24-1222 Zawadi Ya Mungu Iliyofungwa

UJUMBE: 60-1225 Zawadi Ya Mungu Iliyofungwa

PDF

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi. JEZU,

Ee Mwana-Kondoo wa Mungu, Wewe ndiwe Zawadi iliyo kuu ya Mungu iliyofungwa kwa ulimwengu. Umetupa Zawadi iliyo kuu kuliko zote iliyowahi kutolewa, Wewe Mwenyewe. Kabla haujaumba nyota ya kwanza, kabla haujaumba dunia, mwezi, mfumo wa jua, ulitujua sisi na kutuchagua tuwe Bibi-arusi Wako.

Ulipotuona wakati huo, ulitupenda. Tulikuwa nyama ya nyama Yako, mfupa wa mfupa Wako; tulikuwa sehemu Yako. Jinsi Ulivyotupenda na kutaka kushirikiana nasi. Ulitaka kuushiriki Uzima Wako wa Milele nasi. Tulijua basi, tungekuwa Bibi JEZU Wako.

Uliona tungeshindwa, kwa hivyo Wewe ulilazimika kuiandaa njia ya kuturudisha sisi. Tulikuwa tumepotea na bila tumaini. Kulikuwa na njia moja tu, Ilibidi Wewe ufanyike “Uumbaji Mpya”. Ilibidi Mungu na mwanadamu wawe Mmoja. Ilibidi Wewe ufanyike sisi, ili sisi tuweze kuwa Wewe. Hivyo, Ukauweka mpango Wako mkuu utende kazi maelfu ya miaka iliyopita katika bustani ya Edeni.

Umetamani sana kuwa pamoja nasi, Bibi-arusi Wako wa Neno kamilifu, lakini Wewe ulijua kwanza Ilikubali uturudishe sisi kwenye yale yote yaliyokuwa yamepotea hapo mwanzo. Ulingoja na kungoja na kungoja hadi siku hii kuukamilisha mpango Wako.

Siku hiyo imefika. Lile kundi dogo uliloliona hapo mwanzo liko hapa. Kipenzi chako anayekupenda Wewe na Neno Lako kuliko kitu chochote.

Ilikuwa ni wakati Wako wa kuja na kujidhihirisha Mwenyewe katika mwili wa mwanadamu kama ulivyofanya kwa Ibrahimu, na kama ulivyofanya ulipofanyika Uumbaji mpya. Jinsi Wewe umeisubiri kwa hamu siku hii ili uweze kutufunulia sisi siri Zako zote kuu zilizofichwa tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu.

Unamjivunia sana Bibi-arusi Wako. Jinsi Wewe unavyopenda kumwonyesha Yeye na kumwambia Shetani, “Hata ujaribu kuwafanyia nini, wao hawataondoshwa; hawatapatana kuhusu Neno Langu, Sauti Yangu. Wao ni BIBI-ARUSI Wangu wa NENO KAMILIFU.” Wao ni wakupendeza sana Kwangu. Hebu Watazame tu! Kupitia majaribio na majaribu yao yote, wao wanabaki waaminifu kwa Neno Langu. nitawapa zawadi ya milele. Yote niliyo Mimi, Nawapa wao. TUTAKUWA MMOJA.

Tunachoweza tu kusema ni: “JEZU, TUNAKUPENDA. Jalia tukukaribishe nyumbani mwetu. Hebu na tukupake Wewe mafuta na tuioshe miguu Yako kwa machozi yetu na kuibusu. Hebu na tukuambie jinsi tunavyokupenda Wewe.”

Yote tuliyo, tunakupa wewe JEZU. Hiyo ndiyo zawadi yetu Kwako JEZU. Tunakupenda. Tunakuhimidi. Tunakuabudu.

Ninawaalika kila mmoja wenu aungane nasi Jumapili saa 6:00 SITA MCHANA, saa za Jeffersonville,(Ni saa 2:00 MBILI USIKU ya Afrika Mashariki) na umkaribishe JEZU nyumbani kwako, kanisani kwako, ndani ya gari lako, popote uwezapo kuwa, na uipokee Zawadi iliyo kuu kuliko zote iliyowahi kutolewa kwa mwanadamu; Mungu Mwenyewe akizungumza na kushirikiana nawe.

Ndugu. Joseph Branham

60-1225 Zawadi ya Mungu Iliyofungwa