21-1024 Kristo Amefunuliwa Katika Neno Lake Mwenyewe

Ujume: 65-0822m Kristo Amefunuliwa Katika Neno Lake Mwenyewe

PDF

pakua

BranhamTabernacle.org

Mpendwa Bibi-arusi mwenye changamko,

Hatujawahi kamwe kuwa na furaha kama hiyo , au kuridhika zaidi katika maisha yetu. Tunachangamko kwa Ufunuo zaidi ya hapo awali. Ulimwengu unaporomoka. Watu wameingia wendawazimu kabisa. Tunaona vitu ambavyo tumesikia juu ya maisha yetu yote sasa yakitukia mbele ya macho yetu.

Kila Ujumbe tunaosikia upo katika wakati mkamilifu kabisa na kile hasa tunachohitaji kusikia. Ni Chakula Cha Kiroho Kwa Wakati Wake. Tumeridhika Sio mawazo ya mwanadamu, wala Siyo Maneno ya mwanadamu, Ni Maneno ya Mungu Asemayo kupitia Mwanadamu, kumwita Bibi-arusi Wake atoke.

Tunaweza kusema kutoka kwenye kina cha mioyo yetu:

. Ujumbe huu ni Bwana Asema hivi.

. Ni njia iliyotolewa na Mungu kwa ajili ya wakati huu.

. Hauhitaji fasiri yoyote.

. Ni Maneno yasiokosea.

Kusikiliza mifululizo hii ya mwisho ya Ujumbe imekuwa jambo kuu maishani mwangu. Nataka tu kushiriki nukuu baada ya nukuu na kila mmoja. “Je! Ulisikia nukuu hii… sijawahi kuisikia namna hiyo hapo awali… nilisikiliza kanda hiyo mara 4 katika siku chache zilizopita na sikuwahi kulinasa kama nilivyofanya leo hii. Ujumbe huu ni wa sasa zaidi kuliko wakati ulipohubiriwa miaka 56 iliyopita ”.

Hakuna kitu chochote kama ile furaha kubwa ya kujua unasikiliza Sauti safi ya Mungu iliyothibitishwa. Hakuna haja ya wewe kujiami. Hakuna haja ya kujiuliza, je! Hili Linalingana na Neno.? Hivi Hayo ni mawazo yake au ni fasiri yake? Napaswa niende kulikagua kwenye Neno.

Sio sisi, sisi
tunaketi tu, tunapumzika, na kusema AMEN kwa kila Neno, kwani tunajua kila tunachokisikia ni BWANA ASEMA HIVI.

Haiwi vizuri au rahisi kuliko hivyo.

Nimekuwa nikiomba na kumtafuta Bwana naye ananiongoza kuendelea na jumbe hizi za mwisho ambazo nabii alizonena. Najua tumesikiliza Jumbe hizi zifuatazo miezi michache iliyopita, lakini kila wakati tunapozisikia Yeye hutufunulia mengi zaidi na zaidi .

Ninapofikiria juu ya Bibi-arusi Wake, wamekusanyika pamoja kutoka kote ulimwenguni, wakingojea kwa shahuku kubwa kuuanza Ujumbe wao kumsikia Mungu akizungumza nao kwa midomo ya nabii Wake, mimi hufurahi sana. Je! Yeye atatufunulia nini leo hii?

Kuna uamsho mkuu unaotendeka kote ulimwenguni. Bibi-arusi anapaaza sauti , akisema: “Tunataka kusikia kanda. Tunataka kubonyeza play. Tunataka kuungana na Bibi-arusi kwenye Neno ”.

Tunaungana na kuketi pamoja katika Uwepo wa Mwana, kuivishwa , tukijiandaa kwa ajili ya Unyakuo. Ningependa kukualika uje kuivishwa pamoja nasi saa 8:00 nane Mchana , saa za Jeffersonville, ( ni saa 3:00 tatu usiku ya Tanzania) tunapomsikia Mungu akizungumza na Bibi-arusi Wake na kuleta Ujumbe, Kristo Amefunuliwa Katika Neno Lake Mwenyewe 65-0822M .

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma kabla ya kusikiliza Ujumbe:

Kutoka 4: 10-12

Isaya 53: 1-5

Yeremia 1: 4-9

Malaki: 4: 5

Luka Mtakatifu 17:30

Yohana Mtakatifu 1: 1 /1:14 / 7: 1-3 / 14:12 / 15:24 / 16:13

Wagalatia 1: 8

2 Timotheo 3: 16-17

Waebrania 1: 1-3 / 4:12 / 13: 8

2 Petro 1: 20-21

Ufunuo 1: 1-3 / 10: 1-7 / 22: 18-19