21-0912 Chakula cha Kiroho kwa Wakati Wake

UJUMBE: 65-0718e Chakula Cha Kiroho Kwa Wakati Wake

PDF

pakua

BranhamTabernacle.org

Tai wanakusanyika Pamoja.

Mpendwa Kondoo wa Zizi la kondoo wa Mungu,

Katika siku ambazo Bwana wetu Yesu alipokuwa hapa duniani katika mwili, wakosoaji na wasioamini walimwambia:

Hata Lini utatuhangaisha Nafsi Zetu? Kama wewe ndiwe Kristo, utuambie waziwazi.

Kwa mara nyingine, Atazungumza nasi waziwazi na kuwaambia wakosoaji Wake na Bibi-arusi Wake, “Mimi ni mtu anayetoka kwa Mungu, aliyetumwa kutoka kwa Mungu, aliyeteuliwa na Mungu, nikiwa na BWANA ASEMA HIVI ya Kweli . Nimekaa kwa muda mrefu sana katika uwepo wake , nitanena na wewe kama Mungu mwenyewe.

Nataka kusiwe na shaka, na kwako wewe kuamini, mimi ni mjumbe wa Mungu kwako. Ujumbe ambao mimi Ninaounena , na mjumbe, ni kitu kile kile . Sisi ni Mmoja na kitu kimoja. Alinituma kwako kuwakilisha BWANA ASEMA HIVI, Neno kwa Neno.

Kumbuka, Neno la Mungu linasema Yeye hatafanya neno lolote mpaka kwanza anifunulie mimi. Watu wanataka kuweka fasiri zao wenyewe kwa yale ninayosema, lakini Maneno ambayo ninayo Nena na wewe hayahitaji Fasiri yoyote. Wewe sema TU Yale ninayosema.

Nataka pia utambue kwamba Neno lile lile ninalokuambia, pia linaishi ndani yetu. Una mamlaka ya Mungu aliye hai ndani yako. Wewe ndiye Bibi-arusi Kanisa Lililo Hai.

Baada ya Mimi kuondoka, lakini kabla ya ukame kuanza, Mungu amekuandalia mahali pa siri pa kujificha kabla ya hukumu kuipiga dunia. Utakuwa pale unasubiri, unakula Chakula hiki kilichofichwa ambacho atakachokuachia. Utakuwa ukiishi juu ya wema na rehema za Ufunuo wa Yesu Kristo anavyojithibitisha kwako kila siku.

Kwenu ninyi , Kitakuwa Chakula cha Rohoni kwa wakati wake. kingewachefua wengine tumbo. Nitakuwa mnono sana kwao. Lakini kwa ajili yenu, Kondoo Wake, Utakuwa ni Mkate wa Uzima, Yesu Kristo yeye yule jana, leo, na hata milele.

Usisahau, nitakulisha “HUKO”; si mahali pengine, “HUKO”. Watu watakucheka na kusema wewe una kichaa, lakini kile wanachokiita kichaa na Upuuzi , Mungu ataita kikuu . “

Alituambia kwamba huduma kuu ambayo Mungu aliyompa ilikuwa vinafanana kabisa na wakati wa Eliya. Baada ya ukame kuwa unakaribia kwisha, yeye Alimwita atoke na kumpeleka kwenye NYUMBA ya mjane mpaka ukame ulipoisha.

Alisema mjane huyu hakuwa Ameshirikiana na wasioamini au kuchukua alama ya mnyama wakati wa ukame, kwa hiyo alimwita Eliya kumlisha huyu mjane . Alikuwa tayari kufa kwani alikuwa amebaki na keki moja ndogo, kitu kimoja kidogo yule mama alichokuwa anashikilia.

Eliya akamwita huyo mwanamke , “Nipe hicho mimi, kwanza. Kwa kuwa, BWANA ASEMA HIVI, lile pipa halitapunguka wala ile chupa haitaisha, hata siku ile Bwana Mungu atakapoleta mvua juu ya nchi.”

Ilimbidi kumweka Mungu kwanza . Ilimbidi kuamini na kushikilia kila Neno ambalo mjumbe huyo alilosema. Alijua kwamba mjumbe na Ujumbe wake walikuwa kitu kimoja. Maneno aliyomwambia yangetimia , kwa maana ilikuwa Bwana Asema Hivi.

Ndivyo ilivyo leo, ya kwamba Chakula cha Uzima ambacho watoto wanakula, kinafuata Ujumbe wa Mungu, kuwahifadhi katika wakati wa ukame.

Neno lilo hilo limekuja kwetu na liko ndani yetu na tunakula mambo ya siri ya Mungu ambayo ulimwengu umefichwa. Ametufunulia kwamba Ujumbe na mjumbe ni kitu kimoja. Chakula cha kiroho kiko tayari, na kiko katika wakati sasa.

Unakaribishwa kwenye SIKU SIKUU NYINGINE KWA AJILI YA BIBI-ARUSI . Tutatwaa chupa la Mafuta, na Litakuwa Limefurika tena . Kisha tutachota ndani ya pipa la unga, na litajaa tena mpaka juu. Tutaketi mahali pamoja katika ulimwengu wa Roho kutoka kote ulimwenguni, tukiwa tumefichwa mahali petu pa siri, tukiifurahia mana iliyofichwa wakati Mungu anapojithibitisha mwenyewe kwetu.

Njoo ukusanyike katika zizi la Kondoo pamoja nasi Jumapili saa 8:00 nane Mchana , saa za Jeffersonville, (ni saa 3:00 tatu Usiku ya Tanzania)
Tunaposikia Mjumbe wa Mungu akituletea Ujumbe wa Mungu: Chakula cha Kiroho Kwa Wakati Wake 65-0718E.

Sisi tukiwa na dola moja
na senti themanini za kujenga Maskani , watu wengi wa gereji tayari walikuwa wameamua itakuwa gereji yao. Lakini ingali ni zizi la kondoo kwa ajili ya Kondoo wa Mungu.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya kusoma

1 Wafalme 17: 1-7
Amosi 3: 7
Yoeli 2:28
Malaki 4: 4
Luka 17:30
Yohana Mtakatifu 14:12