21-0815 Ile Mbegu Haitarithi Pamoja na Kapi

Ujumbe: 65-0429b Ile Mbegu Haitarithi Pamoja na Kapi

PDF

pakua

BranhamTabernacle.org

Tai wanakusanyika Pamoja.

Mpendwa Mwili wa Mwili Wake,

Nina furaha sana kwamba Mungu habadilishi nia Yake kuhusu Neno Lake. Yeye ni yeye yule jana, leo na hata milele. Jinsi alivyofanya mambo tangu mwanzo, anafanya vile vile leo. Mungu, Mwenyewe, aliyejidhihirisha katika mwili wa mwanadamu, kwa Damu ya Yesu Kristo, kutakasa maisha ili Aweze kujiakisi mwenyewe kupitia huo .

Mjumbe wetu leo hii ​​ana Utambulisho wake wa Kimaandiko kati yetu. Ni Roho Mtakatifu, Mwenyewe, akijifasiria Mwenyewe. Hakuna haja ya kwenda kutoka kwa hili kwenda kwa Lile ili kupata ukweli au fasiri; Roho Mtakatifu amelipa Kanisa Lake Waefeso 4, yote katika mtu mmoja, nabii Wake aliyethibitishwa.

Mtume : Mtume maana yake ni “aliyetumwa,” au, “mmishenari.” Mimi ni mmishenari.

Nabii : Je! Unaniamini mimi kuwa nabii wa Mungu?

Mwinjilisti : “ Fanya kazi ya mhubiri wa injili. Timiliza huduma yako. Utakuja Wakati watakapoyakataa mafundisho Yenye uzima. “

Mchungaji : Mwaniita, “mchungaji wenu”; nanyi mwasema vema, kwa maana ndivyo nilivyo.

Mwalimu : Nataka kuzungumza juu ya Neno, ama kufundisha somo hili la shule ya Jumapili, juu ya Neno la Ile Ishara .

Ni sawa na = Ninajua ninyi, ndugu zetu, mnanitazama mimi kuwa Yakini kwa kile… maadamu ninamfuata Mungu, kama vile Paulo alivyosema katika Maandiko, “nifuateni mimi, kama mimi ninavyomfuata Kristo.”

Ujumbe huu ni Yakini yetu, hivyo tunamfuata yeye kama anavyomfuata Kristo.

Wala Sipuuzi kuwa kuna wengi ambao Mungu anawaita Waefeso 4 watu ambao wamewekwa na kuitwa na Mungu kutimiza ofisi hizi; kwa NEEMA YAKE, mimi ni mmoja wao. Lakini sisi ni wadogo, nabii malaika wa 7 wa Mungu ndiye MKUU.
Kwa wale ambao kote ulimwenguni huiita “Maskani ya Branham ” “kanisa Lao la nyumbani”: mchungaji wetu, huduma yetu iliyo hai, Yakini yetu, Waefeso 4 yetu yote ipo kwenye kanda. Tunaamini ni huduma ya asili ambayo alikuwa nayo wakati alipokuwa hapa duniani.

Ni amani iliyoje, pumziko jinsi gani, hatujawahi kuwa na wasiwasi au kumvuka kiongozi wetu au chujio letu wakati tunaposikia Neno. Ni Neno la Mungu lililohakikishwa na lililothibitishwa, mana safi kila tunapolisikia na tunachotakiwa kufanya ni kuketi chini na kufurahiya mioyo yetu ikiwaka ndani yetu anapozungumza nasi njiani.

Na wote alionipa Baba, watakuja. Kondoo wangu, hua Wangu, huisikia Sauti Yangu. Mgeni hawatamfuata.” Na Sauti ya Mungu ni nini? Ni Neno la Mungu. Sauti ya mtu ye yote ni nini ila ni neno lake? Ni Neno la Mungu; watalisikia Neno la Mungu .

Halafu bado kuna mengi ZAIDI kwa ajili ya Kanisa Lake. Sio tu kwamba tunatambua siku hii na mjumbe wake, Neno la siku hii, Bali furaha kuu ambayo mwanadamu aliyowahi kupewa hatimaye imetimia. SISI NI sehemu ya Roho Wake, sehemu ya Mwili wake; nyama ya nyama Yake, mfupa wa mfupa Wake; Neno la Neno Lake, Maisha ya Maisha yake, SISI NI Bibi-arusi wa Kristo!

Utukufu !! Lisifikiwe Jina la Bwana !! Haleluya !! Bibi-arusi Wake Amejitambua na Anajifanya Mwenyewe Tayari kwa Neno Lake.

Hivyo ndivyo kanisa linavyofanya siku hizi, kwa kuwa Yesu ni Neno Naye ni Bwana Arusi, na Bibi-arusi ni sehemu ya Bwana Arusi. Kwa hiyo Neno ambalo itapaswa litimizwe siku hii ni sehemu ile ile ya Neno lililotimizwa katika siku Zake, na ni Neno lile lile, tukio lile lile, Maisha yale yale .

Njoo upate uzoefu wa Neno lile lile, tukio lile lile, Maisha yaleyale Jumapili hii saa 8:00 Nane mchana, saa za Jeffersonville,( ni Saa 3:00 tatu usiku ya Tanzania) kusikia: Ile Mbegu Haitarithi Pamoja Na Kapi 65-0429B.

Ndugu. Joseph Branham

Maandiko ya Kusoma:

Mathayo 1: 18-20 / 24:24
Luka 17:30
Yohana mtakatifu 5:24
Wagalatia 4: 27-31
Mwanzo 2:15
Isaya 9: 6
Malaki 4