!
MKATE WA KILA SIKU
Akawaambia, Enyi msiofahamu, wenye mioyo mizito ya kuamini yote waliyoyasema manabii! Luka 24:25
25-0208
47-1123 – Wana wa Israeli
Sasa, marafiki, kuna njia moja tu ulimwenguni ambayo unaweza kuponywa, na hiyo ni imani tu katika Mungu. Sasa, haidhuru ni kiasi gani ambacho Mungu ataniruhusu, kwa imani yangu mwenyewe, kuiondoa roho kutoka kwako, isipokuwa uende na umwamini Mungu, na kumtumikia Mungu, na kumtumaini Mungu, itakurudia tena moja kwa moja. Je, Yesu hakusema, “Nenda zako na usitende dhambi tena, au litakujia jambo baya zaidi kuliko hili?”
Usije kamwe katika mstari wa maombi isipokuwa uwe unatarajia kumtumikia Mungu siku zako zote. Hiyo ni kweli. Daima, usiishi kamwe maisha ya dhambi, kwa sababu utakuwa mbaya zaidi, mbaya zaidi. Mungu ameahidi kwamba utakuwa na hali mbaya zaidi kuliko ulivyokuwa hapo kwanza.
MKATE WA KILA SIKU
Angalia, umekuwa mzima; usitende dhambi tena, lisije likakupata jambo lililo baya zaidi. Yohana 5:14
25-0207
61-1015M – Maswali na Majibu
Yesu ndiyo ile Mana iliyofichwa; Kristo ndiye Mana ya kanisa. Mana ni nini? Mana katika Agano la Kale ilikuwa kile kilichoshuka upya toka Mbinguni kila usiku kupea kanisa nguvu katika safari yake. Sivyo? Sasa, katika Agano Jipya ile Mana iliyofichwa ni nini? “Kitambo kidogo na ulimwegu haunioni tena (imefichika); bali ninyi mtaniona, maana nitakuwa pamoja nanyi, hata ndani yenu, hata ukamilifu wa dahari.” Na Kristo ndiye Mana iliyofichwa itokayo kwa Mungu Mbinguni upya kila siku—kila siku.
Hatuwezi kusema, “Vema, majuma mawili yaliyopita nilikuwa na ujuzi mkuu wa Mungu.” Na sasa hivi je? Ona? Kila siku, mpya, baraka mpya, kitu fulani kipya kikija toka kwa Mungu, ile Mana iliyofichwa ikishuka toka kwa Mungu Mbinguni, Kristo. Na tunaila Mana hii ambayo ni Kristo, na Yeye hutupea nguvu safarini kote hata tutakapofika ile—ile nchi kule ng’ambo.
MKATE WA KILA SIKU
Kwa maana chakula cha Mungu ni kile kishukacho kutoka mbinguni na kuupa ulimwengu uzima. Yohana 6:33
25-0206
55-0116A – Mahali pa Mwamini Katika Kristo
Sasa, kama tunaweza kupata mahali petu na kujua ya kwamba ni Neno la Mungu ambalo limeahidi jambo hilo…Hiyo ndiyo sababu Yoshua na Kalebu hawakuwa na woga ya kwamba hawangeweza kutwaa ile—nchi ya ahadi. Kwa sababu hao wengine wote tisa walirudi, ama wale kumi, na kusema, “Hatuwezi kufanya jambo hilo. Mbona, miji hiyo iliyokuwa na kuta ndefu, nasi tunaonekana kama panzi upande wa watu. Wao ni majitu kweli na wana silaha,” na kusema, “Hatuwezi kufanya jambo hilo.” Unaona, walikuwa wakiangalia hisi ya kutoa hoja.
Huwezi kuangalia hisi ya kutoa hoja; huna budi kutazama ahadi ya Mungu. Sasa, Mungu alikuwa tayari amemtuma Malaika Wake, na Malaika alikuwa kambini akisonga mbele. Na ufunuo wa Mungu ulikuwa umeleta Neno la Mungu likidhihirishwa. Na sasa walikuwa tayari kusukumana kuingia katika nchi ya ahadi.
MKATE WA KILA SIKU
Mara Yesu akanyosha mkono wake, akamshika, akamwambia, Ewe mwenye imani haba, mbona uliona shaka? Mathayo 14:31
25-0205
53-0507 – Matarajio
Sasa, hili hapa; lipateni. Ugonjwa, namaanisha dhambi, ni kutoamini. “Asiyeamini amekwisha hukumiwa.” Kwa sababu unaiba, unadanganya, unavuta sigara, una kunywa pombe, unazini, hiyo si dhambi. Hizo ni sifa za dhambi. Unafanya hayo kwa sababu huamini.
Nawe ni mkweli, na mwaminifu, na mwadilifu, na mnyoofu, na mtakatifu na mwenye kuheshimika (si kwa sababu…huo si Ukristo), unafanya hivyo: hayo ni matunda tu ya Ukristo kwa sababu unaamini; ni sifa za imani yako katika Kristo Yesu na kuzaliwa kwako kama mwanawe. Amina. Unaona? Mti mzuri hauwezi kuzaa matunda mabaya (mti mbaya unaweza kuyazaa ), unazaa tu matunda mazuri. “Kwa matunda yao mtawatambua.”
Sasa, kama Roho Mtakatifu akija ndani ya jengo hili usiku wa leo, na kutangaza Neno Lake kuwa ni Kweli, nawe utoke usiliamini, ungekuwa mwenye dhambi. Ikiwa Mungu akikuambia maisha yako yamekuwaje, na jinsi yatakavyokuwa, na kama ukijua kile kilichokuwa ni kweli, na kukuambia kile kitakachokuwa; nawe uondoke huliamini, yatakujia mabaya zaidi kuliko haya. “Nenda zako na usitende dhambi tena.”
MKATE WA KILA SIKU
Kila mti usiozaa tunda zuri hukatwa ukatupwa motoni.
Ndiposa kwa matunda yao mtawatambua. Mathayo 7:19-20
25-0204
54-0404M – Kuishindania Imani
Loh, Mungu anataka kurejesha imani ambayo waliyokabidhiwa wa watakatifu mara moja. Unasema, “Ndugu Branham, hiyo ni imani?” Usichukue kiini macho cha Me—Methodisti, kiini macho cha Kibaptisti, au kiini macho cha Kipentekoste; chukua Biblia. Hebu tuone kile wao walichotenda. Wote walikuwa katika chumba cha juu kwa nia moja, na ghafla, upepo uleule wenye nguvu ukienda kasi ukaja kutoka Mbinguni, ukaijaza nyumba yote walimokuwa wameketi. Umesemaje? Wakasema, “Ohhh, sijui nitende jambo hili au la. Nikienda nje, watanidhihaki. Nikisema jambo lolote, ‘mbona, ndiomana alisema kwenda nje.’” La, bwana.
Roho Mtakatifu alikutana nao, lile kundi la maskini waoga. Walipata uzima nao wakapitia madirishani na milangoni, wakaingia mitaani, na wakatenda kama kundi la wenda wazimu, na kuyumba-yumba na kupiga mayowe na kupiga makelele na kila kitu, kama kundi la watu walevi; mpaka kanisa la kimwili la siku hizo likasema, “Watu hawa wamejaa divai mpya.”
Na sikiliza, ewe dada, wewe uliye na heshima sana kwenye mzunguko wa kushona nguo kanisani kwako, na kadhalika, na una hadhi ya kijamii huko Louisville, New Albany, na Jeffersonville, bikira aliyebarikiwa Mariamu alikuwa mle ndani. Na ikiwa Mungu Mwenyezi alihitaji bikira Mariamu aliyebarikiwa, na Yeye hasingemruhusu aje Mbinguni hadi apate tukio hilo, utawezaje kufika huko kwa lolote pungufu ya hilo?
MKATE WA KILA SIKU
Lakini mimi nitakutolea sadaka kwa sauti ya shukrani; Nitaziondoa nadhiri zangu. Wokovu hutoka kwa Bwana. Yona 2:9
25-0203
63-0901M – Ile Ishara
Kwa ulimwengu, Hiyo ni upuzi mtupu. Bali, kwa Mungu, ndiyo njia pekee. Kitu pekee Yeye anachohitaji tu ni ile Ishara. Haina budi kuweko. Nawe hauwezi kuwa na ile Ishara hata nauli iwe imelipwa, ndipo u mwenyeji wa Ishara ambayo inakupa he—heshima ya Pasi ya bure. “Nitakapoiona ile Damu, nitapita juu yenu.” Ni wakati jinsi gani, huo, ni heshima jinsi gani, kujua ya kwamba unabeba, ndani mwako, Pasi. “Nitakapoiona ile Damu, nitapita juu yenu.” Ndicho kitu pekee ambacho Yeye atatambua. Hamna kingine kinachoweza kuchukua mahali pake; hamna cha kubadilisha, hamna dhehebu, hamna cho chote kingine. Hiyo ndiyo inayohitajika. Mungu alisema, “Hiyo peke yake ndiyo nitakayoangalia peke yake.”
MKATE WA KILA SIKU
Wala msimhuzunishe yule Roho Mtakatifu wa Mungu; ambaye kwa yeye mlitiwa muhuri hata siku ya ukombozi. Waefeso 4:30
25-0202
53-1205 – Ufufuo
Lazima kuwe na wakati ambapo unapaswa kuacha kuwabembeleza watu kitoto. Huwezi kuwapiga-piga mgongoni. Hiyo ndiyo shida leo. Wahubiri wanashughulikia Injili wakiwa wamevaa glavu za kikanisa. Hiyo ndiyo shida yake leo. Tunachohitaji leo ni Injili ngumu, ilionyooka kukuambia wewe ni mwenye dhambi, unaenda kuzimu. Kama huna Roho Mtakatifu uko nje ya Ufalme wa Mungu. Hiyo ni kweli. Huwezi kuamini mambo ya kimbinguni, kwa sababu hujawahi kuzaliwa mara ya pili. Na unapozaliwa mara ya pili huna budi kuamini mambo ya kimbinguni, kwa maana wewe mwenyewe ni wa kimbinguni.
MKATE WA KILA SIKU
Ushiriki taabu pamoja nami, kama askari mwema wa Kristo Yesu. 2 Timotheo 2:3
25-0201
57-0825M – Waebrania, Mlango Wa Pili #1
Mungu daima hushuhudu. Maisha yako yatashuhudu. Sijui ushuhuda wako ukoje, bali maisha yako yananena kwa sauti kubwa sana, sauti yako haiwezi kusikika. Lakini, mwe—mwenendo wako, maisha yako ya kila siku yatashuhudia kwamba wewe u nani. Mungu hushuhudia. Naam. Roho Mtakatifu ni muhuri, na muhuri huchukua pande zote mbili za karatasi. Wanakuona umesimama hapa na wanakuona ukiondoka. Si kanisani tu bali katika kazi ya kila siku. Umetiwa muhuri pande zote mbili, ndani na nje. Kwa furaha uliyo nayo, na kwa maisha unayoishi, umetiwa muhuri, ndani na nje, kwamba unajua umeokoka na ulimwengu unajua umeokoka, kwa maisha unayoishi, kwa maana Mungu anashuhudia. Jina Lake Takatifu litukuzwe!
MKATE WA KILA SIKU
Na Bwana vivyo hivyo ameamuru kwamba wale waihubirio Injili wapate riziki kwa hiyo Injili. 1 Wakorintho 9:14
25-0131
62-0204 – Ushirika
Sasa, miili yetu huhitaji chakula na kinywaji kila siku, kuishi, miili yetu ya kawaida. Kama hatuli chakula kila siku na kunywa, basi miili yetu hudhoofika. Kuna kitu ndani yetu kwamba yatubidi tule chakula. Chakula cha siku moja hakitadumu kwa siku inayofuata. Yakubidi ule chakula kila siku, kuutia nguvu mwili wako unaokufa. Unaweza kuishi bila, lakini u mdhaifu zaidi. Na siku ya pili, bado u mnyonge zaidi. Na siku ya tatu, unakuwa mdhaifu kabisa.
Vema, hicho ndicho ambacho mara nyingi tunatenda katika ulimwengu wa rohoni. Unaona, kila siku yatubidi kushirikiana na Kristo. Yatubidi kuzungumza Naye kila siku. Yatubidi tupatane Naye kila siku. Paulo alisema, “Ninakufa kila siku.” Unaona? “Kila siku, ninakufa; hata hivyo ninaishi, si mimi bali Kristo huishi ndani yangu.” Kwa hiyo, kama mwili wako wa kawaida unahitaji chakula kila siku na maji kila siku, upate kuishi, mwili wako wa kiroho unahitaji Chakula cha kiroho na ushirika pamoja na Bwana kila siku, upate kuishi. Ndiyo.
MKATE WA KILA SIKU
Maneno ya kinywa changu, Na mawazo ya moyo wangu, Yapate kibali mbele zako, Ee Bwana, Mwamba wangu, na mwokozi wangu. Zaburi 19:14
25-0130
56-0122 – Wakati Wa Njia Panda
Siku moja, Biblia inasema, ya kwamba mambo yatatokea katika dunia hii na magonjwa na kadhalika, na watu wote watapigwa tauni, mpaka nyama ya miili itaoza juu yao na kadhalika. Lakini Biblia inasema, “Usimkaribie yeyote kati ya hao walio na Muhuri wa Mungu katika vipaji vya nyuso zao.”
Na Muhuri wa Mungu ni ubatizo wa Roho Mtakatifu. Sasa, ninyi ndugu wa advantisti, sitaki kutokubaliana nanyi kwa kuwa msabato; hakuna Maandiko kwa jambo hilo. Lakini Biblia Waefeso 4:30 inasema, “Wala msimhuzunishe yule Roho Mtakatifu wa Mungu ambaye kwa yeye mlitiwa muhuri hata siku ya ukombozi wenu.”
Na alama ya mpinga-Kristo ni kumkataa huyo Roho Mtakatifu. Ambayo umetiwa muhuri nje ya Ufalme milele, bila, hakuna njia ambayo watasamehewa. Yeye anenaye neno dhidi ya Roho Mtakatifu hatasamehewa kamwe katika ulimwengu huu au ule ulimwengu ujao. Hiyo hapo alama yako ya mnyama na muhuri wa Mungu katika konzi moja ndogo.
Muhuri wa Mungu ni ubatizo wa Roho Mtakatifu. Na alama ya mpinga-Kristo ni kukana jambo hilo. Sasa, umetiwa alama kwa njia moja au nyingine. Je! hutaki kuwa na Roho Mtakatifu leo?
MKATE WA KILA SIKU
Wala msimhuzunishe yule Roho Mtakatifu wa Mungu; ambaye kwa yeye mlitiwa muhuri hata siku ya ukombozi. Waefeso 4:30
25-0129
57-0828 – Waebrania, Mlango Wa Pili #3
Mungu asingeweza kuteseka katika Roho. Ilibidi afanyike mwili, apate kusikia uchungu wa magonjwa, apate kusikia jaribio la tamaa mbaya, kusikia jaribio la kupungukiwa, kusikia jaribio la njaa, kusikia nguvu za mauti. Apate kutwaa juu Yake jukumu la kusimama Mbele ya Roho Yehova mkuu, yule Roho, si Mwanadamu; Roho, kufanya upatanisho kwa ajili ya maisha haya. Basi Yesu alichukua hayo, kusudi apate kutupatanisha, kwa maana anajua jinsi hali ya mambo ilivyo. Unapokuwa mgonjwa, Yeye anajua unavyojisikia. Unapojaribiwa, Yeye anajua unavyojisikia.
MKATE WA KILA SIKU
Jinsi alivyokuwa maskini kwa ajili yenu, ingawa alikuwa tajiri, ili kwamba ninyi mpate kuwa matajiri kwa umaskini wake. 2 Wakorintho 8:9
25-0128
53-0831 – Mungu Alinena na Musa
Makanisa leo hii, mengi yao, yanatafuta wachanganyishaji. Mtu fulani anayeweza kuchanganyisha na labda kufanya kidogo hili na lile, na tafrija ndogo, na kucheza gofu, na labda karamu chache na kadhalika.
Sasa, ulimwengu unatafuta wachanganyishaji wazuri, lakini Mungu anatafuta watenganyishaji, wale watakaojitenga wenyewe. “Tokeni kati yao, enyi watu wangu, msishiriki dhambi zao.” Jitenge…
Huko Misri, wakati mwana-kondoo alipotolewa, Mungu aliweka utofauti. Aliwatenga—Waisraeli kutoka kwa—kutoka kwa Mataifa, na kufanya tofauti kati yao. Na watu wa Mungu ni watu waliotengwa, taifa takatifu, watu wateule, wa kipekee, wenye kutenda kiajabu.
Kwa hivyo ulimwengu hautawaelewa kamwe. Kwa hiyo msiwazie juu ya ulimwengu; wazieni juu ya Mungu. Hilo ndilo jambo kuu.
MKATE WA KILA SIKU
Basi Lutu akajichagulia Bonde lote la Yordani; Lutu akasafiri kwenda upande wa mashariki; wakatengana wao kwa wao. Mwanzo 13:11
25-0127
53-0831 – Mungu Alinena na Musa
Makanisa leo hii, mengi yao, yanatafuta wachanganyishaji. Mtu fulani anayeweza kuchanganyisha na labda kufanya kidogo hili na lile, na tafrija ndogo, na kucheza gofu, na labda karamu chache na kadhalika.
Sasa, ulimwengu unatafuta wachanganyishaji wazuri, lakini Mungu anatafuta watenganyishaji, wale watakaojitenga wenyewe. “Tokeni kati yao, enyi watu wangu, msishiriki dhambi zao.” Jitenge…
Huko Misri, wakati mwana-kondoo alipotolewa, Mungu aliweka utofauti. Aliwatenga—Waisraeli kutoka kwa—kutoka kwa Mataifa, na kufanya tofauti kati yao. Na watu wa Mungu ni watu waliotengwa, taifa takatifu, watu wateule, wa kipekee, wenye kutenda kiajabu.
Kwa hivyo ulimwengu hautawaelewa kamwe. Kwa hiyo msiwazie juu ya ulimwengu; wazieni juu ya Mungu. Hilo ndilo jambo kuu.
MKATE WA KILA SIKU
Basi Lutu akajichagulia Bonde lote la Yordani; Lutu akasafiri kwenda upande wa mashariki; wakatengana wao kwa wao. Mwanzo 13:11
25-0126
61-0108 – Ufunuo, Mlango Wa Nne Sehemu Ya III
Pia, Mungu, ninapoenda huko nje hudumani kukabiliana na adui, jalia nitambue ya kwamba nimezingirwa kila saa kwa maombi. Loo, jinsi ninavyoitegemea ngome hiyo, adui akikaribia, bali najua ya kwamba ngome hiyo inashikilia kwa maana akina mama na baba, na wavulana kwa wasichana, Wakristo, waliozaliwa mara ya pili na wenye ujuzi, watu wanaoelekea Mbinguni wako magotini mwao wakiomba, “Ee Mungu, tupe ukombozi!” Pia, Baba, tunaomba ya kwamba Wewe utatujalia kutoka kwenda katika kambi za adui huko nje na kushinda kila nafsi ya thamani inayongojea. Litekeleze, Bwana, na uwatoe gizani waingie kwenye Nuru. Kwa kuwa tunaomba katika Jina la Yesu. Amina.
MKATE WA KILA SIKU
Akawaambia mfano, ya kwamba imewapasa kumwomba Mungu sikuzote, wala wasikate tamaa. Luka 18:1
25-0125
58-0202 – Epukia Hapa, Njoo Upesi
Loo, ndugu, ni siku ilioje tunayoishi. Biblia ilisema katika siku hii ya kwamba (katika Timotheo wa Pili) “Roho anena waziwazi katika siku za mwisho watu watajitenga na imani, nao watakuwa wakaidi, na wenye kujivuna, wapendao anasa kuliko kumpenda Mungu.”
Nilikuja kanisani hivi majuzi; ilikuwa kuna theluji sana na kubaya kuja hapa. Lakini walikuwa na mchezo wa mpira wa kikapu, na iliwabidi wawafukuze mamia. Ni gani? Mungu wao ni mpira wa kikapu. Na ni yupi Mungu wenu basi? Kipande kikubwa cha hewa kilichopuzwa.
Ninayo furaha kwamba Mungu wetu ni Bwana Yesu Kristo katika Utu wa kufufuka Kwake, Muumba halisi aliye hai Aliyeziumba mbingu na dunia. Lakini wao wanataka kuliona jambo hilo. roho aliye ndani yao anavuta kwenye jambo hilo. Roho aliye ndani ya Mkristo humvuta kwa Kristo. “Mtu awezaje kuja Kwangu asipovutwa na Baba Yangu.”
MKATE WA KILA SIKU
Yafikirini yaliyo juu, siyo yaliyo katika nchi. Wakolosai 3:2
25-0124
58-0202 – Epukia Hapa, Njoo Upesi
Loo, ndugu, ni siku ilioje tunayoishi. Biblia ilisema katika siku hii ya kwamba (katika Timotheo wa Pili) “Roho anena waziwazi katika siku za mwisho watu watajitenga na imani, nao watakuwa wakaidi, na wenye kujivuna, wapendao anasa kuliko kumpenda Mungu.”
Nilikuja kanisani hivi majuzi; ilikuwa kuna theluji sana na kubaya kuja hapa. Lakini walikuwa na mchezo wa mpira wa kikapu, na iliwabidi wawafukuze mamia. Ni gani? Mungu wao ni mpira wa kikapu. Na ni yupi Mungu wenu basi? Kipande kikubwa cha hewa kilichopuzwa.
Ninayo furaha kwamba Mungu wetu ni Bwana Yesu Kristo katika Utu wa kufufuka Kwake, Muumba halisi aliye hai Aliyeziumba mbingu na dunia. Lakini wao wanataka kuliona jambo hilo. roho aliye ndani yao anavuta kwenye jambo hilo. Roho aliye ndani ya Mkristo humvuta kwa Kristo. “Mtu awezaje kuja Kwangu asipovutwa na Baba Yangu.”
MKATE WA KILA SIKU
Yafikirini yaliyo juu, siyo yaliyo katika nchi. Wakolosai 3:2
25-0123
62-0722 – Utuonyeshe Baba Yatutosha
Sasa, mti unapaswa kufanya nini? Unapoupanda, jambo pekee unalopaswa kufanya ni kuumwagilia maji, halafu hauna budi kunywa; majani yako ndani yake, matofaa yako ndani yake, ninii…kila kitu kiko moja kwa moja ndani ya mti huo, lakini unapaswa kunywa maji, hauna budi kunywa zaidi ya kipimo chake. Na unapokunywa, unasukuma nje, unasukuma majani nje, unasukuma maua nje, unasukuma nje matofaa; bali hauna budi kuendelea kunywa, kunywa, kunywa, upate kusukuma nje.
Nasi tunapochukua ahadi ya Mungu, na kuiingiza moyoni mwetu, tunaendelea kuimwagilia maji kwa imani, nayo inaendelea kusukuma nje, kusukuma nje. Haleluya! Kristo anapopandwa ndani ya moyo, Roho Mtakatifu, jambo pekee tunalofanya ni kunywa katika Neno hili la Mungu, Nalo linasukuma nje wokovu, linasukuma nje uponyaji wa Kiungu, linasukuma nje utukufu, linasukuma nje. Kila kitu tunachohitaji kiko moja kwa moja ndani yetu tunapopandwa katika Kristo Yesu.
Hii hapa tafsiri yangu juu Yake, kuhusu kuwa Maji: Yeye ni Chemchemi ya Uzima isiyokauka. Hutawahi kumwomba mengi kupita kiasi. Kamwe huwezi kumwamini kwa mambo makubwa kupita kiasi, anapendezwa na wewe kumwaminia mambo makubwa, huwezi kumwaminia makubwa kupita kiasi.
MKATE WA KILA SIKU
walakini ye yote atakayekunywa maji yale nitakayompa mimi hataona kiu milele; bali yale maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji, yakibubujikia uzima wa milele. Yohana 4:14
25-0122
61-0224 – Msiogope
Yesu alipokuwa Mungu aliyefanyika mwili, Utimilifu wa Mungu ulikuwa ndani Yake, Yeye alikuwa na Roho bila kipimo; sisi tunaye kwa kipimo. Sasa, vipi kama ukitoka nje hapa kuchota kijiko cha—cha maji kutoka baharini? Vema, hilo—hilo ndilo alilokuwa nalo Yesu, bahari nzima, lakini wewe na mimi tuna kijiko, hiyo ndiyo tofauti, hutalikosa kamwe. Si lazima Yeye awe nasi, lakini inatupasa sisi kuwa naye. Lakini kama ukichukua kijiko hicho cha maji na kukipeleka kwenye maabara, kemikali zilezile zilizo katika bahari nzima ziko kwenye kijiko hicho.
Na wakati Mungu, katika Siku ya Pentekoste, aliposhuka kama upepo wenye nguvu ukienda kasi, je! Uliona? Alikuwa ni Nguzo ya Moto. Lakini je! uliona Yeye alijitenga na ile Nguzo ya Moto, akajigawanya Mwenyewe kati ya watu Wake, na Ndimi za Moto zilizogawanyika zikakaa juu ya kila mmoja wao? Mungu akijitenga Mwenyewe kwa Kanisa Lake. Si ajabu Yeye alisema, “Popote walipo wawili ama watatu wamekusanyika katika Jina Langu, nitakuwa katikati yao.
MKATE WA KILA SIKU
Hapana Myahudi wala Myunani. Hapana mtumwa wala huru. Hapana mtu mume wala mtu mke. Maana ninyi nyote mmekuwa mmoja katika Kristo Yesu. Wagalatia 3:28
25-0121
64-0122 – Kumtazama Yesu
Sasa tunaona ya kwamba Mariamu alipata ufufuo na Uzima.
Vivyo hivyo Yairo, maskini kuhani, mwaminio wa kisiri, kwamba alipomwona Yesu na kumwangalia Yeye, alipata ufufuo na Uzima.
Watu wenye njaa walimwangalia Yeye, siku moja, na wakapata mkate wa kudumisha; mfano kwamba wenye njaa leo hii wanaweza kupata Mkate wa Uzima, si kupata kanuni ya imani. Humpati mwanzilishi, humpati mrekebishaji; unapata Uzima unapompata Kristo, Mkate wa Uzima.
Mwizi anayekufa alimwangalia Yeye, katika wakati wa dhiki, naye alipata nini? Alipata msamaha Wake. Ni nani mwingine angalimwangalia? Utawala wa Kirumi usingeweza kumsamehe. Hakuna mwingine yeyote angaliweza kumsamehe. Bali alimwangalia Yesu, katika dhiki yake, ndipo akampata Mtu aliyeweza kumsamehe.
Ndugu yangu, dada, usiku wa leo, ikiwa unaning’inia kama alivyokuwa wakati huo, katika mizani ya hukumu; huku ukijua, kama ungekufa, usiku wa leo, kama mshiriki vuguvugu wa kanisa, ama Mpentekoste vuguvugu, ama chochote kile uwezacho kuwa, unajua unakoelekea. Mwangalie Yeye, usiku wa leo, Yule awezaye kukuweka huru. Yule, usiku wa leo, kama wewe ni mshiriki tu, na hujui kile ufufuo wa Kristo unamaanisha kuishi katika moyo wa mwanadamu, mwangalie Yeye. Yeye ni Mungu, na Yeye pekee. Utapata msamaha kama vile huyu maskini, mwizi shupavu, aliyelowa dhambi alivyopata, huku amening’inia Msalabani.
MKATE WA KILA SIKU
Hapana Myahudi wala Myunani. Hapana mtumwa wala huru. Hapana mtu mume wala mtu mke. Maana ninyi nyote mmekuwa mmoja katika Kristo Yesu.
Wagalatia 3:28
25-0120
47-0412 – Imani Ni Kuwa Na Hakika
Na watu huniambia wana imani na kusema hawawezi kuamini katika uponyaji wa Kiungu? Enyi marafiki, kama huamini katika uponyaji wa Kiungu, umepotea. Hiyo ni kweli. Utafanyaje, kama huwezi kuwa na imani ya kutosha kwa Mungu kuuweka kiraka mwili huu ili kumtukuza ndani yake, ni jinsi gani utakuwa na imani zaidi ya kuamini ya kwamba Mungu atauchukua huu wa kale upatikanao na mauti kuufanya usiopatikana na mauti kutoka kwake kuutwaa juu? Huo ni uponyaji wa Kiungu wa moja kwa moja. Loo, jamani, kutakuwa na mambo ya kutisha ya kukatisha tamaa katika siku ya hukumu, kwenye ufufuo. Hiyo ni kweli.
MKATE WA KILA SIKU
Ila na aombe kwa imani, pasipo shaka yo yote; maana mwenye shaka ni kama wimbi la bahari lililochukuliwa na upepo, na kupeperushwa huku na huku. Yakobo 1:6
25-0119
61-0213 – Na Uzao Wako Utalimiliki Lango La Adui Zake
Mungu anapenda kuonyesha mkono wake wenye nguvu. Ndiyo, anafanya hivyo. Anapenda kuonyesha nguvu zake. Anangojea usiku wa leo kukuonyesha jambo hilo, kumchukua huyo mwenye dhambi na kumgeuza, kumchukua mwanamke huyo mwenye sifa mbaya na kumbadilisha awe mcha Mungu, mwanamke mtakatifu, kumchukua msichana huyo ambaye ameshika njia mbaya, mvulana huyo katika njia mbaya, kuwarudisha mahali, na kuwafanya wana na binti za Mungu kutoka kwao.
Yuko tayari kumchukua mtu huyo anayekufa kwa kansa, ambaye aliye na shida ya moyo, ambaye ni kipofu, yule anayeteseka, kama ataweka tu imani yake mle ndani ya kumgeuza kutoka mautini kuingia uzimani, amwanzishe na ushuhuda.
Anangoja kufanya jambo hilo, anakuweka moja kwa moja kwenye mtego ili kuona unachofanya. Aliwaweka moja kwa moja kwenye mtego ule pale, ilionekana kana kwamba maumbile yenyewe yalikuwa yameficha uso wake. Ndiyo.
Mwandishi mmoja alisema wakati mmoja, ya kwamba walipofika mahali pale, jiulize Musa angefanya nini. Walikuwa na amri moja, “Songa mbele.”
Ikiwa uko katika jukumu, haijalishi ni kitu gani kisimamacho njiani, uzoefu mkubwa zaidi ambao nimewahi kupata ni kulikabili jambo ambalo nisingeweza kulivuka, ama kupita chini yake, nasimama tu hapo na kutazama Mungu akifanya njia ya kulivuka. Hiyo ndiyo njia ya kulifanya, wewe songa mbele tu, endelea kusonga, sukuma pua yako kulikabili. Endelea kusonga tu, endelea tu kusonga mbele, Mungu atafanya njia.
MKATE WA KILA SIKU
Mungu wangu amemtuma malaika wake, naye ameyafumba makanwa ya simba, Danieli 6:22
25-0118
58-1221E – Umoja wa Mungu Mmoja Katika Lile Kanisa Moja
Loo, ni tofauti jinsi gani Kristo ajapo! Jinsi unaweza kuangalia nyuma na kuwazia, “Nilipataje kukaa mbali Nalo? Je, nilipataje kulikataa?” Kila kitu ni tofauti. Huna adui; wote wanaonekana watamu. Unaweza kusamehe kila kitu ambacho kimewahi kufanywa. Adui mbaya kuliko wote, ungeweza kumwombea barabarani, umkumbatie na kumwinua; haidhuru ni wa kanuni gani ya imani, yeye ni mfuasi wa dhehebu gani, yeye ni kiumbe ambaye Kristo alimfia. Huyo Ndiye Mungu anataka ujazwe naye. Huko ndiko kujaza. Huo ndio Ufalme. Hicho ndicho tulicho kitu kimoja ndani yake.
Sisi ni kitu kimoja, basi, sio—si kuendeleza dhehebu, si kuendeleza dini fulani potovu au—au kanuni fulani ya imani. Sisi ni kitu kimoja, kuuendeleza Ufalme wa Mungu. Ndipo tunachukua Ramani Yake, na, kila wakati Biblia iliyobarikiwa inaposema jambo lolote, Roho Mtakatifu ndani yako anapaza sauti, “Ni kweli! Ni Neno Langu!”
MKATE WA KILA SIKU
Kwa maana ndani yake yeye tunaishi, tunakwenda, na kuwa na uhai wetu… Matendo 17:28
25-0117
62-0122 – Kuthibitishwa Kwa Lile Agizo
Biblia ilisema, “Injili ilikuja kwetu sio kwa neno pekee, bali kwa nguvu, madhihirisho ya Roho Mtakatifu.” Kwa maneno mengine, “Ni Roho Mtakatifu akilichukua Neno la Mungu na kulidhihirisha.” Mnaona? Na, vinginevyo, njia pekee ambayo ishara za Marko 16 zingeweza kufuata mwaminio ni kwamba Roho Mtakatifu Mwenyewe alichukue Neno la Mungu na kulidhihirisha kwa watu. Jambo ndilo hilo. Sasa, imani hulifanya Neno hilo liishi. Mnaona?
Neno ni Mungu. “Hapo mwanzo alikuwako Neno, huyo Neno alikuwa pamoja na Mungu, naye Neno alikuwa Mungu.” Ndipo Yesu akasema, “Mkikaa ndani Yangu, na Neno Langu ndani yenu, ombeni mtakalo, mtatendewa.” Mnaona? Hiyo ni kukaa pamoja na Kristo katika Neno. Usiende kulia wala kushoto. Dumu moja kwa moja pamoja nalo. Mnaona? Ndipo basi silo Neno lako hasa, basi. Ni Neno Lake, nalo Neno Lake lina nguvu na mamlaka nyuma Yake.
MKATE WA KILA SIKU
Basi, ndugu zangu wapendwa, mwimarike, msitikisike, mkazidi sana kutenda kazi ya Bwana sikuzote, kwa kuwa mwajua ya kwamba taabu yenu siyo bure katika Bwana. 1 Wakorintho 15:58
25-0116
64-0726E – Mabirika Yavujayo
Ama, wakati mmoja wakati ufufuo wa Kiwelshi ulikuwa unaendelea, kulikuwa na watu mashuhuri kutoka Marekani. Madaktari wengi wa Elimu ya Kiungu walikwenda Welshi, kutafuta ni wapi na kuna nini. Kwa hiyo walikuwa na kosi zao zilizopinduliwa, na kofia zao zenye kizibo, nao walikuwa wakishuka kwenda barabarani.
Basi huyu hapa maskini polisi anakuja, akiizungusha fimbo yake ndogo mkononi mwake, huku anapiga mruzi, “Pale msalabani alipofia Mwokozi wangu, hapo nililia nipate kusafishwa na dhambi; hapo Damu ilipakwa moyoni mwangu, Jina Lake litukuzwe,” huku anatembea barabarani.
Kwa hiyo wakasema, “Huyu anaonekana kuwa mtu wa dini. Tutaenda kumuuliza.”
Nao wakasema, “Bwana!”
Kasema, “Naam, bwana?”
Akasema, “Tumekuja hapa kutoka Marekani. Sisi ni wajumbe. Tumekuja hapa kuchunguza ufufuo wa Kiwelshi, kama unavyoitwa. Sisi ni Madaktari wa Elimu ya Kiungu, na tuko hapa kuuchunguza.” Akasema, “Tunataka kujua mahali ulipo huo ufufuo, na mahali unapofanyika.”
Akasema, “Bwana, mmekwishafika. Mimi ndimi ufufuo wa Kiwelshi.” Amina! “Ufufuo wa Kiwelshi umo ndani yangu. Umo humu.”
Hiyvo ndivyo ilivyo unapoishi karibu na ile Chemchemi ya Maji ya uzima. Hayo ni hai sikuzote, yakibubujika na kububujika, kububujika na kububujika. Hayaishi.
MKATE WA KILA SIKU
Hunihuisha nafsi yangu. Zaburi 23:3
25-0115
55-0223 – Ayubu
Mungu anafanya mambo yote pamoja kwa ajili ya mema kwa wale wanaompenda, nawe unawezaje kutokufaulu? Huwezi tu kutokufaulu; hakuna njia ya kutokufaulu.
Kanisa lingeweza tu kujua jambo hilo. Kama ungeweza kupapata mahali pako katika Kristo, basi mambo haya mengine yote yangefifia tu kama kivuli. Kila mtu anayemjia Mungu, hiyo ni kweli, huna budi kuwa na vivuli vyako, na majaribu, na woga, na kadhalika, lakini usifadhaike tu juu yake. Ni kitu gani mateso kidogo kwa kitambo kidogo, tukijua ya kwamba utukufu wa Mungu utafunuliwa katika siku za mwisho wakati Yesu atakapokuja, wakati sisi tutakapofanana na Yeye? Anafanya kazi tu kila kitu pamoja. Je! Ulijua, labda kama ulikuwa mgonjwa, jambo fulani lilikutokea, ambalo huenda Mungu alilazimika kufanya hivyo ili tu kukuleta karibu zaidi Naye?
MKATE WA KILA SIKU
Kwa kuwa sasa twaishi, ikiwa ninyi mnasimama imara katika Bwana. 1 Wathesalonike 3:8
25-0114
65-1205 – Mambo Yatakayokuwapo
Yesu aliomba jambo moja tu, katika ombi Lake kwa Baba. Unajua lilikuwa ni nini? Jambo moja, baada ya dhabihu yake yote aliyotoa hapa duniani, maisha aliyoishi, njia aliyofuata. Aliomba jambo moja. “Kwamba nilipo Mimi, nao wawepo.” Yeye aliomba ushirika wetu. Hicho ndicho kitu pekee alichomwomba Baba katika maombi, ushirika wenu milele. Kama ukitaka kusoma jambo hili katika Yohana 17, na kifungu cha 24. Basi tunapaswa kumhitaji jinsi gani?
MKATE WA KILA SIKU
hao ulionipa nataka wawe pamoja nami po pote nilipo, wapate na kuutazama utukufu wangu ulionipa; kwa maana ulinipenda kabla ya kuwekwa msingi ulimwengu. Yohana 17:24
25-0113
59-1216 – Roho Mtakatifu Ni Nini?
Nikasema, “Shetani, wewe unayezungumza na dhamira yangu, ningetaka kukuuliza mambo machache. Ni nani ambaye wale manabii wa Kiebrani walinena kwamba Yeye angekuja? Ni nani aliyekuwa Masihi mtiwa mafuta? Ni nini kilikuwa juu ya watu hao waliomwona Yeye hapo awali na kusema habari za maisha Yake, maelfu ya miaka kabla Yeye hajafika hapa? Ni nani aliyetabiri jambo hilo kwa usahihi kabisa? Na hapo alipokuja, wao walisema, ‘Alihesabiwa pamoja na wakosaji,’ Naye alihesabiwa. ‘Alijeruhiwa kwa makosa yetu,’ na alijeruhiwa. ‘Alifanya kaburi Lake pamoja na matajiri, lakini Yeye angefufuka, siku ya tatu,’ Naye akafufuka. Kisha aliahidi Roho Mtakatifu, nami ninaye Huyo. Kwa hiyo ni afadhali uliondokee jambo Hilo, kwa kuwa imeandikwa katika Neno, na kila Neno ni kweli.” Ndipo akaondoka. Mpe tu Neno; hilo linatosha. Yeye hawezi kuvumilia Neno hilo, kwa kuwa limevuviwa.
MKATE WA KILA SIKU
Naye akajibu akasema, Imeandikwa, Mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu. Mathayo 4:4
25-0112
63-0628M – Ee Bwana, Mara Moja Tu Zaidi
Hamna historia yoyote, mahali popote, ambapo kanisa lolote lililopata kuundiwa dhehebu, ila lililoanguka, na kila moja lililoanguka, halikuinuka tena.
Wana wa Israeli, katika mfano, walipaswa kuifuata ile Nguzo ya Moto. Na kila usiku hawana budi kuwa tayari, sio kujiundia dhehebu na kuketi chini hapa, bali kuambatana na ule Moto.
Hivyo ndivyo Mungu anavyowataka watu Wake kufanya, kuambatana na Roho, kufuatana na wakati!
Mnasema, “Vema, Ndugu Branham, tumekuwa na kila namna ya mvua, na mvua za ndani na mvua za nje.” Ninyi mna akili. Sijali ni ufunuo wa aina gani, na jinsi unavyoonekana mzuri, kama haulingani na Neno la Mungu, achana nao. Hii ndiyo ramani ya kupitia nyikani, Neno la Bwana.
MKATE WA KILA SIKU
Sasa, basi, hakuna hukumu ya adhabu juu yao walio katika Kristo Yesu. Warumi 8:1
25-0111
56-0728 – Kufanya Bonde Lijae Mahandaki
Nionyeshe marafiki zako, nitakuambia wewe ni nani. Hebu niingie nyumbani mwako. Hebu acha nione kile kilichowekwa wazi mezani. Hebu nione jinsi Biblia hiyo ilivyowekwa alama. Hebu nione ziko wapi hizo Hadithi za Kweli. Hebu nisikilize ni aina gani ya muziki unauoleta kwenye redio yako. Hebu nione ni aina gani ya picha ulizonazo nyumbani mwako. Nitakuambia umefanywa kwa kitu gani. Ndiyo, bwana. Hayo ndiyo roho yako inakula. Bila kujali ushuhuda wako ukoje, matunda yako yanathibitisha ulivyo. Kweli.
Lo, ni ukweli. Nafsi yako inalishwa kwa kitu fulani. Na vyovyote tabia ya nafsi yako ilivyo, hivyo ndivyo itakavyo—itajidhihirisha. Hiyo ndiyo sababu Yesu alisema, “Kwa matunda yao mtawatambua.”
MKATE WA KILA SIKU
Ndiposa kwa matunda yao mtawatambua. Mathayo 7:20
25-0110
64-0207 – Mzee Ibrahimu
Sasa, Ibrahimu alikuwa mtu wa kawaida tu, hakuwa kitu maalum. Mungu hakumwita kamwe, kadiri tulivyo na kumbukumbu yake, hadi alipokuwa na umri wa miaka sabini na mitano. Mkewe, ambaye, alikuwa dada wa kuchangia mzazi, akiwa na miaka sitini na mitano wakati huo, labda waliishi pamoja tangu walipokuwa vijana sana.
Naye alikuwa tasa, na hakuwa na watoto. Mungu aliagiza utengano kamili, kujitenga wenyewe na ulimwengu, na watu wake wote, na jamaa yake yote. Kulikuwa na jambo maalum kwa yeye kutenda.
Na wakati Mungu anapokutazamia wewe kutenda jambo maalum, Yeye hutaka ujitenge kabisa na shaka yo yote. Yakubidi ufikie utii mkamilifu, kutii asemalo. Mungu hulitaka hilo. Huwezi ukalitenda kwa njia nyingine.
Na, sasa, Yeye sikuzote huweka mfano, na huo ulikuwa mfano Wake, wa kujitenga kabisa na familia yake yote, jamaa yake yote, na kadhalika, kutembea katika maisha yaliyotengwa kwa Mungu.
MKATE WA KILA SIKU
Kwa hiyo, Tokeni kati yao, Mkatengwe nao, asema Bwana, Msiguse kitu kilicho kichafu, Nami nitawakaribisha. 2 Wakorintho 6:17
25-0109
64-0207 – Mzee Ibrahimu
Sasa, Ibrahimu alikuwa mtu wa kawaida tu, hakuwa kitu maalum. Mungu hakumwita kamwe, kadiri tulivyo na kumbukumbu yake, hadi alipokuwa na umri wa miaka sabini na mitano. Mkewe, ambaye, alikuwa dada wa kuchangia mzazi, akiwa na miaka sitini na mitano wakati huo, labda waliishi pamoja tangu walipokuwa vijana sana.
Naye alikuwa tasa, na hakuwa na watoto. Mungu aliagiza utengano kamili, kujitenga wenyewe na ulimwengu, na watu wake wote, na jamaa yake yote. Kulikuwa na jambo maalum kwa yeye kutenda.
Na wakati Mungu anapokutazamia wewe kutenda jambo maalum, Yeye hutaka ujitenge kabisa na shaka yo yote. Yakubidi ufikie utii mkamilifu, kutii asemalo. Mungu hulitaka hilo. Huwezi ukalitenda kwa njia nyingine.
Na, sasa, Yeye sikuzote huweka mfano, na huo ulikuwa mfano Wake, wa kujitenga kabisa na familia yake yote, jamaa yake yote, na kadhalika, kutembea katika maisha yaliyotengwa kwa Mungu.
MKATE WA KILA SIKU
Kwa hiyo, Tokeni kati yao, Mkatengwe nao, asema Bwana, Msiguse kitu kilicho kichafu, Nami nitawakaribisha. 2 Wakorintho 6:17
25-0108
60-1125 – Kongamano
Mtu fulani alisema si muda mrefu uliopita, kasema, “Si—sitaki kumsumbua Mungu, mwajua, ni—najua Yeye ana shughuli nyingi sana.”
Upuuzi.
“Si—sitaki kuninii…”
Vema, huwezi kumaliza baraka zake zilizo nyingi. Je! unaweza kuwazia samaki mdogo kama urefu wa nusu inchi, huko katikati ya Bahari ya Pasifiki akisema, “Afadhali ninywe maji haya kidogo-kidogo, maana huenda nikaishiwa”?
Je, unaweza kuwazia panya mdogo mwenye ukubwa hivi chini ya maghala makuu ya Misri akisema, “Afadhali nile, nijigawie nafaka mbili tu kwa siku msimu huu wa baridi, naweza kuishiwa kabla ya mavuno mapya”?
Huo ni ujinga. Vema, ni ujinga mara mbili zaidi, mara elfu zaidi, kufikiria unaweza kuzimaliza rehema za Mungu mwenye rehema. Mbona, Yeye anajaribu kuingiza njia Yake ndani yako. “Ombeni kwa wingi ili furaha yenu itimizwe.” Hakuna njia ya kumchosha Yeye.
Kama vile pampu, kadri unavyosukuma, ndivyo maji yanavyozidi kuwa safi. Lo, napenda hilo! Endelea tu kusukuma. “Kuishi kwenye mkondo ambapo Utukufu unapotoka.” Nalipenda hilo.
MKATE WA KILA SIKU
… Na kikombe changu kinafurika. Zaburi 23:5
25-0107
64-0401 – Kristo Aliyetambulishwa Katika Nyakati Zote
Yesu Bwana wetu alisema, “Kama ilivyokuwa katika siku za Lutu, ndivyo itakavyokuwa katika kule Kuja,” na angalieni, “wakati Mwana wa Adamu anafunuliwa, kutambulishwa,” Luka 17. “Wakati Mwana wa Adamu, katika siku za mwisho, anafunuliwa. Mwana wa Adamu akifunuliwa, Injili Yake inamtambulisha kama ilivyokuwa katika siku za Lutu.”
Angalia vile wanavyofanya sasa, mataifa yaliyopotoshwa. Loo, jamani! Waangalie walawiti, na angalieni yale tuliyo nayo sasa. Kanisa ni katika mchafuko. Taifa liko katika mchafuko, na kitu hicho chote. Mungu anakitapika, kutoka juu, chini ya ardhi. Kitu hicho chote ni mchafuko.
Kijiografia, na pia kimaumbile, jukwaa limeandaliwa. Si ni wakati wa Mungu kurudi katika mwili wa kibinadamu, “Neno lililo kali kuliko upanga ukatao kuwili, na linalotambua mawazo na makusudi ya moyo,” kujitokeza jukwaani, kumfanya Yesu Kristo yeye yule jana, leo, na hata milele! Ni Neno lililoahidiwa lililogawiwa kwa siku hii. Tunaishi katika siku hii, na Mungu yupo hapa pamoja na sisi, kulidhihirisha hilo na kulifanya kweli.
MKATE WA KILA SIKU
Hivyo ndivyo itakavyokuwa siku ile atakayofunuliwa Mwana wa Adamu. Luka 17:30
25-0106
64-0719M – Sikukuu Ya Baragumu
Na Biblia ilisema Yeye angefukuzwa kanisani, katika Wakati wa Saba wa Kanisa. Yeye angefukuzwa kanisani. Litakuwa jeusi kabisa, na liende…Linakuwa jeusi wapi? Linaingia katika utaratibu huu wa kidini, likaingia kwenye baraza hili la ekumenia, Baraza la Makanisa Ulimwenguni. Hilo…Yeye anatolewa nje kabisa. Neno Lake, wao hata hawawezi kukubaliana Nalo. Mnajua hawawezi. Hawawezi kukubaliana katika makundi yao madogo ya mtaa; wao watakubalianaje katika jambo Hilo? Kwa hiyo, wao wanachukua alama nyingine ya mnyama, sanamu ya mnyama. Kumbukeni, Biblia ilisema, “Kulikuweko na sanamu iliyofanyiwa yule mnyama.”
Na Marekani hii daima imekuwa namba kumi na tatu. Ilianza na mikoa kumi na mitatu, koloni kumi na tatu; nyota kumi na tatu, milia kumi na mitatu; namba kumi na tatu, na daima ni mwanamke. Inatokea katika sura ya kumi na tatu ya Ufunuo. Na, kwanza, ni mwana-kondoo; upole, uhuru wa kunena, uhuru wa dini, na kadhalika; halafu wanapokea mamlaka, na kunena kwa uwezo wote aliokuwa nao yule joka mbele yake. Ni nini? Yule joka alikuwa nini? Rumi. Mnaona, alikuwa na alama, sanamu ya mnyama, iliyoinuka dhidi ya Kanisa halisi la Mungu. Chini ya hayo madhehebu, watakitesa kitu hiki! Lakini, watakapoanza kufanya jambo hilo:
Mwana-Kondoo atamchukua Bibi-arusi Wake awe daima karibu Naye…
MKATE WA KILA SIKU
Na watu wote wakaao juu ya nchi watamsujudu, kila ambaye jina lake halikuandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo, aliyechinjwa tangu kuwekwa misingi ya dunia. Ufunuo 13:8
25-0105
60-0308 – Upambanuzi Wa Roho
Haidhuru yeye ni mwalimu mkuu jinsi gani, jinsi alivyo na nguvu, jinsi alivyo mwenye akili, au karama yake inavyotenda kazi, ikiwa hajaribu kufanikisha jambo fulani kwa faida ya Mwili wa Kristo, upambanuzi wako wa kiroho ungekwambia ya kwamba hilo ni kosa. Haidhuru jinsi ilivyo sahihi, jinsi ilivyo kamilifu, jinsi ilivyo, ni makosa ikiwa haitumiwi kwa ajili ya Mwili wa Yesu Kristo.
Kupata kitu, huenda ikawa ana karama kuu ambayo anaweza kuwavutia watu pamoja kwa akili kuu au kwa nguvu za kiroho, ambazo kwazo angeweza kuwavuta watu pamoja, na huenda ikawa anajaribu kutwaa karama hiyo na kujifanya mwenyewe mashuhuri, ili kwamba atakuwa na jina kubwa, hivi kwamba ndugu wale wengine watamtazama yeye kama mtu fulani mkubwa. Basi hilo ni kosa. Huenda ikawa yeye anajaribu ku—kujenga jambo fulani hapa ambapo anataka kila mtu aondoke kwenye picha na kumwachilia yeye na kundi lake wawe ndio picha. Hilo bado ni kosa, mwaona.
Lakini iwapo ana karama ya Mungu naye anajaribu kuujenga Mwili wa Kristo, basi sijali anatokana na nini. Wewe humpambanui huyo mtu, unapambanua roho, uhai ulio ndani ya huyo mtu. Na hivyo ndivyo Mungu alituambia tufanye.
MKATE WA KILA SIKU
Wapenzi, msiiamini kila roho, bali zijaribuni hizo roho, kwamba zimetokana na Mungu; kwa sababu manabii wa uongo wengi wametokea duniani. 1 Yohana 4:1
25-0104
62-0714 – Sauti Isiyojulikana
Sasa, lakini ikiwa kuna swali…Wanaume waje, waseme, “Je, unafikiri ni kosa kuvuta sigara?”
“Kwa nini kuuliza hilo? Likiwa ni swali niani mwako, achana nalo.” Kwa kuwa chochote usichofanya kwa imani ni dhambi. Kweli. Inabidi iwe ni kwa imani. Basi unawezaje kuvuta sigara na kuwa na imani? Unaona? Ni…Moja kwa moja katika dhamiri yako mwenyewe, inakuonyesha kwamba umekosea. Kwa hivyo ikiwa si la hakika, afadhali uachane nalo, maana hilo linaweza kuwa ndilo jambo moja linalokuweka nje ya Ufalme wa Mungu.
“Loo,” unasema, “Ndugu Branham, jambo moja dogo kama hilo?”
Kitu kimoja kidogo kama hicho kitalisababisha, kutotii tu amri moja ya Mungu.
MKATE WA KILA SIKU
Wala msimhuzunishe yule Roho Mtakatifu wa Mungu; ambaye kwa yeye mlitiwa muhuri hata siku ya ukombozi. Waefeso 4:30
25-0103
53-0405S – Nendeni, Mkawaambie Wanafunzi Wangu
Hivyo ndivyo ilivyo kwa kila mwanaume au mwanamke, anapozaliwa kwa Roho wa Mungu, na kuona ufufuo wa kweli. Hakuna mtu ajuaye ya kuwa Yesu amefufuka katika wafu, isipokuwa amekufa, yeye mwenyewe, katika Kristo Yesu, na kuzaliwa mara ya pili, upya na Roho Mtakatifu. Kila mtu anaamini tu kitheolojia, anaamini tu kinyenzo, anaiangalia tu kwenye karatasi, mpaka Roho Mtakatifu ametoa ushuhuda wa kufufuka kwa Yesu Kristo. Wewe, kutoka kwa vitu vilivyokufa vya maisha, hadi kwenye tumaini jipya na lililo hai katika Kristo Yesu. Kila mwanamume au mwanamke asiye na hilo amepotea, asubuhi ya leo. Hiyo ni kweli.
Loo, ndugu yangu, dada, kuwa sawa na Mungu. Safisha moyo huo, kufikia ambapo kengele za furaha za Mbinguni zinalia, na kuna ufufuo; Yesu anaishi na kutawala moyoni.
MKATE WA KILA SIKU
Kama katika maisha haya tu tumemtumaini Kristo, sisi tu maskini kuliko watu wote. 1 Wakorintho 15:19
25-0102
NUKUU YA LEO! Tarehe 02/01/2025. Alhamisi.
56-0219 – Kuongozwa na Roho Mtakatifu
Na leo hii, hilo ndilo jambo siku hizi tunapowaona watu, na watu wana hali katika siku hii kuruka kitu kidogo cha maua, mpaka inakufanya kushangaa wakati fulani. Usifikiri juu ya-mtu mmoja kuwa zaidi ya mwingine. La, bwana, haidhuru yeye ni nani, kama yeye ni maskini mzee tu hapa nje akitoa trakti mitaani, na ikiwa yeye ni—Billy Graham.
Haijalishi yeye ni nani, ikiwa yeye ni mtumishi wa Mungu, waheshimu wote sawa, kila mmoja. Usiwe na mmoja aliye zaidi ya mwingine na wapendwao. Hatuna jambo hilo. Usifanye hivyo. Na usimheshimu mtu mmoja zaidi ya mwingine. Kuwa…Hebu—hebu kila mtu na awe kwenye kiwango.
Na ndugu na dada, katika Jina la thamani la Yesu, tafadhali mwazieni ndugu yenu mnyenyekevu kama aliye chini zaidi kati ya hao ndugu. Mnaona? Ni kama vile…si—sisemi hivyo ili niwe mnyenyekevu. Ninasema hivyo kutoka moyoni mwangu kwa sababu ninamaanisha. Ni Yesu Kristo ambaye ninajaribu kumwakilisha kwenu (mnaona?), Yesu Kristo Mwana wa Mungu.
MKATE WA KILA SIKU
Bali mkiwapendelea watu, mwafanya dhambi na kuhukumiwa na sheria kuwa wakosaji. Yakobo 2:9
25-0101
53-0405E – Mashahidi
Yesu alijua, kabla mitume hawa hawajaweza kutoka na kuwa mashahidi wa kweli, kwamba iliwabidi kupata tukio la yale waliyokuwa wakishuhudia. Hilo si lingekuwa jambo zuri, leo hii, kama kila seminari ingefanya jambo lile lile, kama kila Mkristo angefanya jambo lile lile? Angekuja tu kanisani na kusema, “Sasa ninamkubali Yesu kama Mwokozi wangu binafsi. Nitakaa papa hapa mpaka nipate ubatizo wa Roho Mtakatifu, kisha nitatoka niwe shahidi.” Mnaona? Mambo yangekuwa tofauti. Je, hamfikirii hivyo? Tusingekuwa na shuhuda hizo zilizolegea, zilizotawanyika.
Watu hushuhudia na kusema wao ni Mkristo, na kutoka nje na kuishi maisha mengine. Naye asiyeamini anaingia na kuona hayo, anasema, “Vema, angalieni pale! Hivyo ndivyo wao…” Naye ibilisi sikuzote atawaelekezea kidole, pia. Unaweza tu kutegemea hilo. Yeye ni mfanyabiashara. Wala usidharau uwezo wake na milki zake za kibiashara, kwa sababu anajua yote yanahusu nini.
MKATE WA KILA SIKU
Mnadhihirishwa kwamba mmekuwa barua ya Kristo tuliyoikatibu, iliyoandikwa si kwa wino, bali kwa Roho wa Mungu aliye hai; si katika vibao vya mawe, ila katika vibao ambavyo ni mioyo ya nyama.
2 Wakorintho 3:3