25-1026 Tazama Aliko Yesu

UJUMBE: 63-1229E Tazama Aliko Yesu

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Wasikilizaji Wa Kanda,

Wakati umefika ambapo kila mtu lazima ajiulize mwenyewe: “Ninapozisikiliza kanda, ni Sauti gani ninayoisikia? Je! ni sauti ya William Marrion Branham tu, au ninaisikia Sauti ya Mungu ya siku yetu? Je! ni neno la mwanadamu, au ninaisikia Bwana Asema Hivi? Je! ninamhitaji mtu fulani wa kunifasiria kile ninachokisikia, au Neno la Mungu halihitaji fasiri yoyote?”

Jibu letu ni: Tunasikiliza Neno Lililonenwa lililofanyika mwili. Tunamsikiliza Alfa na Omega. Tunamsikiliza Yeye, ile Nguzo ya Moto, akizungumza kupitia midomo ya mwanadamu kama alivyosema angefanya katika siku yetu.

Sisi hatumsikii mwanadamu, tunamsikia Mungu, yeye yule jana, leo, na hata milele. Sauti ya Mungu iliyo hai, yenye nguvu kuliko upanga ukatao kuwili, yenye kukata hata kuugawanya mfupa, na kuyatambua mawazo yaliyo moyoni.

Imefunuliwa kwetu ya kwamba kile Yeye alichokuwa wakati alipotembea Galilaya ni jambo lile lile alilo usiku wa leo huku Jeffersonville; jambo lile lile Yeye alilo kwenye Maskani ya Branham. Ni Neno la Mungu likidhihirishwa. Kile alichokuwa wakati huo, ndicho alicho usiku wa leo, na atakuwa hivyo milele. Kile alichosema angefanya, amekifanya.

Mtu huyo si Mungu, lakini Mungu angali anaishi na kuzungumza na Bibi-arusi Wake kupitia mtu huyo. Sisi hatuthubutu kumwabudu mtu huyo, bali tunamwabudu Mungu aliye katika mtu huyo; kwa maana yeye ndiye mtu ambaye Mungu alimchagua kuwa SAUTI YAKE na kumwongoza Bibi-arusi Wake katika siku hizi za mwisho.

Kwa sababu Yeye ametupa Ufunuo huu mkuu wa wakati wa mwisho, tunaweza sasa kujitambua SISI NI NANI, Neno lililofanyika mwili katika siku yetu. Shetani hawezi tena kutulaghai, kwa maana tunajua sisi ni Bibi-arusi Neno bikira Wake aliyerejeshwa kikamilifu.

Sauti hiyo ilituambia: Yote tunayohitaji TAYARI tulikwishapewa. Hakuna haja ya kusubiri. Lilishanenwa, NI YETU, NI MALI YETU. Shetani hana uwezo juu yetu; ameshindwa.

Hakika, Shetani anaweza kututupia magonjwa, huzuni, na maumivu ya moyo, lakini Baba Yeye tayari amekwisha kutupa uwezo wa kumfukuza ATOKE…TUNANENA NENO TU, naye hana budi kuondoka….si kwa Sababu sisi tunasema hivyo, bali kwa sababu MUNGU ALISEMA HIVYO.

Mungu yeye yule aliyewaumba kindi, wakati hapakuwa na kindi. Yule aliyempa Dada Hattie haja ya moyo wake: wanawe wawili. Yule aliyemponya Dada Branham uvimbe kabla ya mkono wa daktari haujamgusa. Yeye ni MUNGU YULE YULE ambaye si tu kwamba yuko pamoja nasi, BALI ANAISHI NA KUKAA NDANI YETU. SISI NI NENO LILILOFANYIKA MWILI.

Tunapotazama na kusikiliza Sauti iliyo kwenye kanda, tunaona na kumsikia Mungu akijifunua katika mwili wa mwanadamu. Tunaona na kusikia ni nani aliyetumwa na Mungu kutuongoza kwenda kwenye Nchi ya Ahadi. Tunatambua ni Bibi-arusi peke yake ndiye atakayekuwa na Ufunuo huo, kwa hiyo tumekuwa tusioogopa. Hakuna haja ya kuwa na wasiwasi, kufadhaika, kuchanganikiwa, kushangaa au kuhofu…SISI NDIO BIBI-ARUSI.

Sikiliza uishi, ndugu yangu, ishi!
Msikilize Yesu sasa upate kuishi;
Kwa maana Imerekodiwa kwenye kanda, haleluya!
Ni kwamba tu tusikilize tupate kuishi.

Loo, Bibi-arusi wa Yesu Kristo, ni siku iliyo kuu jinsi gani tunayoishi. Tunayongojea, dakika baada ya dakika. Siku yoyote tu sasa tutawaona wapendwa wetu, kisha, katika dakika moja, kufumba na kufumbua jicho, tutaondoka mahali hapa na pamoja nao ng’ambo ya pili. Hilo liko karibu sana yaonekana tunaweza kulihisi…UTUKUFU!

Njooni enyi Bibi-arusi, hebu na tuungane kwa mara nyingine tena kwenye Sauti ya Mungu Jumapili hii saa 06:00 MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni saa 1 JIONI ya Afrika Mashariki) tunapomsikia Yeye akizungumza nasi Neno la Uzima wa Milele.

Ndugu. Joseph Branham

Ujumbe: 63-1229E Tazama Aliko Yesu

Maandiko:
Hesabu 21:5-19
Isaya 45:22
Zekaria 12:10
Yohana 14:12