UJUMBE: 60-1205 Wakati Wa Kanisa La Efeso
- 24-1020 Wakati Wa Kanisa La Efeso
- 23-0430 Wakati Wa Kanisa La Efeso
- 20-1108 Wakati Wa Kanisa La Efeso
- 19-0120 Wakati Wa Kanisa La Efeso
- 16-0313 Wakati Wa Kanisa La Efeso – Preliminari
Mpendwa Bibi-arusi Wa Kweli,
Ni wakati mzuri sana jinsi gani tulio nao huku Uzima Wake ukitiririka na kudundadunda ndani na kupitia kwetu, ukitupa uzima. Bila ya Yeye, hakungekuwa na uzima wo wote. Neno Lake ndilo pumzi yetu.
Katika siku hii kuu ya giza, sisi ndio kundi Lake la mwisho ambalo limeinuka; Bibi-arusi Wake wa kweli wa siku ya mwisho ambaye atamsikiliza Roho peke yake, Sauti ya Mungu kwa ajili ya siku yetu.
Jinsi tunavyopenda kumsikia Yeye akituambia, “Kwangu Mimi, umefananishwa na dhahabu safi iliyofuliwa. Haki yako ni haki Yangu. Sifa zako ndio sifa Zangu zenye utukufu. Wewe ndiye Bibi-arusi Wangu wa Kweli wa kupendeza.”
Kama vile vita vyetu vinavyoonekana kuwa vigumu zaidi na zaidi kila wiki, sisi Tunabonyeza Play tu ili kumsikia Yeye akizungumza nasi kwa utamu sana na kutuambia, “Usijali, wewe unaistahili injili Yangu. Wewe ni kitu cha uzuri na furaha. Ninapenda kukutazama pindi unapomshinda adui kwa majaribu na majaribio ya maisha haya.”
Ninaiona taabu yako ya upendo; ni wito mkuu maishani mwako kunitumikia Mimi. Nilijua kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu ya kwamba wewe ungemtambua malaika Wangu mwenye nguvu ambaye ningemtuma awe Sauti Yangu kwako; jinsi ambavyo usingedanganyika wakati ambapo wale mbwa-mwitu wakali wakija huku wakijaribu kudai ufunuo sawasawa. Wewe Hungetoka kwenye Neno Langu, hata kidogo, HATA KWA NUKTA MOJA. Wewe ungekaa na Neno Langu, Sauti Yangu.
Ungeona wakati ninapokufunulia Neno Langu jinsi gani ule Mzabibu wa Kweli na mzabibu wa uongo ile iliyoanza katika Bustani ya Edeni jinsi ingekua pamoja kote katika nyakati zote.
Kile kilichoanza katika kanisa la kwanza kingeendelea katika kila wakati. Jinsi ambavyo katika wakati wa kwanza wa kanisa, ule mzabibu wa uongo wa Shetani ungeanza kujiingiza ndani, na kuwashinda washirika kwa roho yake ya unikolai. Lakini jinsi gani ninavyolipenda hili kwamba wewe tu, Bibi-arusi Wangu mteule, hutadanganywa.
Wiki hii, Nitaliangazia Neno Langu ndani yenu kwa kuifichua ile siri kuu ya ule uzao wa nyoka. Nitawafunulia kwa undani yote yaliyotukia katika bustani ya Edeni; jinsi ambavyo Shetani alivyojichanganya katika jamii ya binadamu.
Litakuwa wazo la kufurahisha sana wakati mtakapotambua kwamba Mimi, Ule Mti wa Uzima katika Bustani ya Edeni, ambao usingeweza kukaribiwa hadi sasa kwa sababu ya kuanguka kwa Adamu, sasa mmepewa ninyi, washindi Wangu.
Hii ndiyo itakuwa thawabu yako. Nitakupa haki ya bustani ya Mungu; ushirika wa daima na Mimi. Kamwe hautatengana na Mimi. Po pote Niendapo, wewe, Bibi-arusi Wangu utakwenda. Kile kilicho Changu Mimi, Nitakishiriki na wewe, Mpendwa Wangu.
Jinsi gani mioyo yetu inavyoenda mbio ndani yetu wakati tunapoyasoma maneno haya. Tunajua ule utimilifu wa ahadi zake unakaribia upesi, na ni vigumu kwetu kusubiri. Na hebu tuharakishe kulitii Neno Lake na hapo tuthibitishe kustahili kwetu kushiriki utukufu Wake.
Ningependa kuwaalika mje kuungana nasi wakati tunapoendelea na somo letu kuu la Nyakati Saba za Kanisa, ambapo Mungu anapotufunulia Neno Lake kwa njia Yake aliyoiandaa, malaika-mjumbe Wake wa saba.
Ndugu. Joseph Branham
Jumapili saa 6:00 sita MCHANA, saa za Jeffersonville. (Ni Saa 1:00 MOJA JIONI ya Afrika Mashariki)
60-1205 Wakati Wa Kanisa La Efeso