25-1005 Ile Ishara

UJUMBE: 63-0901M Ile Ishara

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi Wa Ile Ishara,

Tunapokutana pamoja, hatuzungumzi tu juu ya Ujumbe, tunakutana pamoja kuipaka ile Damu, kuiweka ile Ishara; nayo ile Ishara ni Ujumbe wa wakati huu! Huo ndio Ujumbe wa majira haya! Huo ndio Ujumbe wa wakati huu.

Tumeiweka hiyo Ishara kwetu sisi wenyewe, kwa nyumba zetu, na kwa familia zetu. Hatuonei haya. Hatujali nani anayeijua. Tunataka kila mtu aijue, kila mpita njia aione na ajue: Sisi ni Watu wa Kanda. Sisi ni Nyumba ya Kanda. Sisi ni Bibi-arusi wa Kanda wa Mungu.

Roho Mtakatifu = Ile Ishara = Ujumbe. Yote ni mamoja. Huwezi kuyatenganisha. Baba, Mwana, Roho Mtakatifu = Bwana Yesu Kristo. Huwezi kuwatenganisha.

Ujumbe = Mjumbe. Haidhuru wakosoaji wanasema nini, NABII ALISEMA, huwezi kuwatenganisha.

Mungu ndiye furaha yako. Mungu ndiye nguvu zako. Kuujua Ujumbe huu, Kujua ndio Kweli pekee, tukijua ndio ile Ishara, huo ndio utoshelevu wetu. Wengine waweza kusema, “Ninauamini, ninauamini, ninauamini kuwa ni Kweli. Ninaukubali kama Kweli.” Hayo yote ni mazuri, lakini hata hivyo haina budi kuwekwa.

Nabii alisema Ujumbe huu ndiyo ile Ishara ya wakati huu. Ujumbe huu ni Roho Mtakatifu. Kama unao Ufunuo wowote wa Ujumbe huu unaweza kuona waziwazi saa tunayoishi. Wengi sana wanasema, “Ninauamini. Mungu alimtuma nabii. Ni Ujumbe wa wakati huu,” lakini wao wanajigamba kwa kusema hawaichezi, na hawataicheza, Sauti yenyewe ya ile Ishara katika makanisa yao.

Mungu hakunena kupitia malaika Wake mwenye nguvu na kusema tu jambo fulani isipokuwa lilikuwa na maana. Alituambia yeye alitufundisha kwa mifano na vivuli. Katika Ujumbe huu, nabii anaeleza kwa kina sana kutuambia kile Rahabu na familia yake walichofanya ili WAOKOLEWE, kuwa Bibi-arusi. Alikuwa wazi juu ya kile yeye alichofanya.

Wakati wavulana wa kanda walipocheza “KANDA”…Hebu kidogo, mjumbe huyo alifanya nini? Alicheza Kanda. Kisha Rahabu akafanya nini? Aliifanya nyumba yake kuwa KANISA LA KANDA. Hakuonea haya kusema, “Mnaiona ile kamba nyekundu, hiyo inamaanisha kwamba mimi ni KANISA LA KANDA”.

Unadhani kama angalisema, “Ndiyo, ninamwamini mjumbe na Ujumbe, lakini sisi hatuzichezi Kanda tena kanisani mwetu. Ninaye mchungaji anayesema HAPANA, yeye anapaswa tu kuhubiri na kuyanukuu yale Kanda zinachosema.” Hivi unafikiri angeokolewa…???

Akaweka ile ishara, nayo nyumba yake ikaokolewa, ama angaliangamia kule chini alikokuwa.

Umewasikia wahudumu wengi wakitoa visingizio kuhusu kuzicheza kanda, lakini wengi wao husema: “Nabii hakusema kamwe kuzicheza kanda kanisani.”

Nabii alisema Rahabu aliifanya nyumba yake kuwa kanisa, nalo kanisa lake lilizicheza Kanda. Na kwa sababu alizicheza Kanda kanisani mwake, yeye, na Kanisa lake lote la KANDA, walikuwa chini ya ile Ishara na wakaokolewa. Kila kanisa lingine liliangamia.

Ndugu na dada, tafadhali, sisemi mchungaji hawezi kuuhubiri Ujumbe huu, au ni makosa kama anahubiri. Kwa njia yangu mwenyewe, ninahubiri sasa hivi kupitia barua hii, lakini ufungue moyo wako na usikilize kile nabii asemacho na kukuonya. Kama mchungaji wako hachezi, au hatazicheza, kanda kanisani mwenu kwa kutoa udhuru fulani; chochote kile, kulingana na Neno, haidhuru anasema vipi, ninauamini Ujumbe wa wakati huu, kulingana na kile ninachoamini Neno lisemavyo, ile Ishara, Ujumbe wa saa hii, haijawekwa.

Jumapili hii, ninawaalika mje msikilize pamoja na Maskani ya Branham saa 06:00 MCHANA, saa za Jeffersonville,(ni saa 1:00 JIONI ya Afrika Mashariki) Ujumbe: Ile Ishara 63-0901M. Ikiwa hamwezi kuungana nasi, chezeni Ujumbe wowote wa Ile Ishara, na muiweke.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya kusikiliza Ujumbe:

Mwanzo 4:10
Kutoka sura ya 12
Yoshua sura ya 12
Matendo 16:31 / 19:1-7
Warumi 8:1
1 Wakorintho 12:13
Waefeso 2:12 / 4:30
Waebrania 6:4 / 9:11-14 / 10:26-29 / 11:37 / 12:24 / 13:8, 10-20
Yohana 14:12