Mpendwa Bibi-arusi,
Bwana ameweka moyoni mwangu kuwa na Ujumbe Maalum na Ibada ya Ushirika katika Mkesha wa Mwaka Mpya tena mwaka huu. Ni jambo gani kubwa zaidi tunaloweza kufanya, Enyi marafiki, kuliko kuisikia Sauti ya Mungu ikizungumza nasi, kushiriki Meza ya Bwana, na kuyaweka wakfu tena maisha yetu kwa huduma Yake wakati wa kuukaribisha Mwaka Mpya. Utakuwa wakati mtakatifu jinsi gani kuufungia nje ulimwengu, na kuungana na Bibi-arusi kwa ajili ya huku kukusanyika Maalum katika Neno, tunaposema kutoka mioyoni mwetu, “Bwana, utusamehe makosa yote tuliyofanya mwaka mzima; sasa tunakukaribia Wewe, tukikuomba ikiwa utatushika mkono na kutuongoza mwaka huu ujao. Jalia tukutumikie Wewe zaidi ya tulivyowahi, na kama ni katika Mapenzi Yako ya Kiungu, jalia uwe ndio mwaka wa ule Unyakuo mkuu utakaotukia. Bwana, tunataka tu kwenda Nyumbani kuishi Nawe Milele yote.” Nasubiri kwa hamu kukusanyika kukizunguka Kiti Chake cha Enzi kwa ajili ya ibada hii maalum ya kujiweka wakfu upya, Bwana asifiwe.
Kwa waamini walio katika eneo la Jeffersonville, ningependa kuianza kanda saa 1:00 MOJA JIONI katika saa za eneo letu. Ujumbe kamili na ibada ya Ushirika itakuwa kwenye Redio ya Sauti wakati huo, kama tulivyofanya wakati uliopita. Vifurushi vya divai ya Ushirika vtapatikana Jumatano, tarehe 18 Desemba, kuanzia 7:00 – 11:00 jioni, kwa wewe kuja kuchukua kwenye jengo la YFYC.
Kwa wale ambao wanaishi nje ya eneo la Jeffersonville, tafadhali iweni na ibada hii maalum kwa wakati unaofaa kwenu. Tutakuwa na anuani ya kupakuliwa yenye Ujumbe na Ushirika hivi karibuni.
Tunapokaribia Sikukuu ya Krismasi, nataka nikutakie wewe na familia yako Msimu wa AJABU na SALAMA wa Sikukuu, na KRISmasi Njema, iliyojaa furaha ya Bwana Yesu aliyefufuka…Lile NENO.
Mungu awabariki,
Ndugu Joseph