24-1117 Wakati Wa Kanisa La Sardi

UJUMBE: 60-1209 Wakati Wa Kanisa La Sardi

PDF

BranhamTabernacle.org

Wapendwa Watu Wa Kanda,

Tunajivunia jinsi gani kuitwa “Watu wa Kanda”. Mioyo yetu inaenda mbio kwa changamko kila wiki tukijua tutaungana pamoja ulimwenguni kote kwa kuisikia Sauti ya Mungu ikisema nasi.

Tunajua, bila chembe ya shaka hata moja, tuko katika Mapenzi makamilifu ya Mungu kwa sisi kukaa na Neno Lake; kuisikiliza Sauti Yake kwa njia ya malaika-mjumbe Wake wa saba mwenye nguvu.

Mjumbe Aliyemchagua kwa ajili ya siku yetu ni William Marrion Branham. Yeye ndiye taa ya Mungu kwa ulimwengu, inayoakisi nuru ya Mungu. Yeye anamwita Bibi-arusi Neno Safi Wake aliyechaguliwa atoke kupitia malaika Wake.

Kwa kujifunza kwa makini Neno Lake, Ametufunulia sisi kwa Roho Wake Mtakatifu kwamba William Marrion Branham ndiye malaika ambaye Yeye aliyemchagua kumpa Ufunuo Wake na Huduma Yake kwa ajili ya siku yetu. Tunamwona malaika Wake, NYOTA YETU, katika mkono Wake wa kuume huku akimpa nguvu Zake za kufunua Neno Lake na kumwita Bibi-arusi Wake atoke.

Yeye ametupa Ufunuo mzima wa Yeye Mwenyewe. Roho Mtakatifu akijitambulisha kwetu kupitia maisha ya malaika-mjumbe Wake wa saba; malaika aliyemchagua kuwa macho Yake kwa ajili ya siku yetu.

Jinsi gani mioyo yetu inavyowaka ndani yetu wakati anapotuambia kwa kila Ujumbe kwamba ni kusudi Lake kutuleta Kwake; ya kwamba sisi ni Bibi-arusi Neno Wake.

Yeye anapenda kutuambia mara kwa mara jinsi alivyotuchagua sisi kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu NDANI YAKE. Jinsi tulivyojulikana kimbele na kupendwa Naye.

Jinsi tunavyopenda kumsikia Yeye akinena na kutuambia tulikombolewa kwa Damu Yake na HATUWEZI kamwe kuja hukumuni. Hatuwezi kamwe kuwa katika hukumu, kwa sababu dhambi haiwezi kuhesabiwa kwetu sisi.

Jinsi tutakavyoketi pamoja Na Yeye wakati akichukua kiti chake cha enzi cha duniani cha Daudi, na kutawala pamoja Naye; kama tu Yeye alivyofanya mbinguni, pamoja na uwezo na mamlaka juu ya dunia nzima. Majaribu na majaribio ya maisha haya yataonekana kuwa si kitu wakati huo.

Lakini pia Yeye ametuonya jinsi gani tunavyopaswa kuwa waangalifu. Kwamba katika nyakati zote ile mizabibu miwili ilikua pamoja. Jinsi ambavyo adui daima amekuwa akifanana sana; mdanganyifu sana. Hata Yuda alichaguliwa na Mungu, na kufundishwa katika kweli. Alishiriki maarifa ya zile siri. Alikuwa na huduma ya nguvu aliyopewa naye akawaponya wagonjwa na kutoa pepo katika Jina la Yesu. Lakini yeye hakuweza kwenda hadi mwisho.

Huwezi kuendelea na sehemu tu ya Neno, huna budi kuchukua Neno LOTE. Kuna watu wanaoonekana wanahusika na mambo ya Mungu karibu asilimia mia moja, lakini sio.

Yeye alisema wala haitoshi kwamba Yeye amejihusisha na kanisa zima, ama hata na huduma tano ya Waefeso nne. Yeye alituonya kwamba katika kila wakati kanisa hupotoka, na wala si wafuasi tu bali na kundi la makasisi – wachungaji wako makosani na kondoo pia.

Kwa hiyo kwa shauri lililokusudiwa la mapenzi Yake Mwenyewe, Yeye amejitokeza Mwenyewe katika wakati wetu kama Mchungaji Mkuu katika huduma ya malaika-mjumbe Wake wa saba kuwaongoza watu Wake wairudie ile kweli na zile nguvu nyingi za kweli hiyo.

Yeye yuko ndani ya mjumbe Wake na yeye ambaye angekuwa na utimilifu wa Mungu angemfuata huyo mjumbe kama vile huyo mjumbe alivyo mfuasi wa Bwana kwa Neno Lake.

Ninataka kuwa na utimilifu wa Mungu na kumfuata mjumbe Wake. Hivyo, kwetu sisi, Maskani ya Branham, njia pekee ya kumfuata mjumbe kama vile yeye anavyomfuata Bwana kwa Neno Lake, ni KUBONYEZA PLAY na kuisikia Sauti ya Mungu Safi ikisema nasi maneno ya kutoweza kukosea.

Haitubidi kukisia au kukagua kile tunachosikia, inatubidi tu Kubonyeza Play na kuamini kila Neno tunalosikia.

Nilimsikia Ndugu Branham akisema maneno yafuatayo mapema asubuhi moja kwenye redio ya Sauti. Nilipolisikia Hilo, ikanijia moyoni mwangu kwamba hivi ndivyo Mimi / sisi tunavyojisikia kuhusu kusema:

TUNABONYEZA PLAY TU NA KUZISIKILIZA KANDA.

Ilisikika kama tamshi la Imani yetu kwangu mimi.

Hiyo ndiyo sababu ninaamini katika uponyaji wa Kiungu. Hiyo ndiyo sababu ninaamini katika maono. Hiyo ndiyo sababu ninaamini katika Malaika. Hiyo ndiyo sababu ninaamini Ujumbe huu, ni kwa sababu unatoka kwenye Neno la Mungu. Na chochote nje ya Neno la Mungu, sikiamini. Inaweza kuwa hivyo, lakini hata hivyo nitadumu tu na yale Mungu aliyosema, ndipo niwe na hakika kwamba niko sahihi. Sasa, Mungu anaweza kufanya atakalo. Yeye ni Mungu. Lakini maadamu ninadumu na Neno Lake, basi ninajua hilo ni sawa. Ninaamini hilo.

Utukufu, yeye alilisema KAMILIFU kweli. Huduma zingine zote zinaweza kuwa, kwa sababu Mungu anaweza kufanya atakalo, na yule Yeye anayemtaka kulifanya, Yeye ni Mungu. Lakini maadamu ninadumu na Neno Lake, Sauti Yake, Kanda, basi ninajua hilo ni sawa. Ninaamini hilo.

Ninajua wengi huzisoma barua zangu na kutoelewa kile Mimi ninachosema na kile ninachoamini kuwa ni Mapenzi ya Bwana kwa kanisa letu. Nami niseme tena kwa unyenyekevu kama vile nabii alivyosema: “Barua hizi zimekusudiwa kwa ajili ya kanisa langu peke yake. Wale wanaotamani kuiita Maskani ya Branham kanisa lao. Wale WANAOTAKA KUTAMBULISHWA NA KUITWA WATU WA KANDA”.

Ikiwa hukubaliani na yale ninayosema na ninayoamini, hiyo ni sawa asilimia 100% ndugu zangu na dada zangu. Barua zangu si kwa ajili yenu au dhidi yenu au kwa makanisa yenu. Kanisa lako linajitawala lenyewe nawe ni lazima ufanye kama vile unavyohisi kuongozwa kufanya, bali kulingana na Neno, ndivyo lilivyo na letu, na hiki ndicho sisi tunachoamini kuwa ndio njia iliyoandaliwa na Mungu kwa ajili yetu.

Wote mnakaribishwa kuungana nasi kila Jumapili saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville.( Ni Saa 2:00 MBILI USIKU ya Afrika Mashariki ) Wiki hii, Nyota ya Mungu ya wakati wetu, William Marrion Branham, atakuwa akituletea Ujumbe, 60-1209 Wakati wa Kanisa la Sardi.

Ndugu. Joseph Branham