UJUMBE: 63-0321 Muhuri Wa Nne
- 25-0406 Muhuri Wa Nne
- 23-0813 Muhuri Wa Nne
- 22-0220 Muhuri Wa Nne
- 21-0214 Muhuri Wa Nne
- TAI WANAKUSANYIKA PAMOJA
- 19-0428 Muhuri Wa Nne – Preliminari
- 17-0402 Muhuri Wa Nne
Wapendwa Watakatifu Waliozaliwa Kimbinguni,
Baba anatukusanya pamoja kwa Neno Lake, na kule kuthibitishwa kwa Ufunuo huo kunatupa changamko. Yeye alituchagua kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu, kwa maana Yeye alijua tungekuwa waaminifu kwa Neno Lake kwa uchaguzi wetu wenyewe.
Hebu niliseme hilo tena ili liweze kuzama ndani kabisa. Yeye Alitazama kote katika wakati, hadi mwisho kabisa wa nyakati zote, na KUTUONA SISI… hivi unalisikia hilo? ALIKUONA WEWE, ALINIONA MIMI, na akatupenda, kwa sababu kwa uchaguzi wetu wenyewe, sisi tungedumu NA NENO LAKE.
Wakati huohuo, huenda aliwaita pamoja malaika Zake wote na makerubi na kutuelekezea sisi kidole na kusema: “HUYO NDIYE MWANAMKE MWENYEWE,” “HUYO NDIYE BIBI-ARUSI WANGU,” “HAO NDIO AMBAO NIMEKUWA NIKIWASUBIRI!”
Kama vile Yohana, hiyo ndiyo sababu tunapiga makelele haya yote na kupaza sauti, na kumsifu Bwana, tumechangamshwa na Divai Mpya na tunajua, BILA SHAKA HATA CHEMBE, SISI NI Bibi-arusi Wake.
Ni kama mvua na mvua za ngurumo zote ambazo tumekuwa nazo hapa Jeffersonville wiki hii…Sisi pia tunatuma ONYO kwa ulimwengu.
Bibi-arusi anapokea MVUA YA NGURUMO YA UFUNUO, NAYO INATOA MAFURIKO YA UFUNUO. BIBI-ARUSI AMEJIWEKA TAYARI NAO WAMEJITAMBUA WAO NI NANI. NENDA MAHALI SALAMA UPESI. BONYEZA PLAY AMA UANGAMIE.
Hatuishi katika wakati wa Simba, au wakati wa Ndama, wala Wakati wa Mwanadamu; tunaishi katika WAKATI WA TAI, Naye Mungu ametutumia tai mwenye nguvu, Malaki 4, kumwita Bibi-arusi Wake atoke na kumwongoza.
Litakuwa jambo lenye manufaa jinsi gani Jumapili hii, tutakapokuwa tumeungana pamoja tukiusikiliza Muhuri wa Nne. Itakuwa ni Siku ya Kuzaliwa ya nabii-tai mwenye nguvu wa Mungu.
Hebu na tuisherehekee siku hii ya ajabu na tumshukuru Bwana kwa kututumia mjumbe-tai Wake, ambaye aliyemtuma kutuita tutoke na kilifunua Neno Lake.
Ndugu. Joseph Branham
Ujumbe: Muhuri wa Nne 63-0321
Muda: saa 06:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville (Ni saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki)
Maandiko ya kusoma kwa ajili ya maandalizi.
Mathayo Mt. 4
Luka Mt. 24:49
Yohana Mt. 6:63
Matendo 2:38
Ufunuo 2:18-23, 6:7-8, 10:1-7, 12:13, 13:1-14, 16:12-16, 19:15-17
Mwanzo 1:1
Zaburi 16:8-11
2 Samweli 6:14
Yeremia 32
Yoeli 2:28
Amosi 3:7
Malaki 4