TANGAZO LA IBADA YA USHIRIKA WIKI HII

Ilitumwa jana: Jumatatu, tarehe 23 Septemba, 2024

Ndugu na dada,

Ningependa tuwe na Ibada nyingine ya Ushirika na Kutawadhana Miguu Jumapili hii, tarehe 29 Septemba, Bwana akipenda. Kama tulivyofanya wakati uliyopita, ningewahimiza muanze saa 11:00 KUMI NA MOJA JIONI. kwa masaa ya nchi zenu. Ingawa Ndugu Branham alisema mitume wao walifanya Ushirika kila wakati walipokutana pamoja, Yeye alipendelea kuufanya wakati wa jioni, naye akautaja kama Meza ya Bwana.

Ujumbe na ibada ya Ushirika itakuwa kwenye Redio ya Sauti, na pia kutakuwa na anuani ya faili la kupakuliwa kwa wale ambao hawawezi kuipata Redio ya Sauti Jumapili asubuhi.

Kwa waamini wa eneo la Jeffersonville, tutakuwa na divai ya Ushirika tena itakayopatikana kwa ajili ya kuja kuchukua. Tangazo litatoka hivi karibuni kueleza mahali, siku na saa.

Hakika niko chini ya matarajio kwa sisi kushika agizo hili la thamani ambalo Bwana alilotuachia. Ni fursa ilioje kwetu sisi kuandaa nyumba zetu na kuifungua mioyo yetu kwa ajili ya Mfalme wa Wafalme aingie na kula pamoja nasi Mezani Pake.

Mungu awabariki,

Ndugu Joseph

https://branhamtabernacle.org/en/bt/A9/109403