25-1130 Kile Kipeo

UJUMBE: 64-0705 Kile Kipeo

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Kipeo Cha Mungu,

Uhai wote wa kweli uliokuwemo Katika ubua, kishada, na ganda, sasa unakusanyika ndani yetu, Uzao wa Kifalme wa Mungu, Vipeo Vyake, nasi tuko kwa ufufuo, tayari kwa mavuno. Alfa imekuwa Omega. Ya kwanza imekuwa ya mwisho, na ya mwisho sasa ndiyo ya kwanza. Tumepitia hatua fulani nasi tumekuwa Vipeo Vyake, kipande kilichokatwa kutoka Kwake.

Bibi-Arusi na Bwana-Arusi ni Mmoja!

Mungu alimwonyesha nabii Wake kule kuonekana kimbele kwa kila mmoja wetu tupate kukaguliwa, Vipeo Vyake, katika ono. Aliposimama pale na Bwana akimtazama Bibi-Arusi akipita mbele yake, Yeye Alimwona kila mmoja wetu. Sisi SOTE macho yetu yalikuwa yameelekezwa MOJA KWA MOJA KWAKE YEYE. Alisema tulikuwa watu walio wazuri mno aliopata kuwaona maishani mwake. Tulikuwa na madaha. Tulionekana wazuri mno kwake.

Kumbukeni, hili lilikuwa ni ONO la Bibi-Arusi; vile angeonekana, na kutuambia hasa kile alichokuwa akifanya. Sikilizeni kwa makini.

Yeye atatoka katika mataifa yote, kumkamilisha Bibi-arusi. Kila mmoja wao alikuwa na nywele ndefu na bila kujipodoa, nao ni wasichana wazuri sana. Nao walikuwa wakinitazama. Hao waliwakilisha Bibi-arusi akitoka katika mataifa yote. Mnaona? Yeye…Kila mmoja wao aliwakilisha taifa moja,* walipokuwa wakipiga hatua kikamilifu kulingana na Neno.

Bibi-Arusi, Hebu niliseme hilo tena, BIBI-ARUSI, kutoka kila taifa ati walikuwa wameyaelekeza macho yao kwa mchungaji wao, kundi la watu….HAPANA, hivyo sivyo alivyosema. Wao walikuwa wameyaelekeza macho yao KWA NABII, wakimtazama yeye.
Mradi tu waliyaelekeza macho yao kwa nabii, walikuwa wakipiga hatua kikamilifu. Lakini Kisha yeye anatuonya, jambo fulani lilitukia. Baadhi yao waliyaondoa macho yao kwake na kuanza kuangalia kitu kingine ambacho kiliingia katika machafuko matupu.

Halafu, yanipasa kumwangalia. Atakosa kupiga hatua kwa utaratibu wa hilo Neno nisipomwangalia, wakati anapopita, kama atanikaribia. Labda itakuwa wakati wakati wangu utakapokwisha (mnaona?), nitakapomaliza mwendo, ama cho chote kile.

Yampasa amwangalie, la sivyo atakosa kupiga hatua taratibu wakati anapopita. Lakini kisha anasema labda itakuwa ni wakati wangu, nitakapomaliza mwendo, wakati sipo hapa, Wanaweza kukosa kupiga hatua taratibu kwa kutoyaelekeza macho yao kwake.

Alikuwa akimwonya BIBI-ARUSI waziwazi, Hamna budi kuyaelekeza macho yenu kwenye Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda. Hiyo ndiyo njia iliyoandaliwa na Mungu ya siku hii. Hiyo ndiyo Sauti itakayomunganisha na kumkamilisha Bibi-Arusi. Ukiyaondoa macho na masikio yako kwenye Sauti, Utatoka mstarini na kuingia katika machafuko matupu.

Kila Ujumbe unakuwa wazi zaidi na zaidi. Ni Mungu aliye mkuu Akifunuliwa mbele zetu, akimlisha Bibi-Arusi Wake Mana Iliyofichwa ndiyo tu tunayoweza kula. Ni nono sana kwa wengine wote, bali ni Chakula Kilichofichwa kwa ajili ya Bibi-Arusi.

Ni wakati wa kutoa Shukrani uliyoje Bibi-arusi alionao, akila Neno, akifanyika Bibi-arusi Neno Wake Mkamilifu.

Anasimama peke yake, kama Bwana Arusi, amekataliwa na watu, amedharauliwa na kukataliwa na makanisa. Bibi-arusi yuko hivyo. Ni nini? Ni Kipeo Chake. Mnaona? Ni Neno Yeye analoweza kutendea kazi kwake na kulidhihirisha, likikataliwa.

Njooni muungane nasi Jumapili saa 6:00 MCHANA, saa za Jeffersonville,(ni saa 2 USIKU ya Afrika Mashariki) Wakati Mungu akizungumza kupitia malaika Wake mwenye nguvu, na kutukata na kutuadibisha ili tufanyike Kipeo cha Mungu.

Ndugu Joseph Branham

Ujumbe: 64-0705 Kile Kipeo

Maandiko ya kusoma kabla ya ibada:
Isaya 53:1-12
Malaki 3:6
Mathayo Mt. 24:24
Marko Mt. 9:7
Yohana Mt. 12:24 / 14:19