21-1003 Mungu Wa Wakati Huu Mwovu

UJUMBE: 65-0801m Mungu Wa Wakati Huu Mwovu

PDF

pakua – m4a

pakua – amr 13MB (use Firefox to download)

Mpendwa Bibi-arusi Changamko kwa Ufunuo,

Ni nini kilikuwa kinatukia kote ulimwenguni wikendi hii iliyopita? Ni kitu gani kilikuwa kinatendeka? Vifijo hivyo vyote vilikuwa ni vya nini? Bibi-arusi kutoka kote ulimwenguni waliungana pamoja, na kutengeneza milima kwa plasta, udongo, mchanga na vijiti. WakiKukusanyika kwenye mioto iwakayo , kuimba nyimbo za ibada na kumsifu Bwana. Vijana kwa wazee wote namna moja, wakiwa wamevaa fulana sinazosema Changamko Kwa Ufunuo. Walikuwa kutoka Michigan hadi Florida, kutoka Maine hadi California, kutoka Amerika Kaskazini hadi Amerika Kusini, Ulaya, Afrika, Asia, Australia, kila kona ya dunia. Walikuwa wakisikiliza kwa kuunganishwa katika nyumba zao, wakisikia Sauti ya Mungu ikiwazungumzia moja kwa moja.

Nini kilichovutia? Uzao wa Mungu uliochaguliwa tangu awali ambao hauwezi kufanya vinginevyo isipokuwa kufuata Ujumbe wa wakati huu , ambao wanaamini kila Neno lililonenwa na kinywa cha Mungu, walikuwa wamekusanyika pamoja katika sifa, katika kuabudu, na katika kusherehekea tukio kuu lililotukia katika siku yetu juu ya Mlima Sunset.

Ilikuwa ni Mungu akithibitisha Neno Lake. Ndio maana ya kelele zote hizi . Angalia, ni Mungu akitimiza Neno Lake lililoahidiwa tena, la Ufunuo 10: 1 hadi 7, “Na katika siku za kutangazwa kwa Ujumbe wa malaika wa saba, siri ya Mungu itatimia .”

Ilikuwa ni Mungu akifanya historia. Ilikuwa ni Mungu akitimiza unabii. Lilikuwa jibu la unabii wa nabii. Na tulitamani kuwapo pale ili kupata na kusikia chochote ambacho Yeye alichofanya kupitia nabii Wake.

Tunapuuza ukosoaji wa Asiyeamini na waamini wa kujifanya. Hatuna hoja nao. Tuna jambo moja la kufanya, hilo ni kuamini na kupata kila sehemu yake tuwezayo. Tunakusanyika pamoja kila wiki kama wa moja kusikia Sauti ya Mungu, tunapongojea kuja kwa Masihi.

Ni Saa kuu jinsi gani tunayoishi. Kuona Maandiko yanatimizwa katika maisha yetu. Lakini Alituonya katika Neno Lake kwamba upako wa uwongo ungefanana sana, ungewapoteza KAMA Yamkini walio wateule wa Mungu. Lakini Mungu asifiwe, haitawezekana kumpoteza Bibi-arusi Wake, kwa maana wao watadumu na ile Sauti ya Mungu ya asili, iliyodhihirishwa, na iliyothibitishwa na hawatabadilisha nukta moja au yodi moja. Hawataongeza fasiri yao wenyewe Kwake, lakini kirahisi wataamini KILA NENO.

Tunapaswa kuwa waangalifu sana jinsi gani kama WATAFANANA SANA . Tunashangaa, je yatakuwa ni haya makanisa ya kimadhehebu? Wao Wanaonekana wako nje mbali sana na hata hawafanani. Basi Atakuwa ni nani?

Sasa, makanisa tu baridi, ya kawaida, magumu, na kadhalika, ya theolojia za kujitengenezea, hayo hayangeweza; walio Wateule wasingewajali. Lakini ni kule juu karibu sana na jambo lililo halisi. Kuacha tu Neno moja ndivyo tu unavyopaswa kufanya.

Alisema Hawa hakuondoka tu kirahisi akasema siamini Mungu.Yeye aliamini kosa. Shetani yeye alikubali hilo lilikuwa Neno la Mungu, lakini shida ilikuwa aliweka fasiri yake mwenyewe kwake na ilimfanya hawa aamini uwongo na alihukumiwa nao.

Jalada limeondolewa. Piramidi imefunguliwa. Maandiko yamefunuliwa. Ufunuo Amepewa Bibi-arusi. Ni Yesu Kristo yeye yule jana, leo na hata milele.

Hilo Linamfanya Shetani atukasirikie sana. Anajua amefikia mwisho wake. Yeye Anataka tujiulize sisi ni akina nani. Tunapitia mitihani na majaribu magumu kuliko tulivyowahi kupitia. Wakati mwingine tunajiuliza, kwa nini haya yote yanatutokea?

Sababu yake ni kwamba, ni kumjaribu Yeye, Bibi-arusi Wake. Ni ku-…Wakati amedhihirishwa, akajaribiwa, kuthibitishwa, akathibitishwa kwa Shetani

Utukufu !!! Majaribu na mitihani yetu ni Yeye tu akimthibitishia Shetani SISI NDIYE BIBI-ARUSI WAKE ALIYETHIBITISHWA

Tunaona sasa, wakati huu mwovu ni kuthibitisha, kwa Shetani, Yeye si kama Hawa, ya kwamba Yeye si mwanamke wa namna hiyo. Naye atajaribiwa kwa Neno Lake , Bibi-arusi, kama bibi-arusi wa Adamu alivyojaribiwa kwa Neno. Na bibi-arusi wa Adamu aliamini kila sehemu ya Neno, lote, ila akachanganyikiwa kwenye ahadi moja .

Lakini hatutachanganyikiwa hata kwa Neno moja au kufuata mapokeo yao, Fasiri zao za Neno, tutadumu na NENO LA ASILI.

Kama tuna kinasasauti, tutakusanya kundi la watu pamoja, na tuicheze, na kusikiliza kwa makini, kama vile alivyotuambia tufanye!

Ni kama tu vile uhai wako wa kawaida na tabia inavyoridhiwa na kuzaliwa kwa asili kwa baba yako, ndivyo alivyo Roho wa Mungu, aliyechaguliwa tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu.

Tunashukrani jinsi gani kwamba Roho wa Mungu, kuzaliwa kwetu, kulichaguliwa kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu kuwa na Ufunuo wa Kweli wa Ujumbe Huu.

Unakaribishwa kuja kupata Changamko lile lile kwa ufunuo pamoja nasi Jumapili saa 8:00 nane mchana , saa za Jeffersonville , (ni saa 3:00 tatu Usiku ya Tanzania) tunaposikia: 65-0801M Mungu Wa Wakati Huu Mwovu.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma:

Mathayo Mtakatifu 24/27: 15-23

Luka Mtakatifu 17:30

Yohana Mtakatifu 1: 1 / 14:12

Matendo 10:49

1 Wakorintho 4: 1-5 / 14 sura yote

2 Wakorintho 4: 1-6

Wagalatia 1: 1-4

Waefeso 2: 1-2 / 4:30

2 Wathesalonike 2: 2-4 / 2:11

Waebrania sura ya 7

1 Yohana Sura ya 1 / 3:10 / 4: 4-5

Ufunuo 3:14 / 13: 4 / Sura ya 6-8 na 11-12 / 18: 1-5

Mithali 3: 5

Isaya 14: 12-14