25-1012 Kukata Tamaa

UJUMBE: 63-0901E Kukata Tamaa

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi Wa Kanda,

Sasa, ninyi watu kwenye kanda.

Bwana, tunawezaje kuanza kueleza kile maneno haya madogo sita yanachomaanisha kwetu sisi, Bibi-arusi wa Yesu Kristo? Ndio Ufunuo wa Ujumbe wa saa hii kwetu sisi. Ni Mungu akizungumza kupitia malaika-mjumbe Wake akimwambia Bibi-arusi Wake, “Ninajua mtadumu na Sauti Yangu. Ninajua Neno Langu lililo kwenye kanda hizi vile litakavyomaanisha kwenu. Ninajua mtakuwa na Ufunuo ya kwamba Jumbe hizi nilizozinena kwenye kanda ndio Ishara Yangu ya wakati huu.”

“Nimeiweka Sauti Yangu kwenye kanda hizi za sumaku; kwa maana Jumbe hizi hazina budi kulimalizia Neno lote. Kutakuwako na maelfu mara maelfu ambao wataisikia Sauti Yangu kwenye kanda nao watakuwa na Ufunuo ya kwamba hii ndiyo huduma Yangu. Ndio Roho Mtakatifu wa wakati huu. Ndio Ujumbe Wangu ulio Ishara”

“Nimewatuma wahudumu wengi waaminifu ulimwenguni kote kuitangaza huduma Yangu. Waliporudi, waliniambia, ‘Tumeyatii maagizo Yako kwa kuzicheza kanda Zako. Tumewapata watu walioamini kila Neno. Wamezifanya nyumba zao wenyewe kuwa kanisa kuupokea Ujumbe Wako. Tuliwaambia, wote ambao wangekuja chini ya Ishara Yako, Ujumbe wa saa hii, wangeokolewa.’”

Ni wakati ambapo kila mtu lazima ajichunguze na kujiuliza, Ni ipi njia kamilifu ya Mungu ya siku hii? Neno la nabii halijashindwa hata wakati mmoja. Limethibitishwa kuwa ndiyo Kweli PEKEE, ndicho kitu PEKEE kitakachomuunganisha Bibi-arusi Wake.

Chochote yeye alichokisema kimetukia jinsi vile hasa alivyokisema. Nguzo ya Moto ingali hapa pamoja nasi. Sauti ya Mungu ingali inazungumza nasi kwenye kanda. Nabii amemaliza kutuambia ya kwamba Mungu angepita juu wakati tu atakapoiona ile Ishara. Ni wakati wa kudhikika kwa wote kuingia chini ya Ujumbe huo ulio Ishara.

Tumeuona Mkono mkuu wa Mungu katika wakati huu wa mwisho. Ametupa Ufunuo wa kweli wa Neno Lake nao umekuja chini ya ushahidi wa ile Ishara. Sasa, wakati tuwapo chini ya ushahidi wa ile Ishara, hebu na tukusanyike pamoja na kuula Ushirika kwa kudhikika; kwa maana tunajua kwamba Mungu yuko tayari kutoa hukumu.

Ningependa kuwaalika kila mmoja wenu kusikia na kuwa na Ibada ya Ushirika na Kutawadhana Miguu Miguu Jumapili hii, tunapousikia Ujumbe: Kukata Tamaa 63-0901E.

Ujumbe na Ibada ya Ushirika itakuwa kwenye Redio ya Sauti kuanzia saa 11:00 JIONI. Saa za Jeffersonville. Tafadhali jisikieni huru kuifanya ibada yenu saa 11:00 JIONI. Kwa masaa ya maeneo yenu mkipenda, kama nijuavyo itakuwa vigumu kwa waamini wetu wengi wa nchi za ng’ambo kuianza ibada yenu kwa wakati huo wa huku. Kutakuwa na anuani ya faili la kupakuliwa la ibada.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya ibada:

Kutoka 12:11
Yeremia 29:10-14
Luka 16:16
Yohana 14:23
Wagalatia 5:6
Yakobo 5:16