25-1109 Wa Kipekee

UJUMBE: 64-0614E Wa Kipekee

PDF

pakua – m4a

pakua – amr

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Mungu Aliye Na Ngozi,

Hatuko nyuma ya pazia tena, enyi watoto wadogo, Mungu ameonekana wazi kwetu. Yule Mungu mkuu wa Mbingu na nchi, ambaye daima amejificha Mwenyewe kwa watu kama Nguzo ya Moto ile iliyotoka kwa Mungu na kuishi katika mwili wa duniani unaoitwa Yesu; kisha akarudi kwenye ile Nguzo ya Moto na akamtokea Paulo njiani akielekea Dameski, sasa ameonekana tena wazi kabisa na akakaa tena katika mwili wa mwanadamu ndani ya malaika-Mjumbe Wake, William Marrion Branham, akimwita Bibi-arusi Wake atoke aende Kwake.

Mungu alimweka malaika Wake duniani kujiwakilisha Mwenyewe kama balozi Wake aliyechaguliwa kuingia katika mambo makuu yasiojulikana ya kimbinguni. Yeye anatambua na kuyaleta mambo ambayo akili ya kawaida haiwezi kuyaelewa. Alitumwa kuweka wazi siri ya Mungu na kutabiri mambo yaliyopo, na mambo ambayo yamekuwepo, na mambo ambayo yatakuwepo. Yeye ni Sauti ya Mungu kwa Bibi-arusi.

Ni nini? Mungu, Mungu nyuma ya ngozi, ngozi ya binadamu. Kweli hasa.

Watoa lawama wengi leo hawawezi kutuelewa sisi waaminio wa kweli. Kwao, sisi tumekuwa nati. Wanasema ati sisi ni waamini mungu-mtu tunamwabudu nabii…

Mtoa lawama, siku chache zilizopita, aliniambia, kule chini Tucson. Alisema, “Unajua, watu wengine hukufanya wewe nati, na wengine wanakufanya mungu.”
Nikasema, “Vema, jambo hilo liko sawa kwa namna fulani.” Nilijua anajaribu kunilaumu. Mnaona?
Yeye akasema, “Watu wanafikiri wewe ni mungu.”

Kama jinsi ilivyokuwa wakati Yesu alipokuwa hapa duniani, ni vivyo hivyo leo hii kwa nabii Wake. Watu hawako nyuma ya pazia; wao wamepofushwa kuihusu kweli. Sisi hatutaki lolote ila njia ya Mungu iliyoandaliwa kwa ajili ya siku hii: Yeye Mwenyewe akiwa amefunikwa katika mwili, Sauti ya Mungu iliyorekodiwa na kuhifadhiwa kwa ajili ya Bibi-arusi.

Mungu alipodhihirishwa ulimwenguni, Yeye alikuwa amejificha nyuma ya pazia, nyuma ya ngozi ya Mtu aliyeitwa Yesu. Yeye alikuwa ametiwa utaji na kujificha nyuma ya ngozi ya mtu aliyeitwa Musa, nao walikuwa miungu, si Mungu; bali walikuwa Mungu, yule Mungu mmoja, akibadilisha kinyago Chake tu, akifanya jambo lile lile kila wakati, akileta Neno hili. Mungu alilifanya jinsi hiyo.

Tumeingizwa tu na Neno, Ujumbe wa saa hii. Sasa imetufanya kuwa Neno lililofichwa nyuma ya mwili wa mwanadamu. Bibi-arusi na Bwana-arusi ni mmoja. Mungu ni mmoja, nalo Neno ni Mungu! Tumetiwa hesi kwa Neno.

La kusikitisha, utengano miongoni mwa waaminio leo ni kwamba wao wanahisi tunamtukuza sana nabii wa Mungu aliyethibitishwa. Kinyume chake, wao wanataka kuuweka uongozi huo juu ya wachungaji wao.

Mungu Yeye habadilishi mpango Wake; Anamtuma MTU MMOJA kumwongoza Bibi-arusi Wake. Ni Roho Wake Mtakatifu ndani ya kila mmoja wetu, akituongoza kwa NGUZO YA MOTO.

Neno humjia mmoja. Katika kila wakati, vivyo hivyo, hata katika nyakati za kanisa, tangu wa kwanza hadi wa mwisho. Wengine wana mahali pao, hiyo ni kweli, angalia, lakini kaeni mbali na hiyo Nguzo ya Moto. Unaona?

LAKINI TUNASIKIA NINI LEO…JAMBO LILE LILE.

Mnakumbuka yale Dathani na hao wengine waliyosema kule njiani? Walisema, “Sasa, Musa, hebu ngoja hapa kidogo tu! Unajitukuza sana, unaona. Sasa, wapo watu wengine hapa ambao Mungu amewaita.”

Sisi hatuwapingi wahudumu; Mungu amewaita, Lakini Enyi ndugu na dada, ikiwa mchungaji wenu haiweki Sauti ya Mungu Mwenyewe kuwa ndio Sauti iliyo muhimu zaidi mnayopaswa kuisikia kwa kuzicheza kanda kanisani mwenu, yeye hawaongozi kwenye Njia ya Mungu iliyoandaliwa.

Hiyo ni kweli. Wao, kila mmoja, walikuwa wakifuata vizuri mradi tu waliendelea mbele, lakini wakati mmoja alipojaribu kuinuka na kuchukua nafasi ya Mungu ambayo alikuwa amempa Musa, ambaye alikuwa amekusudiwa tangu zamani na kuchaguliwa kwa ajili ya kazi hiyo, alipojaribu kupachukua, moto ulishuka na ukaifunua nchi na kuwameza moja kwa moja ndani yake. Unaona? Unaona? Kuwa mwangalifu. Unaona?

Tunapaswa sote tuingizwe kwenye Neno hilo lililonenwa na kuwekwa kwenye kanda. Hilo ndio Yakini ya Mungu. Hilo ndilo Neno pekee ambalo Bibi-arusi anaweza kukubaliana kwalo. Wahudumu hawataweza kamwe kumuunganisha Bibi-arusi, ni Sauti ya Mungu iliyo kwenye kanda peke yake.

Mimi siwezi kufanya kitu bila ninyi; ninyi hamwezi kufanya kitu bila mimi; hakuna anayeweza kufanya kitu bila Mungu. Kwa hiyo, sote pamoja linafanya kitu kimoja, ule muungano. Mungu alinituma kwa kusudi hilo; mnaamini jambo hilo; na hapa linatendeka. Ndilo hilo hasa, mnaona, limehakikishwa kikamilifu.

Ni kwa pamoja TU ndipo inafanya KITU KIMOJA, ule muungano. Mungu alimtuma William Marrion Branham kwa kusudi hilo. Basi, ikiwa TU utaliamini Hilo, Litatendeka; limehakikishwa kikamilifu.

Si mimi ninayelisema hilo, Enyi ndugu na dada. NI MUNGU ANAYELISEMA HILO KUPITIA NABII WAKE. Msimruhusu mtu yeyote awaambieni tofauti ama kujaribu kuwafafanulieni kitofauti. NI SAUTI YA MUNGU ILIYO KWENYE KANDA TU NDIYO ITAKAYOMUUNGANISHA NA KUMKAMILISHA BIBI-ARUSI. KWA NJIA NYINGINE YOYOTE, HUTAKUWA BIBI-ARUSI.

Kwa hiyo nafikiri wengi wetu sisi watu wazima tunafikiria vivyo hivyo. Mungu, aliye na ngozi! Linaweza likasikika kama nati, kwa ulimwengu, bali linawavuta watu wote Kwake.

Mnasikia alichotoka kusema? Mungu aliye na ngozi anawavuta watu wote Kwake.

Wakati ulimwengu umetiwa hesi kwa ajili ya nati, sisi tumetiwa hesi kwa Sauti ya Mungu nasi tunaitwa Bibi-arusi. Inatuvuta kututoa katika mchafuko huu, kutuingiza katika Uwepo wa Mungu. Sisi ni nati tuliyotiwa hesi kwa Neno la Mungu.

Njooni na muingizwe kwenye Sauti ya Mungu pamoja nasi Jumapili hii saa 06:00 MCHANA, saa za Jeffersonville, (ni saa 2:00 USIKU ya Afrika Mashariki) huku Ikiwavuta watu wote Kwake.

Ndugu Joseph Branham

Ujumbe: Wa Kipekee. 64-0614E

Maandiko:

1 Wakorintho 1:18-25
2 Wakorintho 12:11